Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

TAMBUA JINSI YA KUJIUNGA NA KUWA MWANACHAMA WA COPYRIGHT SOCIETY TANZANIA (COSOTA)


SPIKA NDUGAI APATA UGENI KUTOKA TAASISI YA UTSS (UNDER THE SAME SUN) LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA

$
0
0
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia)akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu na Mwanzilishi wa Taasisi ya UTSS (Under the Same Sun) Ndg. Peter Ash (kushoto) pale ugeni kutoka Taasisi ya UTSS (Under the Same Sun) ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akizungumza na Mkurugenzi Mkuu na Mwanzilishi wa Taasisi ya UTSS (Under the Same Sun) Ndg. Peter Ash (kushoto) alipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu na Mwanzilishi wa Taasisi ya UTSS (Under the Same Sun) Ndg. Peter Ash (katikati) pale ugeni kutoka Taasisi ya UTSS (Under the Same Sun) ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya UTSS (Under the Same Sun) Ndg. Vicky Ntetema 
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati)akiwa katika picha ya pamoja na ugeni kutoka Taasisi ya UTSS (Under the same Sun) ulioongozwa na Mkurugenzi Mkuu na Mwanzilishi wa Taasisi hiyo Ndg. Peter Ash (wa tatu kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji Ndg. Vicky Ntetema (wa tatu kulia) baada ya kikao kilichofanyika leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

UMOJA WA WAZAZI CCM Z’BAR WAWAASA VIONGOZI KUONGEZA KASI YA UTEKELEZAJI WA AHADI ZAO WALIZOTOA

$
0
0

NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

MAKATIBU wa Wilaya za Umoja wa Wazazi CCM Zanzibar wamewashauri viongozi mbali mbali wa Chama cha Mapinduzi kuongeza kasi ya utekelezaji wa ahadi walizotoa ndani ya taasisi hiyo ili kupunguza changamoto za kiutendaji.

Rai hiyo imetolewa na baadhi ya Makatibu wa Wilaya Sita za Umoja huo Zanzibar mara baada ya kukabidhiwa Komputa zilizotolelewa na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja huo, Bi. Najma Giga ikiwa ni miongoni mwa utekelezaji wa ahadi alizowahi kutoa wakati wa ziara zake Visiwani humo.

Katibu wa Wazazi Wilaya ya Amani , Bi.Mwanaisha Ame Mohamed amesema upatikanaji wa vifaa hivyo utaongeza ufanisi wa kiutendaji ndani ya umoja huo kwani watakuwa na vitendendea kazi vya kisasa vitakavyorahisisha utendaji wa kazi zao.

Aidha Katibu huyo amewataka baadhi ya Wabunge, Wawakilishi na Madiwani ambao bado hawajahamasika kuanza kutekeleza ahadi zao kwa umoja huo na chama kwa ujumla kufuata nyayo za viongozi wenzao walioanza kutatua kero za taasisi hiyo hatua kwa hatua.

“Huu ni wakati wa viongozi mbali mbali wa Chama chetu pamoja na jumuiya zetu kujitokeza kusaidia baadhi ya Mikoa na Wilaya zenye upungufu wa vitendea kazi ili waweze kukamilisha shughuli za uchaguzi kwa ufanisi.”, alisema Katibu Mwanaisha.

Naye Katibu wa Wazazi Wilaya ya Wete Pemba, Bi. Mariam Ali Said amemshukru Naibu Katibu Mkuu wa Wazazi Zanzibar kwa kutekeleza ahadi zake kwa vitendo na kuongeza kuwa vifaa hivyo ni chachu ya kumaliza changamoto za kufuata huduma za uchapaji wa nyaraka za kiofisi masafa ya mbali.

Akizungumza Kaimu Naibu Katibu Mkuu Wazazi Zanzibar, Nd. Mustafa Rashid Kumwalu kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu wa umoja huo Bi. Najma Gina mara baada ya kukabidhi Komputa hizo ametoa wito kwa watendaji wa umoja huo kutumia komputa hizo kwa matumizi yaliyokusudiwa ili shughuli za kiutendaji zifanyike kwa wakati mwafaka.

Nd. Rashid alieleza kuwa lengo la umoja huo ni kuhakikisha watendaji wake wanapata vitendea kazi vya kisasa vitakavyosaidia kutekeleza kwa wakati shughuli za kiutendaji kwa lengo la kwenda sambamba na matakwa ya Katiba ya CCM iliyofanyiwa mabadiliko miezi kadhaa iliyopita.

Aidha alisema Komputa zilizokabidhiwa mpaka sasa ni tisa bado kumi kwa mujibu wa idadi ya komputa zilizoahidiwa kutolewa na Naibu katibu Mkuu wa Umoja huo, ambaye pia ni Mbunge wa kuteuliwa kutoka ndani ya Umoja wa Wazazi Tanzania.

Komputa hizo zina thamani zaidi ya shilingi milioni Saba zimekabidhiwa kwa Wilaya 6 za Umoja wa Wazazi CCM Wilaya ya Amani, Wilaya ya Mfenesini, Wilaya ya Kati, Wilaya ya Kaskazini “B”, Wilaya ya Wete na Wilaya ya Chake Chake Pemba.
 Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Zanzibar , Mustafa Rashid Kumwalu akimkabidhi Katibu wa Wazazi Wilaya ya Kaskazini “B” Unguja , Bi. Salma Shaibu, kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu wa Umoja huo Bi.Najma Giga.
Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Zanzibar Nd. Mustafa Rashid Kumwala akitoa nasaha kwa Makatibu wa Wilaya Sita za Umoja huo kabla ya kuwakabidhi komputa hizo.
Baadhi ya Komputa zilizotolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Zanzibar, Bi.Najma Giga kwa Wilaya Sita za umoja huo Zanzibar.

Kampuni ya Wazawa, yakamilisha hatua za Msingi kuuza hisa zake kwa watanzania - Maxmalipo

$
0
0
Mjumbe wa Bodi ya kampuni ya Maxcom Africa Dr,Donalth Ulomi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza hati iliyopewa kampuni hiyo na Soko la hisa la Dar es salaam (Dar Es Salaam stock Exchange ) na kuanzia sasa itauza hisa zake kwa umma na kubadili jina lake kuwa Maxcom Africa PLC Maxmalipo ni Moja ya Kampuni zilizoanzishwa na kuendeshwa na wazawa watanzania ambayo imeifikia hatua za Mwisho katika kuuza hisa zake kwenye soko la hisa. 

Leo hii wametambulisha hati yao inayowafanya kuwa tayari kwa kuuza hisa kwa watanzania . Kampuni hii ilianzishwa mwaka 2008 na mpaka leo imefika nchi zaidi ya 5 barani Africa.Hafla hiyo ya uzinduzi wa uuzaji wa hisa ulifanyika mapema leo katika makao makuu ya Maxcom Africa Kijitonyama Jijini Dar Es Salaam. 
Mjumbe wa Bodi ya kampuni ya Maxcom Africa Dr,Donalth Ulomi (kulia ) akikata utepe wa kuzindua rasmi uuzaji wa hisa za Maxcom Africa PLC anayeshuhudia ni Mkurungezi wa Uendeshaji wa Maxcom Africa Bw.Ahmed Lusasi mapema leo katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika makao makuu ya Maxcom Africa Kijitonyama Jijini Dar Es Salaam. 
Mjumbe wa Bodi ya kampuni ya Maxcom Africa Dr,Donalth Ulomi (kulia ) akionesha nembo ya jina jipya Maxcom Africa PLC kuzindua rasmi uuzaji wa hisa za kampuni hiyo kushoto kwake ni Mkurungezi wa Uendeshaji wa Maxcom Africa Bw.Ahmed Lusasi mapema leo katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika makao makuu ya Maxcom Africa Kijitonyama Jijini Dar Es Salaam 
waandishi wa habari wakichukua matukio wakati wa hafla ya uzinduzi wa uuzaji wa hisa za Maxcom Africa mapema leo. 
Mjumbe wa Bodi ya kampuni ya Maxcom Africa Dr,Donalth Ulomi akifanya mahojiano na mwandishi wa habari mara baada ya uzinduzi rasmi wa uuzaji wa hisa za Maxcom Africa PLC.Maxmalipo ni Moja ya Kampuni zilizoanzishwa na kuendeshwa na wazawa watanzania ambayo imeifikia hatua za Mwisho katika kuuza hisa zake kwenye soko la hisa. Leo hii wametambulisha hati yao inayowafanya kuwa tayari kwa kuuza hisa kwa watanzania . Kampuni hii ilianzishwa mwaka 2008 na mpaka leo imefika nchi zaidi ya 5 barani Africa mapema leo katika hafla ya uzinduzi ilizofanyika makao makuu ya Maxcom Africa Kijitonyama Jijini Dar Es Salaam.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNE 14,2017

TASAF YAIBUKA KIDEDEA KATIKA SHUGHULI ZA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI.

$
0
0

  Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge ,Kazi, Vijana na Walemavu Mhe. Jennista Mhagama akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ,Bwana Ladislaus Mwamanga Cheti cha Ushindi wa Kwanza katika ya Mifuko ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi nchini.


 Baadhi ya wafanyakazi wa TASAF wakifurahia ushindi wa kwanza ambao Mfuko huo umepata kwa mwaka 2017 kati ya mifuko 19 inayoshughulikia uwezeshaji wananchi kiuchumi.


WAFANYAKAZI WA BENKI YA EXIM TANZANIA WAJITOLEA DAMU

$
0
0
Katika kuunga mkono juhudi za serikali za kuhakikisha benki ya damu nchini inakuwa na akiba ya kutosha, wafanyakazi wa benki ya EXIM wamejitolea damu ili kusaidia wahitaji.

Akizungumza kuhusu utoaji wa damu wa wafanyakazi wa benki ya EXIM, Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali Watu wa benki hiyo, Frederick Kanga amesema ni jambo la kawaida wao kujitolea damu kwani wamekuwa na utaratibu huo kwa muda mrefu na lengo kuisaidia jamii.Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali Watu wa benki ya EXIM, Frederick Kanga.
 
“Tupo katika utaratibu wa kawaida wa kusaidia jamii, ni utaratibu ambao tumekuwa tukiufanya ni kama asili yetu EXIM kutoa damu kwa mwaka wa saba mfululizo tunajitolea kwa ajili ya kusaidia upatikanaji wa damu kwa wahitaji,

“Tumefikia hatua hii ili kushirikiana na jamii kwa watu wenye uhitaji, tunajitahidi sana kusaidia kwenye sekta ya afya jambo hili huwa linafanyika pia kwenye matawi yetu yote nchini, kwa sasa tunayo 33, 12 yapo hapa Dar na 21 yapo mikoani,” amesema Kanga.

Naye Afisa Uhamasishaji wa Mpango wa Taifa wa Damu Salama Kanda ya Mashariki, Fatuma Mjungu alisema mwitikio wa wananchi kujitolea damu kwa sasa ni mkubwa tofauti na ilivyokuwa awali na muhimu kwa sasa ni utolewaji wa elimu kwa wananchi ili wazidi kutoa kwani bado kuna upungufu mkubwa.

Afisa Uhamasishaji wa Mpango wa Taifa wa Damu Salama Kanda ya Mashariki, Fatuma Mjungu.

“Tupo kwenye kampeni ya kuelekea kilele cha siku ya uchangiaji damu kitaifa, tunahitaji kupata chupa za damu 1,500 na mpaka Juni, 12 tulikuwa tumeshapata chupa 735, natoa witio kwa wananchi wajitolee damu kwenye vituo vyetu, changaototo ni elimu sababu wengi wakipata elimu ndiyo wanajitolea,” alisema Mjungu.

Afisa Uhamasishaji wa Mpango wa Taifa wa Damu Salama Kanda ya Mashariki, Fatuma Mjungu.

BALOZI PINDI CHANA AWASILISHA HATI ZA UTAMBULISHO

$
0
0
Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Dkt. Pindi Hazara Chana akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta kabla ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwenye Ikulu ya Eldoret Juni 13,2017. 
Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Dkt. Pindi Hazara Chana wa pili kutoka kushoto akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Kenya (katikati) mara baada ya zoezi la kuwasilisha Hati za Utambulisho kukamilika.

Wafanyakazi wa Hospitali ya Sanitas wajitolea damu

$
0
0


Kuelekea siku ya kuchangia damu duniani, Hospitali ya Sanitas iliyopo Mikocheni imeandaa kambi ya kuchangia damu ambayo ilifanyika siku ya jumanne, Juni 13 2017.

Katika kambi hiyo jumla ya chupa za damu 50 zilikusanywa ambapo wachangiaji walikuwa ni wafanyakazi wa hospitali hiyo na baadhi ya watu kutoka nje ambao walijumuika na wafanyakazi hao hao kwa ajili a uchangia damu kwa ajili ya wahitaji.

Akizungumzia kambi hiyo ya kutoa damu, Meneja Msaidizi wa Hospitali ya Sanitas, Dr. Sajjad Fazel alisema utoaji wa damu huo ni muhimu kwa kusaidia maisha ya watu wengine kwani hata chupa moja ya damu ina muhimu mkubwa na inaweza kusaidia kuoa maisha ya watu watatu.

"Kuna uhaba wa damu, kwa kila Mtanzania ahakikishe kuwa anaonyesha uzalendo na upendo wako kwa Watanzania wenzake kwa kuchangia damu na kuokoa maisha yao," alisema Dk. Fazel.

Dk. Fazel alisema makundi ambayo yana uhitaji mkubwa wa damu ni wajawazito waliokuwa na tatizo wakati wa kujifungua, watoto waliokuwa na upungufu wa damu, watu waliokuwa na ugonjwa wa sikla na watu waliokuwa wamepata ajali na wanaofanyiwa upasuaji.
Meneja Msaidizi wa Hospitali ya Sanitas, Dk. Sajjad Fazel akitoa damu.




TAARIFA KUTOKA JESHI LA KUJENGA TAIFA (JKT)

DC BYAKANWA ASIMAMIA ZOEZI LA UONDOSHAJI WA MIUNDO MBINU YA UMWAGILIAJI KATIKA SHAMBA LA KILIMO CHA KISASA LA MBOWE.

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Hai ,Gelasius Byakanwa akiwa na kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Hai katika lango la kuingilia katika shamba la Kilimo cha Kisasa la Mboga Mboga la Kilimanjaro Vegees Ltd lililopo Nshara Machame.
Mkuu wa wilaya ya Hai,akiwaongoza wajumbe wa kamati ya ulinzi na Usalama ya wilaya Hai ,pamoja na askari Mgambo wakiingia katika shamba la Kilimo cha Kisasa cha Mboga mboga la Kilimanjaro Vegees Ltd linalomilikiwa na Mbunge wa jimbo la Hai,Freeman Mbowe.
Shamba la Kilimo cha Kisasa,(Green House) lililopo Nshara Machame wilaya ya Hai la Kilimanjaro Vegees Ltd .
Mkuu wa wilaya ya Hai,Gelasius Byakanwa akiwa na kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Hai,wakiwa katika moja ya shamba hilo pamoja na asakari polisi wenye silaha wakiondoa miundo mbinu ya umwagiliaji pamoja na unyunyiziaji wa dawa .
Mkuu wa wilaya ya Hai,Gelasius Byakanwa akizungumza katika eneo hilo wakati zoezi la kuondoa miundo mbinu katika eneo hilo ikiendelea.Zoezi hilo limefanyika kwa kile kinachodaiwa shughuli za kilimo kufanyika kando ya mto kinyume cha sharia.
Sehemu ya Shamba la Strawberry kabla ya kuondolewa miundo mbinu.
Askari Mgambo wakiondoa miundo mbinu ya umwailiaji katika shamba la Kilimoa cha Kisasa la Kilimanjaro Vegees Ltd linalomilikiwa na Mbunge wajimbo la Hai,Freeman Mbowe.
Mipira maalumu iliyokuwa ikitumika katika umwagiliaji ikiwa imekatwa katwa .
Asakari Mgambo wakiendelea na zoezi la uondoshaji wa miundo mbinu.
Mkuu  wa wilaya ya Hai,Gelasius Byakanwa akifuatilia zoezi la uondoshaji wa miundo mbinu ya umwagiliaji katika shamba hilo.
Mkuu wa wilaya ya Hai ,Gelasius Byakanwa akisaidia katika uondoshaji wa miondo mbinu katika shamba la kisasa la Kilimanjaro Vegees Ltd linalomilikiwa na Mbunge wa Jimbo la Hai,Freeman Mbowe.
Askari Mgambo wa kikata mipira kwa panga .
Zao la Strawberry ni moja wapo ya mazao yanyolimwa kisasa katika shamba hilo.
Sehemu ya Mazao ambayo tayari yameanza kukomaa katika shamba hilo.
Kilimo cha kisasa cha zao la Nyanya pia kimekuwa kikifanyika katika shamba hilo.
Baadhi ya Green House zikiwa zimeondolewa wavu maalumu wa kuzuia wadudu kuingia ndani.

Na Dixon Busagaga wa Busagaga's Orijino Blog.

MATUKIO KATIKA PICHA: YALIYOJIRI KATIKA KIKAO CHA 47 CHA MKUTANO WA SABA WA BUNGE LA 11 LEO JUNE 14, 2017.

$
0
0
 Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mussa Azzan Zungu akiongoza Kikao cha 47 cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo June 14, 2017 Mjini Dodoma.
 Naibu Waziri wa nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Suleimani Jafo akijibu maswali mbalimbali katika Kikao cha 47 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo June 14, 2017 Mjini Dodoma.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula akijibu maswali mbalimbali katika Kikao cha 47 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo June 14, 2017 Mjini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Dkt Medred Kalemani akijibu maswali mbalimbali katika Kikao cha 47 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo June 14, 2017 Mjini Dodoma.
 Mbunge wa Ileje (CCM) Mhe. Janeth Mbene akiuliza swali katika Kikao cha 47 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo June 14, 2017 Mjini Dodoma.
 Mbunge Viti Maalum (CCM) Mhe. Mwantumu Haji akiuliza swali katika Kikao cha 47 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo June 14, 2017 Mjini Dodoma.
 Mbunge Kyerwa (CCM) Mhe. Innocent Bilakwate akiuliza swali katika Kikao cha 47 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo June 14, 2017 Mjini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt Ashatu Kijaji akijibu swali katika Kikao cha 47 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo June 14, 2017 Mjini Dodoma.
  Mbunge Mdaba (CCM) Mhe. Joseph Mhagama akiuliza swali i katika Kikao cha 47 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo June 14, 2017 Mjini Dodoma.
 Mbunge Tunduru Kusini (CCM) Mhe. Daimu Mpakate akiuliza swali katika Kikao cha 47 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo June 14, 2017 Mjini Dodoma.
  Mbunge Viti Maalum (CCM) Mhe. Angelina Malembeka  akiuliza swali katika Kikao cha 47 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo June 14, 2017 Mjini Dodoma.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mwigulu Nchemba akijadiliana jambo na Mbunge wa Buyungu Mhe.Kasuku Bilago katika Kikao cha 47 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo June 14, 2017 Mjini Dodoma.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati akiwasili Bungeni kuhudhulia Kikao cha 47 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo June 14, 2017 Mjini Dodoma.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akijadiliana jambo na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Prof Jumanne Maghembe katika  Kikao cha 47 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo June 14, 2017 Mjini Dodoma.
Baadhi ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakifuatilia Kikao cha 47 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo June 14, 2017 Mjini Dodoma.

Picha zote na Raymond Mushumbusi MAELEZO Dodoma.

Magreth Sinyangwa wa Kilosa Morogoro azoa Milioni 20 za Biko

$
0
0

Balozi wa Biko Kajala Masanja na mwakilishi wa Bodi Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Humud Abdulhussein, wakihakiki namba ya mshindi wa Sh Milioni 20 kutoka Kilosa, mkoani Morogoro, Magreth Sinyangwa na kumpigia ili kumjulisha juu ya ushindi wake.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MOTO wa bahati nasibu ya Biko ama ‘Ijue Nguvu ya Buku’, umezidi kuchanja mbuga baada ya droo yake ya 14 kufanyika leo jijini Dar es Salaam, huku mkazi wa Kilosa Morogoro, Magreth Sinyangwa, akiwa mwanamke wa kwanza kuzoa jumla ya Sh Milioni 20 zinazotolewa na waendeshaji wa bahati nasibu hiyo inayotikisa hapa nchini.

Droo hiyo iliyompelekea utajiri mshindi huyo wa Morogoro, imechezeshwa na Balozi wa Biko Tanzania, Kajala Masanja na kushuhudiwa pia na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Humud Abdulhussein.
Balozi wa Biko Kajala Masanja akiagana na mwakilishi wa Bodi Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Humud Abdulhussein, mara baada ya kumaliza kuchezesha droo ya 14 ya Sh Milioni 20 iliyochezeshwa leo jijini Dar es Salaam, huku Magreth Sinyangwa akiwa mwanamke wa kwanza kuibuka na mamilioni hayo ya Biko tangu kuanzishwa kwa bahati nasibu hiyo hususan kwa droo kubwa za Sh Milioni 10 hadi 20.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa droo hiyo, Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, alisema moto wa Biko umezidi kuchanja mbuga baada ya kumpata mshindi wao wa Sh Milioni 20, huku kwa mara ya kwanza wakimpata mshindi ambaye ni mwanamke tangu kuanzishwa kwa bahati nasibu yao.

Alisema washindi hao ni wale wanaocheza bahati nasibu yao kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi kwa kufanya miamala kwenye simu zao za M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money, ambapo watatakiwa kuingia kwenye lipa bili au lipa kwa M-Pesa na kuingiza namba ya kampuni ambayo ni 505050 na namba ya kumbukumbu 2456 tayari kwa kucheza.

“Baada ya kuingiza namba ya kumbukumbu pia atatakiwa kuweka kiasi cha kucheza ambacho kinaanzia Sh 1000 na kuendelea ambapo kiasi cha Sh 1000 kitampatia nafasi mbili ambazo ni ushindi wa papo kwa hapo pamoja na donge nono la Sh Milioni 20 kwa Jumapili ijayo kama tulivyompata mwingine kwa droo tuliyochezesha jana.

“Kwa zawadi za papo kwa hapo zinaanzia Sh 5000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja ambapo mshindi hutumiwa fedha zake dakika chache baada ya kupokea ujumbe wa Biko ukimtaarifu juu ya ushindi wake kutokana na kucheza Bahati Nasibu yetu,” Alisema Heaven na kuwataka Watanzania wacheze mara nyingi zaidi ili waweze kujiwekea mazingira mazuri ya kuibuka na zawadi mbalimbali za Biko.

Naye mshindi huyo Magreth Sinyangwa akizungumza kwa simu baada ya kutangazwa mshindi wa Sh Milioni 20 alisema hakuamini kama ameshinda kiasi hicho cha pesa baada ya kujulishwa hivyo na Kajala, huku akisema kuwa amepokea kwa furaha kwa sababu zitamkwamua katika shughuli zake za ujasiriamali.

“Nashukuru Biko kwa kunijulisha juu ya ushindi wangu mnono wa Sh Milioni 20 ambazo kwa hakika zimekuja wakati muafaka kwa sababu tayari nimepata kitu cha kuniletea utajiri mkubwa kutokana na kushinda kwangu donge nono la Biko kama waliyokuwa wanashinda wengine,” Alisema Magreth.

Naye Humud Abdulhussein ambaye ni mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, alisema mchezo wa Biko unafuata kanuni, sheria na taratibu zote zilizowekwa na serikali kwa kusimamiwa vizuri na Bodi yao ili kuhakikisha michezo ya kubahatisha inakuwa salama.

Bahati Nasibu ya Biko imekuwa ikizidi kutoa washindi wengi wa papo kwa hapo na wale wanaoshinda zawadi kubwa ya Sh Milioni 10 hadi 20, huku jumla ya Sh Milioni 500 zikitolewa kwa mwezi Mei pekee, jambo linaloashiria mafanikio makubwa kwa wanaoshiriki mchezo huo wa Biko.

VETA na Airtel watangaza kozi 5 mpya za ufundi stadi kupitia simu ya mkononi

$
0
0
Mamlaka ya elimu ya ufundi Tanzania (VETA) kwa kushirikiana Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kupitia application ya VSOMO leo wametangaza na kuzindua kozi mpya za ufundi stadi za VETA zitakazotolewa  kupitia simu za mkononi ili kuwawezesha watanzania kujiunga na kupata utaalamu na vyeti vya VETA kwa gharama nafuu

Kozi hizo mpya zinazoongezwa katika mfumo wa vsomo ni  Huduma ya chakula na mbinu za kuhudumia wateja, Matengenezo ya kompyuta,umeme wa viwandani, ufundi Bomba wa Majumbani na Umeme wa magari.

Tangu kuzinduliawa kwa mfumo huu wa mafunzo kwa njia ya mtandao kupitia application ya VSOMO mwezi wa Juni 2016 ulianza kutoa kozi mbalimbali za ufundi za VETA ikiwemo Ufundi umeme wa manyumbani, Ufundi pikipiki, Ufundi wa simu za mkononi, Ufundi Alluminium,  Utaalamu wa maswala ya urembo pamoja ma Ufundi wa kuchomea vyuma.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel, Beatrice Singano, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kozi tano mpya kwenye awamu ya pili ya mpango wa kutoa mafunzo ya ufundi stadi kupitia programu ya VSOMO inayoratibiwa na kampuni ya Airtel. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Dk. Bwire Ndazi.

Lengo la mfumo huu likiwa ni kutimiza dhamira ya VETA ya kutanua wigo wa mafunzo ya ufundi stadi nchini na kuongeza idadi ya vijana kujipatia fani mbalimbali za ufundi ili waweze  kuajirika  au kujiajiri.  Mafunzo haya yanawawezesha wanafunzi kujisomea wakati wowote kwa gharama nafuu kupitia simu zao za mkononi za Airtel.

Mfumo huu wa masomo kwa njia ya Mtandao VSOMO,  sasani maarufu kwa vijana ambapo takwimu zinaonyesha zaidi ya vijana 30,000 tayari wamepakua application ya VSOMO, 8000 wamejiandikisha na kati yao 50 wanasoma kozi mbalimbali zilizopo pia wapo waliomaliza na kupata vyeti vya VETA.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Dk. Bwire Ndazi akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kozi tano mpya kwenye awamu ya pili ya mpango wa kutoa mafunzo ya ufundi stadi kupitia programu ya VSOMO inayoratibiwa na kampuni ya Airtel, Dar es Salaam jana.Kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel, Beatrice Singano.

Akiongea wakati wa kuzindua na kutangaza kozi hizo, Mkuu wa chuo cha Veta Kipawa, Eng. Lucius Luteganya alisema “mafunzo ya ufundi kwa njia ya mtandao ya VSOMO yametuwezesha kuongeza wigo na kuwafikia watanzania wengi nchini. Tunaamini bado tunayofursa ya kuongeza wigo  zaidi na kuongeza idadi ya vijana wenye ueledi ili kwenda sambamba na agenda ya serikali ya awamu tao ya uchumi wa viwanda kwa kupata nguvu kazi yenye taaluma muhimu katika kuendesha uchumu wa nchi”

“Tunaamini kozi hizi mpya zitatawavutia vijana wengi kujiandikisha, kusoma na kupata ujuzi zaidi.”  Alisisitiza Eng Luteganya

Eng, Luteganya alisema kuwa  “Ili kupata mafunzo ya VSOMO kupitia Airtel, ukiwa na Airtel pakua application katika google play store, na kujisajiri na kisha chagua kozi inayokidhi mahitaji yao.

ili kuhakikisha tunasimamia viwango vya elimu vilivyowekwa na VETA, wale watakaomaliza masomo yao nadharia kupitia VSOMO watafanya mtihani ili kufaulu na kujiunga na mafunzo ya vitendo katika vituo vya VETA vilivyopo nchi nzima. Vyeti vya kuhitimu mafunzo vitatolewa kwa wale watakaofaulu mafunzo katika hatua zote mbili ya nadharia na vitendo”.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Dk. Bwire Ndazi akionyesha jinsi ya kutumia simu ya mkononi kupata progaramu ya masomo ya mafunzo ya ufundi Stadi VSOMO wakati wa uzinduzi wa programu ya pili ya mfunzo hayo jana.Kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel, Beatrice Singano na Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Dar es Salaam,Habib Burko.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Bi Beatrice Singano Mallya alisema “Tunajisikia furaha kuongeza kozi nyingi zaidi katika mfumo huu  wa masomo kwa njia ya mtandao wa VSOMO  kwani itatuwezesha kufikia idadi kubwa ya vijana wanaosoma kwa kupitia simu zao za mkononi. Lengo letu ni kuhakikisha tunakuwa na kozi nyingi ili kwenda sambamba na matarajio na mahitaji ya wanafunzi na watanzania kwa ujumla”.

Tunapenda kuwapongeza wote waliojiunga na kumaliza kozi zao na kuhimiza wote ambao hawajapakua application ya VSOMO kufanya hivyo kwa kujiandikisha katika mojawapo ya kozi 12 zinazopatikana katika application ya VSOMO kwa gharama nafuu ya shilingi 120,000 tu na  kulipia kwa njia ya Airtel Money kwa kupiga *150*60#.

Tunapenda kuwahimiza vijana kutumia fursa hii na kujiunga na kozi na kujisomea wakati wowote na mahali popote. kozi hizi zinazochukua hadi mienzi mitatu kumalizika lakini pia zinaweza kuisha mapema kulingana na muda utakaotengwa na mwanafunzi kuweka bidii ili kumaliza mapema.

WADAU WA KILIMO WAKUTANA KUJADILI MIKAKATI YA KUBORESHA UWEZESHAJI KWENYE KILIMO NA VIWANDA

$
0
0
Katika kuhakikisha dhamira ya Serikali ya dhamira ya Serikali ya kujenga Uchumi wa Viwanda wadau wa kilimo na viwanda wamekutana ili kuzungumzia nafasi ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Tanzania (TADB) katika  kuhakikisha Benki hiyo inasaidia sekta ya Kilimo nchini.

Wakizungumza katika Kikao hicho kilichoandaliwa na TADB ili kujadili mikakati ya kuboresha uwezeshaji kwenye kilimo na viwanda nchini.
Akizungumza katika kikao hicho Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga amesema kuwa Benki imejipanga kuleta matokeo makubwa kwenye mapinduzi ya kilimo na viwanda hasa vya uchakakataji na usindikaji wa mazao ya kilimo.

Bw. Assenga amesema kuwa mipango hii itasaidia upatikanaji wa mali ghafi kwa viwanda vya ndani hivyo kusukuma ndoto ya Serikali kufikia lengo lake la Kujenga Uchumi wa Viwanda na kuhuisha uwekezaji kwenye Viwanda vidogo vidogo na vya kati vya usindikaji na uchakataji wa mazao ya Kilimo na mifugo.

“Benki imejikita kwenye kusaidia Sekta ya Kilimo iweze kusukuma dhamira ya Serikali ya Uchumi wa Viwanda uweze kutoa matunda yaliyokusudiwa ili kuchagiza na kusaidia Mapinduzi ya Kilimo kutoka kilimo cha kujikimu kwenda cha kibiashara ili kuchangia kwenye ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini,” alisema.

Bw. Assenga amesema katika kuhakikisha azma hiyo inatimia TADB imejipanga kutoa elimu ili kuwajengea uwezowakulima na taasisi mbali mbali za fedha pamoja na vyama vya ushirika kuweza kukopa toka TADB pamoja na kushirikiana na wadau mbali mbali kusaidia uwekezaji mkubwa kwenye Sekta ya Kilimo ili iweze kuinua pato la Taifa na kumkomboa Mwananchi.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji huyo ameongeza kuwa TADB imeanza kujiimarisha  na kuchochea mabenki na taasisisi za fedha kuongeza utoaji wa mikopo na fedha zingine kwenye Sekta ya Kilimo ili kuongoza utoaji mikopo ya uongezaji wa thamani katika shughuli za kilimo.

TADB ni taasisi ya serikali ambayo ilianzishwa kwa ajili ya kutatua ufinyu mkubwa wa upatikanaji wa fedha mikopo kwa ajili ya maendeleo ya kilimo nchini ambao ulikuwa unachangiwa kwa kiasi kikubwa na mikopo mingi kutoka taasisi za fedha kuelekezwa zaidi kwenye upande wa biashara za bidhaa; riba kubwa kwenye mikopo ya kilimo; mikopo ya muda mfupi; masharti magumu ya kukopa bila kuzingatia hali halisi ya sekta ya kilimo  na mazao ambayo inaathiriwa kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya hali ya hewa.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Tanzania (TADB), Bibi Rosebud Kurwijila (kushoto) akizungumza na aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mzee Peniel Lyimo (kulia) wakati wa Kikao cha Wadau wa Kilimo Kujadili Mikakati Ya Kuboresha Uwezeshaji Kwenye Kilimo Na Viwanda kinachofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Biashara ya TADB, Bibi Rehema Twalib (kulia) akizungumza wakati wa Kikao cha Wadau wa Kilimo Kujadili Mikakati Ya Kuboresha Uwezeshaji Kwenye Kilimo Na Viwanda kinachofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Dar es Salaam.
 Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mzee Peniel Lyimo (kulia) akiongoza Kikao hicho.
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga (kushoto) akisisitiza nafasi ya Benki yake katika kuleta matokeo makubwa kwenye mapinduzi ya kilimo na viwanda hasa vya uchakakataji na usindikaji wa mazao ya kilimo.
 Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa TADB wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi, Bibi Rosebud Kurwijila (kushoto) wakifuatilia kwa makini Kikao hicho.
 Washiriki wa Kikao hicho wakifuatilia mawasilisho mbali mbali wakati wa Kikao cha wadau wa kilimo waliokutana kujadili mikakati ya kuboresha uwezeshaji kwenye kilimo na viwanda. Kikao hicho kiliandaliwa na Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Tanzania (TADB).
Wadau wa kilimo waliokutana kujadili mikakati ya kuboresha uwezeshaji kwenye kilimo na viwanda wakiwa katika picha ya pamoja.

WIZARA MALIASILI KUPITIA BODI YA UTALII TTB YATOA SEMINA KWA WABUNGE WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA PIC MJINI DODOMA

$
0
0
NA HAMZA TEMBA - WMU

Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Bodi ya Utalii Tanzania TTB, imefanya semina ya mafunzo ya siku moja kwa wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kwa lengo la kuwajengea uelewa wajumbe hao kuhusu majukumu ya taasisi hiyo ambayo imefanyika jana mjini Dodoma na kuhudhuriwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Ramo Makani na Katibu Mkuu, Meja Jenerali Gaudence Milanzi.

Akizungumza katika semina hiyo, Meneja wa Huduma za Utalii wa taasisi hiyo, Philip Chitaunga alisema bodi hiyo iliyoanzishwa mwaka 1993 ilipewa jukumu la jumla la kukuza sekta ya utalii nchini ikiwemo kutumia mbinu mbalimbali za utangazaji, kuhamasisha uendelezaji wa mazao ya utalii na miundombinu yake, kufanya tafiti za masoko na utalii kwa ujumla pamoja na kuhamasisha uelewa wa watanzania kufahamu umuhimu na faida za utalii.

Alisema taasisi hiyo imefanya juhudi mbalimbali za kutangaza utalii wa Tanzania nje ya nchi ikiwemo kuratibu ziara za waandishi wa habari za kitalii, kuweka matangazo katika magazeti ya utalii ya kimataifa, kushiriki katika maonesho ya utalii ya kimataifa na kutangaza kupitia Televisheni za kimataifa kama CNN ya Marekani.

“Jitihada zingine tulizofanya ni kutumia balozi zetu nje ya nchi na mabalozi wa utalii wa hiari yaani 'Goodwill Ambasadors', kutumia mitandao ya kijamii na matangazo kwenye vyombo vya usafiri vya umma ambapo mwaka 2008 hadi 2009 tulitangaza kwenye mabasi 124 jijini london Uingereza, taxi 100, treni mbalimbali na katika uwanja wa ndege wa Heathrow” alisema Chitaunga.

Alisema jitihada za hivi karibuni za kutangaza utalii zimefanyika kupitia michezo ya Ligi Kuu ya Uingereza ikiwemo timu za mpira wa miguu za Seattle Sounders na Sunderland, kupitia majarida, CD na filamu fupi kwa lugha mbalimbali kama Kiingereza, Kijerumani, Kifaransa na Kiswahili. Pia, kupitia tovuti maalum ya utalii ya taifa (www.tanzaniatourism.gotz), App kwenye ‘Smart Phones’ na kufanya ziara za utangazaji wa utalii yaani Roadshows katika nchi za China, Afrika ya Kusini, bara la Ulaya, Amerika na Australia.

Kwa upande wa jukumu la kuhamasisha utalii wa ndani, Chitaunga alisema bodi imetekelza jukumu hilo kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali vya habari nchini pamoja na mitandao ya kijamii, kushiriki katika maonesho mbalimbambali ya ndani ya nchi kama vile Sabasaba na Kili Fair, kuhamasisha wanafunzi wa shule za msingi, sekondari na vyuo, kuendesha matangazo mbalimbali ya Radio na TV na kuweka mabango maeneo mbalimbali ikiwemo ya mpakani na kwenye viwanja vya ndege.

Aliseme katika kuhamasisha utalii wa ndani, siku za hivi karibu TTB imeingia makubaliano na chama cha wenye mabasi nchini TABOA ambapo filamu mbalimbali zinazohamasisha utalii wa ndani zitaoneshwa katika mabasi zaidi ya 300 ya mikoani.

Akizungumzia kuhusu mafanikio, alisema taasisi hiyo imechangia ongezeko la idadi ya watalii wa kimataifa nchini kutoka 230,166 mwaka 1993 na kufikia 1,284,279 mwaka 2016. Aidha, mapato yameongezeka kutoka Dola za Kimarekani Milioni 146.84 na kufikia Dola za Kimarekani Milioni 2,132 huku sekta hiyo ya utalii ikichangia asilimia 17.5 ya pato la taifa.

Alisema mafanikio mengine yaliyopatikana ni pamoja na Tanzania kupata umaarufu mkubwa zaidi duniani ambapo mitandao na kampuni mbalimbali za safari za kitalii ikiwemo Safari Bookings, Fox News.com na New York Times zimeitambua kama eneo bora la utalii barani Afrika. Aidha, Mlima Kilimanjaro, Bonde la Ngorongoro na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti zimetambuliwa kama miongoni mwa maajabu saba barani Afrika huku kampuni ya World Travel Awards ikiutambua Mlima Kilimanjaro kama kivutio bora zaidi barani Afrika.

“Baadhi ya watu maarufu duniani kutembelea Tanzania kama vile Oprah Winfrey, Bill Gates, Will Smith, Roman Abramovic, David Beckham, Moussa Sissoko na Waziri Mkuu Mstaafu wa Israel, Ehud Barak ni sehemu pia ya viashiria vya mafanikio kwa taasisi yetu kutangaza utalii wa Tanzania nje ya nchi”, alisema Chitaunga.

Aliongeza kuwa, watu maarufu kuja kuandaa filamu zao Tanzania ni sehemu ya mafanikio ya kutangaza utalii wa Tanzania nje ya nchi, “Watu mashuhuri saba kutoka China hivi karibuni wameandaa filamu itakayorushwa katika Anhui TV inayotazamwa na watu zaidi ya milioni 800 duniani” alisema.

Katika jitihada za kutangaza utalii wa Tanzania kupitia shirika la ndege la Air Tanzania Chitaunga alisema, “TTB sasa inaandaa gazeti la Air Tanzania litakalojulikana kama Safari Njema kwa ajili ya kutangaza utalii wa Tanzania na vivutio vyake pamoja na kuimarisha usafiri wa anga kupitia shirika hilo la Umma”.

Alisema pamoja na mafanikio hayo, bodi hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo miundombinu hafifu katika baadhi ya maeneo ya vivutio vya utalii, changamoto ambayo imeanza kufanyiwa kazi na Serikali ikiwemo ujenzi wa reli ya kisasa, uimarishaji wa viwanja vya ndege na kuimarisha shirika la ndege la Air Tanzania.

Alisema changamoto nyingine ni ufinyu wa bajeti ya utangazaji, hofu ya matukio ya ugaidi na mlipuko wa magonjwa katika bara la Afrika, upungufu wa vyumba vya malazi katika baadhi ya maeneo yenye vivutio vya utalii, mtazamo hasi kuwa Tanzania ni ghali na mtazamo kuwa jukumu la utangazaji na uendelezaji utalii ni la Wizara na Taasisi zake pekee. Alisema changamoto zote hizo zinafanyiwa kazi ikiwemo kuhamasisha wawekezaji kuwekeza katika sekta ya utalii na watanzania kuona umuhimu wa utalii na kuutangaza pamoja kuwatoa hofu watalii na kuwawekea mazingira bora na rahisi ya kutembelea Tanzania.

Akizungumzia mipango ya baadaye ya taasisi hiyo, Chitaunga alisema ni pamoja na kutafsiri tovuti ya utalii ya Taifa katika lugha ya Kijerumani, Kichina na Kiswahili, kuendeleza juhudi za kufungua masoko mapya ya utalii kama vile China, Israel, Urusi na India, kuimarisha utangazaji wa utalii kupitia TEHAMA, kuongeza idadi ya mabalozi wa hiari katika masoko mahususi ya utalii, uwekaji wa mabango, tafiti za masoko mapya ya utalii na kuandaa filamu mpya za kuitambulisha Tanzania ndani na nje ya nchi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Albert Obama aliipongeza Wizara na TTB kwa semina hiyo pamoja na jitihada wanazozifanya za kutangaza utalii wa Tanzania ndani na nje ya nchi na kutaka juhudi zaidi ziongezwe huku baadhi ya wabunge waliochangia wakiitaka Serikali iongeze uwekezaji katika bajeti ya utangazaji ili taasisi hiyo iweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

Naye Naibu Waziri wa Maliasili, Mhandisi Ramo Makani alisema ushauri uliotolewa na wabunge hao utafanyiwa kazi na hoja zote zilizowasilishwa zitajibiwa kwa maandishi huku Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi akihitimisha kwa kusema kuwa Wizara imepiga hatua kubwa ya kukabiliana na ujangili ndani na nje ya maeneo ya hifadhi nchini. 
Naibu Waziri wa Maliasili, Mhandisi Ramo Makani (kushoto) akizungumza jana mjini Dodoma katika semina iliyoandaliwa na Wizara hiyo kupitia Bodi ya Utalii Tanzania kwa ajili ya kuwajengea uelewa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu majukumu ya bodi hiyo. Kulia ni Mwenyekiti wa kamati hiyo, Albert Obama. 
Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi (kushoto) akizungumza jana mjini Dodoma katika semina iliyoandaliwa na Wizara hiyo kupitia Bodi ya Utalii Tanzania kwa ajili ya kuwajengea uelewa wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu majukumu ya bodi hiyo. Katikati ni Naibu Waziri wa Maliasili, Mhandisi Ramo Makani na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Albert Obama.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC), Albert Obama (kulia) akizungumza jana mjini Dodoma katika semina iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili kupitia Bodi ya Utalii Tanzania kwa ajili ya kuwajengea uelewa wajumbe wa kamati hiyo kuhusu majukumu ya bodi hiyo. Katikati ni Naibu Waziri wa Maliasili, Mhandisi Ramo Makani na Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi. 
Meneja wa Huduma za Utalii wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Philip Chitaunga (kushoto) akiwasilisha mada ya jumla kuhusu shughuli za taasisi hiyo kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) katika semina iliyoandaliwa na Wizara hiyo kupitia bodi hiyo mjini Dodoma jana. 
Meneja wa Huduma za Utalii wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Philip Chitaunga (kushoto) akiwasilisha mada ya jumla kuhusu shughuli za taasisi hiyo kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) katika semina iliyoandaliwa na Wizara hiyo kupitia bodi hiyo mjini Dodoma jana. 
 Meneja wa Huduma za Utalii wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Philip Chitaunga (kushoto) akiwasilisha mada ya jumla kuhusu shughuli za taasisi hiyo kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) katika semina iliyoandaliwa na Wizara hiyo kupitia bodi hiyo mjini Dodoma jana. 
 Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) wakiangalia video zilizoandaliwa na TTB kwa ajili ya kutambulisha utalii wa Tanzania ndani na nje ya nchi katika semina iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili kupitia bodi hiyo mjini Dodoma jana.

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) na Mbunge wa Viti Maalum, Riziki Lulida akichangia jana mjini Dodoma katika semina iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili kupitia Bodi ya Utalii Tanzania kwa ajili ya kuwajengea uelewa wajumbe wa kamati hiyo kuhusu majukumu ya bodi hiyo. Kulia ni Katibu Mkuu wa hiyo Meja Jenerali Gaudence Milanzi.
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) wakiwa katika semina hiyo iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili kupitia Bodi ya Utalii Tanzania mjini Dodoma jana.
Meneja Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania, Geofrey Meena akifafanua jambo katika semina hiyo iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili kupitia Bodi ya Utalii kwa ajili ya kuwajengea uelewa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu majukumu ya bodi hiyo.

Maadhimisho ya Siku ya Kuchangia Damu Duniani Yafana Muhimbili

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, Mheshimiwa Sophia Njema akizungumza na Jonas Hans Atile (kushoto) ambaye amejitokeza kuchangia Damu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo.
 Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Shirikishi Katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dk. Praxeda Ogweyo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya Siku ya Kuchangia Damu Duniani. Pia Dk. Ogweyo amewataka Watanzania wajitokeze kwa wingi kuchangia damu.
 Mmoja wa Wananchi akishiriki katika maadhimisho ya Siku ya Uchangiaji Damu duniani Leo katika hospitali hiyo.
 Baadhi ya wananchi wakisubiri kuchangia damu Leo katika jengo la Maabara kuu, hospitali ya Taifa Muhimbili.

Baadhi ya Wananchi waliojitokeza kuchangia damu katika Hospitali ya Muhimbili wakiendelea na shughuli ya utoaji damu leo.


Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo imeshiriki katika madhimisho ya Siku ya Kuchangia Damu duniani kwa kuendesha shughuli ya utoaji damu kwa watu mbalimbali ili kukidhi mahitaji ya huduma hiyo kwa wagonjwa wenye uhitaji.

Shughuli hiyo inaendelea katika hospitali hiyo kwenye Jengo la Maabara kuu ambako watu wamekusanyika kwa ajili ya kuchangia damu. Mmoja wa viongozi walishriki katika maadhimisho hayo ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, Mheshimiwa Sophia Mjema pamoja na Watanzania mbalimbali.

Akizungumza katika shughuli hiyo Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi kuchangia damu ili kuokoa maisha ya wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo wakiwamo kinamama na watoto wadogo.

“Nawapongeza wote walifika leo hapa Hospitali ya Muhimbili kuchangia damu, ni jambo la muhimu mmefanya kwa ajili ya kuokoa maisha ya wagonjwa,” amesema Mheshimiwa Mjema.

Naye Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Shirikishi wa hospitali hiyo, Dk Praxeda Ogweyo amewataka wananchi,mashirika  ya umma na yasiyo ya kiserikali, shule, vyuo mbalimbali na taasisi za dini  kujitokeza kuchangia damu hospitali hapo.

Dk Ogweyo amesema kuwa Muhimbili inahitaji wastani wa chupa za damu 100 hadi 120 kwa siku na kwamba damu inayokusanywa ni kati ya chupa 50 hadi 60 na upungufu wa damu ni chupa 60 hadi  hadi 70, hivyo damu inahitajika zaidi.

“Kutokana na hali hii, naomba rai kwa wananchi kujitokeza kwa wingi ili kuokoa maisha ya wagonjwa. Hospitali imejipanga kupitia kitengo chake cha uchangiaji damu kilichopo maabara kuu hivyo karibuni mchangie damu,” amesema Dk Ogweyo.

UZINDUZI WA WIKI YA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA WAFANA LEO MJINI DODOMA

$
0
0
Watoto wa Shule ya Santhome ya Mjini Dodoma wakiongoza watoto wenzao kutoka shule mbalimbali za mji wa Dodoma kuelekea viwanja vya Nyerere Square kushiriki uzinduzi wa maonesho ya Wiki ya Siku ya Mtoto wa Afrika ambayo kilele chake ni tarehe siku 16 juni mwaka huu.
Kilanja Mkuu wa Shule ya Santhome ya Mjini Dodoma Martha Linje akiongoza watoto wenzake kutoka shule mbalimbali za mjini Dodoma kuelekea viwanja vya Nyerere Square kushiriki uzinduzi wa maonesho ya Wiki ya Siku ya Mtoto wa Afrika ambayo kilele chake ni tarehe siku 16 juni mwaka huu.
Baadhi ya watoto kutoka shule za msingi mjini Dodoma wakiwa na mabango ya kupinga ukatili dhidi ya watoto kuelekea viwanja vya Nyerere Square kushiriki uzinduzi wa maonesho ya Wiki ya Siku ya Mtoto wa Afrika ambayo kilele chake ni tarehe siku 16 juni mwaka huu.
Mkurugenzi wa Watoto kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto pamoja na Mbunge viti maalumu ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa uzinduzi wa Maonesho ya Siku ya Mtoto wa Afrika wakipata maelekezo kutoka Maofisa wa Plan International hawapo pichani mara baada ya kutembelea mabanda ya maonesho hayo.

TATIZO LA MKAA JIJINI DAR ES SALAAM KUMALIZWA

$
0
0
Na Tulizo Kilaga, Mafinga

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo amesema tatizo la uhaba wa mkaa jijini Dar es Salaam litakwisha kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Kampuni ya Tractor inayomiliki kiwanda cha kuzalisha na kusambaza mkaa endelevu kilichopo Mafinga mkoani Iringa.

Kiwanda hicho kinatarajia kuanza uzalishaji mwishoni mwa mwezi huu kwa kuzalisha tani 40 za mkaa kwa siku na kuzisambaza katika jiji la Dar es Salaam, Mwanza na Dodoma kwa kuanzia kutokana na miji hiyo kuwa na matumizi makubwa ya mkaa hali inayohatatisha Misitu ya Asili nchini.

Akizungumza mara baada ya kujionea uwekezaji uliofanywa na kiwanda hicho, Prof. Santos alisema kuanzishwa kwa kiwanda hicho kinachozalisha na kusambaza mkaa inaouzalisha kutokana na takataka zitokanazo na uchakataji wa mbao na mabaki ya miti kwa teknolojia ya kisasa kutasaidia kupunguza matumizi makubwa ya mkaa katika miji mikubwa ambayo imekuwa kichocheo cha ukataji wa miti katika mikoa mingine.

Inakadiriwa kuwa karibu hekta 300,000 hadi 400,000 za misitu ya asili huharibiwa kila mwaka kutokana na utengenezaji mkaa.

Prof. Santos alisema kuanzishwa kwa kiwanda hicho kutasaidia kuongeza ufanisi wa matumizi ya mazao ya misitu ya kupanda, utapunguza utegemezi wa nishati ya kuni na mkaa kutoka misitu ya asili na kuongeza uhakika wa upatikanaji wa nishati ya mkaa kwa miji mikubwa nchini sambamba na kuongeza mchango wa sekta ya misitu kwenye ushiriki wa uchumi wa viwanda nchini Tanzania.

Hata hivyo alisema jitihada hizo zitafanikiwa ikiwa watumiaji wa nishati ya mkaa watabadilika na kuwa na mtizamo chanya juu ya matumizi ya mkaa mbadala pamoja na nishati nyingine mbadala.

“Tuongeze kasi katika kukabiliana na mabadiliko ya tabiawatu na kila mmoja kwa nafasi yake atimize wajibu wake ipasavyo, kwa pamoja tutafanikiwa kuinusuri nchi yetu kugeuka jangwa,” alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kiwanda hicho, Bw. Benjamin Lane alisema kiwanda hicho kitazalisha mkaa bora na kuhifadhiwa katika hali ya usafi kwenye mifuko ya kilo 50 na 25 kwa kuanzia ikiwa lengo nikuwa na mifuko hadi ya kilo moja itakayouzwa kwa bei rahisi zaidi ukilinganisha na bei ya mkaa halisi.

Lane alisema kuwa kiwanda hicho kimeamua kuwekeza kwenye uzalishaji mkubwa wa mkaa endelevu kwa lenga la kuiunga mkono serikali kutimiza adhima yake ya kuwa na matumizi endelevu ya misitu kwa faida ya vizasi vya sasa na vijavyo kwa kuhakikisha inatumia takataka zote zitokanazo na uchakataji wa mbao na mabaki ya miti kwa teknolojia ya kisasa kuzalisha mkaa.

Kwa upande wake, Meneja wa Shamba la Miti la Sao Hill, Bw. Saleh Baleko alisem shamba lake lina malighafi ya kutosha kukiwezesha kiwanda hicho kuwa na uzalishaji wa uhakika kutokana na wavunaji wengi nchini kutumia asilimia 70 tu ya eneo lote la uvunaji na kuacha asilimia 30 ikipotea ambayo sasa itatumika kuzalisha mkaa endelevu.

Akizungumza kuhusu mradi huo mmoja wa wananchi, Joyce Jonas alisema mradi huu ni mzuri na kuwaasa wawekezaji wengine kufanya uwekeza mkubwa kwenye mradi wa kuzalisha mkaa endelevu kutokana na kuwepo na mahitaji na matumizi makubwa ya mkaa ukilinganisha na viwanda vilivyopo

BREAKING NYUZZZZ....: Rais Dkt. Magufuli akutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Barrick ya Canada Profesa John L. Thorton

$
0
0
Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli leo amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Barrick ya Canada Profesa John L. Thorton Ikulu jijini Dar es salaam. Katika mkutano huo, uliohudhuriwa pia na Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Paramagamba Kabudi na Balozi wa Canada hapa nchini, Ian Myles umemalizika kwa mafanikio makubwa ambapo pande zote zimekubaliana kukaa meza moja kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali katika sekta ya madini. Habari kamili yaja punde

Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images