Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live

HAKUNA VIBALI KWA AJILI YA KUUZA SHEHENA YA VIROBA ILIYOBAKI- MAKAMBA

$
0
0

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mh. January Makamba amesema kuwa Serikali haina mpango wa kutoa vibali kwa ajili ya kuuza shehena ya kinywaji aina ya viroba vilivyopo stoo kwenye maghala ya Wafanyabiashara wa pombe hiyo.

Aliongea hayo jijini Dar es Salaam alipofanya ziara ya kushtukiza katika ghala la kampuni ya usambazaji wa vinywaji aina ya kiroba ya Temani iliyopo Kimara Temboni jijini Dar es Salaam.

Aliongeza kuwa Serikali ilitoa muda mrefu kuanzia mei 2016 mpaka machi 2017 kwa wenye shehena hiyo ya viroba kuuza na kumaliza mzigo wote uliopo stoo hivyo basi baada ya Serikali kupiga marufuku pombe hiyo, hakuna kibali kitakachotolewa kwa ajili ya kuuza shehena ya mzigo wa viroba uliobaki. 

Akiongea kwa Mh. Waziri , Mkurugenzi wa kampuni hiyo Bi Elizabeth Massawe alisema wanaiomba Serikali iwasaidie ili waweze kupunguza mzigo mkubwa wa viroba ambao wanao katika ghala lao sababu wanapata hasara kubwa na wanatakiwa kulipia kodi ya magahala waliyokodi. .

Katika ziara hiyo ya kutembelea ghala la vinywaji la kampuni ya Tema Enterprise Waziri alikuta shehena kubwa ya katoni 150,000 za viroba zilizofungashiwa katika vifuko vya plastiki.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mh. January Makamba akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Temani ambayo wana ghala la kuhifadhia vinywaji aina ya viroba lililoko Kimara Temboni Bibi Elizabeth Massawe (wa kwanza kushoto) wakati wa ziara yake ya kutembelea ghala hilo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mh. January Makamba akiongea na Waandishi wa Habari mara baada ya kumaliza ziara yake ya kutembelea ghala la kuhifadhia vinywaji la Kampuni ya Temani lililopo Kimara Temboni.
Sehemu ya vinywaji aina ya viroba na vifungashio vilivyopo katika ghala la kuhifadhia vinywaji la Kampuni ya Temani.

ANNA ABDALLAH AWAPONGEZA GIRL GUIDES KWA KUIWAKILISHA VIZURI TANZANIA NJE YA NCHI

$
0
0
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha  Tanzania Girl Guides (TGGA), Anna Abdallah (katikati) akiwa na Girl Guides waliorejea nchini kutoka kwenye programu ya Yess ya kubadilishana uzoefu katika masuala ya uongozi, utamaduni na maadili  katika nchi za Uganda, Madagascar,  Zimbabwe na Zambia. 

Hapo ilikuwa wakati wa hafla maalumu iliyoandaliwa na TGGA  Dar es Salaam kwa ajili ya kuwapongeza na kupata mrejesho wa walichojifunza walipokuwa kwenye programu hiyo inayodhaminiwa na Norwey.Anna Abdallah aliwapongeza wasichana hao wanne kwa kuiwakilisha vizuri TGGA  na Tanzania katika programu hiyo nje ya nchi.

Kutoka kulia ni Ummy Mwabondo alikwenda Zambia, Farida Mjoge aliyekuwa Uganda,  Elizabeth Betha (Madagascar) na Edna Chembele (Zimbabwe)
 Girl Guides hao wakipata msosi wakati wahafla ya chakula cha usiku iliyoandaliwa kwa ajili yao kwenye Hoteli ya Golden Tulip, Oysterbay, Dar es Salaam.
 Anna Abdallah akiotoa nasaha na pongezi kwa Girl Guides kwa kuiwakilisha vizuri TGGA NA Tganzania kwa ujumla, ambapo aliwataka watumie mafunzo waliyoyapata kwa kutoa mafunzo kwa wasichana wenzao nchini.
 Wakiwa na furahani Kamishna Mkuu wa TGGA, Symphorosa Hangi (kushoto), Anna Abdallah (katikati) na Mjumbe wa TGGA, Agnes Makenya
 Katibu Mkuu wa TGGA Tanzania, Grace Shaba akitoa neno la ukaribisho muda mfupi kabla ya Girl Guides waliorejea nchini kutoka nje ya nchi kwenye programu hiyo kuelezea mambo mbalimbali waliyoyafanya na kujifunza
 Grace Shaba akiwatambulisha Girl Guides hao
 i Ummy Mwabondo akielezea kwa njia ya picha kazi mbalimbali alizokuwa anazifanya alipokuwa Zambia
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala, ambaye ni Mjumbe wa  Bodi ya TGGA, Sophia Mjema akitoa ufafanuzi wakati Girl Guides wakielezea mafanikio na changamoto ya mafunzo yao nje ya nchi
 Girl Guides Farida akielezea mambo mbalimbali aliyoyafanya akiwa Uganda kwa muda wa miezi sita.
 Viongozi na wageni waalikwa wakionesha ishara ya TGGA
 Viongozi wa Girl Guides Makao Makuu ya TGGA wakiwa na furaha wakati wa hafla hiyo
 Kamishna Mkuu wa TGGA, Symphorosa Hangi (kushoto), akiwa na Kamishna wa Kimataifa wa TGGA wakijadili jambo
 Sasa ni wakati wa msosi








 Mwenyekiti wa TGGA, Profesa Martha Qorro akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Bodi ya TGGA, Anna Abdala kuzungumza katika hafla hiyo.
 Mwakilishi wa wazazi wa Girl Guides hao, Florence Gondwe akitoa shukrani kwa TGGA kwa kuwapatia wasichana hao fursa ya kwenda nje ya nchi kwenye programu hiyo ambayo alidai itawasaidia sana kimaisha.
 Kamishna Hangi akitoa neno la shukrani kwa viongozi waliohudhuria hafla hiyo pamoja na Girl Guides
 Wakiwa katika picha ya pamoja

Anna Abdallah akiagana na Girl Guides baada ya hafla kumalizika

TUFANYE HAYA KULETA MAPINDUZI YA SOKA TANZANIA

$
0
0

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Soka la nchi yetu linaenda 'halijojo' halina mtiririko wenye mwendelezo makini.Tangu kuanzishwa kwa Taifa hili ni Mara moja tu nchi yetu ilishiriki michuano mikubwa kwa ngazi ya Afrika yaani Afcon.


Ilikua mwaka 1980 ambao tulinyanyaswa sana katika uwanja wa Sululele pale Nigeria. Sululele ndio mtaa aliozaliwa msanii nguli wa Nigeria Wizkid,na anatanbulika kama mfalme wa Sululele.

Vizazi Vingi vimepita tangu mwaka 1980 hadi sasa. Na imekua kama ni suala la kawaida kila nyakati zimekuwa zikilalamikiwa. Na nyakati zikipita waliolalamikiwa kwa viwango vyao nao wanawalalamikia wale wanaocheza kwa wakati ambao waliolalamikiwa hawachezi.

Imekua kama mbio za 'relay' kila mlalamikiwa muda ukimwacha nae husubili wa kumlalamikia. Leo twaweza kuwa na kiwango kizuri tikaridhisha mashabiki lakini kesho tunakuwa kawaida.

TUFANYE HAYA KUNUSURU SOKA LETU.

Katika masuala ya utafiti kuna jambo linaitwa kukusanya taarifa za jambo la utafiti.Pia unatakiwa kufanya mapitio ya maandishi ili kujua tatizo uchunguzalo kama limewahi kuchunguzwa. Baada ya kuchunguza unatazama kufanikiwa au kutofanikiwa kwa utafiti huo.

Katika soka tinapaswa kutumia utafiti wa wenzetu walioporomoka kisoka na wakarudi vyema. Iko mifano mingi lakini tuwatazame Wajerumani na Wabelgiji.

Katika nchi ya Ujerumani baada ya kufanya vibaya katika michuano ya Ulaya mwaka 2000 walirudi katika vitalu 'grassroots' vya soka.

Wataalamu elfu moja walisambazwa nchi nzima kutafuta vipaji vya soka. Wataalamu hao wenye elimu ya ukocha waliingia miji mbali na maeneo ya chini kabisa kufanya kazi hiyo.

Maamuzi ya kuingia vitaluni kusaka vipaji ilitokana na jicho lao kuona hawana ubabe tena Ulaya.Maeneo ya Gelsenkirchen, Bremen, Colony, Munich,Hamburg, Wolfsburg, Frankfurt,Stuttgart yalifikiwa na wataalamu hao.

Uhai wa Ujerumani ulibaki katika vilabu vyao ambapo Mwaka 2001 Bayern Munich walichukua kikombe cha ubingwa wa Ulaya. Mwaka uliofuata klabu ya Bayer Leverkusen walicheza fainali dhidi ya Rael Madrid. Mwaka 2002 wakapoteza fainali dhidi ya Brazili pale Yokohama.

Nyakati hizo zote vijana kumi na mbili toka kwa wataalamu elfu moja walikua wamesambazwa katika vituo vya soka vya vilabu vyote. Ilikua ni mkakati ambao Chama cha soka na wanachama wake yaani vilabu vilikubaliana katika harakati hizo hivyo walilea vijana hao.

Mwaka 2006 walirejea kombe la dunia na kupata kichapo toka kwa Italia katika Nusu fainali palepale nyumbani kwao. Wajerumani walitawanywa akili na magoli ya Simeon Perotta na Alessandro Del Piero.

Wakiwa na vipaji katika vitalu wakaanza kuvichimoa mwaka 2008 katika Euro waliyokuja kupoteza fainali dhidi ya Hispania. Ilikua ni mwanga kwao Kwani 2010 wakavitoa vipaji hivyo na kuvitumia kombe la dunia pale Afrika kusini.

Ilikuwa ni kizazi cha akina Mesut Ozil,Thomas Muller,Manuel Nueur,Jerome Boateng,Sam Khedira,Matt Hummels, na wengineo. Hawa ndo ambao walipatikana vitaluni mwaka 2000.

Matunda ya vitalu vya mwaka 2000 vilikuja kuleta katika fainali ya kombe la dunia 2014.Huu unaitwa uthubutu. 

Ubelgiji nao kwa miaka ya hivi karibuni tumewaona wakibembea sana katika nafasi ya kwanza ya viwango vya soka. Mwaka 2013 na 2014 ilikua viwango vikitolewa basi Ubelgiji inaongoza.

Haikua kazi rahisi kwao lakini walichokifanya hakina tofauti na majirani zao wajerumani. Wao ubelgiji waliwatawanya makocha wakasome ukocha nje ya Ubelgiji. Hivyo wataalamu hao walisambaa Ujerumani na Uholanzi na wakarudi na maarifa ya kutosha nyumbani.

Makocha wale ndio waliosambazwa katika vilabu kama wasaidizi na wengine timu za taifa za vijana. Maarifa waliyoyatumia kwa vipaji vyao yalikuwa yanaleta matunda. 

Wabelgiji pia waliamua kuwatumia Walimu wa shule kupewa mafunzo ya uamuzi wa soka. Imani yao ilikuwa kumfundisha mwalimu wa shule ni rahisi na atashikilia maadili.Mbinu hii imeigwa na hata Cameron. Wanawatumia waamuzi ambao kwa asilimia kubwa ni wenye maadili mazuri.Hoja ya maadili inakuja kwa lengo la kutotaka kutokea kwa masuala ya rushwa. Pia inashauriwa lazima mwamuzi awe na shughuli inayomwingizia kipato.

Mikakati hiyo ilikuja kuwaleta akina Romelu Lukaku Bolingoli,Eden na Thorgan Hazard,Radja Nainggolani, Christian Benteke,Vincent Kompany na wengineo.

TUNAIGA LIPI ILI KUFANIKIWA KAMA TAIFA.

Shirikisho kwa kushirikiana na serikali pamoja na wadau tunapaswa kuiga haya.Kwanza tukubali kuanza upya sio vibaya katika kutaka kufikia malengo.

Tunatakiwa kuiga mfumo wa Ubelgiji kwa waamuzi hivyo chama cha soka kwa kushirikiana na Chama cha waamuzi na serikali kupitia idara ya maendeleo ya michezo iliyo chini ya Yusuph Omary Sengi wachuke walimu na kuwapa mafunzo.

Walimu hawa watakuja kutuelea matunda kutokana na kuwa na maadili ya kiutumishi ambayo wameyaapia katika utendaji wao. Kufanya hivyo kutatuletea waamuzi ambao hawatalalamikiwa kama ilivyo sasa.

Pili tunatakiwa kushirikiana na serikali pamoja na vyama vya soka vya Mkoa kufanya haya. Serikali ya Mkoa ielekeze chama cha soka kupitia kwa maafisa michezo kutafuta maeneo ambayo watajenga vituo vya soka kutokana na mapato ya chama husika. Mfano katika mapato ya michezo kile kinachwa katika klabu kitumike kujengea vituo kwa kutafuta hata msaada kwa wadau ili kufanikisha.

Baada ya kupatikana kwa vituo hivyo vitafutwe vipaji kwa kufanyiwa mchujo na baadae wale wanaofanikiwa waweze kulipiwa na wazazi wao karo ya kulelewa kisoka katika vituo. Na hata kama wako wanaosoma basi watahamishiwa shule katika maeneo ya jirani na kituo.

Upatikanaji na namana ya kutunza vipaji hivyo ni tofauti na ilivyokua kwa Taifa stars Maboresho. Baada ya hapo timu ya taifa ya vijana itapatikana kwa urahisi kama Mkurugenzi wa michezo atafanya kazi bega kwa begani na wasimamizi wa vituo hivyo.

Kufanyika kwa mashindano ya vituo vya soka ni moja ya sehemu ya kujua vipaji vilivyopo katika vituo. Kama sio kutilia mkazo kwa kuwasaidia vijana kufanikiwa kupata hata timu za kuchezea. Kuwatelekeza wakiwa hawajui wapi kwa kwenda ni kitu kibaya ambacho kimezoeleka kufanyika kwetu.

Kama tutakuwa watu tunaolipuuzia soka la vijana haitashangaza Somalia wanashiriki Afcon sisi tukiendelea na singeli zetu.Kujidhatiti ni jambo bora sana ambalo tunalikosa na tunahitaji kupata mafanikio ya zaidi ya sasa kwa vijana wetu.

Kwa upende wa uongozi wa shirikisho uwe wa Sera ya kusaidia wachezaji wanaopata vilabu nje ya nchi. Mfano suala la Abdi banda lingeweza kutatuliwa haraka na shirikisho kwa kusaidia kumwandikia barua Banda huku ikiambatanishwa na nakala ya mkataba wa Simba ambao ulikuwa Tff ili kuwajulisha klabu ya Baroka fc kuwa yuko huru.

Shirikisho la soka la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo liliwahi kuingia katika mtindo huu. Ilikua ni kutaka kuwasukuma wachezaji wakacheze soka nje ya Kongo. Harakati hizo ndizo tulizokuja kuwaona wachezaji kama Romana LuaLua aliyekipiga klabu kama Portsmouth. Hii ilikua baada ya kuona fedheha iliyowakuta Kongo baada ya kuweka rekodi katika vitabu vya michezo kuwa ni timu iliyowahi kufungwa goli nyingi kombe la dunia.

Harakati hizo za kuwatafutia vilabu nje ya Kongo ilikua baada ya rekodi ya kichapo cha goli Tisa kwa bila toka kwa Yugoslavia.Kama vichapo vikubwa tumeshafungwa sana kama timu ya Taifa. Kila Mdau anakumbuka kichapo toka kwa Algeria cha goli saba tukafananishwa na mataifa kama Djibouti.

Kuanza upya sio vibaya la msingi ni kutambua malengo yetu ni nini katika soka.

KAMATI YA OLIMPIKI TANZANIA YATOA MAFUNZO YA UTAWALA NA UONGOZI WA MICHEZO SIMIYU

$
0
0
  Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe.Benson Kilangi(katikati) akizungumza na washiriki wa Mafunzo ya Utawala na Uongozi wa Michezo yaliyoandaliwa na Kamati ya Olimpiki Tanzania(TOC) wakati alipofungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka Mjini Bariadi.
  Mkurugenzi Mkuu wa Mafunzo ya Utawala na Uongozi wa Michezo kutoka Kamati ya Olimpiki Tanzania(TOC) Ndg.Suleiman Jabir akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo kutoka mkoani Simiyu (hawapo pichani) ambayo yanafanyikwa kwa muda wa siku tano Mjini Bariadi.
 Afisa Michezo wa Mkoa wa Simiyu,Ndg.Addo Komba (kushoto) akizungumza katika mafunzo ya Utawala na Uongozi wa Michezo kwa maafisa michezo, viongozi wa vyama vya michezo na walimu wa michezo yaliyoandaliwa na Kamati ya Olimpiki Tanzania(TOC).
 Baadhi ya washiriki wa Mafunzo ya Utawala na Uongozi wa Michezo yaliyoandaliwa na Kamati ya Olimpiki Tanzania(TOC) wakifuatilia Hotuba ya Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe.Benson Kilangi(hayupo pichani) wakati akifungua mafunzo hayo kwaniaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka mjini Bariadi.
 Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe.Benson Kilangi(wa tatu kulia walioketi) katika picha ya pamoja na maafisa michezo, viongozi wa vyama vya michezo na walimu wa michezo wa Mkoa wa Simiyu, wanaoshiriki wa Mafunzo ya Utawala na Uongozi wa Michezo mjini Bariadi ambayo yameandaliwa na Kamati ya Olimpiki Tanzania(TOC); (wa pili kulia) Mkurugenzi Mkuu wa Mafunzo Ndg.Suleiman Jabir
Mkurugenzi Mkuu wa Mafunzo ya Ndg.Suleiman Jabir Utawala na Uongozi wa Michezo kutoka Kamati ya Olimpiki Tanzania(TOC)(kulia) akimkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Itilima, mhe.Benson Kilangi ambaye amefungua mafunzo hayo mjini Bariadi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, MheAnthony Mtaka.

Na Stella Kalinga, Simiyu
Kamati ya Olimpiki Tanzania(TOC) imeanza kutoa mafunzo ya siku tano ya Utawala na Uongozi wa Michezo Mkoani Simiyu, ambayo yamelenga kuleta tija katika kusimamia na kuendeleza Michezo.

Mafunzo hayo yanawahusisha Maafisa Michezo Mkoa na Wilaya, Viongozi wa Vyama mbalimbali vya Michezo  na walimu wa michezo kutoka katika baadhi ya shule za msingi na sekondari mkoani Simiyu.

Mkurugenzi Mkuu wa Mafunzo hayo Ndg.Suleiman Jabir amesema lengo kuu la mafunzo hayo ni kuwasaidia Maafisa Michezo, viongozi wa vyama vya michezo ngazi ya mkoa na wilaya sambamba na walimu wa michezo kupata mafunzo ya kiufundi katika kusimamia na kuendeleza michezo, ambayo hutolewa katika mikoa yote hapa nchini, chini ya usimamizi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania(TOC).

Akizungumzia ushiriki wa wanawake Ndg. Jabir amesema Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) imehakikisha kuwa wanawake wanashiriki kwa asilimia 40 katika mafunzo hayo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa la mwaka 2016 la kuwashirikisha wanawake katika masuala muhimu ya kimichezo ikiwemo suala la uongozi.

Akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe.Benson Kilangi amesema, Utawala na uongozi wa michezo ulio bora ni msingi wa kuongoza na kuendeleza michezo  kwa mujibu wa sheria,kanuni na taratibu.

“Kamati ya Olimpiki imeandaa mafunzo haya kwa wakati muafaka kwa sababu wanahitajika viongozi wenye taaluma ya kisasa ya namna ya kuongoza michezo na wanamichezo,ambao watakwenda na wakati kutenda kazi zao bila mgongano au vurugu “ amesema Kilangi.

Kilangi amewataka washiriki kuhakikisha kuwa wanazingatia mafunzo watakayopata na kuwa mabalozi wazuri katika maeneo yao, ili mafunzo hayo yasiishie tu katika Taasisi walizopo bali elimu hiyo ifike hadi ngazi ya vijiji ambako ndiko kwenye wachezaji wengi.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya ametoa wito kwa washiriki kutumia mafunzo hayo kama chachu katika kufuata taratibu zote za uendeshaji wa vilabu na vyama vya michezo katika mkoa wa Simiyu ikiwa ni pamoja na kufuata katiba.

Ameongeza kuwa pamoja na kuchukulia michezo kama burudani na sehemu ya kuimarisha afya, washiriki hao wanapaswa kuwasaidia wachezaji kutumia michezo kama ajira inayoweza kuwaingizia kipato.

Kwa upande wake Afisa Michezo wa Mkoa, Ndg.Anthony Komba amesema mafunzo hayo yatawasaidia washiriki kusimamia michezo kwa weledi mkubwa, kuibua vipaji na pia yatasaidia vyama vya michezo kusimamia vema vyama vyao, ikiwa ni pamoja na kufuata katiba hali itakayowasaidia kuepuka migogoro katika vyama.

Mafunzo kwa Maafisa Michezo, viongozi wa vyama vya michezo Mkoa na Wilaya pamoja na walimu wa michezo kutoka katika baadhi ya shule za msingi na sekondari Mkoani Simiyu, yanafanyika katika ukumbi wa BARIDECO mjini Bariadi na yatahitimishwa siku ya Ijumaa tarehe 18/08/2017.

WAJUMBE WA BODI YA BARABARA WAFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI MITATU YA BARABARA INAYOTEKELEZWA KATIKA MANISPAA YA UBUNGO

$
0
0
Wajumbe wa bodi ya barabara inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda wakikagua barabara ya Kifuru-Msigani ikiwa ni ziara ya kukagua miradi ya barabara inayotekelezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo. Leo Agosti 14
Wajumbe wa bodi ya barabara inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda wakikagua daraja lililopo kwenye barabara ya Kifuru-Msigani ikiwa ni ziara ya kukagua miradi ya barabara inayotekelezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo. Leo Agosti 14
Picha ya pamoja ya viongozi mbalimbali wakiwa na Wajumbe wa bodi ya barabara inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda wakikagua barabara ya Kifuru-Msigani ikiwa ni ziara ya kukagua miradi ya barabara inayotekelezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo. Leo Agosti 14
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo (Kulia) akiwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Ubungo Ndg James Mkumbo wakati wa ziara ya Wajumbe wa bodi ya barabara inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda wakikagua barabara ya Watani kwa Jongo katika Kata ya Makurumla. Leo Agosti 14
Wajumbe wa bodi ya barabara inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda wakimsikiliza kwa makini Mtaalamu wa Barabara akitoa maelezo kuhusu ujenzi wa barabara ya Kifuru-Msigani wakati wa ziara ya kukagua miradi ya barabara inayotekelezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo. Leo Agosti 14
Muonekano wa Barabara ya Kifuru-Msigani ikiwa katika hatua za awali za ujenzi.Leo Agosti 14

Wajumbe wa bodi ya barabara inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda leo wamefanya ziara katika miradi ya barabara inayotekelezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo kwa lengo la kujua Maendeleo ya utekelezaji wa miradi hiyo.
 
Miradi iliyotembelewa ni Barabara ya Watani kwa Jongo Kata ya Makurumla ambayo ina Urefu wa kilomita 1 na inajengwa kwa kiwango cha changarawe kwa kutumia fedha za Ndani (own source), Barabara ya Ubungo Msewe kutokea  Kimara Baruti yenye urefu wa Kilomita 2.6 inasimamiwa na TAN ROADS, Pia Barabara ya Kifuru – Msigani yenye urefu wa kilomita 4.0 ambayo ina simamiwa na TAN ROAD na inajengwa kwa kiwango cha lami.

Wajumbe wa bodi ya Barabara hiyo wamedhamiria kuhakikisha miradi iliyopangwa  inatekelezwa kwa wakati na kwa ubora ili kuboresha miundo mbinu ambayo itawanufaisha na kuwaletea maendeleo wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.

Wajumbe hao kwa Upande wa Manispaa ya Ubungo ni Mhe. Mbunge wa viti maalumu Suzan Lymo, Mkururugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo, Katibu tawala wa Wilaya Ndg James  Mkumbo  na Wataalamu kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.


DC SHINYANGA AZINDUA MRADI WA KUZUIA UKATILI WA KIJINSIA

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa kuzuia ukatili wa kijinsia.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro amezindua mradi wa kuzuia ukatili wa kijinsia ‘GBV Prevention Project’ unaotekelezwa na Shirika la lisilo la kiserikali la The Voice of Marginalized Community (TVMC) la mjini Shinyanga linalotoa huduma za kijamii kwa vijana ,watoto na wanawake na makundi yasiyojiweza. 

Uzinduzi huo umefanyika leo Jumatatu Agosti 14,2017 katika ukumbi wa Diamond Field Hotel mjini Shinyanga na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa haki za wanawake na watoto wakiwemo wawakilishi wa mashirika yasiyo ya kiserikali,maafisa watendaji wa kata,maafisa tarafa,afisa maendeleo ya jamii,ustawi wa jamii,afisa utamaduni na dawati la jinsia na watoto. 

Akizungumza wakati wa kuzindua mradio huo,Matiro alilipongeza shirika hilo kwa kuelekeza nguvu zake katika mapambano dhidhi ya ukatili wa kijinsia ambao unachangiwa kwa kiasi kikubwa na jamii husika kwa kushindwa kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola pale wahusika wanapobainika. 

“Serikali inatambua kazi nzuri zinazofanywa na mashirika yasiyo ya kiserikali,ili mfanikiwe mnatakiwa mshirikishe wadau kwenye maeneo husika,mmefanya jambo jema kujitambulisha badala ya kuanza kutekeleza mradi kimya kimya kama baadhi ya mashirika vile yamekuwa yakifanya hali inayowafanya washinde kufanikiwa”,alieleza Matiro. 

“Serikali ipo nanyi bega kwa bega,pale mnapokwama tafadhali tupeni taarifa nasi tutawasaidia kadri tutakavyoweza kwani lengo kuu ni kuwahudumia wananchi wetu ili kuzuia vitendo vya kikatili wanavyofanyiwa wanawake na watoto katika jamii”,aliongeza Matiro. 

Mkuu huyo wa wilaya alitumia fursa hiyo kuyakumbusha mashirika na taasisi mbalimbali zinazotekeleza miradi katika jamii kuhakikisha wanashirikiana na jeshi la jadi ‘sungusungu’,viongozi wa kimila pamoja na watu mbalimbali wenye ushawishi katika jamii husika. 

Akitambulisha Mradi huo,Mkurugenzi wa TVMC,Mussa Jonas Ngangala alisema mradi huo unaofadhiliwa na taasisi ya kusaidia asasi zisizokuwa za kiserikali la The Foundation For Civil Society unaolenga kupiga vita vitendo vya ukatili wa kijinsia utatekelezwa katika kata tano katika wilaya ya Shinyanga ambazo ni Usanda,Samuye,Nsalala,Tinde na Didia. 

Ngangala alisema ili kutekeleza mradi huo kikamilifu shirika hilo litashirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo viongozi serikali,dini,wananchi na wadau wengine. 

“Matarajio yetu kupitia mradi huu ni kwamba kufikia mwezi Januari mwaka 2018 kuwepo na mfumo mzuri wa kutoa taarifa za ukatili wa kijinsia kutoka ngazi ya jamii hadi dawati la jinsia kwa kushirikiana na maafisa utamaduni,maafisa watendaji,maafisa maendeleo ya jamii,ustawi wa jamii na mashirika mengine”,alieleza Ngangala. 

“TVMC ambayo walengwa wake wakuu ni watoto na wanawake imekuwa ikishirikiana na serikali katika kutekeleza majukumu yake ya kuhakikisha watoto wanapata ulinzi na usalama ,elimu na afya bora,msaada wa kisheria kwa wanawake na watoto lakini pia matunzo kwa watoto”,alieleza Ngangala. 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi TVMC,Japhet Daud alisema kupitia mradi huo wataibua mijadala kuhusu vitendo vya ukatili wa kijinsia kupitia matamasha,michezo,ngoma za asili,kutoa elimu na mbinu zingine kadha wa kadha. Katika hatua nyingine Daud alisema ili kukabiliana na mimba na ndoa za utotoni pamoja na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi mkoani Shinyanga ni vyema wadau wote wakashiriki katika mapambano hayo badala ya kuiachia serikali pekee. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa kuzuia ukatili wa kijinsia unaotekelezwa na Shirika la lisilo la kiserikali la The Voice of Marginalized Community (TVMC). Kulia ni Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi TVMC,Japhet Daud,kushoto ni Afisa Mtendaji kata ya Usanda,Emmanuel Maduhu. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro akizungumza ukumbini. 
Wadau wa haki za watoto na wanawake wakiwa ukumbini. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa kuzuia ukatili wa kijinsia. 
Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi TVMC,Japhet Daud akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo. 
Mkurugenzi wa Shirika la lisilo la kiserikali la The Voice of Marginalized Community (TVMC),Mussa Jonas Ngangala akitambulisha mradi wa kuzuia ukatili wa kijinsia unaotekelezwa na shirika hilo.
wadau wakiandika dondoo muhimu.
Mkurugenzi wa TVMC ,Mussa Jonas Ngangala akitambulisha mradi huo.
Wadau mbalimbali walioshiriki katika uzinduzi wa mradi huo wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini.
Mkurugenzi wa TVMC ,Mussa Jonas Ngangala akisisitiza jambo ukumbini.
Wadau wakiwa ukumbini.
Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi TVMC,Japhet Daud akielezea kuhusu mbinu mbalimbali watazozitumia katika kufanikisha mradi huo.
Afisa Mtendaji kata ya Usanda,Emmanuel Maduhu akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo. 
Kiongozi wa dawati la Jinsia na watoto Shinyanga,Vivian Zabron akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa mradi wa kuzuia ukatili wa kijinsia. 
Wadau wakiwa ukumbini. 
Afisa Utamaduni wilaya ya Shinyanga,Janeth Elias akichangia hoja ukumbini. 
Wadau wakiwa ukumbini. Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

SHAKA AINGIA PEMBA KWA KISHINDO

$
0
0
Na Mathias Canal, Pemba

Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 15, 2017 amewasili Visiwani Pemba-Zanzibar kwa Ziara ya kikazi.

Ambapo hii Leo atakuwa katika Wilaya ya Chakechake, katika Ziara hiyo Katibu Mkuu UVCCM Taifa atakagua utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya CCM katika kipindi hiki Cha Miaka mitano 2015-2020

Aidha, Shaka atashiriki shughuli Mbalimbali za kijamii sambamba na kuzungumza na Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 15, 2017 akisalimiana na Wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM na Jumuiya zake mara baada ya kuwasili Visiwani Pemba-Zanzibar kwa Ziara ya kikazi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 15, 2017 akisalimiana na Wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM na Jumuiya zake mara baada ya kuwasili Visiwani Pemba-Zanzibar kwa Ziara ya kikazi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 15, 2017 akisalimiana na Wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM na Jumuiya zake mara baada ya kuwasili Visiwani Pemba-Zanzibar kwa Ziara ya kikazi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 15, 2017 akisalimiana na Wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM na Jumuiya zake mara baada ya kuwasili Visiwani Pemba-Zanzibar kwa Ziara ya kikazi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 15, 2017 akisalimiana na Wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM na Jumuiya zake mara baada ya kuwasili Visiwani Pemba-Zanzibar kwa Ziara ya kikazi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 15, 2017 akisalimiana na Wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM na Jumuiya zake mara baada ya kuwasili Visiwani Pemba-Zanzibar kwa Ziara ya kikazi.

FAIDA YA SERIKALI KUGHARAMIA ELIMU BURE NI WANAFUNZI KUFAULU–PROFESA NDALICHAKO

$
0
0

Na Chalila Kibuda , Globu ya Jamii

SERIKALI inatoa sh. bilioni 18.77 kwa ajili ya kugharamia elimu bure ili kila mtanzania apate elimu bora na faida yake kwa serikali hiyo, ni kuona wanafunzi wanafaulu darasa la Saba na Kidato cha Nne na kuendelea na elimu ya kidato cha tano na hadi chuo kikuu.

Hayo ameyasema leo Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako wakati wa uzinduzi mabweni katika shule ya sekondari Nasibugani ambayo ujenzi wake uko katika hatua ya mwisho pamoja na Shule ya Sekondari Mwinyi, ambayo ujenzi umekamilika kwa kuingia wanafunzi katika mabweni hayo wilayani Mkuranga mkoani Pwani .

Profesa Ndalichako amesema serikali ya awamu ya tano imeondoa gharama katika shule ya msingi na sekondari ili kuondosha mzigo kwa wazazi wengine ambao walikuwa wanashindwa kugharamia elimu hiyo.

Amesema mabweni katika shule ya sekondari Nasibugani na Mwinyi zenye Kidato cha Kwanza hadi Sita ni kuongeza sehemu ya kumwezesha mwanafunzi kusoma kwa muda mrefu na pa kondokana na vishawishi vinavyopatikana mtaani.

Aidha amesema kuwa serikali itaendelea kuboresha shule mbalimbali ikiwemo pamoja na makazi ya walimu yaliyo bora pamoja na huduma zingine ikwemo umeme katika shule ya Sekondari Nasibugani.

Amesema kuwa Mkuranga iko nyuma kielimu ni ukweli usiofichika hivyo walimu pamoja na watendaji kuhimiza suala la elimu ili viwanda vilivyopo na wanamkuranga wanufaike na sekta hiyo.

Waziri Profesa Ndalichako amempongeza Mbunge wa Mkuranga Abdallah Ulega kuanzisha Program kwa wanafunzi wa sekondari kuwa Hakuna Kufeli.

Amesema Program hiyo ifanywe kwa vitendo kwa wanafunzi kujitoa zaidi kusoma kwani mtihani uko karibu lakini wakitumia program hiyo watafanya vizuri na kuondoa sifuri katika shule zao na kuanza daraja la kwanza hadi la tatu.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga amesema kuwa wanaomba chuo cha Ufundi katika wilaya hiyo ili vijana waweze kujiunga na kuweza kutumika katika sekta ya viwanda vilivyojengwa Mkuranga.

Amesema kuwa zaidi ya vijana 900 hawana ajira hivyo chuo cha ufundi ni sehemu sahihi kwa vijana na wataendelea kuongeza mwaka hadi mwaka kadiri wnavyohitimu.

Mbunge wa Mkuranga Abdallah Ulega amesema kuwa jitihada mbalimbali katika kuboresha miundombinu ya shule pamoja na serikali kuongeza walimu.Amesema kuwa wanafunzi wanavyofanya vizuri ni furaha na kuweza kuwa nguvu ya uandaji wa vijana katika mapinduzi ya elimu.

 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia , Profesa Joyce Ndalichako akizindua mabweni mawili katika Shule ya Sekondari Nasibugani  iliyopo Wilaya ya Mkuranga.
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia , Profesa Joyce Ndalichako akipanda mti katika shule ya Sekondari Nasibugani.
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia , Profesa Joyce Ndalichako akizindua mabweni mawili yaliyokamilika katika shule sekondari Mwinyi iliyopo Wilaya ya Mkuranga.
 Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga  akizungumza wananchi na wanafunzi katika shule ya Sekondari Nasibugani.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mkuranga, Mshamu Munde akizungumza wananchi na wanafunzi katika shule ya Sekondari Nasibugani.
 Sehemu ya mabweni na nyumba za walimu ambazo zimefikia hatua ya boma
Sehemu ya mabweni na nyumba za walimu ambazo zimefikia hatua ya boma

WADAIWA SUGU WA ANKARA ZA MAJI WAKATIWE HUDUMA

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa RUVUMA DK BILINITH MAHENGE amemwagiza DK ANSEL MTALIMO kuhakikisha manipsaa ya SONGEA inakatiwa maji kutokana na deni wanalodaiwa na mamlaka ya maji safi na taka SOWASA kutokana na wao kuwa vinara wakutolipa akara za maji kwa muda mrefu.  

Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi's visit to Tanzania in pictures

$
0
0
 The plane carrying Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   touches down at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam in Tanzania ahead of his two-day official visit set to open a new chapter for more enhanced bilateral cooperation between the two countries.
  Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   arrives at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam in Tanzania ahead of his two-day official visit
 President Dr. John Pombe Magufuli receives Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   arrives at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 President Dr. John Pombe Magufuli walks with his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   arrives at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
  President Dr. John Pombe Magufuli walks with his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   arrives at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 

  President Dr. John Pombe Magufuli walks with his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   stand for the two countries' National Anthems  at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
  President Dr. John Pombe Magufuli walks with his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   stand for the two countries' National Anthems  at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 The Vice President Hon. Samia Suluhu Hassan, Prime Minister Kassim Majaliwa and other top government officials ready to receive Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi    at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 Government officials receive Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi    at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   inspects the guard of honour at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 President Dr. John Pombe Magufuli introduces Vice President Hon. Samia Suluhu Hassan to the Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi     at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 President Dr. John Pombe Magufuli is introduced to Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi's delegation    at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 The Vice President Hon. Samia Suluhu Hassan, President of Zanzibar Dr. Ali Mohamed Shein, Prime Minister Kassim Majaliwa brave the afternoon drizzle to  receive Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi    at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
  Ululation as Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi    arrives at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
  Traditional dances welcome to Tanzania Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi    at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
  Mount Usambara Brass band welcome to Tanzania Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi    at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 President Dr. John Pombe Magufuli walks welcomes to the state House his  guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  
 President Dr. John Pombe Magufuli offers a giant Makonde carving to his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  
 President Dr. John Pombe Magufuli shakes hands with  his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  
 President Dr. John Pombe Magufuli offers a painting  to his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  
 President Dr. John Pombe Magufuli receives a traditional bowl from his  guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  
 President Dr. John Pombe Magufuli shakes hands with  Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  before their tete-a-tete at the State House in Dar es salaam 
  President Dr. John Pombe Magufuli in a tete-a-tete with his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   at the State House in Dar es salaam 
  President Dr. John Pombe Magufuli walks Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  to the conference room for official talks at the State House in Dar es salaam 
 Traditional dances entertain
  President Dr. John Pombe Magufuli in bilateral talks with  Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  at the State House in Dar es salaam 
 Some Tanzanian Cabinet Minister chat moments before the two leaders make their addresses
 TBC crew busy reportin live the evnt
  Vice President Hon. Samia Suluhu Hassan, President of Zanzibar Dr. Ali Mohamed Shein, Prime Minister Kassim Majaliwa with  President Dr. Magufuli and his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi    at the State House  in Dar es Salaam 
  Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  makes his address  at the State House  in Dar es Salaam 
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  makes his address  at the State House  in Dar es Salaam 
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  makes his address  at the State House  in Dar es Salaam 
 President Dr. John Pombe Magufuli thanks Egyptian President Abdel Fattah El-Sis after his address
 President Dr. John Pombe Magufuli recicoparates with is address
 President Dr. John Pombe Magufuli recicoparates with is address
 President Dr. John Pombe Magufuli recicoparates with is address
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi thanks his host after making his address
  President Dr. John Pombe Magufuli and Egyptian President Abdel Fattah El-Sis share a light moment  after their  addresses
  President Dr. John Pombe Magufuli and Egyptian President Abdel Fattah El-Sis share a light moment  after their  addresses
  President Dr. John Pombe Magufuli and Egyptian President Abdel Fattah El-Sis share a light moment  after their  addresses
  President Dr. John Pombe Magufuli introduces some of his cabinet Ministers to Egyptian President Abdel Fattah El-Sis share a light moment  after their  addresses
 President Dr. John Pombe Magufuli introduces some of his cabinet Ministers to Egyptian President Abdel Fattah El-Sis share a light moment  after their  addresses
 President Dr. John Pombe Magufuli introduces some of his cabinet Ministers to Egyptian President Abdel Fattah El-Sis share a light moment  after their  addresses
  Egyptian President Abdel Fattah El-Sis greets  Zanzibar's Minister for Finance and Planning Dr. Khalid Salum Mohamed
  Egyptian President Abdel Fattah El-Sis greets  Minister of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children, the United Republic of Tanzania Hon. Ummy Ally Mwalimu
   Egyptian President Abdel Fattah El-Sis greets Dr. Charles John Tizeba, Minister for Agriculture, Livestock and Fisheries
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sis greets ProfJumanne Maghembe, Minister for Natural Resources and Tourism

Egyptian President Abdel Fattah El-Sis greets Constitutional and Legal Affairs ministerProf Palamagamba Kabudi
 Former Vice President Dr. Mohamed Gharib Bilali chats with Foremer Prime Minister Mizengo Pinda during a state banguet held in honour of visiting Egyptian President Abdel Fattah El-Sis
  Ruling CCM party Secretary General Abdulrahman Kinana with some of the Egyptian delegation memners during a state banguet held in honour of visiting Egyptian President Abdel Fattah El-Sis
Chief Mufti. Sheikh Aboubakary Zubeiry shares a table with some top government brass during the state banquet
 From left are Acting Chief Justice, Prof Ibrahim Hamis Juma, Former Speaker Mama Anne Makinda and Former Chief Justice Hon. Augustino Ramadhani
 The high table stand at attention as National Anthems of Tanzania and Egypt are played
 All stand at attention as National Anthems of Tanzania and Egypt are played
 All stand at attention as National Anthems of Tanzania and Egypt are played
 All stand at attention as National Anthems of Tanzania and Egypt are played
 All stand at attention as National Anthems of Tanzania and Egypt are played
 All stand at attention as National Anthems of Tanzania and Egypt are played
 All stand at attention as National Anthems of Tanzania and Egypt are played
 Retired Defence and Security Forces top brass stand at attention as National Anthems of Tanzania and Egypt are played. From left they are Former CDF General Mwamunyange, Former IGP Saidi Mwema, Former Tanzania Intelligence and Security Service Rashid Othman, Former CDF General George Waitara and Former Prisons Commissioner General John Casmir Minja 
 Top government oficials at the state banquet
 Some of the heads of parastatals at the state banquet
 The Tanzania Telecommunications Company Limited (TTCL) CEO Mr. Waziri Kindamba (left) shares the table with one of the country's veteran musicians Cosmas  Thobias Chidumule
 Members of the Tanzania All Stars music group members at the State Banquet
 Members of the Tanzania All Stars music group members at the State Banquet
 Members of the Tanzania All Stars music group members at the State Banquet
 Clouds FM Director of Programmes Ruge Mutahaba (right) and other guests  at the State Banquet
 Some of the invited guests  at the State Banquet
 Some of the invited guests  at the State Banquet
Members of the diplomatic corps at the State Banquet
 Members of the diplomatic corps at the State Banquet
 Members of the diplomatic corps at the State Banquet
 Members of the diplomatic corps at the State Banquet

 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi is delighted to meet with Former President Alhaj Ali HassanMwinyi
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi greets former Zanzibar President Dr. Amani Abeid Karume
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  greets former Speaker Hon Pius Msekwa
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi chats with  Former Vice President Dr. Mohamed Gharib Bilali and  Foremer Prime Minister Mizengo Pinda
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi is introduced to Dr. Hussein Mwinyi, Minister for Defence and National Service
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  greets Acting Chief Justice, Prof Ibrahim Hamis Juma

 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  greets the Chief of Staff of the TPDF  Lieutenant General James Mwakibolwa
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi is introduced to top government officials

 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi greets the Chief Mufti of Tanzania Sheikh Aboubakary Zubeiry 
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi greets the Dar es salaam Regional Commissioner Hon. Paul Makonda
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi greets the  Commissioner General of Immigration  Dr. Anna Peter Makakala 
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi greets some of the invited guests
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi greets Prof. Jumanne Abdallah Maghembe, Minister for Natural Resources and Tourism
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi greets  the Minister for Constitutional and Legal Affairs Prof Palamagamba Kabudi 
  President Dr. John Pombe Magufuli and Zanzibar President Dr. Ali Mohamed Shein see off their  guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  
 Zanzibar President Dr. Ali Mohamed Shein  gestures as their guest drives off 
President Dr. Magufuli takes his leave 
 Zanzibar President Dr. Ali Mohamed Shein in a light moment with Former President Alhaj Ali Hasan Mwinyi and Former Zanzibar President Dr. Amani Abeid Karune and Dar es salaam Regional Commissioner Hon. Paul Makonda
The Chief Secretary Ambassador John Kijazi bids farewell to Deputy Speaker Dr. Tulia Ackson. All photos by STATE HOSUE

CHUO KIKUU CHA USHIRIKA MOSHI(MoCU) CHATOA ELIMU YA USHIRIKA KWA WAANDISHI WA HABARI.

$
0
0


Makamu Mkuu wa Cho Kikuu cha Ushirika ,Moshi (MoCU) ,Prof,Faustine Bee akizungumza wakati wa ufunguzi wa Warsha ya siku moja ya Elimu ya Ushirika kwa Waaandishi wa Habari wa mkoa wa Kilimanjaro.
Baadhi ya Watumishi wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) wakishiriki warsha hiyo.
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakifuatilia hotuba ya ufunguzi ilitolewa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) katika Warsha ya siku moja iliyofanyika chuoni hapo.
Naibu wa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi(MoCU) Taaluma Dkt,Kitala Malamsha akizungumza wakati wa ukaribisho wa mgeni rasmi katika ufunguzi wa warsha ya siku moja ya Elimu ya Ushirika kwa Waandishi wa Habari.
Baadhi ya Watumishi wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) wakifuatilia mijadla katika warsha hiyo.

Washiriki wa Warsha ya Elimu ya Ushiriki kwa Waandishi wa Habari wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni rasmi Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) Prof ,Faustine Bee.Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

DKT. KALEMANI AENDELEA KUZINDUA MIRADI YA UMEMEMVIJIJINI AWAMU YA TATU (REA PHASE III MIKOA YA KUSINI NA RUKWA

$
0
0

Na Henry Kilasila - Rukwa

Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Dkt Medard Kalemani ameendelea na ziara za uzinduzi wa Miradi ya Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA PHASE III) ambapo Agosti 14, 2017 alikuwa Mikoani Rukwa katika Kijiji cha Kabwe Wilaya ya Nkasi.

Dkt. Kalemani alisema jumla ya Shilingi Bilioni 42.5 zitatumika kupeleka umeme katika Mkoa huo na kuongeza Mradi huo utatekelezwa katika vipindi viwili tofauti ambapo sehemu ya kwanza itahusisha upelekaji umeme katika vijiji 111.

"Sehemu ya pili itahusisha vijiji 145 ambapo itaanza baada ya kukamilika kwa sehemu ya kwanza. Kufikia mwaka 2021 vijiji vyote vya Mkoa wa Rukwa vitakuwa vimepatiwa umeme".Alisema Dk. Kalemani.

Aidha, Dkt. Kalemani alimtambulisha Mkandarasi atakayejenga Mradi wa REA Mikoani humo Kampuni ya Kitanzania ya Nakuroi Investment Company Limited.

Alimwagiza Mkandarasi kuhakikisha anapeleka umeme Kijiji kwa Kijiji na Kitongoji kwa Kitongoji bila kuruka na sehemu zinazotoa huduma za Kijamii kama Mashule, Zahanati, Magereza, Visima vya maji, Nyumba za Ibada na sehemu mbalimbali.

Pia alitoa maagizo kwa TANESCO kupeleka Ofisi katika Kijiji cha Kabwe na katika maeneo yote yenye Wateja wengi lakini wapo mbali na Huduma za TANESCO.

Aliongeza kwa kuwataka Mameneja na Watalaamu wa TANESCO kutokukaa Ofisini bali wawafuate Wateja.Awali, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji TANESCo, Dkt. Tito E. Mwinuka aliwaomba Wananchi hao wa Kabwe kuwa waaminifu na kutoa ushirikiano kwa Watendaji wa TANESCO kabla na hata baada ya Mradi kukamilika.

"Muitunze miundombinu ya umeme, msiihujum wala kuichoma moto". Alisema Dkt. Mwinuka.Alisema TANESCO imejipanga kuhakikisha Wananchi hao wanapata huduma ya umeme iliyobora na ya uhakika.

Mbunge wa Nkasi, Ali Kessy aliwaeleza Wananchi kuwa mradi huo wa usambazaji umeme vijijini hauna malipo ya fidia hivyo watoe ushirikiano kwa wakandarasi hao wakati wanatekeleza mradi huo.

Mkuu wa Wilaya ya Nkansi Mheshimiwa Saidi Mtanda aliushukuru Uongozi wa TANESCO kwa kwani umekuwa ukitoa ushirikiano pale unapohitajika.
"Mheshimiwa Mgeni Rasmi katika Kijiji cha Nyamare kwenye chanzo cha maji tulileta Mkandarasi akatukadilia bei ya Transifoma milioni 60, tuliwasiliana na uongozi wa TANESCO wametufungia Transfoma kwa pesa zao milioni 24". Alisema Mheshimiwa Mtanda.

Mheshimiwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Dkt Medard Kalemani alimalizia uzinduzi Mkoani Rukwa kwa kuwakabidhi Wazee kumi zawadi ya kifaa cha UMETA.
Naibu waziri Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Dkt Medard Kalemani akifurahia baada ya kuzindua mradi wa REA RUKWA
Naibu Waziri Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani akiwasili eneo la uzinduzi Mkoani Rukwa, akiwa amepokelewa na mwenyeji wake Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mheshimiwa Saidi Mtanda.
Kutoka kushoto Mkurugenzi Mkuu REA, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Dkt. TITO E. Mwinuka katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Kampuni ya Nakuro Investment Company Limited inayojenga Mradi huo wa umeme Mkoani humo. 
Naibu waziri Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Dkt Medard Kalemani akipata maelezo ya namna kifaa cha UMETA kinavyofanya kazi kutoka kwa Bw. Lucas Kusare Afisa Huduma kwa Wateja Mkoa wa Rukwa .

WAZIRI WA ARDHI MH.LUKUVI APOKEA RASIMU YA MKAKATI WA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO ZA MATUMIZI BORA YA ARDHI NCHINI, MJINI MOROGORO

$
0
0
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi amepokea rarmi Rasimu ya Mkakati wa kukabiliana na Changamoto za Matumizi bora ya Ardhi Nchini na kutaja Teknolojia kuwa ni changamoto inayokabili mpango wa matumizi bora ya ardhi inayopelekea kulegalega kwa upangaji, upimaji na umikilishaji wa Ardhi.

Waziri Lukuvi ameyasema hayo mjini Morogoro wakati alipokuwa  akipokea rasimu ya mkakati wa kukabiliana na changamoto za matumizi bora ya ardhi nchini, iliyoonesha na kuainisha mapendekezo katika uandaaji,usimamizi na utekelezaji.

“Tunahitaji teknolojia rahisi ambayo hata ninyi mkondoka serikali inaweza kuhimili, hatupendi mtuambukize teknolojia ambayo itakuwa ni ngumu kwetu, kwakuwa serikali inapopanga gharama kubwa zinajitokeza kwenye picha za anga na zile za chini,” alisema Lukuvi.

Lukuvi alisema kuwa kuhusu fedha si tatizo lakini ukosefu wa teknolojia ndio tatizo kubwa zaidi,hivyo ni vizuri kuyatazama haya mashirika yasiyo ya kiserikali tushirikiane nayo ili yaweze kuangalia ni teknolojia gani rahisi itakayoweza kupunguza gharama za upimaji na upangaji wa ardhi vijijini baada ya kusubiri ndege za anga ambazo ni gharama kubwa.

Aliongeza kuwa Serikali inapenda kuwa na uratibu wa haraka, ulio rahisi ambao wananchi wanaweza kupanga maeneo yao na kuongeza, lakini pia kuondokana na migogoro ya Ardhi.
 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi akifungua rasmi mkutano kwa ajili ya kusikiliza na kupokea  Rasimu ya Mkakati wa Kukabiliana na Changamoto za Matumizi Bora ya Ardhi Nchini, mjini Morogoro.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh. Stephen Kebwe akitoa maelezo juu ya mkutano huo na kuonesha namna gani itakavyoweza kumaliza migogoro ya Ardhi Nchini.
 Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi Dkt. Stephen Nindi akitoa Mhtasari wa mkutano huo wa kuwasilisha Rasimu ya Mkakati wa Kukabiliana na Changamoto za Matumizi Bora ya Ardhi Nchini
 Bw. Gerald Mwakipesile Afisa  Mipango wa Tume ya Mipango na Matumizi ya Ardhi akiwasilisha kwa Mh. Lukuvi Rasimu ya Mkakati wa kukabiliana na Changamoto za Matumizi Bora ya Ardhi Nchini.
Waziri wa Ardhi Mh. Lukuvi pamoja na wajumbe wakifuatilia kwa makini uwasilishwaji wa Rasimu ya mkakati wa kukabiliana na changamoto za matumizi bora ya ardhi nchini
 Bw. Emmanuel Msofe kutoka Idara ya Maliasili na Utalii akichangia jambo na ushiriki wao katika mkakati wa kukabiliana na changamoto za matumizi bora ya Ardhi
 Bw. Victor Mwita kutoka Wizara ya Kilimo na Ufugaji akichangia jambo ni namna gani watakavyo shirikiana katika kuhakikisha changamoto za Ardhi nchini zinakwisha
 Bi. Bertha Luzabiko Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Morogoro akieleza namna wanavyofanya kazi zao na kushirikiana na watu wa ardhi pia ushiriki wao wa kukabiliana na Changamoto za Matumizi bora ya Ardhi Nchini.
 Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Care Nchini Tanzania Bw. Waleed Rauf akielezea namna ya wanavyoshirikiana vizuri na Serikali kuhakikisha jinsi gani matumizi bora ya Ardhi yanaenda sawa na kuongeza kuwa malengo yao pia ni kuona umasikini unapungua kwa kiasi kikubwa katika jamii zetu.
 Mratibu wa Miradi ya Ardhi kutoka Oxfam Naomi Shadrack akichangia jambo kuwa kupitia rasimu hiyo wadau wamefanya kazi kwa pamoja kuhakikisha sekta ya ardhi ambayo inatambuliwa na wengi wakiwemo  wakulima na wafugaji wadogo wadogo inafanyiwa kazi.
 Bw. Anthony Temu, Meneja wa Ukasimishaji Rasilimali Ardhi Vijijini kupitia Mpango wa Kukasirimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania(MKURABITA) akichangia jambo wakati wa mkutano huo
 Bw. Jamboi Baramayegu Kutoka Ujamaa-CORT akichangia juu ya maswala ya ufugaji na kuomba mkakati huu wa kukabiliana na changamoto za matumizi bora ya Ardhi Nchini utambue maeneo ya kulishia mifuko vipindi vyote wakati wa kifukwe na kaingazi pia.
 Kamishna wa Ardhi Nchini Bi. Mary Makondo akichangia jambo na kuelezea mambo mbalimbali yanayohusiana na ardhi na kusisitiza ushirikiano wa sekta zote katika kuhakikisha Mkakati wa kukabiliana na changamoto za matumizi bora ya ardhi unaenda vizuri
Mwenyekiti mpya wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi Bw. Fidelis Mutakyamilwa akitoa neno la Shukurani kwa Mh. William Lukuvi (MB) , Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi baada ya kusikiliza uwasilishwaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kukabiliana na Changamoto za Matumizi Bora ya ardhi na namna Tume itakavyofanya kazi na wadau ili kuhakikisha Mchakato Unafanyika kwa haraka.

 Waziri wa Ardhi Mh. Lukuvi (Kulia) Akikabidhiwa rasmi Rasimu ya Mkakati wa Kukabiliana na Changamoto za matumizi Bora ya Ardhi Nchini kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi Bw. Fidelis Mutakyamilwa(Kushoto)
 Waziri wa Ardhi Mh. Lukuvi (wa kwanza kulia) akimkabidhi Kamishna wa Ardhi Nchini Bi. Mary Makondo(wakatikati) Rasimu ya Mkakati wa Kukabiliana na Changamoto za matumizi Bora ya Ardhi Nchini, wa tatu kutoka kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi Dkt. Stephen Nindi.
 Picha ya pamoja baada ya Waziri wa Ardhi Mh. Lukuvi kupokea rasmi Rasimu ya Mkakati wa Kukabiliana na Changamoto za matumizi Bora ya Ardhi Nchini
 Wadau wakiendelea kufuatilia Mkutano huo
 Mkutano ukiwa unaendelea.
Picha ya Pamoja
Picha zote na Fredy Njeje/Blogs za Mikoa Tanzania

RIDHIWANI AWAFUMBUA MACHO MADIWANI WA CHALINZE KUHUSU MAPATO YA VIJIJI VINAVYOZUNGUKA HIFADHI

$
0
0
MBUNGE wa jimbo la Chalinze ,Ridhiwani Kikwete amewataka madiwani wa halmashauri ya Chalinze ,kukaa na viongozi wa vijiji vinavyozunguka hifadhi ya Saadan na Wamiliki ili kujua mapato wanayonufaika nayo kwa mwaka na changamoto zilizopo.

Amesema zipo sheria zinazojieleza kuwa kila kijiji kinachozunguka hifadhi hupata mapato kwa mwaka kama si mwezi ambapo madiwani na halmashauri hazitambui.

Akizungumza katika kikao cha mwaka cha baraza la madiwani Chalinze,Ridhiwani alieleza,ipo haja ya kujua sheria za maliasili zinazosaidia maeneo yao pamoja na kulinda hifadhi ili kujiongezea kipato.
Aidha alisema kamati ndogo ya bunge ya mazingira na maliasili iliyoketi hivi karibuni kwa lengo la kujiuliza juu ya matatizo yanayoendelea kwenye bunga za hifadhi ikiwemo Wamimbiki inatarajia kufanya kikao na madiwani hao wakati wowote kuanzia sasa.

Ridhiwani alieleza kwamba,kamati hiyo itakwenda kuzungumza na halmashauri na madiwani hao ili kujua changamoto zinazowakabili .
“Wamimbiki ndio njia kubwa ya kupita tembo na wanyama wengine wakali kwenda Saadan na ndio njia ya wanyama wanaotoka Saadan kwenda Ruvuma na Selou”

“Kamati itatakaizungumzie uhifadhi na kutenga mazingira yetu yakae vizuri na kutengeneza vivutio Wamimbiki ili tutengeneze fedha nyingi kwa watalii hasa wa picha”alisema Ridhiwani.

Hata hivyo Ridhiwani alisema,zipo sheria zinazoruhusu ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri kuwa mwanachama kwa jambo hilo ambapo pia kila kijiji kinachozunguka hifadhi kwa mwaka inatakiwa kupata sh milioni.12.
“Kata na vijiji vinavyozunguka Saadan na Wamimbiki lazima mjue hilo,mie ndio nilijua katika kikao hicho hivyo fuatilieni kwenye vijiji vyenu mjue kama huwa wakinufaika na mapato hayo” .

“Unaweza kukuta vijiji havisemi na wakati mwingine vinahitaji fedha hata za madaftari kwa madiwani.;kama kweli havijui suala hili basi kikao chetu na kamati ndogo ya bunge kitasaidia kuleta ufumbuzi wa changamoto zetu”alifafanua Ridhiwani.

Mbali na hayo aliwataka madiwani hao kuendelea kushikamana,kuwa na ushirikiano na kupendana .Mbunge huyo aliwaomba wachapekazi kwa kasi waliyoanza nao ili kuiinua halmashauri hiyo ambayo inatoka kwenye uchanga na kuinua mapato yake zaidi ya sasa.

Nae mwenyekiti wa halmashauri ya Chalinze,Saidi Zikatim alisema wamepokea taarifa za ujio wa kamati hiyo kwani itakuwa mwarubaini wa changamoto mbalimbali zinazowakabili.Alisema bado kuna kero kubwa ya migogoro ya mipaka baina ya hifadhi na wana vijiji na kusababisha mahusiano yasiyo mazuri.

Zikatimu alibainisha ,hifadhi zinapaswa kutoa elimu na kutatua changamoto zinazowagusa na jamii ili kuondoa migongano isiyo ya lazima.

Katika kikao hicho ,diwani wa kata ya Mandela Madaraka Mbonde,alichaguliwa kuwa makamu mwenyekiti kwa kipindi cha mwaka mmoja

CHOUGHULE: NITACHAPA KAZI KUUNGA MKONO JUHUDI ZA JPM

$
0
0

Sharik Choughule
MWENYEKITI Mpya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Kivukoni, Dar ers Salaam, Sharik Choughule ameahidi kufanya kazi kwa uadilifu na umahiri mkubwa kuenzi juhudi za Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli katika ujenzi wa CCM Mpya, Tanzania Mpya.

Amesema, anaamini juhudi zilizoanza kufanywa na Dk. Magufuli zinadhihirisha kwamba zitakifikisha Chama Cha Mapinduzi katika mageuzi ya kweli kukifanya kuwa cha wanachama na kimbilio la wanyonge na pia dhamira ya kuijenga Tanzania mpya ya uchumi wa viwanda itafanikiwa hivyo ni lazima aungwe mkono kwa dhati.

Choughule amesema hayo,  katika salam zake kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kata ya Kivukoni, katikia uchaguzi uliofanyika mwishoni mwa wiki, ambapo salam hizo amezielekeza kwa CCM taifa kwa kuweka mchakato na usimamizi mzuri wa uchaguzi ndani ya Chama.

Amewashukuru pia vuiongozi wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Wilaya ya Ilala na kata hiyo na wanachama kwa ujumla  kwa kuendesha uchaguzi huo vizuri na kwamba ushindi aliopata siyo wake binafsi bali wa wana CCM wote wa kata hiyo, hivyo kilichobaki sasa ni kushikamana na kuijenga CCM mpya yenye kuwajali wanyonge.

Choughule ameahidi kushirikiana na wale aliogombea nao na pia kuhakikisha anashirikiana na wanachama na viongozi wote ili kuifanya CCM katika kata hiyo mbali na kupiga hatua kisiasa lakini pia inapige hatua kiuchumi, kwa kuanzisha miradi ya maendeleo yenye ushirikishwaji wa wanachama wote.

"Kama mnavyojua, CCM katika maeneo mengi imekuwa ikiyumbishwa na kuwa tegemezi, jambo hili si zuri, hivyo moja ya mikakati yangu katika uongozi wangu ni kuhakikisha Chama kinakuwa na miradi ambayo itasaidia kuendesha shughuli za chama badala ya kutegemea wahisani", alisema Choughule.

"Pamoja na kuanzisha miradi lakini nitahakikisha chama kinakuwa imara kwa kuongeza idadi ya wanachama na pia kuchukua nafasi zote za uongozi katika ngazi za serikali za mitaa na udiwani na pia kutoa mchango mkubwa katika kuhakikisha Kivukoni inatoa kura nyingi za kishindo kwa mgombea wa Ubunge na Urais kwa tikteti ya CCM katika Uchaguzi mkuu wa 2020", alisema Choughule .
 MWENYEKITI Mpya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Kivukoni, Dar ers Salaam, Sharik Choughule akiwa viongozi wa CCM Kata hiyo na mwakilishi kutoka Wilaya ya Ilala, baada ya uchaguzi kufanyika mwishoni mwa wiki

TAARIFA KWA UMMA: DAWASCO KUKATA MAJI KUANZIA AGOSTI 14-19, 2017

$
0
0




UBORESHAJI WA MTAMBO WA UZALISHAJI MAJI WA RUVU CHINI

BAGAMOYO MKOANI PWANI.
Shirika la MajiSafi na Majitaka Dar-es-salaam (DAWASCO), linawatangazia wateja wake wote wa Mji wa Bagamoyo Mkoani Pwani kuwa mtambo wa uzalishaji Maji wa Ruvu Chini utakuwa kwenye maboresho kwa wastani wa siku 5, kuanzia siku ya Jumatatu tarehe 14/08/2017 hadi 19/08/2017, hivyo kusababisha baadhi ya maeneo ya Mji wa Bagamoyo kuwa na upungufu wa kiwango cha huduma ya Majisafi.
Sababu ya upungufu wa Majisafi: Maboresho ya Mtambo na mabomba makuu ya usafirishaji na usambazaji Maji.Maeneo yatakayoathirika: Mji Wa Bagamoyo Vijiji Vya Zinga, Mlingotini, Kilomo na Mapande.
Dawasco inawaomba wateja kutunza Maji ya kutosha kuepuka adha itakayojitokeza.
Kwa taarifa zaidi wasiliana nasi kupitia: 

Kituo cha huduma kwa wateja 0800110064 (BURE) au
Dawati la huduma kwa wateja Dawasco Bagamoyo 0743 451 887
www.dawasco.go.tz 
Imetolewa Na:
Ofisi Ya Uhusiano
Dawasco-Makao Makuu.

BENKI YA EXIM TANZANIA YASHEHEREKEA MIAKA 20 YA HUDUMA KWA KUWEKEZA MILIONI 200 KATIKA SEKTA YA AFYA.

$
0
0
Mkuu wa kitengo cha fedha cha benki ya Exim Selemani Ponda akimkabidhi Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Temeke, Husna Msangi jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni zawadi kwa hospitali hiyo kwa kujali jamii na kusheherekea miaka 20 ya Benki ya Exim Tanzania. 
 Mkuu wa kitengo cha fedha cha benki ya Exim Selemani Ponda akizungumza katika Hospitali ya Temeke jijini Dar es Salaam leo wakati wakisheherekea miaka 20 ya benki ya Exim Tanzania pamoja na kutoa msaada wa Vitanda na Magodoro 40 katika hospitali hiyo ikiwa benki hiyo inaijali jamii. Kutoka Kushoto ni Mkuu wa Matawi ya Exim Tanzania, Agnes Kaganda, Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano Benki ya Exim Tanzania, Stanley Kafu. Na kutoka Kulia ni Katibu wa Afya, Sanura Kondo na Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Temeke, Husna Msangi.
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Temeke, Husna Msangi(Katikati) akiwashukuru Benki ya Exim mara baada ya kutoa msaada wa Magodoro na Vitanda 40 katika Hospitali ya Temeke jijini Dar es Salaam leo Kushoto ni Mkuu wa kitengo cha fedha cha benki ya Exim Selemani Ponda na Kulia ni
Katibu wa Afya, Sanura Kondo na Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Temeke, Husna Msangi.

BENKI ya Exim Tanzania imetoa msaada wa vitanda na magodoro 40 katika hospitali ya Wilaya ya Temeke ikiwa ni shukrani yao katika kuadhimisha miaka 20 ya Benki hiyo ya kujali jamii ambapo msaada huo utawekeza shilingi milioni 200 katika sekta ya afya Tanzania. 

Hayo yamesemwa na Mkuu wa kitengo cha fedha cha benki ya Exim Selemani Ponda wakati wa kuwakabidhi vitanda 40 katika hospitali ya wilaya ya Temke jijini Dar es Salaam leo. amesema kuwa
 Mradi huu unalenga kusaidia upungufu wa vitanda katika hospitali nchini hivyo benki ya Exim itatoa magodoro 500 na vitanda katika hospitali za serikali mikoa 13 nchini.
 
 “ Mwaka huu benki ya Exim imefikia hatua muhimu sana. Tunasheherekea miaka 20 ya uvumbuzi na kujitolea kwa jamii. Kwa miaka mingi benki ya Exim imewekeza kwa kiasi kikubwa katika sekta ya afya, mazingira na elimu nchini. Tunatambua juhudi za serikali katika kuboresha huduma za afya hivyo basi tumejitolea mwaka huu mzima kuwekeza katika hospitali za serikali katika maeneo mbalimbali nchini.” amesema Ponda.
 Nae 
Kaimu Mganga Mkuu wa hospitali ya Temeke Dkt. Husna Msangi amesema,kuwa  “ Upungufu wa vitanda katika hospitali ya Tememke ni changamoto kubwa. Tunahitaji vitanda  katika wodi ya watoto na wodi ya wazazi. Msaada huu kutoka benki ya Exim wa hivi vitanda 40 na magodoro utasaidia sana katika kupunguza changamoto hii katika hospitali yetu.”

Ikiwa kama sehemu ya mradi wa “miaka 20 ya kujali jamii” benki ya Exim itatoa msaada wa vitanda 500 na magodoro yake kwa hospitali, katika mikoa ya Mbeya, Iringa, Arusha, Morogoro, Tanga, Dodoma, Kigoma, Kilimanjaro, Shinyanga, Mtwara, Pemba na Unguja.

Benki ABC yazindua huduma mpya za uwakala wa huduma za kibenki

$
0
0
Lengo ni kuwafikia waliowengi na huduma za kibenki kwawasio na akaunti za benki.

Dar es Salaam Tanzania, Jumatatu 14 Agosti 2017 – Ikiwa ni moja kati ya mikakati yake ya kuendelea kuboresha huduma zake kwa kutoa huduma kwa  kila mtanzamia hasa kwa wale wasio na akaunti za Benki, Benki ABC Tanzania leo imezindua huduma za wakala itakayowawezesha wateja wake kupata huduma za kibenki hiyo wakiwa katika mazingira yeyote yale.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi huo, Mkuu wa Kitengo cha Wateja binafsi Bi.Joyce Malai alisema Benki ABC inaendelea kuja na teknolojia mpya katika utoaji huduma ili kukidhi mahitaji ya kibenki kwa wateja wake nchini Tanzania.

Changamoto ya Kipato kidogo na kuhitajika kwa vielelezo vingi wakati wa kufungua akaunti za Benki pamoja na uhaba wa huduma za kibenki kwenye baadhi ya maeneo hapa nchini yamefanya Watanzania wakose huduma za kibenki na hivyo kufanya maendeleo ya kiuchumu ya nchi kuwa finyu. Sisi Benki ABC tumejiandaa kuhakikisha kwamba huduma za uwakala za Benki yetu zinakuwa ni suluhisho kwa Watanzania kupata huduma bora za kifedha wakiwa popote bila ya kupata shida, alisema Joyce.

Aliongeza kuwa kama Benki inayokua kwa kasi hapa nchini, benki ABC inalengo kupanua huduma na uwepo wake kwenye miji mikubwa hivyo huduma za uwakala zitakuwa ni moja ya njia ya kufikia malengo hayo.

Joyce aliongeza kuwa huduma za uwakala za Benki ABC itakuwa na tija kwa Watanzania ambao hawana akaunti za Benki na pia kwa wale ambao wana akaunti lakini badala ya kupoteza muda mwingi kupanga foleni kwenye matawi yao wanaweza kupata huduma hizo kwenye wakala wa Benki hiyo popote pale. Huduma za wakala zitaanza kupatikana jijini Dar es Salaam kupitia Maxcom Afrika. Wateja wa Benki ABC watapata huduma zote za kibenki kupitia wakala wote wa Maxmalipo kwa mkoa wa Dar es Salaam kabla ya huduma hiyo kusambaa nchini kote.

Mkuu huyo wa Kitengo cha Wateja binafsi alisema wakala wa Benki ABC watatoa huduma za kibenki zikiwemo kufanya miamala mbali mbali ambazo hapo awali ziliwalazimu wateja kupanga foleni kwenye matawi ya Benki hiyo zikiwemo kuweka na kutoa fedha, kulipia ankara mbalimbali kama maji, umeme, huduma za kufungua akaunti na kupata au kubadilisha kadi ya Benki. Huduma hizi pamoja na nyinginezo zitapatikana kwa wateja wa Benki ABC kupitia Maxmalipo.

Joyce, aliwahakikishia wateja wa Benki ABC kuendelea kuwa tayari kupata huduma nyingine nyingi zenye tija na manufaa kwa ajili yao. ‘Tutaendelea kuwekeza zaidi kwenye huduma zilizo bora zaidi na kwa kuanza wateja wetu wanaweza kujidhihirishia jinsi huduma za uwakala zitakavyokuwa na tija kwao kwa kurahishisha huduma za kibenki pamoja na kuokoa gharama na muda wa kupanga foleni na kutembea umbali mrefu ili tu kupata huduma za kibenki.

Tumeungana na Maxcom Afrika Plc ambao wana mawakala wengi hapa nchini Tanzania na hivyo tunaamini tutafanikiwa sana kufikia wateja wengi na kufanikisha lengo letu, aliongeza Joyce.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Maxcom Afrika Plc Jameson Kassati alisema kwa sasa mawakala wa Maxmalipo wanafanya miamala zaidi ya 700,000 kwa siku. ‘Tunajisikia fahari sana kushirikiana na Benki ABC ambayo kwa mwaka huu imeshinda tuzo ya kuwa Benki bora na inayokuwa hapa nchini Tanzania, Maxcom Afrika Plc ndio yenye wakala wengi nchini Tanzania ambapo kwa sasa kuna jumla ya wakala 16,000. Maxcom ndio ilikuwa ya kwanza kuzindua huduma za uwakala wa kibenki hapa nchini. Maxmalipo inatumia teknolojia ya utaalamu wa hali ya juu ambapo tumeweza kufanikisha kurahisisha Malipo mbali mbali kwa uharaka zaidi ikiwemo ile ya Malipo ya maji, umeme na mengineyo.

Akiongea kwenye hafla hiyo, meneja wa huduma za uwakala Benki ya ABC Mwita Robi alisema, ‘kwa hapa tulipofikia, matawi ya Benki ABC yatakuwa na umuhimu mkubwa kwani huduma zote za uwakala zitaunganisha na matawi hayo kwa ajili ya kuhakikisha viwango vya huduma zote zakibenki zinapatikana na kuzingatia taratibu zote za utoaji wa huduma za kibenki.

Huduma ya hii ya uwakala kwa mabenki inatolewa duniani kote na inatajwa kuwa moja ya njia rahisi na nyepesi ya kuwafikia wateja wengi hasa wasio na akaunti za Benki, aliongeza Mwita.

Benki ABC ambayo ni moja ya kampuni tanzu za Atlas Mara, ilishinda tuzo ya kuwa Benki bora Afrika kwa mwaka 2017 ambapo bado imeendelea kujidhatiti na kuenea zaidi hapa nchini kwa kufungua matawi mengi zaidi ambapo mwaka huu pia imejipanga kuzindua matawi mawili katika mkoa wa Dodoma na Mwanza.

 Meneja wa Kitengo Binafsi Benki ya ABC Joyce Malai akiongea na waandishi wa habari wa uzinduzi wa huduma za uwakala wa Benki hiyo kwa kushirikiana na Maxcom Africa Plc.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Maxcom Africa Plc Jameson Kasati akizungumza jijini Dar es Salaam na waandishi wa habari jana kwenye hafla ya kushirikiana na Maxcom Africa Plc kutoa huduma za kibenki.
 Meneja huduma za uwakala wa Benki ABC Mwita Robi akionyesha mashine ya uwakala wa huduma za kibenki jijini Dar es Salaam jana mara baada ya kuzindua huduma za hiyo jana.

Serikali yaipongeza Vodacom uorodheshwaji wa hisa DSE

$
0
0
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, amesema, uwekezaji mkubwa utakaofanywa na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania PLC baada ya kuorodheshwa rasmi katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) jana utasaidia kuongeza mapato ya Serikali na kuwezesha wananchi.

Kampuni hiyo jana ilijiorodhesha hisa zake DSE baada ya kuuza asilimia 25%  ya hisa zake ambapo kiasi cha shilingi bilini 476 kimefanikiwa kukusanywa.
Akizungumza wakati wa hafla fupi ya uorodheshaji wa hisa hizo, Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango,  alisema uoredheshwaji huo ni hatua muhimu ya kuwawezesha wananchi kiuchumi.

 “Mgawanyo wa hisa zilizouzwa kwa umma umefanyika kwa kutoa kipaumbele kwa wawekezaji wa ndani ya Tanzania ambapo wamepata aslimia 100% ya maombi yao ya waliofanya katika ununuzi wa hisa zilizouzwa kwa umma na hivyo hivyo wawekezaji wa ndani kupata asilimia 60% na wawekezaji wa kimataifa asilimia 40%,”.

Waziri Mpango alisema kipaumbele kimetolewa kwa wawekezaji wa ndani ili kuwezesha Watanzania kuwa washiriki katika maendeleo ya uchumi wa nchi yao badala ya kuachwa pembeni ya mageuzi na maendeleo ya kiuchumni yanayotokea hapa nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao alimwambia Waziri Mpango kuwa fedha zilizokusanywa zitatumika kufanya uwekezaji zaidi na hivyo kuwafanya wawekezaji wapya kunufaika na uwekezaji wao ndani ya Vodacom Tanzania.

“Tutaendelea kufanya uwekezaji mkubwa na wenye tija kwa ajili ya wanahisa wetu. Vodacom ndiyo kampuni ya simu za mkononi inayoongoza na kupitia uwezeshaji huu wa kimtaji tunatarajia kukuwa zaidi,”alisema
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana Dk John Mduma alisema mafanikio hayo yanaleta chachu ya maendeleo na mageuzi katika sekta ya masoko ya mitaji na fedha hapa nchini na katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, (kulia)akipiga kengele kuashiria kuorodheshwa rasmi kwa hisa za kampuni ya Vodacom Tanzania PLC katika Soko la Hisa la Dar es Salaam jana. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Ian Ferrao na Afisa Mtendaji Mkuu wa DSE Moremi Marwa.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, (kulia) akimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao (katikati) kuhusiana na kufanikisha kuorodheshwa rasmi kwa hisa za kampuni yake katika Soko la Hisa la Dar es Salaam jana.Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa DSE Moremi Marwa.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, (wapili kulia) Mwenyekiti wa bodi ya soko la hisa, John Mduma (kulia) na Afisa Mtendaji Mkuu wa DSE Moremi Marwa wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC,Ian Ferrao akifafanua jambo wakati wa Uzinduzi wa hafla ya kuorodheshwa rasmi kwa hisa za kampuni ya Vodacom Tanzania PLC katika Soko la Hisa la Dar es Salaam jana.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, akiongea wakati wa  hafla ya  Uzinduzi wa kuorodheshwa rasmi kwa hisa za kampuni ya Vodacom Tanzania PLC katika Soko la Hisa la Dar es Salaam jana. Katikati ni Afisa Mtendaji Mkuu wa DSE Moremi Marwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao.

FAIDA YA SERIKALI KUGHARAMIA ELIMU BURE NI WANAFUNZI KUFAULU–PROFESA NDALICHAKO.

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga  akizungumza wananchi na wanafunzi katika shule ya Sekondari Nasibugani.
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akizungumza wananchi na wanafunzi katika shule ya Sekondari Nasibugani.
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia , Profesa Joyce Ndalichako akizindua mabweni mawili katika Shule ya Sekondari Nasibugani  iliyopo Wilaya ya Mkuranga.
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako akipanda mti katika shule ya Sekondari Nasibugani.
  Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia , Profesa Joyce Ndalichako akizindua mabweni mawili yaliyokamilika katika shule sekondari Mwinyi iliyopo Wilaya ya Mkuranga.
.Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mkuranga, Mshamu Munde akizungumza wananchi na wanafunzi katika shule ya Sekondari Nasibugani.

Na Chalila Kibuda , Globu ya Jamii.
SERIKALI inatoa  sh. bilioni 18.77  kwa ajili ya kugharamia elimu bure ili kila mtanzania apate elimu bora ili wanafunzi wanafaulu darasa la Saba na Kidato cha Nne na kuendelea na elimu ya kidato cha tano na hadi chuo kikuu.

Hayo ameyasema leo Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako  wakati wa uzinduzi mabweni katika shule ya  sekondari Nasibugani ambayo ujenzi wake uko katika hatua ya mwisho  pamoja na Shule ya Sekondari  Mwinyi ambayo ujenzi umekamilika kwa kuingia wanafunzi  katika mabweni hayo wilayani Mkuranga mkoani Pwani.

Profesa Ndalichako amesema serikali ya awamu ya tano imeondoa gharama katika shule ya msingi na sekondari  ili kuondosha mzigo kwa wazazi ambao walikuwa wanashindwa kugharamia elimu hiyo.

Amesema mabweni yaliyojengwa katika shule ya sekondari Nasibugani na Mwinyi zenye Kidato cha Kwanza hadi Sita ni kuongeza sehemu ya kumwezesha mwanafunzi kusoma kwa muda mrefu na kuweza kondokana na vishawishi vinavyopatikana mtaani.

Aidha amesema kuwa serikali itaendelea  kuboresha shule na makazi ya walimu yaliyo bora pamoja na huduma zingine ikwemo umeme katika shule ya Sekondari Nasibugani. pia Mkuranga iko nyuma kielimu ni ukweli usiofichika hivyo walimu pamoja na watendaji kuhimiza suala la elimu ili viwanda vilivyopo na wanamkuranga wanufaike na sekta hiyo.

Waziri Profesa Ndalichako amempongeza  Mbunge wa Mkuranga Abdallah Ulega kuanzisha Program kwa wanafunzi wa sekondari kuwa Hakuna Kufeli. Amesema Program hiyo ifanywe kwa vitendo kwa wanafunzi kujitoa zaidi kusoma kwani mtihani uko karibu lakini wakitumia program hiyo watafanya vizuri na kuondoa sifuri katika shule zao na kuanza daraja la kwanza hadi la tatu.
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live




Latest Images