Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46201 articles
Browse latest View live

KITUO CHA UWEKEZAJI (TIC) CHAANDAA MAFUNZO YA SIKU SITA KWA WAJASIRIAMALI JIJINI DAR ES SALAAM

0
0

Bw. Godfrey Mwambe Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) akizungumza na waandishi wa habari wakati akielezea kuhusu kuhusu semina ya wajasiriamali inayotarajiwa kuanyika kwa kipindi cha siku sita kuanzia tarehe 26 Juni Mpaka tarehe 01 Julai katika Hoteli ya New Afrika hapa hapa jijini Dar-es-salaam, Mkutano huo umefanyika katika ofisi za kituo hicho jijini Dar es salaam leo.
Bw. Godfrey Mwambe Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye mkutano huo uliofanyika katika ofisi za kituo hichi jijini Dar es salaam.

………………………………………………………………………………….

Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kwa kushirikiana na Shirika la biashara na Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNCTAD, limeandaa mafunzo maalumu ya kuwajengea uwezo wajasiriamali wadogo mafunzo ambayo yatafanyika kwa kipindi cha siku sita kuanzia tarehe 26 Juni Mpaka tarehe 01 Julai katika Hoteli ya New Afrika hapa hapa jijini Dar-es-salaam.

Lengo la program hii muhimu na endelevu kwa Wajasiriamali wa Kati (SMEs) na makampuni makubwa ni kuwajengea uwezo wafanyabiashara hao wadogo ili waweze kufanyabiashara na kutoa huduma kiufanisi na tija zaidi baina yao na hayo makampuni makubwa ya kigeni yaliyopo hapa nchini. Semina hii itawasaidia pia katika kuongeza mbinu na ujuzi katika kuibua fursa mpya, kudumisha biashara baina ya makampuni madogo na makubwa, kuwafundisha namna ya kupata taarifa sahihi za kibiashara, kuongeza ubora na viwango vya bidhaa na huduma wanazotoa na kuongeza ujasiri katika kuendesha biashara zao.

Vilevile lengo lingine muhimu la programu hii ni kuwaunganisha wafanyabiashara hao na wadau mbalimbali yaani BDSPs kama vile taasisi za fedha, wataalam mbalimbali wa huduma za biashara, masoko, biashara na tafiti mbalimbali ili kuwapa ujuzi wa kisekta mbalimbali zinazolenga katika kuboresha bidhaa na huduma zao.

TIC inategemea kuwa baada ya mafunzo hayo wafanyabiashara hao watakuwa wamejengewa uwezo na mitizamo chanya ili baadae waweze kutoa bidhaa na hudumu zinazokidhi ubora na viwango.

Kama Serikali tumekuwa tukihimiza na kutunga sheria na miongozo mbalimbali kuwafanya wawekezaji wakubwa wa nje na wa ndani kutoa fursa kwa makampuni madogo madogo kufanya biashara nao. Lakini mtakubaliana nami kwamba changamoto kubwa ya utekelezaji wa jambo hili ni kushidwa kuwa na uwezo kwa wajasiliamali wetu kufanya biashara na makampuni haya kiufanisi. Mafunzo haya yanalenga katika kusadia kuondoa changamoto hizo.

Mwisho kabisa, napenda kutoa rai kwa wafanyabiashara watakaopata fursa ya kuweza kujengewa uwezo waweze kuzingatia sana mada zitakazotolewa na wawezeshaji hawa. Nina hakika kwa kufanya hivyo tutaweza kuondokana na changamoto za kutokuwa wadau endelevu katika mfumo wa uchumi wetu.

IMETOLEWA NA MKURUGENZI MTENDAJI TIC,

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JUNE 20,2017

0
0

LEO NI SIKU YA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAKIMBIZI DUNIANI

0
0
 
Mkimbizi akiwasili nchini Tanzania kutoka Burundi baada ya kukimbia machafuko

NDOA NA MIMBA KATIKA UMRI MDOGO

0
0
Meneja wa Utekelezaji wa miradi wa asasi ya Tanzania Communication and Development Center (TCDC) James Mlali 
 
 
Zipo sababu nyingi na ushahidi mwingi wa kisayansi, unaonyesha kuwa, ndoa na mimba katika umri mdogo wa msichana chini ya umri wa miaka 18 ni hatari kwa afya na mstakabali wa maisha yake na mtoto wake.
 
Wasichana wengi wakati huu licha ya kuanza kupevuka wanakuwa hawajakomaa kiakili na uwezo wao ni duni katika maamuzi juu ya kufaa kwa mtu atakayekuwa mwenzi sahihi wa maisha.

Kimwili pia wasichana katika umri huu wanakuwa hawajawa tayari kuyakabili majukumu ya uzazi na unyumba, nyonga za wasichana wanaoendelea kukuwa mara nyingi huwa changa na finyu kiasi kwamba husababisha matatizo mengi ya uzazi wakati wa kujifungua kwa njia ya kawaida.

Wasichana wengi huchelewa kujifungua au huchukuwa saa nyingi za uchungu kabla ya kujifungua, hali hii inaweza kusababisha kifo cha mama au mtoto au wote wawili kama matibabu ya dharura ya upasuaji kwa ajili ya uzazi hayakufanyika. Idadi kubwa ya akina mama wanaojifungua kwa njia ya upasuji ni wale walio na umri mdogo.

Meneja wa Utekelezaji wa miradi wa asasi ya Tanzania Communication and Development Center (TCDC) James Mlali anasema tatizo jingine linaloambatana na mimba katika umri mdogo ni pamoja na kutokwa na damu nyingi pale mimba inapoharibika au wakati wa kujifungua. Wasichana wengi hukabiliwa na tatizo hili ikiwa ni pamoja na kupata uambukizo wa bakteria katika njia ya kizazi pamoja na kupata kifafa cha mimba.

Wasichana wadogo mara nyingi huzaa watoto wenye uzito pungufu au njiti, watoto namna hii hukabiliwa na na hatari pamoja na changamoto nyingi za kiafya katika umri wao chini ya miaka mitano. Watoto wengi hupata matatizo ya mtindio wa ubongo na taahira ya akili. Wasichana wengi wanaozaa katika umri mdogo hupata hali ya aibu na hisia ya kudharauliwa mambo ambayo huongeza mzigo kwa wote mama na mtoto.

Mlali anongeza kuwa wasichana wanao olewa au kupata mimba za utotoni hupeteza fursa na haki ya elimu. Wengi wao hufukuzwa shuleni au wazazi wao hupoteza imani kwao kiasi kwamba, husita kuwaendeleza kimaisha hata baada ya kujifungua, hali hii hufungua mlango kwa msichana kuingia katika umaskini na kuzaa ovyo bila mpangilio. Mzigo huongezeka pale msichana anapolea watoto peke yake kama hakubahatika kuolewa au kama ataachika baada ya kuolewa.

Wasichana wanaoolewa kutokanan na kukosa uwezo wa kukabili matakwa ya unyumba na majukumu yake, wengi hukabiliwa na unyanyasaji, ukatili pamoja na udhalilishaji wa kijinsia ndani ya ndoa. Wengi hupata vipigo vinavyo wasababishia ulemavu wa maisha au vifo.Wengi hutukanwa na kubezwa.Wengi hulazimishwa kuolewa na watu wenye umri mkubwa bila hata kupima damu kwa ajili ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI kabla ya ndoa.

Hali hii huwafanya wasichana wanaoolewa katika umri mdogo kukabiliwa na hatari ya kuambukizwa virusi vya UKIMWI na wengi huwa wajane kabla ya kuwa watu wazima. Wale wanaoachika huwa na uwezekana mkubwa wa kuachika tena pale wanapoolewa kwa mara nyingine. Hii hutokana na athari za kisaikolojia zinazowajengea wasichana hawa doa la kitabia katika jamii na kuwafanya wasione umuhimu wa kudumisha mahusiano ya ndoa kutokana na uzoefu mbaya walioupata katika ndoa za awali.

‘Mara nyingi wasichana wadogo hawana elimu ya kutosha kuhusu muda wa vipindi ambavyo wanaweza kupata ujauzito.. Wengi wao pia kutokana na sababu mbalimbali za kibinafsi na za kijamii, hawapati fursa za kutumia huduma za afya ya uzazi wa mpango’, anaongeza Mlali

Wasichana wengi wanaojihusisha na ngono kabla ya ndoa hupata mimba zisizopangwa, zisizotakiwa na zisizotarajiwa. Jambo hili huleta mzigo mkubwa wa kihisia kwa msichana hasa pale anapokuwa mwanafunzi. Wasichana wengi wanaojikuta katika hali hii hufikiria kutoa mimba kama njia pekee ya ufumbuzi wa tatizo. Wengi hutoa mimba katika mazingira hatarishi na kwa njia zisizozingatia afya na usalama. Hii hutokana na ukweli kuwa, utoaji mimba ni kosa la kisheria na kimaadili katika nchi nyingi.

Wasichana wengi wanaopata watoto katika umri mdogo, hukabiliwa na tatizo la kulea watoto peke yao kwa vile wengi huwa hawajaolewa. Na hata kama wataolewa, wengi huachika mapema. Wengi wao hawana maandalizi kwa ajili ya ndoa na majukumu ya kutunza watoto.
 
Watoto wengi wa akina mama hawa hupata matatizo ya kihisia hasa pale wasipowaona baba zao pale nyumbani kama ilivyo kwa watoto wenzao. Jambo hili huwasababishia athari ziambatanazo na huzuni, fedheha, msongo wa mawazo, kuumwa mara kwa mara, kutofanya vizuri katika masomo yao, kukosa usingizi mara kwa mara na kukosa mapenzi ya baba.

Kutokana na hali, Mlali anasema kuwa ingawa kuachana na ngono kabisa ni jambo zito kwa wasichana wengi wa kizazi kipya kutokana na shinikizo la utandawazi, lakini bado inawezekana. Kinachohitajika ni kujifunza na kujua jinsi ya kutumia uzazi wa mpango kwani ndio njia pekee ya kuepuka mimba za utotoni. Na kwa sababu hiyo kwa wasichana wadogo wataweza kuendelea na elimu na hatimaye kuwa na maisha mazuri ya ukubwani.

RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA RAIS MSTAAFU WA NIGERIA MHE. OLUSEGUN OBASANJO IKULU DAR ES SALAAM

0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimlaki Rais Mstaafu wa Nigeria Mhe. Olusegun Obasanjo aliyemtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo Juni 20, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na  Rais Mstaafu wa Nigeria Mhe. Olusegun Obasanjo aliyemtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo Juni 20, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimsindikiza Rais Mstaafu wa Nigeria Mhe. Olusegun Obasanjo baada ya kufanya naye mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Juni 20, 2017

PICHA NA IKULU

MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA HAI ASHIKILIWA NA POLISI KWA SAA TANO BAADA YA KUMALIZA KIKAO CHA BARAZA

0
0
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai,Hela Mchomvu (Kulia) akiingia katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Hai kwa ajili kuongoza kikao cha baraza hilo.Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Yahana Sintoo.
Mwenyekiti wa Baraza la Halmashauri ya wilaya ya Hai,Hela Mchomvu akiteta jambo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Hai ,Yahana Sintoo wakati wa kikao cha baraza la Madiwani.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Hai,Yohana Sintoo akizungumza wakati wa kikao cha baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo.
Baadhi ya Madiwani wanaounda baraza la Halmashauri ya wilaya ya Hai.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai,Helga Mchomvu akizungumza wakati wa kikao cha baraza hilo.
Baadhi ya watendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Hai wakiwa katika kikao cha baraza hilo.
Diwani Harry Masakia akisoma kanuni za kudumu za Halmashauri wakati wa kikao cha baraza hilo.
Baadhi ya Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Hai.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai,Helga Mchomvu akitoka nje ya ukumbi wa mikutno mara baada a kuhairisha kikao cha baraza hilo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai,akizungumza na askari Polisi waliokuwa nje ya ukumbi wakimsubiri kwa ajili ya kumfikisha kituo cha Polisi.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai,Helga Mchomvu akiongozana na askari Polisi wakati akilekea ofsiini kwake.
Askari Polisi wakiomngojea Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai,Helga Mchomvu nje ya ofisi yake .
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai ,Helga Mchomvu akieleka kito cha Polisi huku  akisindikizwa ana askari Polisi.
Mwenyekiti wa Halmahauri ya wilaya ya Hai ,Helga Mchomvu akiingia kituo cha Polisi Bomang'ombe.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini.

DC HAPI AZINDUA UKARABATI WA BARABARA MBOVU KINONDONI

0
0
*Ni zile korofi na zilizoharibiwa na mvua
*Amkabidhi mhandisi wa manispaa mitambo ya kazi,lita 10,000 za dizeli

Wilaya ya Kinondoni leo imezindua ukarabati wa barabara zenye urefu wa Kilomita 148 ambazo zimeharibiwa na mvua zilizonyesha katika msimu uliopita hali iliyosababisha adha ya usumbufu na foleni kwa wananchi.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Ally Hapi ameeleza hayo wakati akizindua matengenezo hayo na kumkabidhi Kaimu Mkurugenzi wa manispaa ya Kinondoni ambaye pia ni mhandisi wa manispaa hiyo Abdul Digaga mitambo ya ujenzi wa barabara na lita 10,000 za dizeli.

Mafuta na mitambo hiyo inatokana na juhudi za Mkuu huyo wa Wilaya ya Kinondoni kwa kushirikiana na wadau wa kampuni za TOTAL TANZANIA na kampuni ya ujenzi GRAND TECH zilizotoa mitambo na mafuta ya dizeli kama sehemu ya mchango wao kwa DC Hapi kwa juhudi zake na za serikali ya awamu ya tano kwa ujumla katika kuwaletea maendeleo wananchi wa Kinondoni.

Barabara zitakazofanyiwa ukarabati ni barabara zote korofi na zilizoharibiwa na mvua katika kata zote 20 za manispaa ya Kinondoni.

Aidha, DC Hapi ametembelea ujenzi wa barabara ya Nzasa KM 1.2 kwa kiwango cha lami unaofanywa na kampuni ya Esteem chini ya mradi wa Uboreshaji jiji la Dar es salaam (DMDP) ambapo chini ya mradi huo wilaya ya Kinondoni itanufaika na kiasi cha bilioni 22 huku Mfuko wa barabara ikiwa na bilioni 6 zilizoruhusiwa kutumika kukamilisha miradi iliyosimamishwa ya 2016/2017.

"Mbali na juhudi hizi za wadau waliojitolea kunisaidia mafuta na mitambo ya kutengenezea barabara, tunazo bilioni 6 za Mfuko wa barabara na tutanufaika na bilioni 22 za mradi wa Uboreshaji wa jiji la Dar es Salaam.Hivyo wananchi msiwe na wasiwasi, mwaka huu ujao wa fedha ni mwaka wa barabara kwa Kinondoni." Alisema Hapi.

DC Hapi aliwaomba wananchi waliojitokeza kuendelea kumuombea Rais Dr. John Magufuli na wasaidizi wake wote kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuleta maendeleo nchini.

Uzinduzi wa ukarabati huo wa barabara umefanyika katika kata ya Kijitonyama na kuhudhuriwa na wananchi wa eneo hilo.

Biko yampatia Milioni 20 mshindi wa Handeni

0
0
WAENDESHAJI wa bahati nasibu ya Biko, ‘Ijue Nguvu ya Buku’ jana wamemkabidhi jumla ya Sh Milioni 20 mshindi wao Yahaya Ally Khamis, aliyeibuka na ushindi katika droo ya 15, iliyochezeshwa juzi Jumapili, huku akitokea wilayani Handeni, mkoani Tanga. Makabidhiano hayo yamefanyika wilayani hapa katika tawi la benki ya NMB, wilayani Handeni, mkoani Tanga, tayari kwa kuziingiza katika matumizi ya kumkwamua kiuchumi.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema mchezo wao ni rahisi kucheza na kushinda, tofauti na michezo mingine inayotumia akili nyingi pamoja na uzoefu wa kufuatilia mambo mengi ya kukuletea ushindi. Alisema Biko ili mtu ashinde ni kufanya muamala kwenye simu yake ya Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel Money kwa kuanzia Sh 1,000 na kuendelea ambapo namba ya kampuni ni 505050 na ile ya kumbukumbu ikiwa ni 2456, huku mchezaji akiwa haulizwi swali lolote kwenye simu yake.

“Biko hatuulizi mtu swali lolote na ndio maana zaidi ya mtu kufanya muamala ambao Sh 1,000 yake itampatia nafasi ya ushindi wa papo kwa hapo kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni 1,000,000 zinazolipwa kwenye simu mara baada ya kupokea ujumbe wa ushindi, huku nafasi nyingine ikiwa ni kuingia kwenye droo kubwa ya kuwania Sh Milioni 20 ambayo Jumapili iliyopita tulimpata Khamis tuliyomkabidhi leo fedha zake.

“Tumefarijika kuja Handeni kumpatia fedha zake mshindi wetu, huku tukiwaasa Watanzania wote kujitokeza kwa wingi kucheza Biko kwa sababu ni mchezo unaotoa ushindi mzuri na haraka, hivyo chezeni kwa wingi na mara nyingi zaidi ili mjiwekee mazingira mazuri ya ushindi,” Alisema Heaven.

Naye Khamis alisema amekuwa mchezaji mzuri wa bahati nasibu ya Biko, jambo ambalo limemfurahisha kwa kiasi kikubwa baada ya kupata ushindi sambamba na kupelekewa fedha zake wilayani Handeni ambako ndiko shughuli zake za kilimo anakoendelea nako.

“Wakati napokea simu ya ushindi kutoka Biko hakika nilishusha pumzi na kumshukuru Mungu, maana pamoja na mambo mengine ya kimaisha ambayo nakusudia kuyafanya, lakini pia Sikukuu hii kwangu naisherehekea kwa shangwe ya aina yake baada ya kukabidhiwa fedha zangu,” Alisema.
 
Baada ya kukabidhiwa fedha hizo, mshindi mwingine wa Biko wa Sh Milioni 20 anatarajiwa kupatikana kesho Jumatano na Jumapili ijayo ikiwa ni mwendelezo wa kutoa mamilioni ya fedha kwa washindi wao wanaopatikana kwa kucheza bahati nasibu ya Biko, huku mwezi pekee wakitoa zaidi ya Sh Milioni 500 kwa washindi ikiwa ni mwelekeo mzuri wa mchezo huo.

Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, kushoto akimkabidhi hundi ya Sh Milioni 20 Yahaya Ally Khamis, dakika chache kabla ya kuelekea katika tawi la benki ya NMB, wilayani Handeni walipomkabidhi pia kiasi cha fedha taslimu Sh Milioni 20 kama mshindi wa droo ya 15 ya Biko iliyochezeshwa Jumapili iliyopita. Wengine ni majirani na wadau wa Khamis, wilayani Handeni wakishuhudia wakati anakabidhiwa hundi hiyo.
Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, akimkabidhi Sh Milioni 20 mshindi wao wa Handeni, mkoani Tanga, Yahaya Ally Khamis kulia. Makabidhiano hayo yalifanyika katika tawi la benki ya NMB, wilayani Handeni mkoani Tanga jana. Kushoto ni afisa wa NMB, wilayani Handeni akishuhudia makabidhiano hayo.
Mshindi wa Sh Milioni 20 wa Biko, Yahaya Ally Khamis, akiwa katika uso wa furaha baada ya kukabidhiwa fedha zake katika tawi la benki ya NMB, wilayani Handeni, mkoani Tanga jana, baada ya kuibuka na ushindi katika droo.

MAMA JANETH MAGUFULI ATOA VYAKULA KWA VITUO NANE VYA KULELEA WATOTO YATIMA

0
0

 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimkabidhi Hajat Mwanaisha Magambo mkuu wa kituo cha New Life Orphanage cha Boko Dawasco kwa niaba ya viongozi wa  vituo nane vya kulelea yatima na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu waliopewa vyakula kwa ajili ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani pamoja na sikukuu ya Eid el Fitr na Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli  Ikulu  jijini Dar es salaam leo Juni 20, 2017. 

Vituo vilivyopkea vyakula hivyo ni pamoja na New Life kilichopo Boko Dawasco chanye watoto 121, Charambe Islamic kilichopo Charambe (watoto 54), Mwandaliwa Centre kilichopo Mbweni (watoto 94) Al Madina Children Home cha Tandale ( watoto 65), Ijangozaidia Orphanage Centre kilichopo Sinza (watoto 1030, Azam Orphanage kilichopo Mbagala (watoto 51), Hiari Orphanage kilichopo Chang'ombe (watoto41) na CHAKUWAMA (watoto 64) kilichipo Sinza.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimsabahi mmoja wa yatima baada ya kumkabidhi vyakula Hajat Mwanaisha Magambo kutoka kituo cha New Life Orphanage cha Boko Dawasco kwa niaba ya viongozi wa  vituo nane vya kulelea yatima na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu waliopewa vyakula kwa ajili ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani pamoja na sikukuu ya Eid el Fitr na Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli  Ikulu  jijini Dar es salaam leo Juni 20, 2017.
  Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na viongozi wa vituo nane vya kulelea yatima na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu kabla ya kuwakabidhi vyakula kwa ajili ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani pamoja na sikukuu ya Eid el Fitr Ikulu  jijini Dar es salaam leo Juni 20, 2017.

BMT YABARIKI UCHAGUZI TFF, LATOA MAAGIZO

0
0

Baraza la Michezo Tanzania (BMT), limebariki Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) likisema: “Tunaitakia TFF uchaguzi mwema wenye amani, upendo na utulivu.”

Pamoja na baraka hizo, Baraza limeiagiza TFF kuwaelekeza wagombea wote kuzipitia sheria za Baraza la Michezo, Kanuni za Baraza na kanuni za Usajili, hususani kanuni ya 8 (1) na (2). 

Kanuni hiyo ya 8 (1) na (2), inaagiza kuwa endapo wagombea wote watakaoshinda nafasi wanazowania kwa sasa ndani ya TFF, hawana budi kuachia nafasi mojawapo katika uongozi wa mpira kwa miguu katika ngazi ya wilaya au mkoa aliyoshinda awali.

BMT imetoa agizo hilo ikiwa ni kukumbushana juu ya utii wa sheria na kuepuka kushika nyadhifa mbili kwa wakati mmoja.

Katika barua yake iliyoandikwa Juni 19, mwaka huu na kusainiwa na Katibu Mkuu wa BMT, Mohammed Kiganja, Baraza hilo limesema: “Uchaguzi huu usivuruge amani iliyopo nchini. Wagombea wakumbuke kuwa kuna maisha baada ya uchaguzi.”

Baraza limesisitiza kuwepo na haki katika mchakato mzima kuelekea kwenye uchaguzi. Uchaguzi na mchakato wake uwe huru na amani na usiwe ni kichocheo cha uvunjifu wa amani.

Baada ya viongozi kupatikana, watakula kiapo cha utii, na kujaza fomu Namba 5 ya BMT ya utekelezaji majukumu yao kama Kanuni ya 8 (4) inavyoeleza.

Kadhalika, mara baada ya uchaguzi, Baraza limeagiza kuhusisha baadhi ya vifungu vya sheria ya Baraza ili viendane na katiba za TFF na wadau pamoja na kanuni zao.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA

RAIS DKT MAGUFULI KUFUNGUA BARABARA YA BAGAMOYO-MSATA

0
0

NAIBU WAZIRI KALEMANI AKUTANA NA WENYE NIA KUZALISHA UMEME WA UPEPO SINGIDA

0
0
Na Veronica Simba - Dodoma .

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Medard Kalemani amekutana na Ujumbe kutoka Kampuni ya Wind East Africa, yenye nia ya kuzalisha umeme kutokana na nguvu ya upepo mkoani Singida. 

Ujumbe huo ulikutana na Naibu Waziri, hivi karibuni, Makao Makuu ya Wizara, mjini Dodoma.

Katika Kikao hicho, Naibu Waziri aliuambia Ujumbe huo kuwa, Serikali inayo dhamira ya dhati kuwezesha jitihada na miradi mbalimbali ya umeme nchini; hivyo iko tayari pia kutoa ushirikiano kwa Kampuni husika ili iweze kuzalisha umeme wa upepo mkoani Singida.

Hata hivyo, Dk. Kalemani aliutaka Ujumbe kutoka Kampuni hiyo, kuhakikisha wanakamilisha taratibu zote zinazostahili, ikiwa ni pamoja na kuwajibika kwa jamii inayozunguka Mradi husika, kwa kujenga mahusiano mazuri (Corporate Social Responsibility – CSR)

Alimwagiza Kaimu Kamishna wa Nishati, Mhandisi Innocent Luoga, kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), kukaa na watendaji kutoka Kampuni husika na kukamilisha taratibu zote zinazotakiwa kwa mujibu wa sheria, ili Mradi uanze kutekelezwa mapema na hivyo kuwanufaisha wananchi wa Singida.

Kampuni ya Wind East Africa, imedhamiria kuzalisha umeme wa megawati 100 kwa kutumia upepo, mkoani Singida.
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Medard Kalemani (kushoto), akiwa katika kikao na Ujumbe kutoka Kampuni ya Wind East Africa (kulia). Wengine kushoto ni maafisa kutoka Wizara ya Nishati na Madini na kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).
 Kutoka kushoto ni Kaimu Kamishna wa Nishati na Masuala ya Petroli, Mhandisi Innocent Luoga, Afisa Mwandamizi kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi John Kabadi, Afisa kutoka TANESCO, Mhandisi Amos Kaihula na Afisa kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Christopher Bitesigirwe wakiwa katika kikao cha Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Medard Kalemani na Ujumbe kutoka Kampuni ya Wind East Africa (Hawapo pichani).
Ujumbe kutoka Kampuni ya Wind East Africa, wakiwa katika kikao na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Medard Kalemani.

Wakazi wa Kijiji cha Ngulu walia na tatizo la maji

0
0
Mkuu wa Wilaya yaMwanga, mkoani Kilimanjaro, Aaron Mbogho


Wakazi wa Kijiji cha Ngulu kitongochi cha Mkongea wilaya ya Mwanga wamesema kuwa tatizo la maji limekuwa tatizo sugu kwa muda mrefu bila kutatuliwa hali inayosababisha ndoa nyingi kuvunjika. Mkazi wa kijiji hicho, Halima Miraji alisema kuwa tangu mwaka 2004 wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa maji ambapo kwa muda mrefu sasa maji yamekuwa yakitoka usiku wa manane tu.

Halima alisema kuwa mfumo wa maji ulijengwa kwenye kijiji jirani cha Mgagani mwaka 1992 ambapo vijiji vyote viwili vilikuwa vikipata maji kutokea hapo. Hata hivyo, alisema wakati wa mafuriko, miundombinu iliharibika na hivyo kusababisha maji yapungue na ndipo viongozi wa vijiji hivyo viwili walipoamua kuwa maji yawe yanafunguliwa kwenye kijiji cha Ngulu nyakati ya mchana na kijiji cha Ngulu wakati wa usiku.

“Kutokana na changamoto hiyo, wanawake tunalazimika kuamka usiku wa manane kuchota maji kwa kuwa kwa kawaida huwa yanakatika alfajiri,” alisema Halima. Alisema kwa kuwa wanawake ndio wanaochota maji usiku na badhi ya wanaume wachache ambao hawajaoa, kutokana na hilo alisema kuwa badhi ya wanawake walijikuta wakiianza uhusiano na wanaume jambo ambalo limefanya ndoa zao kuvunjika.

Alisema kila mtu hulazimika kuweka ndo moja kwenye foleni ya maji iliyo na watu Zaidi ya hamsini kabla ya mzunguko kurudia mara ya pili, tatu na kadhalika jambo ambalo liliwafanya badhi ya wanawake kuingia kwenye vishawishi wakati wanasubiri kwenye foleni. Alisema kuwa changamoto nyingine, ni kuwa shughuli nyingi kama kilimo, biashara na kutunza familia zimekuwa zikizorota kwa kuwa wanakuwa wamechoka asubuhi baada ya kuchota bmaji usiku kucha.

Mkazi huyo aliyasema hayo wakati Kituo cha tafiti Twaweza ilipokuwa kwenye zoezi la kujifunza hali halisi vijijini (immersion) ambapo wafanyakazi wake wote waliweza kuishi kwa siku tatu na familia za vijiji vya Ngulu kata ya Mwanga. Katika zoezi hili walibaini kuwa kukaa pamoja na jamii huwaleta karibu na hivyo husaidia kueleza changamoto zao zinazowakabili kila siku ambazo zimekuwa kikwazo cha maendeleo.

Kutokana na hilo, Twaweza waliweza kugundua changamoto nyingi, ikiwemo, kwenye sekta ya afya, elimu, maji na kadhalika ambazo zinahitaji ufumbuzi wa haraka. Kutokana na hilo wakazi wa Mwanga walishauri serikali kuhakikisha inakuwa karibu na wananchi wake ikiwezekana kutenga muda wa kuishi kwenye vijiji hivyo ilikuweza kutambua moja kwa moja kero zao na jinsi ya kuzitatua.

Wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Twaweza, Aidan Eyakuze, wafanyakazi wote wa Twaweza wakiwemo wale wa Tanzania, Kenya na Uganda walifunga ofisi na kwenda kwenye vijiji mbali mbali vya mwanga kujifunza hali halisi ya wakazi wa vijijini. Katika mwendelezo huo, mwenyekiti wa Kijiji cha Ngulu Modest Severine alisema kuwa tatizo la maji limekuwa sugu katika kijiji hicho na kuwa weka wakina mama katika wakati mgumu.

Alisema mradi wa maji ulipelekwa kwenye wnwo hilo mwaka 1992 lakini kisima kilijengwa kwenye kijiji cha Mgagao kwa makubaliano kuwa maji hayo yengetumika na wakati wa Mgagao pamoja na Ngulu. “Baada ya mradi kuharibiwa na mafuriko na badhi ya miundombinu kubebwa na maji, viongozi walikubaliana kuwa wakazi wa Ngulu wafunguliwa maji saa nane usiku,” alisema.

Alisema kuwa Mbunge wa jimbo hilo Bw Jumanne Maghembe alipewa tarifa na kuahidi kutatua suala hilo. Alisema kwa mujibu wa mbunge huyo kuna mradi mkubwa wa maji unaoitwa Maji ya Mungu uliokwenye hatua za awali ambao utakuwa unapeleka maji kwenye vijiji vya Ngulu, Mgagao na Pangani.

Wakati huo huo, mjumbe wa serikali ya kijiji cha Ngulu, Kiende Athumani nae alisema kuwa kitongoji cha Mkongea kimekuwa kikikabiliwa na tatizo ya maji kwa muda mrefu. Alisema kutokana na changamoto za maji, wakazi wa …wamekuwa wakitumia maji kumwagia mazao yao jambo ambalo linasababisha maji kutoka kidogo nyakati za usiku.

Alisema kuwa serikali imetariwa kuwa kuna mradi wa maji ya Mungu ambayo ikikamilika itakuwa ikitoa maji kwenye vitongaji mbali mbali ikiwemo mkongea, Kavagala, Kivengere na Mabashara. Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Aaron Mbogho alisema kuwa changamoto ya maji kwenye kijiji cha Ngulu unatafutiwa ufumbuzi.

Alisema mradi wa Maji ya Mungu ukikamilika utakuwa unasambaza maji kwenye wilaya ya Mwanga na Korogwe. “Wakandarasi wapo kwenye eneo la ujenzi, na tunategemea mradi awamu ya kwanza uwe umekamilika ifikapo mwaka 2018,” alisema.

Alisema mradi awamu ya kwanza ukikamilika utakuwa umetatua kero ya maji kwenye wilaya ya Mwanga na Same na hivyo kuhakikisha wakazi wa Kijiji cha Ngulu wana maji ya kutosha. Aliongea kuwa, mradi awamu ya pili utanza pindi awamu ya kwanza utakapokamilika na tatizo la maji litaisha au kupungua kwa kiasi kikubwa.

EFM RADIO KUSAKATA KABUMBU NA WASANII WA BONGO FLEVA KANDA YA ZIWA

0
0
Na Ripota wa Globu ya Jamii

Zaidi ya wasanii kumi na mbili wa timu ya bongo fleva kusakata kabumbu na wadau wao wakubwa wa redio E-fm siku ya Jumamosi tarehe 25/06/2017 katika uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza katika mwendelezo wa kutambulisha masafa mapya ya EFM Radio ya 91.3 fm Mwanza.

Kwa mujibu wa taharifa iliyotlewa na afisa uhisiano wa kituo hicho, Jesca Mwanyika amesema kuwa wakali hao wa bongo fleva na Efm redio watashiriki katika mtanange huo ili kuipa jamii hamasa katika kujikita kwenye michezo mbalimbali ili kuimarisha afya zao na kuepuka hatari ya kupata magojwa yasioambukizwa.

“ mechi hii ni sehemu ya utaratibu wa E-fm ya kuwafikia wadau wao kama ilivyoada yao, vilevile kutoa wito kwa makampuni mbalimbali kuwekeza katika michezo ili kuhamasisha na kuvumbua vipaji vipya katika jamii” amesema Mwanyika .

Mechi hiyo itaenda sambamba na mazoezi ya mbio za mwendo pole (jogging) zikiongozwa na Efm jogging club, Kubandika stika vyombo vya moto, na kuweka kifaa cha kuongeza masafa katika redio za daladala kwa madereva hamsini wa kwanza kufika uwanjani.

KAMPUNI YA MAWASILIANO YA ZANTEL YAJUMUIKA NA WAFANYAKAZI NA WADAU WAKE KWA FUTARI JIJINI DAR

0
0

Afisa wa Kitengo cha Rasilimali watu Zantel, Maryam Khatri (kushoto) akitoa huduma ya chakula kwa Mkurugenzi Mkuu wa Zantel Benoit Janin (kulia) katika tafrija ya futari iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. Tafrija hiyo ilikuwa ni mahususi kwa ajili ya wafanyakazi na wadau wa kampuni hiyo.
Afisa wa Kitengo cha Rasilimali watu Zantel, Maryam Khatri (kushoto) akitoa huduma ya chakula kwa wafanyakazi wa Zantel katika tafrija ya futari iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. Tafrija hiyo ilikuwa ni mahususi kwa ajili ya wafanyakazi na wadau wa kampuni hiyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Zantel wakijumuika kupata futari katika tafrija iliyoandaliwa na Kampuni hiyo katika kipindi hiki cha mfungo Mtukufu wa Ramadhani ambayo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Benoit Janin akizungumza wakati wa tafrija ya futari maalumu iliyoandaliwa na Kampuni hiyo kwa ajili ya wafanyakazi na wadau mbalimbali katika kipindi hiki cha mfungo Mtukufu wa Ramadhani. Tafrija hiyo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam. 

Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali Watu Zantel Joanitha Mrengo akizungumza wakati wa tafrija ya futari maalumu iliyoandaliwa na Kampuni hiyo kwa ajili ya wafanyakazi na wadau mbalimbali katika kipindi hiki cha mfungo Mtukufu wa Ramadhani. Tafrija hiyo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Benoit Janin (wa kwanza kushoto) akifurahia jambo na baadhi ya viongozi wa Kampuni hiyo wakati wa tafrija ya futari iliyoandaliwa na Zantel kwa ajili ya wafanyakazi na wadau mbalimbali katika kipindi hiki cha mfungo Mtukufu wa Ramadhani. Tafrija hiyo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam. 


Baadhi ya wafanyakazi wa Zantel wakijumuika katika tafrija ya futari maalumu kwa ajili yao katika kipindi hiki cha mfungo Mtukufu wa Ramadhani. Tafrija hiyo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam
Meneja Chapa na Mawasiliano wa Zantel, Rukia Mtingwa (kushoto) akitoa huduma ya chakula kwa baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni hiyo waliojumuika na wateja na wadau mbalimbali katika tafrija ya futari iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali Watu Zantel, Joanitha Mrengo (wa pili kushoto) akitoa huduma ya chakula kwa Mkurugenzi Mkuu wa Zantel Benoit Janin (wa kwanza kulia) katika tafrija ya futari iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. Tafrija hiyo ilikuwa ni mahususi kwa ajili ya wafanyakazi na wadau wa kampuni hiyo. Anayeshuhudia (kushoto) ni Afisa wa Kitengo cha Rasilimali watu Zantel, Maryam Khatri.

JESHI LA MAGEREZA LILIVYOBEBA DHAMANA YA TANZANIA YA VIWANDA

0
0
 Na Christina R. Mwangosi, MOHA 

Jeshi la Magereza nchini ni moja kati ya Majeshi yaliyo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi yenye jukumu kubwa la msingi la kuwarekebishwa wafungwa wanaohukumiwa kwa makosa mbalimbali hapa nchini. 

Katika taratibu za Urekebishaji wa wafungwa zipo stadi mbalimbali za kilimo, ufundi na uzalishaji ambazo zinatumika  kuwarekebisha  wafungwa ili hata pale wanapomaliza vifungo vyao na kurudi uraiani waweze kutumia ujuzi walioupata katika shughuli za uzalishaji na hivyo kujiletea maendeleo yao binafsi lakini kuchangia pia katika maendeleo ya nchi yetu.
 Mbali na jukumu hilo la msingi la Jeshi hilo, pia Jeshi hili limekuwa likijishughulisha na shughuli mbalimbali za uzalishaji mali ikiwemo shughuli za kilimo kwa ajili ya chakula kwa wafungwa, utengenezaji wa samani mbalimbali kwa ajili ya matumizi ya ofisi na nyumbani, pamoja na utengenezaji wa viatu shughuli zinazofanyika katika Magereza yaliyopo hapa nchini.

Aidha Jeshi la Magereza nchini lina fursa nyingi ambazo zikitumika vizuri zinaweza   kuwa na mchango mkubwa sana katika kukuza uchumi wa nchi yetu na hivyo kufikia malengo yetu ya kuwa na uchumi wa viwanda. Miongoni mwa fursa hizo ni pamoja na ardhi nyingi yenye rutuba inayofaa kutumika kwa kushughuli za kilimo na matumizi mengineyo ya uzalishaji vikiwemo viwanda.

Kwa muda mrefu sasa jeshi la Magereza limekuwa likitumia kiwanda chake cha Utengenezaji wa Samani mbalimbali kwa ajili ya matumizi ya Ofisi na hata nyumbani kilichopo katika Gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam.
 Kwa upande wake Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza ambaye ndiye Mkuu wa Kiwanda cha Samani cha Ukonga cha Jeshi la Magereza nchini kilichopo jijini Dar es Salaam John Itambu anasema  kwa sasa kiwanda hicho kinafanya shughuli kubwa za aina mbili  ikwemo utengenezaji  wa samani mbalimbali  kwa ajili ya matumizi ya ofisini na nyumbani ikiwemo utengenezaji wa meza, viti, makabati,  vitanda,  meza za chakula na za ofisi,  pamoja na meza za chumbani maarufu kama ‘dressing table’.

Kamishna Msaidizi Itambu anasema kiwanda hicho kinatengeneza samani hizo  kwa kutumia mbao za kawaida zile za asili zenye ubora wa kiwango cha juu na zile za henzerani yaani miti ya  minazi ambazo nazo pia zina mvuto wa hali ya juu pia ikiwemo ubora pia. 

Anasema pamoja na utengenezaji wa samani kiwanda hicho pia kimekuwa kikijishughulisha na utengenezaji wa kazi za mikono ikiwemo mazulia, vikapu, ‘table mates’ pamoja na mazulia ya milangoni.
Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza Itambu ambaye ndiye msimamizi wa shughuli za Kiwanda hicho anasema pamoja na kwamba Kiwanda cha Samani cha Magereza Ukonga kimekuwa kikitengeneza samani zenye ubora wa hali ya juu lakini siku zilizopita kulikuwa na changamoto ya ucheleweshaji wa ‘Oda’  ilikuwa mteja akiagiza samani za aina fulani inachukua muda mrefu kukamilishiwa mahitaji yake wakati mwingine na ubora unakuwa umepunguwa si kwa ubora aliokuwa ameuona kwenye shughuli za Maonyesho ya Sabasaba.

Anasema kwa sasa Kiwanda hicho kimeondoa changamoto hiyo ya ucheleweshwaji na sasa  mteja anapoagiza mahitaji yake ya samani ziwe kwa matumizi ya Ofisi au nyumbani mteja anapata mahitaji yake kwa wakati na kwa ubora wa hali ya juu hakuna tofauti tena ya ubora anaotengenezewa  na ule aliouona kwenye Maonyesho ya SabaSaba.

Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza John Itambu anasisitiza kuwa changamoto kubwa inayowakabili kwa sasa ni ile ya bei za mbao kwa ajili ya kutengeneza samani zao kupatikana kwa shida kwa kuwa mafundi wengi wa mitaani hununua mbao kwa kutumia fedha taslimu na bila kupewa risiti za EFD sasa pale Jeshi la Magereza linapofuata taratibu za kupewa risiti za EFD  wauzaji wa mbao hutoa kipaumbele kwa mafundi wale wa uraiani wenye fedha taslimu badala ya Magereza, hivyo ni muhimu kwa Mamlaka husika kuendelea kutoa elimu kwa wananchi na wafanyabiashara juu ya umuhimu wa kutumia mashine ama risiti za EFD.
‘‘Pamoja na kwamba mara nyingi wateja wanaona bei za bidhaa za kiwanda chetu cha samani ziko juu lakini wataalamu wetu wanachokiangalia ni kuzalisha bidhaa kwa kutumia mbao zenye ubora wa hali ya juu miti hasa ile ya asili, na ndio maana samani zetu zinadumu kwa muda mrefu huwezi kulinganisha ubora wake na bidhaa za mitaani’’ anasisitiza Mkuu wa Kiwanda hicho John Itambu.

Anasema kwa sasa kiwanda kimeanzisha pia kitengo cha Masoko ndani ya Kiwanda chetu cha Samani ambacho kinahusika zaidi na utafutaji wa masoko, pamoja na kusimamia oda zinazotolewa na wateja wa kiwanda hicho ili ziweze kukamilishwa kwa wakati na ubora ule ule waliouona wakati wa Maonyesho ya SabaSaba.

Hata hivyo Kamishna Msaidizi John Itambu anatoa shukrani kubwa kwa Ofisi ya Rais Ikulu ambayo imekuwa ikiunga mkono kiwanda hicho cha samani kwa kununua samani kwa matumizi ya ofisi hiyo, ikiwemo pia ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi pamoja na Mali Asili na Utalii.

‘‘Pamoja na Serikali kutoa Maelekezo kwa Taasisi zote za Serikali kununua samani kwa ajili ya matumizi ya ofisi kutoka kwenye Kiwanda cha Samani cha Gereza la Ukonga bado muitikio ni mdogo bado hatujapata tenda kubwa kutoka kwenye ofisi za Serikali’’. Anaeleza Mkuu wa Kiwanda hicho Kamishna Msadizi John Itambu.

Anasema mpaka sasa wameshatengeneza samani za Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma, Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) pamoja na Ofisi za Bunge  ambao waliotoa oda ya samani kwa ajili ya ofisi za Wabunge kwenye Majimbo yao.

Pamoja utengenezaji wa samani mbalimbali, Kiwanda chetu cha Samani Ukonga Magereza kina kitengo pia kinachojishulisha na ushonaji wa nguo mbalimbali suti na mashati ya wanawake na wanaume, ovaroli pamoja na sare mbalimbali kwa ajili ya matumizi ya ofisi.

Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza John Itambu anasema kwa sasa  Kiwanda kina uwezo wa kuzalisha sare za wafungwa 300 kwa siku, hivyo Kiwanda kina uwezo mkubwa wa kupokea tenda kubwa kutoka kwa wateja mbalimbali hapa nchini.

Kamishna Msaidizi Itambu anasema Kiwanda hiki cha Ukonga  miaka mingi iliyopita kilianza na shughuli za ushonaji wa nguo kwa kushona sare za majeshi yaliyopo hapa nchini kwa kutumia wafungwa waliopo waliosimamiwa na Wataalamu waliopo ndani ya Jeshi la Magereza na kwamba awali wazo kuu lilikuwa ni kuwarekebisha wafungwa kwa njia ya kuwafundisha stadi za ushonaji baadae kiliamua kuanzisha na shughuli za utengenezaji wa samani.

‘‘Awali tulikuwa tukishona zaidi sare za Taasisi mbalimbali za Serikali kwa mfano sare za askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, askari wa Jeshi la Uhamiaji, kwa sasa Kitengo hiki kinachojishughulisha na ushonaji wa nguo mbalimbali  kimekuwa kikipata tenda za kushona sare za madereva na makondakta wa daladala pamoja na sare za askari wa Jiji la Dar es Salaam’’. Anasema Kamishna Msaidizi Itambu ambaye ndiye Mkuu wa Kiwanda cha Samani cha Ukonga Magereza Jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali Projest Rwegasira anasema Kiwanda cha Samani cha Jeshi la Magereza kilichopo Ukonga jijini Dar es Salaam ni moja kati ya  viwanda vya hapa Tanzania vinavyotengeneza samani zenye Ubora wa hali ya juu na ndio maana bidhaa zake zimekuwa zikidumu kwa muda mrefu.

Meja Jenerali Rwegasira anasema yeye binafsi ni miongoni mwa wateja wa Kiwanda hicho cha Ukonga na amekuwa akinufaika na ubora wa samani zinazotengenezwa na Kiwanda hicho kwa kuwa si kwamba zina ubora wa hali ya juu bali pia zinavutia kutokana na wataalamu wake kuwa wabunifu na utaalamu wa kisasa katika utengenezaji wa samani hizo.

Miongoni mwa wateja ambao wamewahi kununua bidhaa hizo kwenye Kiwanda hicho cha Samani cha Ukonga, Johnson Kapeu mkazi wa Mbezi Beach Jijini Dar es Salaam anasema hivi ‘‘Kwa mara ya kwanza nilihudhuria Maonyesho ya SabaSaba kati ya mwaka 2015 na 2016…nakumbuka nilihudhuria Maonyesho haya kama Mtanzania na Mtumishi wa Umma, Rais Mstaafu Kikwete alipotembelea Banda la Magereza ndipo nami nikapata nafasi ya kuona bidhaa za Magereza kweli nilivutiwa na baada ya hapo niliweka oda yangu nikabahatika kupata samani nilizohitaji kwa wakati huo ilikuwa ni Kitanda, Kabati la Nguo na Vyombo ambavyo hadi sasa ubora wake haujapungua hata kidogo. ’’ anasema Bw. Kapeu.

Kwa upande wake mmoja kati ya wananchi ambao wamewahi kushiriki Maonyesho ya SabaSaba Edson Mandira mkazi wa Ukonga jijini Dar es Salaam anasema “Ni kweli kabisa Jeshi la Magereza linatengeneza bidhaa zenye ubora wa hali ya juu na ikiwa wataalamu wake watapata fursa za kutembelea Viwanda vya nje na ndani ya nchi wanaweza kujifunza ujuzi mpya hivyo kuongeza ubunifu zaidi ambao utaendana na soko la sasa ama ushindani wa soko la sasa kwa ujumla.

‘‘Mimi binafsi navutiwa sana na ubora wa samani zinazotengenezwa na jeshi letu la Magereza ila wangeongeza ubunifu kidogo tu… sasa ukichanganya na ubora wao wa hali ya juu wanaweza wakatuzidi hata sisi mafundi wa Keko kwa kweli”. anasisitiza huku akicheka Bwana  Gosbert Remanto ambaye ni fundi seremala Keko DDC.  

Kwa upande wake Ally Abdulkarim mfanyabiashara wa samani eneo la Keko DDC anasema “Binafsi naona Samani za kiwanda cha Magereza ni nzuri ila ndugu mwandishi wenzetu hawa wakiongeza ubunifu kwenye “Finishing”  na kuongeza ubunifu wa kisasa … ndugu mwandishi wakifanikiwa hapo tu wenzetu hawa watafika mbali sana na bidhaa zao zitatuacha tu … 

zitakimbiliwa hapa nchini kwa sababu ya ubora wa hali ya juu,  unajua hawa wenzetu kwenye mbao sio wababaishaji kama sisi huku mtaani. 
Naye Mkuu wa Jeshi la Magereza Nchini, Kamishna Jenerali Dk. Juma Malewa anasema kuwa “Kutokana na Serikali kuhamishia Makao Makuu ya Nchi yetu Mkoani Dodoma  ni wazi kutakuwa na uhitaji mkubwa wa samani kwa ajili ya matumizi ya ofisi na hata majumbani, hivyo Jeshi la Magereza litajenga Kiwanda  kipya kikubwa cha samani  Dodoma ili kukidhi mahitaji halisi ya samani hizo,’’ anasisitiza  Dk. Malewa.

Dr. Malewa anasema ili kukidhi mahitaji halisi  ya samani kwa ajili ya Makao Makuu ya Nchi  yetu  jeshi lina mpango wa kununua vifaa hususani mashine za kisasa  zitakazoweza kuzalisha  samani kwa wingi zaidi na hivyo kutosheleza  mahitaji  ya samani mjini Dodoma.

Hivi karibuni  Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhandisi Hamad Masauni,  akikagua moja ya miradi ya Jeshi la Magereza mkoani Dodoma alisema miradi mingi ambayo inaendeshwa na Jeshi la Magereza nchini kikiwemo kiwanda cha samani cha Gereza  la Ukonga cha jijini Dar es Salaam, kama serikali itasaidia katika kuiwezesha, italisadia taifa kupiga hatua na kuingia katika uchumi wa viwanda.

Wadaiwa Kodi ya Majengo kuburuzwa Mahakamani

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo katika kikao kazi cha kuhamasisha ulipaji wa Kodi ya Majengo.
Meneja wa Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Arusha Ndg. Apili Mbarouk akizungumza katika kikao na wanahabari cha kuwakumbusha wananchi kuhusu ulipaji wa Kodi ya Majengo.
Baadhi ya wataalam waliohudhuria katika Kikao cha Mkuu wa Mkoa kuhamasisha uhamasishaji wa Kodi ya Majengo.

Nteghenjwa Hosseah, Arusha.

Wadaiwa sugu wa Kodi ya Majengo katika Jiji la Arusha watafikishwa Mahakamani mwanzoni mwa mwezi Julai endapo wataendelea kukaidi kutolipa Kodi hiyo katika kipindi hiki cha mwisho wa mwaka wa Fedha 2016/2017 unaomalizika Juni 30.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo katika kikao chake na waandishi wa habari kuwukumbusha wananchi kuhusu umuhimu wa kulipa kodi hiyo mapema kabla ya hatua kazi hazijachukuliwa wale ambao hawajalipa.

Alisema wamiliki wote wa majengo wanatakiwa kulipa Kodi hiyo kwa mujibu wa Sheria lakini hali hairidhishi kwani wengi wao hawajajitokeza kulipa wakati Serikali inategemea Fedha hizo kwa ajili ya Kutekeleza Miradi mbalimbali ya Maendeleo.

Aliongeza kuwa muda uliowekwa kwa ajili ya malipo hayo unaelekea ukikongoni:  Juni 30 itakua ni mwisho na baada ya hapo Sheria kali za Kisheria zitaanza kuchukuliwa kwa wote watakaobainika kuiibia Serikali kwa kutolipa mapato ya majengo wanayoyamiliki.

“Haiwezekani unamiliki nyumba halafu hutaki kuchangia kodi, ninatoa rai kwa wote kulipa kwa hiari kwa sababu baada ya hapo ni Faini ambayo ni mara tano ya kiasi kile ambacho ungetakiwa kulipa kwa sasa au kupelekwa Mahakami kwa mujibu wa Sheria.

Naye Meneja wa Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Arusha Ndg. Apili Mbarouk amesema mpaka Mwishoni wa Mwezi Mei walikuwa wameshafanikiwa kukusanya kiasi cha Tsh Bil.1  na kwa siku zilizobakia wanatarajia kukusanya zaidi ya kiwango walichokusanya kwa sasa.

Pia aliongeza kuwa katika maeneo yote ambayo hayajapimwa na kufanyiwa uthamini wamiliki watalipa Tsh 15,000 kwa mwaka na kwa yale maeneo ambayo yamefanyiwa uthamini wamiliki watalipa kwa kadiri ya thamani ya Majengo yao.

Aidha aliwataka wafanyabiashara na wananchi wote kutoa na kudai risiti kwa kila biashara inayofanyika ili kuhakikisha mapato ya Serikali yanakuwa salama na hayapotei kwa namna yeyote ile.

Katika hili tutaanza ukaguzi katika maeneo yote ya Mji huu kuanzia kwa wafanyabiashara kuhakikisha wanatoa stakabadhi kwa wateja wao na ambaye atabainika hajatoa atapigwa faini ta Tsh Mil 3 na kwa mwananchi ambaye atakuwa amenunua bidhaa bila kudai stakabadhi atatozwa faini ya Tsh 30,000.

Kikao hiki ni muendelezo ya vikao maalumu vya Kazi anavyovifanya Mkuu wa Mkoa wa Arusha pamoja na Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Areusha kuhakikisha mapato ya Serikali yanakusanya kwa ufanisi ili kufikia malengo waliyojiwekea.

TANGAZO LA AJIRA CLEANEX INTERNATIONAL

0
0

ZIARA YA KIMAFUNZO YA MAAFISA WA POLISI KUTOKA CHUO CHA ULINZI RWANDA

0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akizungumza na mkuu wa chuo cha ulinzi cha Taifa cha Rwanda Kamishina wa Polisi wa Rwanda Felix Namhoranye ofisini kwake makao makuu ya Jeshi la Polisi. Kamishina Namhoranye ni kiongozi wa msafara wa maafisa mbalimbali kutoka chuo cha ulinzi cha Taifa cha Rwanda ambao wapo nchini kwa ziara ya mafunzo. Picha na Hassan Mndeme – Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akizungumza na maofisa wa polisi kutoka nchi mbalimbali za Afrika mashariki na Afrika magharibi ambapo wanasoma chuo cha ulinzi cha Taifa cha Rwanda hawapo picha. Kushoto ni mkuu wa chuo cha ulinzi cha Taifa cha Rwanda, Kamishina Felix Namhoranye na kulia ni Kamishina wa Polisi Jamii , Mussa Alli Mussa – picha na Hassan Mndeme – Jeshi la Polisi.
Baadhi ya maafisa wa Polisi kutoka nchi mbalimbali za afrika mashariki na magharibi wanaosoma chuo cha ulinzi wa taifa cha Rwanda wakimsikiliza Mkuu wa Jeshi la Polisi wa Tanzania makao makuu ya Jeshi la ( hayupo picha ) wakati wa ziara yao ya mafunzo hapa nchini. Picha na Hassan Mndeme – Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akiwa katika picha ya pamoja na maafisa wa Polisi kutoka nchi mbalimbali wanaosoma chuo cha ulinzi wa taifa cha Rwanda. Ujumbe huo unaohusisha maofisa wa Polisi kutoka nchi za Afarika mashariki na Afrika magharibi unaongozwa na Kamishina wa Polisi wa Rwanda Felix Namhoranye ambaye ndiye mkuu wa chuo cha ulinzi cha ulinzi cha Rwanda wapo nchini Tanzania kwa ziara ya kijifunza namna taasisi mbalimbali zinavyoendeshwa hapa Tanzania. Picha Hassan Mndeme – Jeshi la Polisi.

Airtel yaleta TABASAMU, yazindua vocha ya shilingi 200 nchini

0
0
Meneja Masoko ya Airtel, Anethy Muga (kulia) na Meneja wa chapa wa Airtel, Arnold Madale (kushoto) wakionyesha vocha mpya ya Airtel Tabasamu itakayouzwa kwa bei ya shilingi mia mbili tu. Katikati  ni Meneja  Uhusiano wa Airtel , Jackson Mmbando .

Meneja Masoko ya Airtel , Anethy Muga( kulia) akiongea wakati wa uzinduzi wa vocha mpya ya Airtel Tabasamu ambayo ni maalumu kwa wateja wa Airtel wa malipo ya awali nchini. (kushoto) Meneja wa chapa wa Airtel , Arnold Madale na (katikati) Meneja Uhusiano wa Airtel , Jackson Mmbando . Vocha hiyo itapatikana kuanzia sasa kupitia maduka yote ya Airtel , wakala na wachuuzi wa vocha za Airtel nchi nzima.

Meneja Uhusiano wa Airtel , Jackson Mmbando (kati) akitoa ufafanuzi juu ya vocha mpya ya Airtel Tabasamu ambayo ni maalumu kwa wateja wake wa malipo ya awali nchini. (kushoto) Meneja wa chapa wa Airtel , Arnold Madale na Meneja Masoko ya Airtel , Anethy Muga (kulia). Vocha hiyo itapatikana kuanzia sasa kupitia maduka yote ya Airtel , wakala na wachuuzi wa vocha za Airtel nchi nzima.
 
· Airtel wazindua vocha ya kiwango cha chini kabisa kwa wateja wa simu za mkononi

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imezindua vocha mpya ya muda wa maongezi kwa wateja wake wa malipo ya awali nchini itakayowaongezea wateja wake TABASAMU pale wanapopiga simu au kuitumia kwa matumizi yoyote ya kuwasiliana au kujiunganisha kwenye vifurushi vya gharama nafuu.

Vocha hiyo mpya ya TABASAMU kwa shilingi 200 inapatikana kwa wachuuzi wote wa vocha za Airtel na kuwawezesha wateja wa Airtel na watanzania wote watakaojiunga na Airtel kumudu gharama za mawasiliano wakati wowote kwa gharama nafuu zaidi

Akiongea wakati wa uzinduzi, Meneja Masoko wa Airtel , Bi Aneth Muga alisema “ Leo tunajisikia fahari kuzindua na kuitambulisha sokoni vocha ya muda wa maongezi ya shilingi 200 itakayowapatia wateja Tabasamu na uhuru wa kuwasiliana na ndugu jamaa marafiki au wale wajasiliamali kuweza kuitumia kupanga mipango yao wakati wowote mahali popote kwa gharama nafuu”

“Tunatambua mawasiliano ya simu ni muhimu katika kuendesha shughuli zetu za kila siku na hivyo kuboreshwa kwa viwango vya vocha kutasaidia sana kuchochea upatikanaji wa huduma ya mawasiliano kwa wote. Tunataka kuendelea kutoa huduma bora za kibunifu na zenye kukidhi mahitaji ya wateja wetu huku tukiwawezesha kutatua changamoto zao za kila siku”. Alieleza Bi, Muga

“Tunaamini kwa kuwezesha upatikanaji wa vocha za shilingi 200 sokoni tumewawezesha zaidi ya watanzania milioni 10 kuunganishwa na huduma za mawasiliano na kufurahia ofa mbalimbal zinazotolewa na Airtel. Aliongeza muga

Ili kuingia vocha ya muda wa maongezi mteja atapiga *104* kisha kuingiza namba zilizokwanguliwa na kubonyesha alama ya reli # na kisha OK. Vocha hiyo itaingia moja kwa moja kwenye Salio lake la kupiga simu na mteja ataamua kuitumia kwa kupiga simu au kujiunga na kifurushi cha shilingi 200 kwa kupiga *149*99#.
Viewing all 46201 articles
Browse latest View live




Latest Images