Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46329 articles
Browse latest View live

DREAMS initiatives Provides safe space for adolescent girls in Shinyanga aiming at prevention of risky HIV behaviors

$
0
0
 Richard Minyako, a Data Manager at Shinyanga-based civil society organization called Rafiki SDO orienting an out of school adolescent girl, Zubeda Said, on how to use a special computer with tailored programs on prevention of risky HIV behaviors as part of the DREAMS Initiative safe space activities rolled out by Jhpiego's Sauti Project.  The DREAMS Initiative in Tanzania is funded by the US Government through PEPFAR and aims to create determined, resilient, empowered, AIDS-free, mentored and safe young women to live healthier lives and achieve their dreams.
 Out-of-school adolescent girls Swaum Mohamed (19) (left) and Rachael Charles (19) (right) using computers with tailored programs on prevention of risky HIV behaviors at a safe space run by Shinyanga-based civil society organization called Rafiki SDO  as part of the DREAMS Initiative package rolled out by Jhpiego's Sauti Project.  The DREAMS Initiative in Tanzania is funded by the US Government through PEPFAR and aims to create determined, resilient, empowered, AIDS-free, mentored and safe young women to live healthier lives and achieve their dreams. 
 Out-of-school adolescent girls  using computers with tailored programs on prevention of risky HIV behaviors at a safe space run by Shinyanga-based civil society organization called Rafiki SDO  as part of the DREAMS Initiative package rolled out by Jhpiego's Sauti Project.  The DREAMS Initiative in Tanzania is funded by the US Government through PEPFAR and aims to create determined, resilient, empowered, AIDS-free, mentored and safe young women to live healthier lives and achieve their dreams.

ETIHAD AIRWAYS PRESENTS MANISH ARORA AT LAKMÉ FASHION WEEK

$
0
0
Designer Manish Arora with Neerja Bhatia Etihad  Airways Vice President Indian Sub Continent along with Etihad Airways crew at Lakmé Fashion Week Winter Festive 2017.
Designer Manish Arora walks the ramp during the final line up for Etihad Airways presents Manish Arora at Lakmé Fashion Week Winter Festive 2017

Models walk the ramp for Etihad Airways presents Designer Manish Arora at Lakmé Fashion Week Winter Festive 2017

Mumbai, INDIA - Etihad Airways presented internationally renowned designer, Manish Arora’s Paris collection at Lakmé Fashion Week last night. The Paris-based designer’s Autumn /  Winter ’17 collection, ‘CosmicLove’ celebrated his 10th anniversary of his French collection with a return to Lakmé Fashion Week.

The offsite show, Etihad Airways presents Manish Arora, featured over 40 models and was attended by over 300 guests. Etihad Airways presented the designer’s collection in a larger-than-life format, with the atrium of the finest luxury mall in the city being transformed into an opulent runway, a first at Lakmé Fashion Week.

MADEREVA KITUO CHA SIMU 2000 WAGOMEA TOZO YA 1000

$
0
0

Mpiga picha wa Globu ya Jamii mapema leo asubuhi amekumbana na adha ya usafiri,kufuatia Madereva katika kituo cha mabasi simu 2000 Manispaa ya Ubungo jijini Dar kugoma kutoa huduma ya usafiri,kwa kile walichodai kupandishiwa tozo kutoka shilingi 500 hadi 1000.

Akizungumza zaidi mmoja wa Madereva wa dala dala katika mgomo huo (hakutaka kujitambulisha jina),alisema kuwa wao hawawezi kulipa tozo hiyo wakati miundombinu ya kituo hicho si rafiki na hairidhishi kabisa kwa vyombo vyao vya usafiri.

"ni vyema wakazirekebisha kwanza changamoto kadhaa zilizopo hapa kituoni,kisha baadae waje na huo mkakati wao wa kutupandishia hiyo tozo yao,lakini kwa sasa itakuwa vigumu kulipa kwa sababu kama unavyoona mazingira yalivyo hapa kituoni",alisema mmoja wa Madereva.

Mpiga picha wa Globu ya Jamii pamoja na kuonja joto ya jiwe ya kukosa usafiri,pia alijionea adha waliokuwa wakiipata abiria wengine waliokuwepo kituoni hapo,huku baadhi ya abiria wakilazimika kutumia usafiri wa piki piki kuwahi kwenye shughuli zao na wengine wakitembea kwa Miguu. 

Mpaka Globu ya Jamii inaondoka kituoni hapo ufumbuzi bado ulikuwa haujapatikana.
 Madereva na Makondakta wakijadiliana kufuatia mgomo huo
Baadhi ya mabasi (dala dala) yakiwa yamepaki kituoni hapo yakisubiri mgomo huo upatiwe ufumbuzi.
 Baadhi ya abiria wakisubiri usafiri kituoni hapo mapema leo asubuhi

Tigo watiliana saini na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Tanzania, Simon Karikari akitia saini ya Mkataba wa Kufikisha Mawasiliano Vijijini na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Eng. Peter Ulanga wakati wa hafla ya kusaini mkataba huo iliyofanyika jijini Dar es Salaam.  Wanaoshuhudia (katikati) ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na  Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa pamoja na maafisa wengine wa mfuko huo. Hafla hiyo ilishirikisha makampuni ya simu nchini.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Tanzania, Simon Karikari akipeana mkono wa pongezi na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Eng. Peter Ulanga mara baada ya kusaini mkataba wa kufikisha mawasiliano  vijijini kwa kampuni za simu Tanzania. Wanaoshuhudia (katikati) ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na  Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa. Hafla iliyoshirikisha makampuni ya simu, ilifanyika jijini Dar Es Salaam mapema wiki iliyopita.
Wakuu wa kampuni za simu Tanzania wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kusaini Mkataba wa Kufikisha Mawasiliano  Vijijini .
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Eng. Peter Ulanga akizungumza na wageni waalikwakwenye hafla ya kusainiana mikataba na makampuni ya simu jijini Dar Es Salaam mapema wiki iliyopita.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na  Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akizungumza na wageni waalikwa kwenye hafla ya kusainiana mikataba na makampuni ya simu jijini Dar Es Salaam mapema wiki iliyopita.

TANZIA;MSIBA MKUBWA NJENJE -BABU FRANCIS AFARIKI DUNIA

$
0
0

 

MWEKA HAZINA wa miaka mingi wa Kilimanjaro Band, ambaye alijulikana kwa wapenzi wengi kutokana na kuwa mkata tiketi wa bendi wa miaka mingi sana, Francis Mnguto, maarufu kwa jina la Babu Francis amefariki leo alfajiri nyumbani kwake Ilala Flats Dar es Salaam. 
 
Kwa miezi kadhaa Babu Francis amekuwa akisumbuliwa na tatizo la figo. Taarifa kutoka kwa familia ni kuwa mazishi yatakuwa Dar es Salaam Jumatano 23 Agosti. Msiba upo nyumbani kwake Ilala Flats Dar es Salaam.

 
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI-AMEN.

GARI LAACHA NJIA NA KUPARAMIA MAWE SEGEREA NJIAPANDA BONYOKWA

$
0
0
 Wakazi wa Tabata Segerea Wilaya ya Ilala wakiwa wanashangaa gari aina ya Land Cluser Prado ambayo imecha barabara na kuvamia Vigingi Vilivyopo kwenye barabara ya kukatisha kwenda Kimara Bonyokwa
 Gari aina ya toyota Land Cluser Ikiwa ipo juu ya mawe mara baada ya kuruka na kuacha njia katika eneo la tabata Segerea njia panda ya kwenda Bonyokwa, gari hiyo imepanda mawe hayo katika harakati za kumkwepa mtu aliyekuwa anakuja mbele yake kwa speed kali hata hivyo katika ajali hiyo Hakuna majeruhi wala mtu aliyefariki wote walitoka Salama
 Gari aina ya toyota Land Cluser Ikiwa ipo juu ya mawe mara baada ya kuruka na kuacha njia katika eneo la tabata Segerea njia panda ya kwenda Bonyokwa, gari hiyo imepanda mawe hayo katika harakati za kumkwepa mtu aliyekuwa anakuja mbele yake kwa speed kali hata hivyo katika ajali hiyo Hakuna majeruhi wala mtu aliyefariki wote walitoka Salama
Gari aina ya toyota Land Cluser Ikiwa ipo juu ya mawe mara baada ya kuruka na kuacha njia katika eneo la tabata Segerea njia panda ya kwenda Bonyokwa, gari hiyo imepanda mawe hayo katika harakati za kumkwepa mtu aliyekuwa anakuja mbele yake kwa speed kali hata hivyo katika ajali hiyo Hakuna majeruhi wala mtu aliyefariki wote walitoka Salama

DC WA UBUNGO KISARE MAKOLI AINGILIA KATI MGOMO WA DALADALA SIMU 2000,AWEKA MAMBO SHWARI

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Ubungo ,Kisare Makoli (pichani kati) akiwa ameongozana na baadhi ya madereva wa dala dala wakielekea  kwenye kituo cha daladala cha Mawasiliano simu 2000 mara baada ya madereva wa Daladala kupinga tozo ya shilingi 1000 kama Ushuru wa magari ambapo awali walikuwa wanalipa shilingi 500
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo ,Kisare Makoli, akizungumza na Madereva Daladala waliopo katika eneo la Simu 2000 mara baada ya kuweka mgomo kupinga tozo ya Shilingi 1000 na kudai kuwa barabara hiyo ni mbovu,Mhe.Makoli ameagiza kuendelea kulipwa tozo hiyo ya zamani ya shilingi 500 badala ya 1000 iliyokuwa imeongezwa,na kwamba madereva waendelee na shughuli zao kusafirisha abiria kama kawaida.

 Mkuu wa Wilaya ya Ubungo ,Kisare Makoli, akizungumza na Madereva Daladala waliopo katika eneo la Simu 2000 mara baada ya kuweka mgomo kupinga tozo ya Shilingi 1000 na kudai kuwa barabara hiyo ni mbovu


 Askari wa kikosi cha Kutuliza Ghasia wakiwa wanaimarisha ulinzi katika eneo la kituo cha Daladala cha Simu 2000

 Askari wa kikosi cha Kutuliza Ghasia wakiwa wanaimarisha ulinzi katika eneo la kituo cha Daladala cha Simu 2000
 Askari wa kikosi cha Kutuliza Ghasia wakiwa wanaimarisha ulinzi katika eneo la kituo cha Daladala cha Mawasiliano Simu 2000.

BENKI YA CRDB YATOA MSAADA GEREZA LA SEGEREA JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0
 Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Benki ya CRDB,Tully Mwambapa wapili kushoto akikabidhi, Mashine za dawa ya kuulia wadudu  kwa mkuu wa gereza la Segerea, Kamishna Msaidizi wa magereza, Godfrey Kavishe kulia ikiwa ni moja ya vitu vyenye thamani ya milioni nane (8,000,000) vilivyotolewa kwa wafungwa wanawake na watoto wa gereza hilo na wafanyakazi wanawake wa benki hiyo. Katikati ni Mkaguzi msidizi wa magereza, Esther Mpotola, Mrakibu wa Magereza, Adeline Mgamtwa na Meneja Uhusiano wa Wawekezaji wa Benki hiyo, Hilda Rwanshane.
 Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Benki ya CRDB,Tully Mwambapa wapili kushoto akiwa katika pichaya pamoja na mkuu wa gereza la Segerea, Kamishna Msaidizi wa magereza, Godfrey Kavishe mbele ikiwa ni moja ya vitu vyenye thamani ya milioni nane (8,000,000) vilivyotolewa  na benki ya CRDB kwa wafungwa wanawake na watoto wa gereza hilo.Katikati ni Mkaguzi msidizi wa magereza, Esther Mpotola, Mrakibu wa Magereza, Adeline Mgamtwa na Meneja Uhusiano wa Wawekezaji wa Benki hiyo, Hilda Rwanshane.
 Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Benki ya CRDB,Tully Mwambapa wapili kushoto akikabidhi  boksi la maziwa ya unga na baadhi ya vitu vya michezo ya watoto  kwa mkuu wa gereza la Segerea Kamishna Msaidizi wa magereza Godfrey Kavishe kulia ikiwa ni moja ya vitu vyenye thamani ya milioni nane (8,000,000) vilivyotolewa kwa wafungwa wanawake na watoto wa gereza hilo na wafanyakazi wanawake wa benki hiyo. Katikati ni Mkaguzi msidizi wa magereza, Esther Mpotola, Mrakibu wa Magereza, Adeline Mgamtwa na Meneja Uhusiano wa Wawekezaji wa Benki hiyo, Hilda Rwanshane.
Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Benki ya CRDB,Tully Mwambapa wapili kushoto akikabidhi, khanga ambazo kwaajili ya kinamama na watoto waliopo gerezani  kwa mkuu wa gereza la Segerea, Kamishna Msaidizi wa magereza, Godfrey Kavishe kulia ikiwa ni moja ya vitu vyenye thamani ya milioni nane (8,000,000) vilivyotolewa kwa wafungwa wanawake na watoto wa gereza hilo na wafanyakazi wanawake wa benki hiyo. Katikati ni Mkaguzi msidizi wa magereza, Esther Mpotola, Mrakibu wa Magereza, Adeline Mgamtwa na Meneja Uhusiano wa Wawekezaji wa Benki hiyo, Hilda Rwanshane.

EFM YAZINDUA TAMASHA LA MZIKI MNENE KWA MIKOA SITA NCHINI.

$
0
0
 Meneja Masoko kutoka kampuni ya Michezo ya Kubahatisha ya Biko, Good Hope Heaven , akizungumza namna kampuni yao ilivyoweza kudhamini Tamasha la Muziki Mnene kupitia bahati nasibu ya Nguvu ya Buku.
 Baadhi ya Watangazaji wa EFM Radio na Tv E Wakifatilia uzinduzi wa Tamasha la Mziki Mnene.
Balozi wa kampuni ya Noah Funishing na Mtangazaji wa Efm Radio, Swebe Santana  akizungumza juu ya kampuni hiyo ilivyojikita katika kudhamini  EFM Joging itakyofanyika katika mikoa yote sita ambapo Tamasha la Muziki Mnene litafanyika.

 Meneja Mkuu wa EFM Radio na Tv E , Denis Busulwa (SEBO), Akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wa uzinduzi wa Tamasha Mziki Mnene litakalo fanyika katika mikoa sita nchini  Sanjari na Kampeni ya Nje Ndani ambayo itarusha vipindi vya Radio kutoka mitaani .
 Afisa Uhusiano na Meneja Matukio wa Efm Radion Tv E , Neema Ukurasi akizungumza juu ya Tamasha la Muziki Mnene litakavyoweza kufika katika mikoa yote ambayo EFM Radio inasikika kwa sasa
 Waandishi wa Habari na Baadhi ya wafanayakazi kutoka Efm Radio na Tv E wakifatilia mkutano wa uzinduzi wa Tamasha la Mziki Mnene.

WABUNGE WA MAREKANI WAIPONGEZA TAYOA.

$
0
0

 Kaimu Balozi wa Marekani Dk. Inmi Patterson akisailimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Vijana Tayoa, Balozi Charles Sanga alipowasili kwenye viwanja vya shirika hilo Bahari Beach Dar es Salaam pamoja na ujumbe wa wabunge watano wa Bunge la Congress la Marekani.
Ujumbe wa wabunge watano wa Bunge la Congress la Marekani wakiangalia ngoma za asili mara baada ya kuwasili kwenye ofisi za Shirika la Vijana Tayoa Bahari Beach Dar es Salaam.
 Kaimu Balozi wa Marekani,  Dk. Inmi Patterson, wa kwanza kushoto akifurahia jambo na ujumbe wa wabunge watano wa Bunge la Congress la Marekani wakati wanazindua redio ya kuelimisha vijana kuhusu mbalimbali kwenye Shirika la Vijana Nchini Tayoa. Wapili kulia ni Mkurugenzi wa Tayoa Peter Masika.
 Vijana wa kikundi cha ngoma za asili wakiburudisha ujumbe wa wabunge watano wa Bunge la Congress la Marekani waliotembelea Shirika la Vijana nchini Tayoa Bahari Beach Jijini Dar es Salaam.
 
Na Mwandishi Wetu
UBALOZI wa Marekani nchini, umesifu kazi zinazofanywa na Shirika la Vijana Nchini (Tayoa), katika kuwainua na kuwahamasiha vijana kujikwamua kiuchumi na kushiriki kwenye shughuli mbalimbali za maendeleo nchini.

Hayo yalisemwa jana na Kaimu Balozi wa Marekani nchini, Dk. Inmi Patterson, wakati ujumbe wa wabunge watano wa Bunge la Congress la Marekani wakiwa na familia zao, ulipotembelea ofisi za Shirika hilo zilizoko Bahari Beach, jijini Dar es Salaam.

Wabunge hao wa Congress walioambatana na Kaimu Balozi wa nchi hiyo ni pamoja na Carly Paul, Bob Goodlatte, Steve King, Blake Farenthold, Mike Bishop na Sheila Jackson Lee.

 Wabunge hao walijionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na Shirika hilo ikiwemo elimu ya bure kuhusu masuala ya Ukimwi kupitia simu za bure, ujasiriamali na miradi mbalimbali ya kuinua vijana.

Balozi alisema yeye na ujumbe wake wamefurahi kuona kazi kubwa zinazofanywa na Tayoa kwa kushirikiana na taasisi za Marekani kama Kituo cha Kudhibiti Maradhi cha Center for Disease Control (CDC).

“Tumefurahi sana kuona kazi zenu na hasa mnavyowashirikisha vijana katika kujikwamua kiuchumi na kutafuta maendeleo, nawapongeza sana Tayoa kwa kazi kubwa mnayofanya,” alisema

Alisema Tanzania na Marekani zimekuwa na uhusiano mzuri na ushirikiano wa muda mrefu ambao umekuwa ukiimarika mwaka hadi mwaka na kuahidi kuwa serikali hizo mbili zitaendelea kushirikiana.

“Inafurahisha sana kuona vijana ambao wanaelimika kupitia vijana wenzao kama wanavyofanya Tayoa, vijana ambao wako tayari kushirikiana na wenzao kuleta maendeleo yao wenyewe na maendeleo ya taifa lao,” alisema

 Mmoja wa wabunge hao, Sheila Jackson Lee, alisifu ubunifu ulioonyeshwa na shirika hilo katika kutekeleza miradi mbalimbali ukiwemo wa kutoa elimu bure kuhusu ugonjwa wa Ukimwi kupitia simu za bure.

“Mkurugenzi wa Tayoa Peter Masika na Mwenyekiti wa Bodi ya Tayoa Balozi Charles Sanga mmefanyakazi kubwa sana, mmetumia muda wenu mwingi kusaidia maendeleo ya vijana, hii kazi mnayofanya si kwa manufaa ya watanzania tu bali dunia nzima,” alisema mbunge huyo

Alisema Tayoa imekuwa mstari wa mbele kuondoa unyanyapaa kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi hali ambayo imesaidia wengi wao kuishi maisha ya matumaini na kujiona wako sawa na wasio na VVU kwenye jamii wanayoishi.

“Marekani ni rafiki wa Tanzania na itaendelea kuwa rafiki kwa kufanyakazi pamoja kama tunavyofanya sasa kupitia shirika letu la CDC ambalo linasaidia miradi ya afya hapa Tanzania nawapongeza sana Tayoa kwa kazi kubwa mnayofanya kuelimisha kuhusu Ukimwi,” alisema

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Tayoa, Peter Masika, alisema wabunge hao wamekuja kuangalia kazi zinazofanywa na Shirika hilo na namna wanavyotumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) kuelimisha vijana masuala mbalimbali ikiwemo Ukimwi kwa njia ya simu bila malipo.

“Wamefurahia sana kazi tunazofanya kwa mfano kwenye huduma za elimu ya Ukimwi kwa njia ya simu simu ambapo kila siku tunahudumia watu 2,000 na mpaka sasa tumehudumia watanzania milioni tano ambao wamepata taarifa sahihi,” alisema Masika.

POLEPOLE AFANYA MAZUNGUMZO NA KAIMU BALOZI WA MAREKANI HAPA NCHINI TANZANIA, LEO

$
0
0
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Humphrey Poloepole akizungumza na Kaimu Balozi wa Marekani hapa nchini Inmi Petterson, katika ukumbi wa Sekretarieti, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM Lumumba jijini Dar es Salaam, leo, Agosti 21, 2017.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Humphrey Poloepole akilipokuwa akimkaribisha Kaimu Balozi wa Marekani hapa nchini Inmi Petterson, katika ukumbi wa Sekretarieti kwa ajili ya mazungumzo, baada ya kuwasili Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM Lumumba jijini Dar es Salaam, leo, Agosti 21, 2017. Picha zote na Bashir Nkoromo.
PICHA ZAIDI>BOFYA HAPA

Kampuni ya Kansai Plascon Tanzania sasa rasmi Arusha

$
0
0
Arusha: Kampuni ya Kansai Plascon Afrika ltd. Ambayo ni kampuni tanzu ya kampuni ya rangi ya Kansai iliyoko Japan, imehitimisha makubaliano yake ya kununua shughuli za rangi za Sadolin nchini Tanzania na nchi nyingine za Afrika Mashariki.  Hii ilitangazwa na Deodatus Makumpa Meneja wa Kanda ya Kaskazini, Plascon Tanzania wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari katika Hotel ya Arusha Jijini Arusha

Kampuni ya rangi ya Kansai ni kampuni ya kimataifa ambayo inaendesha shughuli zake nchini Japan, China, Mashariki ya Kati, Ulaya na Afrika. Bidhaa zake inazotoa zinajumuisha upambaji, Viwanda, rangi za kulinda na mitambo, ina vituo vya utafiti na maendeleo nchini Japan, India na Afrika Kusuni.

“Tumefurahishwa na mafanikio haya. Kupitia haya, tutaweza kutumia nembo yenye nguvu ya urithi wa Kansai, uwezo wa kimataifa wa kiufundi, na utendaji wa kuaminika, kutupatia uwezo mpya, kuweza kupata teknolojia mpya na utambuzi ambao ni muhimu zaidi katika kuendelea kukuza nembo hii,” alisema Makumpa
 
Akiongea kuhusu sababu za kuinunua, Gary van der Merwe, Rais wa Kampuni ya Plascon Afrika Mashariki alisema kwamba makubaliano haya yanadhihirisha nia ya Kansai Plascon katika kujiendeleza zaidi duniani. “Afrika Mashariki ni moja kati ya ukanda ambao unakuwa haraka zaidi kiuchumi barani Afrika. Kwa ukuaji wa kasi wa daraja la kati, kuongezeka kwa nguvu ya utumiaji na kukua kwa miji, huu ni muda muafaka wa kuingiza sokoni bidhaa zetu mbali mbali kwaajili ya kuboresha zaidi mtindo wa maisha yao wakati huo huo tukiwa tunaongeza kuenea kwetu duniani”.

MCHENGA BBALL STARS YAFUFUA MATUAMINI YA UBINGWA SPRITE BBALL KINGS

$
0
0
Nahodha wa Mchenga BBall Stars Mohamed Yusuph akitaka kumtoka nahodha wa kutoka TMT, Isihaka Maoud katika mchezo wa fainali ya tatu ya Michuano ya Sprite BBall Kings uliomalizika kwa Mchenga kushinda kwa lama 87-82 dhidi ya TMTmchezo uliochezwa katika Viwanja vya Don Bosco OysterbayJijini Dar es Salaam.


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Mchezo wa tatu wa Fainali ya michuano ya mpira wa Kikapu ya Sprite BBall Kings imeendelea mwishoni mwa wiki kwa timu ya TMT kukubali kipigo cha pili kutoka kwa wapinzani wao Mchenga BBall Stars wakilipa kisasi kwa alama 87-82 dhidi ya TMTmchezo uliochezwa katika Viwanja vya Don Bosco OysterbayJijini Dar es Salaam.

Katika mchezo wa fainali ya kwanza, Mchenga walifanikiwa kutoka na ushindi wa alama 101-70 vya TMT, lakini fainali ya pili TMT waliweza kujibu mapigo na kuwaadhibu mahasimu wao kwa alama 82-78 dhidi ya Mchenga. 

Kwenye mchezo huo, Mchenga walianza kwa taratibu huku TMT walionekana wako vizuri sana katiia idara zote ikiwemo ulinzi na ushambuliaji lakini mpaka robo ya kwanza inamalizika Mchenga walikuwa wanaongoza ila katika robo ya nne na ya mwisho umakini wa TMT uliweza kuwafanya waanze kutawala mchezo huo na kuepelekea Mchenga kupata ushindi katika sekunde za mwisho wa mchezo huo. 

Kutokana na matokeo hayo timu ya Mchenga BBall Stars imeweza kurudisha furaha kwa mashabiki zao baada ya kupoteza mechi iliyopita katika fainali hizi za Sprite BBall Kings kwa kuchapwa kwa pointi 87-78 na mpinzani wake TMT.

Pamoja na hayo, mechi ya leo iliweza kuonyesha utofauti mkubwa katika mechi zote zilizowahi kuchezwa katika michuano hii, kutokana na wachezaji wa pande zote mbili kuonyesha umahili wao waliyokuwa nao katika kucheza pamoja na kushambulia. 
Mamia ya mashabiki waliyoweza kujitokeza kutazama mtanange wa fainali za Sprite BBall Kings leo Don Bosco Oysterbay 

Kwa upande mwingine, mchezaji Erick Lugora kutoka TMT ameweza kuibuka 'best scorer' kwa pointi 23 akifuatiwa na Marcelo Nyirabu kutoka Mchenga BBall Stars kwa kupata pointi 18 katika mechi ya tatu ya fainali za Sprite BBall Kings. 

Mchenga na TMT zitakutana tena Agosti 23 (Jumatano) ya mwaka huu kucheza game 4 ambapo mchezo huo kwa upande mmoja utaweza kuwa wa mwisho endapo Mchenga BBall Stars akiweza kufunga tena na bingwa wa Michuano ya Sprite BBall Kings 2017 atajinyakulia kitita cha shilimgi Milioni 10 huku mshindi wa pili akipata Milioni 3 na mchezaji bora wa michuano hiyo (MVP) akizawadiwa milioni 2.

Michuano ya Sprite BBall Kings ilianza mapema Mwezi Mei na iliweza kusaili timu 56 na kuanza hatua za mtoano mwezi June katika Viwanja mbalimbali na imechukua takribani miezi mitatu kufikia Fainali, kwa mujibu wa waandaaji michuano hii itakuwa ni endelevu na wanatarajia mwakani kupata timu nyingi zaidi zitakazoshiriki. 
Patashika uwanjani.
Mtanzania anayecheza mpira wa kikapu Nchini Marekani Hasheem Thabeet alikuwa moja ya watazamanji katika Viwanja vya Don Bosco OysterbaY.

Timu ya Polisi Tanzania Yapokea Msaada wa Vifaa vya Michezo Toka NMB

$
0
0
Meneja Mwandamizi Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya NMB, Ally Ngingite (kushoto) akizungumza kabla ya kukabidhi vifaa mbalimbali vya mchezo wa mpira wa miguu kwa ajili ya Timu ya Polisi Tanzania inayoshiriki Ligi Daraja la Kanza Tanzania Bara. Wengine kushoto kwake ni maofisa waandamizi wa Jeshi la Polisi Tanzania walioshiriki kupokea vifaa hivyo vya msaada
IMG_6477
Meneja Mwandamizi Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya NMB, Ally Ngingite (kushoto) akizungumza kabla ya kukabidhi vifaa mbalimbali vya mchezo wa mpira wa miguu kwa Timu ya Polisi Tanzania inayotarajia kushiriki Ligi Daraja la Kanza Tanzania Bara. Kulia ni Naibu Kamishna wa Polisi, Ahmada Khamis wakishuhudia tukio hilo.
IMG_6487
Meneja Mwandamizi Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya NMB, Ally Ngingite (kushoto) akimkabidhi baadhi ya vifaa vya michezo Naibu Kamishna wa Polisi, Adrian Magayane (kulia) vilivyotolewa na NMB kwa ajili ya Timu ya Polisi Tanzania inayoshiriki Ligi Daraja la Kanza Tanzania Bara. Wengine katikati kutoka kushoto ni Kaimu Afisa Mwandamizi Amana, Huduma za Bima na Huduma za Ziada wa NMB, Stephen Adili na Naibu Kamishna wa Polisi, Ahmada Khamis wakishuhudia tukio hilo.
IMG_6515
Baadhi ya maofisa wa Benki ya NMB (kushoto) pamoja na wa Jeshi la Polisi Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya zoezi la kukabidhi vifaa hivyo lililofanyika leo jijini Dar es Salaam, Makao Makuu ya Benki ya NMB. Vifaa hivyo vimetolewa na NMB kwa ajili ya Timu ya Polisi Tanzania inayoshiriki Ligi Daraja la Kanza Tanzania Bara. 
IMG_6468
Sehemu ya Maofisa wa Jeshi la Polisi Tanzania wakiwa katika hafla ya makabidhiano ya vifaa hivyo.
…………………….

Na Mwandishi Wetu
BENKI ya NMB imekabidhi msaada wa vifaa mbalimbali vya mchezo kwa Timu ya Mpira wa Miguu ya Jeshi la Polisi Tanzania inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara. 
Vifaa hivyo ni pamoja na mipira, mabegi ya wachezaji, viatu, tracksuit na jezi mbalimbali vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 13, vilikabidhiwa kwa jeshi la polisi na Meneja Mwandamizi wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa NMB – Ally Ngingite kwa Kamishna wa Polisi – Adrian Magayane.
Akizungumza kabla ya kukabidhi vifaa hivyo jana jijini Dar es Salaam, bwana Ngingite alisema NMB inaamini msaada huo kwa Timu ya Jeshi la Polisi utakuwa chachu ya kufanya vizuri zaidi katika michuano mbalimbali iliyopo mbele yao hususani Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara inayotarajia kuanza hivi karibuni.
“Vifaa tunavyokabidhi leo ni pamoja na jezi, track suti, mabegi, mipira, viatu vya kuchezea na vifaa vingine vingi vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 13,” alisema bwana Ngingite
Msaada huo kwa timu ya jeshi la polisi ni mwendelezo wa kusaidia kukuza sekta ya michezo nchini huku benki hiyo ikijinasibu kuwa imekuwa mshirika mkubwa sana katima maendeleo ya michezo nchini. Mbali na kuisaidia timu ya polisi, NMB pia inaidhamini timu ya Azam MC ya Ligi Kuu Tanzania Bara na imekuwa ikisaidia timu mbalimbali kuendeleza michezo.
Bwana Ngingite alizitaja timu nyingine ambazo NMB imetia Mkono wake hapa nchini ni pamoja na clabu ya Gofu ya Lugalo, Singida United na Clabu ya jeshi ya Gymkana.
Akiongea baada ya kupokea vifaa hivyo, Kamisha wa Polisi – Adrian Magayane alishukuru kwa msaada na kusema kuwa utaongeza chachu ya ushindi na kuhakikisha kuwa wanatinga ligi kuu msimu ujao.
“Tunawashukuru sana NMB, benki hii imekuwa mshirika wetu mkubwa sana katika nyanja mbalimbali, tunaimani tutabeba nembo yao vizuri kwa kufanya vyema kwenye mashindano ya ligi daraja la kwanza.” Alisema Kamishna Magayane.

UBER YAZINDUA HUDUMA YA MADEREVA NA WASAFIRI KUCHATI KWA KUTUMIA PROGRAMU HIYO

$
0
0




Dar es Salaam Tarehe 21 Agosti 2017…Kampuni ya Uber nchini Tanzania imetangaza zana mpya maarufu kama “Kuchati Ndani ya Programu” inayowawezesha madereva na wasafiri kuandikiana ujumbe kwa kutumia programu hiyo bila malipo.


Kinyume na hapo awali ambapo madereva na wasafiri wangetumia Ujumbe Mfupi (SMS) au kupiga simu, zana hii inaleta unafuu kwa madereva na wasafiri hivyo basi kuwapunguzia kadhia ya gharama za kupiga simu sambamba na kuharakisha mawasiliano bila kuondoka kwenye programu ya Uber.


Maboresho haya ni juhudi endelevu za Uber na yanalenga kuimarisha wigo wa wasafiri na madereva wanapotumia programu ya Uber.


Zana hii mpya ni rahisi sana kuitumia. Msafiri anapoita gari, kuna kitufe cha ‘Kuwasiliana’ kwenye menyu inayoonekana chini ya skrini. Wasafiri wanaweza kuwaandikia ujumbe madereva, na madereva vivyo hivyo. Ujumbe utaonesha kwamba umepokelewa baada ya kuutuma.


Kwa upande mwingine, madereva watakiri kwamba wamesoma ujumbe kwa kugusa kwenye programu ya Uber ili watume ujumbe wa ‘bomba’. Ili wasijichanganye barabarani. Aidha wasafiri na madereva wanaweza kuona kama ujumbe wao waliotuma umesomwa.


Meneja Msimamizi wa Uber nchini Tanzania Bw. Alfred Msemo amehoji kwamba, “Kila safari nzuri huanza pale msafiri anapochukuliwa kwa gari, kwa hiyo tunajituma kutafuta mbinu za kumchukua msafiri bila usumbufu wowote kwa msafiri au dereva. Kipengele hiki cha Kuchati kitakuwa afueni kwa wasafiri na madereva wanapotaka kuwasiliana ili kusaidiana kutafuta mwafaka wa changamoto za safari kama vile, kufungwa kwa barabara au kutoa maelezo ya mahali walipo.”


Kadhalika, kipengele hiki kinatoa njia mbadala ya wasafiri na madereva kupiga simu wanapotaka kuwasiliana. Hata hivyo, ili mtu atumie kipengele hiki anatakiwa awe anatumia toleo la sasa la program ya Uber.

               


“Huu ni mwanzo tu wa mchakato wa kuimarisha huduma za kutuma ujumbe moja kwa moja kwenye programu ili kufanikisha wigo wa mawasiliano yasiyo na changamoto kwa wateja wetu, na kuwasaidia kuwasiliana katika ulimwengu wa utandawazi na ulimwengu halisi” amenukuliwa Bw. Msemo.


WANAKIJIJI WA UFYAMBE WALIVYOJIKWAMUA NA KERO YA UMBALI WA ZAHANATI KWA KUANZA UJENZI WA ZAHANATI YA KIJIJI.

Waziri wa Nchi anayeshugulikia Masuala ya Afrika wa Uingereza kuzuru Tanzania Agosti 22 na 23, 2017

$
0
0

Waziri wa Nchi anayeshughulikia Masuala ya Afrika kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Uingereza, Mhe. Stewart Rory atafanya ziara ya kikazi ya siku mbili nchini tarehe 22 na 23 Agosti 2017. 

Mhe. Rory anakuja nchini kwa madhumuni ya kutembelea miradi mbalimbali inayofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Uingereza (Department for International Development – DFID).

Aidha, wakati wa ziara hiyo, Mhe. Waziri Rory amepangiwa miadi ya kuonana na Viongozi wa Serikali akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb).

Baadhi ya miradi ambayo, Mhe. Waziri ataitembelea ni upanuzi wa Bandari ya Dar Es Salaam, Shule ya Msingi Mkoani, Bonde la Mto Msimbazi, Kiwanda cha Nguo cha Tooku kilichopo katika Eneo la Viwanda la Benjamin Mkapa, Mabibo jijini Dar es Salaam na kampuni ya Songas. 

Waziri Rory pia anatarajiwa kushiriki chakula cha mchana na vijana wa Kitanzania katika moja ya migahawa `ya kawaida katika mitaa ya jiji la Dar Es Salaam

Baada ya kukamilisha ziara yake, Waziri Rory ataondoka nchini tarehe 23 Agosti 2017 kurejea London. 


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, 

Dar es Salaam, 21 Agosti 2017

CHAKUA YAOMBA UCHANGIAJI WA SH.200 KWA ABIRIA WANAOSAFIRI KWENDA MIKOANI.

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
CHAMA cha Kutetea Abiria (Chakua) kimewaomba abiria wanaongia katika kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani  cha ubungo kutoa sh. 200 kwa ajili ya kusaidia chama hicho.

Akizungumza na waandishi habari jijini Dar es Salaam,Mratibu wa chama hicho, Monday Likwepa amesema kuwa chama kimekuwa na msaada mkubwa kwa abiria hivyo chama kinahitaji kujiendesha na wadau ni abiria kuchangia kiwango hicho.

Amesema kuwa kiwango hicho  walichopanga kitasaidia kuendesha shughuli za ofisi pamoja na kuweza kushughulika na matatizo ya abiria pale wanapopata usafiri.

Likwepa amesema kuwa abiria wamekuwa wakipata matatizo na kukimbilia chakua hivyo kwa utaratibu wa kuchangia wanawajibu kudai haki zao pale wanapopata usumbufu.

Aidha amesema kuwa wataendelea kutoa elimu zaidi juu ya uchangiaji wa fedha hiyo katika kituo cha ubungo ili wananchi wajue  uchangiaji huo na pamoja na faida zake.
Mratibu Mtendaji wa Chama  Cha Kutetea Abiria(Chakua), Monday Likwepa akizungumza na waandishi wa habari juu ya kuchangia abiria  wanaosafiri katika kituo kikuu cha mabasi Ubungo sh.200 kwa ajili kuendesha shughuli za utetezi wa abiria pale anapopatwa na tatizo. Kushoto ni Mratibu mtendaji wa Chakua, Elias Kalinga na kulia ni Mwenyekit wa wa Taifa wa Chakua, Hassan Mchanjawa.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.

KERO YA MAJI MAHABUSU YA WATOTO YAMALIZWA NA KANISA KATOLIKI.

$
0
0

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu (kushoto) akifungua bomba kuashiria kupokea kisima toka kwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo kulia.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo (katikati) akisisitiza jambo kwa wageni waalikwa wakati akikabidhi kisima kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (Kushoto)  kwa ajili ya mahabusu ya watoto mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kulia ni Padre Timotheo Maganga Mkurugenzi wa Mashirika ya Kipapa Dar es Salaam.
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee  na Watoto, Ummy Mwalimu (kushoto) akisisitiza jambo kwa wageni waalikwa (hawapo pichani) wakati akipokea kisima toka kwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo (katikati) kulia ni Padre Timotheo Maganga.
 Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo (kulia) akikata utepe kuzindua kisma cha maji mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (kushoto) akisisitiza jambo kwa wageni waalikwa wakati akipokea kisima toka kwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo Mkuu (katikati) kulia ni Padre Timotheo Maganga
Picha na Eliphace Marwa - Maelezo.

Na Agness Moshi na Anthony Ishengoma- Maelezo.
Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam leo limekabidhi Kisima chenye thamani ya  Shilingi Milioni kumi na moja laki saba na themanini (Sh. 11,780,000/=) kwa Serikali ili kutatua tatizo la maji katika Mahabusu ya Watoto iliyoko Upanga jijini Dar es Salaam.

Akiongea katika hafla ya makabidhiano ya Kisima hicho Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo amesema lengo kuu la Mchango wa Kanisa katika ujenzi wa Kisima hicho ni kuonesha kuwa Kanisa haliko mbali na Serikali katika shughuli mbalimbali za ujenzi wa Taifa.

Alisema  Kanisa Katolitiki Tanzania linashirikiana na serikali katika juhudi zake za kuwaletea wananchi maendeleo bila kujali itikadi za kidini chama au kikabila ili kusudi wanapotoka kwenye vituo hivyo watambue wamesaidiwa  kutokana na mapenzi mema ya kanisa hilo kwa watu wote.

Naye Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu  amesema ujenzi wa kisima hicho umesaidia serikali kupunguza gharama ya kulipia bili ya maji ambayo kwa mwezi mmoja serikali ilikuwa inalipa Shilingi laki nne kwa ajili ya matumizi ya maji katika mahabusu hiyo.

 Waziri Ummy amesema kutokana na ujenzi wa kisima hicho tatizo la maji limekwisha kwa asilimia  mia moja kwasababu kisima hicho kina uwezo wa kuzalisha lita 5,000 kwa saa.

Aidha amesema kuwa fedha ambazo zimeokolewa na ujenzi wa kisima hicho zitatumika kwa ajili ya kuwakatia Bima ya Afya Watoto wanaozuiliwa katika vituo hivyo ili kuwahakikishia upatikanaji wa matibabu.

Amesema ni muhimu kwa jamii  kufahamu kuwa  ni Mahakama tu  ndio yenye uwezo wa kutoa amri ya watoto kuhifadhiwa katika  mahabusu  hiyo na sio mtu au chombo chochote kingine.

Waziri Ummy alimwambia Kardinali Pengo kuwa hapa nchini kuna Mahabusu 5 ambazo ni Mahabusu ya Watoto Dar es Salaam (Upanga), Mahabusu ya Watoto Tanga, Mahabusu ya Watoto Moshi, Mahabusu ya Watoto Arusha na Mahabusu ya watoto Mbeya.

Amezitaja huduma  zinazotolewa na Wizara yake kwa watoto walioko kwenye Mahabusu hizo kuwa ziko za aina tatu  ambazo ni uhifadhi na utunzaji wa  watoto, huduma za maadilisho kwa watoto ambao tayari Mahakama imewahukumu, na huduma za Kijamii za Marekebisho ya tabia kwa watoto waliokinzana na Sheria.

Wakati huo Mkurugenzi wa Mashirika ya Kipapa Kwa Mkoa wa Dar es Salaam ambaye pia ni  Mwakilishi wa watoto na vijana wainjilishaji mtandaoni Padre Thimotheo Nyasulu  amesema kuwa, wameamua kutoa msaada huo baada ya kuona changamoto hiyo walipotembelea kituo hicho Desemba ,2016 kama sehemu ya matendo ya huruma kwa kanisa.

Aidha Padre Nyasulu ametoa rai kwa Wananchi na waandishi wa habari kutoendelea kuita vituo vya watoto waliokinzana na Sheria Mahabusu na kushauri viitwe vituo vya malezi kwasababu hali hiyo inawafanya kujiona wametengwa hali inayowaongezea adhabu.

Waziri Ummy   alisema Mahabusu  za watoto ni  moja kati ya huduma  kongwe hapa nchini mahususi  kwa  kuwahifadhi watoto walio kinzana na Sheria na ambao kwa sababu moja au nyingine hawakuweza kupata dhamana kwa kesi au  mashauri ambayo yanawakabili  Mahakamani.

RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA RAIS WA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA MAENDELEO LA JAPAN (JICA) IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea jambo  na  Rais wa shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) Bw. Shinichi Kitaoka aliyekutana na kufanya mazungumzo naye leo agosti 21, 2017 Ikulu jijini Dar es salaam.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo  na Rais wa shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) Bw. Shinichi Kitaoka (kushoto) na Balozi wa Japan nchini Mhe. Masaharu Yoshida leo agosti 21, 2017 Ikulu jijini Dar es salaam.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtambulisha Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Joseph Nyamhanga na Mtendaji Mkuu wa Tanroads Mhandisi Patrick Mfugale kwa Rais wa shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) Bw. Shinichi Kitaoka aliyekutana naye leo agosti 21, 2017 Ikulu jijini Dar es salaam.

Viewing all 46329 articles
Browse latest View live




Latest Images