Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

DIAMOND PLUTNUMZ, WIZKID, DAVIDO, MR EAZI, JOHN BOYEGA, ABRANTEE & MORE NOMINATED FOR 2017 AFRICAN PRIDE AWARDS

$
0
0
Following its seminal debut ceremony last July, which saw the likes of Wizkid, Fuse ODG, CEO Dancers and Anthony Joshua take home the biggest prizes of the night, having been voted for by over half a million people online, African Pride Awards is back for its second annual award gala and ceremony, proudly brought to you by Africa Unplugged and Therapy Ent.

Leading the award nominations this year are none other than Wizkid once again, Davido, Mr Eazi, Tekno, Yemi Alade, Shatta Wale, Tiwa Savage and Diamond Platnumz, who are all nominated for the ‘Artist Of The Year (Africa)’ award, with the likes of Maleek Berry, Sona, Moelogo, Eugy, Juls and Ms. Banks representing for the UK, in the ‘Artist Of The Year (UK)’ category.

African movie stars Funke Akindele, AY, John Dumelo, Nana Ama McBrown, Nomzamo Mbatha and Abraham Attah, will be vying for the ‘Outstanding Achievement In Film (Africa)’ award, while the likes of John Boyega, Idris Elba, Maria Gomez, Chucky Venn, and Daniel Kaluuya, are up against each other in the ‘Outstanding Achievement In Film (UK)’ award category.

Also nominated are Nqobile, Ezinne Asinugo, Sherri Silver and GOP Dancers in the ‘Dance/Choreography Of The Year’ category, as well as Bella Naija, Iroko TV, Linda Ikeji, Afrobeat360 and Factory 78, in the ‘African Online Entertainment Platform Of The Year’ category, and Abrantee, Twin B, Julie Adenuga, Maya Jama and Manny Norte, in the ‘Radio Personality Of The Year’ category.

African music legend Awilo Longomba will be honoured with the ‘Lifetime Achievement Award’, while ‘Special Recognition Award’ nods will be presented to Ade Adepitan, SBTV, Link Up TV, GRM Daily, John Boyega, Larry Ekundayo, Eddie Kadi and The Compozers, who are also confirmed to be performing at the award ceremony.

Other award categories being announced via the African Pride Awards website include ‘Outstanding Media & PR Agency Of The Year’, ‘Makeup Artist Of The Year’, ‘African Club/Club Night of The Year’, ‘Event Organiser/Promoter Of The Year’, ‘TV Personality Of The Year’, ‘Radio Personality Of The Year’, ‘African TV Station Of The Year’, ‘Comedian Of The Year’ and ‘Outstanding Disk Jockey Of The Year’, just to mention a few.

Speaking about what to expect from the African Pride Awards this year, Abiodun Osibodu, CEO of Africa Unplugged and Therapy Ent says, “We are so proud yet humbled to have honored so many Africans doing incredible things in the diaspora and in Africa at the first ever APA in 2016. This year we will be honouring more people who have excelled within the community and celebrating our culture and heritage in a bigger way”.

Voting is now open to the public, with the first round of voting to end on July 30, and final public voting set to close on August 10. Winners will be announced at the main award gala and ceremony on August 13, 2017.

Vitale Water, ROK TV and Royal London Hotel & Suites are proud to support the 2017 African Pride Awards.

Advanced tickets for the 2017 African Pride Awards are available right now via:


NBS YAMUAGA MKUU WA UTAWALA WA BENKI YA DUNIA

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa (kulia) akimkabidhi zawadi aliyekuwa Mtaalamu Mkuu Utawala kutoka Benki ya Dunia, Dkt. Verena Knippel wakati wa hafla fupi ya kumuaga mara baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini. Hafla hiyo imefanyika leo jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa (kulia) akizungumza leo jijini Dar esa Salaam wakati wa hafla ya kumuaga aliyekuwa Mtaalamu Mkuu Utawala kutoka Benki ya Dunia, Dkt. Verena Knippel katika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).
Aliyekuwa Mtaalamu Mkuu Utawala kutoka Benki ya Dunia, Dkt. Verena Knippel (kushoto) akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa (kulia) akimpongeza aliyekuwa Mtaalamu Mkuu Utawala kutoka Benki ya Dunia, Dkt. Verena Knippel (kushoto) wakati wa hafla ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa (wa sita kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa NBS pamoja na aliyekuwa Mtaalamu Mkuu Utawala kutoka Benki ya Dunia, Dkt. Verena Knippel (wa tano kushoto) wakati wa hafla ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini.

WATUHUMIWA 4,809 WA DAWA ZA KULEVYA WAKAMATWA

$
0
0
*Heroine, Cocaine, bangi, mirungi na kemikali bashirifu vyakamatwa
* Mashamba ya bangi ekari 569.25 na mirungi ekari 64.5 yateketezwa


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema katika kipindi cha miezi minne, Mamlaka ya Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA) imewakamata watuhumiwa 4,809 na kufungua majalada ya kesi 3,222.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Julai 5, 2017), bungeni mjini Dodoma wakati akitoa hoja ya kuahirisha mkutano wa saba wa Bunge la 11. Bunge limeahirishwa hadi Septemba 5, mwaka huu.

“Katika kipindi kifupi tangu Februari, 2017 Mamlaka hii ilipozinduliwa, imefanikiwa kukamata watuhumiwa 4,809 wakiwa na dawa za kulevya aina ya heroine (gramu 327.173); cocaine (kilo 26.977); bangi (kilo 18,334.83); mirungi (kilo 11,306.67) na lita 6,338 za kemikali bashirifu zilikamatwa bandarini,” amesema.

Amesema mamlaka hiyo kwa kushirikiana na Kamati za Ulinzi za Mikoa imefanya operesheni za kuteketeza ekari 569.25 za mashamba ya bangi na ekari 64.5 za mashamba ya mirungi na kazi hiyo inaendelea. Kutokana na hatua hizo, jumla ya majalada ya kesi 3,222 yamefunguliwa.

“Dawa za kulevya zina athari kubwa kwa ustawi wa familia zetu na Taifa kwa ujumla. Hivyo, napenda kurejea wito wangu kwa Watanzania wote kuunga mkono jitihada za Serikali katika mapambano haya kwa kuendelea kutoa taarifa kuhusu watu wote wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Amesema azma ya Serikali ya awamu ya tano ni kutokomeza kabisa mtandao wa dawa za kulevya nchini kwa kuhakikisha kuwa mapambano dhidi ya dawa za kulevya yanakuwa endelevu, yanafanyika kisayansi na yanaleta mafanikio. “Tuungeni mkono kwenye mapambano haya, ili tutokomeze kabisa mtandao huo,” amesisitiza.


IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
40480 - DODOMA.
JUMATANO, JULAI 5, 2017.

MAONESHO YA SABASABA 2017: HUDUMA ZA PSPF NI "CHAP CHAP", AFISA WA POLISI ASEMA

$
0
0

Modesta Mchopa wa PSPF, (kulia), akimpatia taarifa za michango mwanachama wa Mfuko huo, Afisa wa polisi, E.M Peter, aliyefika kwenye banda la Mfuko huo leo Julai 5, 2017. Afisa huyo wa polisi amesifu utoaji huduma wa wafanyaakzi wa Mfuko huo ambapo alisema yeye ametumia sekunde 30 kupatiwa taarifa yake.(NA K-VIS BLOG/Khalfan Said)
 Mhandisi mwandamizi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bw. Ally R. Shanjirwa (kulia), akimkabidhi kadi yake ya uanachama wa Mfuko huo, kupitia mpango wa uchangiaji wa hiari (PSS), Bi.Julieth Mwiziko, punde tu baada ya kujiunga.
Afisa Uendeshaji wa PSPF, Bi. Irine J. Musetti(kulia),
akimkabidhi kadi yake ya uanachama wa Mfuko huo, kupitia mpango wa uchangiaji wa hiari (PSS), Bi.Sakina Iddi Tundu, punde tu baada ya kujiunga.
 Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Bw. Abdul Njaidi (kulia), akimsaidia mama huyu kujaza fomu za kujiunga na PSPF kupitia mpango wa uchangiaji wa hiari PSS.


 Mwanachama huyu akiwa amepatiwa taarifa za michango yake papo hapo
 Mwanachama akisoma taarifa za michango yake
 Binti huyu akisoma kipeperushi chenye taarifa mbalimbali za PSPF
Bi. Modesta Mchopa, ambaye naye ni afisa wa PSPF aliye kwenye mafunzo. akiwahudumia wanachama hawa wa Mfuko huo waliofika kujua michango yao.
Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Bw. Abdul Njaidi (wapili kushoto), akimwelekeza jambo Mfanyakazi wa PSPF aliye kwenye mafunzo ya vitendo, Bw.Honorath Tillya, (watatu kushoto), huku mwananchi aliyetembelea banda la Mfuko huo (kulia), akijaza kitabu cha wageni. Wakwanza kushoto ni Modesta Mchopa, ambaye naye ni afisa wa PSPF aliye kwenye mafunzo.
Win-God, (kushoto), Afisa wa uendeshaji msaidizi wa PSPF, waliwahudumia wateja.
Afisa uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF anayeshughulikia masuala ya uchangiaji wa hiari (PSS), Bi. Asmahan H. Haji,(kulua), akiwahudumia wananchi waliotembelea banda la Mfuko huo.
 Anna Lukando, katikati anayeangalia camera), ambaye ni Afisa Mipango wa Taasisi ya Ardhi Plan Limited,  ambayo ni mshirika wa PSPF katika masuala ya  viwanja, akiwapatia maelezo wananchi waliofika banda la PSPF ili kupatiwa huduma za uanachama. Wanachama wa PSPF kwa mujibu wa sheria, wanaweza kukopeshwa viwanja na taasisi hiyo.
 Anna Lukando, (kushoto), ambaye ni Afisa Mipango wa Taasisi ya Ardhi Plan Limited,  ambayo ni mshirika wa PSPF katika masuala ya  viwanja, akiwapatia maelezo wananchi waliofika banda la PSPF ili kupatiwa huduma za uanachama. Wanachama wa PSPF kwa mujibu wa sheria, wanaweza kukopeshwa viwanja na taasisi hiyo.
 Afisa Mkuu wa Mifumo ya Kompyuta (TEHAMA), wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bi. Mariam Ibrahim, (kulia), akiangalia jinsi mwananchi huyu anavyojaza fomu ya kujiunga na Mfuko huo kupitia uchangiaji wa Hiari, (PSS), kwenye banda la PSPF lililoko jengo la Wizara ya Fedha na Mipango kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere maarufu kama (sabasaba), barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam ambako kunafanyika maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam.
Afisa msaidizi mwendeshaji wa PSPF, Bw. Musa Mfaki, (kulia), akimuhudumia mwananchi
Bw. Isack Kimaro, (kushoto), Afisa wa uendeshaji PSPF, akimuhudumia mwananchi aliyejiunga kwenye mpango wa PSS
Afisa wa Huduma za Sheria wa Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii, (SSRA), aliye kwenye banda la Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bi. Imani Masebu, (wapili kulia), akiwafafanulia masuala muhimu yahusuyo hifadhi ya jamii wananchi hawa waliofika wkenye banda la Mfuko huo. Kulia ni Afisa Mkuu wa Mifumo ya Kompyuta wa PSPF, Bi. Mariam Ibrahim.
Kikao cha tathmini ya kazi iliyofanyika kutwa nzima katika banda la PSPF kikiongozwa na mkuu wa timu inayoshiriki kuwahudumia wananchi kwenye banda hilo Bw. Abdul Njaidi.

SERIKALI YAPUNGUZA TOZO YA ARDHI KWA ASILIMIA 5

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kuanzia mwaka huu wa fedha, Serikali imepunguza gharama za malipo ya awali ya thamani ya ardhi iliyopimwa kutoka asilimia 7.5 hadi asilimia 2.5.

“Serikali inaendelea kupunguza gharama za umilikaji wa ardhi nchini na katika mwaka wa fedha 2017/2018, imepunguza tozo ya awali ya ardhi iliyopimwa (premium) kutoka asilimia 7.5 ya thamani ya ardhi hadi asilimia 2.5 tu. Natoa wito kwa wananchi kuchangamkia punguzo hili na kujitokeza kupimiwa na kumilikishwa ardhi,” amesisitiza.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Julai 5, 2017), bungeni mjini Dodoma wakati akitoa hoja ya kuahirisha mkutano wa saba wa Bunge la 11. Bunge limeahirishwa hadi Septemba 5, mwaka huu.

Amesema Serikali itahakikisha kuwa kila kipande cha ardhi ya Tanzania kinapimwa ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015. “Serikali imeweka mkakati na mpango kazi wa kuwezesha kufikia lengo la kupanga matumizi bora ya ardhi katika vijiji 1,500 na wilaya tano kila mwaka.”

Amesema Serikali itaendelea kuimarisha Ofisi za Ardhi za Kanda kwa kupeleka wataalam wa kada mbalimbali na kuwawezesha kwa kuwapatia vitendea kazi stahiki. “Kazi ya upimaji wa ardhi haiwezi kufanikiwa bila ya rasilmali watu.Lengo letu ni kuwawezesha wananchi kupata huduma mbalimbali za ardhi katika kanda badala ya kufuata huduma hizo makao makuu ya wizara,” amesema.

Amewasihi watumishi watakaohamishiwa katika ofisi za kanda pamoja na wale waliopo katika Halmashauri, wafanye kazi kwa ushirikiano na watekeleze majukumu yao kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia sekta ya ardhi na kutoa huduma kwa wananchi bila ubaguzi wa aina yoyote.


IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
40480 - DODOMA.
JUMATANO, JULAI 5, 2017.

AMREF YAFANYA MKUTANO NA WADAU KATIKA MAHADHIMISHO YA MIAKA 60

$
0
0
 Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mamhoud Thabiti Kombo, akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa wadau wa Amref  Uliofanyika jijini Dar es Salaam leo
 Mkurugenzi wa Amref Nchini,Florence Temu  akizungumza wakati wa mkutano huo wa wadau uliofanyika katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam


 Mtendaji mkuu wa kurugenzi wa Amref Africa ,Githinji Gitahi akizungumza kwa ufupi Historia ya Amref Hapa nchini na Mafanikio yake katika sekta ya Afya
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Mpoki Ulisubisya akizungumzia namna gani Amref imesaidiakatika sekta ya Afya nchini
 sehemu ya wadau walioshiriki mkutano wa wadau wa Amref  katika Hotel Serena Jijini Dar es Salaam
  sehemu ya wadau walioshiriki mkutano wa wadau wa Amref  katika Hotel Serena Jijini Dar es Salaam
Picha ya Pamoja ya wadau wa Amref na Mgeni Rasmi Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mamhoud Thabiti Kombo

MEYA WA JIJI NA MEYA WA KINONDONI WATEMBELEA BANDA LA (LAPF) MAONYESHO YA SABASABA

$
0
0
Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Mh. Isaya Mwita akizungumza na Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa LAPF Bw. James Mlowe wakati alipotembelea katika banda la Mfuko wa Pensheni wa LAPF kwenye viwanja vya maonyesho ya biashara vya Mwalimu J.K. Nyerere Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam.

Mfuko wa LAPF na Jiji la Dar es salaam wana Mpango kabambe wa kutekeleza ujenzi wa kituo kipya cha mabasi ya kwenda mikoani jijini Dar es salaam utakaogharimu zaidi ya shilingi Bilioni 30.
Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa LAPF Bw. James Mlowe akitoa maelezo kwa Meya wa Jiji na Meya wa Kinondoni Mh. Benjamin Sitta wakati mameya hao walipotembelea katika banda la mfuko huo leo
Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Mh. Isaya Mwita na Meya wa Kinondoni Mh. Benjamin Sitta wakisaini kitabu cha wageni wakati walipowasili katika banda hilo kulia ni Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa LAPF Bw. James Mlowe.
Matukio mbalimbali ya picha yakiontesha baadhi ya wafanyakazi wa LAPF wakiwahudumia wananchi waliofika kwenye banda la mfuko wa Pensheni wa LAPF kwenye Maonyesho ya Sabasaba barabara ya Kilwa leo.

British Council Yatoa Fursa Kujipima Kiingereza

$
0
0
Mkurugenzi Mkazi wa British Council nchini Tanzania Bi. Angela Hennely akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, kuhusu ofa ya jaribibo la mtihani wa Kiingereza inayotolewa na Taasisi yake katika Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF).Kushoto ni Afisa Huduma kwa Wateja na Mauzo Bi. Leonia Kazimoto na Maneja Maendeleo ya Biashara wa Britishi Council Bi. Amata Bosco.
Mkurugenzi Mkazi wa British Council nchini Tanzania Bi. Angela Hennely akitoa maelekezo kwa wanafunzi waliofika katika banda lao kwa ajili ya kufanya majaribio ya somo la lugha ya Kiingereza huduma inayotolewa bure na Taasisi hiyo katika kipindi hiuki cha Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara. Huduma hiyo inatolewa kwa lengo la kutambua kiwango cha uelewa wa mwanafunzi ili kujua Kozi hali anayostahili kujiunganayo.
Baadhi ya wananchi wakifanya mtihani wa majaribio wa lugha ya Kiingereza walipotembelea banda la British Council katika Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) leo. Britishi Council wanatoa huduma hiyo bure kwa lengo la kumpatia fursa mwananchi kutambua daraja hali analostahili kujiunga nalo ikiwa anahitaji kusoma somo la lugha hiyo
Mkurugenzi Mkazi wa British Council nchini Tanzania Bi. Angela Hennely akitoa Aakiwasimamia wananchi waliofika katika banda lao kwa ajili ya kufanya majaribio ya somo la lugha ya Kiingereza, huduma inayotolewa bure na Taasisi hiyo katika kipindi hiki cha Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara. Huduma hiyo inatolewa kwa lengo la kutambua kiwango cha uelewa wa mwanafunzi ili kujua Kozi hali anayostahili kujiunganayo.

Halmashauri Zashauriwa Kuiunga Mkono Serikali Katika Tanzania ya Viwanda

$
0
0
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage akiwatambulisha Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Issaya Mwita (kulia) na Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Benjamin Sitta kwa ugeni kutoka Oman walipotembelea katika Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) leo.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Benjamin Sitta akisalimiana na Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa (LAPF), Bw. James Mlowe alipotombelea banda la Mfuko huo wakati wa Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) leo. Katikati ni Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Issaya Mwita.


Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Issaya Mwita akimwelezea jambo Mkurugenzi Mkuu wa SIDO Tanzania Mhandisi. Profesa Sylivester Mpanduji alipotembelea banda lao katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) leo. Kushoto ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Benjamin Sitta.
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Issaya Mwita na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mh. Benjamin Sitta wakitazama ramani ya miradi ya makazi inayojengwa katika eneo la Kigamboni na Kampuni ya Internatinal Property walipotembelea banda la Kampuni hiyo katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) leo. Kulia ni Afisa Uhusiano wa Kampuni hiyo Bw. Saleh Omar Saleh.
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Issaya Mwita na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mh. Benjamin Sitta wakipata maelezo ya huduma mbalimbali zinazotolewa na Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) walipotembelea banda la Kampuni hiyo katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) leo.
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam akipata huduma ya kupima urefu mara baada ya kupima presha alipotembelea banda la Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) leo.
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Issaya Mwita(kulia) na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mh. Benjamin Sitta (kulia kwake) wakisikiliza namna mfumo wa Automotive unavyofanyakazi banda la VETA katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) leo. Katikati ni Meneja Uhusiano wa VETA Bw. Peter Sitta.

Na: Frank Shija – MAELEZO

…………………………..

Na: Frank Shija -MAELEZO

Halmashauri nchini zimetakiwa kutumia vyema fedha zinazotengwa kwa ajili ya kundi la vijana na wanawake katika kuunga mkono dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuifanya Tanzania inakuwa nchi ya Uchumi wa Kati na Viwanda.

Hayo yamebainishwa leo na Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam alipotembelea Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) mabapo katika ziara hiyo aliambatana na Mstahiuki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Bw. Benjamin Sitta.

“Taasisi za kifedha zinao wajibu mkubwa katika kufikia adhima hii ya Serikali, lakini sisi Serikali za mitaa, Halmashauri ziano wajibu mkubwa kuhakikisha zilie asilimia tano za vijana na tano za wanawake zinakuwa sehemu ya kuchochea ufanikishaji wa dhamira njema ya Serikali,” alisema Mhe. Mwita.

Aidha Mhe. Mwita ametoa pongezi kwa uongozi wa Tantrade kutokana na jitihada zao za kuhakikisha wanasaidia ukuaji wa bidhaa za ndani hasa bidhaa za ngozi ambapo alisisitiza ni vyema wakaendelea kuweka mkazo katika eneo hilo kabla ya kuangalia maeneo mengine.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Benjamin Sitta amesema kuwa Maonesho hayo ya Sabababa yamekuwa na manufaa kwa wafanyabiashara wengi na hata kwa wananchi kuja kujifunza.

Aliongeza kuwa pamoja na wananchi kuja kujifunza lakini pia imekuwa ni fursa kwa wafanyabiashara kutengeneza mahusiano na wafanyabiashara wenzao kutoka nchi nyingine jambo ambalo katika biashara ni muhimu sana.

Nae, Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) Edwin Ratageruka amesema kuwa dhamira yake ni kuhakikisha bidhaa za ndani zinakuwa na soko la uhakika ndani na nchi ya nchi.

Ameongeza kuwa kwa kuanzia wamejikita zaidi katika bidhaa za ngozi ikiwa ni njia pia ya kuwainua wafugaji ambao mazao ya mifugo yao yanatumika katika kutengeneza bidhaa mbalimbali za ngozi.

“Serikali inatambua umuhimu wa kuthamini bidhaa za ndani, ndiyo sababu Ofisi ya Waziri Mkuu iliratibu zoezi ambalo jumla ya vijana 1000 walipatiwa mafunzo ya usindikaji na ushonaji wa ngozi, katika mafunzo yaliyofanyika Chuo cha Teknolojia Dar es Salaam tawi la Mwanza,” alisema Rutageruka.

Rutageruka ameongeza kuwa katika kuendeleza jitihada hizo Gereza la Karanga (Moshi) na Kampuni ya Woisso ya Jijini Dar es Salaam zinatarajia kuanzisha viwanda kwa ajili ya kutengeneza sole ili kuachana na utaratibu wa kuagiza skutoka nje.

Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam yanafanyika huku azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ikiwa ni kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi ya uchumi wa kati na viwanda, kutokana na dhamira hiyo maonesho haya yamepewa kauli mibu isemayo; “Ukuzaji wa Biashara kwa Maendeleo ya Viwanda.”

WAZIRI MKUU AAGIZA KUSIMAMIWA KWA UTEKELEZAJI WA SHERIA ZA NCHI ZENYE LENGO LA KUMLINDA MTOTO WA KIKE

MRISHO MPOTO ATANGAZWA KUWA BALOZI WA PROPERTY INTERNATIONAL

$
0
0
 Mrisho Mpoto akiwa ameshika tuzo ya ,Property International mara baada ya kutangazwa kuwa balozi wa kampuni ya Property International katika maonesho ya kimataifa ya Biashara
 Mtendaji Mkuu wa Property International , Abdulkarim Haleem  akitoa maelezo kwa Mrisho Mpoto mara baada ya kumtangaza kuwa balozi wa kampuni hiyo
Mrisho Mpoto akipata maelezo kutoka kwa wakurugenzi wa kampuni ya Property

TANZIA: MWANAMUZIKI SHAABAN DEDE AFARIKI DUNIA LEO

$
0
0
Mwanamuziki mkongwe Shaaban Dede amefariki dunia leo saa mbili asubuhi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa matibabu kwa takriban wiki mbili, mwanae Hamad Dede amethibitisha. 

Hamad Dede amesema mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa marehemu Mbagala jijini Dar es salaam, na kwamba ratiba na taratibu zote zitatangazwa mara zitapokamilika kupangwa.

Marehemu Dede atakumbukwa kama mmoja wa wanamuziki nguli kutokea nchini Tanzania kwa sauti yake tamu na utunzi wa nyimbo mbalimbali zilizoshika chati akiwa na bendi mbalimbali zikiwemo Tabora Jazz, Bima Lee, Mlimani Park na Mondo Ngoma ambako alikuwa anatumikia hadi mauti yanamkuta.

Globu ya Jamii inatoa mkono wa rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na mashabiki wa Shaaban  Dede kwa kuondokewa na mkongwe huyu wa muziki.



Mola aiweke roho ya marehemu mahala pema peponi - AMIN

Inna Lillahi wa inna ilayhi raji'un


WAZIRI KINDAMBA ATEULIWA KUWA AFISA MTENDAJI MKUU WA TTCL

$
0
0
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) 
Bw. Waziri Waziri Kindamba

VIJUSO VYA MAGAZETI YA ALHAMIS LEO JULY 6,2017

Fahamu miundombinu ya serikali mtandao


MANISPAA YA UBUNGO KUANZA UJENZI WA BARABARA YA KWENDA SHULE YA SHERIA

$
0
0
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi kayombo akielekeza jambo wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua barabara ya Mawasiliano kuelekea Shule ya Sheria (Law school Of Tanzania)
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi kayombo akiwa na viongozi wengine wa shule ya Sheria Tanzania wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua barabara ya Mawasiliano kuelekea Shule ya Sheria (Law school Of Tanzania)
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi kayombo akiwa na viongozi wengine wa shule ya Sheria Tanzania wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua barabara ya Mawasiliano kuelekea Shule ya Sheria (Law school Of Tanzania)
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi kayombo akiwasalimu wanafunzi wa Shule ya Sheria Tanzania wakiwa darasani wakati alipozuru Chuoni hapo wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua barabara ya Mawasiliano kuelekea Shule ya Sheria (Law school Of Tanzania)
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi kayombo akiwa na viongozi wengine wa shule ya Sheria Tanzania wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua barabara ya Mawasiliano kuelekea Shule ya Sheria (Law school Of Tanzania)
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi kayombo akiwa na viongozi wengine wa shule ya Sheria Tanzania wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua barabara ya Mawasiliano kuelekea Shule ya Sheria (Law school Of Tanzania)
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi kayombo akisaini kitabu cha wageni wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua barabara ya Mawasiliano kuelekea Shule ya Sheria (Law school Of Tanzania)
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi kayombo akiwa na viongozi wengine wa shule ya Sheria Tanzania wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua barabara ya Mawasiliano kuelekea Shule ya Sheria (Law school Of Tanzania)
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi kayombo akisikiliza maelezo mafupi kutoka kwa Makamu Mkuu wa Chuo cha sheria Tanzania Dkt Willium Palanjo kuhusu changamoto ya ubovu wa barabara wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua barabara ya Mawasiliano kuelekea Shule ya Sheria (Law school Of Tanzania)
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi kayombo akizungumza na Viongozi wa Shule ya sheria Tanzania wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua barabara ya Mawasiliano kuelekea Shule ya Sheria (Law school Of Tanzania)
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi kayombo akiwa na Viongozi wa Shule ya Sheria Tanzania wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua barabara ya Mawasiliano kuelekea Shule ya Sheria (Law school Of Tanzania)
Kushoto ni Rais wa serikali ya wanafunzi Shule ya sheria Tanzania Ndg Emmanuel Nyanza, Dkt Clement Mashamba muhadhiri shule ya sheria Tanzanai, na Kaimu Mkuu wa Idara ya Ujenzi na Zimamoto, wakati wa ziara ya kikazi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi kayombo ya kutembelea na kukagua barabara ya Mawasiliano kuelekea Shule ya Sheria (Law school Of Tanzania)

Na Mathias Canal, Dar es salaam

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi kayombo Tarehe 6 June 2017 amekagua na kujionea hali ya ubovu wa barabara inayotoka Mawasiliano kuelekea Shule ya Sheria (Law school Of Tanzania) iliyopo katika Kata ya Sinza Jijini Dar es salaam.

Akizungumza mara baada ya kutembelea barabara hiyo katika ziara yake ya kikazi huku akiwa ameambatana na Kaimu Mkuu wa Idara ya Ujenzi na zima moto Ndg Goodluck Mbanga, Mkurugenzi Kayombo alisema kuwa matengenezo hayo yataanza hivi karibuni ili kurahisha huduma za kijamii kwa watumiaji wa barabara hiyo wakiwemo wananchi wa Mtaa wa Mawasiliano na Kata ya Sinza sambamba na wanafunzi wa Shule ya Sheria.

MD Kayombo alisema kuwa Fedha za matengenezo ya barabara hutolewa na Bodi ya Mfuko wa Barabara (Road Fund) ambapo lengo kuu ni kuhakikisha kuwa barabara zinapitika muda wote.

Kiwango cha matengenezo kimefikia wastani wa asilimia 90 kwa matengenezo ya aina mbalimbali hususani ya muda maalumu (Periodic maintenance), sehemu korofi (Spot Improvement), matengenezo ya kawaida (Routine maintenance) na ujenzi wa makalavati huku kiwango kikubwa pia kikitolewa na serikali kwa ajili ya ujenzi wa barabara za lami.

Mwanzoni mwa mwezi Februari serikali ilizitaka Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini kuhakikisha wanasimamia sheria katika utendaji wao wa kazi pamoja na kufanya kazi kwa uadilifu, kutumia weledi wa taaluma zao katika kusimamia suala la usafi wa mazingira,yakiwemo masuala ya kudhibiti biashara holela, uegeshaji wa magari holela na ujenzi holela.

Mkurugenzi Kayombo alisema kuwa barabara hiyo itakuwa na urefu wa kilomita 1.2 hivyo kuhudumia wananchi wengi ambao wanataabika kwa adha ya ukorofi wa barabara hiyo.

Usaili wa kuwasaka warembo wa Miss Grand Tanzania wiki ijayo

$
0
0
Usaili wa kuwatafuta washiriki wa mashindano ya kumtafuta mrembo wa Miss Grand Tanzania utafanyika Julai 10, mwaka huu katika ukumbi wa Dar es salaam Convention Centre, jijini Dar es Salaam.

Zoezi za usaili litakalosimamiwa na wadau wa urembo nchini litaanza saa 4.00 asubuhi na kufikia tamati saa 11.00 jioni.

Mratibu wa mashindano hayo nchini Abraham Mahimbo amewataka warembo wenye vigezo kuichangamkia fursa hiyo kwani ni mashindano yanayokuja kuleta mapinduzi katika fani ya urembo nchini.

Mahimbo amesema mashindano ya Miss Grand Tanzania ambayo yatakuwa chini ya Miss Grand International yanakuja kuleta mapinduzi na kuyapa heshima mashindano ya urembo nchini.

“Warembo wanaojiamini na waliotayari kwa mapinduzi ninawakaribisha katika usaili kwani nafasi hii ni adhimu ambayo hutokea mara moja tu katika maisha,” alisema Mahimbo.

Amevitaja vigezo vya kushiriki mashindano hayo ni umri wa kati ya miaka 18-27, urefu sentimita 168, ambaye hajaoelwa, hajawahi kupata mtoto, ajue utamaduni na matukio yanayoendelea nchini, kisiasa, uchumi, mazingira, matatizo, awe na tabia njema na hajawahi kujihusisha na vitendo vya aibu kama biashara ya ngono.

Alisema siku ya usaili washiriki watatakiwa kuwasilisha vyeti vya kuzaliwa na fomu zinapatikana Swahili Studios- Magomeni, Merry Bright Beauty Point-Tabata, City Star Boutique- Namanga na Infinity Lounge Mbezi Beach.

“Kwa mawasiliano kuhusu ushiriki wa mashindano hayo wawasiliane nami kwa namba ya simu  0717 653 653.”

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AZITAKA TAASISI ZA MAENDELEO YA FEDHA NA JUMUIYA YA MAENDELEO KUSINI MWA AFRIKA (SADC),KUIMARISHA USHIRIKIANO

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amezitaka Taasisi za Maendeleo ya Fedha za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuimarisha ushirikiano na kubadilisha uzoefu katika utendaji wao wa kazi ili kuhakikisha kazi zinazofanywa na Taasisi hizo zinakuwa na manufaa kwa wananchi wa Jumuiya hiyo.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo wakati anafungua Mkutano wa mwaka wa Taasisi za Maendeleo ya Fedha za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema kuwa kama taasisi hizo za kifedha zitafanya kazi kwa kuzingatia ubunifu na uaminifu ana uhakika kuwa malengo waliyojiwekeza yatafikiwa kwa wakati hasa katika uwekezaji katika miradi mbalimbali ya maendeleo.

Ameeleza kuwa bado upo umuhimu mkubwa kwa Taasisi hizo za Kifedha katika nchi za SADC kuendelea kutumia ipasavyo wataalamu wa vyuo vikuu na taasisi za utafiti kwa lengo la kukuza uchumi unaotokana na ujuzi kupitia ubunifu.

Makamu wa Rais pia amehimiza nchi wanachama wa SADC kupitia taasisi za kifedha za nchi hizo kushirikiana katika kuchangia fedha katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo katika nchi wanachama wa jumuiya hiyo.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt Ashatu Kijaji amesema anaimani kubwa kuwa mkutano utasaidia kwa kiasi kikubwa uimarishaji wa utendaji wa kazi katika Taasisi hizo za Maendeleo ya Fedha katika nchi za SADC.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akiteta jambo na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt Ashatu Kijaji

GLOBAL EDUCATION LINK INAENDELEA NA UDAHILI VYUO VIKUU VYA NJE

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MAMLAKA  wa Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA)imejizatiti katika kufanya marekebisho ya sheria ikiwa ni katika kuboresha zaidi manunuzi ya zabuni kwa serikali.

Akizungumza wakati akitembelea banda la PPRA lililopo kwenye jengo la Wizara ya Fedha na Mipango, Afisa Mtendaji Mkuu wa PPRA Dkt Laurent Shirima amesema kuwa maboresho hayo yatalenga katika sehemu tano ambazo zitaboresha manunuzi ya zabuni katika nyanja mbalimbali.

Dkt Shirima amesema kuwa wataboresha manunuzi katika kupunguza gharama za ununuaji wa zabuni, serikali kununua kwa bei za sokoni wakimaanisha bei halisi ya zabuni pia watatoa upendeleo kwa makampuni ya ndani ikiwemo makundi maalumu kama vile wanawake, wazee na vijana.

Ameongezea kuwa, katika maboresho mengine yatakuwa ni katika kuendeleza viwanda kama serikali ya awamu ya tano inavyosisitiza ukuaji wa viwanda huku PPRA ikiangalia zaidi wataalamu wa manunuzi kutoka ndani pia wapo katika hatua za mwisho za kuhamia katika mfumo wa kieletroniki wa ununuzi wa zabuni.

PPRA ni mamlaka inayohusiana na udhibiti wa manunuzi ya Umma ambapo kupitia kwa Mtendaji Mkuu Dkt Shirima amewaondoa hofu wananchi kuwa waiamini taasisi yao kwani mambo mengi ya msingi yameshawekwa wazi na fedha za umma zinahitaji uwajibikaji.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka wa Udhibiti wa Manunuzi ya Umma  PPRA Dkt Laurent Shirima akizungumza na wanahabari wakati alipotembelea banda la Mamlaka wa Udhibiti wa Manunuzi ya Umma PPRA lililopo kwenye jengo la Wizara ya Fedha na Mipango na kuelezea namna wanavyojizatiti katika kuboresha ununuaji wa zabuni kwa serikali.
  Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka wa Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) Dkt Laurent Shirima akimuhudumia mwananchi aliyetembelea banda lao na katika maadhimisho ya 41 ya Monesho ya kimataifa ya Sabasaba leo Jijini Dar es salaam.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka wa Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) Dkt Laurent Shirima akipata maelezo kutoka kwa  mfanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa Taifa (PPF) wakati alipotembelea banda hilo lilipo katika Jengo la Wizara ya Fedha na Mipango  katika maadhimisho ya  41 ya Monesho ya kimataifa ya Sabasaba leo Jijini Dar es salaam.
  Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka wa Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) Dkt Laurent Shirima  akisaini katika kitabu cha wageni wa Wizara ya Fedha na Mipango alipotembelea banda hilo katika maadhimisho ya 41 ya Monesho ya kimataifa ya Sabasaba leo Jijini Dar es salaam.
Afisa Mahusiano Mwandamizi wa Mamlaka wa Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) Mcharo Mrutu akimuhudumia mwananchi aliyetembelea banda lao katika maadhimisho ya  41 ya Monesho ya kimataifa ya Sabasaba leo Jijini Dar es salaam
Mtaalamu wa Mifumo ya Habari wa Mamlaka wa Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) Mapinduzi Muhochi akitoa elimu ya manunuzi ya zabuni kwa mwananchi aliyejitembelea  banda lao  katika maadhimisho ya  41 ya Monesho ya kimataifa ya Sabasaba leo Jijini Dar es salaam. Picha Zote na Emannuel Massaka.

WAZIRI MWIJAGE:WATANZANIA PENDENI BIDHAA ZA NGOZI ZINAZOZALISHWA TANZANIA.

$
0
0
 .Waziri wa Viwanda , Biashara na Uwekezaji , Charles Mwijage  akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Biashara na Uhusiano wa Kiwanda cha Bora  Sylivery  Buyaga (wa pili kulia)  juu ya kiwanda  hicho kinavyofanya kazi.jijini Dar es Salaam.
 .Waziri wa Viwanda , Biashara na Uwekezaji , Charles Mwijage akionyesha ubora wa kiatu kinachotengenezwa na kiwanda cha Bora.jijini Dares Salaam.
Waziri wa Viwanda , Biashara na Uwekezaji , Charles Mwijage akitembelea kiwanda cha Cha Bora ambacho kilibinafsishwa  na sasa kimeanza uzalishaji wa bidhaa ya ngozi utaokafanya kozi kupata soko.jijini Dar es Salaam.
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live


Latest Images