Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46205 articles
Browse latest View live

RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI ATEMBELEA SHULE YA SEMINARI KATOKE ALIYOSOMA

0
0
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Akimuonyesha Mkewe Mama Janeth Magufuli kitanda alichokuwa akitumia kulala wakati akisoma kidato cha tatu katika shule ya seminari katoke iliyopo Biharamulo Mkoani Kagera, ambapo amemweleza mkewe kuwa alivunja hilo dirisha na mpaka leo halikutengenezwa ambapo leo hii amekabidhi kiasi cha shilingi milioni moja ili kukarabati dirisha na madirisha mengine ya shule hiyo, Mh Rais yupo mkoani Kagera kwa ziara ya siku mbili mkoani humo, 19 julai 2017.
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, akiingia kwenye  Bweni alilokuwa akilala wakati akisoma kidato cha tatu katika shule ya seminari katoke iliyopo Biharamulo Mkoani Kagera wakati akiwa kwenye ziara ya siku mbili mkoani humo, 19 Julai 2017
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli, akiongea na Wanafunzi Shule ya Seminari Katoke iliyopo Biharamulo Mkoani Kagera wakati akiwa kwenye ziara ya siku mbili mkoani humo, 19 Julai 2017.
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli, akiwa katika picha ya pamoja na Wanafunzi Shule ya Seminari Katoke iliyopo Biharamulo Mkoani Kagera wakati akiwa kwenye ziara ya siku mbili mkoani humo, 19 julai 2017
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli, akisalimiana na kuwaaga Wanafunzi Shule ya Seminari Katoke iliyopo Biharamulo Mkoani Kagera wakati akiwa kwenye ziara ya siku mbili mkoani humo, 19 julai 2017

SPORTPESA YATOA SHUKRANI KWA WANAHABARI, SERIKALI, VYOMBO VYA DOLA NA WANANCHI KUFANIKISHA ZIARA YA EVERTON

0
0
 Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa Kampuni ya Sportpesa, Tarimba Abbas akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo,  ambapo alitoa shukrani kwa wanahabari, vyombo vya dola, serikali na watanzania kwa kufanikisha ziara ya timu ya Everton ya Uingereza hapa nchini. PICHA , HABARI NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG

Akizungumza wakati wa mkutano huo, Tarimba alisema kuwa ziara ya Everton nchini imekuwa ni ya mafanikio makubwa kimichezo, kiuchumi, kijamii na hasa kuutangaza vilivyo utalii wa Tanzania Duniani.

Tarimba hakusita pia kuishukuru Ikulu kwa kuwapa sapoti kubwa kufanikisha ziara ya Everton hasa katika masuala ya kumpata mgeni rasmi, Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan pamoja na kuruhusu  vyombo vya dola kwa ajili ya usalama wa timu hiyo.

"Kwa niaba ya SportPesa ambao ndiyo wadhamini wakuu wa timu hiyo, tutakuwa wachoyo wa fadhila kama tutashindwa kuwashukuru wadau wote ambao kwa namna moja ama nyingine walituunga mkono  katika kuhakikisha kuwa maandalizi ya ziara hii yanafanikiwa." Alisema Tarimba na kuongeza kuwa...

Napenda Kumshukuru Rais  John Magufuli kwa kutoa baraka zake, lakini pia nipende kumshukuru  Makamu wake Samia Suluhu Hassan kwa moyo wake wa utayari wa kuwapokea wageni wetu ."

Alimshukuru pia Waziri wa Habari, Utamadjuni Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe  kwa niaba ya wizara hiyo kwa kuwa bega kwabega  katika jukumu hilo hizo. Pia hakusita kutoa pole kwa waziri huyo kwa kufiwa na mkewe.
 Tarimba akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo uliofanyika Makao Makuu ya kampuni hiyo, Oysterbay Dar es Salaam.

 Tarimba akifafanua jambo wakati wa mkutano huo na vyombo vya habari.
Wanahabari wakisilkiliza majibu ya maswali yao waliyomuuliza Tarimba

VIJUSO VYA MAGAZETI YA ALHAMIS LEO JULAI 20,2017

0
0

MAKILAGI: WATAKAOTUMIA RUSHWA UCHAGUZI HUU UWT TUTAWATIA ADABU

0
0
NA BASHIR NKOROMO

Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) imeapa kuwa ya mfano katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa wagombea wa nafasi mbalimbali katika Jumuia hiyo watakaobainika kutumia rushwa au kufanya vitendo vyovyote vinavyokiuka kanuni za Uchaguzi.

Kiapo hicho kimetolewa jana jijini Dar es Salaam, na Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo, Amina Makilagi wakati akitangaza maazimio ya Kikao Cha Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UWT kilichofanyika juzi Makao Makuu ya Jumuiya hiyo, jiijini.

"Tunashukuru kwamba baada ya Mwenyekiti wetu wa CCM, Rais Dk. John Magufuli kuonyesha anapambana na rushwa kufa na kupona na kwa dhati kabisa, kila mtu amemuelewa na sisi UWT tunaahidi kumuunga mkono kwa kuhakikisha katika uchaguzi huu hatutakuwa na mzaha, yeyoyote atakayebainika kutumia rushwa hatutamuonea aibu hata awe nani", alisema Makilagi.

Alisema, uchaguzi kwa ngazi ya Matawi umefanyika kwa asilimia 95, ngazi ya Kata vikao vya uchujaji vinaendelea na kwa ngazi ya Wilaya, Mkoa na Taifa uchaguzi unaendelea.

Makilagi alisema, kuanzia Julai 2 – 10, 2017 wanachama walipochukua fomu na kuzirejesha jumla ya wanachama 7,643 wamejitokeza kugombea nafasi mbalimbali ambapo kwa nafasiya Mwenyekiti wa UWT waliochukua fomu za kuomba kuteuliwa kugombea ni wanachama 34, nafasi ya Makamu Mwenyekiti wanachama 14, wajumbe wa NEC Bara 33, Baraza Kuu 73, Wawakilishi Vijana 15 na Wazazi 15, Upande wa Zanzibar wajumbe wa NEC ni 13 na Baraza Kuu ni 40.

Alisema hatua hiyo ya wanachama kujitokeza kwa idadi kubwa kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kuliko chaguzi zilizopita kumethibitisha imani yao kubwa kwa Jumuiya na Chama Cha Mapinduzi.

"Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UWT imewapongeza wanachama wote waliojitokeza kuchukua fomu za kugombea. Pia, inatoa mwito kwa wanachama wote kuendelea kuzingatia Kanuni za Uchaguzi na Maadili kwa kutotangaza nia, kutounda makundi na safu za kampeni pamoja na kujizuia kutoa na kupokea rushwa.

UWT inasisitiza kuwa, rushwa ni adui wa haki. Tutakuwa Jumuiya ya mfano, kwani hatutamvumilia yeyote atakayejihusisha na vitendo vya rushwa", alisema Makilagi. KUSOMA TAARIFA KAMILI YA KIKAO CHA BARAZA HILO/>BOFYA HAPA

RAIS DKT MAGUFULI AMPOKEA RAIS NKURUNZIZA WILAYANI NGARA MKOANI KAGERA.

0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe magufuli akiwa ameambatana na mgeni wake  Rais wa Burundi,Pierre Nkurunziza aliewasili mapema leo katka uwanja wa mpira wa Lemela mjini Ngara,Rais Dkt Magufuli amempokea Rais Nkurunziza akiwa kwenye ziara yake kikazi mkoani Kagera.

Aidha Rais Nkurunziza baada ya kupokelewa na Mwenyeji wake Rais Dkt Magufuli,alipata wasaa wa kuwasalimia wananchi mbalimbali waliofika kumpokea katika uwanja huo wa mpira mjini Ngara.

WAZIRI MWAKYEMBE AWASHUKURU WATANZANIA KWA KUMFARIJI KUTOKANA NA MSIBA WA MKEWE.

0
0
Na Shamimu Nyaki-WHUSM

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt Harrison Mwakyembe amewashukuru viongozi wote wa Serikali, Sekta binafsi, Taasisi za Kidini vyombo vya habari na watanzania wote waliomfariji katika msiba wa mke wake Bibi Linah Mwakyembe uliotokea Julai 15 mwaka huu.

Akizungumza wakati wa Misa ya mazishi ya mke wake huyo iliyofanyika jana nyumbani kwake Kyela Mhe. Mwakyembe ameeleza kuwa amefarijika sana kwa upendo ulioonyeshwa na kila mtu kwa nafasi yake katika kipindi hiki kigumu na kuahidi kuendelea kushirikiana nao katika kila jambo.

“Mimi na wanangu tumefarijika sana kwa kuona jinsi ambavyo Watanzania na wana Kyela mlivvyokuwa na upendo kwetu mmetupa faraja na mmetutia nguvu na mmetuoshesha ushirikiano mkubwa katika jambo hili tunaomba mwenyezi Mungu awabariki sana na asanteni sana”Alisema Mhe Waziri Mwakyembe.

Kwa Upande wake Mhe.Amos Makala Mkuu wa Mkoa wa Mbeya wakati akitoa salamu za pole kwa niaba ya wanachi wa mkoa wake amesema wananchi wa Mbeya watamkumbuka marehemu  mama Linah Mwakyembe kwa moyo wake wa kujitolea kusaidia jamii katika mambo mbalimbali ikiwemo kufundisha jamii kumcha Mungu pamoja na Ujasiriliamali uliosaidia wanawake wa Kyela kujiajiri.

“Wananchi wa Mbeya tunakupa pole sana Mhe. Mwakyembe pamoja na familia yako lakini pia tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa maisha ya mama Linah hapa duniani ambayo yameleta faida kwa jamii tunamuomba mwenyezi Mungu amlaze mahala pema peponi amina lakini na wewe pia tunakuombea Mungu aendelee kukupa uvumilivu na uamini kuwa hili nalo litapita”.Alisema Mhe Makala.

Marehemu Bibi Linah Mwakyembe ameagwa na kuzikwa jana nyumbani kwake Kyela na ameacha watoto watatu.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt Harrison Mwakyembe

SITAVUMILIA HATI CHAFU KATIKA HALMASHAURI YOYOTE MKOANI KWANGU-DKT NCHIMBI

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Singia Dkt Rehema Nchimbi amesema hatavumilia kuona halmashauri inafanya uzembe na kupata hati chafu ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Fedha za Serikali kwakuwa itamchafua yeye na taswira ya uongozi wote wa Mkoa wa Singida.

Dkt Nchimbi ametoa kauli hiyo mapema jana wakati wa baraza maalumu la madiwani wa Manispaa ya Singida la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za serikali ambazo amesema hoja nyingi zimetokana na uzembe.

Amesema licha ya kuipongeza Manispaa ya Singida kwa kupata hati safi, uwepo wa hoja umedhihirisha kuwa kuna baadhi ya watendaji wanafanya kazi kwa uzembe na kutofuata taratibu na sheria hivyo wajirekebishe haraka.

Dkt Nchimbi ameongeza kuwa hoja nyingi zinajitokeza kwa kukosa umakini na watendaji kufanya kazi kwa mazoea hali ambayo ikiendelea inaweza kuipelekea manispaa kupata hati isiyoridhisha hivyo kupata hati safi kuwaongezee nguzu ya kuboresha utendaji kazi wao.

Aidha amewashauri wakuu wa idara na watumishi wengine kuitendea haki manispaa yao kwa kuchapa kazi kuwa wadilifu na kufuata sheria kwani wakifanya hivyo wataepuka hoja zisizo za lazima na kuharakisha maendeleo.

Dkt Nchimbi amewasisitizia matumizi ya muda kuwa yenye tija ambapo amelaani kitendo cha kutumia muda mwingi kwenye vikao ambavyo havina tija bali watumie muda kidogo kwenye vikao na muda mwingi kutatua kero za wananchi, huku akiahidi kufuatilia matumizi ya muda unaotumika kwenye vikao.

Ameongeza kuwa watendaji wote wanapaswa kubadilika na kuendana na kasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Hapa kazi tu ili waweze kupunguza hoja na kufuta zile zisizo za lazima.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt Angelina Lutambi amewaasa watendaji kuitumia vema dhamana ya utumishi wa umma kwa kuhakikisha wanaleta mabadiliko ya kimaendeleo.

Dkt Lutambi ameongeza kuwa watumishi wa umma wanapaswa kufahamu kuwa jutendaji wao ukilega lega athari yake inamkumba mwananchi kwakuwa atachelewa kupata maendeleo, hivyo bidii katika utumishi umma ni muhimu.

Amewasisitizia kuwa mikakati na malengo ya maendeleo ya kimkoa na kitaifa haitaweza kufikia endapo watendaji hawatakuwa waadilifu na wakiendekeza uzembe hivyo wajitume kwa bidii kwa manufaa ya taifa kwa ujumla.

Naye Diwani Viti maalumu Magreth Malecela amemshukuru Mkuu wa Mkoa Dkt Nchimbi kwa kuwapa vyeti ambavyo vilitolewa kwa madiwani wote waliopata mafunzo ya usimamizi wa ruzuku na miradi ya serikali.

Malecela ameongeza kuwa ushirikiano na ushauri wanoaupata kutoka kwa Dkt Nchimbi utaisaidia manispaa kuwa na maendeleo huku akiahidi kwa niaba ya madiwani wenzake kuwa watafuata maelekezo na ushauri kwa manufaa ya manispaa ya Singida.
 Mkuu wa Mkoa wa Singia Dkt Rehema Nchimbi akizungumza na Meya wa Manispaa ya Singida Gwae Chima Mbua kabla ya kuanza kwa baraza Maalumu la madiwani wa Manispaa ya Singida kujadili hoja za Mkaguzi wa Fedha za Serikali.
 Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida Bravo Kizito Lyampembile akifungua baraza Maalumu la madiwani wa Manispaa ya Singida kujadili hoja za Mkaguzi wa Fedha za Serikali.
 Baadhi ya Viongozi wa Manispaa ya Singida wakifuatilia baraza Maalumu la madiwani wa Manispaa ya Singida kujadili hoja za Mkaguzi wa Fedha za Serikali.
  Madiwani wa manispaa ya Singida wakifuatilia baraza Maalumu la madiwani wa Manispaa ya Singida kujadili hoja za Mkaguzi wa Fedha za Serikali.
Madiwani wa manispaa ya Singida wakiwa wamesimama kuridhia hoja katika baraza Maalumu la madiwani wa Manispaa ya Singida kujadili hoja za Mkaguzi wa Fedha za Serikali.

ELIMU SAHIHI ITUMIKE KWANZA KABLA YA MATUMIZI YA SHERIA KWA WAKEKETAJI

0
0
Elimu sahihi juu ya madhara ya ukeketaji ya muda mfupi na mrefu inatakiwa itolewe kwa jamii kabla ya kuwachukulia hatua baadhi yao wanaoendelea kufanya vitendo vya ukeketaji licha ya uwepo wa sheria kali.

Rai hiyo imetolewa mapema leo na Mratibu wa Mradi wa Kupinga Ukeketaji (WOWAP) Nasra Suleiman katika semina ya kupinga Ukeketaji iliyofanyika katika Kata ya Msange Wilayani Singida, kwa ushirikiano wa Ofisi ya Ustawi wa Jamii Mkoa wa Singida na mradi huo kwa ufadhili wa shirika la WAAF-Japan.

Mratibu huyo amesema nguvu ya sheria itasaidia kuondoa ukeketaji endapo wananchi wengi watakuwa na uelewa wa kutosha juu ya madhara ya ukeketaji na kuamua kwa hiyari kuachana na mila hiyo.

“Sheria isiwe nguvu pekee ya kupambana na ukeketaji, tukifanya hivyo itafikia kipindi tutakwama kwa kiasi kikubwa kwa kuwa watu wataendelea kukeketa kwa kificho ili wasikamatwe, lakini kila mwana jamii akiwa na elimu ya kutosha ya madhara hayo, nguvu ya sheria itatumika tu kwa wachache watao kaidi”, amesisitiza Nasra.

Ameongeza kuwa Watendaji wa kata na vijiji wana uwezo mkubwa wa kubadilisha mtazamo na mila ya ukeketaji kwa kuelimisha wananchi wao hasa baada ya semina zinazoandaliwa na miradi au mashirika Fulani kwakuwa zinawajengea uwezo ili waweze kutoa elimu sahihi na mbinu za kuelimisha.

Nasra amesisitiza kuwa jukumu la elimu lisiachwe kwa sekta binafsi kama mradi wake wa WOWAP pekee bali liwe jukumu la jamii nzima huku akifafanua kuwa elimu inayotakiwa kutolewa ni ile inayoelezea madhara ya ukeketaji na sio kuwakataza kwa kigezo cha kutii sheria pekee.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii kata ya Msange Magni Oisso amesema katika kata hiyo ukeketaji umekufanyika kwa siri sana kwa kuogopa mkono wa sheria huku wahanga wakiwa watoto wachanga na wale waliomaliza kliniki.

Oisso amesema kumekuwa na usiri mkubwa huku wakeketaji wakibadili mbinu namna za kujificha wasigundulike kwa jamii ambayo elimu imeanza kuwafikia baadhi yao.

Aidha amependekeza kuwa ili kukomesha ukeketaji moja ya njia ni kutoa elimu katika vituo vya kutolea huduma za uzazi na mtoto ili mtoto aweze kunusurika pia elimu itolewe shuleni kwa ngazi zote kuanzia darasa la awali hadi la saba.

Akichangia mada katika semina hiyo mzee maarufu na mwenyeji wa Msange Bi Greta Musa Nyonyi amesema elimu ni bora zaidi kuliko kuwaogopesha wanajamii kwa kutumia sheria kwakuwa watatafuta namna ya kutekeleza azma yao kwa usiri ili kukwepa mkono wa sheria na sio kuacha.

Greta ameongeza kuwa kwa sasa kutokana na kuwa wakeketaji wamebainika kuwa wanakeketa watoto wachanga na hugundulika wakienda kliniki baadhi yao wanabadili mbinu na kusubiri mtoto amalize kliniki ndipo anakeketwa.

Naye Mzee wa Kimila Hosea Mnyambi amesema yeye amekulia katika familia ya wakeketaji na wamekuwa wakirithishwa mbinu za ukeketaji kizazi hadi kizazi ila kutokana na kuwepo kwa sheria, dini kuhubiri madhara ya ukeketaji, mila hiyo wameiacha.

Amesema wachache wanaoendelea kufanya vitendo hivy o ha wanawake wamekuwa wakifanya kwa usiri mkubwa huku akina baba wakiwa hawana taarifa ya kinachoendelea na endapo mtoto anafariki hudanganywa ugonjwa uliopelekea kifo cha mtoto.

Mzee Mnyambi amesema elimu iendelee kutolewa hasa kwa kutumia vyombo vinavyoaminika mfano vyama vya siasa, dini na vikundi vya kuweka na kukopa pamoja na kuiweka agenda ya ukeketaji kwa vikao vya Kata na vijiji.

Semina ya kupinga ukeketaji Kata ya Msange imefanywa na mradi wa WOWAP kwa ushirikiano wa maafisa ustawi wa jamii mkoa wa Singia kwa watendaji wa kata na vijiji, watoa huduma za afya, polisi, waalimu, wawakilishi wa viongozi wa dini, maafisa ustawi wa jamii na maendeleo ya jamii, wazee maarufu na wa kimila ili wawe mabalozi wa kusambaza elimu hiyo kwa jamii inayo wazunguka.
 Mzee maarufu na mwenyeji wa Msange Bi Greta Musa Nyonyi akichangia hoja katika semina ya kupinga Ukeketaji iliyofanyika katika Kata ya Msange Wilayani Singida.
 Mratibu wa Mradi wa Kupinga Ukeketaji (WOWAP) Nasra Suleiman akizungumza na washiriki wa semina ya kupinga Ukeketaji iliyofanyika katika Kata ya Msange Wilayani Singida.
 Afisa Maendeleo ya Jamii kata ya Msange Magni Oisso akichangia hoja katika semina ya kupinga Ukeketaji iliyofanyika katika Kata ya Msange Wilayani Singida.
 Washiriki wa semina ya kupinga ukeketaji iliyoandaliwa na Mradi wa WOWAP wakifuatilia kwa umakini filamu fupi ya Ukeketaji iliyofanyika katika Kata ya Msange Wilayani Singida.
Mzee wa Kimila Hosea Mnyambi akichangia hoja katika semina ya kupinga Ukeketaji iliyofanyika katika Kata ya Msange Wilayani Singida.


NAIBU WAZIRI WA MAJI AFANYA ZIARA CHALINZE

0
0
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe akisisitiza jambo wakati wa ziara yake  ya kukagua hatua iliyofikiwa katika mradi wa ukarabati  na upanuzi wa mtambo wa maji chalinze na na ujenzi wa mfumo wa kusafirishia maji pamoja na matenki yakuhifadhia maji. Kulia ni Mkurugenzi mtendaji wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Chalinze (CHALIWASA)Mhandisi Christer Mchomba na kushoto ni Msimamizi wa mradi huo kutoka kampuni ya WAPCO inayotekeleza mradi huo.
Mafundi wakiendelea na Kazi ya ujenzi wa matanki ya kuhifadhi na kusambaza maji katika Jimbo la Chalinze.
Baadhi ya mitambo ikiwa katika moja ya maeneo unakotekelezwa mradi  huo utakaonufaisha wakazi wa Jimbo la chalinze na sehemu ya Wilaya ya Handeni.
Sehemu ya mabomba yakiwa katika moja ya maeneo unakotekelezwa mradi huo.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe (wapili kushoto) akioneshwa ramani ya mradi huo na hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wake wakati wa ziara yake  ya kukagua mradi huo  wa ukarabati  na upanuzi wa mtambo wa maji chalinze na na ujenzi wa mfumo wa kusafirishia maji pamoja na matenki yakuhifadhia maji.

(Picha zote na Frank Mvungi-MAELEZO)

JAFO:TUNATAKA KASI KATIKA UTEKELEZAJI MIRADI

0
0
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo amewataka wakandarasi wa ujenzi wa miundombinu ya barabara na majengo katika halmashauri zote nchini kuzingatia mikataba ya ujenzi, huku akiwaonya tabia ya kuchelewesha kukamilisha miradi kwa wakati.

Jafo aliyasema hayo katika ziara ya kikazi ya kutembelea miradi ya barabara na madaraja wilayani Kisarawe.Amesema Ofisi ya Rais, Tamisemi haitofumbia macho wakandarasi ambao wameshinda tenda za ujenzi na kuonesha uwezo mdogo.

“Pia hatutafumbia macho ucheleweshaji wa miradi bila sababu yeyote ya msingi kinyume na matarajio yaliyoainishwa ndani ya mkataba,”amesema Jafo.

Naibu Waziri Jafo katika ziara zake hivi karibuni ikiwemo ujenzi wa daraja la Twangoma lililopo wilaya ya Temeke mkoani Dar es salaam amekuwa akisisitiza wakandarasi kuzingatia ubora wa madaraja yanayojengwa  nchini ili yaweze kudumu kwa muda mrefu. 

Jafo amemaliza ziara yake leo wilayani Kisarawe na anatarajia kuendelea na ziara yake ya kikazi mkoani Morogoro, Songwe, Njombe, Singida, Tabora, Kagera, Mwanza na Mara.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa na wataalam wa ujenzi wa daraja la Kologombe linalounganisha Kijiji cha Gwata na Dololo wilayani Kisarawe.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akikagua maendeleo ya ujenzi wa barabara za mji wa Kisarawe.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akipata maelekezo kuhusu ujenzi wa barabara ya kisarawe mjini kutoka kwa Mhandisi wa Halmashauri Mbena.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua ujenzi wa daraja la Kologombe wilayani Kisarawe.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa na walimu wa sekondari Gwata alipotembelea kukagua ujenzi wa madaraja wilayani Kisarawe.

CHINA YAIJENGEA UWEZO IDARA YA FORODHA YA TANZANIA

0
0
 Naibu Kamishna wa forodha na Maboresho ya Vihatarishi Hatari wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Bw. James Mbunda (Kushoto) na akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa Ubalozi wa China anayeshughulikia Uchumi na Biashara, Bw. Lin Zhiyong, wakati wa kufungua mafunzo kuhusu Takwimu na kudhibiti Vihatarishi hatari vya Forodha, yanayotolewa na Chuo cha Forodha cha Shanghai-China, Jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali watu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Grace Sheshui akiwakaribisha watoa mafunzo ya Takwimu na Udhibiti Vihatarishi hatari vya Forodha, yanayotolewa na Chuo cha Forodha cha Shanghai-China, Jijini Dar es Salaam.
 Naibu Kamishna wa Forodha na Maboresho ya Vihatarishi Hatari wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Bw. James Mbunda, akizungumza na na watoa mafunzo ya Takwimu na Udhibiti Vihatarishi hatari vya Forodha, yanayotolewa na Chuo cha Forodha cha Shanghai-China, Jijini Dar es Salaam, kushoto kwake ni Mwakilishi Mkazi wa Ubalozi wa China anayeshughulikia Uchumi na Biashara, Bw. Lin Zhiyong.
 Baadhi ya maafisa kutoka Wizara ya Fedha na Mipango wakisikiliza kwa makini maelezo ya awali ya mafunzo ya kutoka kwa Mwakilishi Mkazi wa Ubalozi wa China anayeshughulikia Uchumi na Biashara, Bw. Lin Zhiyong, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam.
 Maafisa kutoka Wizara ya Fedha na Mipango na wengine (kulia) na wakufunzi wa Takwimu na Udhibiti Vihatarishi hatari vya Forodha wakisikiliza maelezo ya awali wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
 Mkufunzi Mkuu wa masuala ya forodha kutoka Chuo cha Forodha cha Shanghai, China, Profesa Sun Hao (kulia) akizungumza jambo wakati wa hafla ya ufunguzi wa mafunzo ya siku 14 ya maafisa wa Forodha kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, katika ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dae Salaam.
 Naibu Kamishna wa Forodha na Maboresho ya Vihatarishi Hatari wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Bw. James Mbunda (wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wakufunzi, pamoja na maafisa wa forodha kutoka TRA, baada ya ufunguzi wa mafunzo ya siku 14 kuhusu masuala ya forodha, katika ukumbi wa Wizara ya fedha na Mipango, Jijini, Dar es Salaam.
Mwakilishi Mkazi wa Ubalozi wa China anayeshughulikia Uchumi na Biashara, Bw. Lin Zhiyong (Kushoto) na Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali watu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Grace Sheshui (kulia) wakipeana mkono baada ya ufunguzi wa mafunzo ya masuala ya forodha yanayotolewa na Chuo cha  Forodha cha Shanghai, China, mafunzo yanayofanyika katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM).

Benny Mwaipaja, Dar es Salaam
Kiwango cha biashara kati ya Tanzania na China kimefikia Dola bilioni 4.7 katika kipindi cha mwaka 2015 na kwamba kiwango hicho kinatarajiwa kuongezeka zaidi.

Mwakilishi Mkuu Mkazi wa Masuala ya Uchumi na Biashara, kutoka Ubalozi wa China hapa nchini, Bw. LIN Zhiyong, amesema hayo Jijini Dar es Salaam, wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya forodha kuhusu Maboresho na Vihatarishi hatari vya kiforodha, yanayotolewa kwa maafisa wa forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania na wataalamu kutoka Chuo cha Forodha cha Shanghai-China.

Bw. Zhiyong amesema kuwa uhusiano wa Tanzania na China ni wa kihistoria na kwamba hivi karibuni nchi yake iliipatia Tanzania seti 3 za makontena ya vifaa vya kisasa kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa mizigo katika Bandari ya Dar es Salaam, vyenye uwezo mkubwa wa kugundua pembe za ndovu, dawa za kulevya na silaha zinazosafirishwa kimagendo kutoka ndani na nje ya nchi.

 Alisema pia kuwa hivi sasa nchi yake ni kama imeondoa kabisa kodi kwa bidhaa za Tanzania zinazosafirishwa kwenda China hadi kufikia asilimia 97, na kwamba anatarajia kuona wafanyabishara wa Tanzania wakichangamkia fursa hiyo na kuongeza kiwango cha bidhaa za Tanzania zenye ubora zinazosafirishwa kwenda nchini mwake.

Bw. Zhiyong, amezishauri Idara za Forodha za Tanzania na China kuimarisha ushirikiano na kukuza biashara na uwekezaji kwa faida ya pande zote mbili.

Akizungumzia kuhusu sekta ya elimu, Mtaalamu huyo wa masuala ya Uchumi na Biashara amesema kuwa hadi mwishoni mwa mwaka uliopita, Watanzania 5,000 wako nchini China wakipatiwa mafunzo mbalimbali kupitia Wizara ya Biashara ya nchi hiyo kwenye vyuo mbalimbali.

Alisema kuwa wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma nchini China wameiletea sifa kubwa Tanzania kutokana na umahili wao mkubwa katika masomo pamoja na nidhamu ya hali ya juu jambo linalowafanya wawe mabalozi wazuri wa nchi yao ndani na nje ya nchi kwa ujumla.

Akifungua mafunzo hayo ya majuma mawili, Naibu Kamishna wa Maboresho ya vihatarishi hatari, kutoka Idara ya Forodha ya Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Bw. James Mbunda, amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wafanyakazi wa idara hiyo wa kukabiliana na vihatarishi vyote vya masuala ya forodha kwa bidhaa zinazoingia na kutoka nchini kwenda nje ya nchi.

Amesema kuwa mafunzo hayo yameratibiwa na Serikali kupitia Wizara ya Utumishi ikiwa ni hatua ya Serikali ya kuboresha utendaji kazi wa idara hiyo kwa manufaa ya Taifa kwa ujumla.

Ameyataja baadhi ya masuala watakayopewa utaalamu na wakufunzi watano kutoka Chuo hicho cha Forodha cha Shangai wakiongozwa na Profesa wa masuala ya forodha Bi. Sun Hao, ni pamoja na kupitia sheria mbalimbali za forodha, misamaha ya kodi, udhibiti wa biashara, namna ya kukabiliana na watu wasio tii sheria na vigezo vya utoaji leseni.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AANZA ZIARA YA MKOA WA SONGWE

0
0
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Chiku Galawa baada ya kuwasili Mkwajuni wilayani Songwe kuanza ziara ya mkoa wa Songwe Julai 20, 2017. Kulia ni mkewe Mary.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Songwe, Elias Nawela  baada ya kuwasili Mkwajuni wilayani Songwe kuanza ziara ya mkoa wa Songwe Julai 20, 2017. Kushoto ni  Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Chiku Galawa. 
 Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa akisalimia wakati Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  (kulia) alipozungumza na watumishi wa umma na viongozi wa dini  kwenye ukumbi wa Chuo cha Uuguzi cha  Kanisa Katoliki cha Mwambani wilayani Songwe, Julai 20, 20117. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Chiku Galawa.  
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi wa umma na viongozi wa dini wa mkoa wa Songwe kwenye ukumbi wa Chuo cha Uuguzi cha Kanisa Katoliki cha Mwambani wilayani Songwe, Julai 20, 2017. Kushoto ni Mkewe Mary na Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Chiku Galawa.
Baadhi ya watumishi wa umma na viongozi wa dini wa mkoa wa Songwe wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  wakati alipowahutubia kwenye ukumbi wa Chuo cha Uuguzi cha Kanisa Katoliki cha Mwambani wilayani Songwe, Julai 20, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

SHAKA APONGEZA WAGANGA NA WAUGUZI MKOANI KIGOMA

0
0
Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) umesema serikali ya awamu ya tano itaendelea kuwajali na kuwahudumia wagonjwa kwa kupeleka idadi ya waganga, wauguzi, dawa na utoaji wa vifaa tiba katika zahanati vituo vya afya na hospitali za wilaya nchini .

Pia Serikali itafanya kila linalowezekana kuhakikisha katika kila Kata na Wilaya kunajengwa zahanati na vituo vya afya ili kunusuru pia kupunguza vifo vya kina mama wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano .

Msimamo huo umetolewa jana na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka alipotembelea katika kituo cha Afya cha kijiji cha Nguruka Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma katika siku ya pili ya ziara yake kuona utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya ccm katika maendeleo ya kisekta.
Shaka alisema serikali ya Chama Cha Mapinduzi zina wajibu wa kufuatilia kwa karibu na kujua kama yale yote yalioahidiwa katika ilani , yanayotimizwa na iwapo yanawafikia na kuwahudumia wananchi kama inavyokusudiwa na serikali Kuu kwa wananchi wake. 

Alisema pamoja na kukabiliwa na upungufu wa idadi ya Waganga na Wauguzi katika Kituo cha Afya Nguruka, waliopo wamekuwa wakijituma bila kuchoka huku wakitoa huduma kwa njia makini na sahihi ili kunusuru na kutibu wagonjwa . 

"Serikali ya CCM katu haitapuuzia dhamana waliopewa na wananchi kwa kuiweka madarakani kidemokrasia , maeneo yote ya kisekta yataendelea kupata huduma bora kwa wakati stahili hususan eneo la Afya kwa upelekaji vifaa tiba, dawa, Waganga na Wauguzi " Alisema Shaka .

Alisema katika kuonyesha serikali kujali matatizo ya wagonjwa hivi karibuni Rais John Magufuli amepeleka shilingi milioni kumi katika kituo cha Afya Nguruka kwa ajili ya kufanyika upanuzi wa wodi ya wazazi huku kanisa la shalom likijenga wodi hiyo. 
"Rais wetu hapati usingizi kwa raha kutokana na kufikiria wanachi wake, kila wakati amwkuwa akiwahimiza wataalam wa huduma za afya na watendaji dhamana wa serikali watimize wajibu wao bila kuchoka. Huuu ndiyo uungwana alionao kiongozi wetu na kila mmoja wetu sasa lazima awajibike 'Alisema Shaka mara baada ya kutazama wodi hiyo.

Aidha Kaimu huyo Katibu Mkuu wa UVCCM aliwataka watendaji wa halmashauri ya wilaya ya Uvinza kujiongeza katika mikakati ya ubunifu, utendaji unaoonekana na kujali maisha ya watu, matumizi bora ya fedha za ruzuku ya umma toka serikali kuu na kuhakikisha wanawatibia wagonjwa kwa wema. 

Kwa upande wake Mganga Mkuu Msaidizi wa Kituo cha Afya Nguruka Dk Beatrice Mtasigwa alimueleza Shaka licha kukabiliwa na upungufu wa Waganga na Wauguzi, wamekuwa wakiwahudumia wagonjwa mbalimbali toka vijiji vyote wanaofika kituoni kati 80 hadi 120 kwa siku. 

Dk Mtasigwa alisema hatua ya ujenzi na upanuzi wa wodi ya wazazi , uwepo wa badhi ya vifaa tiba vya kisasa utasaidia kwa kiasi kikubwa kunusuru maisha ya kina mama wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano. 

Naye Mbunge wa Vijana Mkoa Kigoma Zainab Katimba alitoa shilingi laki mbili na kumkabidhi Mganga Mkuu Msaidizi wa Kituo hicho cha Afya kusaidia kununulia shuka ambazo zitatumika katika wodi ya wazazi.

Katimba alisema bila kina mama hakutakuwa na Taifa kwasbabau nchi na mataifa yote yanajazwa na nguvu za kina mama ambazo ndiyo wazazi wanaoleta neema ya kupatikana watoto duniani , wataalam wa fani mbalimbali, viongozi, wabunge na wanasiasa.
Shaka anaendelea na ziara yake ya kikazi katika wilaya ya Kigoma Mjini kabla ya kuelekea Kibondo, kasulu, Buhigwe, Kakonko na Kigoma vijijini mkoani hapa.

WAZIRI LUKUVI AMSIMAMISHA MUWEKEZAJI WA MKONGE MKOANI TANGA.

0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiongea na wakazi wa kata ya Mnazi wilaya ya Lushoto mkoni Tanga waliozuia msafara wake na kumpa malalamiko kuhusu mashamba matatu yaliyotelekezwa na mmiliki wa mashamba hayo bila kuendelezwa na kusababisha migogoro. 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akikagua mashamba ya katani yanayomilikiwa na kampuni ya Le-Mash Enterprises Limited yaliyopo kata ya Mnazi wilayani Lushoto mkoani Tanga. 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akikagua miundombinu na mazingira ya kazi ya mwekezaji wa kampuni ya Le-Mash Enterprises Limited ambaye ameshindwa kuindeleza tangu akabidhiwe mwaka 1997. 
Mazingira ya shamba yaliyotelekezwa na mmiliki wake wa kampuni ya Le-Mash Enterprises Limited ambaye ameshindwa kuindeleza tangu akabidhiwe mwaka 1997. 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiongea na Kamishna wa Ardhi Kanda ya Kaskazini Bwana Leo Komba kuhusu hatua zilizochukuliwa na ofisi yake hadi sasa kwa mmiliki ambae ameshindwa kuwa na sifa za umiliki na hajalipa kodi ya ardhi tangu mwaka 2004 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiongea na wakazi wa kata ya Mnazi wilayani Lushoto mkoani Tanga kuhusu shamba hilo linalostahili kufutwa kama ilivyopendekezwa na ofisi ya Mkoa wa Tanga na ofisi ya Kamishna wa Ardhi Kanda ya Kaskazini kwa kuwa mmiliki. 
Baadhi ya mitambo iliyochakaa ambayo mwekezaji wa kampuni ya Le-Mash Enterprises Limited ameshindwa kuiendeleza tangu akabidhiwe mwaka 1997 kwa kurithi mashine na mitambo hiyo kutoka kwa mkoloni tangu mwaka 1937. 
Baadhi ya mitambo iliyochakaa ambayo mwekezaji wa kampuni ya Le-Mash Enterprises Limited ameshindwa kuiendeleza tangu akabidhiwe mwaka 1997 kwa kurithi mashine na mitambo hiyo kutoka kwa mkoloni tangu mwaka 1937.


……………………………………………………………………………..

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi amesimamisha umiliki wa mwekezaji wa mashamba ya katani yanayomilikiwa na kampuni ya Le-Mash Enterprises Limited yaliyopo kata ya Mnazi wilayani Lushoto mkoani Tanga.

Waziri Lukuvi amefikia uamuzi huo baada ya wakazi wa eneo hilo kuzuia msafara wake na kupata malalamiko mengi kutoka kwa wananchi hao na viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Lushoto wakimlalamikia Waziri kuhusu mashamba matatu ya Mnazi yaliyotelekezwa na mmiliki wa mashamba hayo bila kuendelezwa na kusababisha migogoro kwa awakazi wa Mnazi.

Baada ya kupokea malalamiko hao Waziri Lukuvi aliamua kutembelea mashamba hayo na kuyakagua ili kujionea hali halisi na kuwasikiliza wananchi ambao wamekuwa wanakabiliwa na mgogoro huu kwa miaka mingi.

Baada ya kutembelea na kujiridhisha Waziri Lukuvi amesema kwamba shamba hilo linastahili kufutwa kama ilivyopendekezwa na ofisi ya Mkoa wa Tanga na ofisi ya Kamishna wa Ardhi Kanda ya Kaskazini kwa kuwa mmiliki ameshindwa kuwa na sifa za umiliki kwa kuwa hajalipa kodi ya ardhi tangu mwaka 2004, hajalipa wafanyakazi wake kwa muda mrefu, miundombinu yake na mazingira ya kazi hayaridhishi na ameshindwa kuliendeleza shamba hilo tangu akabidhiwe mwaka 1997 kwa kurithi mashine na mitambo ileile ya mkoloni ya mwaka 1937.

Aidha, katika ziara hii Waziri Lukuvi amekutana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martin Shigela na Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Joel Bendera ili kutatua migogoro ya mipaka iliopo kati ya Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara na Wilaya ya Kilindi mkoani Tanga ikiwa ni muendelezo wa mikutano ya kuutafutia ufumbuzi mgogoro huu ambao umesababisha uvunjifu wa amani.

Waziri Lukuvi anatekeleza agizo la Waziri Mkuu Mhe. Khassim Majaliwa ambae alimuagiza Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi kutatua mgogoro huu uliodumu kwa miaka mingi kati ya Wilaya hizo mbili pindi alipofanya ziara yake mkoani Tanga.

Mnamo tarehe 18 Januari, 2017 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alifanya ziara Wilayani Kilindi katika Kijiji cha Mafisa na kuzungumza na wanachi Kijijini hapo kuhusiana na mgogoro huo na kutoa maagizo kwa viongozi wa kuchaguliwa kuacha kutumia nafasi zao vibaya kuongoza kwa mihemko au ushabiki kwa kuwa kufanya hivyo kunapelekea wananchi kufuata ushabiki na kuvunja sheria zilizopo.

Ili kutekeleza agizo hili wakuu wa mikoa hii miwili wakiongozwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi wamekutana ikiwa ni muendelezo wa vikao vya kulitafutia ufumbuzi suala hili.

NAIBU WAZIRI MPINA AFANYA ZIARA USIKU KUBAINI UHARIBIFU WA MAZINGIRA UTOKANAO NA UCHIMBAJI WA MCHANGA.

0
0

NA EVELYN MKOKOI

Katika hali isiyoya kawaida, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina, amefanya ziara ya Oparesheni maalum kwa kushirikiana na jeshi la Police kitengo cha FFU ili kuweza kubaini uharibifu wa mazingira unaofanywa kwa uchimbani na uchotaji wa mchanga katika vyanzo vya maji na maeneo mengine.

Akiwa katikati ya Mto Mpigi uliopo katika mpaka wa Dar es salaam na Bagamoyo usiku wa kuamkia leo, naibu Waziri Mpina alisema kuwa watu wanaochimba na kuchota mchanga kiholelea watachukuliwa hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kutozwa faini kwa mujibu wa sheria, kutaifishwa kwa magari yao na hata kufikishwa mahakamani.

“kama mnavyoona hapa na kama tulivyosikia kutoka kwa mtu wa DAWASA haya mabomba ya maji yanayopita katika mito yanaharibika kutokana na shughuli hizi na serikali inaweza kuingia gharama kubwa sana kurekebisha mabomba haya kama bomba hili Mtaalam amesema hapa itagharimu kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 80 kutengeneza bomba hili.” Alisema Mpina.

Aidha Mpina alisema ukiachilia mbali uharibifu wa Miundo Mbinu hiyo ya Maji pamoja na Mazingira wananchi wnaweza pia kukosa maji kwa takribani muda wa wiki mbili.

“Mabomba haya yalikuwa chini ya mchanga lakini kwa sasa hivi yananing’inia kutokana na uchimbaji wa mchanga na mto unazidi kupanuka na maji yanakwenda kwenye makazi ya watu na kusababisha mafuriko, na madhara kwa miundombinu mingine kama vile ya umeme na barabara ambapo serikali imeijenga kwa gharama kubwa”. Alisisitiza Mpina

Alongeza kwa kusema kuwa hakuna mtu yoyote atakaye ruhusiwa kuchimba mchanga katika maeneo yasiyo ruhusiwa na wanachi wajihepushe na uharibifu wa mazingira Mpina alisisitiza kuwa serikali haizuii wananchi kuchimba mchanga bali inakataza wanachi kuchimba mchanga kiholela na kuharibu mazingira.

Naibu Waziri Mpina alisema kuwa uungwaji mkono wa sehemu nyingine ya serikali kama vile Halmashauri na vyombo vingine vya ulizi na usalama ni mkubwa na ndo maana katika opareshi hiyo hawakuweza kukuta shughuli zozote zikiendelea katika muda huo,na wahalifu wameanza kuona kuwa serikali haina mzaha na ndiyo maana team ya oparesheni hiyo imekuwepo katika eneo la tukio kwa muda huo wa usiku.

“Oparesheni hii ni agizo na zoezi hili litaenda Nchi nzima, na tumeanzia Dar es Salaam , Halmashauri zote zinatakiwa kutenga maeneo maalum kwa ajili ya kufanyika kwa shughuli hii.” Aliongeza Mpina.

Aliwaasa viongozi wasingojee Waziri NEMC au wa Viongozi wajuu kuwatembelea na kufanya zoezi hili.

Kwa upande wake Afisa kutoka DAWASA Bwana Abel Chibelene wao kama wamiliki wamiundombinu hiyo ya maji kwa mkoa wa Dar es Salaam na Pwani wamefanya jitihada za kutosha kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzai na usalama, na kufikia hatua ya kuweka walinzia katika miundombinu hiyo lakini bado wananchi wamekuwa wakiendelea na shugulizi hizo ambazo si salama kwa mazingira na miundombinu hiyo muhimu ya maji.

Opareshi hiyo ya kamata kamata ya wachimba mchanga, imeanzishwa na Naibu Waziri Mpina na kuwa ni agizo kwa Halmashauri zote na miji nchini kutekeleza zoezi hilo.
 
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akiwa na mchanga mkononi akiwasikiliza maafisa wataalam katikati Afisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais ambaye pia ni katibu wake Bw. Daniel Sagata, na kulia ni Afisa kutoka DAWASA Bw. Abel Chibelenge akieleza kuhusu uharibifu wa mazingira unaofanywa na wananchi kati kati ya mto Mpigi katika eneo la Mpaka wa Bagamoyo na Dar es Salaam, ambapo uharibifu huo Umeharibu eneo ambapo limepita Bomba kubwa la maji safi (halipo pichani) linalo safirisha maji kutoka Mtambo wa kuzalisha maji wa Ruvu Chini na kuhudunia seheu ya mkoa mkoa wa Pwani na Jiji la Dar es Salaam, Bomba ambalo lipo hatarini kuharibika.
Afisa Mtaalam kutoka DAWASA Bw. Abel Chibelenje (kulia) akimuonyesha Naibu Waziri Mpina Sehemu ya mto Mpigi ( haipo Pichani, iliyoharibiwa vibaya kutokana na shughuli za uchimbaji wa mchanga. (Picha na Evelyn Mkokoi)

RC SHINYANGA AKUTANA NA WAWEKEZAJI NA WAFANYABIASHARA WA MKOA WA SHINYANGA

0
0
Alhamis Julai 20,2017 Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack amekutana na wawekezaji na wafanyabiashara wa mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kufahamiana na kujadili mambo kadha wa kadha ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika mkoa wa Shinyanga.

Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga na kukutanisha wawekezaji na wafanyabiashara kutoka wilaya zote za mkoa wa Shinyanga.

Akizungumza katika kikao hicho,Telack alisema huu ni mwaka wa pili wa utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Taifa wa miaka mitano 2016/2017 – 2020/2021 wenye dhima ya kujenga uchumi wa viwanda ili kuchochea mageuzi ya maendeleo ya watu.

“Ili kutimiza malengo ya mpango huu lazima serikali ifanye kazi kwa ushirikiano wa karibu na sekta binafsi na nyinyi ni sehemu ya sekta binafsi na ili kudumisha ushirikiano huo serikali imeanzisha mabaraza ya biashara katika ngazi ya taifa,mikoa na wilaya”,alieleza Telack.

Aidha alisema uwekezaji ni moja ya shughuli zinazochochea kasi ya ukuaji wa uchumi wa mkoa wa Shinyanga na taifa kwa ujumla ambapo hadi sasa mkoa huo una jumla ya viwanda 81,ambapo viwanda vikubwa ni 18,viwanda vya kati 9 na vidogo 54.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akitoa hotuba yake wakati wa kikao chake pamoja na wawekezaji na wafanyabiashara mkoa wa Shinyanga leo Alhamis Julai 20,2017.
Wafanyabiashara,wawekezaji na wadau mbalimbali wa maendeleo wakiwa ukumbini  Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akizungumza katika kikao hicho ambapo aliwahamasisha wafanyabiashara kushirikiana na kupeana fursa mbalimbali
Kaimu Mwenyekiti wa wafanyabiashara mkoa wa Shinyanga Jackton Koy akizungumza katika kikao hicho.  Kushoto ni Kaimu Mwenyekiti wa wafanyabiashara mkoa wa Shinyanga Jackton Koy,katikati ni mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack akifuatiwa na katibu tawala mkoa wa Shinyanga,Albert Msovela.
Kikao kinaendelea
Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu akichangia hoja katika kikao hicho  Wawekezaji na wafanyabiashara wakiwa katika kikao.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Nyabaganga Talaba akichangia hoja ukumbini
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Shinyanga,Said Pamui akizungumza katika kikao hicho  Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Muliro Jumanne Muliro aliyehamishiwa mkoa wa Kinondoni akizungumza ukumbini.
Kikao kinaendelea
a
Mkurugenzi wa SHUWASA Injinia Sylivester Mahole akichangia hoja ukumbini.
Meneja wa Ustawi wa Jamii na Kampuni ya Acacia Bulyanhulu,Elias Kasitila akizungumza katika kikao hicho.
 Meneja wa Ustawi wa Jamii na Kampuni ya Acacia Bulyanhulu,Elias Kasitila akichangia hoja ukumbini.
Wafanyabiashara na wawekezaji wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini.
Kikao kinaendelea  Mkurugenzi wa Hasmukh Group, Kishan Hasmukh akichangia hoja wakati wa kikao hicho.
Meneja wa Ustawi wa Jamii na Kampuni ya Acacia Bulyanhulu,Elias Kasitila (kushoto) na Meneja Uendelevu mgodi wa Buzwagi George Mkanza wakiwa katika kikao hicho
Wawekezaji wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini.
Kikao kinaendelea
Kikao kinaendelea.
Wadau wakiwa ukumbini
Mwekezaji Gilitu Nila Makula akizungumza ukumbini.
Mkurugenzi wa Soud Group,Hilal Soud akichangia hoja wakati wa kikao hicho
Katibu wa Wafanyabiashara mkoa wa Shinyanga Macelina Lauo akizungumza wakati wa kikao hicho.  Meneja Uendelevu mgodi wa Buzwagi George Mkanza  akifuatilia kwa umakini kilichokuwa kinaendelea ukumbini.
Tunafuatilia kinachoendelea....
Mwenyekiti wa waendesha bodaboda manispaa ya Shinyanga Wenceslaus Modest akichangia hoja
Kikao kinaendelea
Picha zote Kadama Malunde - Malunde1 blog

UHAMISHO WA WATUMISHI WA UMMA UFANYIKE KWA MAKINI

0
0
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akizungumza na viongozi na watumishi wa umma wa Segerea alipofanya ziara ya kikazi  ili kupokea maoni, ushauri na kusikiliza kero za watumishi wa umma leo Jijini Dar es Salaam.
  Katibu Tawala wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Bw. Edward Mpogolo akiwatambulisha baadhi ya watumishi na viongozi wa Segerea waliohudhuria kikao kazi kilichowakutanisha na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) Jijini Dar es Salaam.
 Meneja Masoko kutoka kampuni ya Watumishi (Watumishi Housing Company), Bw. Raphael Mwabuponde, akiwasilisha mada kuhusu taratibu za kupata nyumba kwa Watumishi wa Umma wakati wa kikao kazi cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) na Watumishi wa Umma wa Segerea, Jijini Dar es Salaam.
 Mbunge wa Jimbo la Segerea, Mhe. Bonnah Kaluwa akitoa salamu wakati wa kikao kazi na kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb), leo Jijini Dar es Salaam.  
 Mkazi wa Segerea, Bw. Juma Kali akiwasilisha hoja maalum wakati wa kikao kazi kilichowakutanisha watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala - Segerea  na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) leo Jijini Dar es Salaam.
Mtumishi wa Umma kutoka Tabora, Bw. John Joseph akiwasilisha hoja wakati wa kikao kazi kilichowakutanisha watumishi wa umma Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kutoka Segerea na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) leo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) amezitaka Taasisi za Serikali kuratibu suala la uhamisho wa watumishi wa umma kwa makini pale inapohitajika kufanya hivyo Ili kuepuka kero na usumbufu kwa watumishi. 

Waziri Kairuki (Mb) amesema hayo leo katika kikao kazi na Watumishi wa Umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala eneo la Segerea, jijini Dar es Salaam.

Mhe. Kairuki amesema uhamisho lazima ufanyike kwa mtumishi wa umma endapo kukiwa na sababu za msingi sana. “Naomba ieleweke kuwa uhamisho una taratibu zake hivyo kila mwajiri ni mwajiri akazifuata.” Mhe. Kairuki alisisitiza.

Ameongeza kuwa imebainika wapo baadhi ya watumishi wa umma wanawasilisha sababu mbalimbali kwa waajiri kuomba kuhama wakiwa na nia ya kukwepa kukaguliwa sifa zao za elimu. 

Waziri Kairuki amesisitiza kuwa uhamisho usifanyike kwa mtumishi ambaye anaonekana kuwa na matatizo.

“Baadhi ya waajiri wamekuwa na tabia ya kuwahamisha watumishi wa umma ambao wameonekana kuwa na tatizo na kuwahamishia sehemu nyingine, uhamisho wa namna hii haukubaliki, tatizo la mtumishi linatakiwa kufanyiwa kazi kwenye kituo chake cha kazi na sio kupeleka tatizo sehemu nyingine.” Mhe. Kairuki ameongeza.

Mhe. Kairuki yupo katika ziara ya kikazi katika mkoa wa Dar es salaama ambapo leo ni siku ya tisa akiwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala-Segerea kwa kukutana na watumishi wa umma wa kada zote katika vikao kazi.

Waziri Kairuki katika vikao kazi amehimiza watumishi wa umma nchini kubadili mtindo wa maisha, kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi, kujiepusha na ugonjwa wa UKIMWI, na Magonjwa Sugu Yasiyoambukizwa (MSY). 

Lengo la kukutana na watumishi wa umma ni kusikiliza malalamiko, ushauri na changamoto zinazowakabili katika maeneo yao ya kazi ili kuweza kuzifanyia kazi na kuleta mabadiliko katika Utumishi wa Umma nchini ili kufikia malengo yaliyopangwa na Serikali.

SADC Kuendelea Kusimamia Amani Katika Nchi Wanachama

0
0
Na. Bushiri Matenda- MAELEZO

Serikali ya Tanzania imesema itaendelea kushirikiana na nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuhakikisha kunakuwa na amani na mshikamano miongoni mwa nchi wanachama wa Jumuiya hiyo.

Akizungumza wakati akifungua mkutano wa 19 wa Mawaziri wa Jumuiya hiyo leo Jijijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga alisema kuwa Tanzania itaendeleza jitihada zinazofanywa na SADC kwa nchi wanachama katika kuendelea kuimarisha  Ushirikianao katika Siasa, Ulinzi na Usalama.

“Nawasilisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wetu wa SADC ambaye anaamini kuwa mkutano huu unatuleta pamoja katika kujenga ushirikiano wetu zaidi kuhakikisha kuwa tunaendelea kuwa na amani, umoja, mshikamano na ustawi kati ya nchi wanachama,” alisisitiza Dkt. Mahiga

Dkt. Mahiga alisema kuwa nchi wanachama zimeendelea kuwa eneo lenye usalama na ustawi kwa kuzingatia hatua ambazo zimekuwa zikichukuliwa na umoja huo kupitia kamati mbalimbali zilizoundwa kushughulikia mageuzi katika nchi za Lesotho hali iliyosaidia Taifa hilo kufanya uchaguzi wa wabunge mwezi June 2017 kwa amani. 

Aliongeza kuwa katika mkutano huo watajadili swala la uhuru wa wananchi wan chi wanachama kutokuwa na vikwazo wanapotaka kuingia nchi nyingine,kuwa na Kikosi maalum cha Jeshi kwa ajili ya ulinzi wa amani,mikakati ya kusimamia masuala ya mawasiliano na habari, hali itakoyochochea maendeleo kati ya nchi wanachama.

Pia SADC kwa kuzingatia kifungu cha 7 (1) cha itifaki ya umoja huo kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, nchi wanachama zitakuwa na sera na mikakati inayofanana katika kupambana na rushwa kwa kuzingatia mapendekezo ya Kamati ndogo ya mapambano dhidi ya rushwa yatakayojadiliwa katika mkutano huu.

Katika kutekeleza azma yakuondoa tatizo la rushwa kwa nchi wanachama Balozi Dkt. Maiga alizitaka nchi wanachama kuendelea kutekeleza itifaki hiyo katika kutokomeza rushwa katika nchi wanachama.

Aidha Balozi Maiga amewaalika wajumbe wa mkutano huo kutembelea vituo vilivyopo hapa nchini ikiwemo mlima Kilimanjaro, Serengeti, Visiwa vya Zanzibar na Mafia ili kujionea vivutio vilivyopo katika maeneo hayo.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa SADC Mhe. Stergomena Tax amesema kuwa Umoja huo utaendelea kushughulikia mgogoro wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, pia amewaomba nchi wanachama na washirika wa maendeleo kuendelea kuchangia katika Jumuiya hiyo  ikiwemo Umoja wa Ulaya (EU) .

Mkutano wa 19 wa Mawaziri wa nchi wanachama unafanyika Jijini Dar es Salaam ukilenga kujadili maswala ya Siasa, Ulinzi, Usalama na Ushirikiano ndani ya Jumuiya hiyo.
 Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Dr. Stergomena Tax akitoa neno la utangulizi wakati wa mkutano wa 19 wa Kamati ya Mawaziri wa Nchi za Jumuiya hiyo inayojadili ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama mapema hii leo Jijini Dar es SalaamA.
 Waziri wa Mambo ya nje na Ushirkiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Mawaziri wa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (hawapo pichani) wakati akifungua mkutano wa 19 wa Kamati hiyo unaojadili ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama mapema hii leo Jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Mawaziri wa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya nje na Ushirkiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (hayupo pichani) wakati akifungua mkutano wa 19 wa Kamati hiyo unaojadili ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama mapema hii leo Jijini Dar es Salaam. (Picha na Eliphace Marwa – MAELEZO)

RAIS WA BURUNDI AWASILI NCHINI KWA ZIARA RASMI NA KUPOKELEWA NA MWENYEJI WAKE RAIS DKT. JOHN MAGUFULI - NGARA MKOANI KAGERA

0
0
Rais wa Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza akiwasalimia wananchi wa Mji wa Ngara kwenye Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Posta Mjini Ngara 20 Julai 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Rais wa Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza mara baada ya Rais wa Burundi kuwahutubia wananchi wa Mji wa Ngara kwenye Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Posta Mjini Ngara 20 Julai 2017.
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia mamia ya wananchi wa Mji wa Ngara kwenye Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Posta Mjini Ngara Mkoani Kagera 20 Julai 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpokea Rais wa Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Lemela mjini Ngara Mkoani Kagera Julai 2017
Rais wa Jamuhuri ya Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza akiwapungia wananchi alipowasili katika viwanja vya Lemela mjini Ngara Mkoani Kagera Julai 20,2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Rais wa Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza wakiwa wamesimama wakipokea salamu za heshima kutoka kwa majeshi ya ulinzi na usalama.
Rais wa Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza akikagua graride la lililoandaliwa na jeshi la ulinzi la Tanzania JWTZ katika viwanja vya Lemela mjini Ngara Mkoani Kagera Julai 20,2017
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mgeni wake Rais wa Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza mara baada ya Kumpokea katika Uwanja vya Lemela mjini Ngara Mkoani Kagera 20 Julai 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Rais wa Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza akiwasalimia wananchi wa Mji wa Ngara kwenye uwanja wa Lemela mjini Ngara Mkoani Kagera 20 Julai 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiteta Jambo na Rais wa Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza Mara baada ya kumpokea katika Mji wa Ngara kwenye uwanja vya Lemela mjini Ngara Mkoani Kagera 20 Julai 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Rais wa Jamuhuri ya Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza kwa maongezi mjini Ngara Mkoani Kagera 20 Julai 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na ujumbe wake katika mazungumzo maalum ya kiserikali na Rais wa Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza na ujumbe wake Mjini Ngara Mkoani Kagera 20 Julai 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza pamoja na mama Janeth Magufuli katika Maongezi.
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na mgeni wake Rais wa Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza wakiwapungia mikono wananchimwa mji wa ngara wakati wakiwasili katika uwanja wa posta mjini Ngara kwa ajili ya mkutano wa hadhara.
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na mgeni wake Rais wa Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza wakiwapungia mikono wananchi wa mji wa Ngara waliohudhulia katika uwanja wa posta mjini Ngara kwa ajili ya Mkutano wa hadhara.
Umati wa ananchi wa mji wa Ngara waliohudhulia katika uwanja wa posta mjini Ngara kusikiliza Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika uwanja wa posta mjini Ngara 20 Julai 2017.
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na mgeni wake Rais wa Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza katika uwanja wa Lemela Mjini Ngara Mkoani Kagera 20 Julai 2017 baada ya kumaliza ziara yake Rasmi ya kiserikali Nchini. PICHA NA IKULU.

TAMASHA LA USALAMA BARABARANI KUFANYIKA AGOSTI 5 MWAKA HUU UWANJA WA TAIFA

0
0
 Naibu Waziri  wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu Tamasha la Usalama Barabarani linalotarajiwa kufanyika mapema mwezi wa nane, mwaka huu katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam,ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli. Kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi,Fortunatus Musilimu. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi, Fortunatus Musilimu, akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani) kuhusu Tamasha la Usalama Barabarani linalotarajiwa kufanyika mapema mwezi wa nane, mwaka huu katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli. Kushoto ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani,Mhandisi Hamad Masauni. 
Waandishi wa  Habari wakimisikiliza Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni wakati wa Mkutano uliohusu Tamasha la Usalama Barabarani linalotarajiwa kufanyika mapema mwezi wa nane,mwaka huu katika Uwanja wa Taifa,Jijini  Dar es Salaam, ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk. John Magufuli.Kushoto ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi,Fortunatus Musilimu.

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Viewing all 46205 articles
Browse latest View live




Latest Images