Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

MKUU WA MKOA WA ARUSHA,MRISHO GAMBO AMPONGEZA MFUGAJI ALIYEJENGA HOTELI

$
0
0



Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania(KKKT)Dayosisi ya Kaskazini Kati,Solomon Masangwa akizumza katika sherehe ya uzinduzi wa hoteli ya Eseriani Kata ya Levolosi jijini Arusha na kumpongeza mmiliki kwa kufuga kisasa na kuwekeza kwa kutoa ajira na kuongeza huduma bora kwa wageni wanaofika Arusha.

Mkuu wa wilaya mstaafu,,Peter Toima akitoa salamu zake kwa wananchi walihudhuria.


Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akizungumza katika sherehe hiyo,kulia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)mkoa wa Arusha,Michael Lekule Laizer.


Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania(KKKT)Dayosisi ya Kaskazini Kati,Solomon Masangwa akikata utepe kuashiria uzinduzi wa hoteli hiyo wanaoshuhudia kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Arusha,Michael Lekule Laizer na Mkuu wa mkoa,Mrisho Gambo.

Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akizindua hoteli ya Eserian ,kulia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)mkoa wa Arusha,Michael Lekule Laizer.

Mmiliki wa hoteli ya Eserian,Issaya Yassi(kulia)akimweleza Mkuu wa mkoa,Mrisho Gamb(wa pili kushoto),Askofu Masangwa(kushoto) na Mwenyekiti CCM mkoa wa Arusha,Michael Lekule Laizer namna alivyotumia mifugo kuwekeza kwenye nyumba ya wageni.

Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akiangalia mandhari ya hoteli ya Eserian akiwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)mkoa wa Arusha,Michael Lekule Laizer.

Mfanyabiashara maarufu wa jijini Arusha,Philemon Mollel maarufu kwa jina la Monaban (kushoto) akikabidhiwa tuzo maalumu na Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo iliyotolewa na shirika la kidini World Mission International kwa kutambua mchango kwa jamii.

TAARIFA KWA UMMA

TBS YAWASHAURI WAZALISHAJI WADOGO WADOGO WA BIDHAA KUTUMIA FURSA YA BURE YA UKAGUZI

$
0
0

Wazalishaji wadogo wadogo wa bidhaa nchini wameshauriwa kutumia fursa ya bure ya ukaguzi wa bidhaa zao inayotolewa na Shirika la Viwango Tanzania TBS.

Hayo yamesemwa na Afisa Masoko Mwandamizi kutoka katika shirika hilo,Gladnes Kaseka pichani kushoto juu wakati akiongea na waandishi wa habari kwenye maonyesho ya tano ya biashara ya Mkoa wa Tanga .

Alisema kuwa licha ya TBS kutoa fursa hiyo lakini bado wazalishaji wadogo na wakati wameshindwa kuitumia fursa hiyo kwa ukamilifu wake na kusababisha kuendelea kuwepo kwa bidhaa ambazo hazina nembo ya ubora.

"Bado wazalishaji wetu wengi hawajaweza kuifikia fursa hiyo ambayo itaweza kuwasaidia kuhakikisha wanazalisha bidhaa zenye ubora lakini wataweza kuingiza bidhaa zao kwa urahisi katika masoko ya ushindani tofauti na sasa" alisema Kaseka.

Aidha alisema kuwa bado wanaendelea na jitihada za kuhakikisha wanaziondosha katika soko bidhaa ambazo ni hafifu kwa kufanya ukaguzi wa Mara kwa Mara katika masoko na maeneo yote yanayohusika na shughuli za uuzaji wa bidhaa.

Nae Mfanyabiashara Aisha Kisoki alisema kuwa changamoto kubwa ni muingiliano wa bidhaa kutoka nje ambazo kwa hapa nchini zinauzwa kwa bei rahisi tofauti na wanazozizalisha.

Alisema kuwa iwapo TBS wataweza kudhibiti uingiaji usio rasmi wa bidhaa kutoka nje utasaidia sana wafanyabiashara wa ndani ya nchi kuona umuhimu wa kuweka nembo bidhaa zao.
Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

TIMU YA WILAYA YA UMISETA WILAYANI MBOGWE YAKABIDHIWA BENDERA YA UWAKILISHI MASHINDANO YA UMISETA

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri  ya wilaya ya Mbogwe ndg Elias Kayandabila Akiongea na team ya UMISETA ya  Wilaya wakati akifunga mashindano hayo kwa ngazi ya wilaya.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri  ya Mbogwe Ndg Elias kayandabila akiwakabidhi wanamichezo bendera ya michezo  ya Wilaya 

Timu ya Wilaya ya UMISETA imekabidhiwa bendera ya michezo ya Wilaya na kutakiwa kwenda kuiwakilisha wilaya kwenye mashindano ya UMISETA
 

KAMPUNI YA ALLIANCE ONE YAANDAA UTARATIBU WA KUPANDA MITI KWA KILA MSIMU WA KILIMO WILAYANI KASULU.

$
0
0
TUMBAKU ni zao ambalo husababisha uharibifu wa Misitu katika uzalishaji wa tumbaku ya Mvuke, kwa kukabiliana na Changamoto hiyo Kampuni ya kuuza na Kununua tumbaku ya Alliance one Wilayani Kasulu imeandaa utaratibu wa kupanda Miti kwa kuwashirikisha Wakulima kutoa Ardhi yao na halmashauri kwa kupanda hekta 288 kwa kila msimu wa kilimo lengo ikiwa ni kuhakikisha kuni zinazotumika katika uchomaji wa tumbaku zinatoka katika chanzo endelevu cha miti wanayoipanda. 

Akizungumza mara baada ya makabidhiano ya Mashamba ya Miti hekta 144 jana yalitooteshwa kwa kipindi cha mwaka 2014 - 2015 katika Kijiji cha Mganza na Chogo kata ya Heru juu baina ya halmashauri na kampuni hiyo Meneja uzalishaji jani katika Kampuni hiyo, David Mayunga, alisema kampuni hiyo inajihusisha na uendelezaji wa nishati mbadara ya kuchomea tumbaku, kuborsha mabani ya kuchomea iliyaweze kutumia kuni chache.

Mayunga alisema uzalishaji wa tumbaku ya Mvuke unategemea kiasi kikubwa cha kuni hapa Tanzania na Nchi nyingine pia na husababisha uteketezaji wa misitu, kampuni hiyo wamedhamilia kuwa ifikapo mwaka 2020 uzalishaji wa tumbaku utatumia kuni kutoka katika vyanzo endelevu ambapo Wakulima na serikali watatoa maeneo yao waweze kupandiwa miti lengo ikiwa ni kuinua uzalishaji wa tumbaku pamoja na Wakulima.

Alisema tumbaku ni zao la pili kwa Tanzania linalo ingiza fedha za kigeni, kampuni hiyo inafanya zoezi hilo katika maeneo ambayo yanalima tumbaku ilikuweza kiwasaidia Wakulima kutunza mazingira na kufanya biashara ya tumbaku bila kiathiri mazingira, kwa kipindi kilicho pita zao la tumbaku limeshuka sana kutokana na Wakulima wengi kushindwa kulima kutokana na gharama ya zao hilo.

"Pamoja na malengo tuliyonayo ya kuinua zoezi la upandaji miti tunakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa Ardhi hili linatokana na baadhi ya Wananchi kuzuia mashamba yao yasipandwe miti kwa kuhofia kwamba watazulumiwa, kukosekana kwa ushirikiano baina ya Viongonzi na kampuni hili linasababisha kampuni kushindwa kupanda miti kwa malengo yaliyo pangwa", alisema Mayunga.

Alisema zoezi hilo kwa misimu ilyopita walifanikiwa kwa asilimia 85% na siku ya jana walikabidhi kiasi cha hekta 68.7 kwa kijiji cha Chogo na hekta 76.4 zitakabidhiwa Kwa wananchi walioyoa mashamba yao katika kijiji cha Mganza, hata hivyo aliwaomba Wananchi kuendelea kujitolea mashamba yao waweze kupandiwa miti hiyo kwakuwa faida ya miti hiyo wataipata wao na sio kampuni na gharama zote za upandaji na usimamizi zitafanywa na Kampuni.

Kwa upande wake Katibu tawala wa Wilaya ya Kasulu Titus Mguha aliishukuru kwampuni hiyo kwaniaba ya serikali kwa hatua ya kuanza kupanda miti katika Vijiji hivyo hatua hiyo itasaidia kuboresha mazingira na kurudisha misitu kwa maeneo ambayo yalikuwa yameharibiwa na Wakulima na wafugaji na kwasasa watatumia misitu yao binafsi.

Alisema Wananchi wanatakiwa kutoa ardhi kwa Kampuni hiyo kwakua kampuni hiyo inalengo zuri la kuhakikisha Wakulima Watumbaku hawaangaiki kutumia misitu ya asili na badala yake watatumia miyi ambayo wanaipanda katika Misitu hao na kuweza kufanya kilimo cha tumbaku bila kuathiri misitu ya asili.

Nae Mwenyekiti Wa halmashauri ya Mji wa Kasulu , Twallib Mangu alisema Wao kama halmashauri watajitahidi kuingiza suala hilo la upandaji miti katika vikao vyao na Madiwani waweze kuwahamasisha Wananchi wao kitoa ardhi zao kwaajili ya kupandiwa miti ilikuhakikisha na wao wananufaika na mradi huo na kuweza kupata mafanikio ya uhifadhi wa misitu.

Aidha aliiiomba kampuni hiyo kuandaa mikataba itakayo waonyesha ni jinsi  gani Mwananchi atanufaika na mradi huo na kampuni itanufaika na nini ilikuwaondoa Wananchi wasiwasi wa kuhofia kuibiwa , na aliwaomba Wananchi kuwatumia Wanansheria wa Halmashauri kabla ya kusainishwa mikataba hiyo na kuweza kujitokeza kwa wingi waweze kupandiwa miti hiyo.

Baadhi ya Wananchi Lisa Ramadhani na Hatibu Juma waliipongeza sana kampuni hiyo na kuishukuru kwa kuwapandia moti na kwamba miti huiyo itawasaidia kupata kuni na kupata mbao za kujengea na manufaa mengi hivyo wakotayari kujitolea mashamba yao iliwaweze kupandiwa miti hiyo.

Wenceraus Mbuyeko alisema yeye kwa upande wake atatoa hekari 16 waweze kumpandia miti katika shamba lake kwakuwa faida anaziona na baadhi ya Wananchi waliopandiwa miti wanaendelea kunufaika na miti hiyo, kampuni hiyo inamipango mizuri ya kuweza kuinua kilimo cha wakulima wa tumbaku.
 Meneja wa uzalishaji jani wa kampuni ya Alliance one David Mayunga  akisain hati ya makabidhiano ya mashamba ya  miti kwa Halmashauri ya Wilaya ya kasulu.
Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa kasulu Twallib Mangu, akisaini baadhi ya mikataba ya makabidhiano baina ya kampuni ya Alliance one na halmashauri.

TANZIA: MZEE NDESAMBURO AFARIKI DUNIA

$
0
0
Taarifa iliyoifikia Globu ya Jamii hivi punde inaeleza kuwa Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo wa Jimbo la Moshi Mjini na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Kilimanjaro, Mzee Philemone Ndesamburo amefariki Dunia asubuhi ya leo katika Hospitali ya KCMC, Mkoani humo. 

Katibu wa Chadema mkoa wa Kilimanjaro, Basil Lema amethibitisha muda huu juu ya kifo hicho na kwamba bado haijafahamika chanzo cha kifo chake.

Kwa sasa mwili wa marehmu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti hospitali ya rufaa ya KCMC .

Ndugu wakiwemo watoto wa marehemu wamefika Hospitalini hapo na kuomba mwili wa marehemu kufanyiwa uchunguzi kutokana na kifo kuwa ni cha ghafla.

Lema alisema, Mzee Ndesamburo alifika ofisini kwake majira ya asubuhi na alionekana mwenye afya njema, ilipofika majira ya saa nne hali ilibadilika na kushindwa kuendelea na majukumu yake.

Ndipo walipomkimbiza KCMC kwa ajili ya matibabu na alifariki dunia akiwa kitengo cha emergency, Taarifa zaidi tutajulishana kadri zitakapokuwa zikitufikia.

BALOZI SEIF ASHIRIKI MSIBA WA MAMA MZAZI WA NAIBU KATIBU MKUU MSTAAFU WA CCM ZANZIBAR

$
0
0
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimfariji Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM Zanzibar Ndugu Vuai Ali Vuai aliyefiwa na Mama yake Mzazi Bibi Mwanaisha Hassan Vuai aliyezikwa kijijini kwao Bwejuu Mkoa wa Kusini Unguja.
Waumini wa Dini ya Kiislamu wakimsalia Bibi Mwanaisha Hassan Vuai katika Msikiti wa Ijumaa Bwejuu aliyefariki Dunia jana katika Hospitali ya Global alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu.
Baadhi ya Waumini wa Dini ya Kiislamu na Viongozi wa Serikali na Kisiasa wakimuombea Dua Marehemu Bibi Mwanaisha Hassan Vuai baada ya kumsalia kwenye Msikiti wa Ijumaa wa Bwejuu Mkoa Kusini Unguja.
Baadhi ya Waumini wa Dini ya Kiislamu na Viongozi wa Serikali na Kisiasa wakimuombea Dua Marehemu Bibi Mwanaisha Hassan Vuai baada ya kumsalia kwenye Msikiti wa Ijumaa wa Bwejuu Mkoa Kusini Unguja.
Balozi Seif Ali Iddi kushoto akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa Kusini Unguja Nd. Ramadhan Abdullah Ali wakati wa msiba wa Mama Mzazi wa Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM Zanzibar hapo Bwejuu Mkoa Kusini Unguja.

                                                     Picha na – OMPR – ZNZ.

Isome Programu ya shughuli za Siku ya Mazingira Duniani itakayofanyika kijijini Butiama, kuanzia Juni 3-4 2017


OLE NASHA AHIMIZA MATUMIZI YA MBEGU BORA KWA WAKULIMA

$
0
0
Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole Nasha (kushoto) akitambulishwa wafanyakazi wa kampuni ya Monsanto Tanzania baada ya ofisi yao kufunguliwa hapa nchini eneo la Njiro mkoani Arusha, kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Monsanto Afrika, Dk Shukla Gyanendra. Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole Nasha (kushoto) akikagua ghala la mbegu bora zenye uwezo wa kumpa mkulima mazao bora.Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole Nasha akizungumza jambo baada ya kukagua ghala la mbegu bora za kampuni ya Monsanto zenye uwezo wa kumpa mkulima mazao boraMeneja Kiongozi wa kampuni ya mbegu ya Monsato Tanzania, Frank Wenga akieleza mipango kamambe ya kuwafikishia mbegu bora wakulima kote nchini.
Wageni mbalimbali waliohudhuria uzinduzi wa ofisi ya Monsanto Tanzania.Meneja Kiongozi wa kampuni ya mbegu ya Monsato Tanzania, Frank Wenga akifafanua jambo kwa waandishi wa habari . Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole Nasha akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa kampuni ya Monsato na mawakala wa mbegu nchini waliohudhuria uzinduzi wa kampuni wa ofisi ya kampuni hiyo jijini Arusha.

DC MBULU: AWAOMBA WANANCHI KUMUUNGA MKONO RAIS MAGUFULI

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Chelestino Mofuga amewataka wananchi wamuunge mkono Rais John Mafuguli, katika kuhakikisha anasimamia rasilimali za watanzania na kufanikisha maendeleo ya sekta mbalimbali.

Kwa mujibu wa Mofuga, wakati inakaribia miaka miwili ya utawala wa Rais Magufuli amefanikisha maendeleo mengi ambayo yangeweza kufanyika kwa kipindi cha utawala wamuda wa miaka 40.

Akizungumza na wananchi wa wilaya ya Mbulu, alisema miongoni mwa maendeleo hayo ni kuzindua na kuanza kwa ujenzi wa reli ya umeme, kuhamisha makao makuu ya nchi Dodoma mpango uliodumu tangu mwaka 1973 na kuanza maandalizi ya ujenzi wa barabara za ghorofa kwenye jiji la Dar es salaam.

Alisema amefanikisha kuongezeka kwa pato la Taifa kupitia ukusanyaji wa kodi kutoka sh850 bilioni kwa mwezi alipokuwa anaingia madarakani hadi kufikia sh1.2 trilioni kwa mwezi hivi sasa.

Alisema pia Rais Magufuli amefanikisha ununuzi wa ndege na kufufua shirika la ndege la ATCL, kutoa elimu bure kwa shule za msingi na sekondari jambo linaloongeza usajili wa wanafunzi mara mbili.

"Amegundua watumishi wenye vyeti feki 9,932 na watumishi hewa 19,706 ambao mishahara yao ilikuwa inatumiwa na watu wachache badala ya kupelekwa kwenye shughuli za maendeleo za wananchi ikiwemo elimu, afya na maji," alisema Mofuga.

Alisema Taifa lilishuhudia historia nyingine baada kupokea ripoti ya tume aliyounda ya kuchunguza mchanga wenye dhahabu (makinikia) yenye wajumbe nane wenye taaluma mbalimbali za uhandisi na kuchukua hatua stahiki mara baada ya kupokea.

"Kwenye taarifa hiyo ilibainika kuwa thamani ya madini yote kwenye makinikia ni makontena 277 yenye thamani ya sh829.4 bilioni kwa viwango vya wastani na viwango vya juu ni sh1.4 bilioni yaani dhahabu iliyokuwa kwenye makontena 277 ni sawa na lori mbili za tani saba ba pick up tani 1.5," alisema Mofuga.

Alisema Taifa lilikuwa linahitaji kiongozi aina ya Rais Magufuli kwa muda mrefu na kutokana na utekelezaji huo unaofanyika wananchi wanatakiwa kumuunga mkono ili aongeze jitihada za kuhakikisha Tanzania inafika kwenye nchi ya maziwa na asali.

Mmoja kati ya wakazi wa eneo hilo Yohana Amnaay alisema pamoja na jitihada hizo za Rais Magufuli pia mkuu huyo wa wilaya ya Mbulu Mofuga, amekuwa na utaratibu mzuri wa kutatua kero za jamii hasa migogoro ya ardhi kwa kukutana na wananchi.

"Kila alhamisi DC wetu amekuwa na utaratibu wa kukutana na wananchi hivyo kupitia nafasi hiyo jamii imekuwa inatatuliwa kero zake kuliko kukaa na kusubiri viongozi wakubwa wafike Mbulu ndiyo wananchi wafikishe malalamiko yao kwao," alisema Amnaay.'

MWENGE WA UHURU WAKABIDHIWA WILAYANI UBUNGO UKITOKEA WILAYA YA KINONDONI

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mheshimiwa Kisare Makori amekabidhiwa Mwenge wa Uhuru na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe Ally Happi tayari kwa kuzuru katika Miradi mitano ya Maendeleo katika Manispaa ya Ubungo.

Akizungumza wakati wa Makabidhiano hayo Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori amesema kuwa Mwenge wa Uhuru umezuru kwa Mara ya Kwanza katika Wilaya mpya ya Ubungo hivyo historia mpya imeandikwa.

Alisema kuwa Mwenge wa Uhuru Kwa Mwaka 2017 katika Wilaya ya Ubungo utakimbizwa umbali wa Kilomita 46 na gharama ya Miradi yote Mwenge utakapopita ni Zaidi ya Bilioni 2.8

Mwenge wa Uhuru Mwenye kauli mbiu ya kutilia msisitizo kushiriki Kukuza Uchumi wa Viwanda kwa Maendeleo ya Nchi yetu umebeba jumbe mbalimbali ikiwemo ile ya Mapambano dhidi ya dawa za kulevya, tuwajali na tuwasikilize watoto na vijana utakapomaliza kutembelea Miradi ya Maendeleo katika Wilaya ya Ubungo utaelekea Mkoani Pwani.

Katika mbio za Mwenge Umebaba ujumbe mwingine wa kuhamasisha kupungua kwa maambukizi ya Virusi vya Ukimwi, Unyanyapaa na vifo vitokanavyo na UKIMWI.

Aidha watanzania wameombwa kushiriki kutokomeza Malaria kwa Manufaa ya Watanzia na jamii kwa ujumla.

Imetolewa Na;
Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo

MATUKIO KATIKA PICHA: YALIYOJIRI KATIKA KIKAO CHA 38, MKUTANO WA SABA BUNGE LA 11 MJINI DODOMA LEO MAY 31, 2017.

$
0
0
 Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Andrew Chenge akisoma dua ya kuliombea Bunge katika  kikao cha 38 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 31, 2017.
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mhe.Dk.Medard Kalemani akiwasilisha Randama za Makadirio na Matumizi ya Wizara yake  kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 katika kikao cha 38 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 31, 2017.
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 38 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 31, 2017.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza jambo na Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Harrison Mwakyembe katika kikao cha 38 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 31, 2017.
 Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Mhe.George Masaju akifuatilia jambo kutoka kwa Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Dk.Suzan Kolimba  katika kikao cha 38 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 31, 2017.Kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Ajira,Kazi,Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Prof Jumanne Maghembe akimskiliza Mbunge wa Mtama(CCM) Mhe.Nape Nnauye katika kikao cha 38 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 31, 2017.
 Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe.Khamis Kigwangalla akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 38 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 31, 2017.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 38 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 31, 2017.
 Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mhe.Dk Charles Tizeba akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 38 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 31, 2017.
  Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mhe.Ritta Kabati akiuliza swali katika kikao cha 38 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 31, 2017.
 Mbunge wa Arumeru Mashariki(CHADEMA) Mhe.Joshua Nassari akifurahi jambo na Mbunge wa Momba(CHADEMA) Mhe.David Silinde katika kikao cha 38 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 31, 2017.
 Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA) Mhe.Catherine Ruge akiuliza swali katika kikao cha 38 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 31, 2017. 
Mbunge wa Iramba Mashariki(CCM) Mhe.Allan Kiula akiuliza swali katika kikao cha 38 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 31, 2017. 

Picha zote na Daudi Manongi, MAELEZO, DODOMA.

MILIONI 180 ZAKUSANYWA MWEZI MEI KUTOKANA NA MAKOSA YA BARABARANI TABORA.

$
0
0

Na Tiganya Vincent, RS- Tabora

31 Mei, 2017

Jumla ya shilingi milioni 180 zimekusanywa na Jeshi la Polisi mkoani Tabora katika kipindi cha Mwezi huo kutokana na makosa mbalimbali yaliyofanywa na waindeshaji wa vyombo vya moto.

Takwimu hizo zilitolewa jana mjini Tabora na Kamanda wa Mkoa wa Tabora Wilbroad Mtafungwa wakati wa mkutano na waandishi wa habari ofisi kwake wakati akitoa ufafanuzi juu ya jitihada mbalimbali wanazozifanya katika kukabiliana na vitendo vya uhalifu mkoani humo.

Alisema makusanyo hayo yametokana tozo kwa madreva wa magari, pikipiki na bajaji na waendesha baiskeli walivunjia Sheria za Usalama barabarani katika kipindi hicho.

Kamanda alitaja baadhi ya makosa ni madereva wa Bodaboda kutovaa kofia ngumu wao na abiria wao , madereva wa magari kuendesha bila kuwa na leseni, mwendokasi, kutozingatia alama za barabara na kupakia abiria zaidi ya uwezo wa chombo cha usafiri.

Kamanda Mtafungwa alitoa wito kwa watu wote wanaoendesha vyombo vya moto Mkoani Tabora kuepuka kuvunja Sheria za Usalama Barabarani ili waokoe fedha wanazozipata zitumike kusaidia familia zao katika  matumizi mengine ya maendeleo badala kulipa faini.

“Naomba waendeshaji wa vyombo vya moto kuzingatia Sheria za Usalama barabarani ili wasipigwe faini ambazo zinawafanya watoe fedha ambazo zingewesaidia wao na familia katika shughuli mbalimbali” alisema Kamanda huyo wa Mkoa wa Tabora.

Aidha , alitoa wito kwa vijana wote wanaoendesha Bodaboda na baiskeli maarufu kama daladala kujisajili katika vituo(vijiwe) na kukaa katika maeneo yao waliopagwa na viongozi wao ili kuwasaidie kuwafichua baadhi ya Wahalifu kujificha katika usafiri huo.

Kamanda Mtafungwa alisema kuwa hatua hiyo itasaidia kuwabaini baadhi ya wahalifu ambao wanapenda kujificha katika kazi hiyo kwa kutokubali kukaa eneo moja kwa hofu ya kubainika uovu wao.

Katika hatua nyingine Jeshi la Polisi Mkoani Tabora linawashikilia watu sita wakiwemo madereva wa bodaboda wawili kwa tuhuma za kuvunja nyumba usiku na kuiba na wengine kununua mali inayodhaniwa ni ya wizi.

Kamanda Mtafungwa alisema kati ya watuhumiwa hao wanne walikiri kuhusika na uvunjaji nyumba na kuiba mali na wengine wawili walikutwa na mali zinazodhaniwa kuwa za wizi.

Aliwataja waliokamatwa kwa tuhuma za kuvunja nyumba ni Issa Maganga(27), Salum Maganga(19), Hamis Malale(24) na Amri Salum (20) wote wakazi wa Ipuli katika Manispaa ya Tabora .Kamanda Mtafungwa aliongeza kuwa walikutwa na mali zinazodhaniwa kuwa za wizi ni kuwa nia Maganga Salum(28) na Hussein Salum (28) wote wakazi wa Kiloleni Manispa ya Tabora.

Alivitaja vitu vilivyokamatwa ni pamoja na tairi za baiskeli 21, mzani mmoja na mawe yake, mikasi saba ya baiskeli , minyororo nane ya baiskeli, televisheni mbili inchi 32 , solar inchi 24 na kandambili jozi saba.

Vingine ni sigara pakiti 20 , Betri za radio jozi 18 , dawa za meno aina ya Whitedent na mafuta ya kujipaka.Alisema kuwa watuhumiwa hao walishindwa kudhibitisha uhalali wa mali hizo na hivyo nao wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani wakajibu makosa yanayowakabili.

Kamanda huyo alitoa wito kwa vijana mkoani Tabora kuacha kujiingiza katika vitendo vitakavyosababisha kukamatwa na hatimaye kupelekwa Mahakamani na kuongeza kuwa ni vema wakashiriki katika shughuli mbalimbali kama vile kilimo cha bustani ili kujipatia kipato halali badala ya kufikia kuvunja nyumba na maduka ya watu wengine.

SIX YEARS IN HEAVEN

$
0
0
Time is a healer so people say
It is now six years since God took you away
You went into a sleep that was long and deep
The vacant place you left in our home, will never be filled

Our darling mother, wife, sister, grandmother, we will always remember you

Your special smile

Your caring heart

That warm embrace, you always gave us

And most importantly, the astounding legacy you left behind

In our heart you will forever remain, Dr Helen IgobekoLugina


Helen, the bole of our family tree you are dearly missed by:

Husband – MaxmillianLugina

Son – Dr. Emmanuel Lugina

Daughter – Mary LuginaZangira

Son in law – Richard Zangira

Daughter – RoselindaLugina Reuben

Son in law – Kelvin Reuben

Granddaughter – Gabriella Zangira

Grandson – Nathan Zangira

Granddaughter – Joanna Reuben

Granddaughter – Juliana Reuben


Family and friends

TAIFA STARS KUANZA MAZOEZI USIKU NCHINI MISRI KUJIANDAA NA LESOTHO

$
0
0
Alfred Lucas, Misri.
TIMU ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' inatarajia kuanza mazoezi jioni ya leo  kujiandaa na mchezo wa kuwania nafasi muhimu ya kucheza fainali za Kombe la Mataiafa ya Afrika (AFCON) za mwaka 2019 zitakazofanyika NCHINI Cameroon.

Stars walioingia majira ya saa 7 usiku na kufikia katika mji wa Alexandria, Misri uliweza kuwasili salama na kwa niaba ya timu nzima, Kocha Mkuu, Salum Shabani Mayanga pamoja na viongozi wengine akiwamo Mkuu wa Msafara, Wilfred Kidao walishukuru Mungu kwa kusafiri salama hadi kufika hapa Alexandria kwa ajili ya kambi ya wiki moja kujindaa kucheza na Lesotho.

Akizungumza mara baada ya kukagua viwanja vya mazoezi leo asubuhi, Kocha Mayanga amesema  “Programu ya mazoezi kwa timu hii itaanza leo saa 2.00 usiku ingawa siku nyingine nitafanya asubuhi na jioni.”

Taifa Stars inayopiga kambi nchini Misri, inajiandaa na mchezo dhidi ya Lesotho utakaofanyika Juni 10 mwaka huu kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam mchezo uliopangwa  kuanza saa 2.00 usiku.

Mchezo dhidi ya Lesotho ni muhimu kwa Tanzania ikiwa ni mechi ya kwanza kwa Taifa Stars katika Kundi ‘L’ wakiwa na timu za Uganda na Cape Verde kuwania nafasi muhimu ya kucheza fainali za Kombe la Mataiafa ya Afrika (AFCON) za mwaka 2019 zitakazofanyika NCHINI Cameroon.

Wachezaji wanaounda kikosi hicho cha Kocha Salum Mayanga akisaidiwa na Novatus Fulgence ambaye ni kocha msaidizi Patrick Mwangata - kocha wa makipa pia yumo Meneja wa timu, Danny Msangi; Mtunza Vifaa, Ally Ruvu, Daktari wa timu ni Richard Yomba na Daktari wa viungo ni Gilbert Kigadye ni makipa Aishi Manula (Azam FC), Benno Kakolanya (Yanga SC) na Said Mohammed (Mtibwa Sugar). Walinzi wa pembeni wako Shomari Kapombe (Azam FC), Hassan Kessy (Yanga SC), Mohammed Hussein (Simba) na Gadiel Michael.

Walinzi wa kati ni Erasto Nyoni (Azam FC), Salim Mbonde (Mtibwa Sugar), Abdi Banda (Simba SC) na Nurdin Chona (Tanzania Prisons) ilihali viungo wa kuzuia ni Himid Mao (Azam FC) na Jonas Mkude kutoka Simba SC ambaye kwa sasa anapatiwa matibabu baada ya kupata ajali.

Viungo wa kushambulia Salum Abubakar (Azam FC), Said Ndemla (Simba SC) na Mzamiru Yassin (Simba) wakati viungo wa pembeni ni Simon Msuva (Yanga SC), Shizza Kichuya (Simba SC) na Farid Mussa (Teneriffe, Hispania). Washambuliaji wapo Mbwana Samatta (KRC Genk- Ubelgiji), Ulimwengu (AFC Eskilstuna – Sweden), Ibrahim Ajib (Simba SC), Mbaraka Yusufu (Kagera Sugar) na Abdurahman Mussa (Ruvu Shooting).
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Salum Mayanga (kulia) akikagua Uwanja ambao timu itautumia kwa ajili ya mazoezi kwenye kambi ya Tolip Sports City, Alexandia, Misri. Wengine ni kutoka kushoto Mkuu wa Msafara (HOD), Wilfred Kidao ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi ya TFF, Meneja wa timu, Danny Msangi na Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Novatus Fulgence.
Madakatari na lishe :Madaktari wa Taifa Stars, Dk. Gilbert Kigadye (aliyesimama kushoto) na Dk. Richard Yomba (aliyesimama kulia) wakitoa maelekezo ya chakula hitajika kwa baadhi ya wachezaji wa Taifa Stars.
Kocha wa Taifa Stars, Salum Mayanga (kulia) na viongozi wengine wakikagua ukumbi wa mazoezi ya viungo ‘Gym’.

BODI YA KWANZA YA CHUO CHA TAALUMA YA UREKEBISHAJI TANZANIA YAZINDULIWA

$
0
0
 Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa akitoa hotuba ya ufunguzi wa Bodi ya Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga, Dar es salaam leo Mei 31, 2017.
 Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia hotuba ya Mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga, Dar es salaam leo Mei 31, 2017.
 Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania ambaye pia ni Katibu wa Bodi hiyo Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza – SACP. Gideon Nkana akitoa historia fupi ya Chuo.
 Baadhi ya Wajumbe wa Bodi hiyo wakifuatilia hotuba ya Mgeni rasmi.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Dkt. James Jesse akitoa neno la shukrani baada ya hotuba ya Mgeni rasmi.
 Wajumbe wa Sekretarieti ya Bodi ya Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania wakitekeleza majukumu yao katika hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo.
 Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa(wa kwanza kulia) akiteta jambo na baadhi ya Wajumbe wa Bodi kabla ya uzinduzi rasmi uliofanyika Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga, Dar es salaam leo Mei 31, 2017.
 Wajumbe wa Bodi ya Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania wakiongozwa na mwenyeji wao Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, SACP. Gideon Nkana(wa kwanza kulia) kutembelea mazingira ya chuo hicho.
 Muonekano wa mbele wa Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania.
 Mgeni rasmi Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania. Walioketi kutoka kulia ni SACP. Gideon Nkana, Godfrey Semango na Dkt. Zena Mabeho. Kutoka kushoto ni DCP. Ally Lugendo, Bi. Catherine Jorome na Dkt. James Jesse. Waliosimama(kushoto) ni SACP. Dkt. Kato Rugainunura(katikati) ACP. Charles Novart na wa kwanza kulia ni SACP. Uwesu Ngarama(Picha zote na Kitengo cha Habari na Mawasiliano – Jeshi la Magereza)

NEEC NA TSN WASAINI MAKUBALIANO UHAMASISHAJI WA WANANCHI JUU YA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI

$
0
0
 Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC),Bi. Beng’I Issa kushoto na Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Magazeti ya TSN (Tanzania Standard Newspapers) Dk. Jim Yonazi kulia wakisaini makubaliano ya kufanya kazi pamoja ya uhamasishaji na uelimishaji wananchi juu ya uwezeshaji wananchi kiuchumi. Kazi hiyo itaanza na kongamano  la uwezeshaji wananchi linalotarajia kufanyika mjini Dodoma Juni 10, 2017 ambapo mgeni rasmi ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.(Picha na Mwanadishiwetu, Dar es Salaam).
 Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uuwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC),Bi. Beng’I Issa kushoto na Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Magazeti ya TSN (Tanzania Standard News PaperS), Dk. Jim Yonazi kulia wakibadilishana nyaraka baada ya kusaini  makubaliano ya kufanya kazi pamoja ya uhamasishaji na uelimishaji wananchi  juu ya uwezeshaji wananchi kiuchumi. Kazi hiyo itaanza na kongamano  la uwezeshaji wananchi linalotarajia kufanyika mjini Dodoma Juni 10, 2017 ambapo mgeni rasmi ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC),Bi. Beng’I Issa kushoto na Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Magazeti ya TSN (Tanzania Standard Newspapers), Dk. Jim Yonazi kulia (wote waliokaa) wakisaini makubaliano ya kufanya kazi pamoja ya uhamasishaji na uelimishaji wananchi juu ya uwezeshaji wananchi kiuchumi. Kazi hiyo itaanza na kongamano  la uwezeshaji wananchi linalotarajia kufanyika mjini Dodoma Juni 10, 2017 ambapo mgeni rasmi ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na waliosimama kulia ni Meneja Mauzo na Masoko, Bw. Januarius Maganga na k

wananchi wamekuwa na uelewa wa utekelezaji wa bajeti katika kipaumbele- Tacosode

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

BARAZA la Vyama vya Hiari na Maendeleo ya Jamii (Tacosode) limesema wananchi wamekuwa na uelewa kuhamasisha bajeti kuwa na kipaumbele kwa changamoto zinazowakabili.

Hayo ameyasema leo Meneja wa Miradi wa Tacosode, Koga Mihama wakati akizungumza waandishi wa habari juu wananchi kuwa na uelewa kuweka umuhimu bajeti katika halmashauri kutatua changamoto zinazowakabili.

Koga amesema kuwa uelewa huo umetokana na elimu waliopata katika mradi wa uhamasishaji wananchi kushiriki katika masuala ya afya katika kuangalia vipaumbele vya bajeti uliokuwa ukitekelezwa katika Mikoa ya Iringa pamoja na Dodoma.

Amesema kuwa wananchi mradi huo katika utekezwaji wake katika Halmashauri ya Iringa pamoja na Kongwa mkoani Dodoma wananchi wamekuwa na mwamko katika masuala ya afya ushiriki kwa kuchangia katika huduma za afya.

Koga amesema kuwa mradi huo ni wa miaka minne lakini umekuwa na matokeo katika wilaya ambazo umetekelezwa kwa wananchi kuwa na mwamko katika masuala ya huduma za afya kwa kuchangia hata nguvu zao pale panapobidi.

Aidha amesema kuwa mradi huo ukiisha wanaweza kufanya katika sekta zingine ili kuwa maendeleo ya katika masuala mbalimbali kutatuliwa.

Meneja wa Miradi wa Tacosode, Koga Mihama akizungumza na waandishi wa habari juu ya baraza hilo linavyofanya kazi katika mradi wa afya, leo jijini Dar es Salaam, Kulia ni Afisa Habari,Said Juma na Kushoto ni Afisa mradi wa Tacosode, Nobelrich Ekonea

MAJALIWA ATEMBELEA MAONYESHO YA UJENZI WA NYUMBA

$
0
0
*Ataka VIGUTA iende kwenye halmashauri, ihamasishe watumishi
*Asema Watanzania wanataka nyumba bora, hawana muda wa kusimamia ujenzi

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezitaka Halmashauri za wilaya nchini ziangalie uwezekano wa kuwapatia watumishi wake nyumba za bei nafuu kwa malipo kidogo kidogo.

Amesema Halmashauri za wilaya kupitia mapato ya ndani, japo si makubwa zinaweza kuandaa mazingira yatakayowawezesha watumishi wake kupata nyumba kupitia mpango wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu unaofanywa na Muungano wa Vikundi vya Vicoba Tanzania (VIGUTA). 

Ametoa wito huo leo (Jumatano, Mei 31, 2017) mara baada ya kutembelea maonyesho ya Mpango wa Ujenzi wa Nyumba za Waheshimiwa Wabunge (Low Cost Housing) yanayoendelea kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma. 

Waziri Mkuu aliwashauri viongozi wa VIGUTA wafanye mawasiliano na Halmashauri zote na akawataka watenge muda wa kuzitembelea Halmashauri hizo ili kuonyesha nia na uwezo wao wa kujenga nyumba za gharama nafuu ambazo malipo yake hulipwa kidogo kidogo kwa lengo la kuboresha maisha ya Watanzania.

“Watanzania wengi hivi sasa wanapendelea nyumba ndogo, nzuri na ambazo zimekamilika. “Wengi wao, na hasa wafanyakazi, siku hizi wana shughuli nyingi na hawana muda wa kujenga nyumba na kuzisimamia wenyewe kama zamani. Hivyo, wanahitaji makampuni yanayoweza kuwanjengea nyumba na wao wakalipa kidogo kidogo,” amesisitiza.

Aliwaaasa viongozi wa VIGUTA wahakikishe kuwa wanajenga nyumba zenye ubora unaokubalika ili waweze kuaminika hali ambayo itawawezesha kupata wateja wengi zaidi.

“Katika kipindi hiki ambacho Serikali inahamia Dodoma, Muungano wa Vikundi vya VICOBA au VIGUTA unayo nafasi kubwa ya kuwapatia watumishi wanaohamia nyumba za kuishi kupitia mpango wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu,” Waziri Mkuu alisema.

Alisema watumishi wengi wanaoingia gharama kubwa kwa kuishi katika nyumba za kupanga huku wakilipa kodi, sasa wamepata kimbilio kwani wanaweza kujengewa nyumba kwa muda mfupi na kwa bei nafuu na wakalipa kidogokidogo kwa kipindi cha hadi miaka 15.

Naye, Mwenyekiti wa VIGUTA Taifa, Dkt. Salmin Ibrahim Dauda alimweleza Waziri Mkuu kwamba wana uwezo wa kujenga nyumba kwa gharama ya shilingi milioni 12, milioni 15, milioni 25 na milioni 60 kutegemeana na ukubwa wa nyumba.

Alisema wameweka viwango tofauti ili kuwawezesha Watanzania wenye kipato cha chini kumiliki nyumba zao wenyewe.

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

S. L. P. 980,

40480 - DODOMA. 
JUMATANO, MEI 31, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama picha za nyumba wakati alipotembelea Maonyesho ya Mpango wa ujenzi wa Nyumba za Gharama Nafuu kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Mei 30, 2017. Maonyesho hayo yameandaliwa na Muungano wa Vikundi Vya Vicoba Tanzania (VIGUTA) .Kushoto ni Mwenyekiti wa Taifa wa VIGUTA, Dkt. Salmin Ibrahim Dauda.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi kifo cha Philemon Ndesamburo

Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images