Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

MANTRACK TANZANIA YAONESHA MAPINDUZI MAPYA YA TEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA UJENZI NCHINI.

$
0
0
Katika kuunga juhudi za Serikali ya awamu ya tano ya kuleta maendeleo kwa wananchi kampuni ya magari ya Mantrack Tanzania jana imeendesha warsha fupi yenye lengo la kutambulisha vifaa na teknolojia mpya itakayoongeza ufanisi wa kazi hasa katika sekta ya ujenzi.

Akizungumza na waandishi wa habari, mwakilishi wa kampuni ya Mantrack Tanzania alisema kuwa wameleta vifaa vipya vitakavyoendana na kasi ya maendeleo ya Serikali ya awamu ya tano ya kuhakikisha Tanzania mpya inajengwa na uchumi bora na yenye miundombinu bora.

“Vifaa hivi ni imara na vinatumia teknolojia mpya na ya kisasa inayosaidia utendakaji wa shughuli za ujenzi kuwa rahisi. Tumeamua kuja na kasi ya serikali mpya ya kutenda vitu kwa urahisi na kwa ufanisi wa hali ya juu”.

Tuna wakaribisha wadau wa ujenzi wafike kujionea wenye tunachosema. Alisema. Warsha hiyo imefanyika katika karakana ya Mantrack Tanzania iliyopo karibu na jengo la Quality Plaza barabara ya Nyerere na ilihudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka makampuni mbalimbali ya ujenzi hapa nchini waliofika kushuhudia vifaa hivyo vinavyofanya kazi.

Mwakilishi wa ManTrack Tanzania akitoa maelezo mbalimbali kwa wadau juu ya teknolojia mpya na bidhaa zao mbalimbali.



Tigo imechangia kisima kwa wakaazi wa Mji Mpya mkoani Morogoro

$
0
0


Mkuu wa wilaya ya Morogoro mjini, Regina Chonjo (katikati) akikata utepe kuzindua kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro. Wanaoshuhudia kutoka kulia ni Meneja wa huduma za jamii Tigo, Halima Okash, Ofisa Mkuu wa Ufundi na Taarifa wa Tigo (CTIO) Jérôme Albou,  na  Diwani wa mji mpya Wence Kalogelezi

Mkazi wa Mji mpya akiwa kabeba ndoo ya maji mara baada ya uzinduzi wa kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro.

Mkuu wa wilaya ya Morogoro mjini, Regina Chonjo (katikati) akihutubia wakazi wa Mji mpya mara baada ya  kuzindua kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro.

Mkuu wa wilaya ya Morogoro mjini, Regina Chonjo akiwa katika picha ya pamoja  na Wakazi wa Mji Mpya Mkoani Morogoro mara baada ya uzinduzi w kisima hicho. kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro.

·        Uchangiaji huu ni ishara ya shukurani kwa wakaazi hao kwa kuzima moto katika kituo cha data cha Tigo.


Tarehe 27 Julai 2017 – Tigo Tanzania imechangia kisima chenye thamani ya TZS milioni 17 kwa hosipitali ya Mji Mpya na maeneo yanayoizunguka katika mkoa wa Morogoro kama mkono wa shukurani kwa wakaazi kwa kuhatarisha maisha yao wakati wakipambana na moto ambao ulilipuka katika kituo cha data cha kampuni katika eneo hilo.

Kwa mujibu wa Tigo, uchimbaji wa kisima hicho pia ulikuwa sambamba na nia ya kampuni hiyo kusaidia ustawi wa jamii ambako Tigo inaendesha  shughuli zake.

Akizungumza katika sherehe za makabidhiano zilizofanyika katika hospitali ya mji mpya katika manispaa ya mji wa Morogoro Afisa Ufundi na Taarifa wa Tigo (CTIO) Jerome Albou alielezea matarajio yake kwamba kisima hicho kitawafikisha mbali sana katika kuondoa suala la upungufu wa maji katika hospitali na pia kutoa maji safi na salama ya uhakika kwa jamii inayokizunguka.

“Tunawashukuru sana watu wa Mji Mpya kwa kuonesha kujali na kujitoa wakati wa kupambana na moto ambao karibu uteketeze kabisa kituo cha Data mapema mwaka huu. Kweli Tigo ina deni kwa wanajamii, serikali ya mtaa na viongozi wa ulinzi na usalama wa manispaa kwa kuitika  kwa wakati kuhakikisha kuwa hakuna uharibifu mkubwa unasababishwa wakati wa moto,” alisema Albou.   

“Kwa hiyo msaada huu, unakuja kutimiza ahadi walioiweka Tigo kwa wakazi wa Mji mwema wa kuwapatia maji safi na salama kama namna ya kutambua juhudi zao katika kulinda mali za kituo hicho cha data.”

Albou alibainisha kwamba uchangiaji huo unakamilisha idadi ya vijiji 20 ambavyo vimenufaika kutokana na jitihada za Tigo za kutoa maji safi na salama nchi nzima, ikiwa inawasaidia zaidi ya watu 187,000.

Mwaka huu, Tigo ina mpango wa kuchimba visima zaidi katika maeneo yanayohitaji ambayo zaidi ya watu 350,000 wanatarajiwa kunufaika katika jitihada zetu za kusaidia juhudi za serikali za kuondoa upungufu wa maji safi na salama nchini.

Makabidhiano yalishuhudiwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dr Kebwe Stephen Kebwa ambaye aliishukuru Tigo kwa kufikiria kutoa msaada huo. Alisema kwamba kisima hicho kitasaidia utoaji wa huduma bora za kiafya katika hospitali ya Mji Mwema na kusaidia katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Aliwaomba wasamaria wema wengine kujitokeza na kuunga mkono juhudi za kuondoa upungufu wa maji katika mkoa huo.

Tunapenda kuishukuru Tigo kwa kutusaidia katika juhudi zetu za kutoa huduma za kiafya za uhakika katika eneo hili kwa kutatua tatizo lililokuwepo la upungufu wa maji. Tunaamini kwamba upatikanaji wa maji safi na salama karibu na wakaazi pia itaongeza uzalishaji wa kiuchumi hasa kwa wasichana na wanawake ambao hawatakuwa wanapoteza muda mwingi wa kutafuta maji safi na salama sehemu zingine. Hii itawapatia wasichana fursa ya kuhudhuria masomo kwa uhuru na kuipa jamii fursa ya kuhudhuria kwa ufanisi katika shughuli zao za maendeleo ya Taifa,  Alisema Dr Kebwe. 

Mchezaji yoso wa kikapu kupata mafunzo ya NBA Afrika Kusini

$
0
0
Balozi wa mchezo wa mpira wa kikapu nchini, Jokate Mwegelo akikabidhi bendera ya Taifa kwa mchezaji Chipukizi, Jesca Ngaise (katikati) wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye kituo cha michezo za Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park. Anayeshuhudia zoezi hilo ni Kocha maarufu wa mpira wa kikapu Tanzania, Bahati Mgunda.
Balozi wa mchezo wa mpira wa kikapu, Jokate katika picha ya pamoja na baadhi ya wachezaji chipukizi wa mpira wa kikapu kwenye viwanja vya JMK Park.
Balozi wa mchezo wa mpira wa kikapu, Jokate akisalimiana na wachezaji chipukizi wa mpira wa kikapu kwenye viwanja vya JMK Park.
Baba Mzazji wa Jesca, Julius Ngaise akizungumza


………………………………………………………………………..


Na Mwandishi wetu


Balozi wa mchezo wa mpira wa kikapu nchini, Jokate Mwegelo ametoa rai kwa wasichana na wazazi kuwaruhusu watoto wa kike kushiriki katika michezo mbalimbali ili kukuza vipaji na kujiingizia kipato.


Jokate alitoa rai hiyo wakati wa kukabidhi bendera kwa mchezaji chipukizi wa mpira wa kikapu nchini, Jesca Julius Ngaise ambaye anaondoka leo kwenda nchini Afrika Kusini kushiriki katika mafunzo ya juu mchezo huo yatakayoendeshwa na makocha wa kimataifa wa ligi ya NBA ya Marekani.


Amesema kuwa Jesca ambaye ni mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Juhudi ya Ukonga, amepata nafasi hiyo baada ya kuchaguliwa na jopo la makocha na kuweka historia ya kuwa msichana wa kwanza wa Tanzania kuhudhuria mafunzo hayo.


“Hii ni faraja kwa Tanzania, makocha wa kimataifa wameona kipaji cha Jesca ambaye ni nahodha wa timu ya Taifa ya wasichana ya wachezaji wa chini ya miaka 16, ameiwezesha Tanzania kushika nafasi ya tatu katika mashindano ya Afrika Mashariki nchini Kenya, sasa tunampa bendera na kuiwakilisha nchi katika kozi hiyo, ni sifa kubwa kwake na kwa Taifa,”


“Michezo ni ajira,wachezaji wengi wa mpira wa kikapu wanalipwa vizuri, hii ni fursa kwa Jesca na wachezaji wasichana, bidii inakuwezesha kufanikiwa, Jesca ni mfano wa kuigwa na sasa anaingia katika vitabu vya kihistoria kwa kuwa msichana wa kwanza kupata mafunzo ya NBA, akifanya vizuri anaweza kwenda Marekani,” alisema Jokate.


Kwa upande wake, Jesca aliwashukuru wote walioshirikiana nao katika mchezo wa mpira wa kikapu na kuahidi kufanya vyema katika kliniki hiyo.


Alisema kuwa hakuamini kupata nafasi hiyo na kuwaomba wasichana wenzake kujishughulisha katika michezo kwani fursa ya kufanikiwa ipo.


“Ni faraja kwangu, wazazi wangu, walimu na wadau wa michezo kwa ujumla, ni heshima kwa Taifa kwani naiwakilisha nchi katika mafunzo hayo, sitawaangusha, nitafanya vizuri na ninaamini makocha wa NBA watavutiwa na kipaji changu na kusonga mbele,” alisema Jesca.


Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania (TBF), Mwenze Kabinda amempongeza Jesca kwa kupata nafasi hiyo na kuomba kuongeza bidii kwani hiyo ndiyo njia ya mafanikio.

WAFANYAKAZI WA MV LIEMBA WATAKIWA KUWAJIBIKA

$
0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa, amewataka manahodha na mabaharia wa meli ya MV. Liemba kufanyakazi kwa ubunifu na uadilifu ili kuiwezesha meli hiyo kujiendesha kibiashara.

Akizungumza na wafanyakazi wa meli hiyo Prof. Mbarawa, ameelezea kuridhishwa na mabadiliko yanayoendelea katika meli hiyo na kuwataka wasibweteke bali waongeze ubunifu.“Hakikisheni mnatoa huduma bora kwa wateja wenu na kupata faida ili serikali na wadau wengine wawaamini na kutumia huduma yenu”, amesisitiza Prof. Mbarawa.

Waziri Prof. Mbarawa ameitaka meli hiyo kuongeza safari zake kutoka awamu tatu hadi kumi kwa mwezi ili kuhuisha huduma za usafiri na uchukuzi katika Ziwa Tanganyika. 

Prof. Mbarawa ambaye yuko katika ziara ya ukaguzi wa miundombinu mkoani Kigoma amepata fursa ya kukagua utendaji wa meli ya MV. Liemba, kupata chakula cha pamoja na wafanyakazi wake katika meli hiyo na hatimae kutoa maelekezo kwa manahodha na mabaharia wa meli hiyo kongwe hapa nchini.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akipata chakula na manahodha na mabaharia wa meli ya MV Liemba inayofanya safari katika Ziwa Tanganyika.
Muonekano wa meli kongwe ya MV. Liemba ikiwa imetia nanga katika bandari ya Kigoma, meli hiyo imeatkiwa kuongeza safari zake kutoka awamu tatu hadi kumi kwa mwezi.

MPINA AWAPONGEZA VIONGOZI WA MIKOA WILAYA NA HALMASHAURI NCHINI WALIOTEKELEZA KIKAMILIFU AGIZO LA USIMAMIZI WA USAFI WA MAZINGIRA.

$
0
0

NA EVELYN MKOKOI –MASWA

Naibu waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na mazingira Mhe. Luhaga Mpina, amewapongeza viongozi wa mikoa wilaya na halmashauri nchini waliotekeleza kwa kiwango cha kuridhisha agizo la kusimamia utekelezaji wa siku ya kitaifa ya kufanya usafi na kuhakikisha usafi wa mazingira katika maeneo yao unaimarishwa.

Mpina ameyasema hayo leo Wilayani Maswa alipokuwa akishiriki zoezi la kufanya usafi kitaifa na kuongeza kuwa majina ya viongozi hao pamoja na wale ambao wamezembea kutekeleza agizo hilo yatafikishwa kwa Mhe. Rais na Mhe. Makamu kwa hatua za kiutendaji.

“Hatuwezi kufikia mapinduzi ya uchumi wa viwanda kama taifa litaendelea kuwa chafu kwani tutaendelea kupoteza nguvu kazi nyingi kutokana na maradhi yanayosababishwa na uchafu, hivyo viongozi wa mikoa na wilaya wana jukumu kubwa la kusimamia usafi wa mazingira.” Alisisitiza Mpina.

Naibu Waziri Mpina aliongeza kwa kusema kuwa serikali imeona kuwa usafi ndio afya na usafi ndio maisha na ndio maana Serikali imeitenga siku ya Jumamosi ya mwisho wa mwezi kuwa ni siku maalum kwa ajili ya usafi wa Mazingira. 

Akiwa ziarani wilayani Maswa Mhe. Mpina alibaini changamoto mbalimbali za kimazingira zinazoikumba wilaya hiyo ikiwa ni pamoja na upungufu wa matundu ya vyoo katika soko la Maswa, mazingira yasiyoridhisha ya kufanyia biashara sokoni na ukosefu wa maji katika machinjio ya wilaya, ambapo aliekeza uongozi wa Halmashauri kuhakikisha ndani ya miezi mitatu changamoto ya upungufu wa matundu ya choo iwe imefanyiwa kazi, kuwepo kwa mabanda ya kisasa ya kufanyia biashara katika soko hilo na kuhakikisha kunakuwepo na maji ya kutosha wakati wote katika machinjio.

Kwa Upande wake kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Bw. Vivian Christopher, alieleza kuwa Halmashauri yake imetenga fedha kwa ajili ya kushughulikia changamoto hizo katika Bajeti wilaya kwa mwaka wa fedha 2017/2018.

Pichani Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina Akizungumza na Baadhi ya wakazi wa Halmashauri ya Wilaya wa Maswa (hawapo katika picha)  leo baada ya kukamilika kwa zoezi la usafi.




VIJUSO VYA MAGAZETI YA JUMAPILI LEO JULY 30,2017

TANZANIA SIYO LANGO LA KUPITISHIA DAWA ZA KULEVYA-MAJALIWA

$
0
0
*Aagiza kuimarishwa kwa ukaguzi wa watu, magari na mizigo mipakani

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania siyo lango la kupitishia dawa za kulevya kwenda nchi za nje hivyo ameagiza ulinzi uimarishwe katika mipaka yote.

Amesema kunatabia ya baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu kutumia Tanzania kama njia ya kupitisha dawa za kulevya kwa ajili ya kupeleka nchi za Afrika ya Kusini, Malawi na Zambia.

Alitoa kauli hiyo jana jioni (Jumamosi, Julai 29, 2017) alipozungumza na watumishi wa kituo cha forodha cha Kasumulu kilicho katika mpaka wa Tanzania na Malawi wilayani Kyela.

Waziri Mkuu alisema ili kuhakikisha jambo hilo linadhibitiwa ni vema ukaguzi wa watu wanaopita kwenye maeneo hayo pamoja na mizigo ukaimarishwa.“Endeleeni kufanya upekuzi wa kina wa magari, watu na mizigo yote yote katika mipaka yetu. Tanzania siyo lango la kupitishia dawa za kulevya na Serikali haitakubaliana na jambo hilo.”

Pia aliwataka viongozi hao kuhakikisha biashara zote za magendo zinazifanyika mipakani, zikiwemo za kubadilisha fedha zinadhibitiwa kwa kuwa zinaikosesha Serikali mapato.

Alisema ni vema yakawepo maduka ya kubadilishia fedha katika maeneo hayo ili kudhibiti biashara hiyo ambayo kwa sasa inafanywa kimagendo huku Serikali ikikosa kodi.“Biashara za magendo zidhibitiwe katika maeneo haya na yaanzishwe maduka ya kubadilishia fedha ili biashara hiyo ifanyike kihalali. Pia imarisheni vyanzo vya mapato.”

Pia Waziri Mkuu aliwataka Maofisa wa Uhamiaji katika mikoa hiyo ya mipakani kuhakikisha wanadhibiti uingiaji holela wa raia wa kigeni kwa lengo la kuimarisha ulinzi nchini.

Waziri Mkuu alisema katika baadhi ya maeneo kwa sasa zimeanza kuonekana silaha ambazo hapo awali hazikuwepo na ndizo zinazosadikiwa kutumika katika matukio ya kihalifu.Awali, Bw. Taniel Magwaza ambaye ni Afisa Mfawidhi wa Uhamiaji alisema watahakikisha wanafanya kazi kwa weledi katika kupambana na biashara za magendo kwenye mpaka huo.

Alisema mbali na kupambana na biashara za magendo pia watadhibiti uingiaji wa wahamiaji haramu kwa kushirikiana na watumishi idara zote waliopo katika mpaka huo wa Kasumulu.Bw. Magwaza alisema katika doria zilizofanywa mwaka 2016/2017 jumla ya wahamiaji haramu 87 walikamatwa na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Alisema wahamiaji hao walitokea nchi za Malawi (30), Ethiopia (47), Burundi (6) Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) (4), ambapo baadhi walirudishwa makwao na wengine walifungwa katika Gereza la mkoa wa Mbeya.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAPILI, JULAI 30, 2017

IGP SIRRO AMALIZA ZIARA YAKE MIKOA YA KANDA YA ZIWA KWA KISHINDO

$
0
0

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akizungumza na baadhi wa Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoa wa Singida, wakati alipofika katika Ofisi ya Mkuu wa mkoa huo kwa lengo la kujitambulisha na kuzungumza na askari na maofisa wa Jeshi hilo pamoja na kujua changamoto wanazokutananazo wakitekeleza majukumu yao. Picha na Jeshi la Polisi.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akizungumza na askari na maofisa wa Jeshi hilo na kuwataka wafanyekazi kwa kutenda haki na kusimamia misingi ya sheria na taratibu, IGP Sirro yupo mkoani Singida kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kujitambulisha na kuzungumza na askari na kujua changamoto wanazokutananazo wakitekeleza majukumu yao. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akizungumza na kikosi cha Polisi wanawake baada ya kukagua gwaride la heshima lililoandaliwa kwa ajili yake alipowasili mkoani Singida, kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kujitambulisha na kuzungumza na askari na kujua changamoto wanazokutananazo wakitekeleza majukumu yao. Picha na Jeshi la Polisi.

………………………………………………………………………

Na Jeshi la Polisi Nchini

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, amemaliza ziara yake katika mikoa ya kanda ya ziwa pamoja na mkoa wa Singida, huku akiacha morali kwa watendaji wa Jeshi hilo hatua ambayo italiwezesha ieshi hilo kufanyakazi zake kwa weledi katika kukabiliana na matishio ya uhalifu na wahalifu.

IGP Sirro, amefanya ziara hiyo ikiwa ni mkakati wake aliojiwekea tangu alipoteuliwa kuwa Mkuu wa Jeshi hilo kwa lengo la kujitambulisha na kuzungumza na askari na maofisa ili kujua namna wanavyotekeleza majukumu yao ya kazi za Polisi.

Katika mazungumzo yake IGP Sirro, amewataka askari na maofisa kutimiza wajibu wao kwa kutenda haki na bila uwoga wala kumuonea mtu muhali jambo ambalo litarahisisha upatikanaji wa taarifa za uhalifu na wahalifu katika jamii.

Hata hivyo, katika mabaraza ya kuzungumza na askari na maofisa baadhi ya hoja kadhaa ziliibuliwa kwa baadhi ya askari waliopata nafasi ya kutoa mawazo yao, ambapo IGP Sirro aliahidi kuzishughulikia mapema ili kuzidisha morari katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Aidha, katika ziara yake IGP Sirro, alipata fursa ya kukutanana Wajumbe wa Kamati za Ulinzi na Usalama ya mkoa huku masuala kadhaa ya kiusalama na mbinu na mikakati ikijadiliwa katika kamati hizo na kuahidi kutoa ushirikiano utakaowezesha kukabiliana na matishio mbalimbali ya kiuhalifu.

Viane Kundi wa Iringa ajishindia Milioni 20 za Biko

$
0
0

*Issa naye achota Mil 10 zake.

Na Mwandishi Wetu, Dar es SalaamBAHATI Nasibu ya Biko ‘Ijue Nguvu ya Buku’ imezidi kushika kasi baada ya droo yake ya 27 kutua kwa Viane Kundi wa mjini Iringa, nchini Tanzania aliyevuna jumla ya Sh Milioni 20, huku Ally Issa Kumburu mkazi wa Mwananyamala, jijini Dar es Salaam naye akivuna Sh Milioni 10 za Tamasha la Komaa Concert, lililofanyika jana na kudhaminiwa kwa kiasi kikubwa na Biko.
Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Emmanuel Ndaki, kushoto akiandika dondoo katika droo ya Komaa Concert iliyorudiwa leo asubuhi baada ya jana kutopaatikana mshindi katika Tamasha la Komaa lililoandaliwa na EFM Radio na kudhaminiwa na Bahati Nasibu ya Biko Tanzania. Kulia ni Balozi wa Biko, Kajala Masanja.
Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Emmanuel Ndaki, kushoto akiandika dondoo katika droo ya 27 ya Biko ambapo Viane Kundi wa Iringa, alitangazwa mshindi na kuzoa Sh Milioni 20 za Biko. Kulia ni Balozi wa Biko, Kajala Masanja.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Paulo Makonda, akizungumza na wadau wa muziki waliofurika katika Tamasha la Komaa Concert lililoandaliwa na EFM Radio kwa udhamini mkubwa wa Bahati Nasibu ya Biko 'Ijue Nguvu ya Buku'. Katika Tamasha hilo lililokwenda na kumpata mshindi wa Sh Milioni 10 limempata Ally Issa Kumburu wa Mwananyamala, aliyepatikana katika droo iliyochezeshwa leo baada ya ndani ya tamasha kutopokea simu kutokana na wingi wa watu na kelele za uwanjani Tanganyika Packers, Kawe. Mwingine pichani ni Mkurugenzi wa EFM Radio, Denis Busurwa (Sebo). Picha na Mpigapicha Wetu.

Msanii nyota wa muziki wa Bongo Fleva, Dogo Aslay, pichani akiwachezesha mashabiki wake waliofurika katika Tamasha la Komaa Concert lililoandaliwa na EFM Radio kwa udhamini mkubwa wa Bahati Nasibu ya Biko 'Ijue Nguvu ya Buku'. Katika Tamasha hilo lililokwenda na kumpata mshindi wa Sh Milioni limempata Ally Issa Kumburu wa Mwananyamala, aliyepatikana katika droo iliyochezeshwa jana baada ya ndani ya tamasha kutopokea simu kutokana na wingi wa watu na kelele za uwanjani Tanganyika Packers, Kawe.


Droo zote mbili zilichezeshwa leo jijini Dar es Salaam kwa kuendeshwa na Balozi wa Biko, Kajala Masanja na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Emmanuel Ndaki, ambapo ni matokeo ya kutopatikana kwa mshindi wa tamasha la Komaa Concert, lililofanyika juzi katika Viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika droo hiyo ya 27, Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema kupatikana kwa washindi hao ni sehemu ya kuendelea kugawa fedha kwa kwa wote wanaoshinda katika mikoa mbalimbali ya Tanzania, akiwamo Kumburu wa Komaa Concert, mkazi wa Mwananyamala, jijini Dar es Salaam na Viane aliyejinyakulia Sh Milioni 20 akitokea mkoani Iringa.

Alisema Viane amekuwa mshindi wa Sh Milioni 20 wa droo ya 27, ambapo anakuwa mmoja kati ya washindi wengi wanaojichotea zawadi nono ya Sh Milioni 20 kutoka Biko kwa droo ya Jumapili na Jumatano, pamoja na zawadi za papo kwa hapo kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja zinazolipwa moja kwa moja kwenye simu za washiriki wao, huku akiwataka Watanzania wacheze mara nyingi zaidi ili wajiwekee nafasi nzuri za kushinda zawadi za papo kwa hapo pamoja Milioni 20 kwa droo ya Jumatano na Jumapili.

“Jinsi ya kushinda Biko ni rahisi kwa sababu mshiriki anapaswa kufanya muamala kwenye simu yake kama vile Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel Money ambapo ataweka Sh 1,000 na kuendelea, huku namba yetu ya Kampuni ni 505050 na ile ya kumbukumbu ni 2456,” Alisema Heaven na kuwataka Watanzania kuendelea kucheza Biko ili waibuke na ushindi.

Naye Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Emmanuel Ndaki, alisema washindi wote wawili wamepatikana kwa kupigiwa simu, huku akisema kuwa droo ya Tamasha la Komaa Concert imerudiwa ili kujenga uhalisia, baada ya washindi wote wa jana kutopokea simu.

“Bodi yetu ipo makini kufuatilia michezo hii ya kubahatisha, hivyo tunawapongeza washindi wote wawili wa Komaa Concert ambaye ni Kumburu wa Mwananyamala pamoja na binti wa Iringa, anayejulikana kama Viane ambaye naye ameingia kwenye orodha ya washindi wa mamilioni ya Biko,” Alisema.

Kwa kutangazwa washindi wa Biko, Watanzania hao wenye bahati wanatarajiwa kukabidhiwa fedha zao mapema wiki ijayo, ikiwa ni mwelekeo wa Biko kutoa mamilioni ya fedha kwa washindi wao, huku kwa mwezi Mei na Juni pekee ikitoa zaidi ya Sh Bilioni moja kwa washindi mbalimbali wa bahati nasibu yao.

JAFO AHIMIZA WANANCHI KUTUNZA MIRADI YA MAJI

$
0
0
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo amewataka wananchi wa wilaya ya Ukerewe kutunza miradi ya Maji kwa kuwa serikali inaigharamia kwa fedha nyingi.

Jafo aliyasema hayo alipotembelea mradi mkubwa wa maji wa Kazilamkanda ambao utahudumia vijiji vipatavyo 13 wilayani humo.

Amesema serikali inafanya jitihada za kuwatatulia wananchi wake kero mbalimbali ikiwemo ya upatikanaji wa huduma ya maji, hivyo ni vyema wakatunza miundombinu ya miradi hiyo ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

Akikagua mradi huo, Jafo alimpongeza Mkandarasi aliye jenga chanzo na tanki la kuhifadhia maji la lita 680,000 ambaye ni Lutare Make Enginnering Ltd kwa kazi nzuri.

Amesisitiza kukamilishwa kwa usambazaji wa Maji katika vijiji vyote 13 kabla  ya Disemba 30 mwaka huu.

Naibu Waziri huyo amesisitiza kulazwa mabomba yaliyo na ubora ili kuepusha kupasuka kwa mabomba endapo mabomba hayo yatakuwa hayana viwango na kusababisha hasara kubwa kwa wananchi na halmashauri baada ya kukabidhiwa mradi husika.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akizungumza na wananchi wa kijiji cha Rutala wilayani Ukerewe mkoani Mwanza juu ya utunzaji wa miradi ya maji.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akipata taarifa kuhusu miradi ya maji wilayani Ukerewe.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akifanya ukaguzi wa tenki la maji.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akifanya ukaguzi wa mashine za kusukumia maji.

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII MHANDISI RAMO MAKANI, AMUAGIZA MKUU WA WILAYA YA MUHEZA KUSHUULIKIA MGOGORO WA HIFADHI YA MSITU WA DEREMA WILAYANI HUMO

$
0
0
Na Hamza Temba - WMU - Muheza, Tanga
.............................................................................

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani ameuagiza uongozi wa Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga kukutana na wakulima 879 wa vijiji vitano katika Tarafa ya Amani Wilayani humo kwa ajili kufanya uhakiki wa malipo ya fidia ya mazao waliyolipwa na Serikali ili kupisha eneo la hifadhi ya msitu wa Derema.


Mhandisi Makani ametoa agizo hilo jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Msasa IBC, Tarafa ya Amani, Wilayani Muheza kufuatia malalamiko ya wananchi hao kupunjwa malipo yao wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani humo kwa ajili kutatua mgogoro wa ardhi uliodumu kwa zaidi ya miaka 15 baina Serikali na wananchi wa vijiji hivyo vya Kisiwani, Kwemdim, Msasa IBC, Antakae na Kambi.


Akisoma risala ya wakulima hao mbele ya Naibu Waziri Makani, Mwenyekiti wa Kamati ya wakulima hao, Mohammed Rama Shesha alidai kuwa jumla ya wakulima 1,128 wa vijiji hivyo wanailalamikia Serikali kwa kuwalipa viwango pungufu vya malipo ya fidia ya mazao yao tofauti na viwango vilivyolipwa na Serikali mwaka 2002 kupitia mradi wa FINIDA. Aidha, alidai kuwa kuna baadhi ya mazao pia hayakulipiwa kabisa fidia hizo.


Akizungumzia viwango vya fidia hizo Shesha alisema wananchi walilipwa Shilingi 28,800 kwa mche mmoja wa iliki na Shilingi 11,000 kwa mche mmoja wa mgomba. Alidai viwango hivyo vilibadilika kuanzia mwaka 2005 ambapo walilipwa Shilingi 3,315 kwa kila mche mmoja badala ya Shilingi 5,100 kama ilivyoainishwa kwenye viwango vya Serikali hivyo akaomba walipwe kiasi kilichobakia cha shilingi 1,785.


Akitolea ufafanuzi wa malalamiko hayo, Naibu Waziri Makani alisema idadi kamili ya wananchi waliohakikiwa katika eneo hilo ni 879 na sio 1,128 kama alivyodai mwenyekiti huyo. Aidha, alisema viwango vilivyotumiwa kuwalipa wananchi hao mwaka 2002 sio vya Serikali na kwamba vilitumiwa na mradi wa FINIDA uliofadhiliwa na Serikali ya Finland kwa ajili ya kulipa fidia wananchi wa mpakani na hifadhi hiyo ili kufanikisha zoezi la kuanisha mpaka wa hifadhi hiyo na kusaidia Serikali kutimiza azma ya kuhifadhi eneo hilo.


Alisema viwango halali vya Serikali vilivyopo kisheria kwa ajili ya kulipa fidia ya mimea hiyo ni kuanzia Shilingi 5,100 kwa kiwango cha juu kwa mmea uliokoma kufikia kiwango cha uzalishaji, Shilingi 3,315 kwa mmea wenye mwaka mmoja na Shilingi 2,040 kwa mmea wenye mwezi mmoja. Alisema viwango vingine vya malipo kwa kiwango cha chini ni Shilingi 204, Shilingi 102 na Shilingi 51.


Alisema Serikali iliamua kulipa kiwango cha Shilingi 3,315 kwa mazao yote ikiwemo yale yaliyostahili kulipwa kiwango cha chini kabisa cha Shilingi 51 ili kuweka uwiano na kurahisha zoezi hilo la malipo. Alihoji kama kuna mwananchi yeyote aliyelipwa chini ya kiwango hicho japokuwa kulikuwepo na wengine mazao yao yalistahili kulipiwa viwango hivyo, hakuna aliyejitokeza.


Kufuatia ufafanuzi huo aliuagiza uongozi wa Wilaya ya Muheza kutumia kipindi cha mwezi mmoja kuanzia leo Jumatatu kuonana na wakulima hao ili kuhakiki malipo yao na hatua zaidi ziweze kuchukuliwa kama kuna yeyote aliyezulumiwa apewe haki yake. 


"Kwa wale ambao tayari wana kumbukumbu zao vizuri wazilete mbele ya Serikali, kupitia wao pengine tunaweza kupata picha ya jumla pengine kulikua na mapungufu kwenye malipo. Kuanzia jumatatu ijayo Mhe. DC tulitekeleze hilo la kukusanya nyaraka kwa wale walizonazo tuweze kuzilinganisha na zile tulizokua nazo Serikalini tujadiliane nao kwamba ni kitu gani kimebaki tofauti katika maeneo yale yale mliyofanyiwa uhakiki", alisema Mhandisi Makani.


Alisema kwa wale ambao wamepoteza nyaraka zao za malipo wataandaliwa utaratibu maalum wa uhakiki kwa kuwa kumbukumbu zote za malipo zipo kwenye Kompyuta za halmashauri ya Wilaya ya Muheza.


Alisema lengo la Serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha inamaliza kabisa migogoro ya ardhi nchini. “Tutahakikisha tunaboresha zaidi usimamizi wa uhifadhi wa rasilimali zetu za misitu, wanyamapori na nyinginezo kuhakikisha migogoro hiyo inapungua kwa kasi kuelekea kwenye sifuri, zero rate", alisema Makani.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Mwanaisha Tumbo alisema, Serikali ya Wilaya imepokea maelekezo hayo na itayafanyia kazi na kwamba maafisa wa Halmashauri watafika katika kila kijiji siku ya Jumatatu na Jumatano kwa ajili ya kuendesha zoezi hilo la uhakiki.


Akizungumzia zoezi la fidia Mkuu huyo wa Wilaya alisema pamoja na wananchi hao kulipwa fidia za mazao yao ambayo yalilipwa kwa awamu tatu, asilimia 50 mwaka 2005, asilimia 25 mwaka 2006 na asilimia 25 mwaka 2008, pamoja na asilimia 23 kama fidia ya ucheleweshaji wa deni, Serikali pia itawapa maeneo ya fidia ambapo kila mwananchi aliyeathirika eneo lake atapewa ekari tatu.


Alisema eneo ambalo limeanishwa kwa ajili ya kuwagawia wananchi hao ni lililokuwa shamba la mkonge Kibaranga ambalo lina ukubwa wa hekta 1370 sawa na ekari 3425 na lilikua likimilikiwa na Bodi ya Mkonge, eneo hilo lilitolewa tamko ya kufutiwa umiliki wake na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli mwezi Julai, 2016.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (katikati), akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Msasa IBC wilaya ya Muheza mkoani Tanga jana wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani humo kwa ajili kutatua mgogoro wa hifadhi ya msitu wa Derema. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Mwanaisha Tumbo. 
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (katikati), akimuonesha mwenyekiti wa kamati ya wakulima wa vijiji vitano vya tarafa ya Amani, Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga, Mohammed Ramadhani Shesha viwango halali vya serikali vya kulipia fidia za mazao kwa wananchi waliondolewa katika eneo la hifadhi ya msitu wa Derema wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani humo jana kwa ajili ya kutatua migogoro wa hifadhi hiyo. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Mwanaisha Tumbo.  
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (kulia), akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Msasa IBC wilaya ya Muheza mkoani Tanga jana wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani humo kwa ajili kutatua mgogoro wa hifadhi ya msitu wa Derema.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani, (wa tatu kushoto), akiangalia eneo la Msitu wa hifadhi ya Derema na viongozi wa wilaya ya Muheza Muheza wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani humo jana kwa ajili ya kutatua mgogoro wa hifadhi hiyo. 
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (kulia), akisalimiana na wananchi wa Kijiji cha Msasa IBC wilaya ya Muheza Mkoani Tanga jana wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani humo kwa ajili ya kutatua mgogoro ya hifadhi ya msitu wa Derema. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (kushoto), akimuonesha mwenyekiti wa kamati ya wakulima wa vijiji vitano vya tarafa ya Amani, Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga, Mohammed Ramadhani Shesha (kulia) viwango halali vya serikali vya kulipia fidia za mazao kwa wananchi waliondolewa katika eneo la hifadhi ya msitu wa Derema wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani humo jana kwa ajili ya kutatua migogoro wa hifadhi hiyo. 

DED ILEJE AINGIA DARASANI 'KUPIGA' CHAKI

$
0
0
 Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ileje Mkoani Songwe Haji Mnasi akiwa darasani kufundisha wanafunzi wa shule msingi alizotembea katika ziara yake
 Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ileje Mkoani Songwe Haji Mnasi akiwa darasani kufundisha wanafunzi  huku wanafunzi wakiwa makini kusikiliza nini wanachofundishwa na Mkurugenzi hiyo.

Na Fredy Mgunda,Ileje

Katika hali isiyozoeleke kwa watumishi wengi wa Idara ya Elimu wilayani Ileje mkoani Songwe  kwa Mkurugenzi Mtedaji wa Halmsahauri ya wilaya hiyo kwa kuingia kwenye baadhi  ya shule za msingi na kufundisha.

Mkurugenzi huyo Ndugu Haji Mnasi ambaye kitaaluma ni mwalimu aliamua kufanya hivyo katika ziara  ya kushtukiza aliyoifanya kweye shule za Nyerere,Rungwa na Itumba zilizopo katika kata za Itumba na Isongole Tarafa ya Bulambya.

Akiwa katika shule ya Msingi Nyerere aliweza  kufundisha masomo ya Kiiingeriza,Hisabati na Kiswahili, pia aliweza kupima uelewa wa wanafunzi pamoja na kutoa maswali machache ya kuandika.

Ziara hiyo iliweza pia kumfikisha katika Shule ya Msingi Rungwa ambapo aliweza kuzungumza na walimu akiwapa moyo katika kuwapatia elimu bora wanafunzi akiwapa moyo wa utendaji kazi akiwataka kuzingatia  maagizo mbalimbali ya serikali.

Pia Mkurugenzi huyo,aliyekuwa amefuatana na mmoja wa viongozi wa Idara ya Elimu Msingi akiwa Rungwa aliweza kuzungumza na mafundi waliokuwa wakiendelea na ujenzi ambapo aliwataka kumaliza kazi kwa wakati wakifuata viwango vinavyotakiwa.

Ziara yake kwa siku hiyo ilishia katika shule ya Msingi Isongole ambako alipata fursaa kufuwatathimini wanafunzi wa Darasa la Saba ambao walikuwa wametoka kumalizia mtihani wa Moko ya Wilaya.

Mara baada ya kumalizia ufundishaji kwa masomo ya Hisabati,Kiswahili na Kiingereza Mkurugenzi huyo aliwapongeza walimu wa shule hiyo kwa jinsi walivyowaanda wanafunzi wao ambao wanatarajiwa kufanya Mtihani wa Taifa siku chache zijazo.

Walimu kwa upande wao walimpongeza mwajiri wao kwa kuweza kutembelea shule yao na kuzungumza nao wakisema hali hiyo imewapaa ari ya kufanya kazi wakishauri ziara hiyo iendelee na kwa shule zingine

Mwalimu Denis Umbo alisema kuwa ,kitendo cha mwajili wao kuingia darasani hakijawatia moyo wa kufanya kazi tu bali ameitendea haki  taaluma yake na kujionea hali halisi ilivyo mashuleni badala ya kusubiri taarifa za mezani.

Si hayo tu yaliyojili katika shule hiyo pia Mkurugenzi  alibahatika kuzungumza na  wananchi waliokuwa kwenye mkutano  ambao pamoja na mambo mengine walitarajia kujadili masuala mbalimbali ya shule likiwemo la chakula cha mchana  kwa wanafunzi na taaluma.

Mnasi aliwataka wazazi hao kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali ya Awamu  ya Tano juu ya utoaji elimu bure kwa watoto wote hapa nchini.

MBUNGE ROSE TWEVE WATENDAJI FANYENI KAZI ACHENI MAJUNGU

$
0
0

Mbunge wa viti Maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi CCM Rose Tweve akizungumza na madiwani na wananchi wa halmashauri ya Mafinga Mjini wakati wa baraza la madiwani
Mwenyekiti wa halmashauri ya Mafinga Mjini Charles Makoga akizungumza wakati wa baraza la madiwani lilofanyika katika ukumbi wa halmashauri hiyo
Baadhi ya madiwani,viongozi pamoja na wananchi waliohudhuria baraza la madiwani lilofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya Mafinga Mjini.

Na fredy Mgunda, Mafinga.

Mbunge wa viti Maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi CCM Rose Tweve amewata watendaji wa halmashauri ya Mafinga Mjini kufanya kazi kwa kujituma na kuwa tumikia wananchi wa Jimbo la Mafinga Mjini ambalo linaongozwa na mbunge Cosato Chumi.

Akizungumza wakati wa baraza la madiwani wa halmashauri ya Mafinga Mjini alisema kuwa watendaji wengi wamekuwa wakilalamikiwa kutokana na kufanya kazi chini ya kiwango na kuwapelekea wananchi kuwa na changamoto ambazo hazina sababu.

"Hivi watendaji kitu gani kinachosababisha msifanye kazi kwa weledi kama ambavyo mlivyokuwa mnaomba kazi,jamani serikali ya awamu ya tano haitaki mfanye kazi kwa mazoea kama zamani saizi mnatakiwa kufanya kazi kutokana na kasi ya kimaendeleo ya serikali ya awamu ya tano"alisema Tweve

Tweve alisema kuwa watendaji wanaohusika na sekta ya maji katika halmashauri ya Mafinga Mjini wamekuwa hawafanyi kazi kwa weledi kwani tatizo kuwabambikia bili wananchi limekuwa Sugu na kuongeza malalamiko mengi huko mitaani hivyo lazima mbadilike maana swala la bili limekuwa kero sana hapa Mafinga Mjini lazima mlitafutie ufumbuzi.

"Toka nimerudi nimekuwa nikipokea malalamiko mengi yanayohusu bili za maji naombeni tembeleeni nyumba kwa nyumba kuandika bili sahihi na sio kutoa bili kwa kukisia hii inaalibu sura nzima ya viongozi wa halmashauri ya Mafinga Mjini, narudia tena watendaji fanyeni kazi kwa kujituma acheni mazoea kazini"alisema Tweve

Aidha Tweve alimuomba Mwenyekiti wa halmashauri hiyo kuhakikisha wanafanya kazi za wananchi na sio kukaa tu ofisini kitu kinachosababisha kuongezeka kwa matatizo kwa wananchi, hivyo mtalazimika kuwafuata wananchi kujua changamoto zinazowakabili wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa halmashauri ya Mafinga Mjini Charles Makoga alisema kuwa ahakikisha watendaji wote wanaenda kufanya kazi kwa wananchi na kuacha kufanya kazi kwa mazoea kama ilivyokuwa miaka ya huko nyuma na kuendelea kutekeleza Sera za chama cha mapinduzi CCM na kuendena na kasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John pombe Magufuli na kuwaletea maendeleo wananchi.

"Watendaji wangu mmekisikia alichosema mbunge Rose Tweve kuhusu wajibu kwa kweli hii ni aibu kubwa inatupaswa kujilekebisha ili kuendelea kutekeleza Sera za serikali ya awamu ya tano la sivyo nitaanza kuwatumbua mmoja baada ya mmoja ili kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi wa halmashauri ya Mafinga Mjini"alisema Makoga

Lakini Makoga aliwasifu wabunge Wawili ambao ni mbunge Cosato Chumi na Rose Tweve kwa kufanya kazi kwa nguvu na kuleta maendeleo ya wananchi wa wilaya ya Mufindi kwa ujumla maana kila siku tunapata mambo mapya ya kimaendeleo kupitia migongo yao na kuwaomba waendelee kutafuta njia nyingine za kuiletea maendeleo Mufindi.

"Miaka yote tungekuwa na wabunge kama hawa wawili leo hii Mufindi ingekuwa mbali sana kimaendeleo kutokana na Juhudi zao tunaziona maana saizi kila secta wameigusa kwa kuleta maendeleo au mikakati ya kutatua changamoto za maeneo husika" alisema Makoga

Nao baadhi ya watendaji wa halmashauri hiyo wasema kuwa bado wazitafutia ufumbuzi changamoto za Mji wa Mafinga licha ya kuwa na ufinyu wa bajeti za kimaendeleo kwenye miradi waliyoiomba hivyo wakipewa bajeti na kuajiri baadhi ya watumishi kila kitu kitaenda vizuri na changamoto za wananchi zitatuliwa kwa wakati.

WITO WATOLEWA KWA WANANCHI KUTOA USHIRIKIANO KWA WADADISI WA UTAFITI WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya Wadadisi wa Utafiti wa Awamu ya Pili wa Kutathmini Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotarajia kufanyika mwezi Agosti mwaka huu. Mafunzo hayo yamefungwa leo katika ukumbi wa Chuo cha Mipango mkoani Dodoma.
PICHA 2
Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Ladislaus Mwamanga akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya Wadadisi wa Utafiti wa Awamu ya Pili wa Kutathmini Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotarajia kufanyika mwezi Agosti mwaka huu. Mafunzo hayo yamefungwa leo katika ukumbi wa Chuo cha Mipango mkoani Dodoma.
PICHA 3
Mmoja wa Wadadisi Maro D. Maro akitoa neno la shukrani wakati wa kufunga mafunzo ya Wadadisi wa Utafiti wa Awamu ya Pili wa Kutathmini Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotarajia kufanyika mwezi Agosti mwaka huu. Mafunzo hayo yamefungwa leo katika ukumbi wa Chuo cha Mipango mkoani Dodoma.
PICHA 4
Baadhi ya Wadadisi na Wasimamizi wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa (hayupo pichani) wakati wa kufunga mafunzo ya Wadadisi wa Utafiti wa Awamu ya Pili wa Kutathmini Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotarajia kufanyika mwezi Agosti mwaka huu. Mafunzo hayo yamefungwa leo katika ukumbi wa Chuo cha Mipango mkoani Dodoma.
PICHA 5
Baadhi ya Wadadisi na Wasimamizi wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa (hayupo pichani) wakati wa kufunga mafunzo ya Wadadisi wa Utafiti wa Awamu ya Pili wa Kutathmini Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotarajia kufanyika mwezi Agosti mwaka huu. Mafunzo hayo yamefungwa leo katika ukumbi wa Chuo cha Mipango mkoani Dodoma. (PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO)
……………………………………………………………………………………..
Na: Veronica Kazimoto-Dodoma

 WITO umetolewa kwa viongozi wa Serikali na wananchi kwa ujumla kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Wadadisi watakaopita maeneo mbalimbali nchini kukusanya taarifa kwa ajili ya Utafiti wa Awamu ya Pili wa Kutathmini Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotarajia kufanyika mwezi Agosti mwaka huu.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kufunga mafunzo ya Wadadisi wa utafiti huo iliyofanyika leo mkoani Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Ladislaus Mwamanga amesema utafiti huo ni muhimu katika kunusuru kaya maskini nchini hivyo haina budi viongozi na wananchi kutoa ushirikiano kwa Wadadisi wa utafiti husika.
 
“Kwa namna ya pekee nawaomba Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya, Wakurugenzi wa Manispaa na Halmashauri, viongozi wa kata na vijiji na wananchi wote kwa pamoja mtoe ushirikiano wa hali ya juu kwa Wadadisi watakapokuwa katika maeneo yenu wakikusanya taarifa za utafiti huu”, amesema Mwamanga.
 
Nae Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa amesema lengo la kufanya mafunzo hayo ilikuwa ni kuwawezesha Wadadisi kufahamu taratibu zote zinazohusu kazi ya ukusanyaji taarifa na mbinu zinazotakiwa ili kupata taarifa sahihi kutoka kwenye kaya mbalimbali nchini.
 
Jumla ya Wadadisi 85 wamemaliza mafunzo ya siku 20 ya Utafiti wa Awamu ya Pili wa Kutathmini Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini yaliyoandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa kushirikiana na TASAF.


JAFO AWAJIA JUU WATAALAM WA AFYA NA AFISA MANUNUZI WILAYA YA UKEREWE

$
0
0


Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua chumba cha upasuaji kilichopo katika moja ya kituo cha Afya wilayani Ukerewe.
jf (2)
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akizungumza na wananchi katika hospitali ya wilaya ya Ukerewe.
jf (3)
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua majengo ya kutolea huduma katika Hospitali ya Ukerewe.
jf (4)
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua mfumo wa ukusanyaji mapato kwa njia ya kielektroniki katika hospitali ya wilaya ya Ukerewe.
jf (5)
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Frank Bahati katika ukaguzi wa miradi ya Afya.
jf (6)
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa Afya wilayani Ukerewe.
…………………………………………………….
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo amewajia juu Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya(DMO), Afisa Manunuzi, na mwakilishi wa Mweka hazina wa halmashauri ya wilaya ya ukerewe baada ya kushindwa kutoa ufafanuzi sahihi juu ya ununuzi wa dawa chini ya mfuko wa Afya wa pamoja (Busket Fund).

 Akiwa katika ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani humo, Jafo amefika kwenye hospitali ya wilaya ya ukerewe na kuwaomba wananchi waliokuwepo hospitalini hapo kueleza changamoto wanazozipata wanapofika hospitalini hapo.

 Kufuatia changamoto walizoeleza wananchi, Jafo alionyesha kukerwa kutokana na maafisa hao kushindwa kujibu hoja ya wananchi waliokuwa wakilalamika kwamba wanapofika kwenye hospitali hiyo mara nyingi wataalam wamekuwa na kauli mbaya sambasamba na kukosa dawa. 
 Jafo aliwageukia wataalam hao kwa kuwauliza ni kiasi gani cha fedha za basket fund wamepokea kwa mwaka Fedha 2016/2017 na kiasi gani kilitumika kununua dawa na vifaa tiba.

 Kutokana na Jafo kuhoji fedha hizo, wataalam hao wote walishindwa kufahamu, jambo lililomkera Naibu Waziri Jafo.

 Alisema ameshangazwa na kitendo cha wataalam wahusika kushindwa kutambua mambo ya msingi ambayo wanapaswa kuyasimamia ili kutatua kero ya afya kwa wananchi.

 Jafo aliwajulisha wananchi kuwa halmashauri yao imepokea jumla ya sh.milioni 727.4 ambapo 33% ilipaswa kununulia dawa na vifaa tiba.
 Naibu Waziri Jafo amewataka watumishi wote kusimamia mipango ya serikali ili kutatua kero za  wananchi ili kuleta maendeleo katika jamii.

WAZIRI MKUU AWAASA WATUMISHI WANAOFANYAKAZI VIWANDANI

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi wa umma wa wilaya ya Rungwe Julai 30, 2017. Kulia ni Naibu Spika, Dkt. Tulia Ackson na kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wa kiwanda cha gesi cha TOL Gasese Limited kilichopo katika kijiji cha Ikama wilayani Rungwe Baada ya kuwasili kiwandani hapo Julai 30, 2017 Kushoto ni Naiobu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana viongozi wa kiwanda cha chai cha Katumba wilayani Rung wakati alipowasili kiwandani hapo kukagua shuguli za kiwanda hicho Julai 30, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitembelea kiwanda cha chai cha Katumba wilayani Rungwe Julai 30, 2017. Kulia ni Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla na kushoto ni Meneja Uzalishaji wa kiwanda hicho, Ramadhani Kampasili. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akitazama chai iliyosindikwa na kufungashwa tayari kwa kuuzwa wakati alipotembelea kwianda cha chai cha Katumba wilayani Rungwe Julai 30, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri )
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi wa Rungwe baada ya kutembelea kiwanda cha Chai cha Katumba Julai 30, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezokutoka kwa Mkutugenzi wa Ufundi, Bw. McJohn Mbiri (kulia Kwake) kuhusu mitambo ya kuzaisha gesi ya hewa ya ukaa wakati alipotembelea kiwanda cha TOL Limited kilichopo katika kijiji cha Ikama wilayani Rungwe Julai 30, 2017. Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wazee wa Busokelo baada ya kuwasili kwenye uwanja wa michezo wa Kandete katika jimbo la Busokelo kuhutubia mkutano wa hadhara Julai 30, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifuhia ngoma ya asili baada ya kuwasili kwenye uwanja wa michezo wa Kandete katika jimbo la Busokelo mkoani Mbeya kuhutubia mkutano wa hadhara Julai 30, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Baadhi ya watumishi wa umma wa wilaya ya Rungwe wakati alipozungumza nao leo Julai 30, 2017.

…………………………………………………………………..

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasihi Watanzania wanaofanya kazi katika viwanda mbalimbali nchini kufanya kazi kwa bidii na kuwa waaminifu.

Amesema Tanzania imedhamiria kukuza uchumi wake kupitia sekta ya viwanda hivyo ni vema watakaopata fursa ya ajira katika viwanda hivyo kuwa waadilifu.

Ameyasema hayo leo (Jumapili, Julai 30, 2017) wakati akizungumza na wafanyakazi wa kiwanda cha gesi cha Ikama kilichoko wilayani Rungwe.

Waziri Mkuu amesema wakati Serikali ikiendelea kuwakaribisha wawekezaji nchini, wananchi walioajiriwa kwenye maeneo hayo wawe waaminifu.

“Mnatakiwa muwe waaminifu, msibebe kitu chochote ndani ya kiwanda bila ya ridhaa ya wamiliki kwa kuwa mtaonyesha taswira mbaya kwa wawekezaji.”

Amesema uaminifu wao ndio utawezesha Watanzania wengi kupata ajira kwenye viwanda hivyo ambavyo vimejengwa katika maeneo yao.

Awali, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa kiwanda hicho kinachomilikiwa na kampuni ya TOL Gases, Mhandisi Harold Temu alisema kiwanda kinauwezo wa kuzalisha tani 46 kwa siku.

Alisema gesi inayozalishwa kiwandani hapo ni ya Carbon Dioxide ambayo inauzwa nchini na nchi jirani za Zambia, Malawi, Zimbabwe na Congo.

Mhandisi Temu alisema wateja wakubwa wa gesi hiyo ni viwanda vya kutengenezea soda, bia na pia hutumika katika kuhifadhia chakula na kwenye vifaa vya kuzimia moto.

Mapema Waziri Mkuu alitembelea kiwanda cha kuchakata majani ya chai cha Katumba, ambapo alisema Serikali inaimarisha Ushirika wa zao hili ili wakulima waweze kupata tija.

Benki ya Watu wa Zanzibar PBZ Yaibuka Kidedea Katika Mwajiri Bora Katika Ushirikishwaji na Chama cha Wafanyakazi ZAFICOW.

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi ZAFICAW Bi. Rihii Haji Ali, akimkabidhi Cheti Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Ameir Khafidh cha Mwajiri Bora Katika Ushirikiano na ZAFICOW kwa mwaka 2017. wakati wa hafla ya Bonaza la Wafanyakazi wa PBZ lililofanyika katika ufukwe wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi ZAFICAW Bi. Rihii Haji Ali, akimkabidhi Cheti Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Ameir Khafidh cha Mwajiri Bora Katika Ushirikiano na ZAFICOW, wakati wa hafla ya Bonaza la Wafanyakazi wa PBZ lililofanyika katika ufukwe wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja. 
 Viongozi wa PBZ na wa ZAFICOW wakiimbi wimbo wa ushirikiano wa Wafanyakazi wakati wa hafla hiyo ya kukabidhiwa Cheti zilizofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Zanzibar. 
Wafanyakazi wa Benki ya Watu wa Zanzibar wakiimbi wimbo wa Wafanyakazi wa Mshikamano wakati wa mkutano wao na Mwenyekiti wa ZAFICOW wakati wa hafla ya bonaza la Michezo lililowashirikisha Wafanyakazi wa PBZ, 
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar ZAFICOW Bi. Rihii Haji Ali akitzungumza wakati wa mkutano huo na wafanyakazi wa PBZ kujuwa wajibu wao katika kazi na kuwataka kujiunga na Chama hicho kwa faida yao na maslahi kwa muajiri wao.Pia alikabidhi Kadi kwa Wanachama wapya ya PBZ 10 waliojiunga na kuwakabidhi Kadi za Uwanachama. 
Watendaji wa PBZ wakifuatilia mkutano huo na Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar Bi Rihii Haji Ali alipokuwa akizungumza na wafanyakazi hao wakati wa Tamasha la Bonaza la Wafanyakazi wa PBZ lililofanyika katika viwanja vya Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.
Wafanyakazi wa PBZ wakifuatilia mkutano huo na Uongozi wa PBZ na ZAFICOW uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Visiter Inn Jambiani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Ameir Khafidh akimkabidhi Kadi ya Mwanachama mpya wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar ZAFICOW Ndg. Suleiman Abdi, baada ya kujiunga na Chama hicho wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Ameir Khafidh akimkabidhi Kadi ya Mwanachama mpya wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar ZAFICOW Ndg. Bakari Hussein, baada ya kujiunga na Chama hicho wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Ameir Khafidh akimkabidhi Kadi ya Mwanachama mpya wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar ZAFICOW Bi. Fatima Ali Denge, baada ya kujiunga na Chama hicho wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Ameir Khafidh akimkabidhi Kadi ya Mwanachama mpya wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar ZAFICOW Bi. Mkunga Mohammed Saleh, baada ya kujiunga na Chama hicho wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.
Mkurugenzi Mtendajio wa Benki ya Watu wa Zanzibar Ngd Juma Ameir Khafidh akimkabidhi zawada ya fedha shilingi miliono moja kwa kuibuka Mfanyakazi Bora wa Benki ya Watu wa Zanzibar kwa mwaka 2017  Ndg. Juma Ameir Makame (kulia) akishuhudia Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar (ZAFICOW) Bi. Rihii Haji Ali hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja. 
Mfanyakazi wa Benki ya Watu wa Zanzibar Ndg.Haji Masoud, akikisoma Cheti cha Mwajiri Bora Katika Ushirikishwaji katika Chama  cha Wafanyakazi cha ZAFICOW, wakati wa kukabidhi na Uongozi wa ZAFICOW.  
Afisa Muandamizi Masoko wa Benki ya Watu wa Zanzibar PBZ Ndg. Anasi Rashid akizungumza na kutowa maelekezo wakati wa Mkutano huo wa Wafanyakazi na Uongozi wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar Wafanyakazi Zanzibar (ZAFICOW)  
Mkurugenzi Rasilimali Watu PBZ Ndg. Mohammed Omar (kulia) akimkabidhi zawadi maalum iliyotolewa na Wafanyakazi wa PBZ kwa Boss wao wakati wa Mkutano huo na Wafanyakazi wa PBZ Zanzibar hafla hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Zanzibar. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Ndg Juma Ameir Khafidh akitowa nasaha zake kwa Wafanyakazi wakati wa mkutano huo ulioambatana na michezo mbalimbali iliowashirikishwa Wafanyakazi kujumuika pamoja na kubadilishana mawazo Bonaza hilo limefanyika katika ufukwe wa Hoteli ya Visiter Inn Jambani.Mkoa wa Kusini Unguja.  
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg. Juma Ameir Khafidh akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo na Wafanyakazi uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Visiter Inn Jambiani Zanzibar.




Wafanyakazi wa PBZ wakipata viburudisho ya maji ya madafu baada ya mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.

Imeandaliwa na Othmanmapara.blog.
Zanzinews.com
othmanmaulid@gmail.com
Mobile.0777424152.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA JUMATATU LEO JULAI 31,2017

MAMA NAMAINGO ‘AWAFUNDA’ AKINAMAMA WA GREEN VOICES KILIMOBIASHARA NA UJASIRIAMALI

$
0
0


Mkurugenzi wa Namaingo, Biubwa Ibrahim


Mratibu wa Mradi wa Green Voices kutoka Hispania, Alicia Cedaba, akiwapa majukumu washiriki wa warsha hiyo.


MKURUGENZI Mtendaji wa kampuni ya Namaingo Business Agency, Biubwa Ibrahim, amewataka akinamama wanatekeleza mradi wa Green Voices Tanzania kuwa wabunifu na kutokata tamaa katika shughuli wanazozifanya.

Akizungumza wakati wa kufunga semina ya siku sita ya mafunzo yaliyowashirikisha akinamama 15, Biubwa alisema kwamba, ubunifu, jitihada na kutokata tamaa ndiyo silaha kubwa katika mafanikio, huku akiwahimiza watafute fedha bila kuchoka.

“Lazima muwe wabunifu, halafu ni dhambi kubwa kukata tamaa bali mnatakiwa kuongeza jitihada katika mradi yenu,” aliwahimiza.

Aidha, alisema kwamba, mafanikio yoyote hayawezi kuja kwa siku moja, hivyo wanapaswa kuwa wavumilivu daima ili waweze kufanikiwa.

Akinamama hao wa Green Voices wanatekeleza miradi mbalimbali ya kilimo inayoendana na mapambano dhidi ya uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi, ambayo inadhaminiwa na taasisi ya Women for Africa Foundation ya Hispania inayoongozwa na makamu wa rais mstaafu wa nchi hiyo, Bi. Maria Tereza Fernandes de la Vega.

Biubwa alisema, wajasiriamali wengi wanaposhindwa kuona faida ya shughuli wanazozifanya huvunjika moyo mapema, lakini hilo lisiwe kikwazo kwao kwani wanapaswa kukaa chini na kutafakari njia mpya ya kuendesha biashara ama miradi yao.

“Inabidi kujiuliza wewe mwenyewe kama hapo ulipo ndipo mahali sahihi, vinginevyo usife moyo unapoona mambo hayaendi, bali angalia wapi ulipokosea na ujipange upya halafu utaona matokeo yake,” alisema.

Akaongeza: “Mimi nilianza na mtaji wa shilingi elfu nne tu, nimepitia changamoto nyingi ikiwemo kudhulumiwa fedha, lakini katu sikukata tamaa nimeendelea kupambana na mpaka sasa kupitia kampuni yangu nimeweza kusajili wakulima 400,000 nchi nzima.”
Mwanahabari mshiriki wa mradi wa Green Voices, Farida Hamisi, akipokea cheti kutoka kwa Alicia Cedaba, Mratibu wa Green Voices kutoka Hispania. Katikati ni muwezeshaji wa mafunzo hayo, Dkt. Olomi kutoka taasisi ya IMED.

Mradi wa Green Voices unatekelezwa nchini Tanzania pekee, ambapo akinamama 10 kati ya 15 wanaendesha miradi mbalimbali ya kilimo, ufugaji wa nyuki, ukaushaji wa mboga na matunda pamoja na utengenezaji wa majiko rafiki katika jitihada za kupambana na mabadiliko ya tabianchi.


Akinamama walioanzisha miradi hiyo – miradi na mikoa watokayo vikiwa kwenye mabano –ni Regina Kamuli (Mkuranga, Pwani – Majiko Banifu), Abiah Magembe (Kisarawe, Pwani – Usindikaji wa Muhogo na Mtama), Magdalena Bukuku (Kinondoni, Dar es Salaam – Kilimo cha Uyoga), Mariam Bigambo (Dakawa, Morogoro – Ufugaji wa Nyuki), na Esther Muffui (Morogoro – Ukaushaji wa Mboga na Matunda).


Wengine ni Farida Makame (Kilimanjaro – Majiko ya Umeme-Jua), Leocadia Vedastus (Ukerewe, Mwanza – Kilimo na Usindikaji wa Viazi Lishe), Monica Kagya (Kisarawe, Pwani – Ufugaji wa Nyuki), Dkt. Sophia Mlote (Kinyerezi, Dar es Salaam – Kilimo Hai cha Nyanya na Mbogamboga), na Evelyn Kahembe (Uvinza, Kigoma – Kilimo cha Matunda).

Mradi huu wa Green Voices ambao mwaka huu uko katika awamu ya pili, ulizinduliwa Julai mwaka 2016 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan.

Katika awamu ya pili kinamama hawa wameendelea kuboresha kilimo cha mazao yao kinachozingatia uhifadhi wa mazingira na mabadiliko ya tabia nchi katika mikoa sita nchini.

“Pamoja na kilimo, Mradi wa Green Voices umaeandaa mafunz mbalimbali ya kuongeza ujuzi katika kilimo (climate smart agricultura) pamoja na mafunzo ya jinsi ya kuandaa mazao au bidhaa wanazozalisha kupitia kilimo,” alisema Mratibu wa Green Voices nchini Tanzania Secelela Balisidya.

Katika kutekekelza hilo, Green Voices kupitia mfadhili wake, Women for Africa Foundation, walishiriki katika mafunzo mbalimbali ya Mbinu bora za kuweka nembo na kufungasha bidhaa za vyakula, Viwango vya Ubora, na Kanuni za uchakataji wa vyakula.

Mafunzo hayo ambayo yalifanyika Julai 16 -22, 2017 yalizinduliwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), Selemani Jaffo, ambaye aliahidi kuwapa ushirikiano akina mama hao.


Utengenezaji bidhaa na ufungashaji


Kwa siku sita baada ya kuzinduliwa kwa mafunzo, akinamama hao walijifunza kuhusu Mchango wa kilimo katika mabadiliko ya tabianchi, Jinsi ya kuweka mazingira bora ya umwagiliaji, Mikakati ya biashara katika ujasiriamali wa kilimo, Utafutaji wa rasilimali na mkakati wa kuongeza mtaji, Ukuzaji wa mtaji kupitia Vicoba, na Mbinu za uongozi.


Akinamama hao walipata fursa ya kutembelea Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) ambapo ilikutana na wajasiriamali walio katika hatua za juu za kufungasha na kuuza bidhaa zao, ambapo walipata nafasi ya kubadilishana nao mawazo ili kuongeza ujuzi wao.


Katika mafunzo hayo, Linus Gedi ambaye ni mtaalam wa ubora wa chakula na viwango kabla ya kuvipeleka sokoni, aliwaeleza washiriki kwamba ni muhimu kufungasha na kuweka nembo kwani inasaidia kuhifadhi bidhaa na inarahisisha mteja kutambua hiyo ni bidhaa ya aina gani, imetengenezwa wapi na ina mchanganyiko gani.



Akinamama wanaotekeleza mradi wa Green Voices walipotembelea Ofisi za SIDO jijini Dar es Salaam.

“Ni muhimu sana kuhakikisha chakula hakisababishi maradhi, lakini pia kinafikia malengo ya walaji, hii huepusha sumu kwenye chakula, mchanganyiko usiofaa, upotevu wa chakula, kupoteza bidhaa na kuepukana na masuala ya kisheria,” alisema Linus.

Alisema uzalishaji wa chakula unatakiwa kuzingatia mbinu bora za uzalishaji na pamoja na usafi.

Aidha, aliwataka kuzingatia ubora, usafi na viwango vya chakula wanachozalisha ili kifikia malengo ya walaji.

Kwa upande wake, Richard Jackson akielezea umhimu wa kunadi bidhaa, alisema ni lazima kuwa na mikakati imara ya masoko ili kuhakikisha mjasiriamali anapata faida.

Alisema ni vizuri kujua wateja maalum na wateja wa ujumla na nini hasa wanahitaji ikiwa ni pamoja na namna ya kuwafikia.

“Ni lazima kujua kati ya wanaohitaji bidhaa zako, ni nani ambao siyo wateja wako walengwa na kwa nini wateja wanunue bidhaa zako na siyo kwa washindani wako? Lazima ujue tabia zao na ukubwa wa soko lako,” alisema Jackson.

Aidha, alisema ni muhimu kuwajua wateja wako ili kuelewa mahitaji yao na kwa nini wananunua bidhaa wanazonunua pamoja na kutambua mambo yanayowaudhi ili usiwakwaze.

Kwa upande wa uchangishaji fedha na kutafuta mitaji kwa biashara na kilimo, Rais wa VICOBA Endelevu Tanzania, Devota Likokola, alieleza jinsi mfumo wa VICOBA Endelevu unavyoweza kuwasaidia kinamama wa Green Voices kupata mitaji ya kuendeleza miradi yao.

NIC NDANI YA MAONESHO YA 12 YA TUME YA VYUO VIKUU TANZANIA MWISHONI MWA WIKI

$
0
0
Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es Salaam, wakipewa maelezo na Afisa Mwanadamizi wa Shirikala Bima la Taifa(NIC) Konjeta Mwaipopo juu ya namna ya kujiunga na huduma za bima wakati walipotemblea banda la Shirika hilo, kwenye maonesho ya 12 ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) yaliyomalizika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mkazi wa Dar es Salaam, ambaye ni mjasiriamali Manoko Marikishua (kushoto) akipewa maelezo na Afisa Bima wa shirika la Bima la Taifa (NIC)) juu ya bima ya mazao wakati alipofika kwenye banda la Shirika hilo, kwenye maonesho ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) yaliyomalizika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.
Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam,wakipata maelezo juu ya huduma za bima toka kwa Afisa Bima wa Shirikala Bima la Taifa (NIC)) wakati walipofika kwenye banda la Shirika hilo, kwenye maonesho ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania yaliyomalizika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam

Viewing all 46334 articles
Browse latest View live


Latest Images