Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live

MBUNGE GULAMALI AFANYA ZIARA YA KUONA MAENDELEO YA UFUFUAJI WA KIWANDA CHA MANONGA GENERY

$
0
0
 Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali (kushoto) akioneshwa moja kamba na mmiliki wa kiwanda cha Manonga Genery, Urvesh Rajan zinatokana na zao la pamba katika kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho leo Wilayani Igunga kata ya Choma. Katikati ni katibu wa kiwanda cha Nyuzi Tabora. ( Picha zote na Raymond Urio ) 
 Mmiliki wa kiwanda cha Manonga Genery, Urvesh Rajan akizugumza na Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali (katikati), alipotembelea kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho leo Wilayani Igunga kata ya Choma. Kushoto ni Mwenyekiti wa Igombensabo Lazaro Ngullo .
 Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akipewa moja ya maelezo ya mashine ya ya zao la pamba ndani ya kiwanda cha Manonga Genery, leo alipotembelea kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho kilichopo Wilayani Igunga kata Choma.
 Mmiliki wa kiwanda cha Manonga Genery, Urvesh Rajan akimpa maelekezo Mbunge wa Manonga Seif Khamis Gulamali ndani ya kiwanda hicho (katikati), leo alipotembelea na kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda kilichopo Wilaya ya Igunga kata ya Choma.
 Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali (kushoto) akizungumza na Mwenyekiti wa Igombensabo.
 Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akiongozana na viongozi wa serikali pamoja na wahandisi alipotembelea kiwanda hicho leo kilichopo Wilayani Igunga kata ya Choma.
 Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali (katikati) akisikiliza kwa makini maelekezo kutoka kwa mmiliki wa kiwanda cha Manonga Genery, Urvesh Rajan leo alipotembelea kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho kilichopo Wilayani Igunga kata Choma.
Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akisaliamiana kwa furaha na mmiliki wa kiwanda cha Manonga Genery, Urvesh Rajan leo alipotembelea kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho kilichopo Wilayani Igunga kata Choma.

NA RAYMOND URIO
Mbunge wa Jimbo la Manonga kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Seif Khamis Gulamali leo ametembelea kiwanda cha Manonga Ginery kinachohusika na kutengeneza pamba, kilichokuwa kimesimama kwa takribani miaka ishirini (20) bila ya kufanya.

Mapema leo hii Mbunge Gulamali aliwasili katika eneo la kiwanda hicho, iliyopo Jimbo la Igunga Kata ya Choma akiwa pamoja na Mmiliki wa kiwanda hicho, ndugu Urvesh Rajan pamoja na viongozi wa Serikali za mitaa, wahandisi na mafundi wa viwanda.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea na kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho ili kianze kufanya kazi upya, baada ya kukaa kwa miaka kadhaa bila ya kufanya kazi, Mbunge Gulamali alisema, leo nimekuja kuoana maendeleo ya kufufuliwa wa kiwanda hichi ikiwa ni sehemu ya kutaka kutimiza tena ahadi yangu niliyo itoa kwa wanachi wa Igunga na Manonga kwamba lazima kiwanda cha Manonga Ginery, kianze kazi ili wananchi waweze kunufaika katika zao biashara ya pamba na wengine kupata ajira kwa kuendesha maisha na kukuza uchumi wa viwanda nchini.

" Leo nimekuja kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hichi ikiwa ni sehemu yangu ya ahadi niliyo itoa kwa wananchi wangu wa jimbo la Manonga pamoja na Igunga kwamba lazima kiwanda hiki kifanye kazi tena, ili biashara ya zao la pamba lirudi tena na wananchi na waweze kupata ajira katika kiwanda hichi pia kukuza uchumi wa nchi ya Viwanda.

" Kufufuliwa kwa kiwanda hiki ni fursa kubwa ya maendeleo kwa jamii ya wana Igunga na Manonga na hasa wakulima wa zao la pamba hata kwa wananchi wanao lilia ajira, hivyo fursa kwa sasa iko wazi, alisema Gulamali.

Hata hivyo Mbunge Gulamali alisema kuwa bila kumpa ujumbe mmiliki wa kiwanda hiki na kutompa matakwa ya wananchi basi ingekuwa sicho kilichotokea leo, kwahiyo nimetumia uongozi wangu kwaajili ya wananchi wangu ili kuona maendeleo yakiendelea tena katika swala kiwanda na kuona zao la pamba likirudi tenaa kwa kasi katika Jimbo la Igunga na Manonga.

Lakini pia Mbunge Gulamali amewataka wakulima wa zao la pamba kuanza kulima kwa kasi kilimo cha hicho kwa kuwa sasa kiwanda hiki kitaanza kufanya kazi, hivyo juhudi na jitihada zenu ndio itakayoweza kufanya kiwanda hiki kiendelee kwa kuwa nao wanategemea pamba toka kwenu na wao waweze kuuza kwa wafanya biashara wakubwa wa nje ya mipaka na ndani ya nchi.

Hata hivyo Mmiliki wa kiwanda hicho, ndug, Urvesh Rajan amemshukuru Mbunge Gulamali sambamba na uongozi wa serikali wa kata ya Choma kwa kuweza kuvumilia kwa kipindi chote tangia kiwanda kilivyo simama na hata pale alitoa ombi lake la kukufua tena kiwanda waliweza kumsikilliza na hivyo ni jambo la kushukuru.

Lakini pia mmiliki wa kiwanda hicho ndug, Rajan ametoa ombi kwa wakulima wa zao la pamba kuweza kujitaidi kulima zao hili kwa kasi, kwa kuwa kiwanda kinategmea sana zao hili na si zao jingine, hivyo pesa watakayo ilipa toka kwawakulima wana imani nao itarudi pale watakapo wauzia wafanya biashara na ndio kiwanda kitazidi kuendelea.

" Ninafurahi Mbunge Gulamali ameitikia wito wangu kwa kuja na kuona maendeleo ya kutaka kufufua kiwanda hichi hivyo, ni jambo zuri kuona kiongozi akiwa sambamba na wewe na mwenye kutaka maendeleo,

" haitochukua muda tutaaenda kuanza kazi hivyo nina waomba wakulima wa zao hili kuchangamkia fursa kwenye ulimaji kwa kuwa fedha watapata za kuendesha maisha hata ajira pamoja na kukuza uchumi wa nchi yetu, alisema. Rajan.

Hata hivyo Mwenyekiti wa kijiji cha Choma, Ndug, Emmanuel Methew alisema kuwa kitendo kilichofanyika leo cha mbunge kuja kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hiki ni kitu kizuri kutokana ni mikaa mingi kutofanya kazi hivyo wakulima walikuwa wanapata tabu katika zao hili, hata mwishowe kukata tamaa katika kulima zao hili kutokana na kufa kwa kiwanda hiki.

"Kiwanda kufufuliwa tena ni jambo zuri hivyo nina imani kuwa wakulima watarudisha nguvu zao kwa kasi kwenye zao hili la pamba kwakuwa ndio moja ya zao kubwa katika mkoa wa Tabora, alisema Methew.


UNCDF YAWEZESHA UFUGAJI SAMAKI KIBIASHARA BWAWA LA KALEMAWE

$
0
0

SERIKALI ya Tanzania, imeshukuru Mfuko wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNCDF) kwa kuwezesha watanzania kupambana na umaskini kupitia miradi wanayoidhamini au kuitafutia fedha. Kwa miongo miwili UNCDF imekuwa ikifanya kazi kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia ofisi ya rais Tawala za Mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) katika mpango wa kupeleka madaraka kwa umma na shughuli za maendeleo ya kiuchumi . 

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhandisi Mussa Iyombe katika hotuba yake iliyosomwa na Katibu Tawala wa mkoa wa Kilimanjaro Aisha Amour kwenye ufunguzi wa kongamano la siku 2 la Wadau wa Ufugaji Samaki Kibiashara Bwawa la Kalemawe lililoko wilaya ya Same mwishoni mwa wiki.

“Tunafurahishwa kwa namna ya pekee na UNCDF kwa jitihada zake zinazoendeshwa kupitia katika Mpango wa Ufadhili Miradi ya kiuchumi (LFI),” alisema Iyombe na kuongeza: “Tunapokutana hapa tunapewa fursa na kufunuliwa uzoefu wa ushiriki wa UNCDF katika miradi mbalimbali, safari hii tukishuhudia hatua yake ya kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Same katika Mkoa wa Kilimanjaro.” Meneja wa Shamba la Samaki la Ruvu, Khambo Kanthenga (kulia) akitoa maelezo kuhusu mradi wa ufugaji samaki katika shamba hilo kwa viongozi mbalimbali wa Serikali wa wilaya ya Same na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) waliofanya ziara fupi ya mafunzo juu ya ufugaji wa samaki kibiashara katika shamba hilo lililopo wilaya ya Bagamoyo. Kushoto ni mbunge wa Jimbo la Same Mashariki, Mh. Naghenjwa Kaboyoka na Watatu kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Same, Rosemary Staki pamoja na Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Mitaji ya Maendeleo (UNCDF)-Tanzania, Peter Malika (wa pili kulia).

 Pamoja na kushukuru kwa hatua mbalimbali zilizofikiwa na taasisi hiyo katika kusaidia watanzania, aliwataka wakazi wa Same kuhakikisha kwamba mradi huo ulioundiwa kampuni ili kwenda kibiashara unafanikiwa na kuwa mfano kwa wengine. Halmashauri ya wilaya ya Same, na jamii inayozunguka bwawa la Kalemawe wanashirikiana na UNCDF kuboresha miundo mbinu ya bwawa hilo na kuwezesha uwapo wa uwekezaji kwa kuanzisha kampuni. 

Kampuni hiyo iliyosajiliwa ya Kalemawe Dam Investment Limited katika mpango maalum (SPV) inamilikiwa na wadau mbalimbali ikiwemo Halmashauri ya wilaya ya Same, halmashauri ya vijiji sita, wakala wa serikali, watu binafsi pamoja na makundi ya kijamii. Kuwapo kwa kampuni hiyo ni juhudi zinazofanywa za kuwezesha uhusiano mahsusi wa kibiashara unaohusisha ubia wa Serikali, Binafsi na jamii (PPCP) kwa kutoa umiliki linganifu mpaka katika ngazi za chini za mamlaka za kijiji, ambazo kimsingi ndizo wamiliki wa maliasili muhimu ya ardhi kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi ya Vijiji ya Mwaka 1999.  Viongozi mbalimbali wa Serikali wa wilaya ya Same na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) wakiwa kwenye ziara fupi ya mafunzo kuhusu ufugaji wa samaki kibiashara katika shamba la ufugaji samaki la Ruvu lililopo wilaya ya Bagamoyo.

Mradi huo wa Ufugaji wa Samaki Kibiashara wa Bwawa la Kalemawe ni zao la ushirikiano kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Same, Kata za Ndungu na Kalemawe, asasi zisizo za kiserikali na wadau wa maendeleo walioazimia kukarabati na kufufua bwawa hilo na mfumo wake wa kilimo cha umwagiliaji. UNCDF kwa kushirikiana na wabia wake waitwao Mikono Tayari (ambao ni kundi linaloundwa na washirika kutoka Tanzania na Norway) ni wataalamu katika mradi hu wa ufugaji samaki kwa pamoja na SPV ya Same na washirika wake. 

Katika kongamano hilo Mkuu wa wilaya ya Same Rosemary Staki amesema wilaya yake ipo tayari kutekeleza mradi huo ambao una manufaa makubwa si tu kwa watu wa Kalemawe na vijiji vinavyozunguka bali pia na halmashauri ya wilaya ya Same.  Meneja wa Shamba la Samaki la Ruvu, Khambo Kanthenga (kulia) akitoa maelezo kuhusu vyakula vinavyotumika kulisha samaki wanaofugwa kwenye shamba hilo kwa viongozi mbalimbali wa Serikali wa wilaya ya Same na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) waliofanya ziara fupi ya mafunzo juu ya ufugaji wa samaki kibiashara katika shamba hilo lililopo wilaya ya Bagamoyo.

Akishiriki katika mjadala aliwataka wanakalemawe kutambua umuhimu wa mradi huo na kwamba hicho ni kichocheo cha ukuaji wa uchumi wa watu binafsi na jamii kwa ujumla. Mradi huo ambao ni sehemu ya programu kubwa ya kubadili watu wenye makazi kuzunguka bwawa hilo umelenga katika siku za usoni kuzalisha samaki na vifaranga vyake. 

Ili kuwa na uelewa mkubwa wa kufanya biashara hiyo ya samaki, madiwani na wenyeviti wa serikali za mitaa za vijiji vinavyotengeneza kampuni hiyo ya Kalemawe walitembelea shamba la samaki Ruvu ambapo waliona shughuli mbalimbali zinazoendelea katika shamba hilo ili iwe mfano kwao Pamoja na kuuza samaki shamba hilo ambalo lipo kilomita 20 kutoka Bagamoyo na kilomita 13 hivi kutoka Mlandizi linafuga samaki aina ya sato na hutotolesha vifaranga laki moja kila wiki kwa kulingana na oda zilizopo.  Ziara ya mafunzo ikiendelea katika shamba la kufuga samaki la Ruvu lililopo wilayani Bagamoyo. Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Staki (wa pili kushoto) na Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Mitaji ya Maendeleo (UNCDF)-Tanzania, Peter Malika (katikati) pamoja na ujumbe ulioambatana nao kwenye mafunzo hayo ukitazama jambo katika shamba hilo.

Mmoja wa viongozi katika mradi huo Khumbo Kanthenga alisema kwamba mradi huo ambao bado unapanuliwa kufikia mabwawa sitini kwa sasa umelenga kutoa vifaranga kwa mujibu wa oda na pia kuuza samaki ambao wapo tayari kuingia sokoni samaki hao wanafikia gramu 350 na kuendelea. Naye Mbunge wa Same Mashariki, Naghenjwa Kaboyoka ambaye alikuwapo katika kongamano hilo alielezea haja ya wananchi wengi kutambua mipaka yao na kuhakikisha kwamba dhamira safi iliyopo ya kufufua bwawa hilo na kubadilisha maisha ya wananchi inafikiwa. 

Wakifunga Kongamano hilo UNCDF ili shukuru ushirikiano mkubwa wa karibu ambao umeonyeshwa na washiriki wa warsha hii ya wadau kuanzia serikali kuu, mkoa, willaya na viongozi wa vijiji sita vinavyohusika na utekelezaji wa mradi na pia iliahidi kua mashirika mengine ya umoja wa mataifa watashirikishwa kuwa sehemu ya utekelezaji wa mradi huu na miradi mingine mbalimbali katika eneo hili la bwawa la samaki.  Eneo ambalo linaandaliwa kwa ajili ya bwawa la kufugia samaki katika shamba la kufugia samaki la Ruvu lililopo wilayani Bagamayo. Wafanyakazi wa shamba la kufugia samaki la Ruvu wakitega nyavu kwa ajili ya kuonyesha samaki katika moja ya mabwawa kwenye shamba hilo wakati wa ziara hiyo fupi ya mafunzo. Mmoja wa wafanyakazi wa shamba hilo akiwa ameshikilia samaki aina Sato wanaofugwa kwenye shamba hilo. Meneja wa Shamba la Samaki la Ruvu, Khambo Kanthenga (tisheti nyekundu) akitoa maelezo katika chumba maalum cha kutotolea vifaranga vya samaki kwa viongozi mbalimbali wa Serikali wa wilaya ya Same na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) waliokuwa kwenye ziara fupi ya kupata elimu juu ufugaji wa samaki kibiashara katika shamba hilo lililopo wilaya ya Bagamoyo. Mshauri wa Shamba la Samaki la Ruvu, Per Gjoede akitazama mabwawa ya samaki katika shamba la kufugia samaki la Ruvu lililopo wilayani Bagamoyo. Mkurugenzi wa Shamba la Samaki la Ruvu, Daudi Makobole (wa pili kulia) akibadilishana mawazo na Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Staki (kulia) pamoja na Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Mitaji ya Maendeleo (UNCDF)-Tanzania, Peter Malika (kushoto), Mshauri wa Shamba la Samaki la Ruvu, Per Gjoede (wa pili kushoto) baada ya kuhitimisha ziara fupi ya mafunzo katika shamba hilo. Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Mitaji ya Maendeleo (UNCDF) nchini, Peter Malika akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufungua warsha ya siku mbili ya wadau wa mradi wa ufugaji wa samaki kibiashara katika bwawa la Kalemawe iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Mgeni rasmi Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhandisi Aisha Amour akizungumza wakati ufunguzi wa warsha ya siku mbilli ya wadau wa mradi wa ufugaji wa samaki kibiashara katika bwawa la Kalemawe iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Staki. Mkuu wa wilaya ya Same, Rosemary Staki akitoa salamu kwa wadau wa mradi wa ufugaji wa samaki kibiashara katika bwawa la Kalemawe wakati wa warsha hiyo iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Ofisa Mwandamizi anayeshughulikia uwekezaji katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Mitaji ya Maendeleo (UNCDF), Imanuel Muro akisimamia majadiliano kuhusu wa kampuni ya bwawa la Kalemawe lililopo wilayani Same mkoani Kilimanjaro wakati wa warsha ya siku mbili ya wadau wa mradi wa ufugaji samaki kibiashara katika bwawa hilo iliyoandaliwa na UNCDF na kufanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Mkiurugenzi Msaidizi Idara ya Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Dr. Charles Mhina akitoa maoni kwenye warsha ya siku mbili ya wadau wa mradi wa ufugaji wa samaki kibiashara katika bwawa la Kalemawe iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa kijiji cha Misufini kata ya Ngungu wilaya ya Same, Omari Mganga akiwasilisha maoni wakati wa warsha ya siku mbili ya wadau wa mradi wa ufugaji wa samaki kibiashara katika bwawa la Kalemawe iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa kijiji cha Mgandu kata ya Bendera wilaya ya Same, Merina Mhando akichangia maoni katika warsha ya siku mbili ya wadau wa mradi wa ufugaji wa samaki kibiashara katika bwawa la Kalemawe iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Mtaalamu wa Mawasiliano na Ushirikiano wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Mitaji ya Maendeleo (UNCDF) nchini, Jacqueline Namfua-Mwombela na Mshirika wa Programu UNCDF, Andulile Mwabulambo wakifurahi jambo wakati wa warsha hiyo iliyofanyika wmishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Pichani juu na chini ni washirki wa warsha ya siku mbili ya mradi wa ufugaji wa samaki kibiashara katika bwawa la Kalemawe iliyoandaliwa na UNCDF na kufanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.   Mgeni rasmi Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhandisi Aisha Amour katika picha ya pamoja na washiriki wa warsha hiyo.

RC Rukwa aagiza operesheni ya usafi wa vyoo wilaya nzima

$
0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen amemuagiza afisa afya wa wilaya ya Kalambo kuhakikisha anakagua usafi wa vyoo na maeneo yanayo zunguka nyumba kwa wilaya nzima ili kujiepusha na ugonjwa wa Kipindupindu katika Wilaya hiyo.
 Ametoa agizo hilo katika mkutano na wananchi siku ya usafi wa mwisho wa mwezi maarufu kama “Magufuli Day” baada ya Mkuu huyo kukagua nyumba 12, maduka ya wafanyabiashara pamoja na soko katika makao makuu ya wilaya hiyo huku nia ikiwa ni kutaka kujua hali ilivyo wanakojisaidia, wanakohifadhi taka pamoja na hali ya upatikanaji wa maji katika eneo hilo.
 Katika ukaguzi huo amebaini kuwa wananchi wengi husafisha nje ya nyumba tu huku nyuma ya majumba yao hali ikiwa mbaya jambo ambalo hupelekea kuibuka kwa kipindupindu na kuisababishia serikali kuwa katika wakati mgumu kwa magonjwa ambayo yanaweza kuzuilika endapo usafi utazingatiwa.
 “Leo nilipenda nione usafi wa matai, nimeuona na nimetoa “marks” 60, Nimepita karibu maeneo mbali mbali, usafi mnaoufanya ni wakuficha uchadu kidogo, huku mbele kusafi lakini nyuma kuchafu sana, nawaomba hilo mlirekebishe” Alisema.
Pia aliishauri halmashauri hiyo ya kalambo kuweza kusimamia sharia za usafi zilizopo bila ya huruma ili kuleta mabadiliko na kuitaka halmashauri hiyo kutenga fedha za makusanyo ya ushuru ili kuweza kuboresha hali ya usafi katika mji huo.

Mwezi mmoja uliopita Wilaya hiyo ilikumbwa na ugonjwa wa kipindupindu na kuua mtu mmoja na kuwaacha wengine ishirini katika hali mbaya jambo ambalo serikali haitaki ijirudie.

“Juzi hapa kulitokea kipindupindu kule Kijiji cha Samazi, hapana hatutaki watu wafe kwa kipindupindu, sasa nimeona choo kinamwaga maji machafu kinyesi kinatoka nje bata wanapokea wanakula, hatupo salama,” Alimalizia.

Pamoja na hayo Mh. Zelote alisisita kuwa usafi ni wa kila siku si lazima kusubiri jumamosi ya mwisho wa mwezi na kueleza kuwa siku hiyo imewekwa maalum ili kuwakumbusha wananchi kuwa wanahitajika kufanya usafi maeneo wanayofanyia biashara pia na kuwa usafi ni muhimu.

MCHENGA YATINGA FAINALI SPRITE BBAAL KINGS, KURASINI VS TMT MBABE KUPATIKANA KESHO

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

TIMU ya mpira wa Kikapu ya Mchenga Bball Stars imefanikiwa kuingia hatua ya fainali moja kwa moja baada ya kutoka na ushindi katika mchezo wa pili wa nusu fainali kwa kuinyuka Flying Dribblers vikapu 114 dhidi ya 52.

Katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya Sprite Bball Kings 2017, Mchenga walifanikiwa kutoka na ushindi wa vikapu 119 dhidi ya 70 vya Flying Dribblers na kupelekea Mchenga kwenda hatua ya fainali baada ya kuibuka kidedea katika michezo miwil baina ya mitatu.

Michuano hiyo ya Sprite Bball Kings 2017 inayoendelea katika viwanja vya Don Bosco Oysterbay ilizikutanisha timu nyingine katika mchezo wa pili wa nusu fainali baina ya Kurasini Heat dhidi ya TMT.

Kutokana na ushindi wa TMT wa mchezo wa pili kwa kuibuka kidedea kwa kuwabamiza Kurasini Heat vikapu 92 dhidi ya 61 huku katika mchezo wa kwanza Kurasini Heat wakiibuka kidedea kwa kushinda alama za vikapu 87 kwa 80.

Mchezo wa nusu fainali ya tatu ili kuweza kumpata mshindi atakayeungana na Mchenga katika hatua ya fainali, mchezo huo utapigwa siku ya Kesho katika Viwanja vya Don Bosco.

Fainali ya mchezo huo inatarajiwa kuanza siku ya Jumamosi katika Uwanja wa Ndani wa Taifa ikichezwa katika hatua tano ili kuweza kumpata bingwa wa Sprite Bball Kings 2017 na kuondoka na kitita cha Milion 10 huku mshindi wa pili akichukua Milion 3 na mchezaji bora wa Mashindano (MVP) akijinyakulia milion 2.
 Mpambano baina ya Mchenga (Nyeupe) dhidi ya Flying Dribblers (Bluu) ulimalizika kwa Mchenga kuingia katika hatua ya fainali baada ya kuibuka na ushindi aktika michezo miwili ya nusu faimali ikiwa inazisubiri timu za Kurasini Heat na TMT watakaovaana kesho katika fainali ya tatu Viwanja vya Don Bosco Oysterbay.

UZINDUZI WA BARAZA LA WAZALISHAJI WAFANYIKA ZANZIBAR.

$
0
0
Waziri wa Biashara Viwanda na Masoko Balozi Amina Salum Ali akiangalia bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na Wafanyabishara wa Zanzibar katika Uzinduzi wa Baraza la Wazalishaji lililofanyika katika Hoteli ya Grand Palace Malindi mjini Unguja.
Katibu wa Baraza la Wazalishaji Zanzibar Madam Cheherezade Chukh akitoa hotuba ya makaribisho katika uzinduzi wa Baraza la Wazalishaji lililofanyika katika Hoteli ya Grand Palace Malindi mjini Unguja.
Mwenyekiti wa Baraza la Wazalishaji Zanzibar Ahmed Yussuf Baalawy akizungumza machache katika uzinduzi wa Baraza la Wazalishaji lililofanyika katika Hoteli ya Grand Palace Malindi mjini Unguja.
Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara  Wenyeviwanda,Kilimo na Utalii (ZNCCIA)Taufiq Tourky akitoa hotuba na kumkaribisha Mgeni Rasmi katika  Uzinduzi wa Baraza la Wazalishaji lililofanyika katika Hoteli ya Grand Palace Malindi mjini Unguja .
Baadhi ya Wageni waalikwa waliohudhuria katika  uzinduzi wa Baraza la Wazalishaji lililofanyika katika Hoteli ya Grand Palace Malindi mjini Unguja.
Mgeni Rasmi Waziri wa Biashara Viwanda na Masoko Balozi Amina Salum Ali akitoa hotuba ya Uzinduzi wa Baraza la Wazalishaji lililofanyika katika Hoteli ya Grand Palace  Malindi mjini Unguja.

PICHA NA-YUSSUF SIMAI ALI/MAELEZO ZANZIBAR.

TAMA MUHIMBILI KUADHIMISHA SIKU YA WAKUNGA KATIKA WIKI YA UNYONYESHAJI

ZANTEL YATOA ELIMU KUHUSU HUDUMA ZAKE KWA WAKAZI WA MBAGALA NA KONGOWE JIJINI DAR

$
0
0

Afisa Usajili wa Kampuni ya Mawasiliano ya Zantel, Hussein Ahmed Abdallah (kushoto) akifafanua jambo kwa mteja mara baada ya Kampuni hiyo kuwatembelea wakazi wa Mbagala jijini Dar es salaam mwishoni mwa juma na kutoa elimu kuhusiana na huduma zake.
Afisa wa Zantel Kassongo Faraji (katikati) akifafanua jambo kwa mteja mara baada ya Kampuni hiyo kuwatembelea wakazi wa Mbagala jijini Dar es salaam mwishoni mwa juma na kutoa elimu kuhusiana na huduma zake.
Afisa wa Zantel, Abdallah Mabuga (kulia) akifafanua jambo kwa mkazi na mfanyabiashara wa Mbagala Zakhem Juma Pazi (katikati) mara baada ya Kampuni hiyo kuwatembelea wakazi wa Mbagala jijini Dar es salaam mwishoni mwa juma na kutoa elimu kuhusiana na huduma zake. Kushoto ni Afisa usajili wa Kampuni ya Mawasiliano ya Zantel, Hussein Ahmed Abdallah.
Afisa wa Zantel Thadey Lucas (kulia) akimsajili Mkazi wa Mbagala, Hamdan Ally (katikati) mara baada ya Kampuni hiyo kuwatembelea wakazi wa Mbagala jijini Dar es salaam mwishoni mwa juma na kutoa elimu kuhusiana na huduma zake. Anayeshuhudia kushoto ni mkazi wa Kongowe Abdul Ally.
Maafisa wa Zantel Rehema Tarimu (kushoto) na Hussein Ahmed Abdallah (kulia) wakimsajili mteja mpya mara baada ya kampuni hiyo kuwatembelea wakazi wa Kongowe jijini Dar es salaam mwishoni mwa juma na kutoa elimu kuhusiana na huduma zake.
Muuzaji wa bidhaa za Zantel, Madeline Amos akizungumza na mteja mara baada ya Kampuni ya Zantel kuwatembelea wakazi wa Mbagala jijini Dar es salaam mwishoni mwa juma na kutoa elimu kuhusiana na huduma zake.




WASHIRIKI 15 WATAJWA KATIKA MASHINDANO YA EUROPEAN YOUTH FILM

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MASHINDANO ya European Youth Film 2017 imewatangaza washiriki 15 waliofanikiwa kuingia hatua hiyo baada ya kutengeneza filamu fupi zenye maudhui tofauti.

Shindano hilo liliwashirikisha washiriki zaidi ya 120 na kuwachuja na kufikia 35 na tayari wamewapata washiriki 15 walioingia katika
kinyang'anyiro hicho na maamuzi yatakuwa mikononi mwa wananchi.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa utangazaji wa washiriki hao, Balozi wa Umoja wa Ulaya Roeland Van De Geer amesema kuwa wameziangalia filamu hizo katika maudhui tofauti na wamechujwa kwa kushirikiana na Bodi ya Filamu nchini.
Balozi wa Umoja wa Ulaya Roeland Van De Geer akizungumza na waandishi wa habari wakati wa utangazaji wa washiriki 15 waliofanikiwa kuingia hatua hiyo baada ya kutengeneza filamu fupi zenye maudhui tofauti.Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Huduma za Ufundi wa Bodi ya Filamu Wilhad Tairo na Kulia ni Afisa wa habari wa Umoja wa Ulaya Sussane Mbise.
Kaimu Mkuu wa Huduma za Ufundi wa Bodi ya Filamu Wilhad Tairo akuzungumza na kuupongeza Umoja wa Ulaya kwa mashindano waliyoaanzisha ya kuibua vipaji kwa waandaaji wadogo wa Filamu nchini, kushoto ni Mratibu wa mashindano Mussa Sakala.

De Geer amesema kuwa, filamu hizo 15 zitaoneshwa katika maeneo ya wazi ndani ya Jiji la Dar es salaam kwenye Viwanja vya Biafra Agost 5, Zakhem Agosti 12, Mwembe Yanga Agosti 19 na ukimbi wa Alliance Francais Septemba 02 ambapo washiriki watano wataingia hatua ya fainali.

Kaimu Mkuu wa Huduma za Ufundi wa Bodi ya Filamu Wilhad Tairo amesema kuwa mashindano haya yana tija kubwa sana katika kuibua vipaji ya sanaa na zaidi lazima tuanze kuangalia kutoka chini ili kupata waandaaji wapya na wenye ubunifu katika sekta ya sanaa hususani Filamu.

Mashindano hayo yatafikia tamati mwezi Septemba mwaka huu na yanaratibiwa na Umoja wa Ulaya nchini Tanzania.

KILA MTU KUWA NA BIMA YA AFYA-WAZIRI UMMY MWALIMU

$
0
0
Na chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema kuwa kiu yake katika sekta ya afya ni kuona kila mtu ana bima ya afya.

Waziri Ummy ameyasema hayo leo wakati wa uzinduzi wa Kadi ya Bima ya Afya kwa Mtoto ‘Toto Kadi’ , amesema kuwa taifa kuwa lina maendeleo linatokana na msingi wa afya  ambapo msingi huo unatokana  na kuwa watoto wanaopata huduma za afya kwa uhakika.

Amesema kuwa  gharama za kulipa matibabu katika ukuaji watoto na hali uchumi  ni kubwa lakini kuwepo kwa bima hiyo kutanya wazazi kuwa na  furaha wakati wote hata ikitokea ugonjwa bima ndio inamaliza matatizo.
Ummy amesema kuwa wakati  anaingia madarakani alikutana na Rais Dk. John Pombe  Magufuli  alichoendanacho ilikuwa ni kuongeza ghrarama lakini Rais alisema hakuna kuongeza ghrama yeyote cha msingi waangalie jinsi ya kusaidia watanzania kuwa na bima.

Aidha Waziri  Ummy amewaomba Mfuko wa  Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)  kuja na bima ya mama mjamzito itakayotumika wakati ujauzito na badaa ya kujifungua.

Ummy amesema kuwa kampeni hiyo iwe endelevu kwa nchi nzima ili watoto wote kuwa na bima ya afya hapo tutakuwa tunajenga taifa lenye msingi bora wa afya.Waziri  huyo ameitaka kuweka utaratibu wa kubandika mabango katika kila kumbi za starehe ili wanavyotumia vinywaji waweze kuangalia watoto kama wana kadi ya afya bima ya afya.

Nae Mwenyekiti wa Bodi NHIF, Anne Makinda amesema kuwa wanafanya kazi nguvu kuhakikisha watanzania wanapata huduma za afya  pamoja na kulipa watu wanaotoa huduma kwa bima ya afya.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akikata Utepe kuashiria uzinduzi wa bima ya afya ya Mtoto 'Toto Kadi' leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akiangalia muundo wa kadi ya bima ya afya ya Mtoto mara baada ya kuzindua leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akipeana Mkono na Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF, Anne Makinda  mara baada ya kuzindua bima  kadi ya bima ya afya kwa watoto leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF, Anne Makinda akimpa kadi Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa NHIF, Bernad Konga ,mara baaya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu kuzindua kadi ya afya ya Mtoto leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumza katika uzinduzi wa bima ya afya kwa mtoto katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bernad Konga akizungumza juu ya mpango wa bima ya afya ya Mtoto katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza juu ya bima ya afya kwa mtoto katika jiji la Dar es Salaam wakati uzinduzi wa bima hiyo katika viwanja vya mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Dorothy Gwajima akizungumza juu ya mkakati wa wizara katika utekelezaji wa bima ya afya.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu  akipata maelezo kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bernad Konga akimpa maelezo katika banda la NHIF.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu  akingalia jinsi maafisa  wa NHIF wanavyofanya kazi katika usajili kadi ya bima ya afya kwa Mtoto.  
Sehemu ya wawakilishi mbalimbali wa Sekta ya Afya na Jamii pamoja na watendaji wa NHIF  katika uzinduzi wa bima ya Afya kwa Mtoto.
Baadhi ya wananchi wa watoto wakiwa katika uzinduzi wa bima ya afya ya Mtoto katika viwanja vya Mnazi Mmoja.

Watendaji mbalimbali katika uzinduzi wa bima ya afya ya mtoto.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akiteta jambo na Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF, Anne Makinda (Kulia) Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bernad Konga.

Balozi wa Toto Kadi, Mrisho Mpoto akitumbwiza wakati wa uzinduzi wa kadi hiyo.
Mrisho Mpoto akishukuru baada ya kupewa ubalozi.


Wakicheza katika uzinduzi  wa bima ambayo ni bima ya afya ya Mtoto katika viwanja vya  Mnazi mmoja 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akiwa na Watoto waliopata Kadi ya Bima ya Afya ya Mtoto.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akiangalia muundo wa kdi ya bima ya afya hya mtoto.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akimpa kadi mtoto mara baada ya kuzindua bima ya afya ya Mtoto.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu  akiwa katika picha ya pamoja watendaji wa NHIF.




Picha mbalimbali katika uzinduzi bima ya afya ya mtoto

KAMATI YA MAKINIKIA YA TANZANIA YAANZA MAZUNGUMZO NA BARRICK GOLD CORPORATION JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0

Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati Maalum iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kufanya mazungumzo na uongozi wa Barrick Gold Corporation juu ya biashara ya madini yanayochimbwa na migodi ya kampuni hiyo hapa nchini akiulaki ujumbe wa kampuni hiyo kabla ya kuanza kwa mazungumzo hayo leo tarehe 31 Julai, 2017 Jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU 
  

Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati Maalum iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kufanya mazungumzo na uongozi wa Barrick Gold Corporation juu ya biashara ya madini yanayochimbwa na migodi ya kampuni hiyo hapa nchini akipata picha ya pamoja na ujumbe wa kampuni hiyo kabla ya kuanza kwa mazungumzo hayo leo tarehe 31 Julai, 2017 Jijini Dar es Salaam 
Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati Maalum iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kufanya mazungumzo na uongozi wa Barrick Gold Corporation juu ya biashara ya madini yanayochimbwa na migodi ya kampuni hiyo hapa nchini akizungumza akiwa na Afisa Mwendeshaji Mkuu wa kampuni hiyo Bw. Richard Williams kabla ya kuanza kwa mazungumzo hayo leo tarehe 31 Julai, 2017 Jijini Dar es Salaam.

JAFO:ACHENI KUFANYA KAZI KWA MAZOEA

$
0
0
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo alipotembelea eneo la mapokezi la hospitali ya Tarime na kuagiza lijengwe banda kwa ajili ya kukaa wananchi badala ya kukaa juani kama ilivyo hivi sasa.
Watumishi wa Halmashauri mbili za Tarime wakiwa katika mkutano wa pamoja na Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo.
Majengo yaliyojengwa na wadau wa mgodi wa North Mara kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Tarime.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa Halmashauri ya wilaya ya Tarime.

……………………………………………………………….

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo amewataka watumishi wa halmashauri ya mji wa Tarime na Halmashauri ya wilaya ya Tarime kuacha tabia ya kufanyakazi kwa mazoea.

Jafo aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na wafanyakazi wa halmashauri hizo mbili wakati wa ziara yake leo wilayani Tarime mkoani Mara.

Katika ziara hiyo, Jafo alifanikiwa kutembelea miradi ya afya, elimu, daraja na ujenzi wa nyumba za watumishi.

Jafo ameiagiza viongozi wa halmashauri hizo mbili kukaa na kufanya maamuzi ya majengo ya halmashauri ya wilaya ya Tarime yaliyopo ndani ya eneo la halmashauri ya mji yatumike kwa matumizi ya kiofisi ya halmashauri ya mji.

Aidha ameagiza fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa halmashauri ya mji zihamishiwe halmashauri ya wilaya ili waende kuanza ujenzi wa ofisini katika eneo lao badala ya kukaa ndani ya eneo la halmashauri mji.

“Kitendo hichi kinawakosesha wananchi haki yao ya kupata huduma kwa ukaribu jambo ambalo ndilo lilikuwa msingi wa kugawa halmashauri hizo,”amesema Jafo

Naibu Waziri Jafo amemaliza ziara yake na kuelekea wilaya ya Rorya, mkoani Mara.

BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA -AfDB KUSHIRIKI UJENZI WA RELI YA KATI YA KISASA TANZANIA

$
0
0
Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (kulia) akisikiliza kwa makini maelezo ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, Kanda ya Afrika Mashariki Dkt. Nyamajeje Weggoro (hayupo pichani) kuhusu ushirikiano mzuri na Benki hiyo katika Maendeleo ya kiuchumi nchini Tanzania, Makao Makuu ya Wizara ya Fedha, Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Kanda ya Afrika Mashariki, Dkt. Nyamajeje Weggoro (hayupo pichani) alipokutana naye ofisini kwake Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (kulia), akiishukuru Benki ya Maendeleo ya Afrika, AfDB, kwa namna inavyoshirikiana na Tanzania kukuza uchumi wake, wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo anayesimamia Kanda ya Afrika Mashariki, Dkt. Nyamajeje Weggoro, Jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, Kanda ya Afrika Mashariki, Dkt. Nyamajeje Weggoro, akizungumza namna Benki yake itakavyofadhili ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwando cha Kimataifa (Standard gauge) pamoja na kuhuisha Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania-TANESCO, alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (hayupo pichani), Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, anayehudumia Kanda ya Afrika, Dkt. Nyamajeje Weggoro (katikati) akimwonesha Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), zawadi ya picha, baada ya kumalizika kwa mazungumzo yao, Jijini, Dar es Salaam
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Kanda ya Afrika Mashariki Dkt. Nyamajeje Weggoro (kushoto) na Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (wa pili kushoto) na Afisa Mwandamizi toka AfDB na Idara ya Fedha za Nje, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa mkutano kati yao Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (kulia) akiwa ameongozana na mgeni wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Kanda ya Afrika Mashariki Dkt. Nyamajeje Weggoro (kushoto) mara baada ya kumalizika kwa mkutano kati yao, Jijini Dar es Salaam.

……………………………………………………………………

Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam

Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) imeahidi kushirikiana na Tanzania kujenga mradi mkubwa wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (SGR) kwa kuipatia mkopo wenye masharti nafuu.

Ahadi hiyo imetolewa Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo anayesimamia kanda ya Afrika Mashariki, Dkt. Nyamajeje Weggoro, alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji.

Dkt. Weggoro amesema kuwa Benki yake imeridhika na utendajikazi wa Serikali ya Awamu ya Tano ikiongozwa na Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli na hivyo kuifanya Bodi ya Wakurugenzi ya Benki hiyo kukubali kufanikisha ujenzi wa Reli hiyo kwa ajili ya maendeleo ya nchi.

Amesema kuwa Reli ya Kati kwa Kiwango cha Kimataifa ni muhimu kwa uchumi wa Taifa lakini pia kwa uchumi wa nchi za Maziwa Makuu kwa kuunganisha nchi kama vile Rwanda, Burundi, Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na baadae itaunganishwa na Reli ya Kaskazini upande wa Kenya.

“Benki iko tayari na inasubiri Tanzania ilete mapendekezo ama maombi ili yafanyiwekazi, tutakaa pamoja ili tuone Benki itasaidia kiasi gani na Benki pia inaweza kuwatafuta wadau wengine tunaosaidiana nao katika miradi mikubwa kama hii” Aliongeza Dkt. Weggoro

Mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (Standard gauge), yenye urefu wa kilometa 2,561 umepangwa kugharimu kiasi cha Dola bilioni 7.6 za Marekani, sawa na shilingi za Kitanzania Trilioni 16, awamu ya kwanza imeanza kujengwa kuanzia Dar es Salaam hadi Morogoro na baadae awamu nyingine zitafuata.

Aidha, Dkt. Weggoro amesema Benki yake itashirikiana na Serikali kuboresha utendajikazi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) hasa upande wa muundo wake na madeni makubwa yanayolikabili shirika hilo ili liweze kuchangia ipasavyo ukuaji wa uchumi wa viwanda.

“Benki itatoa fedha ili kulifanya shirika hilo lifanyekazi kwa ufanisi zaidi, tunajadiliana na tutawashirikisha pia wadau wengine zaidi ili uamuzi wa Serikali wa kuifanya nchi iwe ya viwanda uweze kufanikiwa” Alifafanua Dkt. Weggoro

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kujaji, ameishukuru AfDB kwakuwa mshirika mkubwa wa kimkakati wa maendeleo kwa kusaidia miradi mbalimbali ikiwemo barabara, nishati ya umeme, kilimo na huduma za jamii.

Dkt. Kijaji amesema kuwa uwekezaji wa AfDB hapa nchini umefikia Dola bilioni 1.8 huku asilimia 74.5 za uwekezaji huo iko kwenye sekta ya miundombinu, ambapo barabara imechukua asilimia 51.4, Nishati (10.1%), Maji na Usafi wa Mazingira (13%) na Sekta nyingine za huduma za jamii, kilimo na masuala ya fedha (25.5%).

Amesema kuwa uamuzi wa Benki hiyo kuamua kusaidia ujenzi wa mradi mkubwa wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (SGR) pamoja na kuihuisha TANESCO ni hatua muhimu itakayochochea ukuaji haraka wa uchumi wa nchi.

Ameitaja miradi mingine ya kimkakati iliyotekelezwa kupitia msaada na mkopo nafuu kutoka Benki hiyo kuwa ni ujenzi wa barabara ya lami inayoanzia Afrika Kusini-Cairo-Misri-Tanzania, kuanzia mkoani Iringa, Dodoma hadi Babati mkoani Manyara, inayotarajiwa kukamilika katika kipindi cha takriban miezi miwili ijayo.

MAKAMU WA RAIS AZINDUA MPANGO MKAKATI WA WATER AID TANZANIA

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa Water Aid Tanzania kwa mwaka 2016-2021 wenye kauli mbiu "Kuweka Maji na Usafi wa Mazingira kuwa kitovu cha Maendeleo"iliyofanyika  kwenye hotel ya HyattRegency jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Mhandisi Gerson Lwenge wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa Water Aid Tanzania kwa mwaka 2016-2021 wenye kauli mbiu "Kuweka Maji na Usafi wa Mazingira kuwa kitovu cha Maendeleo"iliyofanyika  kwenye hotel ya HyattRegency jijini Dar es Salaam. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Mohamoud Thabit Kombo wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa Water Aid Tanzania kwa mwaka 2016-2021 wenye kauli mbiu "Kuweka Maji na Usafi wa Mazingira kuwa kitovu cha Maendeleo"iliyofanyika  kwenye hotel ya HyattRegency jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akionyesha kitabu maalumu chenye mpango mkakati wa Water Aid ​

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassana leo amezindua Mpango Mkakati wa Water AID Tanzania .

Katika mkutano huo uliofanyika kwenye hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Mhandisi Gerson Lwenge, Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Mahmoud Thabit Kombo, Mkurugenzi wa Water Aid Kanda ya Afrika Mashariki Bi. Olutayo Bankole –Bolawole,Mkurugenzi WaterAid Tanzania Dkt. Ibrahim Kabole na wadau mbali mbali wa maji, afya na mazingira.

Mpango Mkakati wa miaka mitano wa Water Aid Tanzania wenye lengo la “ Kuweka Maji Safi na Usafi wa Mazingira (WASH)” katika mipango ya Maendeleo ya Jamii.

Makamu wa Rais aliwapongeza  Water Aid Tanzania kwa mpango wake huo, alisema Maji ni rasilimali ambayo haijawahi kutosheleza  mahitaji ya dunia na hapa kwetu pia kwani kuna mahitaji makubwa ya maji kwa ajili ya shughuli za kijamii, kiuchumi na kuhuisha na kutunza mazingira.
Vilevile  vyanzo vya maji vinaathiriwa sana na Ukame,kufurika n, kuvuruga mtiririko asilia, mabadiliko ya hali ya hewa ongezeko la idadi ya watu na viumbe wengine (Wanyama).

Mpango wa Water Aid Tanzania wa miaka mitano  utawezesha kuiweka Tanzania kwenye ramani ya matumizi endelevu ya rasilimali ya maji na utachangia katika utekelezaji wa malengo tuliyojiweka ya kupeleka huduma ya maji safi na salama kwa wananchi kulingana na Sera yetu ya Maji na pia kutekeleza ahadi tulizozitoa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya 2015.

Makamu wa Rais alisema Serikali kwa kushirikiana na wadau mbali mbali imeendelea kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika maeneo ya vijijini ambapo utekelezaji huo umeendelea kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji vijijini ambapo kwa mwezi Juni 2017 jumla ya watu 22,952,371 sawa na asilimia 72.58 ya wananchi waishio vijijini wanapata maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400 kama sera ya maji ya mwaka 2002 inavyoelekeza huku katika Miji Mikuu  ya mikoa kutoka asilimia 86 hadi asilimia 95, katika miji mikuu ya Wilaya , miji midogo na miradi ya Kitaifa kutoka asilimia 60 hadi asilimia 75 na katika jiji la Dar es Salaam kutoka asilimia 72 hadi asilimia 95 ifikikapo 2020.

Makamu wa Rais alisisitiza suala la usafi wa mazingira na kuhakikisha tunalinda afya zetu tusishambuliwe na magonjwa ya milipuko kama  vile kipindu pindu na homa za matumbo.  “Sote tunajukumu kubwa kuhakikisha tunapata maji na kuzungukwa na Mazingira safi”.

Makamu wa Rais aliwaagiza wanaohusika na usimamizi wa miradi ya maji na usafi wa mazingira kuongeza jitihada zaidi ifikapo 2020 idadi ya wananchi wanaopata maji iwe imeongezeka kufikia malengo tuliyojiwekea.
Mwisho, Makamu wa Rais aliwashukuru wawakilishi wa mashirika yote ya Maendeleo, wafadhili binafsi na Watendaji wengine ikiwa pamoja na Sekta Binafsi na Taasisi za Kidini ambazo zimesaidia katika upatikanaji wa huduma za maji na usafi wa mazingira na kuboresha mazingira.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AZUNGUMZA NA WATUMISHI WA MANISPAA YA MBEYA

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi wa Umma, Viongozi wa Dini na Viongozi wa Taasisi Binafisi wa Manispaa ya Mbeya kwenye ukumbi wa Benjamin Mkapa jijini Mbeya Julai 31, 2017.  Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla na Kulia ni Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
 Baadhi ya Watumishi wa Umma, Viongozi wa Dini na Viongozi wa Taasisi Binafsi wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye ukumbi wa Benjamin Mkapa jijini Mbeya julai 31, 2017. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi Mkuu wa TAKUKURU wa Mkoa wa Mbeya, Mhandisi Emmanuel Kyabo taarifa zinaoonyesha ubadhirifu uliofanywa na baadhi ya watendaji katika ujenzi wa soko la Mwanjelwa jijini Mbeya ili afanye uchunguzi wa kina  na kumshauri Waziri Mkuu hatua zinazostahili kuchukuliwa kwa wanatakaobainika kuwa wamefanya makokosa. (PIcha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WANANCHI MONDULI KUNUFAIKA NA MAJI

$
0
0

Mkurugenzi wa kampuni ya Smart Vision ya Korea, Seo Young Kim (kushoto) na Andrew Chung ambaye ni mbunifu wa mtambo wa kusafisha maji wakionyesha mtambo huo kwenye uzinduzi wake kwenye kitongoji cha Irmorijo Kijiji cha Emairete Wilayani Monduli Mkoani Arusha
Mkurugenzi wa kampuni ya Smart Vision ya Korea, Seo Young Kim (kushoto) na mchungaji wa kanisa la Enyora Daniel Vengei wakiwa kwenye uzinduzi wake katika kitongoji cha Irmorijo Kijiji cha Emairete Wilayani Monduli Mkoani Arusha.
Wananchi wa kitongoji cha Irmorijo Kijiji cha Emairete Wilayani Monduli Mkoani Arusha wakishuhudia uzinduzi wa mtambo wa kusafisha maji na kuyachuja uliofanywa na kampuni ya Korea ya Smart Vision.

………………………….
Zaidi ya kaya 700 za wananchi wa Kitongoji cha Irmorijo Kijiji cha Emairete Wilayani Monduli Mkoani Arusha, waliokuwa wanatumia maji ya kwenye bwana wanatarajia kunufaika na mradi wa kusafisha maji na kuchuja maji kuwa safi uliozinduliwa Kijiji hapo.

Awali, wananchi hao walikuwa wanatumia kwa shughuli mbalimbali ikiwemo kupika, kufua, kuoga na kunywa maji hayo ya bwawa ambayo pia yalikuwa yanatumiwa na mifugo ya eneo hilo.

Mkurugenzi wa kampuni ya Smart Vision ya Korea, Seo Young Kim akizungumza jana kwenye uzinduzi wa mradi alisema lengo ni jamii ya eneo hilo kunufaika na maji safi na salama yanayochujwa kupitia ubunifu wao.

Kim alisema kwa kuanza kuwanufaisha wananchi wa eneo hilo, wanatarajia kugawa majiko rafiki ya mazingira 22 na mitambo ya kuchuja na kusafisha maji ya bwawa kuwa safi na salama 22 kwa kaya 22 zitakazowanufaisha zaidi ya watu 220.

Alisema Smart Vision kupitia uwekezaji wa Korea Trade-Investment Promotion Agency. (KOTRA) jamii ya eneo hilo itanufaika na na mradi huo wenye lengo la kuondokana na matumizi ya maji yasiyo safi wala salama ambayo yanasababisha magonjwa ya tumbo.

“Jamii ya eneo hili kupitia mchungaji wa kanisa la Enyorata Daniel Vengei, walileta maombi kwetu kuwa wanatatizo la maji, hospitali na shule, ndipo tukaona tuanze kutatua hili suala la maji ndipo tukaleta mitambo hii ya kuchuja na kusafisha maji,” alisema Kim.

She said goal of project, Smart Vision head about maasai water problem in Korea. Smart Vision developed water purifier to help maasai people overcome water problem.

Kim said now Smart Vision a Korean Environmental company launches water project ina Tanzania, hopes to expand project to other parts of Tanzania where there is lack of drinking water.

“This project was aided financially bya KOTRA (Korea Trade-Investiment Promotion Agency) who supports international business of Korean companies, specifically, the KOTRA branc in Dar es salaam gave Smart Vision immense support in order to help people suffering from lack of drinking water though the water purification project,” said Kim.

She said people who helped with project is Director of Smart Vision Seo-Young Kim, Manager of Smart Vision, Hyun-Jung Chung and Purifier developer and volunteer, Andrew Chung.

Mkazi wa Kitongoji cha Emairete Rose Lemomo alisema alisema awali walikuwa wanakabiliwa na tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama lakini kupitia mradi huo wataondokana na maradhi ya tumbo yaliyokuwa yakiwakabili hasa watoto.

Lemomo aliwashukuru wote waliohusika na kufanikisha mradi huo, kwani hivi sasa watakuwa wanachota maji bwawani na kuyachuja na kuyasafisha kupitia mitambo hiyo.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Irmorijo, Mirishi Songoyo alishukuru shirika la Smart Vision kwa kufanikisha mradi huo wa maendeleo ambao utainufaisha jamii ya eneo hilo walioteseka kwa muda mrefu juu ya suala la maji.

“Tunawaomba wananchi watakaofikiwa na mradi huu kuhakikisha wanawasaidia na wale ambao bado wanasubiri kupatiwa majiko na mitambo ya kuchuja na kusafisha maji,” alisema Songoyo.

Mwalimu wa shule ya msingi Irmorijo, Stephen Laizer aliwataka wananchi wote waliofanikiwa kupatiwa mradi huo kuhakikisha wanautunza ili kunufaika nao kwa muda mrefu kwani wameteseka kwa miaka mingi kwenye tatizo la maji.

“Wageni wanapokuja kwenu inawabidi kuwashukuru hata kama hawajaacha chochote ila hawa wametuletea teknolojia ya maji, wanaweza kutufanyia mengine mazuri,” alisema Laizer.

KAMPUNI YA PIMAK YAFUNGUA DUKA LA KUUZA VYOMBO JIJINI DAR

$
0
0
KAMPUNI ya kimataifa inayojihusisha na utengenezaji na uuzaji wa vifaa vya mbalimbali vya mapishi kwenye hoteli , PiMAK imefungua duka hapa nchini lililopo Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.

Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Ali Donmez alisema, kampuni hiyo imebainisha soko kubwa la bidhaa zake hapa ambapo imekuwa ikifanya biashara kwa muda mrefu kwa kushirikiana na mawakala, na kwa sasa licha ya kufungua duka hilo lakini bado inaona kuna fursa kubwa zaidi za uwekezaji.

Akizungumzia kuhusiana na bidhaa hizo, alisema kuwa ni bidhaa kwa ajili ya matumizi ya hoteli, migahawa na huduma kubwa za mapishi vikiwamo vya kukatia nyama, kuhokea mikate, kuoshea vyombo, kupikia na huduma nyingine za kihoteli. 

Aliongeza kampuni hiyo imeshafanya kazi hapa nchini kwa miaka minne ikishirikiana na mawakala ambapo vifaa hivyo vinatumiwa na hoteli nyingi hapa nchini, huku akiweka wazi kuwa inatoa huduma za utengenezaji wa bidhaa hizo pia. 

"Kampuni hii ina miaka 25 na makao yake makuu ni Instabul, Uturuki kwa Tanzania tumekuwapo kwa miaka minne tukifanya biashara kwa kushirikiana na mawakala lakini leo tumefungua (jana) tumefungau duka letu huku tukiwa na lengo na kuja kuanzisha kiwanda cha uundwaji wa vifaa hivi hapa hapa nchini" alisema Donmez. 

Pia alisema kuwa kampuni hiyo kwa miaka ya baadae itafungua kiwanda hapa nchini kwa lengo la kurahisha upatikanaji wa bidhaa zake kwenye soko la Afrika Mashariki na Kati na pia kuongeza ajira zaidi kwa watanzania.
Kampuni hiyo kwa sasa inafanya kazi nchi 16 na kwa hapa nchini imeshaajiria wafanyakazi 15 huku ikitoa huduma za ukarabati wa vifaa vya upishi hoteli mbalimbali nchini.
 
Mmiliki wa Kampuni ya PiMAK, Riza Ergun akikata utepe kuashiria uzinduzi wa duka la kuuza vifaa mbalimbali vya mapishi lililofunguliwa eneo la Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. 
Mmiliki wa Kampuni ya PiMAK, Riza Ergun akiwa na wadau kadhaa waliojitokeza kwenye uzinduzi huo wakisoma menu ya baadhi ya vifaa vinavyouzwa dukani hapo mara baada ya kuzinduliwa
Wafanyakazi na wageni waliojitokeza siku hiyo ya uzinduzi wa duka la kuuza vifaa mbalimbali vya mapishi wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kufunguliwa eneo la Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

BALOZI WA KUWAIT ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye, akimkabidhi zawadi Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem (kushoto), baada ya mazungumzo na Balozi huyo alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi hilo, jjini Dar es Salaam leo. Katika Kikao hicho Balozi huyo aliahidi kushirikiana na Jeshi kubadilishana utaalamu katika masuala ya kukabiliana na majanga mbalimbali. Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye, akizungumza na Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem (Wakwanza kulia) alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi hilo jijini Dar es Salaam leo. Katika Kikao hicho Balozi huyo aliahidi kushirikiana na Jeshi hilo kubadilishana utaalamu katika masuala ya kukabiliana na majanga mbalimbali. Wengine ni Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo. Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem, akizungumza wakati wa kikao na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye (katikati) na Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo, alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi jijini Dar es Salaam leo. Katika Kikao hicho Balozi huyo aliahidi kushirikiana na Jeshi hilo kubadilishana utaalamu katika masuala ya kukabiliana na majanga mbalimbali.Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye, akiongozana na Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem (kulia) alipowasili  Makao Makuu ya Jeshi hilo jijini Dar es Salaam leo kwa mazungumzo yaliyohusisha ushirikiano kati ya Majeshi ya nchi hizo kubadilishana Utaalamu katika masuala ya kukabiliana na majanga mbalimbali.Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem, akisalimiana na Maafisa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakati alipowasili Makao Makuu ya Jeshi hilo jijini Dar es Salaam leo kwa mazungumzo na Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, Thobias Andengenye(hayupo pichani). Katika Kikao hicho Balozi huyo aliahidi kushirikiana na Jeshi hilo kubadilishana utaalamu katika masuala ya kukabiliana na majanga mbalimbali.Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye, akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem (katikati) baada ya kikao cha mazungumzo yaliyohusisha ushirikiano kati ya Majeshi ya nchi hizo katika kubadilishana Utaalamu katika masuala ya kukabiliana na majanga mbalimbali.Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji



Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Nchini, liko katika mkakati wa kuingia ushirikiano na Serikali ya Kuwait katika shughuli zake za kukabiliana na majanga ya moto ikiwa ni juhudi zake katika kuyafikia maeneo mengi nchini. 

Akizungumza alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji jijini Dar es salaam, Balozi wa Kuwait Nchini, Jasem Al-Najem, alisema serikali ya Kuwait ipo tayari kubadilishana mafunzo na kutoa msaada wa vifaa kwa Jeshi hilo.

“Ni vema tukatengeneza mpango ambao wataalam wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kutoka nchini Tanzania wataweza kubadilishana uzoefu na wataalamu kutoka nchini Kuwait kwa ajili ya kujifunza mbinu mbalimbali za kukabiliana na majanga pindi yanapotokea, ’’ Alisema Balozi huyo.

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye alimshukuru kwa kumtembelea na kusema kuwa ujio wa balozi huyo, umefungua ukurasa mpya kwa upande wa misaada na mafunzo kwa Askari wa Jeshi hilo, kwani watapata fursa ya kubadilishana uzoefu na kuongeza tija kwa Jeshi lake.

“Tutapata nafasi ya kubadilishana uzoefu na kupata mafunzo kutoka Nchi ya Kuwait na kuongeza ufanisi katika majukumu yetu ya kila siku, lengo ikiwa ni kukabiliana na majanga mbalimbali yakiwemo ya moto,’’ alisema Kamishna Jenerali.

Katika kikao hicho Balozi wa Kuwait, Nasem Al-Najem alipokea taarifa ya changamoto zinazolikabili jeshi hilo ikiwemo uhaba wa vitendea kazi huku akiahidi kuzifanyia kazi na akisisitiza mchakato wa kusaini makubaliano ya hiari ukamilike kwani utakuwa msaada wa kutekeleza kwa haraka program za mafunzo ya muda mfupi.


IMEANDALIWA NA KITENGO CHA HABARI NA ELIMU KWA UMMA-MAKAO MAKUU YA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI.

WAUMINI WA KANISA LA EFATHA MJINI SONGEA WACHANGIA DAMU

$
0
0
Waumini wa kanisa la EFATHA MINISTRY lililopo katika manispaa ya SONGEA mkoani RUVUMA wamejitokeza kwa wingi kuchangia damu kwa watu wenye uhitaji wa damu, ambapo zoezi hilo la kuchangia limefanyika kanisani hapo. PHILIPO GUNI ni baba wa kiroho katika kanisa hilo anasema kutokana na mateso mengi wanayoyapata ndugu zetu hususani akina mama wajawazito na watu wanaopata ajali ndicho kilicho wasukuma zaidi.habari kamili hii hapa video yake

MSAFARA WA MAGARI YA KIZAMANI KUANZA ZANZIBAR

$
0
0

Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Rashid Ali Juma mwezi ujao,anatarajia kuzindua msafara wa magari ya zamani mjini humo ili kuamsha aina mpya ya utalii.

Msafara huo unatarajiwa kuanzia Hyatt Park hoteli iliyopo mjini Zanzibar na kumalizikia Melia hoteli Kiwengwa.

Waziri Juma amesema hayo leo na kuongeza kuwa lengo la safari hiyo ni kuamsha aina mpya ya utalii itakayopelekea watalii wengi kuja nchini.

Amesema magari hayo ya miaka ya 60 yalikuwa yakitumiwa na wafalme na masultani, lakini hadi leo yanaweza kutembea."Utalii unachangia pato la Zanzibar kwa asilimia 27 huku ukichangia asilimia 80 ya fedha za kigeni kwani mambo mengi ya kitalii yamekuwa ya kawaida".

Amesema kwa kushirikiana na Hyatt hoteli tumekuja na mbinu mpya ya kuwavutia watalii wengi zaidi.Amesisitiza kuwa hakutakuwa na mbio za magari bali ni msafara wa magari hayo ya zamani ambayo yatatembea umbali wa kilomita 30 na kwa kuanzia yatakuwa magari sita, matatu ya watu binafsi na matatu ya Hyatt.

Aidha amewahakikishia usalama wa kutosha katika msafara huo ambapo vyombo vya ulinzi vitakuwa vikisindikiza mwanzo mpaka mwisho wa safari.
Nae Meneja mkuu wa Hyatt hoteli Garry Friend alisema msafara huo utaanzia Hyatt park hoteli Zanzibar ukipitia mji mkongwe na kumalizikia Melia Kiwengwa Agosti 26 ambayo ndiyo siku ya ufunguzi rasmi. 

Amesema lengo la kutumia magari hayo yaliyotumika miaka ya 60 ni kusisimua utalii."Watu wengi watavutiwa na aina hii ya utalii" alisema Friend.
 Waziri wa Habari utalii Utamaduni Sanaa na Michezo Mh.Rashidi Juma Kushoto Akizungumza na Waandishi wa Habari mapema Jijini Leo
Kulia ni Meneja Mkuu wa Hyat Hotel Bwn Garry Friend

TANZANIA EXCELS IN STATISTICAL CAPACITY AMONG SUB-SAHARAN AFRICAN NATIONS, WB REPORT SHOWS

$
0
0
A graph showing Tanzania as a second country among  Sub - Saharan countries in better statistical capacity. According to the World Bank report,  Tanzania scored 90 percent for periodicity, 80 percent for source data and 50 percent for methodology which contributed to an overall of 73.3 percent. 

Tanzania has been ranked second, behind South Africa in statistical capacity among Sub-Saharan African nations. 
This is according to the World Bank (WB) 2016 Statistical Capacity Indicator (SCI). 
WB has been assessing national statistical capacity in developing countries since 2004 and has produced overall SCI score as well as scores for three categories, Methodology, Source Data and Periodicity. Regional overall and specific category SCI are also produced to allow for comparison.

For every dimension, a country is scored against specific criteria, using information available from the WB, IMF, UN, UNESCO, and WHO. 

A composite score for each dimension and an overall score combining all three dimensions are derived for each country on a scale of 0 - 100. A score of 100 indicates that the country meets all the criteria. 

The statistical methodology aspect measures a country’s ability to adhere to internationally recommended standards and methods, by assessing guidelines and procedures used to compile macroeconomic statistics and social data reporting and estimation practices by looking at an updated national accounts base year, use of the latest Balance of payment, external debt reporting and IMF’s Special Data Dissemination Standard and enrolment data reporting to UNESCO.

On source data, this measures data collection activities in line with internationally recommended periodicity, and whether data from administrative systems are available and reliable for statistical estimation purposes and periodicity of population and agricultural censuses, the periodicity of poverty and health related surveys, and completeness of vital registration system coverage.

The third aspect concerned with the periodicity and timeliness looks at the availability and periodicity of key socio-economic indicators of which nine are MDG indicators.

Tanzania scored 90 percent for periodicity, 80 percent for source data and 50 percent for methodology which, contributed to an overall SCI of 73.3 percent. Although this overall score ranks Tanzania as second behind South Africa (82.2%) there is still room for improvements, especially in methodology.  

The National Bureau of Statistics (NBS) is committed to continuing strengthening of the National Statistical System.
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live




Latest Images