Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live

TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI YAITAHADHARISHA CUF

0
0
Na Margareth Chambiri, NEC

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imekishauri Chama cha Wananchi (CUF) kumaliza mgogoro unaoendelea ndani ya Chama hicho kwani unaweza kusababisha kupoteza nafasi za Udiwani katika Uchaguzi Mdogo unaotarajiwa kufanyika wakato wowote kuanzia sasa.

Tahadhari hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume hiyo Bw. Kailima Ramadhani katika mahojiano maalum Ofisini kwake kuhusu tuhuma  mbalimbali zilizoelekezwa Tume hiyo ikiwemo suala la Uteuzi wa Wabunge wa Viti Maalum kupitia CUF.
Bw. Kailima amesema mvutano unaoendelea ndani ya Chama cha Wananchi (CUF) hauna tija, hivyo ameshauri pande mbili zinazovutana kukutana na kumaliza tofauti zao kwani hali hiyo itawanyima nafasi ya kutoa wagombea kwenye uchaguzi huo mdogo.

 ‘Mimi niwashauri, CUF wana mgogoro wao wamalize mgogoro wao. Ni vizuri wakutane wamalize mgogoro wao kwani hii inaweza kuwaletea matatizo wagombea wakati wa Uchaguzi.’ alisesema Kailima na kusisitiza kuwa mgogoro ndani ya chama hicho hauna tija na badala yake unakidhoofisha. 

Amesema Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, inakitaka Chama cha Siasa kumsimamisha Mgombea mmoja kwa nafasi moja, lakini pia mgombea wa nafasi ya Rais na Mbunge  lazima fomu yake isainiwe na Viongozi wa ngazi ya Taifa wanaotambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa.

‘Lakini ukisoma Maelekezo ya Vyama vya Siasa na Wagombea yanasema iwapo chama cha Siasa kina mgogoro ni lazima fomu zake zisainiwa na kiongozi wa juu wa ngazi ya Mkoa, sasa kwa hali hii iwapo CUF wasipokutana watapoteza nafasi.’ Amesema Mkurugenzi huyo wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.  

Bwana Kailima amesema Tume ya Taifa ya Uchaguzi inatambua taarifa za Vyama vya Siasa iliyowasilishwa na Msajili wa Vyama vya Siasa na kwa Chama cha CUF viongozi wanaotambuliwa na Tume hadi hivi sasa ni Mwenyekiti Prof. Ibrahim Lipumba na Katibu Mkuu ni Maalim Seif Sharif Hamad. 

‘Tume inatambua kuwa Mwenyekiti wa CU ni Prof. Ibrahim Lipumba, Inatambua Katibu Mkuu wa CUF ni Maalim Seif Sharif Hamad na Naibu Katibu Mkuu upande wa Bara ni Magdalena Sakaya’ amesema.

Amesema Tume haijazuiliwa na Mahakama wala na Msajili wa Vyama vya Siasa kwamba isifanye mawasiliano na Viongozi hawa, na kubainisha kuwa Tume itaendelea kufanya mawasiliano na Viongozi mpaka hapo itakavyoelekezwa vinginevyo na Msajili wa Vyama au Mahakama.

Mkurugenzi huyo wa Uchaguzi amesema Tume inafanya kazi kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na Taratibu na kwamba mawasiliano ya Tume na Chama cha Siasa ni kwa mujibu wa maelekezo ya Msajili wa Vyama vya Siasa ambaye ndiye anayesajili Vyama vya Siasa nchini.  

Aidha katika hatua nyingine Bwana Kailima ameelezwa kusikitishwa na taarifa za upotoshaji zinazoihusisha Tume kwenye kikao cha Wanasheria kwa lengo la kumshauri Spika wa Bunge kuhusu Chama cha Wananchi CUF na kubainisha kuwa taarifa hizo hazina ukweli wowote.

 Akielezea hatua zinazoweza kuchukuliwa na Tume dhidi ya upotoshwaji unaofanywa na baadhi ya Wanasiasa na Vyombo vya Habari kuhusu utendaji kazi wa Tume Kailima amesema Tume itatumia Mamlaka zinazohusika na usajili ingawa hata hivyo amesisitiza kuwa ni vyema Vyama vya Siasa vitumie Wanasheria wao kusoma Sheria na taratibu za Uchaguzi ili kupata habari sahihi.

‘Hatua ya kwanza tunayochukua ni hii ya kuelimisha Chama pengine ni bahati mbaya lakini hatua ya pili ni ya kuzitaarifu mamlaka Kwa upande wa Vyama ni Msajili wa Vyama kwa upande wa Vyombo vya Habari vya Magazeti tunamtaarifu Msajili wa Magazeti ili ashughulike nao’ lakini kubwa tunawashauri jamani someni au ulizeni Tume,’ amesema Kailima. 

VIJIJI VYOTE KUWA NA UMEME IFIKAPO 2021 –DKT. KALEMANI

0
0
Na Tiganya Vincent
Serikali imesema kuwa jumla ya vijiji 7873 na vitongoji vyake vyote hapa nchini vitakuwa vimeshaunganisha na umeme chini ya Mradi wa Umeme Vijijini Awamu wa Tatu ifikapo mwaka 2021.

Kauli hiyo imetolewa jana mjini Tabora  na Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani wakati alipomtembelea Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bw. Aggrey Mwanri.
Dkt. Kalemani alisema REA III itasaidia kukamilisha vijiji vilivyobaki ambavyo havijaunganishwa na umeme ifikapo mwaka 2021 kwa ajili ya kuchochea maendeleo ya uchumi kati kuelekea uchumi wa viwanda.
Alisema kuwa lengo la Serikali ni kutaka wananchi wote hata wale wanaoishi visiwani waweze kufikiwa na huduma ya umeme kwa ajili ya matumizi yao na kwa ajili ya uendeshaji wa viwanda.
Aidha kwa upande wa Mkoa wa Tabora alisema vijiji vipatavyo 510 na vitongoji vyake vinatarajiwa kuwa vimeshaunganishwa na umeme wa uhakika wa ifikapo mwaka 2021 kupitia mradi wa REA III.
Aliongeza kuwa ili kuhakikisha lengo hilo la kuunganisha vijiji vyote vinakuwa na umeme, Serikali imeamua kuweka Wakandarasi wengi katika kila mradi na kuwaagiza kugawa kazi kwa Wakandarasi wadogo ambao ni wazawa na wenye sifa ili kurahisisha kazi na kuifanya iwe na ufanisi.
Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bw. Aggrey Mwanri alisema kukamilika kwa mradi wa REA III utaufanya mkoa huo kukua kwa kasi zaidi na kutoa wito kwa wawekezaji kuja kuwekeza katika viwanda vya sekta mbalimbali ikiwemo za usindikaji wa mazao ya kilimo na mifugo na uchimbaji madini.
Alisema kuwa hivi sasa Mkoa huo unazidi kuimarika katika miundombinu ya barabara , reli , anga na upatikanaji wa maji  na umeme wa uhakika na hivyo kutokuwepo na vikwazo katika uzalishaji.
Uzinduzi wa uunganishwaji mradi wa umeme vijijini kwa awamu ya tatu unatarajiwa kufanyika tarehe 1 Agosti 2017 katika Wilaya ya Sikonge kwa niaba ya Wilaya zote za Mkoa wa Tabora.

RAIS DK.SHEIN AZUNGUMZA NA UONGOZI BODI SHIRILA LA MELI,BANDARI NA MAMLAKA YA USAFIRI BAHARIN

0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji pamoja na Uongozi wa Bodi ya Wakurugenzi  wa Mamlaka ya Usafirishaji Baharini na Uongozi wa Mamlaka ya Usafirishaji  Baharini katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji pamoja na Uongozi wa Bodi ya Wakurugenzi  ya Shirika la Meli na Uongozi wa Shirika la Meli Zanzibar katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo.
 Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi  ya Shirika la Meli na Uongozi wa Shirika la Meli Zanziba wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji pamoja na Bodi hiyo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo (Picha na Ikulu).

MWENYEKITI CHARLES MAKOGA : SHERIA MPYA KUTUMIKA KUKUZA MAPATO YA MJI WA MAFINGA

0
0
Mwenyekiti wa halmashauri ya Mafinga Mjini Charles Makoga akizungumza wakati wa baraza la madiwani wa halmashauri hiyo
Baadhi ya madiwani wa halmashauri ya Mji wa Mafinga wakiwa katika baraza pamoja na wataalamu mbalimbali wa halmashauri hiyo.


Na fredy Mgunda, Mafinga

Halmashauri ya Mji wa Mafinga mkoni Iringa inatarajia kukuza mapato katika mwaka Mpya wa 2017/2018 kutokana na kuanza kuzitumia sheria mpya za ukusanyaji mapato pamoja na kuvijua vyanzo vingine vya mapato ambavyo ndio vitasababisha kukuza uchumi wa halmashauri hiyo.

Akizungumza wakati wa baraza la madiwani Mwenyekiti wa halmashauri ya Mafinga Mjini Charles Makoga alisema kuwa sheria mpya walizoletewa toka mwezi wa tano zinawapa nafasi ya kuanza kuzitumia wakati wa kukusanya mapato katika maeneo ambayo walikuwa hawakusanyi.

"Tulikuwa hatukusanyi mapato katika maeneo ya stand,sehemu za maegesho ya magari,sokoni na maeneo mengine kwa kuwa sheria zilikuwa bado si rafiki kwetu kwenda kukusanya mapato ila kwa mwaka unaoanza tutakusanya mapato na kukuza mapato kutoka asilimia 56 hadi kuvuka lengo la serikali la asilimia 80" alisema Makoga

Makoga aliwataka wananchi na viongozi kushiriana kukusanya mapato kulingana vyanzo ambavyo madiwani wameviolozesha kwa manufaa ya halmashauri ya Mafinga Mjini ambavyo vipo kisheria kutoka serikali kuu.

Jamani naombeni mchango wetu kufanikisha swala hili la kukusanya mapato ili tufikie lengo la serikali kwa kuwa mwaka huu hatufikia lengo hilo ni aibu kubwa kwa serikali hii ya awamu ya tank ambayo inaenda kwa kasi kubwa kwa kukuza uchumi wa nchi.

Nao baadhi ya madiwani wa halmashauri ya mji wa mafinga Zacharia Vang'ota wa kata changarawe,Chesco lyuvale wa Kata ya kinyanambo walimtaka Mwenyekiti wa halmashauri hiyo kuzisimamia ipasavyo sheria ambazo zimetungwa na halmashauri pamoja na serikali ya jamhuli ya muungano wa Tanzania chini ya Rais Dr John pombe Magufuli ili kukuza mapato katika halmashauri hiyo.

"Ukiangalia hapa Mafinga tunavyanzo vingi vya mapato lakini watalaamu wetu hawavifanyii kazi ndio maana sisi madiwani tumeamua kuanzia sasa vyanzo vyote tulivyovibainisha leo kwenye baraza vifanyiwe kazi haraka sana ili kukuza mapato ya halmashauri yetu"walisema madiwani

Kwa upande wao baadhi ya wananchi wa Mafinga Mjini walisema kuwa Mji huo una changamoto nyingi hivyo serikali ya mji inatakiwa kuanza kuzitumia hizo sheria Mpya haraka ili hata wananchi wayatambue maeneo yanayopaswa kulipa kodi na kuewezesha halmashauri kukuza mapato na kutatua changamoto za Mji wa Mafinga.

"Angalieni nyie waandishi Mafinga maji ni tatizo kubwa,Barbara bado hazijatengenezwa hasa huku mitaani kwetu,Mji bado mchafu kila mtu anatupa takataka anavyotaka kwa kuwa hakuna mtu wa kumkamata ila ukiangalia sheria Mpya zipo lakini hazifanyiwi kazi na Mafinga maeneo ya maegesho ya magari hayalipiwi wakati miji mingine ni moja vya mapato hivyo viongozi wanapaswa kuanza kuzitumia sheria Mpya" walisema wananchi

NBC YASHEREHEA MIAKA 50 PAMOJA NA KUZINDUA KLABU YA BIASHARA JIJINI MWANZA.

0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella (katikati), akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi baada ya kuzindua Klabu ya Biashara mjini Mwanza hivi karibuni. Kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya NBC, Dk. Kassim Hussein. NBC imezindua Klabu ya Biashara iliyopewa jina la ‘NBC B-Club’ katika miji ya Kahama na Mwanza kwa kuandaa semina kwa wafanyabishara wajasiriamali.   NBC B-Club itasaida  huduma zisizo za kifedha kupitia mafunzo maalumu kwa kushirikiana  na wadau mbalimbali kuhusu mbinu za uendeshaji wa biashara na kuwajengea uwezo katika kuziendesha kwa ufanisi hivyo kukuza biashara hizo. 
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi akihutubia wakati sherehe za uzinduzi rasmi wa Klabu ya Biashara jijini Mwanza hivi karibuni. Wengine kutoka kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya NBC, Dk. Kassim Hussein, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, aliyekuwa mgeni rasmi na Mkurugenzi wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Filbert Mponzi.
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akihutubia wakati wa semina ya wafanyabiashara katika uzinduzi rasmi wa Klabu ya Biashara ya NBC mjini Mwanza. Wengine kutoka kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya NBC, Dk. Kassim Hussein, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi na Mkurugenzi wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Filbert Mponzi. 
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella (katikati), akizungumza na ujumbe wa viongozi wa NBC waliofika ofisi kwake kumtembelea wakiongozwa na Dk. Kassim Hussein (kulia kwake) na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theoblad Sabi (kushoto kwake). NBC ilizindua klabu za biashara katika miji ya Kahama na Mwanza pamoja na kusherehekea miaka 50 tokea ilipoanzishwa.    
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi akizungumza katika sherehe za maadhimisho ya mika 50 ya benki hiyo mjini Mwanza.
 
 Mjumbe wa Bodi ya NBC, Dk. Kassim Hussein (mwenye tai nyekundu), Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Theobald Sabi na  Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mary Tesha pamoja na wateja na waalikwa wengine wakijipiga picha maarufu kama ‘selfie’ kama moja ya shamrashamra za maadhimisho ya miaka 50 ya NBC jijini Mwanza.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AKAGUA MIRADI WILAYA YA MBEYA MJINI

0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua Methadone Clinic ambao ni maalum kwa kuwahudumia na kuwapa ushauri nasaha waathirika wa madawa ya kulevya kwenye . hospitali ya Rufaa ya Mbeya Julai 31, 2017. Kushoto ni Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PMO_7118
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa  Salim Jessa  (wanne kushoto) ambaye ni  Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha Malumalu kilichopo Iyunga jijini Mbeya  wakati alipoembelea kiwanda hichi Julai 31, 2017.  Watatu kushoto ni Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson Mwansasu. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PMO_7147
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa  Salim Jessa  (kulia) ambaye ni  Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha Malumalu kilichopo Iyunga jijini Mbeya  wakati alipoembelea kiwanda hicho Julai 31, 2017. Kushoto kwake ni Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson Mwansasu. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PMO_7255
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akipokea maua kutoka kwa mtoto , Felista (4) wa Shule ya Wenye Ulemavu ya Child Support Tanzania ya jijini Mbeya baada ya kuwasili kwenye kiwanda cha vinywaji baridi cha SBS – PEPSI kilichopo eneo la Iyunga jijini Mbeya Julai 31, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PMO_7266
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na watoto wa Shule Wenye Ulemavu ya Child Support Tanzania ya jijini Mbeya baada ya kuwasili kwenye kiwanda cha vinywaji baridi cha SBS- Pepsi kilichopo Iyunga jijini Mbeya Julai 31, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PMO_7364
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitembelea kiwanda cha vinywaji baridi  cha SBS- Pepsi kilichopo eneo la Iyunga jijini Mbeya, Julai 31, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PMO_7413
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia wakazi wa Mbeya baada ya kuwasili kwenye Viwanja vya  Ruanda Nzove jijini humo kuhutubia mkutano wa hadhara, Julai 31, 2017. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PMO_7422
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta jambo na Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PMO_7441
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia mkutano wa hadhara kwenye Viwanja vya  Ruanda Nzove jijini Mbeya Julai 31, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

DC MNDEME AMPONGEZA MAVUNDE KWA KUTATUA KERO YA MAJI KWA WANANCHI WAKE

0
0
Mkuu wa wilaya ya Dodoma Christine Mndeme akiwa ameketi katika mmoja ya kaya za wakazi wa Mhande akipata chakula baada ya kuzindua mradi wa maji.
Mkuu wa wilaya ya Dodoma Christine Mndeme akifurahi jambo na wafadhili wa mradi wa maji wa Mhande kutoka Canada.
Wananchi wa Mhande wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Chritine Mndeme katika uzinduzi wa mradi wa maji wa kijiji hicho.
Mkuu wa wilaya ya Dodoma Christine Mndeme pamoja na Father Fransis wakifungua bomba la maji kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Mhande.
Mkuu wa wilaya ya Dodoma Christine Mndeme akifurahi jambo na akina mama wa kijiji cha Mhande
Mkuu wa wilaya ya Dodoma Christine Mndeme akisalimiana na father Fransis
Mkuu wa wilaya ya Dodoma Christine Mndeme akiteta jambo na Brother Anthony ambaye ni muasisi wa mradi wa CPPS.
Mkuu wa wilaya ya Dodoma Christine Mndeme akikagua eneo la pampu ya maji ya mradi wa maji wa Mhande.
Mkuu wa wilaya ya Dodoma Christine Mndeme akicheza ngoma baada ya kuzindua mradi wa maji
Mkuu wa wilaya ya Dodoma Christine Mndeme akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mhande

……………………………………………………………..

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Christine Mndeme leo amezindua mradi wa Maji katika kijiji cha Mhande,Kata ya Ngh’ong’hona ambao umefadhiliwa na Shirika shirika la wamishionari wa damu takatifu ya Yesu(CPPS) uliogharimu kiasi cha Sh.Milioni 35.

Mradi huu umetokana na maombi ya Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Anthony Mavunde kwa Shirika la hilo kusaidia kutatua changamoto ya Maji katika kata hii ya Ngh’ongh’ona ambayo wananchi wake wamekuwa wakisumbuliwa na tatizo kubwa la upatikanaji maji safi na salama.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mndeme amelishukuru shirika hilo la CPPS kwa ufadhili wa mradi huo na kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Anthony Mavunde kwa kuwa mstari wa mbele kutatua kero za wanachi wake hususani kero kubwa ya Maji katika kata ya Ngh’ongh’ona.

Amesema kutatuliwa kwa kero hiyo kumewatua kina mama ndoo kichwani kwa kuwa walikuwa wakienda kuchota maji umbali mrefu.

“Mwili unahitaji maji unapotafuta maji mbali roho inasononeka hata muda wa kusali unaukosa, tunashukuru sana shirika hili lakini wananchi tuna wajibu wa kuutunza mradi huu ambao ni wa thamani kubwa sana,”amesema

Hata hivyo amesema hatasita kuwachukulia hatua watu watakaoharibu miundombinu ya mradi huo wa maji huku akiwataka kuunda kamati ya maji ili kuendesha mradi huo.

Aidha amesema kwa kushirikiana na Mavunde watashughulikia upatikanaji wa umeme katika mradi huo wa maji ili uweze kutoa huduma ipasavyo kwa wananchi.

Naye, Diwani wa Kata hiyo Philipo Nangu amesema wananchi hao wamekuwa wakipata adha kubwa ya maji na kulazimika kutembea umbali wa zaidi ya kilomita 10 kufuata huduma hiyo vijiji jirani jambo lilosababisha kushindwa kufanya shughuli za kimaendeleo.

Kadhalika, Mavunde amesema amefanikiwa kupata ufadhili wa Shirika la GIZ la Ujerumani ambao watasaidia kusambaza huduma hiyo ya maji katika kata yote ya Ngh’ong’hona ili kumaliza changamoto ya Maji kwenye eneo hilo.

MANISPAA YA KINONDONI YAKABIDHIWA SHULE YA SEKONDARI MAENDELEO

0
0

Meya wa Manispaa ya Kinondoni,Benjamin Sitta akizungumza na watumishi  wa serikali na wanafunzi mapema jana katika hafla ya kupokea msaada wa shule ya sekondari ya Maendeleo yenye thamani ya sh milioni 800 iliyojengwa na kampuni ya magari ya (KIA) ya Korea Kusini na Good Neighbors jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Good Neighbour ambao ndio wadhamini wa shule hiyo,Namun Heo akizungunza na watumishi wa serikali katika hafla ya kukabidhi majengo ya shule ya sekondari ya Maendeleo yenye thamani ya sh milioni 800 iliyojengwa na kampuni ya magari ya (KIA) ya Korea Kusini na Good Neighbors,jijini Dar es Salaam. 
Meya wa Manispaa ya Kinondoni,Benjamin Sitta (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Good Neighbour,Namun Heo (kulia) wakisani hati ya makabidhiano ya shule ya sekondari ya Maendeleo iliyojengwa na kampuni ya magari ya (KIA) ya Korea Kusini na Good Neighbors,mapema jana jijini Dar es Salaam.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni,Benjamin Sitta (wa kwanza kushoto) akiwa ameambata na watumishi wa serikali wakikagua moja ya majengo ya shule hiyo. 

Muonekano wa shule ya sekondari ya Maendeleo yenye thamani ya sh milioni 800 iliyojengwa na kampuni ya magari ya (KIA) ya Korea Kusini na Good Neighbors jana jijini Dar es Salaam.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

JAFO APONGEZA MSHIKAMANO WA VIONGOZI NA WATENDAJI RORYA

0
0
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikata utepe na kuweka jiwe la msingi katika shule ya sekondari Nyamtinga wilayani Rorya.
Baadhi ya vyumba vya madarasa vilivyokaguliwa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo.
Mbunge wa Vitimaalum Agnes Marwa akizungumza na wananchi wakati wa ziara ya Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akizungumza na wananchi wa Rorya na kuwapongeza kwa ujenzi wa madarasa na mabweni.

………………………………………………………………..
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo amewapongeza viongozi na watendaji wa wilaya na halmashauri ya wilaya ya Rorya kwa mahusiano mazuri waliyonayo katika kuwaletea wananchi maendeleo.
Jafo alitoa sifa hizo alipokuwa wilayani humo kwa ziara ya kikazi ya kukagua miradi na kuongea na watumishi .

Katika ziara hiyo, Jafo alifanikiwa kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa, mabweni, maabara, na vyoo kwa sekondari ya Nyamtinga na Nyamunga ambapo majengo hayo yamebainika kujengwa kwa ubora wa kuridhisha. 

Ujenzi wa miundombinu hiyo imegharimu zaidi ya sh.milioni 500 kutoka serikali kuu kwa lengo la kuboresha elimu hapa nchini
Kwa upande wake,Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mara, Agness Marwa amempongeza Naibu Waziri huyo kwa kufika wilayani Rorya na kwamba amekuwa Waziri pekee aliyefanikiwa kutembelea wilayani humo katika kipindi hiki cha serikali ya awamu ya tano. 

Mbunge huyo ameishukuru serikali kwa upendo wake wa kuisaidia wilaya hiyo miradi ya maendeleo. Naibu Waziri Jafo leo amekamilisha ziara yake ya kikazi ya siku sita ya kukagua miradi ya maendeleo na kuongea na watumishi kwa mkoa wa Kagera na Mara na anaendelea na ziara yake katika mikoa mingine.

Dkt. Harrison Mwakyembe awaahidi BFT kuwatatulia kero ya eneo la Mafunzo

0
0
Na Benedict Liwenga-WHUSM.

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaana Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amewaahidi Shirikisho la Masumbwi Tanzania (BFT) kuwatatulia kero ya eneo la kufanyia mafunzo pamoja na ofisi ambalo limekuwa likiwakabili kwa muda mrefu zikiwemo na changamoto nyingine za Shirikisho hilo.

Mhe. Mwakyembe ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na baadhi ya Viongozi na wajumbe mbalimbali wa shirikisho hilo ikiwa ni sehemu ya kutambua utendaji kazi wao na changamoto zinazowakabili ili ziweze kutatuliwa.

Dkt. Mwakyembe amesema kwamba, kutokana na tatizo la ukosefu wa eneo rasmi la ofisi na sehemu ya kufanyia mafunzo, yeye atawasiliana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi ili kuona namna gani wanaweza kupata eneo kwa ajili ya kulisaidia shirikisho hilo kwa ajili ya kujenga ofisi na eneo la kufanyia mazoezi.

Sambamba na hilo, ameupongeza uongozi wa shirikisho hilo kwa kazi wanazozifanya na kuwataka wazidi kushirikiana na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) hususani katika kupeana taarifa zinazohusu maendeleo ya mchezo wa masumbwi nchini.

“BFT jitahidini muwe na ushirikiano wa karibu na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na msifanye mambo yenu kimya kimya, muwasiliane kwa karibu na BMT kwani hii itasaidia Wizara kushughulikia kero zenu mbalimbali kuliko mkichelewa kutoa taarifa mapema”, alisema Dkt. Mwakyembe.

Aidha, amewahakikishia kuwa, yupo tayari kutafuta wafadhili ndani na nje ya nchi ili waweze kulisaidia shirikisho hilo kutatua kero za uhaba wa vifaa, rasilimali fedha pamoja na ukosefu wa mafunzo kwa makocha.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo, Yusuph Singo amelitaka shirikisho hilo kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu za Serikali ikiwemo kujenga tabia ya ulipaji kodi, kuwaelimisha Wanamasumbwi kuachana na tabia chafu wanapokuwa michezoni pamoja na kuachana na kujihusisha na madawa ya kulevya.

Kwa upande wao Viongozi wanaounda shirikisho hilo pamoja na wajumbe kwa pamoja wamemuahidi Waziri Mwakyembe na Wizara kwa ujumla kuzingatia masuala mbalimbali ikiwemo kuboresha suala la mawasiliano kati ya Shirikisho na Wizara, kufuatilia suala la mikataba mbalimbali na uwajibikaji yakinifu.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akionyesha Jarida la Mpango Mkakati la Shirikisho la Masumbwi Tanzania (BFT) mara baada ya kufanya nao mazungumzo katika Ofisi za Wizara 01 Agosti, 2017 Jijini Dar es Salaam.

MSANII NAHREEL NA WASANII WENGINE WA MUZIKI WAENDELEA KUSUKA KOLABO COKE STUDIO 2017

0
0
 Nahreel aniwa na Aika (wa kwanza kulia) akiwa na wasanii wenzake katika studio za Coke Studio jijini Nairobi nchini Kenya.
Msanii Nahreel.
Mtayarishaji wa muziki na mwanamuziki nguli nchini Nahreel , akishirikiana na magwiji wengine wa kutengeneza muziki barani Afrika wanaendelea kusuka kolabo za wanamuziki wanaoshiriki onyesho la Coke studio linalotarajiwa kuanza kuonyeshwa kwenye vituo vya luninga mapema mwezi Septemba mwaka huu.
Ms ambaye jina lake halisi ni, Emmanue Mkono, amefanya nyimbo nyingi bora za wasanii mbalimbali nchini ambazo zinatamba katika soko la muziki ndani na nje ya nchi pia ni mmoja wa wanamuziki wa kundi machachari la NEVY KENZO.
Akiongea kuhusu onyesho hili akiwa jijini Nairobi nchini Kenya, Nahreel amesema kuwa misimu minne ya Coke Studio Africa imekuwa na mafanikio makubwa katika kuutangaza muziki wa Bongo Flava barani Afrika. Washiriki wamejiongezea mashabiki, wamejifunza mambo mengi kuhusu muziki kama burudani, muziki kama taaluma na muziki kama biashara na tena si tu kutoka kwa wasanii wenzao wa Afrika, bali wa Marekani pia.
Baadhi ya wakali wa kutengeneza muziki anaoshirikiana nao msimu huu ni Yuvir Pillay Nivedan a.k.a Sketchy Bongo kutoka Afrika ya Kusini na Kiff No beat kutoka nchini Ivory Coast.
Kwa upande wa ma DJ wapo Tafinha kutoka Angola, Laura Beg kutoka Mauritius, Jah Prayzah na Slapdee from Central Africa Republic, Bisa Kdei na Worlasi kutoka Ghana, Betty G kutoka Ethiopia, Bruce Melodie, Shellsy Baronet na Mr. Bow kutoka Msumbiji , Denise kutoka Madagascar ,Ozane kutoka Togo na Freeda kutoka Namibia.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Coca-Cola msimu wa Coke Studio mwaka huu utakuwa umesheheni burudani za muziki motomoto wenye vionjo vya Kiafrika kutokana na kuwaweka wasanii pamoja kutoka nchi 16 za Afrika na kushirikiana kufanya kolabo ambapo onyesho lake litaonyeshwa kwenye vituo vya luninga kwenye nchi zaidi ya 30 barani Afrika.
Wasanii wanaoshiriki Coke Studio msimu huu wanatokea katika nchi za Africa ya Kusini, Rwanda, Angola, Zimbabwe, Togo, Madagascar, Mauritius, Kenya, Uganda, Tanzania, Nigeria, Ghana, Msumbiji, DRC, Ethiopia, Cameroon. The last edition featured Kenya, Uganda, Tanzania, Nigeria, Ghana, Mozambique, DRC, Ethiopia, Cameroon, Cote d’ Ivoire, and Togo.
Tangia onyesho hili lianzishwe limekuwa kiungo kikubwa cha kuwakutanisha wanamuziki wa Afrika kufanya kazi kwa pamoja na kupiga muziki wenye vionjo kutoka sehemu mbalimbali za Afrika ikiwemo kuleta burudani kubwa kwa washabiki wa muziki wa kiafrika na kuwaunganisha waafrika hususani vijana kupitia muziki.
Wasanii wa Tanzania wanaoshiriki msimu huu wa Coke Studio 2017 ambao watafanya kolabo na wanamuziki kutoka nchini nyingine za Afrika ni Rayvanny, Izzo Bizness, Ali Kiba, na Nandy.Baadhi ya wasanii wakali wengine kutoka Tanzania waliowahi kushiriki onyesho hili ni Lady Jay Dee,Diamond Platinumz,Vanessa Mdee,John Makini,Shaa ,Ben Paul,Fid Q na kikundi cha Zanzibar Culture music Taarabu.

Mkuu wa Mkoa Iringa akabidhi Milioni 20 za Biko kwa mshindi wao

0
0
*Ally Issa Kumburu naye akabidhiwa Mil 10 zake Dar es Salaam 

MKUU wa Mkoa Iringa, Amina Masenza, jana ameshiriki kumkabidhi mshindi wa Sh Milioni 20 wa mjini Iringa, Viane Kundi, ambaye aliibuka na ushindi wa fedha hizo katika droo ya 27 iliyochezeshwa mwishoni mwa wiki.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, RC Masenza alimpongeza mshindi huyo pamoja na kumtaka atumie fedha hizo kujikwamua kiuchumi kutokana na mamilioni hayo.

Alisema mchezo wa bahati nasibu ni moja ya sekta inayoweza kuinua uchumi wan chi endapo washindi watazitumia fedha zao kwa uangalifu, huku akiwahamasisha Watanzania, wakiwamo akina mama kucheza kwa wingi.

“Biko ni mchezo mzuri hata mimi nitaanza kucheza, hivyo naomba Watanzania wote tucheze Biko ili tuweze kuibuka na zawadi mbalimbali za Biko, ukizingatia kuwa pesa hizi zitakuwa mwangaza kwa washindi wote,” Alisema.

Naye Mratibu wa Matukio na Mawasiliano wa Biko, Hassan Melles, alisema Biko ni mchezo unaotoa ushindi kwa kiasi kikubwa kwa washindi wake kuzoa zawadi za papo kwa hapo kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja inayoingia kwenye simu ya mshindi dakika chache baada ya kushinda.

“Bahati nasibu yetu inachezwa kwa njia ya ujumbe wa maandishi kwa kufanya miamala kwenye simu za Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel Money ambapo namba ya kampuni ni 505050 na ile ya kumbukumbu ni 2456,” Alisema.

Naye Viane mshindi wa Biko Milioni 20 Iringa, aliishukuru Biko, huku akisema fedha zake ataziingiza kwenye biashara ili ziweze kukuza uchumi wake, ukizingatia kuwa ndio kusudio lake kuu kuingia kwenye michezo ya kubahatisha.

“Nitafanya biashara kama sehemu ya kutimiza ndoto zangu kwakuwa tangu mwanzo nilikuwa namuomba Mungu niweze kushinda donge nono la Biko,” Alisema.

Katika hatua nyingine, mshindi wa droo maalum ya Komaa Concert iliyofanyika jana, Ally Issa Kumburu, naye alikabidhiwa Sh Milioni 10 zake alizoshinda katika tamasha la burudani lililodhamiwa na Biko.

“Nashukuru kwa kukabidhiwa fedha zangu leo jijini Dar es Salaam, katika tawi la benki ya NMB, ambapo ndio nimeamini kuwa nimeshinda, ukizingatia kuwa watu tulikuwa wengi na kila mtu alitaka ashinde,” Alisema huku akishuhudiwa na Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven.

Heaven aliwakumbusha Watanzania kuendelea kucheza Biko ili wajivunie zawadi za papo kwa hapo pamoja na Sh Milioni 20 zinazotoka katika droo ya Jumatano na Jumapili.


Mkuu wa Mkoa Iringa, Mheshimiwa Amina Masenza wa pili kutoka kulia akimkabidhi Sh Milioni 20 mshindi wa Biko droo ya 27, Viane Kundi wa mjini Iringa aliyeibuka kidedea Jumapili iliyopita. Wa kwanza kushoto ni Mratibu wa Matukio na Mawasiliano wa Biko, Hassan Melles na kulia ni mtumishi wa NMB, Iringa,
Mshindi wa Biko wa Sh Milioni 20 Viane Kundi akifurahia fedha zake baada ya kukabidhiwa jana mjini Iringa katika benki ya NMB.

Mshindi wa Sh Milioni 20 wa Biko kutoka mkoani Iringa, Viane Kundi akiwa na mume wake pamoja na mtoto wao wakifurahia donge nono la Biko baada ya kukabidhiwa katika benki ya NMB Mkoani Iringa.
Naye Mshindi wa droo maalum ya Komaa Concert ya Sh Milioni 10, Ally Issa Kumburu jana alikabidhiwa fedha zake katika benki ya NMB, tawi la Bank House, Posta, jijini Dar es Salaam. Kumburu ni mkazi wa Mwananyamala, jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Mheshimiwa Paulo Makonda wa pili kutoka kushoto akipiga picha ya pamoja kwenye zulia jekundu baada ya kuwasili katika Tamasha la Komaa Concert mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe na kudhaminiwa na Biko. Wengine pichani ni Mkurugenzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, James Mbalwe wa pili kutoka kulia, Mkurugenzi wa Biko, Charles Mgeta kushoto na Sadick Elimusu, Meneja Udhibiti wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania. Picha na Mpigapicha wetu.

WAZIRI MKUU ATEMBELA KIWANDA CHA PEPSI NA MABO

0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea kiwanda cha kampuni ya SBC Tanzania Ltd kinachotengeneza vinywaji baridi pamoja na kiwanda cha kiwanda cha kukata na kung’arisha mawe ya asili (mabo) cha Marmo Granito Mines Tanzania Ltd, vilivyoko katika eneo la Iyunga Mjini Mbeya.

Amevitembelea viwanda hivyo kwa lengo la kukagua utekelezaji wa sera ya kujenga uchumi wa viwanda nchini, ambao ndiyo kipaumbe cha Serikali ya Awamu ya Tano. Waziri Mkuu alivitembelea viwanda hivyo jana jioni (Jumatatu, Julai 31, 2017), akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Mbeya.

Akiwa katika kiwanda cha Pepsi, Waziri Mkuu alikagua maendeleo ya ujenzi wa upanuzi wa kiwanda  hicho kwa ajili ya kuanza uzalishaji wa vinywanji baridi kwenye chupa za plastiki, ambapo amewasihi Watanzania kupenda kutumia bidhaa zinazozalishwa kwenye viwanda vya ndani.

Pia Waziri Mkuu aliishauri kampuni hiyo kuendelea kupanua uwekezaji wake hapa nchini kwa kuwa Tanzania ina sera na mazingira mazuri ya uwekezaji. Kiwanda hicho kilijengwa mwaka 1999 kikiwa na wafanyakazi 75 na kwa sasa kina wafanyakazi 190.

“Nawashauri muendelee kuwekeza Tanzania kwani mbali na utulivu wa kisiasa pia sera na mazingira yake ya uwekezaji ni mazuri.”

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi kampuni SBC Tanzania Ltd. Bw. Atif Dar alisema kiwanda cha Mbeya ni cha pili kwa ukubwa wa mauzo ya vinywaji baridi vinavyotengenezwa na kampuni hiyo kikitanguliwa na kiwanda cha mkoa wa Dar es Salaam.

Alisema kwa sasa wanachukua soda zilizofungwa katika chupa za plastiki kutoka katika kiwanda chao cha Dar es Salaam, ambapo waliamua kupanua kiwanda hicho ili waanze kutengeneza soda zilizofungwa katika chupa za plastiki mkoani Mbeya baada ya mahitaji kuongezeka.

Bw. Dar alisema gharama za uwekezaji huo ni dola za Marekani milioni 3.5, ambapo mradi huo unatarajiwa kuanza rasmi Novemba 2017 ambapo mbali na kuuza katika soko la mikoa ya Nyanda za Juu Kusini pia watasafirisha katika nchi za Zambia na Malawi.

Pia Bw. Dar alimkabidhi Waziri Mkuu hundi ya sh. milioni 10 kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vifaa tiba katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Mbeya, ikiwa ni sehemu ya mchangamo wa kiwanda hicho katika uboreshaji wa shughuli mbalimbali za kijamii.

Awali Waziri Mkuu alitembelea kiwanda cha Marmo Granito Mines Tanzania Ltd
Waziri Mkuu alisema mbali na kukuza uchumi na kuongeza fursa za ajira nchini, viwanda hivvyo ndivyo vitakavyowawezesha wananchi tununua bidhaa kwa bei nafuu tofauti na ilivyo sasa kwa kuwa vitu vingi vinaagizwa kutoka nje ya nchi.

Pia aliwataka Watanzania wote hususani mashirika, taasisi, asasi na mamlaka za Serikali kujenga utamaduni wa kupenda kununua na kutumia na bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na  viwanda vilivyopo hapa nchini ili viweze kuimarika na kusaidia kutatua tatizo la ajira.
                            
Alitoa kauli hiyo badaa ya kutembelea kiwanda cha kukata na kung’arisha mawe ya asili (mabo) cha Marmo Granito Mines Tanzania Ltd, kilichoko katika eneo la Iyunga Mjini Mbeya. Kiwanda hicho kinatumia malighafi za hapa nchini.

Waziri Mkuu alisema mbali na kukuza uchumi na kuongeza fursa za ajira nchini, viwanda hivvyo ndivyo vitakavyowawezesha wananchi kununua bidhaa kwa bei nafuu tofauti na ilivyo sasa kwa kuwa vitu vingi vinaagizwa kutoka nje ya nchi.
 

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, AGOSTI 1, 2017

DKT. ALBINA CHUWA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU UNAOENDELEA MKOANI DODOMA

0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina  Chuwa (wa pili kulia) akizungumza na mmoja wa mafundi wanaojenga Jengo Jipya la Makao Makuu ya ofisi hiyo mkoani Dodoma wakati alipotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi huo. Wa kwanza kushoto ni Mhandisi John Ainainyi Njau kutoka Benki ya Dunia - Tanzania.
 Muonekano wa Jengo Jipya la Makao Makuu ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu linalojengwa mkoani Dodoma.
 Baadhi ya mafundi wakiwa wanaendelea na kazi ya ujenzi wa Jengo Jipya la Makao Makuu ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) linalojengwa mkoani Dodoma.
Baadhi ya Wakurugenzi na Maafisa waandamizi  wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wakiwa katika picha ya pamoja wakati walipotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo Jipya la Makao Makuu ya ofisi hiyo mkoani Dodoma. (PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO).

SERIKALI, WADAU KUANDAA RIPOTI YA KWANZA YA KITAIFA YA UTEKELEZAJI WA HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU NCHINI

0
0
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mara ya kwanza imeanza maandalizi ya ripoti ya utekelezaji wa haki za watu wenye ulemavu tangu Tanzania kuridhiria Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Watu wenye ulemavu mwaka 2009.

Katika kufanikisha suala hili, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeandaa kikao kazi kinachoshirikisha wadau wa haki za watu wenye ulemavu nchini ili kushirikiana katika maandalizi ya rasimu ya awali ya ripoti ambayo itajadiliwa,kuboreshwa na hatimaye kuwasilishwa katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa ikiwa ni hatua stahiki katika utekelezaji wa Mkataba wa Haki za watu wenye Ulemavu.

Kikao kazi hiki kinafanyika Mkoani Morogoro kuanzia leo tarehe 31 Julai 2017 mpaka tarehe 2 Agosti 2017 kwa lengo mahususi la kua na uelewa wa pamoja wa mfumo wa uandaaji ripoti za haki za watu wenye ulemavu wa Umoja wa Mataifa,kujadili na kutathmini utekelezaji wa Sheria ya Watu wenye Ulemavu,kutoa elimu kwa wadau kuhusu usimamizi na ulinzi wa haki za watu wenye ulemavu na kuandaa rasimu ya awali ya haki za watu wenye ulemavu.

Akifungua kikao kazi hicho,Ndugu Erick Shitindi , Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Vijana,Kazi,Ajira na Watu wenye Ulemavu ameeleza kuwa kwa mujibu wa kifungu cha 35 sehemu ya i na ii, ya Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Watu wenye Ulemavu, kila nchi inapaswa kuwasilisha ripoti ya kitaifa miaka miwili mara baada ya kuridhia mkataba husika jambo ambalo Tanzania haijwahi kulitekeleza kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa fedha kwa ajili ya maandalizi ya ripoti hiyo.

“Kwa mantiki hiyo,maandalizi ya ripoti hii yamekuja wakati muafaka na itaifanya Tanzania kuingia katika historia ya kutekeleza mikataba mbalimbali ya haki za binadamu ikiwemo haki za watu wenye ulemavu na kwa ujumla nchi ilishaanza kuchukua hatua ikiwa ni pamoja na kutunga Sheria ya watu wenye ulemavu (The Persons with Disabilities Act,2010)”.anasistiza Katibu Mkuu Shitindi.

Naye Bi. Sarah Mwaipopo, Mkurugenzi anayeshughulikia masuala ya Katiba na Haki za Binadamu,kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ameeleza kua Serikali inao wajibu kisheria kuratibu maandalizi ya ripoti na kutolea taarifa masuala mbalimbali ya utekelezaji wa haki za binadamu nchini kama ilivyoainishwa katika kifungu cha 14 cha Sheria ya Utekelezaji wa Majukumu ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ( Section 14 of the Attorney General (Discharge of Duties) Act,2005).

Pamoja na Katiba, Sheria na Mikataba mbalimbali ya Kimataifa kutambua haki za watu wenye ulemavu, Bwana Coomaaravel Pyaneandee, ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Haki za watu wenye ulemavu ya Umoja wa Mataifa aneleza kuwa zipo changamoto ambazo zimeendelea kuwepokatika usimamizi na utekelezaji wa haki za watu wenye ulemavu ambazo ni pamoja na ukosefu wa takwimu sahihi za idadi ya watu wenye ulemavu,unyanyapaa katika jamii na ngazi ya familia,kukosekana mfumo mzuri wa elimu jumuishi,asasi za kiraia kushindwa kutumia nafasi yake kufanya kazi vizuri na serikali hivyo kushindwa kupaza sauti ipasavyo,kutokua na uelewa kuhusu watu wenye ulemavu na mahitaji yao na ukosefu wa miundombinu stahiki katika sehemu mbalimbali kwa watu wenye ulemavu.

Wadau wanaoshiriki katika maandalizi ya rasimu ya awali ya ripoti ya haki za watu wenye ulemavu ni Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Tanzania Bara na Zanzibar,Chama cha watu wenye Ualbino Tanzania,Shirikisho la Watu wenye Ulemavu Tanzania, Tume ya Uchaguzi Tanzania Bara na Zanzibar, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora,Chama cha Walemavu wenye Utindio wa Ubongo,Chama cha Wazazi wenye watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi,Wizara ya Habari, Sanaa,Utamaduni na Michezo,Jeshi la Polisi Tanzania,Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii,Wizara ya Afya Zanzibar,Chama cha Watu walioumia Uti wa mgongo Tanzania,Under the Same Sun,Wizara inayoshughulikia masuala ya uwezeshaji wazee,watoto na watu wenye ulemavu Zanzibar na Chama cha Wasiiona Tanzania na Ofisi ya Taifa ya Takwimu.

JESHI LA ZIMAMOTO LAZINDUA KAMPENI YA NAMBA YA DHARURA 114 KUKABILIANA NA MAOKOZI YA MAISHA NA MALI

0
0
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uokoaji, Thobias Andengenye, akizungumza wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Namba ya Dharura 114, itakayotumiwa na wananchi kutoa Taarifa za majanga ya moto, ajali, mafuriko, tetemeko la ardhi na majanga mengine. Wengine ni Katibu Mtendaji wa Taasisi isiyo ya Kiserikali inayojishughulisha na kuzuia Uhalifu, ajali (UAC), Elliot Andrew na Naibu Kamishna Rasilimali Watu wa Jeshi hilo, Billy Mwakatage (kulia). Uzinduzi huo umefanyika leo Makao Makuu ya Jeshi, jijini Dar es Salaam. Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uokoaji, Thobias Andengenye, akikabidhiwa kipeperushi na Katibu Mtendaji wa Taasisi isiyo ya Kiserikali inayojishughulisha na kuzuia Uhalifu, ajali (UAC), Elliot Andrew(kushoto), wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Namba ya Dharura 114, itakayotumiwa na wananchi kutoa Taarifa za majanga ya moto, ajali, mafuriko, tetemeko la ardhi na majanga mengine. Kulia ni Naibu Kamishna Rasilimali Watu wa Jeshi hilo, Billy Mwakatage. Uzinduzi huo umefanyika leo Makao Makuu ya Jeshi, jijini Dar es Salaam. Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uokoaji, Thobias Andengenye, akionyesha kipeperushi   wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Namba ya Dharura 114, itakayotumiwa na wananchi kutoa Taarifa za majanga ya moto, ajali, mafuriko, tetemeko la ardhi na majanga mengine. Wengine ni Katibu Mtendaji wa Taasisi isiyo ya Kiserikali inayojishughulisha na kuzuia Uhalifu, ajali S(UAC), Elliot Andrew na Naibu Kamishna Rasilimali Watu wa Jeshi  wa jeshi hilo, Billy Mwakatage(kulia).Uzinduzi huo umefanyika leo Makao Makuu ya Jeshi,jijini Dar es Salaam.Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uokoaji, Thobias Andengenye, akionyesha mfano wa uwekaji stika yenye Namba ya Dharura 114, itakayobandikwa kwenye vyombo vya usafiri na maeneo mengine kwa ajili ya  kutumiwa  na wananchi kutoa Taarifa za majanga ya moto, ajali, mafuriko, tetemeko la ardhi na majanga mengine. Uzinduzi huo umefanyika leo, Makao Makuu ya Jeshi, jijini Dar es Salaam. Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.
 Maafisa wa Jeshi waliohudhuria Uzinduzi wa Kampeni ya Namba ya Dharura 114, itakayotumiwa na wananchi kutoa Taarifa za majanga ya moto, ajali, mafuriko, tetemeko la ardhi na majanga mengine, wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uokoaji, Thobias Andengenye (hayupo pichani) wakati wa Mkutano na Waandishi wa Vyombo vya Habari. Uzinduzi huo umefanyika leo, Makao Makuu ya Jeshi hilo, jijini Dar es Salaam. Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uokoaji, Thobias Andengenye (watano kulia), akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo, Viongozi na Wadau walioshirikiana na Jeshi hilo kuwezesha  Uzinduzi wa Kampeni ya Namba ya Dharura 114, itakayotumiwa na wananchi kutoa Taarifa za majanga ya moto, ajali, mafuriko, tetemeko la ardhi na majanga mengine. Uzinduzi huo umefanyika leo, Makao Makuu ya Jeshi, jijini Dar es Salaam.Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA HABARI NA ELIMU KWA UMMA-JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI, MAKAO MAKUU

WATUMISHI HOUSING WAPELEKA MRADI WA NYUMBA 500 MKOANI DODOMA

0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

KATIKA juhudi za kuunga mkono uamuzi wa serikali wa kuhamishia shughuli za serikali katika Mkoa wa Dodoma, Kampuni ya Watumishi Housing imepanga kuwajengea watumishi nyumba bora na za kisasa Mkoani humo.

Kampuni hiyo yenye dhamana ya uwekezaji katika nyumba ikiwa ni mpango wa taifa wa makazi kwa watumishi imeamua kuwekeza katika Mkoa wa Dodoma na wameshapata eneo la Njedengwa lenye ukubwa wa  hekari 55 likiwa limeshapimwa tayari kwa ujenzi wa nyumba 500.

Akielezea mikakati hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi Housing Fredy Msemwa amesema kuwa katika awamu ya kwanza ya ujenzi wa nyumba hizo zitajengwa nyumba 159 na zitakuwa kwa ajili ya watumishi watakaokuwa wamehamia Mkoani Dodoma na wale wanaoishi haoo.

Msemwa amesema, eneo la Njedengwa ni eneo ambalo limeendelezwa tayari likiwa lina huduma zote za kijamii ikiwemo barabara ya lami, maji, umeme na miundo mbinu mingine ambayo inalifanya kuwa eneo bora zaidi kwa makazi ya watumishi na yatai ujenzi umeshaanza na utakamilika baada ya miezi nane (8) na zitakuwa katika mfumo wa aina mbili zile zilizoisha kabisa na zitakazokuwa zimeisha kwa asilimia 80.

Nyumba hizo zitakuwa na mahitaji ya kutosha kabisa kwa watumishi wa umma wa kipato tofauti na utapatikana kwa njia ya mkopo endelevu kupitia benki washirika huku nyumba zilizokamilika kabisa zitauzwa kwa shilingi milioni 56 na zile zilizokamilika kwa asilimia 80 zitakuwa kwa milioni 46 zote zikiwa pamoja na VAT.

Mbali na hilo, Msemwa amesema wamepokea msaada wa vifaa vya upimaji wa viwanja na miji kutoka benki ya Dunia kwahiyo itarahisisha katika upimaji wa viwanja na pia kuanza kutoa huduma zote za makazi kuanzia uuzaji wa viwanja vilivyopimwa pamoja na nyumba zilizokamilika na huduma hii itaanzia mkoani Dodoma.
  Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi Housing Fredy Msemwa  akielezea namba walivyojizatiti katika kuiunga mkono serikali uamuzi wa kuhamishia shughuli za serikali katika Mkoa wa Dodoma ikiwa imepanga kuwajengea watumishi nyumba bora na za kisasa Mkoani humo.
Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Watumishi Housing Raphael Mwabuponde akiwaelezea waandishi wa habari namna ya watumishi kupata nyumba hizo zitakazojengwa katika Mkoa wa Dodoma.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa wanafuatilia mkutano huo.

RAIS DKT MAGUFULI APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO WA MABALOZI WATANO WALIOTEULIWA KUZIWAKILISHA NCHI ZAO HAPA NCHINI

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Benedict Mashiba kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Tanzania nchini Malawi Benedict Mashiba akila kiapo cha uadilifu kwa Viongozi mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Malawi Benedict Mashiba mara baada ya tukio la uapisho Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za utambulisho kutoka kwa Balozi wa Vietnam hapa nchini Nguyeni Kim Doahn, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Vietnam hapa nchini Nguyeni Kim Doahn akipigiwa wimbo wa Taifa mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Balozi wa Vietnam hapa nchini Nguyeni Kim Doahn mara baada ya kumaliza mazungumzo pamoja na kupokea Hati za Utambulisho Ikulu jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Vietnam hapa nchini Nguyeni Kim Doahn katikati akipigiwa wimbo wa Taifa mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Indonesia hapa nchini Prof. Ratlan Pardede, Ikulu jijini Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Indonesia hapa nchini Prof. Ratlan Pardede, Ikulu jijini Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Vatican hapa nchini Mhashamu Askofu Mkuu Marek Solcynski, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Balozi wa Vatican hapa nchini Mhashamu Askofu Mkuu Marek Solcynski mara baada ya kupokea Hati zake za Utambulisho Ikulu jijini.
Balozi wa Ujerumani hapa nchini Dkt. Detlef Wachter akipigiwa wimbo wa Taifa mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kukabidhi Hati zake Utambulisho.
Balozi wa Ujerumani hapa nchini Dkt. Detlef Wachter akijitambulisha kabla ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Ujerumani hapa nchini Dkt. Detlef Wachter mara baada ya kupokea hati zake za Utambulisho Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za utambulisho kutoka kwa Balozi wa Uganda hapa nchini Richard Tumisiime Kabonero Ikulu jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma ya Brass Bendi ya Jeshi la Polisi ambayo ilifika Ikulu kwa ajili ya mapokezi ya Mabalozi mbalimbali kutoka nje ya nchi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Brass Bendi ya Jeshi la Polisi Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

SERIKALI YAONGEZA MUDA WA KUNYONYESHA KWA WATUMISHI WA UMMA NA MASHIRIKA NA SEKTA BINAFSI

0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii .

SERIKALI imeongeza masaa ya unyonyeshaji kwa watoto kwa watumishi wa serikali, mashirika pamoja sekta binafsi ili kuwezesha watoto kuwa na afya bora inayotokana na maziwa ya mama.

Hayo ameyasema Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati akifungua Wiki ya Unyonyeshaji, amesema kuwa mama mzazi baada ya kumaliza miezi mitatu ataingia kazini 3:30 na kuondoka saa 7:30 katika kumuwezesha mama kunyonyesha mtoto bila kuingiliwa na majukumu ya kikazi.

Ummy amesema kuwa watendaji wa Umma na mashirika pamoja na taasisi lazima wafanye hivyo katika kutambua umuhimu wa mama mzazi kunyonyesha kwa muda uliowekwa kwa kipindi cha miezi sita.

Amesema kuwa ni gharama kubwa katika kuhudumia watoto walio na utapiamlo ambao unatokana moja ni kukosa maziwa ya mama kwa muda mrefu hivyo kuepuka ni njia rahisi ikiwemo kutengwa kwa masaa hayo.

Waziri Ummy amesema kuwa suala la lishe lazima liangaliwe kwa ukaribu na wadau wote katika kuweza kuwaondoa watoto katika utapiamlo ambao unafanya kudumaa kwa akili.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Chakula na Lishe Nchini(TFNC), Joyceline Kaganda amesema jitihada mbalimbali zimekuwa zikifanyika juu ya masuala ya lishe na wadau kwa mifumo mbalimbali.

Amesema kuwa wiki ya unyonyeshaji wa kina mama ni muhimu katika katika ukuaji wa mtoto wa kumjenga katika afya bora.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Lishe nchini (Panita), Tumaini Mkindo amesema serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk. Pombe Magufuli imwemeka kipaumbele katika ubaoreshaji wa lishe nchini.

Amesema kuwa sera zimeweza kuongezeka katika masuala ya lishe ikiwa eneo la kipaumbele katika mpango wa taifa wa miaka mitano pamoja mikoa na halmashauri kuwa na bajeti ya lishe.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akipata maelezo juu masuala ya lishe kutoka kwa mtaalam wa lishe wa Taasisi ya Chakula lishe nchini (TFNC),Neema Joshua wakati maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji leo.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumza wakati wa ufunguzi wa wiki ya unyonyeshaji na uzinduzi usambazaji taarifa kwa njia ya simu leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chakula na Lishe Nchini(TFNC), Joyceline Kaganda akizungumza juu ya mikakati ya lishe na umuhimu wa unonyeshaji leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Lishe nchini (Panita), Tumaini Mkindo akitoa salamu za mashirika yasio ya kiserikali yanavyofanya kazi katika sehemu ya lishe kwa kuwa miradi mbalimbali.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akibonyesha kitufe kuashiria uzinduzi wa taarifa kupitia simu za mikoni katika ufunguzi wa wiki ya unyonyeshaji leo.
Sehemu ya wadau katika ufunguzi wa wiki ya unonyeshaji leo jijini Dar es Salaam.

WAKUU WA VYUO VYA MAENDELEO YA JAMII WAENDELEA NA MAFUNZO KUHUSU UDHIBITI WA VIASHIRIA HATARISHI KATIKA UTENDAJI WA VYUO MKOANI MOROGORO

0
0
Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii na Mwenyekiti wa Mafunzo Bw. Paschal Mahinyila akiwakaribisha washiriki katika mafunzo Wakuu wa vyuo hao kuhusu Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti mkoani Morogoro leo tarehe 01.08.2017. 
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii Bw. Patrick Golwike (kushoto) akifafanua umuhimu wa uadilifu kwa Wakuu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii(hawapo pichani) katika utendaji kazi wa vyuo wakati wa mafunzo kwa wakuu wa vyuo hao kuhusu Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Uendeshaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro leo.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Bibi Deodata Makani(kulia) akifafanua mambo mbalimbali ya kiutawala kwa Wakuu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii nchini katika mafunzo kwa wakuu wa Vyuo hao kuhusu Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro leo.
Mhasibu Mkuu kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Bibi Fatuma Oloo(kulia) akisisitiza jambo kuhusu udhibiti wa fedha kwa wakuu wa vyuo vya Maendeleo ya Jamii nchini katika mafunzo kwa wakuu wa vyuo hao kuhusu Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro.
Mkurugenzi wa Ugavi na Manunuzi kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Bibi Martha Chuma (katikati) akifafanua mambo mbalimbali yahusuyo ugavi na manunuzi kwa wakuu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii nchini katika mafunzo kwa wakuu wa Vyuo hao kuhusu Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro.
Mkuu wa Kitengo cha Sheria kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Bi. Vickness Mayao(kulia) akitoa maelekezo kuhusu mikataba na masuala mbalimbali ya kisheria kwa wakuu wa vyuo vya Maendeleo ya Jamii nchini katika mafunzo kwa wakuu wa Vyuo hao kuhusu Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro.
Mkaguzi wa ndani kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Bibi. Elightness Mchome(katikati) akifafanua umuhimu wa kuepuka hoja za ukaguzi kwa wakuu wa vyuo vya Maendeleo ya Jamii nchini katika mafunzo kuhusu Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo hivyo yanayoendelea katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro.
Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Monduli Bw. Salim Mgalla(kulia) akiuliza swali kwa wawezeshaji katika mafunzo kwa wakuu wa vyuo vya Maendeleo ya Jamii nchini katika mafunzo kwa wakuu wa vyuo hao kuhusu kuhusu Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro
Baadhi ya wakuu wa vyuo vya Maendeleo ya Jamii Nchini wakifuatilia wawasilishaji mada(hawapo pichani) katika mafunzo kwa wakuu wa vyuo hao kuhusu Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro.
Mratibu wa Usimamizi wa Viashiria Hatarishi Bw. Moris Jackson akifafanua masuala mbalimbali yahusuyo Viashiria Hatarishi kwa wakuu wa vyuo vya maendeleo ya Jamii Nchini katika mafunzo kwa wakuu wa vyuo hao kuhusu Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro.
Kaimu Mkuu wa Chuo (Utawala, Mipango na Fedha) Kutoka Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ruaha Bi.Nadhaherieth Mshighath akiuliza swali kwa wawasilishaji mada (hawapo pichani) katika mafunzo kwa wakuu wa vyuo hao katika mafunzo kwa wakuu wa vyuo hao kuhusu Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro.
Watendaji kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na washiriki kutoka Vyuo vya Maendeleo ya Jamii nchini wakifuatilia kwa makini mafunzo ya Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii nchini yanayofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro leo 01.08.2017. 

Picha na Erasto Ching’oro WAMJW.
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live




Latest Images