Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

Bayport yaikomboa Halmshauri mpya ya Chalinze kwa kuwapatia kompyuta

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri mpya ya Chalinze mkoani Pwani, Edes Lukoa mwenye koti jeusi, akipokea msaada wa kompyuta mbili kutoka kwa Mratibu wa Masoko wa Bayport Fiancial Services, Mercy Mgongolwa. Wanaoshuhudia ni Meneja wa Kanda ya Kati Christopher Kihwele kushoto kwa Mercy na Meneja wa wa Bayport Bagamoyo Francis Sumila na Katibu wa Mbunge wa Chalinze Ridhiwan Kikwete Idd Swala kulia kwa Mkurugenzi wa Chalinze.


Na Mwandishi Wetu, Chalinze

TAASISI ya Kifedha ya Bayport Financial Services, jana iliikomboa Halmashauri mpya ya wilaya Chalinze kwa kuipatia kompyuta mbili kwa ajili ya kupunguza changamoto za upungufu wa vifaa vya kiutendaji, ikiwa ni miezi michache tangu kuanzishwa kwa Halmashauri hiyo mpya.

Kompyuta hizo zilipokewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Edes Lukoa katika ofisi yake, ikiwa na lengo la kuhakikisha kuwa Halmashauri hiyo inatimiza wajibu wake wa kuwatumikia wana Chalinze na Watanzania kwa ujumla kwa kutumia kompyuta hizo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze Edes Lukoa akipokea kompyuta mbili kutoka kwa Taasisi ya Bayport Financial Services ikiwakilishwa na Mratibu wa Masoko Mercy Mgongolwa.

Akizungumza jana katika makabidhiano hayo wilayani Chalinze, Mratibu wa Masoko wa Bayport Financial Services, Mercy Mgongolwa, alisema kwamba lengo la kuipatia kompyuta hizo linatokana na dhamira ya kuona wilaya hiyo inasonga mbele kimaendeleo.

Alisema kugawa kompyuta hizo ni mwendelezo wa nia yao baada ya kuzindua ugawaji wa kompyuta hizo 205 zilizoanza kusambazwa katika ofisi mbalimbali za serikali baada ya kuzinduliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki.

“Tumefika katika Halmashauri hii kutoa kompyuta kwa Halmashauri ya Chalinze huku ikiwa tumeshafikisha msaada kama huu katika maeneo mbalimbali ya Tanzania kama vile Morogoro, Mwanza, Mara, Mbeya, Kilimanjaro na kwingineko. 

"Tunaamini kwamba msaada huu utakuwa na dira nzuri kwa watumishi wa umma wa Halmashauri hii ambayo ni mpya, hivyo ni madhumuni yetu kuona wanapata vitendea kazi vizuri ili wafanikiwe kuwatumikia Watanzania,” Alisema Mercy.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Edes Lukoa aliwashukuru Bayport kwa msaada wa kompyuta kwa ajili ya ofisi yao ambayo ni mpya baada ya kugawanywa kutoka katika Halmashauri ya Wilaya Bagamoyo.
“Tumepokea kwa furaha msaada wa kompyuta hizi na tunaamini kwa dhati kabisa itapunguza au kurahisisha utendaji kazi katika ofisi zetu za Halmashauri ya Chalinze kama wenyewe mlivyokusudia kwa kuanzisha utaratibu wa msaada huu.

“Tunaahidi kwamba tutazitumia vizuri kompyuta hizi pamoja na kufikisha huduma iliyokusudiwa kwa watu wote, ukizingatia kwamba kukua kwa sayansi na teknolojia kunalazimisha ofisi kutumia kompyuta ili kurahisisha utendaji kazi,” Alisema Lukoa.

Zoezi la kutoa msaada wa kompyuta katika ofisi mbalimbali za serikali lilianza mwishoni mwa mwaka jana, ambapo katika maeneo yote ambayo wamepeleka vifaa hivyo wamepokea vizuri na kuahidi utendaji kazi mzuri kwa utumia rasilimali hizo, huku Bayport ikiendelea kusambaza vifaa hivyo katika maeneo mengine yaliyopangwa na serikali kwa kupitia Wizara ya Utumishi.

UWANJA WA NAMFUA WATOA MATUMAINI KWA WANA SINGIDA.

$
0
0
Uwanja wa Namfua uliopo manispaa ya Singida ambao ukarabati wake umefikia hatua ya kuridhisha umeanza kutoa matumaini kwa wananchi wa Singida ambao wamekuwa wakifuatilia kwa karibu ukarabati wake.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akiwa pamoja na Mkuu wa Usalama wa Taifa Mkoa wa Singida wamefanya ziara ya kushtukiza kujionea hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa uwanja huo ambao utatumika kama uwanja wa nyumbani wa timu ya Mpira wa Miguu iliyobeba jina la mkoa ‘Singida United’.

Dkt. Nchimbi amesema anaridhishwa na kasi ya utengenezaji wa uwanja wa Namfua unaomilikiwa cha chama cha Mapinduzi Mkoa wa Singida huku akiupongeza uongozi wa CCM mkoa wa hatua ilipofikia uwanja huo kwakukwa ni tegemeo la fursa nyingi hasa za wajasiriamali wadogo.

“Chama cha Mapinduzi kimetengeneza fursa na ajira nyingi kwa wajasirimali mkoani Singida kwa kuukarabati Uwanja huu ili uweze kutumika na timu ya Singida United ambayo inatupa heshima kubwa wana Singida”, ameongeza Dkt. Nchimbi.

Ameongeza kuwa wananchi wa Singida wana hamu kubwa ya kuziona timu kubwa zinazocheza ligi kuu Tanzania bara zikicheza katika uwanja wa Namfua na hivyo kuitumia fursa hiyo kufanya biashara mbalimbali.

Aidha Dkt. Nchimbi amesema kuwa uwanja huo utakuwa ni chanzo cha mapato kwa mmiliki wa uwanja huo ambaye ni CCM Mkoa wa Singida, huku timu zitakazocheza, TFF na Manispaa ya Singida watapata mgao wao kulingana na taratibu zilizopo.

Kwa upande wao vijana waliokuwa wakishuhudia ukarabati wa uwanja huo wamesema wamejiandaa kuuza bidhaa kama jezi na vipeperushi vya timu kubwa huku wakisema watatoa kipaumbele katika kuuza na kuvaa jezi za timu yao ya Singida United.

Wameongeza kuwa uwanja huo ni faraja kwa kila mjasirimali mkoani Singida wakitoa mfano kwa wamiliki wa hoteli, nyumba za kulala wageni, wauzaji wa vinywaji na bidhaa ambazo zinapatikana mkoani Singida kwa ubora mkubwa ambazo ni asali, mafuta ya alizeti, kuku wa kienyeji, vitunguu bora na Viazi vitamu watapata wateja wa kutosha.  
 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akikagua ujenzi wa uwanja wa Namfua uliopo Manispaa ya Singida, kulia kwake ni Mkuu wa Usalama wa Taifa Mkoa wa Singida.
 Uwanja wa Namfua uliopo Manispaa ya Singida ukiendelea kukarabatiwa.
  Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akikagua ujenzi wa uwanja wa Namfua uliopo Manispaa ya Singida, kulia kwake ni Mkuu wa Usalama wa Taifa Mkoa wa Singida.
Uwanja wa Namfua uliopo Manispaa ya Singida ukiendelea kukarabatiwa.

Miss tz akabidhiwa gari lake

$
0
0

Hatimaye Miss Tanzania, Diana Edward Lukumay amekabidhiwa zawadi yake ya gari baada ya kusubiria tokea mwezi Oktoba mwaka jana.

Kampuni ya Lino International Agency ilishindwa kukabidhi zawadi ya gari kwa wakati baada ya mdhamini wa kwanza aliyeahidi kutoa zawadi hiyo kujitoa hatua za mwisho baada ya shindano hilo kuhamia Mwanza.

Hatua ya kukabidhiwa zawadi mrembo huyo imetokana na agizo la serikali wa Kampuni ya Lino International Agency kukabidhi zawadi za warembo walioshiriki katika mashindano ya mwaka jana ifikapo mwishoni mwa mwezi huu.

Kutokana na agizo hilo, kampuni ya Lino International Agency ilianza upya juhudi za kutafuta zawadi kwa mrembo huyo na kuzipata kampuni mbili, kampuni ya uzalishaji na usambazaji wa vipodozi asilia, Grace Product Ltd na duka la kuuza vito ;a Gift Jewellers ambapo kwa pamoja waliamua kununua gari aina ya Suzuki Swift yenye thamani ya Sh milioni 9.

Mbali ya kununua zawadi hiyo, kampuni hizo pia zililifanikisha usajili wa gari hiyo na kupewa namba ya usajiliwa,T625DKL.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa zawadi hiyo, Diana aiwataka warembo wanaoshiriki katika mashindano ya Miss Tanzania kuwa wavumilivu ili kukabiliana na changamoto mbalimbali za mashindano hayo zinazotokana na matatizo ya kiuchumi.

“Nimefurahi sana kukabidhiwa gari langu, nimeisubiri kwa muda mrefu na unatakiwa kywa mvumilivu ili kuendelea kuwa na nidhamu, na sasa kwa kupitia gari langu, nitafanya kampeni yangu ya kupiga vita mimba za utotoni na unyanyasaji kwa wanawake kupitia kampuni yake aliyoisajili,” alisema Diana.

Mrembo huyo pia aliwaomba warembo wajitokeza kushiriki katika mashindano ya hayo pamoja na matatizo yaliyowakumba wao.

“Mashindano mazuri sana yenye kujenga mtu na kumpatia kipato, tokea nimalize mashindano, nimeweza kupata dili mbalimbali ambazo sikutaka kuziweka wazi kwenye jamii, zimekuwa ni shughuli zangu za kila siku,” alisema.

Mkuu wa Itifaki wa Kampuni ya Lino, Albert Makoye aliwashukuru wadhamini wao na kwa sasa wanaanza pilika pilika za mashindano ya mwaka huu.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Grace Products ltd, Elizabeth Kilili alisema kuwa ameamua kudhamini zawadi ya gari kutokana na kuvutiwa na mashindano na hasa Diana ambaye anatumia vipodozi vya asili.

Mhasibu Mkuu wa duka la Gift Jewellers, Faudhia Salum alisema kuwa wamemua kuwezesha zawadi ya gari hiyo, kama moja ya shughuli zao za kijamii. Salum alisema kuwa wao kama wauzaji wa vito wamefarijika sana kusaidia mashindano hayo na hasa ukizingatia kuwa vito vingi uvaliwa na akina dada kwa lengo la kupendeza.
 Ofisa wa Basata akikabidhi funguo kwa Miss Tanzania 2016/2017 Diana Lukumai  kama ishara ya kumkabidhi mrembo  huyo gari yake aina ya Suzuki Swift pembeni yake Mkurugenzi wa Grace Products Ltd Elizabeth Kilili.
 Miss Tanzania 2016/2017 Diana Lukumai akiingia ndani ya gari yake mara baada ya kukabidhiwa
 Miss Tanzania 2016/2017 Diana Lukumai akifurahi mara baada ya kuingia ndani ya gari yake
 Mkuu wa Itifaki wa Kamati ya Miss Tanzania , Arbart Makoye akizungumza na Waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi gari
 Mkurugenzi wa Grace Products Ltd Elizabeth Kilili na Mumewe  wakikabidhi kadi ya gari kwa Miss Tanzania 2016/217 Diana Lukumai
 Mkurugenzi wa Grace Products Ltd Elizabeth Kilili. akizungumza na Miss Tanzania 2016/2017 Diana Lukumai katika duka la ke lililopo City Mall jijini Dar es Salaam.

TANESCO YAWAOMBA WANANCHI KUTOA TAARIFA MAPEMA WAONAPO HITILAFU YA UMEME ILIYOSABABISHWA NA MVUA AUKITU KINGINE

$
0
0

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
SHIRIKA la Umeme Tanzania, (TANESCO), limewaomba wateja wake na wananchi kwa ujumla kutoa taarifa mapema mara inapotokea hitilafu ya umeme iliyosababishwa na mvua au sababu nyingine.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo Mei 11, 2017, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka, (pichani juu), alisema, sambamba na hilo pia wananchi wasifanye shughuli au kukaa chini ya miundombinu ya umeme.
“Lakini tunawaomba wananchi watoe taarifa haraka maeneo yenye mafuriko au mkusasnyiko wa maji mengi ili wataalamu wetu waweze kuchukua hatua za haraka.” Alisema.
Dkt. Mwinuka pia alisema endapo kuna nyaya, nguzo au kifaa chochote cha umeme kimepata hitilafu na kinahatarisha maisha ni vema uangalizi au alama ikawekwa ili kuwapa hadhari wapiti njia na watoto wasikaribie eneo hilo wakati mafundi wa TANESCO wakichukua hatua za marekebisho.
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini Tanzania (TMA), katika taarifa yake iliyotoa Mei 9, 2017 imeonya kuwa maeneo ya Pwani ya Kaskazini ikiwemo visiwa vya Unguja na Pemba, yatakabiliwa na vipindi vifupi vya mvua kubwa inayozidi milimita 50 ndani ya saa 24 kuanzia Mei 10 hadi 12, 2017. 

Aidha kwa upande wake, mtaalamu wa masualaya umeme kutoka TANESCO, Mhandisi Simon Kihiyo, amewahakikishia wananchi kuwa miundombinu ya TANESCO iko imara na salama, na hitilafu  zinazotokea za hapa na pale nyingizinasababishwa na sababu za kibinadamu, au za kimazingira kama vile nguzo za umeme kugongwa na magari, au miti kuangukia nguzo. 

"Naomba nitoe angalizo kwa wateja wetu, kama pametokea hitilafu yoyote ya umeem nyumbani kwako, ni vema ukatoa taarifa TANESCO au ukamtafuta fundi wa umeme mwenye taaluma badala ya kushughulikia tatizo hilo wewe mwenyewe ilihali ukiwa huna utaalamu na masuala ya umeme, kwani hiyo ni hatari."

Naye kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO Leila Muhaji amesema, katika kipindi hiki cha mvua kuna athari ndogo ndogo zimetokea kwenye miundombinu ya TANESCO hususan nguzo za umeme, lakini akatoa hakikisho kuwa mafundi wa TANESCO wanekuwa wakichukua hatua za haraka kurekebisha athari katika miundombinu ya umeme pindi tu zinapotokea.


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Dkt. Tito Mwinuka, (katikati), akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Me11, 2017. Dkt. Mwinuka ametoa hadhari kwa wananchi kutogusan miundombinu ya Tanesco hususan nyaya zilizoanguka, au kufanya shughuli yoyote karibu na miundombinu yab umeme katika kipindi hiki cha mvua kubwa zinazoendela kunyesha nchini. Kulia ni Mhandisi Simon Kihiyo, na kushoto ni Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Leila Muhaji.

 Mhandisi Simon Kihiyo, akitoa ufafanuzi wa kitaalamu kuhusu hatua za kuchukua pindi hitilafu ya umeme inapotokea
 Dkt. Mwinuka (kushoto) na MhandisiKihiyo, wakati wa mkutano huo leo
 Dkt. Mwinuka akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake
 Waandishi wa habari wakiwa kazini
  Waandishi wa habari wakiwa kazini
 Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Leila Muhaji, akitoaufafanuzi zaidi wa hatua za kuchukua endapo wateja au wananchi wataona hitlafu ya umeme kwenye maeneo yanayowazunguka
 Mhandisi Kihiyo, (kulia0na Kaimu Meneja Uhusianowa TANESCO Leila Muhaji katika mkutano na wanahabari
Mhandisi Simon Kihiyo, (kulia), Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Leila Muhaji (kushoto) na Afisa Uhsiano wa Shirika hilo, Henry Kilasila wakijadiliana jambo.

TADB YAKARIBISHWA KUWEKEZA ARUSHA

$
0
0
Wito umetolewa kwa Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Tanzania (TADB) kuchangamkia fursa za uwekezaji katika serkta ya kilimo na mifugo kwa kuwapatia mikopo wakulima wanaojishughulisha katika sekta hizo.

Wito huo umetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Mkoa wa Arusha, Bw. Richard Kwitega wakati akizungumza na ugeni kutoka TADB walipomtembelea Ofisini kwake kuzungumzia fursa za uwekezaji mkoani Arusha.

Bw. Kwitega amesema kuwa mkoa wa Arusha una fursa nyingi za uwekezaji hasa katika maeneo ya kilimo na ufugaji.

Akizungumza wakati wa mazungumzo hayo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Bw. Francis Assenga alisema uanzishwaji wa TADB unatokana na Serikali kutambua umuhimu wa uwekezaji wenye tija kwenye maeneo yote ya sekta ya Kilimo na kuleta mapinduzi ya dhati ya Kilimo ili kuwezesha upatikanaji wa mikopo na mitaji ya riba nafuu  ikiwa ni pamoja na kuhamasisha mabenki na taasisi zingine za fedha nchini kutoa mikopo zaidi kwenye sekta ya Kilimo.

Bw. Assenga mkoa wa Arusha utaingizwa rasmi katika mpango wa biashara wa Benki na ametoa wito kwa wakulima na wafugaji wa mkoa wa Arusha kuchangamkia fursa zinazotolewa na TADB.
Katibu Tawala Mkoa wa Mkoa wa Arusha, Bw. Richard Kwitega (katikati) akizungumza na ugeni kutoka TADB wakati walipomtembelea Ofisini kwake kuzungumzia fursa za uwekezaji mkoani Arusha. Ugeni uliongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), Bw. Francis Assenga (kushoto) akizungumza na Katibu Tawala Mkoa wa Mkoa wa Arusha, Bw. Richard Kwitega (hayupo pichani) wakati walipomtembelea Ofisini kwake kuzungumzia fursa za uwekezaji mkoani Arusha. Kulia ni Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Augustino Chacha.
Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Augustino Chacha (kulia) akizungumzia fursa za mikopo inayotolewa na Benki wakati akizungumza na Katibu Tawala Mkoa wa Mkoa wa Arusha, Bw. Richard Kwitega (hayupo pichani). Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), Bw. Francis Assenga.
Meneja wa Uendelezaji wa Biashara wa TADB, Bw. Geofrey Mtawa (kulia) akitoa takwimu za mahitaji ya mikopo ya mkoa wa Arusha. Kushoto ni Afisa Mwandamizi wa Uendelezaji wa Biashara wa TADB, Bw. George Nyamrunda.
Katibu Tawala Mkoa wa Mkoa wa Arusha, Bw. Richard Kwitega (kushoto) akimkabidhi muhtasari wa maeneo ya uwekezaji Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), Bw. Francis Assenga (kulia).
Katibu Tawala Mkoa wa Mkoa wa Arusha, Bw. Richard Kwitega (kushoto) akimkaribisha Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Tanzania (TADB), Bw. Francis Assenga (kulia) wakati walipomtembelea Ofisini kwake kuzungumzia fursa za uwekezaji mkoani Arusha.

WAZIRI MKUU MAJALIWA AWAHAKIKISHIA WATANZANIA UPATIKANAJI WA SUKARI YA KUTOSHA NCHINI IKIWEMO KIPINDI CHA MFUNGO WA RAMADHANI

HUDUMA ZA AFYA ZISIFUNGWE WAKATI WA ZOEZI LA USAFI-MAJALIWA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa ngazi mbalimbali waweke utaratibu utakaoruhusu huduma za afya kuendelea kutolewa kwa wananchi katika maeneo yao hata kama zoezi la usafi la kila mwezi litakuwa linaendelea.

Serikali imeweka utaratibu wa wananchi kushiriki katika shughuli za usafi wa mazingira siku ya Jumamosi ya mwisho wa mwezi, zoezi ambalo linashirikisha watu wote wakiwemo wafanyabiashara na watoa huduma nyingine zoezi linalofanyika kuanzia saa 12.00 asubuhi hadi saa 4.00 asubuhi. 

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Alhamisi, Mei 11, 2017) Bungeni mjini Dodoma katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu wakati akijibu swali la Mheshimiwa Abdallah Ulega mbunge wa Mkuranga.

Mheshimiwa Ulega alitaka kupata kauli ya Serikali kuhusu maeneo ya kutolea huduma mbalimbali zikiwemo za afya ambayo hufungwa wakati wa zoezi la usafi linalofanyika kila mwezi nchini, jambo linalosababisha kero kwa wagonjwa na wengine wenye dharula.

Waziri Mkuu amesema “Hospitali na maeneo mengine ya kutolea huduma za afya hayawezi kufungwa, viongozi wa maeneo husika waweke utaratibu mzuri utakaoruhusu huduma hizo ziendelee kutolewa bila ya kuathiri zoezi la usafi wa mazingira,”.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali imeagiza tani 131,000 za sukari ili kukabiliana na upungufu uliopo nchini. Amesema Serikali iko macho na inajua maeneo yanayohitaji kuboreshwa kulingana na mahitaji.
 
 “Mahitaji ya sukari nchini kwa mwaka ni tani 420,000, ambapo tunazalisha tani 320,000, hivyo tunaupungufu wa tani 100,000 hata hivyo tumeagiza tani 131,000 na tayari tani 80,000 zimewasili nchini, ambapo kati yake tani 35,000 zimeingizwa sokoni,” amesema.

Ametoa kauli hiyo wakati akijibu swali lililoulizwa na Mheshimiwa Jaku Hashim Ayoub aliyetaka Serikali iwahakikishie wananchi upatikanaji wa sukari hususan katika kipindi cha mwezi Mtukufu wa Ramadhani unaotarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
DODOMA.
ALHAMISI, MEI 11, 2017.

Waziri Mhagama Afanya Ziara Mradi Wa Nyumba Za CDA Dodoma

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista akiwa katika ziara yake kukagua hatua za ukarabati wa nyumba za CDA zilizopo Kikuyu Dodoma kushoto kwake ni Mkurugenzi wa CDA Mhandisi Paskasi Muragili.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Mhandisi Paskasi Muragili akieleza hatua za ukarabati wa nyumba za Kikuyu kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama wakati wa ziara yake tarehe 11 Mei, 2017 Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akizungumza jambo na Mkurugenzi wa CDA Mhandisi Paskasi Muragili wakati wa ziara yake kukagua maendeleo ya mradi wa nyumba za Kikuyu tarehe 11 Mei, 2017 Dodoma. 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (mb) akisalimiana na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Mhandisi Paskasi Muragili wakati wa ziara yake katika Ukarabati wa nyumba za Kikuyu Dodoma, tarehe 11 Mei, 2017 wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Ofisi ya Waziri Mkuu Bw.Issa Nchasi
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiangalia mazingira ya nyumba za mradi wa CDA zinazoendelea kukarabatiwa kwa ajili ya watumishi watakao hamia Dodoma awamu zijazo wakati wa ziara yake Kikuyu Dodoma. 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ziara yake ya kukagua ukarabati wa mradi wa nyumba za Kikuyu unaoendelea Mjini Dodoma. (PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU- DODOMA

…………………….

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Jenista Mhagama amefanya ziara katika mradi wa nyumba wa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma ili kujiridhisha na kazi ya ukarabati inayoendelea.

Ziara hiyo ilifanyika leo Mei 11, 2017 kwa lengo la kukagua hatua zilizofikiwa na CDA ili kuhakikisha watumishi wa Serikali wanaotarajiwa kuhamia kwa awamu zilizobaki wanaishi kwenye makazi mazuri.

“Tunatarajia ifikapo 28 Juni, mwaka huu CDA iwe imemaliza na kukabidhi nyumba za familia 48 kwa watumishi wa awamu ya pili wanaotarajiwa kuhamia mwezi Julai,”Alisema Waziri Mhagama.

Aidha, Waziri Mhagama alieleza kuwa nyumba zilizokarabatiwa awamu ya kwanza na ambazo tayari zinakaliwa na watumishi mazingira yake ni mazuri kwani hadi hivi sasa hakuna malalamiko yoyote aliyoyapata kutoka kwa watumishi hao.

“Hadi sasa tayari ukarabati umefikia asilimia 80 na sisi kama Serikali tunajukumu la kuisimamia CDA ili kufikia Juni mwaka huu nyumba ziwe zimekabidhiwa zote ili kuwapa mazingira mazuri watumishi wanaotarajiwa kuja awamu mbili zilizobaki”alisisitiza Waziri.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu, Mhandisi. Paskasi Muragili alieleza jitihada za ukarabati zinaendelea vizuri na zipo hatua za mwisho na tayari wameandaa mazingira ya kugawa kazi kwa wazabuni zaidi ya mmoja ili kufikia lengo la kumaliza ukarabati kwa wakati.

“Hadi sasa tunatarajia kupata mzabuni atakaye shughulikia ukarabati wa nyumba 78 za awamu ya tatu na mkataba unatarajiwa kusainiwa mwezi Juni ili kuendana na kasi ya Serikali ya kufikia adhma yake ya kuhamia Dodoma”.Alisema Mhandisi Muragili

Waziri Mhagama alimalizia kwa kusisitiza kuwa ukarabati ukamilikie kwa wakati ili ifikapo mwaka 2020 Serikali iwe imehamia Dodoma kwa Awamu zote tatu.

“Tumeamua,tunatekeleza na tunawahakikishia Watanzania wote ifikapo mwaka 2020 Serikali yote itakuwa imehamia Dodoma”.Alisisitiza Waziri

MATUKIO MBALIMBALI YA WAZIRI MKUU LEO BNGENI MJINI DODODA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni Freeman Mbowe, bungeni mjini Dodoma Mei 11, 2017    
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akijibu maswali ya papo kwa papo Bungeni mjini Dodoma Mei 11, 2017.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Mbunge wa Nkasi, Ally Bungeni mjini Dodoma Mei 11, 2017. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akijadili jambo na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu bungeni mjini Dodoma Mei 11, 2017.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Nchi,  Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama bungeni mjini Dodoma Mei 11, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Rombo Roman Joseph Selasini, kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma Mei 11, 2017, katikati ni Mbunge wa Vunjo na Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi James Francis Mbatia, (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

RAIS DKT. MAGUFULI PAMOJA NA MGENI WAKE RAIS WA AFRIKA KUSINI JACOB ZUMA WAHUDHURIA KATIKA JUKWAA LA WAFANYABIASHARA JIJINI DAR

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wafanyabiashara mbalimbali wa nchini pamoja na Afrika ya Kusini wakati aliposhiriki pamoja na Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma katika Jukwaa hilo  la Wafanyabiashara  jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma akisoma hotuba yake katika Jukwaa hilo la Wafanyabiashara wa Tanzania na Afrika Kusini lililofanyika jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma mara baada ya kutoka kwenye Jukwaa hilo la Wafanyabiashara wa Tanzania na Afrika Kusini lililofanyika jijini Dar es Salaam.
 Sehemu ya Wafanyabiashara mbalimbali wa Tanzania na Afrika Kusini waliohudhuria katika Jukwaa hilo la Wafanyabiashara jijini Dar es Salaam.

PICHA NA IKULU

DC KASESELA AFUNGUA WARSHA YA KUJENGA UELEWA KUHUSU PROGRAMU YA KUENDELEZA SEKTA YA KILIMO AWAMU YA PILI (ADSP 2)

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Richard Kasesela akizungumza wakati wa kufungua warsha ya siku tatu ya kuwajengea wadau uelewa wa pamoja kuhusu programu ya kuendeleza sekta ya kilimo Awamu ya pili nchini Agricultural sector Development Programme (ASDP 2), Programu inayotarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2017/2018 hadi 2027/2028. Leo Mei 11, 2017 Katika Ukumbi wa Hazina Mjini Iringa
Meya wa Manispaa ya kinondoni Mheshimiwa Benjamini Sitta ambaye pia ni mwenyekiti wa warsha akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha ya siku tatu ya kuwajengea wadau uelewa wa pamoja kuhusu programu ya kuendeleza sekta ya kilimo Awamu ya pili nchini Agricultural sector Development Programme (ASDP 2), Programu inayotarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2017/2018 hadi 2027/2028. Leo Mei 11, 2017 Katika Ukumbi wa Hazina Mjini Iringa
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha ya siku tatu ya kuwajengea wadau uelewa wa pamoja kuhusu programu ya kuendeleza sekta ya kilimo Awamu ya pili nchini Agricultural sector Development Programme (ASDP 2), Programu inayotarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2017/2018 hadi 2027/2028. Leo Mei 11, 2017 Katika Ukumbi wa Hazina Mjini Iringa
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Richard Kasesela mara baada ya ufunguzi wa warsha ya siku tatu ya kuwajengea wadau uelewa wa pamoja kuhusu programu ya kuendeleza sekta ya kilimo Awamu ya pili nchini Agricultural sector Development Programme (ASDP 2), Programu inayotarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2017/2018 hadi 2027/2028. Leo Mei 11, 2017 Katika Ukumbi wa Hazina Mjini Iringa
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo Na Mathias Canal, Dar es salaam akiteta jambo na Meya wa Manispaa ya kinondoni Mheshimiwa Benjamini Sitta ambaye pia ni mwenyekiti wa warsha wakati wa warsha ya siku tatu ya kuwajengea wadau uelewa wa pamoja kuhusu programu ya kuendeleza sekta ya kilimo Awamu ya pili nchini Agricultural sector Development Programme (ASDP 2), Programu inayotarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2017/2018 hadi 2027/2028. Leo Mei 11, 2017 Katika Ukumbi wa Hazina Mjini Iringa



Na Mathias Canal, Iringa 


Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Richard Kasesela amefungua warsha ya siku tatu ya kuwajengea wadau uelewa wa pamoja kuhusu programu ya kuendeleza sekta ya kilimo Awamu ya pili nchini Agricultural sector Development Programme (ASDP 2), Programu inayotarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2017/2018 hadi 2027/2028.

Alisema kuwa ili kukuza na kuendeleza sekta ya kilimo nchini wataalamu wote nchini wanapaswa kubadilishana ujuzi na kushauriana namna ya kuwa na kilimo chenya tija kuliko kuficha ujuzi walionao kwa muktadha wa maeneo husika pekee waliyopo hivyo ni vyema kutumia ujuzi wao kwa makubaliano na maelekezano kwani jambo hilo litachochea zaidi ukuzaji wa sekta ya kilimo nchini Tanzania.

Dc Kasesela ameyasema hayo wakati Akizungumza kwenye ufunguzi wa warsha hiyo inayofanyika katika Ukumbi wa Hazina Mjini Iringa, warsha inayowahusisha Makatibu Tawala wasaidizi upande wa uchumi kutoka mkoa wa Iringa na Pwani na Maafisa kilimo wa mikoa, Meya wa Manispaa/Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa halmashauri za Manispaa/wilaya, Wachumi wa Manispaa/Wilaya na Maafisa Kilimo wa Manispaa/Wilaya kutoka Katika Halmashauri za Manispaa na Wilaya kutoka Mkoa wa Pwani na Dar es salaam.

Dc Kasesela ameeleza kuwa Programu hii ya ASDP 2 imeandaliwa baada ya kukamilika kwa awamu ya kwanza ya ASDP 1 iliyotekelezwa kuanzia mwaka 2006/2007 hadi 2013/201 huku akiwapongeza waandaaji wa warsha hiyo ambao ni OFISI ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na kutaraji kutekelezwa na wadau mbalimbali kama vile Wizara za sekta ya kilimo, Wahisani, Sekta binafsi, Taasisi zisizo za kiserikali, Wakulima Wafugaji, na Wavuvi.

Dc Kasesela amesema kuwa Utekelezaji wa ASDP 2 utazingatia malengo ya mpango wa maendeleo wa miaka mitano (2016-2021), Mkakati wa Taifa wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi pamoja na Dira ya maendeleo ya Tanzania (2025).

Alisema kuwa Programu hiyo imezingatia vipaombele vya vizara ya Kilimo, Ufugaji na uvuvi na imelenga kutatua changamoto na kuchochea kasi ya ukuaji wa sekta ya kilimo, Kuongeza pato la Taifa, Kuboresha kipato cha wakulima wadogo na usalama wa chakula na lishe nchini.

Sambamba na hayo pia alisema kuwa wadau wote wa ASDP 2 wanapaswa kusimamia na kutekeleza kwa weledi maeneo makuu manne ya utekelezaji wa Programu hiyo ambayo ni Usimamizi wa Matumizi ya maji na ardhi (Sustainable Water and Land use Management),, Kuongeza tija na faida katika kilimo, mifugo na uvuvi (Enhanced Agricultural productivity and profitability).

Maeneo mengine ya kusimamiwa vyema na wadau ni Biashara na Uongezaji wa thamani kwenye mazao (Commercialization and Value Addition, na Viwezeshi vya sekta, Uratibu, Ufuatiliaji, na Tathmini ya sekta (Sector Enablers, Coordination and Monitoring and Evaluation).

RUFAA DHIDI YA MBUNGE WA BUNDA MJINI ESTER BULAYA YATIMBA MAHAKAMA YA RUFAA JIJIJI DARES SALAAM

$
0
0
 Aliyekuwa  kuwa Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Steven  Wassira  akiwa katika jengo la Mahakama ya Rufaa jijiji Dares Salaam akizungumza jambo na baadhi ya mawakili kabla ya kusikiliza kwa Rufaa ya kesi yake dhidi ya Mbunge wa Bunda mjini Ester Bulaya.  Katika kesi hiyo jopo la majaji watatu  wa Mahakama ya Rufaa limepanga kuendelea na kesi hiyo Jumatatu ijayo ya Aprili 15, mwaka huu. Uamuzi huo umetolewa  leo  Aprili 11, mwaka huu katika Mahakama hiyo  baada ya  Pande zote mbili  kutoa maelezo  ya sababu za rufaa.
Wakili wa Mbunge  wa Jimbo la Bunda Mjini, Tundu Lissu  akizungumza  jambo na mara baada kikao kilichokuwa kinasikiliza ombi la rufaa lilifunguliwa na  wapigakura wanne wa Jimbo la Bunda, kupinga  hukumu ya  Mahakama Kuu Kanda ya  Mwanza, kuhusu ushindi wa mbunge wa jimbo hilo, Ester Bulaya.
Wakili  Constantine  Mutalemwa  akifafanua  jambo kwa baadhi  ya waandishi  wa habari  mara baada kikao kilichokuwa kinasikiliza ombi la rufaa lilifunguliwa na  wapigakura wanne wa Jimbo la Bunda, kupinga  hukumu ya  Mahakama Kuu Kanda ya  Mwanza, kuhusu ushindi wa mbunge wa jimbo hilo, Ester Bulaya.(PICHA NA MAGRETH  KINABO)

WENYEVITI NA MAKAMU WENYEVITI WA KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE WAKUTANA NA WABUNGE WA BUNGE LA UMOJA WA ULAYA

$
0
0

Mwenyekiti wa Bunge, Mhe. Mussa A. Zungu akifafanua jambo wakati wa semina ya pamoja iliyoandaliwa na Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya dhidi ya Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa kamati za kudumu za Bunge, ikilenga kubadilishana uzoefu wa kiutendaji wa kazi, katika kikao kilichofanyika leo katika Hoteli ya Dodoma Mjini.
Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mary Nagu akizungumza jambo katika semina ya pamoja iliyoandaliwa na Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya dhidi ya Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa kamati za kudumu za Bunge, ikilenga kubadilishana uzoefu wa kiutendaji wa kazi, katika kikao kilichofanyika leo katika Hoteli ya Dodoma Mjini.
Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe. Naghenjwa Kaboyoka akizungumza jambo wakati wa semina ya pamoja iliyoandaliwa na Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya dhidi ya Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa kamati za kudumu za Bunge, ikilenga kubadilishana uzoefu wa kiutendaji wa kazi, katika kikao kilichofanyika leo katika Hoteli ya Dodoma Mjini.
Mjumbe wa Wabunge Vijana wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Abdallah Ulega akifafanua jambo wakati wa semina ya pamoja iliyoandaliwa na Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya dhidi ya Wabunge Vijana wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika kikao kilichofanyika leo katika Hoteli ya Dodoma Mjini.
Mwenyekiti wa Wabunge Vijana wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Upendo peneza akizungumza wakati wa semina ya pamoja iliyoandaliwa na Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya dhidi ya Wabunge Vijana wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania, katika kikao kilichofanyika leo katika Hoteli ya Dodoma Mjini.
Mwenyekiti Mwenza, Mhe. Dkt. Raphael Chegeni akiongoza semina ya pamoja ya iliyoandaliwa na Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya dhidi ya Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa Kamati ya Kudumu za Bunge, katika kikao kilichofanyika leo katika Hoteli ya Dodoma Mjini.

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

Government Launches 'Nipo Tayari' Campaign

$
0
0
Minister for Health, Community Development, Gender, Elderly and Children, Honorable Ummy Mwalimu (MP) speaks during the launches of sanitation campaign in Dodoma.








TANZANIA needs to end open defecation and have all people using improved toilets, to reflect the status of a middle-income country.

The Minister for Health, Community Development, Gender, Elderly and Children, Honorable Ummy Mwalimu (MP) and stakeholders conveyed this in Dodoma during a Call to Action event. The minister called for the national sanitation campaign, “To carry out a much bigger campaign far beyond the dimensions of the Mtu ni Afya.”

The National Sanitation Campaign launched in 2012 is ramping up its efforts to accelerate household sanitation improvements. The use of poor quality toilets and the practice of open defecation is a leading cause of illness and death from cholera, diarrheal diseases, and costs the country 1% of its GDP each year. Poor sanitation is also a major contributor to stunted growth of about 2.7 million children in Tanzania. Children who are more likely than their peers to struggle in school and earn less as adults.

The campaign is setting out new activities ranging from promoting improved toilets, hand washing with soap, water treatment at point of use, sanitation in schools and health care facilities to the provision of adequate toilets on highways and bus stops.

“I would request each one of you to join the government efforts of ensuring access to improved sanitation and hygiene,” said the Minister,to the assembled government staff, development partners, the private sector and public.

Over the past 25 years, open defecation has remained a problem. For instance, in 1990 the report shows that 10% of rural population had no toilets, 13% in 2000, 16% in 2011 and 13% in 2016. And over 55% of Tanzanians use unimproved toilets that are as damaging to health and the economy.

A World Bank assessment indicates that Tanzania is losing 1 percent of its GDP due to poor sanitation and hygiene. This is too high for a country like Tanzania that is aspiring for a mid-income economy by 2025. Moreover, UNICEF estimates a loss of 1.7 million children each year due globally to diarrhea and pneumonia which can both be prevented by a simple act of hand washing with soap and use of improved toilets.

As a step toward addressing the financing gap, the government has started allocating local funds into sanitation as exemplified by the 2017/18 budget for Ministry responsible for Regional Administration and Local governments. To facilitate the country achieve the access to improved Sanitation and Hygiene, the minister has called upon all the stakeholders to join the government efforts of ensuring access to improved sanitation becomes a reality.

“NIPO TAYARI”

MVUA ZAHARIBU MIUNDOMBINU YA BARABARA MKURANGA

$
0
0

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Kutokana na mvua zinazoendelea katika maeneo tofauti barabara mbili zimekata mawasiliano na kufanya baadhi huduma za kijamii kushindwa kufanyika.

Barabara zilizokata mawasiliano ni barabara ya Chamanzi kwenda Kibamba  pamoja na barabara ya barabara ya Mkuranga kwenda Hoyoyo.

Akizungumza kwa njia ya simu kutoka Dodoma, Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega amesema kuwa hali ya barabara katika jimbo lake ziko katika hali mbaya kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Amesema kuwa ameomba barabara ya Kimazichana kwenda Kibamba kuingizwa katika barabara za Tanroads ili ziweze kuangaliwa kutokana umuhimu wake katika uchumi wa nchi.

Diwani wa Kata ya Tengerea , Shaban Manda amesema kuwa barabara ya Mkuranga kwenda Hoyoyo makaravati yaliyowekwa hayawezi kuhimili mvua ikiwa kubwa.

Amesema wakandarasi wanatakiwa kushirikisha wananchi katika uwekaji wa madaraja na makaravati kutokana na wao ndio wanajua sehemu zenye matatizo.Manda amesema kuwa wakati mwingine sehemu zinazowekwa makaravati hayana umuhimu ndio maana mvua zikinyesha nayo yanakwenda na maji .

Mwenyekiti wa Kijiji cha Kimazichana , Omary Ndeu amesema hali mbaya kwa wananchi wa Mbezi na Kibamba hawawezi kufika kimazichana ambapo huduma za kijamii na biashara ndio zinafanyika.
Wananchi wakishuka katika daladala inayofanya safari zake Kibamba , Kimazichana na Dar es Salaam kwa ajili ya kuvuka kutokana na barabara hiyo kukatika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
Vijana wakitengeneza barabara ya dharula kwa ajili ya kupitisha magari na kupata kipato kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha. Picha zote na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii.
Barabara ya Mkuranga kwenda Hoyoyo ikiwa imekatika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
Diwani wa Kata ya Tengerea, Shaban Manda akizungumza na Michuzi Blog juu ya barabara hiyo kukatika na kukatika kwa mawasiliano.

TASISI YA KUIMARISHA HUDUMA ZA AFYA TANZANIA (THPS) YAANDAA MKUTANO WA SIKU MOJA WA WADAU WA MAPAMBANO YA VVU NA UKIMWI ZANZIBAR

$
0
0
Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo akifungua mkutano wa wadau wa mapambano ya ukimwi Zanzibar katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mbweni.
Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo akizindua Mpango Mkakati wa miaka mitano wa THPS katika mkutano wa wadau wa mapambano ya ukimwi uliofanyika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mbweni, anaeshirikiana nae katika uzinduzi huo ni Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Redempta Mbatia.
Mkurugenzi Mtendaji wa THPS Dkt. Redempta Mbatia akizungumza na wadau wa mapambano ya ukimwi Zanzibar katika mkutano wa siku moja uliofanyika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mbweni.
Muhudumu Mkuu wa huduma za mama na mtoto na huduma za upimaji vvu kwa jamii kutoka Hospitali ya Mwembeladu Mwanakhamis Alawi Nguzo akipokea zawadi maalum kutoka Waziri wa afya Mh. Thabit Kombo baada ya kuwa kituo bora katika mapambano ya ukimwi kipindi cha miezi mitatu Octoba – Disemba.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya kuimarisha huduma za afya Tanzania (THPS) Dkt. Redempta Mbatia akimkaribisha Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo alipowasili kufungua mkutano wa wadau wa mapambano ya ukimwi Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mbweni.
Na Ramadhani Ali-Maelezo


Taasisi zinazojishughulisha na mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU) na ukimwi Zanzibar zimetakiwa kuelekeza nguvu katika makundi maalum ambayo maambukizi bado ni makubwa.

Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo alitoa ushauri hao alipokuwa akifungua mkutano wa siku moja wa wadau wa mapambano ya ukimwi uliotayarishwa na Taasisi ya kuimarisha huduma za afya Tanzania (THPS) na kuzindua mpango mkakati wa miaka mitano wa taasisi hiyo katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mbweni.

Alisema wakati Zanzibar inajivunia kuwa na asilimia chini ya moja ya maambukizi ya VVU, katika makundi maalumu maamukizi yapo kwa asilimia 10 hadi 19 ambapo ni hatari.

Aliyataja makundi hayo kuwa ni vijana wanaojidunga sindano za madawa ya kulevya, wanawake wanaofanya biashara ya ngono na wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao.

Alisema kunapokuwa na kikundi kidogo cha watu wenye hali kubwa ya maambukizi ya VVU hatari ya maambukizi inaelekea kwenye jamii.

“Makundi maalum yanaonekana kuwa ni daraja la maambukizi ya Virusi vya Ukimwi kutoka kwao kuja kwenye jamii, ”alisisitiza Waziri wa Afya.

Aliongeza kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeridhia kuyafanyia kazi malengo ya dunia ya kutokomeza kabisa maambukizi ya VVU ifikapo mwaka 2030 hivyo mashirikiano zaidi yanahitajika katika kufikia malengo hayo.

Hata hivyo alieleza kuwa ushiriki wa wananchi katika kupima VVU bado hauridhishi na wale wanaopima na kubainika na maambukizi wengi wao hawajiungi kwenye huduma za tiba na wachache wanaotumia dawa hawazitumii ipasavyo.

Waziri wa Afya alikumbusha kuwa wakati huu ambapo Zanzaibar inatekeleza Mpango wa kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa ujauzito lakini wanaume hawajitokezi kupima afya zao.

“Akinababa tuwasindikize wake zetu kliniki ili na sisi tupimwe Virusi vya ukimwi, hivi sasa tupo chini ya asilimia tano wakati wenzetu Tanzania Bara wamefikia asilia 80, “Waziri Mahmoud alihimiza.

Mkurugenzi Mtendaji wa THPS Dkt. Redempta Mbatia alisema katika kupambana na ukimwi Zanzibar, taasisi hiyo imekuwa ikiwajengea uwezo wafanyakazi wa afya na taasisi nyengine zinazoshiriki katika mapambano hayo.

Aidha alisema wamekuwa wakisaidia masuala ya uongozi pamoja kuimarisha utawala bora na kusaidia vifaa tiba katika Hospitali na vituo vya afya ili kuhakikisha huduma za afya zinakuwa endelevu na kufikia malengo yaliyowekwa.

RAIS WA AFRIKA KUSINI JACOB ZUMA AWASILI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MWENYEJI WAKE RAIS DKT. MAGUFULI

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma wakati wa Nyimbo za Mataifa mawili (Tanzania & Afrika Kusini)  zikipigwa katika viwanja wa Ikulu jijini Dar es Salaam. 
 Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma akipita kukagua Gwaride la Heshima aliloandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma wakati wakiangalia vikundi vya ngoma za asili vilivyokuwa vikitumbuiza ndani ya viwanja vya Ikulu kwa Heshima ya ugeni huo wa Rais wa Afrika Kusini.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma kabla ya kuanza mazungumzo yao Rasmi Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma wakati wakielekea kwenye ukumbi wa mkutano kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya Kimaendeleo yahusuyo mataifa hayo mawili ya Tanzania na Afrika Kusini.
 Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma akipunga mkono wakati akiwasili Ikulu akiwa pamoja na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wanahabari mara baada ya kumaliza mazungumzo na mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma, Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma kabla ya kuanza kuzungumza na wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma akisoma hotuba yake wakati akizungumza na wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma mara baada ya kuzungumza na wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam.
  Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma akipiga ngoma wakati alipowasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma akizungumza jambo na Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Rais Dkt. John Pombe Magufuli
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mama Sizakele Zuma Mke wa Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma mara baada ya kufika ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akifurahia jambo pamoja na Mama Sizakele Zuma Mke wa Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma aliyeambatana na msaidizi wake Ikulu jijini Dar es Salaam.
Vikundi vya Matarumbeta vikitoa burudani wakati Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma alipowasili Ikulu jijini Dar es salaam. PICHA NA IKULU

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO IJUMAA MAY 12,2017

MAMA JANETH MAGUFULI AMKARIBISHA MAMA SIZAKELE ZUMA OFISINI KWAKE DAR ES SALAAM

$
0
0
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli (kulia) akiwa ameongozana na Mke wa Rais wa Afrika ya Kusini Mhe. Jacob Zuma, Mama Sizakele Zuma, wakati  wakielekea kwenye ofisi yake anayoendeshea shughuli za kijamii ikiwa ni pamoja na  kusaidia wazee walemavu na wale walioathirika na ugonjwa wa ukoma jijini Dar es salaam siku ya Alhamisi. Mama Zuma alikuwa ameongozana na mumewe aliyekuwa katika ziara ya kikazi nchini.
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli (kulia) akiwa na Mke wa Rais wa Afrika ya Kusini Mhe. Jacob Zuma, Mama Sizakele Zuma,  kwenye ofisi yake anayoendeshea shughuli za kijamii ikiwa ni pamoja na  kusaidia wazee walemavu na wale walioathirika na ugonjwa wa ukoma jijini Dar es salaam siku ya Alhamisi. Mama Zuma alikuwa ameongozana na mumewe aliyekuwa katika ziara ya kikazi nchini.
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli (kulia) akiwa katika mazungumzo na Mke wa Rais wa Afrika ya Kusini Mhe. Jacob Zuma, Mama Sizakele Zuma,  kwenye ofisi yake anayoendeshea shughuli za kijamii ikiwa ni pamoja na  kusaidia wazee walemavu na wale walioathirika na ugonjwa wa ukoma jijini Dar es salaam siku ya Alhamisi. Mama Zuma alikuwa ameongozana na mumewe aliyekuwa katika ziara ya kikazi nchini.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli (kulia) akipeana mikono na Mke wa Rais wa Afrika ya Kusini Mhe. Jacob Zuma, Mama Sizakele Zuma,  kwenye ofisi yake anayoendeshea shughuli za kijamii ikiwa ni pamoja na  kusaidia wazee walemavu na wale walioathirika na ugonjwa wa ukoma jijini Dar es salaam siku ya Alhamisi. Mama Zuma alikuwa ameongozana na mumewe aliyekuwa katika ziara ya kikazi nchini.

LG YAZINDUA BIDHAA YA MPYA YA KIYOYOZI INAYOTUMIA UMEME MDOGO NA RAFIKI KWA MAZINGIRA

$
0
0

KAMPUNI ya vifaa vya Umeme ya Life Good (LG) imezindua viyoyozi ambavyo ni rafiki kwa mazingira kwa gharama za kuweza kumuda kwa kila mtanzania.

Akizungumza na katika hafla ya uzinduzi wa viyoyozi hivyo , Kaimu Mkurugenzi wa Idara Ushauri wa Wakala wa Majengo Nchini (TBA), Mhandisi Mtapuli Juma amesema vifaa vya LG vina ubora katika matumizi ya nishati ya umeme.

Amesema kuwa kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi ni muhimu kutumia vifaa vya umeme ambavyo ni rafiki wa mazingira bila kufanya hivyo itakuwa tunaharibu mazingira kwa vizazi vijavyo.

Amesema kutokana na mabadiliko ya tabia nchi hakuna mtu anayeweza kukwepa katika kutumia vifaa ambavyo vinakuwa ni rafiki wa mazingira.

Nae Mkurugenzi Mtendaji LG Electronics Afrika Logistics, Janghoon Chung, amesema kuwa wamefanya utafiti na kuona kuna mahitaji ya viyoyozi ambavyo vitakuwa ni rafiki wa mazingira na kutaka watu watumie bidhaa hiyo.

Amesema viyoyozi hivyo vinatumia nishati ndogo hali ambayo inafanya kila mtu kuweza kumudu matumizi ya viyoyozi pamoja na kulinda mazingira .Aidha amesema kuwa watu wanatakiwa kutumia vifaa ambavyo vinakuwa rafiki wa mazingira ambapo LG wameweza kuzalisha bidhaa kutokana na mahitaji ya sasa yaliyopo.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara Ushauri wa Wakala wa Majengo Nchini (TBA), Mhandisi Mtapuli Juma akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi wa viyoyozi iliyofanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Legency jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji LG Electronics Afrika Logistics, Janghoon Chung akingumza na waandishi habari juu ya ubora wa viyoyozi vya LG iliyofanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Legency jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Masoko Afrika Mashariki LG Electronics , Moses Marji akizungumza wakati wa uzinduzi wa bidhaa mpya kutoka LG
Meneja wa bidhaa za LG Afrika Mhandisi , Singh Chana akizungumza juu ya umuhimu wa bidhaa za LG katika uhifadhi wa Mazingira
Mkurugenzi Mtendaji LG Electronics Afrika Logistics, Janghoon Chung Akimkabidhi zawadi ya Televisheni mmoja wa washindi wa bahati nasibu iliyochezeshwa katika semina ya uzinduzi wa bidhaa mpya za Lg Tanzania , Ramachandran Veeraman
Watumbuizaji wa bendi ya Borabora wakiwa wanatoa burudani jukwaani
Afrika Mashariki Bendi ya muziki ya Borabora ikitoa burudani kwa watu waliofika katika mkutano huo.
sehemu ya wafanyakazi wa LG wakiwa katika picha ya pamoja
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images