Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

MAALIM SEIF AONGOZA HARAMBEE YA MADRASSA MUUMINI KIWALANI KUWEZESHA KUPATIKANA MILIONI SABA

$
0
0
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala , Omary Kumbilamoto akikabidhi mchango wake wa shilingi laki tatu katika harambee ya kuchangia Madrassa ya Muumini Islamiya iIliyopo kiwalani Dar es Salaam
Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita akikabidhi mchango wake kwa Katibu mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad kwa ajili ya Muumini islamiya.
Katibu mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad akiongoza harambee ya uchangiaji wa Madrasa Kiwalani Temeke jijini Dar es Salaam ambapo aliwezesha kupatika kwafedha zaidi ya Milioni 7 kwa ajili ya ununuzi wa kiwanja kipya cha Madrasa hiyo
Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita akizungumza wakati alipokuwakitoa ahadi yake ya Milioni moja kwa ajili ya Madrasa hiyo na aliweza kuwasilisha shilingi laki tano papo hapo na kuongeza ahadi ya bati 70 na mifuko 50 ya Saruji.
Diwani wa Kata Mianzini , Kassim Mshamu ambaye ndio mlezi wa Madrasa ya Muunin Islamiya akiwakaribisha wageni katika arambee yakuchangia madrasa
Sheikh Anuary Jongo akitoa Darasa juu ya waslamu na umuhimu wa kuchangia nyumba za ibada hili waweze kujenga ukaribu na Mungu hasa katika kumi hili la mwisho la mwezi mtukufu wa Ramadhani
Sehemu ya washiriki wa arambee hiyo wakipata futari iliyoandaliwa na Madrasa Muumin Islamiya
Katibu mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad akiteta na Mkurugenzi wa uchaguzi wa Chama Cha Wananchi CUF , Shaweji Mketo
Sehemu ya watoto wa Madrasa ya Muumini Islamiya wakipata futari mara baada ya kumalizika kwa harambee hiyo
Vijana wa Kiislamu wakitoa Nashid kwa ajili ya kuleta burudani kwa watu waliofika katika arambee hiyo
sehemu ya vijana wa Madrassa ya Muumin Islamiya wakinyosha mikono wakati wa utambulisho

Waziri wa Habari akutana na Wasanii wa Filamu na Waandishi wa Habari wa AFm Dodoma leo

$
0
0
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (Katikati) akiwa na waandishi wa habari wa A Fm Radio walipomtembelea Bungeni leo.
 Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe Dkt. Harrison Mwakyembe na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura wakiwa katika picha ya pamoja na wasanii wa Filamu, Ndg Nice Mtunze na Bi Lydia Mgaya walipowatembelea Bungeni leo.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe Dkt. Harrison Mwakyembe na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura wakiwa katika picha ya pamoja waandishi wa habari wa A Fm Radio walipomtembelea Bungeni leo.

TFF YATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI MSIBA WA ALLY YANGA

$
0
0
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amepokea kwa mshtuko na majonzi makubwa taarifa ya kifo cha shabiki maarufu wa Young Africans, Ally Mohammed anayefahamika zaidi kwa jina la Ally Yanga, kilichotokea jana Jumanne Juni 20, 2017 kwa ajali ya gari iliyotokea mkoani Dodoma.

Katika salamu za rambirambi kwa uongozi wa Young Africans, familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Ally Yanga ambako Rais Malinzi amewaasa kuwa na moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu kwao na kwa huzuni amewafariji akisema: “Sisi sote ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake tutarejea.”

“Hakika nimeshtushwa na taarifa za kifo cha Ally Yanga ambaye nimejulishwa kuwa kilitokea katika ajali ya gari huko Dodoma. Kifo hiki kimefanya wanafamilia wa mpira wa miguu kupoteza hazina ya hamasa popote pale uwanjani,” amesema Rais Malinzi.

“Binafsi nilimjua Ally Yanga katika masuala ya mpira wa miguu hasa akishabikia Young Africans na timu zote za taifa bila kujali kuwa ni Twiga Stars (Timu ya taifa ya wanawake), Taifa Stars, Serengeti Boys au ile Ngorongoro Heroes,” amesema Malinzi.

“Hivyo, nawatumia Young Africans salamu zangu za rambirambi nikiwapa pole kwa kuondokewa na mmoja wa mashabiki mwenye mvuto wa kipekee katika hamasa uwanjani, lakini pia alikuwa akisapoti timu za taifa,” amesema Rais Malinzi.

Aidha, Malinzi amesema: “Nawatumia pole wanachama wote wa Young Africans kwa kuondokewa na Shabiki mahiri Ally Yanga. Nawapa pole pia familia, ndugu, jamaa na marafiki ambao wamepoteza mhimili wao.

“Naungana nao katika msiba huu ambao pia ni msiba wetu sote wanafamilia ya mpira wa miguu. Naungana nao pia kumwomba Mwenyezi Mungu aiweke peponi roho ya Marehemu Ally Yanga. Amina.”

Inna Lillah wa Innalillah Rajaun.
……………………………………………………………………………………………….
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA

TAZAMA LIVE UZINDUZI WA MTAMBO WA MRADI WA MAJI WA RUVU JUU-PWANI

RC WA TANGA MH MARTINE SHIGELLA AFUNGU MAFUNZO YA KUMALIZA MAFUNZO YA AWALI

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Tanga Mh. Martine Shigella amewataka wahitimu wa mafunzo  ya awali ya kijeshi ya vijana operasheni Magufuli awamu ya pili wa kujitolea kutumia mafunzo waliyoyapata kwa kuwa wazalendo na kufanya kazi kwa niaba ya Taifa la Tanzania.

Hayo ameyazungumza wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya kumaliza mafunzo ya awali ya kijeshi ya vijana operesheni Magufuli awamu ya pili  wa kujitolea yaliyofanyika kwenye  Kituo namba  835KJ Mgambo JKT  kilichopo Kata ya Kabuku Wilayani Handeni.

Mkuu wa Mkoa amesema kuwa mafunzo ya ukakamavu wa mwili, uzalishaji mali, masuala mazima ya ulinzi na usalama na mafunzo ya kijeshi yatumike kwa uzalendo na kuwa mfano bora kwa jamii itanayowazunguka.

“ Nendeni mkawe mfano bora wa kuigwa  kwenye familia zenu na wazazi wenu wamekuja hapa kuwashuhudia, Sisi kama Serikali tunawaamini” alisema Shigella.

Ameongeza kuwa Mh. Rais alipoamua kurudisha mafunzo haya alitambua umuhimu mkubwa kwa Taifa letu sababu anajua mahitaji ya sasa na ya baadae wakati lengo kuu likiwa ni kuleta usawa na uzalendo kwa wasomi na wasio wasomi.

Amewataka wakatimize wajibu wao wa kuwa raia wema na kuwa walinzi wa Taifa kwa kupitia mafunzo ya ulinzi na usalama waliyoyapata huku akieleza kuwa Serikali inapambana na changamoto za kukabiliana na wahalifu  ambao hawataki kuwa kama wanadamu wengine.

 “ Nina imani kubwa na nyinyi kwamba mtaendelea kuwa waadilifu, waaminifu na kuendelea kupiga vita vitendo vya rushwa na ubadhilifu wa mali za umma na kwamba mtakuwa kimbilio la wanyonge na watu wenye matatizo makubwa” alisema Shigella.

Amewasisitiza kuendelea kujiendeleza kielimu ili waweze kupata ajira zinazolingana na hadhi zao. Waje wafanye kazi kwenye viwanda na kwamba rasilimali watu isitegemewe kutoka nje ya Tanga na Tanzania.

Ameeleza kuwa watakaofanya kazi kwenye viwanda watoke Tanzania kwa maana Tanga kuna viwanda vingi vinatarajiwa kuwepo na hivyo nguvu kazi itahitajika ya kutosha na angependezwa kuona miongoni mwao wanatoka JKT Mgambo.

Mwisho amewataka wahitimu kuongeza jitihada za uzalishaji mali hasa kwa kipindi hiki tunachoendea kua Tanzania ya Viwanda  kwani  ili Viwanda viwe na thamani,  wasomi na upatikanaji wa bidhaa zitakazohitajika viwandani hazinabudi kuwepo wakati wote na kwa wingi.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe alimshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kutenga muda wake kuweza kujumuika pamoja katika kufunga mafunzo hayo. Alieleza kuwa kuhusu suala la maji atalishughulikia kwa pamoja na Viongozi wa Halmashauri na kwamba atahakikisha maji yanafika Wilayani Handeni .

 Mafunzo ya awali ya Kijeshi kwa Vijana wa kujitolea Operesheni Magufuli yalifunguliwa tarehe 2Jan 2017 yakiwa na jumla ya Vijana 1083 kati yao wasichana 270 na wavulana 813 idadi ya vijana 5 hawakuweza kumaliza mafunzo  kutokana na kijana 1 kufariki, 3 kutorokaa wenyewe na 1 aliahirisha mafunzo hivyo kufanya idadi kubaki 1078.

Mafunzo waliyoyapata ni  uzalishaji mali, huduma za jamii , michezo, mafunzo ya kijeshi ya (Ulinzi na usalama wa Taifa na mafunzo ya kijeshi ya mbinu za kivita,elimu ya mapigano, matumizi ya silaha ndogondogo, usalama na utambuzi, uokoaji, huduma ya kwanza, usomaji ramani, sheria  za kijeshi) n.k.

Alda Sadango
Afisa Habari
Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh Martin Shigella akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo.
 Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh Godwin Gondwe akizungumza na wakati wa kufunga Mafunzo.
 Wahitimu wa Mafunzo wakiwa kwenye Gwaride

 Picha ya pamoja na Baadhi ya wahitimu.
 


Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh Martin Shigella akitoka kukagua gwaride

WAZIRI MKUU AMUAGIZA MKURUGENZI WA MISUNGWI AITISHE KIKAO KESHO SAA 4

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Bw. Eliud Mwaiteleke aitishe kikao na wananchi wa Kigongo na kutafuta ufumbuzi wa tatizo la eneo la kujenga soko. 

Ametoa agizo hilo leo jioni (Jumatano, Juni 21, 2017) wakati akizungumza na mamia ya wakazi na wajasiriamali wanaotumia kivuko cha feri cha Kigongo waliokuwa wakimsubiri avuke kwenda Busisi, wilayani Sengerema. 

"Mkurugenzi haya mambo ya mipango, mipango na kupanga hayaleti tija kwa wananchi. Hivi hamjui kuwa wananchi wanahitaji kuwa na soko katika eneo hili ili waweze kuuza mazao yao au samaki?"

"Ninakuagiza Mkurugenzi, kesho Alhamisi, saa 4 njoo na Afisa Biashara wako, Mwenyekiti wa kijiji na watu wako pamoja na Diwani wa hapa, itisheni kikao na muonyeshwe eneo la soko ili mliingize kwenye mipango yenu," alisema. 

Waziri Mkuu alisema Serikali ya awamu ya tano haitaki kusikia lugha za michakato wakati wananchi wanaendelea kuteseka.

Awali, Waziri Mkuu alimwita Mkurugenzi huyo ili aeleze amejipanga vipi kwenye Halmashauri yake kutatua tatizo la soko kwa wananchi wa Kigongo. 

Akitoa majibu mbele ya Waziri Mkuu, Bw. Mwaiteleke alisema hawajawahi kupata mpango kutoka kwenye kata hiyo na kwa hiyo akawasihi wananchi waibue mpango huo na kuuwasilisha kwenye Halmashauri ili wao waweze kutenga fedha za kujenga soko.

Mapema, Mwenyekiti wa Kijiji cha Kigongo, Bw. Sebastian Kisumo alimweleza Waziri Mkuu kwamba eneo hilo linakabiliwa na tatizo la soko pamoja na uhaba wa maji. 

Kuhusu maji, Waziri Mkuu alisema Serikali imetenga sh. bilioni 2.5 kwa ajili ya mradi wa maji wa kutoka Ziwa Victoria eneo la Itelele ambao utasambaza maji kwenda Misungi, Usagara hadi Kigongo Feri. 

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU, 
JUMATANO, JUNI 21, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza Juni  21, 2017 akiwa njiani kueleakea Chato ambako atakuwa na ziara ya siku mbili. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

OBASANJO PRAISES PRESIDENT MAGUFULI AND TELLS AFRICAN LEADERS TO EMULATE HIM

$
0
0
Nigeria retired President Olusegun Obasanjo has hailed President United Republic of Tanzania Dr. John Pombe Magufuli for being exemplary leader in Africa in spearheading the country’s economic development and safeguarding national interests.

Mr. Obasanjo, one of the prominent African leaders, made those remarks today when he paid a courtesy call to President Magufuli at the state house.
Mr. Obasanjo lauded President Magufuli’s efforts to attract investors from all corners of the world and praised his determination and desire to make sure the country is adequately benefiting from those investments. 
        
“President Magufuli’s efforts to make sure foreign investments benefiting the country is a crucial one and should be emulated by other African leaders because it is the only way that the continent can make economic headways” said Mr. Obasanjo.

According to the statement from state house signed by the Director of Presidential Communications, Mr. Gerson Msigwa quoted former president of Nigeria saying that he was impressed by the state of the economy Tanzania’s which he said it is on “the right track”.   
        
“I have visited various countries including Mozambique, Malawi and now I am in Tanzania. In all those countries, my discussions are focused on economic development and most importantly how our countries can sufficiently benefit from investments in various areas of the economy” Mr. Obasanjo noted.

He added that Africa can no longer afford to let foreign investors rip off the continent resources and left African with very little to share.

RAIS DKT. MAGUFULI AZINDUA RASMI MRADI WA MAJI WA RUVU JUU MLANDIZI MKOANI PWANI PIA AZINDUA VIWANDA VINGINE MKOANI HUMO

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Maji Mhandisi Gerson Lwenge, Balozi wa India hapa Nchini Sandeep Arya, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo pamoja na Viongozi wengine wa Mkoa wa Pwani na Serikali akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Mradi Mkubwa wa Maji wa Ruvu Juu Mlandizi Mkoani Pwani.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Waziri wa Maji Mhandisi Gerson Lwenge mara baada ya kuzindua rasmi Mradi wa huo wa Upanuzi wa mtambo wa kusafisha maji Ruvu juu Mlandizi Mkaoni Pwani.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Archard Mutalemwa  mara baada ya kuzindua mradi huo Mkubwa wa maji.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia hatua za usafishaji wa maji katika kituo cha kusafisha maji ya Ruvu juu Mlandizi Mkoani Pwani, kushoto ni Mtendaji mkuu wa DAWASCO Eng. Cyprian Luhemeja akitoa maelezo
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma pamoja na Balozi wa India hapa nchini Sandeep Arya mara baada uzinduzi wa mradi huo mkubwa wa kusafisha na kuzalisha Maji kwa miji ya Pwani na Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia ujumbe aliotumiwa na Waziri mkuu wa India Narendra Modi kupitia Luninga kabla ya kudua Mradi huo wa maji.
 Sehemu ya Mradi huo wa maji wa Ruvu juu Mlandizi Mkoani Pwani
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia Mfuko wa sandarusi pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Eng. Evarist Ndikilo kabla ya kuzindua kiwanda cha Global Packing kilichopo Kibaha mkoani Pwani.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifungua kiwanda cha kutengeneza  matrekta URSUS kilichopo Kibaha mkoani Pwani.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilijaribu Trekta mojawapo katika kiwanda cha kutengeneza  matrekta URSUS kilichopo Kibaha mkoani Pwani.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Waziri wa Viwanda na Biashara Charles Mwijage kabla ya kufungua kiwanda cha Nondo cha Kilua Steel Group kilichopo Mlandizi mkoani Pwani.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akipeperusha bendera kuashiria kuiruhusu treni ya TRL kusafirisha nondo kutoka kwenye kiwanda cha Nondo cha Kilua Steel Group kilichopo Mlandizi mkoani Pwani.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli   pamoja na viongozi wengine akifungua kiwanda hicho cha nondo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka jiwe la msingi kwenye sehemu ya kiwanda cha kutengeneza  matrekta URSUS kilichopo Kibaha mkoani Pwani.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia kabla ya kuzindua Mradi wa maji wa Ruvu juu Mlandizi mkoani Pwani.
PICHA NA IKULU

BENKI YA KCB TANZANIA YAFUTURU NA WATEJA WAKE MWANZA

$
0
0

Mkuu wa Masoko na Mawasiliano ya Umma wa Benki ya KCB Bi. Christine Manyenye akiwakaribisha wateja na wafanyakazi wa Benki ya KCB kwenye hafla ya futari Mwanza.
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya KCB, Bw. Cosmas Kimario akizungumza na wateja na wafanyakazi wa Benki ya KCB Mwanza kwenye hafla ya futari.
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya KCB, Bw. Cosmas Kimario (wapili kulia) akipata futari pamoja na wateja wa benki hiyo. Hafla hiyo ya futari iliandaliwa na benki ya KCB kwa ajili ya wateja wake Jijini Mwanza.
Baadhi ya wateja wa Benki ya KCB walio kwenye mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani Jijini Mwanza wakiwa kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo.
Baadhi ya wateja wa Benki ya KCB walio kwenye mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani Jijini Mwanza wakiwa kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo.
Baadhi ya wateja wa Benki ya KCB walio kwenye mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani Jijini Mwanza wakiwa kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo.
Mjumbe wa Bodi ya Kiislamu wa Benki ya KCB Sheikh Twaha Bane akizungumza na wateja na wafanyakazi wa Benki ya KCB kwenye hafla ya futari Mwanza.
Mkuu wa Huduma za Kiislamu wa Benki ya KCB Bw. Rashid Rashid akizungumza na wateja na wafanyakazi wa Benki ya KCB Mwanza kwenye hafla ya futari.
Meneja wa Benki ya KCB Tawi la Mwanza Bw, Joseph Njile akiwashukuru wateja na wafanyakazi wa Benki ya KCB kwa kuhudhuria hafla ya futari.

…………………………………………………………………………..

Benki ya KCB Tanzania imefuturisha wateja wake wa Mwanza katika hoteli ya JB Belmont. Hafla hiyo ilihudhuriwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Bw. Ahmed Msangi, wajumbe wa bodi ya huduma za kiislamu wa benki ya KCB, wafanyakazi na wateja wa benki hiyo.

Akizungumza wakati wa futari hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya KCB Cosmas Kimario alisema kuwa futari hiyo ipo ndani ya vipaumbele vya benki kuwekeza katika jamii na kuboresha uhusiano na wateja wake.

“Benki ya KCB Tanzania inadhamini uwajibikaji kwa jamii ambayo kwa kiwango kikubwa inalenga maeneo ya vipaumbele vya Elimu, Afya, Mazingira, Ujasiriamali na malengo yake hasa ni kujikita katika masuala ya ubinadamu”, Kimario alisema na kubainisha kwamba tangu ilipofunguliwa hapa Tanzania mwaka 1997, benki hiyo imekuwa ikijikita katika kuisadia jamii.

“Mwezi huu mtukufu unaamrisha watu kujirudi, kuutambua na kuuheshimu uwepo wa Mungu. Pia unatukumbusha kufanya yale yampendezayo Mungu na ndio maana benki ya KCB tumeona umuhimu wa kukutana hapa jioni hii ili kufuturu pamoja” alisema Kimario.

Bw. Kimario alieleza kuwa, benki ya KCB inakitengo maalumu kwa ajili ya huduma za Kiislamu inayoitwa “Sahl Banking” na huduma hiyo hupatikana katika matawi

yote 14 ya benki hiyo. “Benki ya KCB ndio ya kwanza kuanzisha huduma zinazozingatia shari’ah hapa nchini na inazidi kuimarisha huduma hizo kwa kuzingatia muongozo husika. Huduma hizo bora ni akaunti za biashara kwa watu binafsi na taasisi mbalimbali, jamii (community account), akiba (savings account), watoto, hijja n.k.

Alimaliza kwa kuwataka wale ambao bado hawajajiunga na benki ya KCB kujiunga leo na kupata huduma za kibenki kwa haraka, usalama na bila usumbufu.

WAISLAMU TABORA WAMEOMBWA KUMUNGA MKONO RAIS JPM KATIKA VITA DHIDI WAHUJUMU RASIMALI ZA TAIFA.

$
0
0
Na Tiganya Vincent.

WAISLAMU Mkoani Tabora wametakiwa kuunga mkono juhudi zilizoanzishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli za kupambana kikundi la watu wachache ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakinufaika na rasilimali ya nchi hii na kuwaacha watu wengi wakiwa maskini licha ya utajiri waliojariwa na Mungu.

Kauli hiyo imetolewa jana mjini Tabora na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ibrahim Mavumbi wakati wa futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa huo Bw. Aggrey Mwanri.

Alisema kuwa Rais Magufuli haipaswi kuachiwa pekee vita aliyoanzisha , bali anatakiwa kuungwa mkono na watu wote wenye mapenzi mema na nchi hii kwani kiongozi huyo amesaidia kuwafumbua macho na kuona kuwa wameibiwa sana na walikuwa wakiendelea kuibiwa na kikundi cha watu wachache kwa maslahi yao binafsi na sio ya watu wengi.

Sheikh Mavumbi aliongeza kuwa Rais Magufuli ameonyesha mapenzi makubwa kwa nchi yake na wananchi wake na kukwerwa na umaskini wa wananchi wake uliosababishwa na tamaa ya watu wachache waliokuwa wakinufaika wakati nchi ikibaki na mashimo ambayo wakati mwingine yanaweza kusababisha vifo kwa watu kutumbukia ndani yake.

Alisisitiza kuwa sio vizuri kupuuza juhudi kubwa anaozifanya Rais Magufuli kwa kushirikiana na viongozi wenzake za kusimamia rasilimali za nchi na kutetea haki za wanyonge ambao walikuwa wakidhulumiwa na watu wachache  kwa maslahi yao binafisi

Sheikh Mavumbi aliongeza kuwa Rais Magufuli anataka kutupeleka ambapo kila raia wa nchini hii atakunufaika na utajiri wa nchi hii ambao wamejariwa na Mungu.

Alisema kuwa Waislamu wa Mkoa wa Tabora wanamueombea dua katika mapambano yake ya kuhakikisha kuwa rasimali ya hapa nchini zinawanufaisha wanyonge na zinaleta maendeleo kwa wananchi wengi na Tanzania kwa ujumla.

Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bw.Mwanri aliwashukuru Waislamu kwa nia yao njema ya kumuombea na kumuunga mkono Rais Magufuli na Serikali yake katika mapambano hayo ya ukumbozi wa kiuchumi kwa wanyonge.

Alisema kuwa vita hiyo ni kubwa ni vema  Watanzania wote bila kujali tofauti za dini, kabila , vyama wakashikamana na kumuunga mkono Rais Magufuli ili hatimaye matunda ya vita hivyo yaweze kuwanufaisha watu wengi.

Mkuu huyo Mkoa alisema kuwa Wakazi wa Mkoa wa Tabora wanamuunga mkono na wako nyuma yake katika mapambano hayo na hawako tayari kuona watu wachache wanabeza juhudi hizo ambazo zinalenga kuwakomboa wanyonge.

Naye Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Misheni ya Tabora Newton Maganga aliwaomba wakazi wa Tabora kuwa kitu kimoja katika kukabiliana na matatizo mbalimbali yanayokwamisha maendeleo bila kujali tofauti zao.

VIPIMO BINAFSI VYA VIRUSI VYA UKIMWI KUFANYIWA UTAFITI NCHI NNZIMA

AGPAHI YAENDELEA KUTOA HUDUMA ZA KISAIKOLOJIA KWA WATOTO NA VIJANA

$
0
0
Mkurugenzi wa Miradi kutoka shirika la Ariel Glaser Pediatric Aids Healthcare Initiative (AGPAHI) Dk. Safila Telatela akizungumza wakati wa kufungua Ariel Camp (Kambi ya Ariel) ya siku tano kuanzia June 19,2017 - June 23,2017 iliyokutanisha watoto na vijana 50 kutoka mikoa ya Shinyanga,Mwanza na Geita jijini Mwanza.Picha na Kadama Malunde-Malunde1 blog
Mratibu wa Ukimwi wa Mkoa wa Mwanza Dk. Pius Maselle akifungua kambi ya watoto na vijana 'Ariel Camp' katika hotel ya Lesa Garden jijini Mwanza.Wa kwanza kushoto ni Mratibu wa Miradi AGPAHI mkoa wa Shinyanga,Dk. Gastor Njau akifuatiwa na Mratibu wa Ukimwi mkoa wa Geita Dk. Joseph Odero. Wa kwanza kulia ni Mratibu wa Miradi AGPAHI mkoa wa Mwanza, Olympia Laswai akifuatiwa na Mkurugenzi wa Miradi AGPAHI, Dk. Safila Telatela. 
*****
Jumla ya watoto 8,615 kutoka  mikoa ya Tanga, Mara, Mwanza,Geita, Simiyu na Shinyanga wamepatiwa huduma za Virusi vya Ukimwi na Ukimwi ikiwemo kupatiwa dawa za kupunguza makali ya VVU (ARVs) katika kipindi cha kuanzia mwaka 2011 hadi mwezi Machi 2017.
Huduma hizo zimetolewa na shirika la Ariel Glaser Pediatric Aids Healthcare Initiative (AGPAHI) linalojihusisha na mapambano dhidi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) na Ukimwi kwa kushirikiana na Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto.
Takwimu hizo zimetolewa na Mkurugenzi wa Miradi kutoka AGPAHI,Dk. Safila Telatela wakati wa kufungua Kambi ya Ariel 'Ariel Camp' ya siku tano inayokutanisha watoto na vijana wenye umri kuanzia miaka 10 mpaka 17 kutoka mikoa ya Shinyanga,Geita na Mwanza inayofanyika katika Hotel ya Lesa Garden jijini Mwanza.
Dk. Telatela alisema watoto hao ni sawa na asilimia 5 kutoka jumla ya watu 189,806 waliopatiwa huduma na shirika hilo  katika kipindi hicho na shirika linaendelea na kazi ya kutoa matunzo na tiba za VVU katika vituo 553 katika mikoa hiyo sita.
 Alisema pia wanafanya kazi ya  kutokomeza maambukizi ya VVU kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto katika vituo 631.
Aidha Dk. Telatela alisema wamefanikiwa kuunda vikundi zaidi ya 65 vya watoto na vijana katika mikoa ya Shinyanga na Simiyu ambapo takribani watoto 2640 wamenufaika na vikundi hivyo.
“Kuanzia mwezi Oktoba 2016, shirika letu limeongeza wigo wa kutoa huduma kutoka mikoa miwili ya Shinyanga na Simiyu na sasa imekuwa  sita na tunafanya kazi ya kutoa matunzo na tiba za VVU katika vituo 553 kwenye mikoa hii sita”,alieleza Dk. Telatela.
“Shirika letu limekuwa likiandaa kambi kwa ajili ya watoto na vijana kwa lengo la kuwakutanisha ili kujifunza mambo mbalimbali kuhusu afya, stadi za maisha, kupata ushauri wa kisaikolojia kutokana na changamoto wanazokutana nazo na pia huduma za kitabibu kutoka kwa daktari wa watoto katika kipindi chote cha kambi na kuwafanya kuwa mabalozi wa huduma za watoto katika jamii zao”,aliongeza.
Naye Mgeni rasmi wakati wa ufunguzi wa kambi hiyo, Mratibu wa Ukimwi wa Mkoa wa Mwanza, Dk. Pius Maselle alitoa rai kwa mikoa mipya ya AGPAHI (Geita,Tanga,Mara na Mwanza) kufanya jitihada za ziada katika uundaji wa vikundi vya watoto na vijana ili idadi ya watoto watakaonufaika na huduma za kisaikolojia iwe kubwa.
Aidha Dk. Maselle alitoa shukrani kwa shirika la AGPAHI kwa jitihada mbalimbali linazofanya katika mapambano dhidi ya VVU na Ukimwi nchini kwa ufadhili wa Watu wa Marekani kupitia shirika  la Centres for Disease Control and Preventation (CDC),mfuko wa kusaidia Watoto wenye VVU Kwa hisani ya watu wa Uingereza (CIFF) na Shirika la Development Aid From People to People (ADPP - Mozambique).
HII HAPA HOTUBA FUPI YA UFUNGUZI WA KAMBI YA WATOTO NA VIJANA (ARIEL CAMP) 2017 ILIYOTOLEWA NA MKURUGENZI WA MIRADI AGPAHI,DR. SAFILA TELATELA

Ndugu,

·         Mgeni rasmi - Mratibu wa Ukimwi wa Mkoa wa Mwanza,

·         Mratibu wa Ukimwi wa Mkoa wa Geita,

·         Wafanyakazi wa AGPAHI,

·         Watumishi wa afya walioambatana na watoto (walezi wa watoto)

·         Watoto wa Kambi ya Ariel,

·         Waandishi wa Habari,

·         Mabibi na Mabwana.

Habarini za asubuhi!

Awali ya yoye, napenda kuchukua fursa hii kuwakaribisha wageni wote katika hafla hii fupi ya ufunguzi wa kambi yetu ya nane (8) tangu kuanzishwa kwa shirika la AGPAHI mwaka 2011. Pia napenda kutoa shukrani kwenu wote kwa kujumuika na sisi hapa siku hii ya leo, Asanteni sana!

Nichukue fursa hii kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa shirika la AGPAHI kuwashukuru wafanyakazi wenzangu wa AGPAHI na walezi wa watoto kutoka Geita, Shinyanga na Mwanza kwa kushiriki katika kuandaa kambi hii tangu hatua za awali za kuwachagua watoto na vijana huko vituoni kwao, kuwasafirisha na kuwafikisha hapa Lesa Garden – Mwanza. Hongereni sana na Mungu awabariki!

Ndugu mgeni rasmi, napenda kutoa shukrani kwa Watu wa Marekani kupitia shirika lao la CDC ambao ndio wahisani wa kambi hii.   Hata hivyo tuna wafadhili wetu wengine wa miradi kama vile Children Investment Fund Foundation (CIFF) and Development aid from People to People (ADPP - Mozambique). Tunawashukuru sana.

Ndugu mgeni rasmi,Shirika la AGPAHI ni shirika lisilo la kiserikali linaloendeshwa na watanzania na watanzania wenyewe ndio sisi hapa
Shirika letu lilianzishwa mwaka 2011 kutokana na dira ya serikali ya Tanzania na ile ya wafadhili  yaani serikali ya Marekani kutaka wazawa (serikali pamoja na mashirika yasiyo ya serikali) kuendesha miradi mbalimbali inayoshughulikia masuala ya VVU na UKIMWI na masuala ya afya ya mama na mtoto ili kuwa na miradi endelevu.

Kuanzia mwezi Oktoba 2016, shirika letu limeongeza wigo wa kutoa huduma kutoka mikoa 2 hadi sita ambayo ni Tanga, Mara, Mwanza, Geita, Simiyu na Shinyanga. Huduma zitolewazo ni pamoja na tiba na matunzo kwa watu wenye VVU, kuzuia maambukizi ya VVU toka kwa mama kwenda kwa mtoto, uchunguzi wa awali na tiba ya saratani ya shingo ya kizazi na kutoa huduma shirikishi za kifua kikuu na UKIMWI sehemu za migodini.

Takwimu

Ø  AGPAHI inafanya kazi ya kutoa matunzo na tiba za VVU katika vituo 553 kwenye mikoa sita (Tanga, Mara, Mwanza,Geita, Simiyu na Shinyanga).

Ø  Huduma ya kutokomeza maambukizi ya VVU kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto katika vituo 631.

Ø  Kutoa huduma ya uchukuaji wa sampuli ya damu kavu kwa watoto katika vituo 631.

Ø  Huduma shirikishi za kifua kikuu na Ukimwi katika maeneo manne (5) ya migodi (Mererani, Iyenze, Mwime, Kalole, Kakola na Mwazimba).

Ø  Hadi mwezi Machi 2017, jumla ya watu waliowahi kupata huduma za VVU/Ukimwi ikiwemo kupata dawa za kupunguza makali ya VVU (ARV) ni 189,806 kati yao watoto walikuwa 8615, hii sawa ni asilimia 5%.

Ø  AGPAHI pia inatoa huduma mseto za uzazi wa mpango katika vituo vya ushauri nasaha na upimaji wa hiari na tiba na matunzo vinavyowezeshwa na AGPAHI.

Kwa kutambua umuhimu wa watoto na vijana, Shirika la AGPAHI lilianzisha huduma za kisaikolojia kwa kupitia vikundi vya watoto tangu mwaka 2011 pindi lilipoanzishwa (ambapo Shirika lilikuwa linafanya kazi katika mikoa ya Shinyanga na Simiyu). Huduma hizo zilihusisha uundwaji wa vikundi vya watoto na vijana katika vituo vya kutolea huduma za afya (yaani CTC). 
Kwa sababu ya umuhimu wa vikundi hivi, AGPAHI imeshaanza juhudi za makusudi za kuanzisha vikundi kwenye mikoa minne (4) ambayo tumeanza kufanya kazi tangu Oktoba 2016 (Mwanza, Mara, Geita na Tanga). Azma yetu ni kuhakikisha tunawaunganisha watoto na vijana wengi kwenye huduma za kisaikolojia kwa kupitia vikundi.

Kutokana na uundwaji wa vikundi vya huduma za kisaikolojia kwa watoto na vijana, AGPAHI ilifanya juhudi za kuanzisha kambi za watoto ambazo hufanyika mara moja au mbili kwa mwaka. Kambi hii tunayoizindua leo ni kambi ya nane (8) kufanyika chini ya uratibu wa shirika la AGPAHI (kwa mwaka huu hii ni kambi ya pili kufanyika). Kambi nyingine za awali zimeshanyika katika mikoa ya Kilimanjaro, Kagera na Mwanza. Utaratibu huu wa kuwapeleka watoto na vijana kwenye kambi zilizopo maeneo tofauti ni mzuri kwani unasaidia kuwafundisha mambo mengi kuhusu nchi, historia na tamaduni bila kusahau masomo wanayopata wakiwa kambini.

Ndugu mgeni rasmi,

Kambi hii inahusisha watoto na vijana kutoka katika mikoa ya Geita, Shinyanga na Mwanza yenye jumla watoto 50 na watumishi wa afya (walezi wao) 11. Watoto pamoja na watumishi wa afya wametoka katika vituo mbalimbali kama walivyotambulishwa awali. Wana umri kati ya miaka 10 -17.

Washiriki wa kambi wakiwa hapa kambini hufundishwa kuhusu afya na makuzi, lishe, stadi za maisha, elimu sahihi kuhusu VVU na Ukimwi, ufuasi mzuri wa dawa pamoja na unyanyapaa na unaguzi. 
Pia hupata ushauri wa kisaikolojia kutokana na changamoto wanazokutana nazo na pia huduma za kitabibu kutoka kwa daktari wa watoto katika kipindi chote cha kambi. 
Vilevile, naomba kuchukua fursa hii, kuwasihi watoto na vijana kuzingatia elimu na kanuni za afya kama wanavyoelekezwa na wataalam wa afya na endeleeni kuwa wanachama wazuri katika vikundi vyenu na muwe mabalozi wa kuwahamasisha watoto na vijana wenzenu kujiunga na vikundi.

Mwisho ningependa kuwashukuru watumishi wa afya mliokuja na watoto kutoka Geita, Shinyanga na Mwanza. Nawasihi muendelee kuwajenga na kuwasimamia watoto ili wawe mabalozi wazuri kwa wengine, ili baadae tujivunie ushiriki wao katika kambi ya Ariel 2017. 
ASANTENI KWA KUNISIKILIZA!

KATIBU MKUU OFISI YA MAKAMU WA RAS AKUTANA NA WATUMISHI WA OFISI -KITUO CHA DAR ES SALAAM

$
0
0
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala Ofisi ya Makamu wa Rais, Samuel Mwashamba akimkaribisha Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais ili azungumze na Watumishi wa Ofisi ikiwa ni maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais  Profesa Faustin Kamuzora (katikati) akiongea wakati wa mkutano wake na Watumishi wa Ofisi yake walioko Dar Es Salaam, ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma.
Mmoja wa Watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais Bwana Aidan Mtuhi akichangia maoni yake wakati wa Mkutano huo.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais waliohudhuria Mkutano huo wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (hayupo pichani).

RAIS DKT MAGUFULI AWAANDALIA FUTARI WANANCHI WA MKOA WA PWANI

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 21 Juni, 2017 amefuturisha wananchi wa mkoa wa Pwani na kuwataka waumini wa dini ya Kiislam na madhehebu mengine kuendeleza umoja na mshikano uliopo kwa muda mrefu kwa lengo la kudumisha amani nchini.

Mhe. Rais Magufuli amesema anaungana na waumini wa dini ya Kiislamu nchini katika kumi la mwisho la Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa kuwaombea kumaliza kwa amani ibada ya Funga ya Ramadhani ikiwa ni kutekeleza nguzo ya nne kati ya nguzo tano ya dini ya kiislam.

Amesema kwa mujibu wa dini ya Kiislamu ibada ya Funga ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni muhimu kwani ni njia sahihi ya kujirekebisha kuachana na matendo maovu yanayoweza kusababisha kutenda dhambi.

‘’Ramadhani ni ibada muhimu kwa Waislaam kwani ndio mwezi ambao huchoma dhambi zao na kutenda matendo mema hivyo ni muhimu kwa ndugu Waislaam kuendeleza yote mema ambayo wanafanya katika kipindi hiki cha mwezi wa Ramadhani ikiwa ni pamoja na kuliombea Taifa.’’

Kwa upande wake Sheikh Mkuu wa Tanzania Mufti Aboubakar Zubeir Ali ametaka wananchi wa Tanzania bila kujali itikadi za kidini kuendelea kuliombea Taifa ili lizidi kuendelea kuwa na amani.
Nae Kaimu Sheikh wa mkoa wa Pwani Sheikh Hamisi Mtupa amemshukuru Rais Magufuli kwa ukarimu wake wa kuwaaandalia futari wananchi wa mkoa wa Pwani ikiwa ni pamoja na makundi maalum ya watoto yatima wa kituo cha Bulome Foundation cha mjini Kibaha mkoani Pwani. 

Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Kibaha, Pwani
21 Juni, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwa katika foleni ya kunawa na kisha kuchukua chakula leo Jumatano Juni 21, 2017  katika futari aliyowaandalia wananchi wa mkoa wa Pwani katika Ikulu ndogo ya Kibaha ambayo ilihudhuriwa pia na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir Ali  pamoja na viongozi wengine wa dini, serikali, vyama na watoto wanaolelewa kwenye vituo mbalimbali vya yatima mkoani humo.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Magufuli (wa pili kulia) akichukua chakula leo Jumatano Juni 21, 2017 katika futali aliyowaandalia wananchi wa mkoa wa Pwani futari katika Ikulu ndogo ya Kibaha ambayo ilihudhuriwa pia na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir Ali pamoja na viongozi wengine wa dini, serikali, vyama na watoto wanaolelewa kwenye vituo mbalimbali vya yatima mkoani humo.

 Kina mama wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kibaya Mhe. Asumpta Mshama wakichukua chakula wakati wa futari iliyoandaliwa na  Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa wananchi wa mkoa wa Pwani katika Ikulu ndogo ya Kibaha 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitoa neno la shukrani leo Jumatano Juni 21, 2017  wa waliohudhuria  futari aliyowaandalia wananchi wa mkoa wa Pwani katika Ikulu ndogo ya Kibaha.
 Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir Ali  akizungumza machache na kuomba dua baada ya futari iliyoandaliwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa wananchi wa mkoa wa Pwani katika Ikulu ndogo ya Kibaha.

 Sehemu ya waalikwa wakiitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir Ali  baada ya   futari iliyoandaliwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa wananchi wa mkoa wa Pwani katika Ikulu ndogo ya Kibaha.





VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS JUNE 22,2017


WANAWAKE WA KANISA LA PENTEKOSTE TANZANIA WAFANYA KONGAMANO LA TATU JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0

 Askofu Saldonie Simon Sinde akiwasalimia Wakina mama katika Kongamano la Tatu la Wanawake wa Muungano wa Makani ya Pentekoste Tanzania (UW-MMPT), lililoanza Katika Kanisa hilo Sinza Afrika Sana Dar es Salaam jana. Askofu Sinde pia alivitambulisha vitabu vyake viwili alivyoviandika.
 Mama Askofu, Obedi Fabian, Ruth Obedi akizungumza katika kongamano hilo.
 Maaskofu wa Kanisa hilo wakionesha kitabu cha Mbinu ya Kufundisha Watoto kilichoandikwa na Askofu Sinde (wa kwanza kushoto), ambacho kinauzwa shilingi 8000. Kutoka kulia ni Askofu Obeid Fabian Hofi, Eliezar Isacka Mauge, Methusela John Mperana Askofu, Erasto Makala.
 Naibu Katibu Mkuu wa Misheni, Joyce Innocent akisherehesha kongamano hilo.
 Kongamano likiendelea.
 Wakina mama wakiwa kwenye kongamano hilo.



 Usikivu katika kongamano hilo.
 Taswira katika kongamano hilo.
 Maombi yakifanyika.
 Kwaya ya Praise Team ikitoa burudani ya nyimbo za kusifu.
 Viongozi wa muungano wa wanawake wa Kanisa hilo.
 Viongozi hao wakionesha mshikamano.
Furaha katika Kongamano hilo.

WANAWAKE VIONGOZI KATIKA MASOKO WAMUOMBA RAIS MAGUFULI KUTEMBELEA KATIKA MASOKO AONE MIUNDOMBINU ILIVYO

$
0
0

Ofisa Mradi wa 'Mpe Riziki Si Matusi' kutoka Shirika la Equality for Growth (EfG), Suzan Sita (kulia), akitoa mada katika Warsha ya Siku tatu ya kuwajengea uwezo viongozi wa Umoja wa Wanawake Masokoni iliyohusu ukatili dhidi ya wanawake na haki zao iliyoandaliwa na shirika hilo inayoendelea katika Hoteli ya Lamada Ilala jijini Dar es Salaam jana.
Viongozi hao wakiwa katika warsha hiyo.
Warsha ikiendelea.
Warsha hiyo. Kulia ni Mwezeshaji Sheria kutoka Soko la Tabata Muslim, Irene Daniel.
Taswira katika ukumbi wa mikutano.
Mwezeshaji Sheria wa Soko la Temeke Sterio, Batuli Mkumbukwa akichangia mada.
Mwezeshaji Sheria katika Soko la Ilala Mchikichini, Consolata Cleophas, akichangia mada. (kulia) ni Mwezeshaji Sheria kutoka Soko la Tabata Muslim, Aisha Juma na kushoto ni Verdiana Gervas kutoka Soko la Ilala.
Mwezeshaji Sheria kutoka Soko la Ilala Mchikichini, Bupe George akichangia mada.
Mwezeshaji Sheria wa Soko la Kigogo Kisambusa, Mariam Rashid akichangi mada.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wafanyabiashara masokoni Tanzania, Betty Mtewele akichangia jambo.
Mfanyabiashara kutoka Soko la Gongolamboto, Elika Mwakyusa akichangia.
Mwezeshaji Sheria katika Soko la Temeke Sterio, Johanitha Katunzi akichangia mada.
Mshiriki wa warsha hiyo  akichangia jambo.
Mwezeshaji Sheria kutoka Soko la Tabata Muslim, Aisha Juma akichangia jambo.
Mwezeshaji Sheria kutoka Soko la Kiwalani Kigilagila, Bisura Juma akichangia jambo.

Na Dotto Mwaibale

VIONGOZI Wanawake katika masoko jijini Dar es Salaam wamemuomba Rais Dk.John Magufuli atembelee masoko wanayofanyia shughuli zao ili aone changamoto ya miundombinu katika masoko hayo.

Mwito huo ulitolewa Dar es Salaam jana na Mwezeshaji wa Sheria katika Soko la Ilala Mchikichini, Consolata Cleophas  wakati akichangia mada kwenye warsha ya siku tatu ya kuwajengea uwezo viongozi wa umoja wa wanawake masokoni iliyohusu ukatili dhidi ya wanawake na haki zao iliyoandaliwa na Shirika la Equality for Growth (EfG)

Alisema wafanyabiashara wakiwemo wanawake wamekuwa wakilipa ushuru kila siku katika masoko hayo lakini manispaa husika zimeshindwa kuwajengea miundombinu kama vyoo bora, umeme na maji hivyo kuwa changamoto kubwa kwao.

"Tumekuwa tukitoswa ushuru wa shilingi 500 kwa siku kwa kila mfanyabiashara lakini hatuoni jitihada zozote zinazochuliwa na hizi manispaa zetu za kutuwekea miundombinu bora ndio maana tunamupomba Rais wetu afanye ziara katika masoko tunayofanyia kazi ili tuzungumze naye na kuiona changamoto hii tuliyonayo" alisema Cleophas.


Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wafanyabiashara masokoni Tanzania, Betty Mtewele alisema wakati ufike manispaa ziweke wazi sheria ya ulipaji wa ushuru kwa mfanyabiashara ambaye hakufika sokoni kwa zaidi ya miezi miwili kutokana na kuumwa kwani anapo pona na kurudi katika eneo lake la kazi anatakiwa kulipa ushuru wa muda huo wote ambao hakufanya biashara wakati alipokuwa akijiuguza.

"Tunaomba manispaa zetu ziweke wazi jambo hili kwani limekuwa ni changamoto kubwa sana kwetu" alisema Mtewele.

Mwezeshai wa Sheria katika Soko la Kigogo Sambusa Mariam Rashid alisema zabuni za uzoaji taka katika masoko zinapaswa kuangaliwa kwa karibu kwani wengi wanaozipata hawana uwezo wa kufanya kazi hiyo hivyo kusababisha masoko mengi kuwa na changamoto ya mlundikano wa takataka ambapo alishauri kuondoa mfumo dume katika masoko unaotoa tenda hizo na badala yake zitolewe fursa kwa wanawake ili waweze kuingia katika kamati za masoko ili nao waweze kuchangia katika mambo mbalimbali.

Elika Mwakyusa aliomba manispaa ya Ilala kutenga eneo la soko Gongolamboto ambako hakuna soko kwani eneo wanalofanyia biashara zao ni la mtu binafsi hivyo wamekuwa na changamoto kubwa ikiwemo kumlipa ushuru mkubwa mtu huyo.

Mwezeshaji sheria wa Soko la Vingunguti wa Simba, Maimuna Mungi alisema ushirikishwaji wa wanawake katika maamuzi mbalimbali katika soko hilo hakuna kutokana na kuwepo kwa mfumo dume jambo ambalo limechangia wanawake wafanyabiashara katika soko hilo kushindwa kuzipatia kusaidiwa changamoto walizonazo.

Mwezeshai Sheria kutoka Soko la Temeke Sterio, Batuli Mkumbukwa aliomba asilimia 10 ya fedha za makusanyo ya ushuru zibaki katika masoko husika ili zisaidie ujenzi wa miundombinu.

Ofisa Mradi wa Mpe Riziki si Matusi kutoka EfG Suzan Sitha alisema lengo la warsha hiyo ni kuwaongezea uelewa viongozi wanawake masokoni kuhusu ukatili dhidi yao pamoja na kupanga mikakati ya kuendeleza kampeni za kupunguza ukatili dhidi ya wanawake masokoni baada ya mradi kuisha.

Alitaja lengo lingine ni kutambua haki za wanawake na wahanga wa ukatili dhidi ya wanawake pamoja na kuwakumbusha viongozi juu ya wajibu wao na utunzaji wa kumbukumbu za vikundi.

Sitha alisema warsha hiyo imewashirikisha viongozi wanawake kutoka masoko  ya Manispaa ya Ilala na Temeke jijini Dar es Salaam, ambayo ni Ilala Boma, Gongolamboto, Mombasa, Kiwalani, Mchikichini, Kigogo Fresh, Kigogo Sambusa, Chamazi, Kiustu, Kinyerezi, Feri, Temeke Sterio, Buguruni, Gezaulole, Tabata Muslim na Vingunguti kwa Simba.

Alisema karibu changamoto zote zilizopo katika masoko zinalingana kubwa ikiwa ni miundombinu mibovu licha ya  wafanyabiashara kulipa ushuru na kuwa mradi huo wa Mpe Riziki Si Matusi upo katika Wilaya ya Temeke na Ilala jijini Dar es Salaam ambapo mradi mkubwa wa Sauti ya Mwanamke Sokoni  upo katika mikoa tisa hapa nchini.

Milioni 20 za Biko zaenda kwa Ramadhan wa Dodoma

$
0
0
DONGE nono la Sh Milioni 20 la bahati nasibu ya Biko ‘Ijue Nguvu ya Buku’, droo ya 16, leo limeenda kwa mshindi wao Ramadhan Juma Hussein, mwenye maskani yake mjini Dodoma, ikiwa ni mara ya kwanza kwa Makao Makuu ya Nchi ya Tanzania kupata mshindi wake katika droo kubwa inayofanyika Jumatano na Jumapili.

Ushindi wa Ramadhan umekuja siku chache baada ya kukabidhiwa fedha zake mshindi wa Handeni, mkoani Tanga, Yahaya Ally Khamis, aliyekabidhiwa pesa mapema wiki hii.

Akizungumza katika droo hiyo leo mchana, Balozi wa Biko, Kajala Masanja alimpongeza Ramadhan kwa kuibuka na ushindi mnono wa Sh Milioni 20, huku akiwataka Watanzania wote kucheza kwa wingi na mara nyingi ili wazoe mamilioni ya Biko.

“Naomba kutangaza kwamba mshindi wetu wa Jumatano hii wa Sh Milioni 20 ni Ramadhan anayetokea mjini Dodoma, ambaye pia amekiri kucheza Biko mara kwa mara pamoja kuwahi kushinda zawadi za papo kwa hapo ambao zinatoka kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja zinatoka kila dakika kwa wale wanaocheza bahati nasibu yetu.

Mchezo huu unachezwa kwa kupitia ujumbe mfupi wa maandishi kwenye mitandao ya simu ya Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel, ambao huingiza namba ya kampuni ambayo ni 505050 na ile ya kumbukumbu 2456, baada ya kufanya muamala kuanzia Sh 1,000 na kuendelea na kupata nafasi ya kuwania zawadi za papo kwa hapo bila kusahau kuingia kwenye droo kubwa ya Sh Milioni 20,” Alisema Kajala.

Naye Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema Biko imezidi kukolea baada ya kumpata mshindi wa Dodoma kwa mara ya kwanza tangu waanze kuchezesha bahati nasibu yao, huku akiwapongeza wote waliowahi kushinda donge nono la Biko kutoka kwenye mikoa mbalimbali ya Tanzania.

“Ni furaha kubwa kuona Dodoma wameibuka na donge nono la Biko, huku nikiamini kuwa kucheza Biko ni rahisi pamoja na kuweza kuibuka na ushindi wa zawadi za papo hapo bila kusahau zawadi kubwa ya Sh Milioni 20 inayotoka mara mbili kwa wiki,” Alisema Heaven.

Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Emmanuel Ndaki, aliwataka Watanzania kuchangamkia fursa mbalimbali za uwapo wa bahati nasibu ya Biko, akisema kwamba ni rahisi kucheza pamoja na urahisi pia wa kuibuka na ushindi.

“Uwapo wa mwakilishi wa Bodi kwenye droo ya Biko unatokana na dhamira ya kuhakikisha kwamba kila kitu kinakwenda sawa, hivyo niwatoe hofu Watanzania kuwa Biko ni mchezo halali unaofuata sheria zote za nchi,” Alisema Ndaki.

Mara baada ya kutangazwa mshindi katika droo iliyofanyika jana, jijini Dar es Salaam, Biko itamkabidhi mshindi wao huyo wa Dodoma jumla ya Sh Milioni 20 kwa ajili ya kuziingiza kwenye majukumu yake ya kimaisha, huku dalili za kupanua biashara zake kuwa kubwa baada ya kutangaza kwamba ni mjasiriamali wa simu mkoani Dodoma.
Balozi wa Biko Kajala Masanja kulia akiwa kwenye tukio la kumtafuta mshindi wa Sh Milioni 20 wa droo ya 16 ya Biko, ambapo bwana Ramadhan Hussein wa Dodoma aliibuka kidedea na kuzoa kiasi hicho cha pesa kutoka Biko. Kushoto ni mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Emmanuel Ndaki.

DC SHINYANGA AWAUMBUA HADHARANI VIONGOZI WA UPINZANI WANAOKWAMISHA MIRADI YA MAENDELEO,AONYA SIASA ZA MAJITAKA

$
0
0

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro amewataka wananchi wa kijiji cha Mwamagunguli kata ya Kolandoto manispaa ya Shinyanga kuacha kuchanganya siasa kwenye masuala maendeleo kwani inakwamisha shughuli za maendeleo na kusababisha kero katika jamii.

Matiro ameyasema hayo jana June 21,2017 baada ya kutatua mgogoro wa mradi wa maji ya kisima kirefu katika kijiji hicho ambapo viongozi wa eneo hilo kuanzia ngazi ya kitongoji hadi kata na wananchi walikuwa hawatumii maji hayo wakidai kuwa yana chumvi na hata yakitumika kupikia chakula yanakibadilisha na kuwa na rangi ya njano.

Kufuatia utata huo wa mradi huo ambao ujenzi wake ulikamilika tangu Mwaka 2014 kwa gharama ya shilingi milioni 294.6,Mkuu huyo wa wilaya aliamua kufika katika kijiji hicho ili kubaini ukweli wa madai ya wananchi hao.

Baada ya kufika katika kijiji hicho akiwa ameambatana na baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hiyo pamoja na viongozi wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga walizungumza na wananchi wa eneo hilo ambao walisisitiza kuwa maji hayo hayafai mbele ya mkuu wa wilaya.

Mmoja wa wananchi hao,Shija Luhende aliuponda mradi huo wa maji mbele ya mkuu huyo wa wilaya akidai kuwa maji ya mradi huo wa kisima kirefu ukiyapikia kwenye ugali au wali chakula kinakuwa cha njano kutokana na kuzidi kwa chumvi hivyo hayafai kwa matumizi ya binadamu.

Naye Mwenyekiti wa kamati ya maji katika kijiji hicho Grace Jackson alisema mradi huo wa maji wameshindwa kuuendesha kutokana na kupata hasara kwani kila wanaponunua umeme wa Shilingi 100,000/= kisha kusukuma maji kwenye tanki,wanapouza maji hayo kwa wananchi wamekuwa wakiishia kupata shilingi 3,000/= tu huku maji nayo yakikauka kwenye tanki bila ya kujua yameishaje na hivyo kuona mradi huo hauna faida zaidi ya kupata hasara. 

Kufuatia hali hiyo,ili kumaliza utata,mkuu wa wilaya aliagiza maji kutoka kwenye kisima yajazwe kwenye tanki na kusukumwa ili serikali ijiridhishe kama kweli maji hayo yana chumvi nyingi.

Mkuu huyo wa wilaya aliamua kuyanywa maji hayo katika mkutano wa hadhara na kudhibitisha kuwa ni mazuri tena yanafaa kwa matumizi ya binadamu huku viongozi waliokuwa katika mkutano huo pamoja na wananchi wakinywa maji hayo huku wakishangilia kuwa ni maji mazuri hayana chumvi.

Matiro hakuishia kunywa maji tu,pia aliagiza chakula kipikwe jirani na nyumba iliyopo karibu na mkutano huo wa hadhara kisha kiletwe mbele ya wananchi ili kuona kama kimebadilika na kuwa na rangi ya njano.

Chakula kilichopikwa ni wali ambao haukubadilika rangi hali iliyowafanya wananchi waanze minong’ono ya hapa na pale wakidai kuwa walichezewa akili zao kwa kudanganywa na viongozi wao kuanzia ngazi ya kitongoji waliowaaminisha kuwa maji hayo hayafai kwa matumizi ya binadamu.

Baada ya kunywa maji hayo na kuona wali haujabadilika rangi wananchi hao,walianza kutoboa siri kuwa mradi huo uliingizwa siasa ndani yake kutoka kwa viongozi wao kutoka vyama vya upinzani (Chadema) ili serikali ionekane imeanzisha mradi mbovu.

Mmoja wa wananchi hao,Joyce Mugoswa alitoboa siri kuwa maji hayo walikuwa hawajawahi kuyatumia zaidi ya kuambiwa tu kuwa ni mabaya na yana chumvi nyingi na yakipikiwa chakula chote kina kuwa cha njano na hivyo kulazimika kwenda kufuata huduma hiyo ya maji umbali mrefu katika hospitali ya Kolandoto.

"Ukweli mkuu wa wilaya, mradi huu wa maji ulitawaliwa na siasa ,tulikuwa tukiambiwa maji ni mabaya tusichote, tutakufa na hivyo kuingiwa na hofu ,kumbe tunaacha maji mazuri kabisa" ,alisema Magoswa. 

Aidha baada ya wananchi kujiridhisha kuwa maji hayo ni salama waliukubali mradi huo wa maji,huku baadhi ya wafuasi wa Chama Cha Maendeleo (Chadema) waliokuwa eneo la mkutano wakianza kuondoka mmoja baada ya mwingine baada ya kuumbuliwa hadharini. 

Mkuu huyo wa wilaya alionya siasa kwenye masuala ya maendeleo na kutoa onyo kwa atayeendekeza siasa za maji taka na kukwamisha miradi ya maendeleo kutonufaisha wananchi, atakula naye sahani moja kwa sababu huyo ni mhujumu uchumi .

"Nilichobaini hapa ni kwamba kuna watu wanaleta siasa kwenye masuala ya maendeleo,kamwe hatutakubali kuona watu wanakwamisha shughuli za maendeleo,hebu fikiria akina mama walikuwa wanatumia muda mrefu kufuata huduma ya maji wakati maji yapo hapa tena hayana tatizo lolote,siasa za majitaka zilishapitwa na wakati,huu muda wa kazi tuwaletee maendeleo wananchi", alieleza Matiro. 

Matiro aliukabidhi mradi huo chini ya uongozi wa sungusungu ndani ya wiki moja wakishirikiana na wataalam wa manispaa ya Shinyanga ili kuona kama hizo hasara za kuendesha mradi zitajitokeza tena. 


 Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na wakazi wa kijiji cha Mwamagunguli.
Wananchi wa kijiji hicho wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro 
Mmoja wa wananchi hao Shija Luhende akiuponda mradi huo wa maji mbele ya mkuu huyo wa wilaya kuwa maji yake ukiyapikia kwenye ugali au wali chakula kina kuwa cha njano kutokana na kuzidi kwa chumvi na hayafai kwa matumizi ya binadamu
Mwenyekiti wa kamati ya maji Grace Jackson akielezea jinsi mradi wa maji unavyoendeshwa kwa hasara 
Wananchi wakiwa kwenye mradi wa maji kabla mkuu wa wilaya hajaanza kunywa maji hayo  Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akinywa maji yaliyokuwa yanadaiwa kuwa hayafai kwa matumizi ya binadamu

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akinywa maji Mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga,Geofrey Mwangulumbi akinywa maji yaliyodaiwa kuwa hayafai kwa matumizi ya binadamu
Mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga,Geofrey Mwangulumbi akiinua bakuli baada ya kumaliza kunywa maji
Wananchi wakinywamaji hayo ya mradi wa kisima kirefu ambao walikuwa wameukataa baada ya kurishwa maneno kuwa ni mabaya ukipikia chakula kina kuwa cha njano.

Wananchi wakiendelea kunywa maji
Kila mmoja akataka kunywa maji....
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga akiwa ameshikilia sahani yenye wali uliopikwa kwa maji yaliyokuwa yanadaiwa kuwa ukiyatumia kwa chakula,chakula kinabadilika na kuwa na rangi ya njano
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akionesha wali uliopikwa kwa maji ya kisima kirefu cha maji...Wali huo haukubadilika rangi... Picha zote na Marco Maduhu-Malunde1 blog

SKYTRAX HAT-TRICK FOR ETIHAD AIRWAYS FIRST CLASS

$
0
0
Linda Celestino, Etihad Airways Vice President Guest Experience Delivery, receives the Skytrax World Airline Awards for World’s Best First Class Airline, World’s Best First Class Onboard Catering and World’s Best First Class Airline Seat.
  • Airline wins three major awards for its industry-leading First Class at the annual World Airline Awards
Etihad Airways has once again been presented with three coveted awards for the World’s Best First Class, Best First Class Onboard Catering, and Best First Class Airline Seat at the annual Skytrax World Airline Awards. The event was held at the Musee de l’Air et de l’Espace, as part of the bi-annual Paris Airshow.

The prestigious World Airline Awards are widely considered to be a global benchmark of airline excellence. Winners are chosen based on the votes and findings of a ten month survey of over 19 million air travellers from 105 countries. The survey covers over 325 airlines, from the largest international airlines to smaller domestic carriers, measuring quality standards for 41 KPIs across front-line product and service factors in the airport and onboard environments.

Linda Celestino, Etihad Airways Vice President Guest Experience Delivery, said: “This is a great honour for us – particularly as these awards mark the culmination of a global consumer satisfaction survey of millions of travellers around the world. Our First Class experience is unlike any other and has been tailored around exact requirements of those who wish to enjoy a truly bespoke hospitality experience, with the finest in-flight dining and amenities, incomparable levels of privacy and the genuine warmth and care for which we are known.

“These awards not only recognise our drive for innovation and a superior guest experience, but also reinforce our commitment to First Class travel - an experience for which we have set the industry benchmark.”

In recent years, Etihad Airways has won numerous accolades for its First Class service and cabin designs. This also marks the third time the airline has won all three First Class award categories at the World Airline Awards.

Edward Plaisted, Chief Executive Officer of Skytrax, said: "Etihad Airways continues to be a market leader in first class air travel, illustrated by their excellent performance in this First Class section of the awards. It is a remarkable display of consistency to yet again secure this very prestigious set of awards and we congratulate them on this achievement."

Etihad Airways offers First Class private suites on a large number of its widebody fleet of aircraft. The A380 First Class cabin boasts nine First Apartments, unique living spaces which at 39 square feet in area, and feature a Poltrona Frau leather armchair and a separate ottoman which converts into a full-length 80.5 inch long bed. A dedicated shower room is available for exclusive use by First Class guests.

The Boeing 787s are equipped with eight private First Suites in a unique curved aisle setting, an airline industry first, with a 10 per cent increase in personal space. The forward and aft facing suites feature a large Poltrona Frau leather armchair which converts into an 80.5 inch fully-flat bed. They also feature 24 inch TV monitors, large dining tables for dual dining, personal wardrobes and privacy doors.

Etihad Airways’ three-class configured longhaul fleet of Boeing 777s and Airbus A330/A340 family aircraft also feature private First Class suites, with Poltrona Frau leather seating and cutting-edge features and amenities.

More information on Etihad Airways’ First Class service is available on:
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images