Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46205 articles
Browse latest View live

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AKABIDHIWA VIFAA TIBA VYA UZAZI ZAIDI YA 200 NA BALOZI WA KUWAIT HAPA NCHINI

0
0

Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan akitazama moja ya Dawa,mara baada ya kukabidhiwa mapema leo Ikulu jijini Dar,vifaa tiba vya uzazi zaidi ya 200 na Balozi wa Kuwait hapa nchini,Mhe,Jasem Al-Najem,vifaa hivyo vitasambazwa katika hospitali mbalimbali kwa Tanzania Bara na Zanzibar.

Balozi wa Kuwait hapa nchini Jasem Al- Najem amemkabidhi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan vifaa tiba vya uzazi zaidi ya 200 ambavyo vitasambazwa katika hospitali mbalimbali kwa Tanzania Bara na Zanzibar.

Makabidhiano ya vifaa hivyo vya uzazi yamefanyika leo Ikulu ya Dar es Salaam ambapo Balozi wa Kuwait hapa Nchini Jasem Al- Najem amesema Serikali ya nchi hiyo imetoa vifaa hivyo kama hatua ya kuendelea kudumisha na kuendeleza mahusiano mazuri kati ya nchi hiyo na Tanzania.

Amesema kuwa Serikali ya Kuwait imetoa vifaa hivyo ikiwa ni awamu ya kwanza na lengo ni kutoa vifaa hivyo zaidi ya 1000 vyenye thamani ya shilingi milioni 40 kwa wanawake wajawazito na waliojifungua katika hospitali mbalimbali nchini.

Mara baada ya kupokea msaada huo, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ameishukuru Serikali ya Kuwait kwa msaada huo ambao utasambazwa katika hospitali mbalimbali kwa Tanzania Bara na Zanzibar.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema msaada huo utasaidia sana wanawake wajawazito na waliojifungua kupata vifaa za uzazi ambavyo vinahitajika wakati wanamke mjamzito anapojifungua na baada ya kujifungua.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa vifaa hivyo vitaanza kusambazwa kuanzia mwezi huu na mchakato wa kuainishwa hospitali zitakazopata msaada huo unaendelea.

Makamu wa Rais pia amesisitiza kudumishwa kwa mahusiano mazuri yaliyopo kati ya nchi ya Kuwait na Tanzania kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa pande zote Mbili.

Aidha Balozi huyo wa Kuwait hapa nchini Jasem Al- Najem amemhakikishia Makamu wa Rais kuwa Serakali ya Kuwait itaendelea kusaidia Serikali ya Tanzania katika uimarishaji wa sekta ya afya na elimu nchini ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na za msingi

TAMKO LA SERIKALI KUHUSU MATUMIZI YA PICHA ZA MARAIS WASTAAFU KATIKA MAGAZETI NA MITANDAO YA KIJAMII KUHUSU SAKATA LA USAFIRISHAJI WA MCHANGA WA MADINI NJE YA NCHI

0
0


RE: ETIHAD AIRWAYS APPOINTS NEW GENERAL MANAGER IN OMAN

0
0

ETIHAD AIRWAYS APPOINTS NEW GENERAL MANAGER IN OMAN
 
Etihad Airways, the national airline of the United Arab Emirates (UAE), has announced the appointment of Hassan Al Yousuf as its new General Manager for the Sultanate of Oman.  
       
Based at the airline’s offices in Muscat, Hassan is responsible for leading Etihad Airways’ commercial operations in Oman, as it continues to grow its presence and operations across the region.
 
Hassan was previously based in Perth, Australia, as an Assistant General Manager, leading the team in achieving its revenue targets for 2016 and driving collaboration with Etihad Airways’ equity partner, Virgin Australia.
 
Hareb Al Muhairy, Etihad Airways’ Senior Vice President Sales in the UAE & GCC, said:  “Hassan’s promotion is a recognition of his hard work and we are delighted to have him drive our continued commercial success in Oman.
 
“Etihad Airways is committed to developing and rewarding the hard work of our Emirati aviation leaders.”
 
During his career, Hassan has shown strong commercial, strategic, analytical and leadership skills. Prior to this position, Hassan was a Pricing Manager for the Indian Subcontinent (ISC) and Central Asia, tasked with achieving greater revenue generation for the region.
 
Hassan is a UAE national and holds a Master’s in Business Administration. He joined the airline in December 2010 as a Graduate Manager and brings with him over six years’ of aviation experience.
 
Etihad Airways, which began flying to Muscat in March 2006, currently operates three daily flights between Abu Dhabi and the capital of Oman. The service provides passengers with connections between Oman and the UAE, and wider access to key destinations across Etihad Airways’ global network including the Indian Subcontinent, Asia, Europe and North America. The services combine with two new daily services operated by its codeshare partner, Oman Air.

SERIKALI YAIONGEZEA BAJETI TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA NCHINI.

0
0
Na Benny Mwaipaja, WFM-Dodoma

Serikali imeiongezea Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini kiasi cha shilingi bilioni 2.6 katika Bajeti yake ya mwaka 2017/2018 kwa kutambua na kuthamini majukumu yake katika Taifa.

Kauli hiyo imetolewa Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango (MB),Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maaluum (CCM), Mhe. Mwantumu Dau Haji aliyetaka kujua mpango wa Serikali kuiwezesha Tume hiyo kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Mhe. Mwantumu Haji amesema kuwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imekuwa ikitengewa fedha kidogo sana katika bajeti kwa zaidi ya miaka mitatu mfululizo hali inayosababisha Tume hiyo kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

Akijibu swali hilo, Dkt. Kijaji alisema kuwa katika mwaka wa fedha 2017/18, Serikali imetenga bajeti ya Sh. 6,166,978,000 kwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 42.31 ya bajeti ya mwaka 2016/17 ambayo ilikuwa Sh. 3,557,589,200.

Alisema kuwa viwango vya ukomo wa bajeti kwa mafungu, hutegemea vipaumbele vya Taifa na maoteo ya mapato katika kipindi husika hivyo ongezeko la ukomo wa bajeti ya Tume hiyo kwa mwaka 2017/18 linaonesha dhahiri kuwa Serikali inatambua umuhimu wa Tume hiyo pamoja na majukumu yake.

Dkt. Kijaji aliongeza kuwa Serikali inaendelea kuimarisha mikakati ya ukusanyaji wa mapato ya ndani il kuhakikisha mafungu yote ya kibajeti ikiwemo Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora yanaendelea kupata fedha za kutosha ili kutekeleza majukumu yao kikamilifu.

“Napenda kulitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba, tarehe 01/06/2017 Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alizindua mfumo wa ukusanyaji mapato ya ndani ujulikanao kama ‘Revenue Gateway System’ ikiwa ni moja ya mikakati ya Serikali kuimarisha ukusanyaji mapato yake yatakayowezesha upatikanaji wa fedha za kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi”, alifafanua Dkt. Kijaji.

RAIS DKT MAGUFULI ATEUA MWENYEKITI WA BODI YA KITUO CHA UWEKEZAJI TANZANIA (TIC).

0
0

KOCHA MKUU WA STARS MAYANGA ATANGAZA KIKOSI CHA COSAFA

0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Kocha Mkuu wa timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Salum Shabani Mayanga, leo Jumatano Juni 14, 2017 ametangaza majina ya wachezaji 22 watakaounda kikosi kinachokwenda kushindana kuwania Kombe la Castle Cosafa nchini Afrika Kusini.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Bia ya Serengeti, inatarajiwa kuanza kambi rasmi kesho Jumapili Juni 18, mwaka huu. Kambi hiyo itakuwa kwenye Hoteli ya Urban Rose, iliyoko Mtaa wa Jamhuri katikati ya jiji la Dar es Salaam.

 Afisa habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) Alfred Lucas amesema kuwa kikosi hicho ambacho kimechaguliwa kimeweza kuongeza baadhi ya wachezaji wengine ikiwa pia ni katika kukiandaa kikosi hicho kwa ajili ya Michuano ya Mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN).

Lucas amesema Taifa Stars inajiandaa na michuano ya Cosafa inayotarajiwa kuanza  Juni 25, mwaka huu. Michuano hiyo, inaandaliwa na Baraza la Mpira wa Miguu la nchi za Kusini mwa Afrika ambako Tanzania - mwanachama wa Cecafa, imepata mwaliko kushiriki.

Tanzania imepangwa kundi A ambako wapinzani wake ni Mauritius, Malawi na Angola wakati Kundi B ni Msumbiji, Shelisheli, Madagascar na Zimbabwe. Timu za Botswana, Zambia na Afrika Kusini kadhalika Namibia, Lesotho na Swaziland zitakuwa na mechi maalumu (play off) ili kuingia robo fainali.

Lucas amesema kwa mujibu wa Mayanga, kikosi hicho kinaundwa na makipa Aishi Salum Manula (Azam FC), Benno David Kakolanya (Young Africans SC) na Said Mohammed Said (Mtibwa Sugar FC).

Walinzi wa pembeni upande wa kulia ni Shomari Salum Kapombe (Azam FC) na Hassan Hamis Ramadhan ‘Kessy’ (Young Africans SC) wakati upande wa kushoto wapo Gadiel Michael (Azam FC) na Amim Abdulkarim (Toto Africans FC).

Walinzi wa kati ni Erasto Nyoni (Azam FC), Salim Hassan Abdallah (Mtibwa Sugar), Abdi Banda (Simba SC) na Nurdin Chona (Tanzania Prisons) wakati viungo wa kuzuia kuwa ni Himid Mao (Azam FC) na Salmin Hoza wa Mbao FC.

Kadhalika wako viungo wa kushambulia ambao ni Mzamiru Yassin Selembe (Simba), Simon Happygod Msuva (Young Africans SC), Raphael Daudi (Mbeya City) na Shizza Ramadhani Kichuya (Simba SC).

Katika safu ya ushambuliaji wamo Thomas Emmanuel Ulimwengu (AFC Eskilstuna – Sweden), Mbaraka Abeid Yusufu (Kagera Sugar), Stamili Mbonde, Elius Maguli (Dhofar SC) na Shabani Idd Chilunda (Azam FC).
Afisa habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) Alfred Lucas 


WAKAZI WA MJI WA SONGEA WAJITOKEZA KWA WINGI KUCHANGIA DAMU

0
0
Kila ifikapo juni 14 ya kila mwaka ni siku ya kuchangia damu kwa hiari ,katika mkoa wa ruvuma Wakazi wa manispaa ya songea wamejitokeza kwa wingi kuchangia damu Lakini licha ya wananchi kujitokeza kwa wingi manispaa ya MANISPAA YA SONGEA yakabiliwa na uhaba wa damu katika hospitali ya RUFAA YA MKOA WA SONGEA,KITUO CHA AFYA MJIMWEMA kama anavobainisha msimamizi wa shughuli za mahabara MAGRETHI NGONYANI. HABARI KAMILI HII HAPA VIDEO YAKE.

MAKONDA KUBADILI JESHI LA POLISI KWENDA KISASA KATIKA KUKABILIANA NA UHALIFU

0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amesema jeshi la Polisi katika Mkoa huo linatakiwa  kuwa la mfano wa kuigwa katika kukabiliana na kila wimbi la uhalifu, ili wananchi waishi kwa amani kutokana na umuhimu wa biashara.

Makonda ameyasema hayo leo wakati wa kupeleka magari  26 ya polisi  kwenye ukarabati katika gereji  iliyoko  maeneo ya Utalii mkoani Kilimanjaro, kwa ajili ya matengenzo pamoja na ufungaji wa Kamera katika magari  hayo alipokuwa anazungumza na jeshi la polisi leo  Osterbay  jijini Dar es Salaam.

Amesema katika kukabiliana na rushwa na jeshi hilo, watafunga kamera katika kila kituo ndani ya jiji la Dar es Salaam,  ambapo OCD , kanda maalumu, pamoja  na Mkuu wa Jeshi la Polisi  wataweza kuona kile ambacho kinafanyika. 

Makonda amesema jeshi la Polisi Mkoa wa Dar es Salaam linatakiwa kuwa la kisasa zaidi katika kukabiliana na uhalifu wa kila namna ikiwa ni pamoja na kuwa na vifaa vya kisasa.

Amesema katika maboresho hayo wataweka Kompyuta kila kituo ili  kuachana na kuandika maelezo katika karatasi na mtu yeyote,  baada ya kuwekwa kompyuta hizo asikubali kuandikiwa maelezo katika karatasi.
Aidha amesema kuna baiskeli ziko njiani ambazo zitagawiwa kwa polisi ikiwa ni sehemu ya kukabiliana na uhalifu katika mazingira ambayo kifaa hicho kinaweza kupita.

 Nae Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya  amesema Jeshi la Polisi kanda maalumu inakabiliwa na changamoto ya magari pamoja na mafuta na kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi katika kukabiliana na wahalifu wa kila namna .

Amesema kuwa kutokana maboresho hayo yataweza kubadilisha hata takwimu zilizo katika kipindi hiki zisirudie kutokana na maboresho hayo.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza na watendaji  mkoa  na polisi katika hafla ya upelekaji wa gari 26 ya jeshi la polisi katika matengenezo mkoani Kilimanjaro leo jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya (wa pili kutoka kulia) akitoa ufafanuzi kuhusu magari yaliyoharibika  kwa ajili ya kwenda katika matengenezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda  (kulia) na watatu kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni , Ally Hapi leo katika Kituo cha Polisi Osterbay jijini Dar es Salaam.
 Moja ya gari mbovu ya Polisi ikiwa tayari kwa kusafirishwa kwa ajili matengenezo mkoani Kilimanjaro katika hafla iliyofanyika katika Kituo cha Polisi cha Osterbay jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akiwa katika picha ya pamoja  Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa pamoja na Wanajeshi wataopeleka magari kwa ajili ya matengenezo mkoani Kilimanjaro katika hafla iliyofanyika leo katika kituo cha Osterbay jijini Dar es Salaam.


MAKAMU WA RAIS APOKEA TAARIFA YA KIKOSI KAZI KUTOKA MBEYA

0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea taarifa kutoka kwa Mkuu wa mkoa wa Mbeya Ndugu Amos Makala ya kikosi kazi cha mkoa wa Mbeya kuhusu mapendekezo ya marekebisho ya mpaka kati ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na Vijiji kati ya Wilaya ya Mbarali na Chunya (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mkuu wa mkoa wa Mbeya Ndugu Amos Makala wakati wa uwasilishwaji wa taarifa ya kikosi kazi cha mkoa wa Mbeya kuhusu mapendekezo ya marekebisho ya mpaka kati ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na Vijiji kati ya Wilaya ya Mbarali na Chunya (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza mbele Mkuu wa mkoa wa Mbeya Ndugu Amos Makala pamoja na kikosi kazi chake wakati wa uwasilishwaji wa taarifa ya kikosi kazi cha mkoa wa Mbeya kuhusu mapendekezo ya marekebisho ya mpaka kati ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na Vijiji kati ya Wilaya ya Mbarali na Chunya (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na  Mkuu wa mkoa wa Mbeya Ndugu Amos Makala pamoja na kikosi kazi chakemara baada ya kupokea  taarifa ya kikosi kazi cha mkoa wa Mbeya kuhusu mapendekezo ya marekebisho ya mpaka kati ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na Vijiji kati ya Wilaya ya Mbarali na Chunya (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amewaagiza Wakuu wa wilaya nchini kuchukua hatua stahiki katika kulinda na kuhifadhi mazingira katika wilaya zao ili kukabiliana uharibifu mkubwa wa mazingira kwenye misitu na vyanzo vya maji ili visikauke na kuleta athari kwa binadamu na viumbe wengine.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo mara baada ya kukabidhiwa Taarifa ya Kikosi Kazi cha Mkoa wa Mbeya na Mkuu wa mkoa wa huo Amos Makalla kuhusu Mapendekezo ya Marekebisho ya mpaka kati ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na Vijiji katika wilaya za Mbarari na Chunya - Ikulu, Jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema tatizo la uharibifu wa mazingira katika baadhi ya wilaya nchini ni kubwa hivyo kuna umuhimu mkubwa kwa Wakuu wa wilaya kwa ushirikiano na watendaji wengine katika kukabiliana na hali hiyo kwenye maeneo yao.

Amesema kabla ya hatua kuchukuliwa ni vizuri wananchi wakaelimishwa kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa mazingira kabla ya kuondolewa kwenye maeneo waliyovamia ikiwemo maeneo ya vyanzo vya maji.

Makamu wa Rais pia amepongeza timu ya wataalamu wa kikosi kazi cha Mkoa wa Mbeya kwa kazi kubwa na nzuri waliyoifanya inayolenga kuokoa mfumo wa ikolojia katika Bonde la Mto Ruaha Mkuu.

Kwa upande wake, Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla amemweleza Makamu wa Rais kuwa aliamua kuunda kikosi kazi hicho kwa ajili ya kushughulikia mgogoro wa mpaka kati ya wananchi wa wilaya ya Chunya na Mbarali na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, uharibifu wa mazingira na upotevu wa maji kwenye Mto Ruaha Mkuu.

 Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla baada ya kukabidhi taarifa ya kikosi kazi kwa Makamu wa Rais amesema kikosi kazi hicho kimependekeza vijiji Tisa kati ya 33 ambavyo vina mgogoro na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha viondolewe kabisa kwenye eneo la hifadhi na vijiji vingine Vinne vinatakiwa kufutwa na wananchi kuhamishwa kwenye maeneo hayo na Serikali itawalipa fidia na kuratibu eneo watakapohamishiwa.

SERIKALI YAJIDHATITI KUTOKOMEZA MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE KUFIKIA 2020.

0
0

NA WAMJW  DAR ES SALAAM

 SERIKALI imejidhatiti kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ili kutimiza malengo ya kujenga uchumi wa viwanda na afya bora mpaka kufikia 2020.

Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Kambi wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka unaolenga kupitia shughuli za mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.

“Tunataka mpaka kufikia 2020 tuwe tumetokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi  kipaumbele  kama mabusha na matende ili kuweza kuinusuru nchi katika aina hii ya magonjwa yanayojitokeza katika nchi zinazoendelea hususan Tanzania” alisema Prof. Kambi.

Aidha Prof. Kambi amesema kuwa licha ya kudhibiti mabusha na matende pia wamejidhatiti kuzuia ugonjwa wa usubi na kichocho kabla ya kufikia 2025 ili kuendana na mpango wa dunia wa kudhibiti magonjwa hayo.
Kwa upande wake Mratibu wa Mpango wa Taifa Wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Dkt. Upendo Mwingira amesema kuwa wananchi wanatakiwa wajitokeze kupata dawa na tiba za magonjwa hayo kwan hazina madhara kwa binadamu.

Mkutano huo uliokutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya afya  kutoka duniani kote umelenga kupata mpango kazi wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa mwaka 2017 na 2018 ili kuweza kupata njia za kudhibiti magonjwa hayo kama vile mabusha na matende, kichocho na usubi.
Mganga Mkuu wa Serikali Prof Bakar Kambi akiwasirisha mchango wake mbele ya wadau wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele (Hawako kwenye picha) katika  mkutano wa mwaka wa mapitio ya shughuli za mpango wa Taifa wa wa udhibiti wa magonjwa hayo uliyofanyika Kunduchi jijini Dar Es salaam.
Mratibu wa Mpango wa taifa wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Dkt Upendo Mwingira akifuatilia kwa ukaribu mjadala uliokuwa ukiwasilishwa na Mganga Mkuu wa Serikali Prof Bakar kambi (hayupo kwenye picha) katika mkutano wa mwaka wa mapitio ya shughuli za mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele, anaefuatia ni Mkurugenzi wa Idara ya Afya TAMISEMI Dkt. Ntuli  Kapologwe na mkurugenzi wa kinga  Dkt Neema Ruzibamayila.
Wadau kutoka nchi mbali mbali wakifuatilia mjadala kwa ukaribu katika mkutano wa mwaka wa mapitio ya shughuli za mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele uliofunguliwa na Mganga Mkuu wa Serikali Prof Bakar Kambi (Hayupo kwenye Picha) uliyofanyika Kunduchi jijini Dar Es salaam.
Wadau wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele wakiwa kwenye picha ya pamoja ikiongozwa na Mganga Mkuu wa Serikali Prof Bakar Kambi katika mkutano wa mwaka wa mapitio ya shughuli za mpango wa Taifa wa magonjwa hayo uliyofanyika Kunduchi jijini Dar Es salaam.

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU D9 CLUB

0
0

Watumiaji wa Jumia Travel kwenye simu waongezeka kwa 33%

0
0
Dar es Salaam, Juni 14, 2017.Jumia Travel kwa kushirikiana na Google wameachia matokeo ya utafiti kuhusu maendeleo ya programu za mtandaoni (Progressive Web App - PWA) kwa kulinganisha na matumizi ya programu za kawaida za Android na IOS.

Ripoti ya utafiti huo inaonyesha kwamba kufuatia uimarishwaji kwenye vipengele vyote vya PWA, kampuni imeweka wazi kwamba kumekuwa na ongezeko la watumiaji wapya kwa 33% ukilinganisha na tovuti ya simu iliyopita. Pia kitu kingine cha kuzingatia ni kwamba kutokana na maboresho mapya kwenye PWA yameonyesha idadi ya watumiaji imeizidi ile programu ya awali kwa zaidi ya mara 12 na inazidi kukua, wakati nusu ya idadi ya watumiaji waliokuwa wanatembelea mtandao na kuondoka imepungua.      

Timu ya Jumia imeitengeza upya tovuti yake ya kwenye simu za mkononi kwa kutumia teknolojia za PWA na matokeo ya utafiti huu yameonyesha mafanikio mapya yaliyojieonyesha hususani katika nyanja za uhifadhiji wa nafasi, ukaachi wa chaji wa betr na matumizi ya data ya intaneti. Uunganishwaji wa mfumo wa PWA kwenye tovuti ya Jumia kwenye simu umechochea matokeo mazuri zaidi kwa watumiaji, kuongezeka kwa watumiaji na hasa, kupungua kwa kiwango cha wasiokuwa wakitumia mtandao.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Jumia Travel, Bw. Paul Midy amesema kuwa, “Tunafanya kazi kwenye soko lililotawaliwa kwa kiasi kikubwa na watumiaji wa simu, kwa hiyo tunalenga kuleta teknolojia ya kisasa kabisa inayolenga kutumika kwenye masoko yote hata maeneo ambayo kasi ya intaneti ina changamoto.”

Ameendelea kwa kusema kuwa lengo la kampuni ni kuiinua teknolojia na kuendelea kuwekeza kwenye rasilimali zitakazowaletea matokeo mazuri watumiaji, “Afrika ni soko ambalo linatumia simu kwa kiasi kikubwa, ndiyo kwanza tunaanza, na tunaamini kwa kuwatengenezea mazingira mazuri na rafiki ya matumizi ya simu ni jitihada kubwa katika kuyatimiza mahitaji ya wateja wetu.”

Naye kwa upande wake Meneja Mkaazi wa Jumia Travel Tanzania, Bi. Fatema Dharsee ameongozea kuwa, “Matokeo ya utafiti huu uliofanywa na Google kwa kushirikiana nasi ni ishara nzuri kwetu kuonyesha kwa namna gani tunavyokuwa hususani katika maboresho ya huduma zetu. Ukizingatia kwamba watumiaji wa simu za mkononi mpaka hivi sasa Tanzania wapo zaidi ya milioni 40, ambayo ni sawa na ueneaji wa asilimia 83. Matumizi hayo kwa kiasi kikubwa yamechochewa na ueneaji wa intaneti ambao umekua na kufikia asilimia 19.86 kwa mwaka 2016 kutokea asilimia 17.26 mwaka 2015 nchi nzima kwa mujibu wa ripoti ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).”

“Ripoti inasema kwamba mtandao wa Jumia Travel kwenye simu za mkononi umeongezeka kuwa na watumiaji kwa 33%, idadi ya watumiaji wanaoutembelea na kuondoka imepungua kwa 50%, idadi ya watumiaji imeongezeka mara 12 ukilinganisha na ya wale wa Android na IOS, inatumia kiwango cha data mara tano chini zaidi, kiwango cha data kinachotumika katika kufanya miamala ni mara mbili chini zaidi, wakati nafasi inayohitajika kuihifadhi kwenye simu imepungua kwa mara 25 chini zaidi na pia ni rahisi zaidi kufanya maboresho ya mara kwa mara. Hivyo basi, takwimu zote hizi ni dhahiri kwamba maboresho ya kurahisisha huduma zetu hayana kikomo na Google wamelidhihirisha hilo kupitia ripoti yao ya kitaalamu zaidi juu ya programu yetu,” alihitimisha Bi. Dharsee.    

Ripoti iliyotolewa na Kituo cha Kimataifa cha Data (IDC) inaonyesha kwamba Afrika kiwango cha uingizwaji wa simu za mkononi kimeongezeka kwa kasi kwenye kila robo ya mwaka, na soko linatarajiwa kuongezeka maradufu, na hivyo kuchangia thelethi moja ya simu zote zinazosafirishwa kufikia mwishoni mwa mwaka 2017. Hii itazidi kuimarisha zaidi idadi ya wateja wanaopendelea kufanya manunuzi kwa njia ya simu. Pia ni tahadhari zaidi kwa wadau wa sekta ya biashara mtandaoni kuendana na mpango mkakati wa kutumia simu zaidi katika kuendesha shughuli zao.

FUTURU BURE NA NIKOHUB

0
0
HABARI ya mjini kwa sasa ni hii, ambayo imeingizwa na Kampuni ya Nikohub, inayokuwezesha mtu yoyote mahali ulipo kuweza kufuturu bure kwenye mwezi huu wa Ramadhani.
 
Kampuni ya Nikohub, inakuwa ya kwanza nchini kuungana na Waislamu wote kwenye mwezi huu Mtukufu wa Mfungo wa Ramadhani, ambapo kwa kuzingatia umuhimu wa kila mmoja aliye kwenye mfungo huo, kushiriki naye kwa kumuwezesha kupata futari bure popote pale alipo.

“Kufuatia ukuaji wa mfumo wa Sayansi na Teknorojia hapa nchini, Nikohub tunakuwezesha kufuturu mahali popote endapo tu utaweza kujiunga nasi kwa ku-download App yetu ya Nikohub, kwenye simu yako. App hiyo ipo kwenye play store, ukishaidownload, jiunge ili uonekane moja kwa moja kwenye ‘system’ ya Nikohub.

“Ukimaliza hivyo vyote, unatakiwa kutuma ujumbe mfupi wa maneno ‘SMS’ au tupigie simu namba 0765-80 24 57, ili uweze kupata maelekezo ya jinsi ya kufuturu bure popote pale utakapokuwa kwa muda huo.

“Kumbuka kujiunga kwako na App ya Nikohub, utaweza kuwa mmoja kati ya watu 100 ambao kila siku tumekuwa tukiwafuturisha bure.”

KIPINDI MAALUM RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA MWENYEKITI WA BARRICK GOLD CORPORATION JUNE 17,2017

0
0

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS JUNE 15,2017

0
0

FILAMU YA KISOGO YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM.

0
0
  Msanii wa Filamu nchini Salim Ahmed maarufu Gabo Zigamba (kushoto) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa filamu yake fupi ya Kisogo mapema jana jijini Dar es Salaam, kulia ni Afisa Mawasiliano wa Kampuni ya Sarafu Media Bw. Myovela Mfwaisa. 
 Afisa Habari wa Kampuni ya Sarafu Media Bw. Myovela Mfwaisa (katikati) kushoto akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa filamu fupi ya Kisogo mapema jana jijini Dar es Salaam, kushoto Msanii wa filamu hiyo Bw. Salim Ahmed maarufu Gabo Zigamba na kulia ni Mtaalam wa TEHAMA toka Kampuni ya Uhondo Bw. Amon John. 
 Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia filamu fupi ya Kisogo wakati ikizinduliwa na msanii wa filamu hiyo Salim Ahmed maarufu Gabo Zigamba.

Picha zote na Eliphace Marwa - Maelezo

DC KASESELA AKESHA KUANZIA SAA MBILI ASUBUHI HADI SAA SITA USIKU MGODINI NYAKAVANGALA KUOKOA MAITI YA MCHIMBAJI

0
0
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiwa katika mgodi wa nyakavangala uliopo katika Kata ya malengamakali Mkoani Iringa wakati wa Juhudi za kuuokoa mwili wa marehemu viskadi nyenza katika shimo alilosimama Mkuu huyo wa Wilaya.
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela akisaiadiana na wachimbaji madini katika mgodi wa nyakavangala ili kuokoa mwili wa marehemu Nyenza
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela alipokuwa akiwasili katika mgodi wa nyakavangala uliopo Kata ya malengamakali Mkoani Iringa.



Na Fredy Mgunda, Iringa.

Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela alilazimika kufanya kazi ya uokoaji wa maiti ya mchimbaji madini katika mgodi wa Nyakavangala bwana Vaspa nyenza mkazi wa Itengulinyi Kata ya Ifunda wilaya ya Iringa kwa takribani masaa kumi na nane

Kasesela alisema kuwa alianza kazi hiyo majira ya saa mbili asubuhi alipowasili katika mgodi huyo wa Nyakavangala lakini yeye,waandishi wa habari na viongozi wengine wa wilaya ya Iringa walijitahidi kuokoa mwili wa marehemu hadi majira ya saa sita usiku lakini zoezi hilo lilikuwa likiendelea

"Hadi saizi tumepiga dua zote lakini hali ngumu sijui nini kinaendelea katika hili shimo maana waokoaji kila wakiukaribia mwili wa marehemu miamba laini inavungika na kujaza udongo ndani ya shimo ndio maana mmeniona naangaika na ndugu wa marehemu kujaribu kusali huku na kule lakini hali ni ngumu hadi muda huu wa saa tano usiku"alisema Kasesela

Aidha Kasesela aliwataka ndugu wa marehemu na viongozi mbalimbali kuwa na subila wakati wanalishugulikia swala la kuokoa mwili wa mpendwa wao kwa kuwa wameshaukaria mahali ulipo.

"Ungalia tayari kichwa na kiwiliwili vimeshaonekana kwa hiyo tumebakiza sehemu ndogo tu naombeni tuwe wavumilivu kwa kuwa tuvumilia toka siku ya jumapili hadi usiku huu basi tuungane kumuombea mwenzetu ili tutoe mwili wake ukiwa salama" alisema Kasesela

Haya yamemkuta mchimbaji mwenzenu hivyo nawataka kuwa makini wakati wa uchimbaji wa madini katika mgodi huu wa nyakavangala la sivyo mgodi huu utafungwa sio muda.

Lakini mwili wa Vaspa Nyenza umepatikana saa 7 na dakika 50 usiku na msafara kuelekea mortuary umeanza na Mazishi kufanyika Kijiji cha Itengulinyi Ifunda kesho asubuhi kuanzia saa 3 au 4 hivi

Kwa upande wake Chief inspector Mayunga Ngele aliwataka wachimbaji wote kutochimba tena kwenye mashimo yaliyozuiliwa ili kuepusha ajali mbalimbali hapo mgodini kwa kuwa hata huyo marehemu na wenzake walishakatwa kuchimba katika shimo hilo ambalo lilikuwa kwenye hali mbaya ya kuanguka.

"Tamaa ndio zimemponza huyu marehemu maana tuliwakataza lakini mwenyewe waliingia kinyemela kwa lengo la kwenda kuchimba kwa wizi kwenye shimo lilokataliwa ndio maana yamewakuta hayo kama wangekuwa wameusikia ushauri wetu basi tusingefika hapa tulipo usiku huu "alisema inspector Ngele

Naye Thomas masuka mmiliki wa mgodi wa Nyakavangala alimshukuru mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela kwa jitihada zake za kuhakikisha kila kitu kianda kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa na serikali na kuahidi kuwa gharama za kuuokoa mwili hadi kuufikisha kwako ni kwake na ndugu hawatalipia pesa yoyote ile.

"Kuanzia kutokea kwa kifo chake,uokoaji na kuusafirisha mwili wa marehemu huyu gharama zote nitazilipa mimi kama mmiliki wa mgodi huu kwa mujibu wa sheria za madini hata angekuwa Mwananchi wa kigoma,Mwanza, Mbeya, Bukoba na sehemu yoyote ile ndani ya Tanzania basi ni wajibu wangu kuhakikisha mwili wa marehemu unafika mali pake kwa usalama unaotakiwa" alisema Masuka

Mbunge Abdallah Ulega amfumua Tundu Lissu Bungeni Dodoma

0
0

Kampuni ya Wazawa, yakamilisha hatua za Msingi kuuza hisa zake kwa watanzania - Maxmalipo

0
0

Mjumbe wa Bodi ya kampuni ya Maxcom Africa Dr.Donalth Ulomi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza hati iliyopewa kampuni hiyona ambayo inaiwezesha Kampuni kumilikiwa na Umma wa watanzania.

Akiongea na Wanahabari Dr. Ulomi amesema kwamba Kuanzia Sasa Kampuni ya Maxcom Africa itatambulika kwa Jina la Maxcom Africa Public Limited Company (Maxcom Africa PLC) . Kampuni hii maarufu kwa jina la Maxmalipo ni Moja ya Kampuni zilizoanzishwa na kuendeshwa na wazawa watanzania ambayo imeifikia hatua za Mwisho katika mchakato wa kuanza kuuza hisa zake kwenye soko la hisa. Dr. Olumi amewaambia wanahabari kwamba wanasubiri kibali cha wasimamizi wa Soko la Hisa ili waweze Kuorodhesha Kampuni yao katika Soko hilo

Kampuni hii ilianzishwa mwaka 2008 na mpaka leo imefika nchi zaidi ya 5 barani Africa.Hafla hiyo ya uzinduzi wa uuzaji wa hisa ulifanyika mapema leo katika makao makuu ya Maxcom Africa Kijitonyama Jijini Dar Es Salaam.

Mjumbe wa Bodi ya kampuni ya Maxcom Africa Dr. Donalth Ulomi (kulia ) akikata utepe wa kuzindua rasmi Jina Lipya la Kampuni ya Maxcom Africa PLC anayeshuhudia ni Mkurungezi wa Uendeshaji wa Maxcom Africa Bw.Ahmed Lusasi mapema leo katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika makao makuu ya Maxcom Africa PLC Kijitonyama Jijini Dar Es Salaam.
Mjumbe wa Bodi ya kampuni ya Maxcom Africa Dr,Donalth Ulomi (kulia ) akionesha nembo ya jina jipya Maxcom Africa PLC na kushoto kwake ni Mkurungezi wa Uendeshaji wa Maxcom Africa Bw.Ahmed Lusasi mapema leo katika hafla ya uzinduzi wa Jina jipya la Kampuni hiyo iliyofanyika makao makuu ya Maxcom Africa PLC Kijitonyama Jijini Dar Es Salaam
Mjumbe wa Bodi ya kampuni ya Maxcom Africa Dr. Donalth Ulomi akifanya mahojiano na mwandishi wa habari mara baada ya uzinduzi rasmi wa Jina Jipya la Kampuni ya Maxcom Africa PLC.

Mjumbe wa Bodi ya kampuni ya Maxcom Africa Dr. Donalth Ulomi akifanya mahojiano na mwandishi wa habari mara baada ya uzinduzi rasmi wa Jina Jipya la Kampuni ya Maxcom Africa PLC.

BONGO MOVIE SHINYANGA YAMPONGEZA RAIS MAGUFULI SAKATA LA MADINI KWA KUMPA FILAMU HII FUPI "TANGANYIKA KARNE 18"

0
0
Kundi la Uigizaji wa Filamu ‘Bongo Movie Shinyanga’ limempongeza rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa hatua anazozichukua katika kulinda rasilimali za nchi hususani madini ya Tanzania.
Mwenyekiti wa Bongo Movie Shinyanga, Juma Songoro amesema rais Magufuli anapaswa kuungwa mkono na wananchi wote wa Tanzania na wazalendo wote."Wasanii wa filamu mkoa wa Shinyanga tunampongeza sana rais Magufuli kwa hatua anazozichukua kulinda nidhamu na rasilimali za nchi,tunamuombea kila la heri atufikishe tunapopatarajia,tumeandaa filamu hii kama zawadi yetu kwake na na watanzania wote",amesema Songoro.
 
Katika kufikisha pongezi hizo,Bongo Movie Shinyanga wameandaa Filamu fupi inaitwa'Tanganyika Karne ya 18' inayoonesha  jinsi nchi za nje zinavyoiba madini ya Tanzania.
TUMIKA DAKIKA ZAKO 3 TU KUTAZAMA FILAMU HII HAPA CHINI
Viewing all 46205 articles
Browse latest View live




Latest Images