Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live

HATIMAYE BULEMBO AKUBALI SHINIZO, ACHUKUA FOMU KIMYAKIMYA LEO MJINI DODOMA

$
0
0
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Alhaj Abdallah Bulembo akikabidhiwa fomu ya na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo mkoa wa Dodoma, Gama Juma, leo.

Hatimaye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania, Alhaj Abdallah Bulembo ametii shinikizo lililokuwa likitolewa na Wazee, viongozi na wanachama wa Jumuiya hiyo kumuomba agombea tena nafasi yake.

Hayo yametimia kufuatia Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Alhaji Bulembo kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea nafasi hiyo, katika Ofisi za Jumuiya ya Wazazi mkoa wa Dodoma leo mchana, huku akifanya tukio hilo kimyakimya tofauti na ilivyozoeleka ambapo baadhi ya wawania uongozi husindikizwa na wapambe na waandishi wa habari.

Licha ya kwenda kimyakimya, lakini taarifa zilizopatikana mjini hapa, zimesema kwamba alifika kwenye Ofisi za hizo za Wazazi mkoa wa Dodoma mda wa saa nane mchana akijiedesha kwa gari namba T888 DFB aina Toyota Land Cruser lenye vioo vya giza, na kukabidhiwa fomu hizo na Mwenyekiti wa Jumuia wa mkoa Gama Juma.

Mapema mwaka huu Alhaj Bulembo alitamka katika katika moja ya vikao rasmi vya Jumuiya ya Wazazi kwamba hatagombea tena nafasi yake ya Uenyekiti, kauli ambayo ilidumu kwa mda mrefu lakini baadaye Baadhi ya Wazee akiwemo Balozi Job Lusinde na baadhi ya viongozi na Wanachama wa Jumuia hiyo wakanza kutoa kauli za kumsihi abatilishe uamuzi wake huo wa kutogombea tena.

Maombi hayo yaliripotiwa kutolewa kwa nyakati na sehemu tofauti hapa nchini, wakiwemo Makatibu wa Jumuia hiyo kutoka mikoa ya Tanzania Bara na Zanzibar, ambao kwenye Semina moja iliyofanyika mjini hapa, mwezi uliopita, walimsihi Alhaj Bulembo kuchukua fomu huku wakisisitiza kwamba ikibidhi watamlipia fedha za fumu hizo.

Kufuatia mwaka huu wa 2017 kuwa mwaka wa Uchaguzi wa Viongozi ndani Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake ikiwemo Jumuiya hiyo ya Wazazu Tanzania na Jumuia za Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT), UVCCM kuanzia ngazi ya Tawi hadi Taifa CCM ilitangaza kuanza kutolewa fomu kwa wanaohitaji rudhaa za uongozi kwa ngazi hizo, kuanzia leo Julai 20217.

Kulingana na msimamo wa sasa wa CCM baada ya mabadiliko makubwa iliyofanya Dodoma, ambayo pamoja na kutaka kuwa na viongozi wenye nia za dhati na wenye kuguswa na shida za wananchi, bila shaka wanaowania uongozi katika kinyang’anyiro cha uchaguzi huo watalazimika kuwa wamejipima vya kutosha kulingana na sifa zilizotajwa.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA JUMATATU LEO JULY 3,2017

LAPF YAONGEZA WATEJA WA PENSHENI KATIKA MAONESHO YA SABASABA

$
0
0
 AfisaMatekelezo wa LAPF Agnes William akizungumza na mmoja wa wateja waliotembelea banda la mfuko huo wa hifadhi ya jamii katika maonesho ya kimataifa ya Sabsaba
 Mhasibu wa LAPF, Betty Mlewa akiwasikiliza wateja waliotembelea banda la mfuko huo wa hifadhi ya Jamii katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba jijini Dar esSalaam
 Afisa Mfumo Robert Daniel na Afisa Matekelezo ,John Mwita wakiwaelekeza wateja jinsi ya kujaza fomu ya kujiunga na mfuko wa Pensheni wa LAPF katika maonesho ya 41 ya Biashara  Sabasaba jijini Dar es Salaam
 Afisa Ugavi wa LAPF ,Charles Makyao akitoa maelezo kwa mteja alipotembelea banda la mfuko huo wa hifadhi ya Jamii katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba jijini Dar esSalaam
 Wateja waliotembelea banda la mfuko huo wa  Pensheni wa LAPF   katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba jijini Dar esSalaam wakipatiwa huduma
 Wateja waliotembelea banda la mfuko huo wa  Pensheni wa LAPF   katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba jijini Dar esSalaam wakipatiwa huduma

MAONESHO YA SABASABA 2017: WENGI WAJIUNGA NA PSPF KUPITIA MPANGO WA UCHANGIAJI WA HIARI PSS

$
0
0
 Meneja wa mpango wa uchangiaji wa Hiari, (PSS), wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi. Mwanjaa Sembe, (kulia), akimkabidhi kadi ya uanachama wa Mfuko huo kupitia mpango wa uchangiaji wa hiari, Mwanafunzi wa chuo cha Uhasibu (TIA), Bi.Demetriz Bayona, baada ya kujiunga na Mfuko huo leo Julai 2, 2017. 

Wananchi wengi waliotembelea banda la Mfuko huo leo, wamejiunga na mpango huo baada ya kupatiwa elimu na faida ambazo mwanachama anapata endapo atajiunga na mpango wa uchangiaji wa hiari ambapo kujiunga hakuna masharti isipokuwa kwa mtu yeyote mwenye kazi ya kumuingizia kipato na atatakiwa kuchangia au kuweka akiba ya kima cha chini cha shilingi elfu 10 kila mwezi. 

Miongoni mwa faifa ambazo mwanachama aliyejiunga na mpango huo ni pamoja na kujipatia bima ya afya, itakayomuwezesha kupata matibabu yeye mwanachama na wategemezi wake watatu. Lakini pia kujipatia mafao mablimbali yakiwemo fao la elimu, lakini pia mkopo wa nyumba na viwanja kutegemea na akiba ambayo mwanachama amejiwekea.
 Wanachama wapya wa PSPF wakijaza fomu za kujiunga na mpango wa PSS
 Bi Amina Mtoo akijaza fomu za kujiunga na uanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF kupitia mpango wa uchangiaji wa hiari, (PSS), leo Julai 2, 2017
 Mwanachuo wa chuo cha Uhasibu jijini Dar es Salaam, Bi.Demetria Bayona, akisikiliza kwa makini faida za kujiunga na PSPF kupitia  mpango wa PSS kutoka kwa afisa wa Mfuko huo. Baada ya kuelewa faida zake, Mwanachuo huyo hatimaye alijiunga na kupatiwa kadi yake ya uanachama ndani ya dakika 20.
 Menenja wa Mpango wa uchangiaji wa hiari, (PSS), wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bi. Mwanjaa Semba, (kulia), akitoa somo kwa mwananchi aliyetembelea banda la Mfuko huo kwenye maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam leo Julai 2, 2017
 Meneja Usimamizi wa na utawala wa mifumo ya TEHAMA, wa  Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bw. Bernard Ntelya, (kushoto), akimpatia maelezo mwananchi huyu aliyetembelea banda la PSPF Julai 2, 2017
 Afisa kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii, (SSRA), (kulia), akifuatilia jinsi maafisa wa PSPF wanavyotoa huduma kwa wanachama na wananchi wanaotembela banda la Mfuko huo. SSRA imeweka maafisa wake kila banda la linalotoa huduma ya hifadhi ya Jamii ili kusikiliza malalamiko ya wanachama husika wa Mfuko hiyo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw. William Erio, (kushoto), akikaribishwa na Afisa Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bi. Coletha Mnyamani alipotembelea banda hilo leo Julai 2, 2017.
 Afisa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bw. Isack Kimaro, (kulia), akimuhudumia mwananchi huyu aliyefika kupata huduma kwenye banda la Mfuko huo leo Julai 2, 2017.
 Afisa wa PSPF, (kushoto), akimuhudumia mwananchi huyu aliyefika kupata huduma za Mfuko huo
 Bw. Kimaro (kulia), akimsaidia kutambua michango yake mwanachama huyu aliyefika kwenye banda la PSPF
 Afisa uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF anayeshughulikia masuala ya uchangiaji wa hiari (PSS), Bi. Asmahan H. Haji, akiwajibika ipasavyo kwenye dawati lake
 Bi Asmahan (kulia), akimkabidhi kadi ya uanachama wa PSPF kupitia mpango wa PSS, Bi.Amina Mtoo, ambaye alisindikizwa na mchumba wake, Bw. Ayoub Issa, leo Julai 2, 2017
 Afisa Uhusiano wa PSPF, Bi. Coletha Mnyamani, (kulia), akimkabidhi kadi ya uanachama wa PSPF, Bi. Gloria P. Nyange, akiwa na mwanae wa miaka minne Winprecious Noel baada ya kujiunga na PSS.
 Bi Mnyamani akimkabidhi kadi na nyaraka mbalimbali zinazoelezea jinsi mwanachama huyu mpya Bw.Kamaga Salim Kilolo, aliyejiunga na mpango wa uchagiaji wa hiari PSS.
 Mwananchi akijaza fomu chini ya usaidizi wa Afisa uendeshaji msaidizi wa PSPF
 Bi Asmahan H. Haji, (kulia), akimkabidhi kadi ya uanachama wa PSPF, Bi.Sabah A. Dossa, baada ya kujiunga na mpango wa PSS.
 Kabla ya kujiunga na mpango wa PSS, Bi. Amina Mtoo, (wakwanza kushoto) na mchumba wake, Bw. Ayoub Issa, walipata fursa ya kupewa elimu ya kina juu ya kujiunga na mpango huo na faida ambazo mwanachama atapata ikiwemo bima ya afya ambayo itawahusu wawili hao na wategemezi wao wawili
Bi. Mnyamani akimuhudumia mstaafu

NIDA YAIBUKA MSHINDI WA KWANZA KATIKA KUNDI LA BANDA BORA KWA WIZARA NA TAASISI ZA SERIKALI

$
0
0
 Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NIDA ndugu Alphonce Malibiche akipokea tuzo toka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr. John Pombe Joseph Magufuli wakati wa sherehe za ufunguzi rasmi wa maonyesho ya 41 ya Kimataifa ya Sabasaba yaliyofanyika hivi karibuni. NIDA ilikuwa mshindi wa kwanza katika kundi la banda bora kwa Wizara na Taasisi za Serikali.
 Wananchi wakijaza fomu za maombi ya Vitambulisho vya Taifa na huduma kwenye Banda la NIDA wakati wa maonyesho ya 41 ya Kimataifa ya Sabasaba. 
 Wananchi wakipata huduma kwenye banda la NIDA, ambapo huduma ya Usajili na Utambuzi inatolewa, kuchukua alama za kibaiolijia pamoja na utoaji Vitambulisho kwa wale watakaokidhi vigezo. 
 Baadhi ya Watumishi wa NIDA walioshiriki kufanikisha Maonyesho hayo wakiwa na nyuso za furaha baada ya kupokea Tuzo ya ushindi. Kutoka kulia ni Edna Wanna, akifuatiwa na Agnes Gerrald, Raymondn Sengate na Sarah Mashalla.
 Katikati ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na mratibu wa Banda la Maonyesho la NIDA akiwa ameshikiliwa Tuzo ya Ushindi pamoja na Ndugu Alphonce Malibiche Kaimu Mkuu wa Idara ya Uzalishaji Vitambulisho (kushoto) na kulia ni Ndugu Jamal Kaoneka wa Idara ya Uhamiaji wadau wakuu wa NIDA katika kufanikisha Usajili wa Vitambulisho.
Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi mtendaji wa TRL ndugu Masanja Kadogosa akiwa kwenye picha ya pamoja na maafisa wa NIDA baada ya kutembelea Banda la NIDA na kuwapongeza kwa ushindi wa kishindo. Wengine katika picha kushoto ni ndugu Gideon Ndalu Mkurugenzi wa Mifumo ya Tehama NIDA na katikati ni Ndugu Alphonce Malibiche Kaimu Mkuu wa Idara ya Uzalishaji Vitambulisho.

BRITISH COUNCIL YAANZA KUWAHUDUMIA WANAOTAKA KUJIFUNZA KINGEREZA KATIKA VIWANJA VYA SABASABA

$
0
0
 Meneja Biashara wa kituo cha kijufunza Kingereza cha British Council ,Amata Bosco akizungumza na mmoja wa vijana waliofika kutika kujiunga na programu za British Council hili waweze kuongeza kingereza kwa ufasaha
 Ofisa Huduma kwa wateja ,Leonia Kazimoto  akizungumza wateja waliotembelea banda la British Council katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam  ambapo wanatoa huduma ya mafunzo ya kingereza
 Sehemu ya wadau wa British Council wakiwa wanajisomea ndani ya banda la Tasisi hiyo lililopo katika Viwanja vya Sabasaba


ACCESS BANK YAWA KIVUTIO CHA WAJASILIMALI NA WAFANYABIASHARA KATIKA MAONYESHO YA SABASABA

$
0
0
 Meneja Masoko wa Benki ya Access Bank ,Sijaona Simon akizungumza na Mmoja wa Wateja waliotembelea Banda la benki hiyo hili kuweza kujipatia huduma mbalimbali zinazotolewa ikiwemo mikopo na akaunti ya malengo Maalum

 Afisa Mikopo wa Access Bank , Marggoreth Riziki  akizungumza na mmoja  wateja juu ya huduma zinazotolewa na benki hiyo ikiwemo mikopo kwa wajasiliamali wadogo
 Afisa Mikopo wa Access Bank , Godbless Exaud  akizungumza na mmoja  wateja juu ya huduma zinazotolewa na benki hiyo ikiwemo mikopo kwa wajasiliamali wadogo
 Afisa Mikopo wa Access Bank ,  Isaak Malaba akikabidhi zawadi ya mfuko wa Acces Bank kwa mmoja wa wateja waliotembelea banda lao
 Afisa Mikopo wa Access Bank , Marggoreth Riziki na Godbless Exaud wakiwahudumia wateja ndani ya Sabsaba
 Afisa Mikopo wa Access Bank , Magdalena Kijuu akikabidhi Zawadi ya T-Shirt kwa mteja aliyefungua Akaunti katika banda lao la Maonyesho  ya Sabasaba
Afisa Mikopo wa Access Bank , Alex akitoa huduma mteja
 Sehemu ya Wateja waliofika katika Banda hilo
wafanyakazi wa Accs Bank wakiwa katika picha ya pamoja ndani ya banda la Maonyesho Sabasaba

MAONESHO YA SABASABA 2017;MAMLAKA YA UDHIBITI WA UNUNUZI KATIKA SEKTA YA UMMA (PPRA), YATOA ELIMU

$
0
0
Meneja Usimamizi na Utawala waMifumo ya TEHAMA, wa Mamlaka ya Udhibitiwa Ununuzi katika Sekta ya Umma (PPRA), Bw.Bernard Ntelya, (kulia), akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensehni wa PPF, Bw. William Erio, alipotembeela banda la Mamlaka hiyo Julai 2, 2017.


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
MAMLAKA ya Udhibitiwa Ununuzi katika Sekta ya Umma, (PPRA), kama zilivyo taasisi nyingine za serikali, imeweka banda lake kwenye jingo la Wizara ya Fedha na Mipango, wakatihuuwa maonesho ya 41 ya biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Viongozi na maafisa wa juu wa serikali wamepata fursa ya kutembelea banda hilo ili kujua huduma wanazotoa kwenye banda hilo, ambapo maafisa wa PPRA, wamekuwa wakitoa elimu na kugawa vipeperushi vyenye maeelzo mbalimbali ya kazi za Mamlaka hiyo, lakini na taarifa zinazoeleza sheria ya manunuzi ya umma na umuhimu wake.
Mamlaka hiyo imeanzishwa kwa sheria ya manunuzi ya Umma CAP 410 kama ilivyobadilishwa na Sheria ya Manunuzi ya Umma ya namba 7 ya mwaka 2011 ambayo inatoa Mamlaka ya kusimamia manunuzi ya umma kwa taasisi zote za Umma (Serikali), upande wa Tanzania Bara.
Kwa mujibu wa maafisa wa PPRA walioko kwenye banda hilo, wanasema, malengo makuu ya PPRA ni kuhakikisha manunuzi yote kwenye taasisi za umma, yanafanyika kwa usawa katika shindani, uwazi, bila unyanyasaji ili mwisho wa siku watoa huduma watoe huduma inayolingana na thamani ya fedha wanazolipwa kwa maendeleo ya taifa, (Value for Money).
Aidha wamesema, PPRA inao wajib u wa kuweka viwango katika mfumo wa manunuzi ya umma katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (upande wa Tanzanai Bara).
Afisa Mwandamizi wa PPRA, Bw. Mcharo Mrutu, (kulia), akimpatia vipeperushi vyenye taarifa mbalimbali za PPRA, Mkurugenzi Mkuu wa PPF, Bw. William Erio
Bw. Mrutu, (kulia), akizungumza na Mwananchi huyu aliyetembelea banda la Mamlaka hiyo
Bw. Ntelya(kulia), akifafanua jambo kwa mwananchi huyu aliyefika kujua shughuli za PPRA

PBZ YAWAKARIBISHA WADAU KUFUNGUA AKAUNTI KATIKA BANDA LAKE LA MAONESHO LA SABASABA

$
0
0
 Afisa Teknohama wa Islamic Benki ya PBZ ,Rahma Ali akizungumza na mmoja wateja waliofika katika banda lao la Maonyesho lililopo katika Viwanja vya Maonyesho ya Sabasaba  ambapo benki hiyo inawezesha kufungua akaunti ya Islamic benki na kuwezesha kupata mkopo usiokuwa na riba.
 Afisa Mahusiano wa PBZ -Bank LTD ,Aisha  Ali Mohd akizungumza na mmoja wa wadau waliofika katika banda la PBZ kupata maelekezo namna ya kufungua Akaunti kwenye benki hiyo


 Afisa  Masoko  PBZ Bank, Anas  Rashid Ramadhani akizungumza na wateja juu ya huduma za mikopo na ufungaji wa akaunti katika benki hiyo pamoja na ununuzi wa Viwanja kwa njia ya mkopo ambao utalipwa ndani ya miaka 10 wakati wa Maonyesho ya Sabasaba
 Wafanyakazi wa PBZ ,Hamyer Said na Biubwe Vuai wakimuelekeza mteja aliyefika katika banda hilo faida za Islamic Bank
 Salehe Abdalah akizungumza na mmoja wa wateja waliofika katika banda la Benki ya watu wa Zanzibar PBZ kutaka kufungua akaunti wkati wa Maonesho ya Sabasaba


Mwajuma Njaritu wa PBZ Islamic Bank akizungumza na mteja faida za huduma hiyo kwa waislamu

MAONESHO YA SABASABA 2017; PPF WAJIZOLEA SIFA YA KUTOA HUDUMA BORA KWA WANACHAMA NA WANANCHI WANAOTEMBELEA BANDA HILO

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw. William Erio, (mwenye suti), akiungana na wafanyakazi wenzake kuhudumia wananchi wakati wa maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa uya Dar es Salaam leo Julai 2, 2017. Wananchi wengi waliotembelea banda hilo wamefurahishwa na huduma zitolewazo na wafanyakazi wake kwa kwa jinsi wanavyosikiliza na kutoa huduma kwa wanachama na wananchi wengine. miongoni mwa maswali mengi yaliyoulizwa mara kwa mara ni kuhusu mpango wa uchangiaji wa hiari ujulikanao kama "Wote Scheme), unaotoa fursa kwa wajasiriamali wadogo kama mama lishe madereva wa bodaboda, wamachinga na mtu yeyote anayefanya kazi halali ya kumuingizia kipato anavyoweza kujiunga na mpango huo na hatimaye kupata faida mbalimbali ikiwemo bima ya afya na mikopo kwa wajasiriamali wadogo,
 Wananchi wakipatiwa maelezo kuhusu shughuli na huduma zitolewazo na PPF.
 Meneja wa elimu kwa wanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw. Kwame Temu, (kushoto), akitoa maelezo kwa mwananchi huyu aliyetembelea banda la Mfuko huo lililoko jengo la Wizara ya Fedha na Mipango kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere kuinakofanyika maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam leo Julai 2, 2017
  Wananchi wakipatiwa maelezo kuhusu shughuli na huduma zitolewazo na PPF.
  Wananchi wakipatiwa maelezo kuhusu shughuli na huduma zitolewazo na PPF.
 Wafanyakazi wa PPF, wakiwa makini katika kuwahudumia wananchi waliofika banda la Mfuko huo



 Mkurugenzi Mkuu wa PPF, Bw. William Erio, (kushoto), akizungumza jambo, wakati alipokutana na muigizaji mkongwe hapa nchini, Mzee Jangala, (wapili kushoto), wakati akitembelea bustani daraza ya Jeshi la Magereza, kwenye maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam, leo Julai 2, 2017. Wengine pichani kutoka kulia ni Bi. Yunge Saganda wa Jeshi la Magereza, Bi. Lulu Mengele, Meneja Uhusiano wa PPF na Bi Jannet Ezekiel Afisa Uhusiani Mwandamizi wa Mfuko huo
Mama Anna Mkapa, (kushoto),  ambaye ni  Mwenyekiti wa Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote, (EOTF), na Mke wa Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, akizungumza jambo na Mkurugenzi Mkuu wa PPF, Bw. William Erio, (wapili kushoto), Mama Mwantumu Mahiza, wakati alipotembelea banda la EOTF linalowakusanya wajasiriamali mbalimbali kuitoka nchini kote leo Julai 2, 2017
 Mjasiriamali kutoka mkoani Kigoma, Bi.Dporothy Timoth Takwe, (kushoto), akitoa maelezo ya ladha nzuri ya dagaa wa ziwa Tanganyika, wakati mama Mkapa, Mkurugenzi Mkuu wa PPF na mmoja wa viongozi wa televisehni ya Agape, (kulia), wakati walipotembelea banda la mjasiriamali huyo lililoko jengo la EOTF
 Mama Mkapa, Mkurugenzi Mkuu Erio, wakitazama bidhaa zilizofungwa vizuri na wajasiriamali wa Tanzania
Bw. Erio akisaini kitabu cha wageni kwenye banda la Magereza

MAONESHO YA SABASABA 2017: WENGI WAJIUNGA NA PSPF KUPITIA MPANGO WA UCHANGIAJI WA HIARI PSS

$
0
0
 Meneja wa mpango wa uchangiaji wa Hiari, (PSS), wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi. Mwanjaa Sembe, (kulia), akimkabidhi kadi ya uanachama wa Mfuko huo kupitia mpango wa uchangiaji wa hiari, Mwanafunzi wa chuo cha Uhasibu (TIA), Bi.Demetriz Bayona, baada ya kujiunga na Mfuko huo leo Julai 2, 2017. Wananchi wengi waliotembelea banda la Mfuko huo leo, wamejiunga na mpango huo baada ya kupatiwa elimu na faida ambazo mwanachama anapata endapo atajiunga na mpango wa uchangiaji wa hiari ambapo kujiunga hakuna masharti isipokuwa kwa mtu yeyote mwenye kazi ya kumuingizia kipato na atatakiwa kuchangia au kuweka akiba ya kima cha chini cha shilingi elfu 10 kila mwezi. Miongoni mwa faifa ambazo mwanachama aliyejiunga na mpango huo ni pamoja na kujipatia bima ya afya, itakayomuwezesha kupata matibabu yeye mwanachama na wategemezi wake watatu. Lakini pia kujipatia mafao mablimbali yakiwemo fao la elimu, lakini pia mkopo wa nyumba na viwanja kutegemea na akiba ambayo mwanachama amejiwekea.
 Wanachama wapya wa PSPF wakijaza fomu za kujiunga na mpango wa PSS
 Bi Amina Mtoo akijaza fomu za kujiunga na uanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF kupitia mpango wa uchangiaji wa hiari, (PSS), leo Julai 2, 2017
 Mwanachuo wa chuo cha Uhasibu jijini Dar es Salaam, Bi.Demetria Bayona, akisikiliza kwa makini faida za kujiunga na PSPF kupitia  mpango wa PSS kutoka kwa afisa wa Mfuko huo. Baada ya kuelewa faida zake, Mwanachuo huyo hatimaye alijiunga na kupatiwa kadi yake ya uanachama ndani ya dakika 20.
 Menenja wa Mpango wa uchangiaji wa hiari, (PSS), wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bi. Mwanjaa Semba, (kulia), akitoa somo kwa mwananchi aliyetembelea banda la Mfuko huo kwenye maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam leo Julai 2, 2017
 Meneja Usimamizi wa na utawala wa mifumo ya TEHAMA, wa  Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bw. Bernard Ntelya, (kushoto), akimpatia maelezo mwananchi huyu aliyetembelea banda la PSPF Julai 2, 2017
 Afisa kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii, (SSRA), (kulia), akifuatilia jinsi maafisa wa PSPF wanavyotoa huduma kwa wanachama na wananchi wanaotembela banda la Mfuko huo. SSRA imeweka maafisa wake kila banda la linalotoa huduma ya hifadhi ya Jamii ili kusikiliza malalamiko ya wanachama husika wa Mfuko hiyo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw. William Erio, (kushoto), akikaribishwa na Afisa Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bi. Coletha Mnyamani alipotembelea banda hilo leo Julai 2, 2017.
 Afisa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bw. Isack Kimaro, (kulia), akimuhudumia mwananchi huyu aliyefika kupata huduma kwenye banda la Mfuko huo leo Julai 2, 2017.
 Afisa wa PSPF, (kushoto), akimuhudumia mwananchi huyu aliyefika kupata huduma za Mfuko huo
 Bw. Kimaro (kulia), akimsaidia kutambua michango yake mwanachama huyu aliyefika kwenye banda la PSPF
 Afisa uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF anayeshughulikia masuala ya uchangiaji wa hiari (PSS), Bi. Asmahan H. Haji, akiwajibika ipasavyo kwenye dawati lake
 Bi Asmahan (kulia), akimkabidhi kadi ya uanachama wa PSPF kupitia mpango wa PSS, Bi.Amina Mtoo, ambaye alisindikizwa na mchumba wake, Bw. Ayoub Issa, leo Julai 2, 2017
 Afisa Uhusiano wa PSPF, Bi. Coletha Mnyamani, (kulia), akimkabidhi kadi ya uanachama wa PSPF, Bi. Gloria P. Nyange, akiwa na mwanae wa miaka minne Winprecious Noel baada ya kujiunga na PSS.
 Bi Mnyamani akimkabidhi kadi na nyaraka mbalimbali zinazoelezea jinsi mwanachama huyu mpya Bw.Kamaga Salim Kilolo, aliyejiunga na mpango wa uchagiaji wa hiari PSS.
 Mwananchi akijaza fomu chini ya usaidizi wa Afisa uendeshaji msaidizi wa PSPF
 Bi Asmahan H. Haji, (kulia), akimkabidhi kadi ya uanachama wa PSPF, Bi.Sabah A. Dossa, baada ya kujiunga na mpango wa PSS.
 Kabla ya kujiunga na mpango wa PSS, Bi. Amina Mtoo, (wakwanza kushoto) na mchumba wake, Bw. Ayoub Issa, walipata fursa ya kupewa elimu ya kina juu ya kujiunga na mpango huo na faida ambazo mwanachama atapata ikiwemo bima ya afya ambayo itawahusu wawili hao na wategemezi wao wawili
Bi. Mnyamani akimuhudumia mstaafu

IDRIS SULTAN LANDS MAJOR PART IN HOLLYWOOD/EAST AFRICAN PRODUCTION

$
0
0
New York City - July 3rd, 2017 — After weeks of a closely guarded audition process, 2014 Big Brother Africa-Hotshots winner Idris Sultan is cast in the upcoming American motion picture ‘Ballin...On the Other Side of the World,' to be directed by Harvey White, an American music director and editor turn filmmaker who’s worked with Chris Brown, Mariah Carey, Lady Gaga and Tamia to name a few. As a film editor, he’s worked on films such as 'Think Like A Man 2,''The Wedding Ringer,' and ‘King of The Dance Hall,’ with Whoopi Goldberg.

Written by Torino Von Jones, the story is about a young Kenyan boy (Kunjani), whose parents are victims of a violent crime. One day on the schoolyard, the thirteen year old is noticed by an American priest who sees him playing basketball and believes he has potential for greatness in the NBA. The two develop a friendship and a mentorship begins. (King) to be played by Sultan, is a very charming, but an extremely dangerous gangster who has another idea and wants Kunjani to join his gang of criminals and will stop at nothing to make it happen.

Last seen in the Tanzanian film ‘Kiumeni,’ which marked his feature film debut, Idris will be in Zanzibar next week for ZIFF (Zanzibar International Film Festival) to screen ‘Kiumeni’ during ZIFF’s Swahili Day on July 14th, with the producer and star Ernest Napoleon. Earlier this year, Mr. Napoleon made history when he was appointed president of the American production and distribution company D Street Media Group based in New York City, with offices in Berlin, Buenos Aires and Cape Town.

D Street’s CEO and executive producer Dexter Davis became aware of Idris from a private screening of ‘Kiumeni’ in the United States and thought he would be great for one of the leading roles. “Idris Sultan has what it takes to become an international star and our upcoming film ‘Ballin…On the Other Side of the World’ is a perfect fit. We’re considering Mr. Sultan for other movies as well, said Davis. The team is now looking forward to casting the American and Kenyan parts and can’t wait to do a major talent search for the actors in Kenya and other East African countries including Tanzania if necessary.”

The story takes place in New York City and a major city in Africa. The producers are deciding which African country the production will be filmed and looking at the beginning of the new year to start shooting. The film’s budget is set at $5 Million U.S. dollars and will also star two American A-list actors to play the priest and his best friend.
 
 ‘Ballin’ is another example of D Street’s commitment to put African talent and Africa on display in productions for the international market. The company is also behind the action-packed heist film ‘The Blue Mauritius,’ which is shooting in Cape Town and seeing South African star Pearl Thusi team up with Eric Dane (Grey’s Anatomy) and John Rhys-Davies (Lord of the Rings,) and many more international stars from around the world.

Vigogo IPTL, Rugemalira na Habinder Sethi, waongezewa mashtaka, Sita ya utakatishaji wa fedha

$
0
0
Na Karama Kenyunko.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewasomea upya mashtaka, washtakiwa Harbinder  Singh Sethi na James Burchard  Rugema rila kwa kuwaongezea mashtaka na kufanya idadi yao kufikia 12.

Mapema mwezi uliopita, washtakiwa hao walipandishwa kizimbani hapo baada ya kusomewa mashtaka sita kabla ya leo kuwa 12.

Katika mashtaka hayo ambayo ni ya uhujumu uchumi yapo pia matano ya utakatishaji wa fedha na kuisababishia Serikali hasara ya USD 22, 198,544.60 na Sh 309,461,300,158.27.

Mashtaka hayo ni, kula njama, kujihusisha na mtandao wa uhalifu , kughushi,  kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu kuisababishia Serikali Hasara na kutakatisha fedha.

Washtakiwa wamesomewa mshtaka yao mapya na wakili wa Serikali, Shedrack Kimaro mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.

Katika shtaka la kwanza inadaiwa, Rugemarila Mkurugenzi wa VIP na mmiliki mwenza wa zamani wa IPTL na Sethi ambaye ni Mwenyekiti Mtendaji wa PAP,    kati ya oktoba 18 ,2011 na Machi 19 , 2014 jiji Dar es Salaam walikula njama katika nchi za Afrika Kusini, Kenya na India ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Imedaiwa kuwa, Oktoba 18,2011na Machi 19,2014 washtakiwa hao wakishirikiana na watumishi wa umma walitekeleza mtandao huo wa uhalifu kwa lengo la kujipatia faida.

 Aidha katika shtaka la tatu linalomkabili  Sethi peke yake imedaiwa, Oktoba 10,2011 katika mtaa wa Ohio Ilala, akiwa na nia ya ulaghai alighushi fomu namba 14 a ya usajili wa makampuni  na kuonyesha yeye ni mtanzania anayeishi Kitalu namba 887 Mtaa wa Mrikau Masaki wakati akijua ni uongo.

Seth pia anadaiwa kutoa nyaraka ya kughushi ambayo ni fomu namba 14a ya usajili wa kampuni kwa ofisa msajiri wa kampuni,Seka Kasera kwa njia ya kuonesha kwamba yeye ni mtanzania na Mkazi wa Mtaa wa Mrikau.

Imeendelea kudaiwa kuwa, Novemba 28/29, 2011 na Januari 23,2014 katika Makao Makuu Benki ya Stanbic Kinondoni  na Benki ya Mkombozi tawi St Joseph kwa ulaghai washtakiwa hao walijipatia kutoka Benki Kuu ya (BOT), walijipatia USD 22,198,544.60 na Tsh 309, 461,300,158.27.   

Aidha wanadaiwa kuisababisha hasara, serikali ya kiasi hicho cha fedha.

Katika shtaka la saba, inadaiwa kati Novemba 29,2013 na January 23, 2014 maeneo tofauti Dar es Salaam kwa pamoja walitakatisha fedha kwa kuchukua fedha kutoka BOT USD 22,198,544.60 na Tsh 309,461,300.27 wakati wakijua fedha hizo zao la kujihusisha na genge la uhalifu.

Sethi peke yake anadaiwa pia kuwa Novemba 29,2013 katika tawi la kati la Benki ya Stanbic Tanzania wilaya ya Kinondoni,  alitakatisha fedha kwa kuchukua BOT USD 22,198,544.60 wakati akijua fedha hizo zimetokana na zao la kujihusisha na genge la uhalifu.

Aidha Sethi anadaiwa kutakatisha shilingi 309,461,300,158.27 kutoka BOT wakati akijua fedha hizo zimetokana na zao la kujihusisha na genge la uhalifu.

Katika shtaka la kumi, inadaiwa Januari 23, 2014 katika Benki ya Mkombozi tawi la St Joseph Cathedral, Rugemarila  alitakatisha, Sh 73,573, 500,000 kutoka kwa Seth wakati akijua fedha hizo zimetokana na zao la kujihusisha na genge la uhalifu.

Kwa upande wa shtaka la 11, Kimaro alidai kuwa Januari 23,2014 katika benki ya Mkombozi tawi la St Joseph Cathedral, Rugemarila alitakatisha fedha USD 22,000,000 kutoka kwa Seth wakati akijua fedha hizo ni zao la uhalifu.

Shtaka la 12, Seth anadaiwa kuwa Januari 28,2014 katika tawi la kati la Benki ya Stanbic wilaya ya Kinondoni alihamisha Rand (zar 1,305,800 kwenda kwenye akaunti namba 022655123 katika Standard bank Land Rover Sandton Johannesburg wakati akijua katika kipindi anahamisha fedha hizo zimetokana na zao la kujihusha na genge la uhalifu.

Washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu kitu chochote kwa sababu mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo na washtakiwa wamerudishwa rumande kwa kuwa mashtaka ya utakatishaji wa fedha hayana dhamana.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika na kesi hiyo itatajwa tena Julai 14,201.
 Mtuhumiwa James Burchard  Rugemarila akirejeshwa rumande 
Mtuhumiwa Harbinder  Singh Sethi wakirejeshwa rumande

Dkt Kalemani apiga marufuku uagizaji wa Nguzo, Nyaya na Transfoma kutoka nje ya nchi.

$
0
0

Na Teresia Mhagama, DSM 

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani amepiga marufuku uagizaji wa nguzo za umeme, nyaya na transfoma nje ya nchi na kuliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuhakikisha kuwa linanunua vifaa husika kutoka kwa wazalishaji wa ndani. 

Dkt. Kalemani aliyasema hayo wakati wa kikao chake na watendaji wa TANESCO, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na wazalishaji wa nguzo za umeme, transfoma na nyaya za umeme kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam. 

Alisema kuwa kikao hicho kililenga kukutanisha pande mbili yaani REA, TANESCO na wazalishaji wa vifaa vya umeme ili kufahamu mahitaji halisi ya vifaa vya umeme na kampuni zinazotengeneza vifaa hivyo, kuieleza Serikali kama wanao uwezo wa kuzalisha vifaa husika kwa kuzingatia ubora unaohitajika. 

“Tumedhamiria kusambaza umeme kwa kasi mijini na vijijini hivyo tunahitaji kufahamu uwezo wenu wa uzalishaji, tuelezeni hali halisi na kama kuna changamoto tuzijadili hapa na kufikia suluhisho kwani msimamo wa Serikali ni kutumia vifaa vya umeme vinavyozalishwa ndani ya nchi,” alisema Dkt. Kalemani. 

Aliongeza kuwa ingawa Serikali imeamua kutumia vifaa vya umeme vinavyozalishwa ndani ya nchi, kampuni husika zinapaswa kuzalisha vifaa vyenye ubora ili kuiondolea TANESCO gharama ya kubadilisha miundombinu ya umeme mara kwa mara na kwamba vifaa husika viuzwe kwa gharama itakayofaidisha pande zote mbili. 

Kwa upande wa mahitaji ya Transfoma, kampuni ya TANELEC, inayozalisha transfoma hizo ilieleza kuwa ina uwezo wa kutengeneza transfoma 10,000 zenye ukubwa tofauti kwa mwaka huku mahitaji ya REA na TANESCO yakiwa ni transfoma 8000 kwa mwaka hivyo watakidhi mahitaji ya hapa nchini. 

Kwa upande wa kampuni inayotengeneza nyaya za umeme ya East African Cables, ilieleza kuwa ina uwezo wa kutengeza nyaya za urefu wa kilomita 14,000 zenye uwezo wa msongo wa kati (medium voltage) kwa mwaka huku mahitaji ya TANESCO na REA yakiwa ni kilomita 10,100. 

Kampuni hiyo pia ilieleza kuwa ina uwezo wa kutengeneza nyaya za umeme za urefu wa kilomita 38,000 zenye uwezo wa msongo wa chini (low voltage) huku mahitaji ya REA na TANESCO yakiwa ni kilomita 31,000 kwa mwaka hivyo itaweza kukidhi mahitaji ya nyaya hizo nchini. 

Kuhusu uwezo wa wazalishaji wa nguzo nchini, kampuni zilizohudhuria kikao hicho zilieleza kuwa zina uwezo wa kuzalisha nguzo takribani 1,200,000 kwa mwaka huku mahitaji ya TANESCO na REA yakiwa ni nguzo 1,000,000 kwa mwaka. 

Dkt. Kalemani alitoa wito kwa kampuni hizo za Tanzania kuhakikisha kuwa wanatekeleza mahitaji ndani ya wakati na viwango vinavyokubalika ili kuweza kuhakikisha kuwa Sekta ndogo ya Umeme inaivusha nchi kwenda uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. 
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (wa kwanza kushoto) akiwa katika kikao na watendaji wa TANESCO, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na wazalishaji wa nguzo za umeme, transfoma na nyaya za umeme kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam.
 Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo ( wa kwanza kushoto) akiwa katika kikao na  watendaji wa TANESCO, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na wazalishaji wa nguzo za umeme, transfoma na nyaya za umeme kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni  Kaimu Kamishna wa Nishati, Mhandisi Innocent Luoga (wa pili kushoto),  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Dkt. Gideon Kaunda (wa tatu kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa  TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka.
Baadhi ya wazalishaji wa nguzo za umeme, transfoma na nyaya za umeme wakiwa katika kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam ambacho kiliongozwa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (hayupo pichani).

WATAFITI WAASWA KUTOFUNGIA TAFITI ZAO KABATINI

$
0
0
Na Ripota wa Globu ya Jamii,

SERIKALI imetoa wito kwa taasisi za elimu ya afya na mashirika mbalimbali yanayofanya tafiti za afya hapa nchini kuhakikisha tafiti hizo zinafika kwa wadau na wananchi kwa ujumla ili zilete tija zaidi kwa jamii badala ya kuzifungia kwenye ofisi zao.

Wito huo wa serikali ulitolewa mwisho wa wiki jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Elimu ya juu, Wizara ya Elimu, Sayansi, teknolojia na mafunzo ya Ufundi, Profesa Sylvia Temu alipomuwakilisha Katibu Mkuu Wizara hiyo, Dk. Leonard Akwilapo kwenye hafla ya kuhitimisha Mkutano wa tano wa kisayansi ulioandaliwa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS).

“Kwa sasa tunaelekea kwenye uchumi wa viwanda na miongoni mwa sekta muhimu ambazo pia zinatarajia wawekezaji ni pamoja na sekta ya afya hivyo basi muelekeo na mapendekezo ya tafiti za afya ndio zitakazoweza kuwasaidia wadau na serikali kufahamu aina ya ukwekezaji huo pamoja na maeneo gani yanafaa kulingana na mahitaji. Tafiti hizi zikifungiwa kwenye makabati tafsiri yake ni kwamba hata hii mikutano itakosa tija pia.’’ alisisitiza.

Aliongeza kuwa Serikali kwa kiasi kikubwa inajitahidi kutumia tafiti hizo katika kuandaa sera mbalimbali zinazohusiana na masuala ya afya huku akitoa pongezi kwa uongozi wa chuo hicho kwa kuendelea kuandaa wataalamu wanaoandaa tafiti hizo kwa weledi na ufanisi mkubwa.

“Zaidi umuhimu wa mkutano huu ni pale unapowakutanisha wataalamu wa afya tena katika ngazi tofauti wakiwemo wale waliobobea pamoja na wanafunzi na hivyo kuwa kama jukwaa kwa wao kuweza kubadilishana ujuzi. Jumla ya tafiti 160 tofauti za afya zimewasilishwa kupitia mkutano huu ambapo tafiti 70 kati ya hizo zilijadiliwa kwa kina na wataalamu hawa,’’ aliongeza.

Awali, akizungumza kwenye hafla hiyo Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa MUHAS, Prof. Appolinary Kamuhabwa alisema nyingi kati ya tafiti zilizowasilishwa kwenye mkutano huo wa siku mbili zilijikita katika vipaumbele vya taifa yakiwemo masuala ya HIV/AIDS, kifua kikuu, afya ya uzazi na mtoto, magonjwa yasiyo ya kuambukiza, ajali pamoja na magonjwa ya kitropiki yaliyosahaulika.

“Ndio maana tunaishukuru sana serikali ya Sweden kupitia Shirika la Sida ambao kwa kushirikiana na wadau wengine wamewezesha mkutano huu muhimu.,’’ alisema Prof Kamuhabwa huku akibainisha kuwa chuo hicho kimejipanga kuhakikisha tafiti hizo zinawafikia walengwa ikiwemo Serikali, mashirika na taasisi mbalimbali pamoja na wananchi kwa ujumla.
 Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano wa Tano wa Sayansi ya Afya waChuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS) Dk. Irene Kida akitoa majumuisho ya Mkutano huo mbele ya Mkurugenzi wa Elimu ya juu, Wizara ya Elimu, Sayansi, teknolojia na mafunzo ya Ufundi, Profesa Sylvia Temu (wa tatu kushoto meza kuu) wakati wa hafla fupi ya kuhitimisha mkutano huo uliofanyika kwa mwishoni mwa wiki  jijini Dar es Salaam. Wengine ni pamoja na walimu na uongozi wa chuo hicho akiwemo Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa MUHAS, Prof. Appolinary Kamuhabwa ( wa pili kushoto)
Mkurugenzi wa Elimu ya juu, Wizara ya Elimu, Sayansi, teknolojia na mafunzo ya Ufundi, Profesa Sylvia Temu (wa pili kushoto) akisikiliza maelezo kuhusiana na dawa za asili zinazoandaliwa na kitengo cha tiba asili katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS) alipotembelea maonyesho ya shughuli zinazofanywa na MUHAS mara baada ya kuhitimisha Mkutano wa tano wa kisayansi ulioandaliwa na chuo hicho jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. Wanaoshuhudia ni pamoja na viongozi wa Chuo hicho akiwemo  na Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa MUHAS, Prof. Appolinary Kamuhabwa (kushoto)


MAKAMU WA RAIS AHUDHURIA MKUTANO WA 29 wa UMOJA WA FRIKA MJINI ADDIS ABABA

$
0
0
Picha ya pamoja 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amemwakilisha Rais wa John Pombe Magufuli katika mkutano wa AU katika Makao makuu ya Umoja huo Addis Ababa- Ethiopia.Mkutano umefunguliwa hii Leo Jijini Addis Ababa- Ethiopia.
Mkutano wa AU katika Makao makuu ya Umoja huo Addis Ababa- Ethiopia uliofunguliwa leo hii eo Jijini Addis Ababa- Ethiopia ukiendelea

Mkutano wa 29 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) amefunguliwa rasmi Jijini Addis Ababa- Ethiopia ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli anawakilishwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan katika mkutano huo

Mkutano huo wa Wakuu wa Nchi na Serikali unaofanyika katika Makao Makuu ya Umoja wa Afrika Jijini Addis Ababa- Ethiopia na utajikita katika kujadili masuala mbalimbali yanayohusu umoja huo ikiwemo hali ya ulinzi na usalama katika Bara la Afrika hasa kwenye nchi za Sudan Kusini, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo- DRC na Libya.

Aidha, Viongozi hao watajadili hali ya usalama kwenye baadhi ya nchi ambazo ziliathiriwa na kundi la Boko Haram za Nigeria, Niger, Chad na Cameroon.

Wakuu hao wa Nchi na Serikali wa AU pia watajadili kwa kina kuhusu uanzishwaji wa eneo huru la kibiashara katika bara la Afrika kwa ajili ya kuliendeleza Bara hilo kwa ajili ya kukuza biashara baina ya nchi wanachama, uwekezaji, kuondoa vikwazo vya kibiashara pamoja na kupunguza utegemezi kwa masoko ya nje.

Mambo mengine yatakayojadiliwa na Viongozi hao ni bajeti ya Umoja huo, mpango mkuu kuhusu hatua za kivitendo za kuzuia mapigano katika Afrika kufikia mwaka 2020, maboresho katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na maboresho ya kitaasisi katika AU.

Kwa upande wa Tanzania, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan anaongoza ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo ambao unahudhuriwa pia na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt Augustine Mahiga na Waziri wa Kazi,Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Maudline Cyrus Castico pamoja na Watendaji wengine wa Serikali. Kauli Mbiu ya Mkutano wa mwaka huu ni Kuimarisha Mgawanyiko wa Idadi ya Watu Kupitia Uwekezaji katika Vijana. (Harnessing Demographic Divident Through Investments in the Youth)

UMEWAHI KUSOMA KITABU CHA NEEMA YA GESI NA MAFUTA TANZANIA? MAWAZO YA MWANDISHI NA HATUA ZA RAIS ZINAENDANA?

$
0
0
Albano Midelo ni Mwandishi wa kitabu cha Neema ya Mafuta na Gesi Tanzania, Azungumzia sababu za kuandika kitabu hicho ambacho kimeanza kuzaa matunda kutokana nay ale aliyoyaandika, Je amepata mafanikio gani katika uandishi wa kitabu hicho ? pia azungumzia vitabu vingine anavyoviandaa kuviingiza sokoni.

Benki ya NIC yakabidhi misaada mbalimbali katika kituo cha watu wenye mahitaji maalumu Mburahati

$
0
0
Wafanyakazi wa Benki ya NIC wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali ya kibinadamu katika kituo cha watu wenye mahitaji maalumu (jina limehifadhiwa) kilichopo Mburahati Jijini Dar Es Salaam.
 Mkurugenzi mkuu wa uendeshaji wa benki ya NIC, Bi Beatrice Kyanzi akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali ya kibinadamu katika kituo kimoja cha watu wenye mahitaji maalumu (jina linahifadhiwa) kilichopo Mburahati Jijini Dar Es Salaam
Picha ya Pamoja.Picha zote na Josephat Lukaza - Lukaza Blog

PBZ YAWAKARIBISHA WADAU KUFUNGUA AKAUNTI KATIKA BANDA LAKE LA MAONESHO LA SABASABA

$
0
0
 Afisa Teknohama wa Islamic Benki ya PBZ ,Rahma Ali akizungumza na mmoja wateja waliofika katika banda lao la Maonyesho lililopo katika Viwanja vya Maonyesho ya Sabasaba  ambapo benki hiyo inawezesha kufungua akaunti ya Islamic benki na kuwezesha kupata mkopo usiokuwa na riba.
 Afisa Mahusiano wa PBZ -Bank LTD ,Aisha  Ali Mohd akizungumza na mmoja wa wadau waliofika katika banda la PBZ kupata maelekezo namna ya kufungua Akaunti kwenye benki hiyo

 Afisa  Masoko  PBZ Bank, Anas  Rashid Ramadhani akizungumza na wateja juu ya huduma za mikopo na ufungaji wa akaunti katika benki hiyo pamoja na ununuzi wa Viwanja kwa njia ya mkopo ambao utalipwa ndani ya miaka 10 wakati wa Maonyesho ya Sabasaba
 Wafanyakazi wa PBZ ,Hamyer Said na Biubwe Vuai wakimuelekeza mteja aliyefika katika banda hilo faida za Islamic Bank
 Salehe Abdalah akizungumza na mmoja wa wateja waliofika katika banda la Benki ya watu wa Zanzibar PBZ kutaka kufungua akaunti wkati wa Maonesho ya Sabasaba


Mwajuma Njaritu wa PBZ Islamic Bank akizungumza na mteja faida za huduma hiyo kwa waislamu

RAIS AZUNGUMZA NA BODI YA (ZURA) ZANZIBAR

$
0
0

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) alipokuwa akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Ardhi,Maji,Nishati na Mazingira na Uongozi wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Maji na Nishati Zanzibar (ZURA) katika kikao cha siku moja kilichofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja.

Baadhi ya Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Maji na Nishati Zanzibar (ZURA) wakiwa katika mazungumzo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) katika ukumbi wa Ikulu MJini Unguja leo
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Maji na Nishati Zanzibar(ZURA) Ng,Haji Kali alipokuwa akitoa mchango na kuelezea maendeleo waliofikia katika Mamlaka hiyo walipokuwa na Kikao cha siku moja cha Uongozi wa Wizara ya Ardhi,Maji,Nishati na Mazingira na Uongozi wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Maji na Nishati Zanzibar (ZURA) ambapo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) akiwa Mwenyekiti wa Kikao hicho kilichofanyuika leo Ikulu Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.] 03/07/2017.
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live




Latest Images