Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

JARIDA LA WIZARA YA ARDHI , NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI

$
0
0
TOLEO Na. 8 LA JARIDA LA WIZARA YA ARDHI , NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetoa jarida lake la mwaka (Toleo Na. 8). Jarida hili haliuzwi. Kuna nakala chache ambazo zinapatikana Wizarani katika Kitengo cha huduma kwa mteja. Aidha, kutakuwa na nakala nyingine chache ambazo zitasambazwa katika maeneo mbalimbali kama; Wizarani na katika Ofisi za Halmashauri nchini.
Jarida hili litapatikana pia hivi karibuni kwenye tovuti ya Wizara (www.ardhi.go.tz).

Mwananchi pata nakala yako upate kuhabarika kuhusu shughuli na matukio mbalimbali ya Wizara.

Na. Kitengo cha Mawasiliano Serikalini – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

SIMBA YATANGULIA FAINALI YA FA

$
0
0
Mshambuliaji wa Simba, Mohamed Ibrahim ‘Mo’ (kushoto), akishangilia na beki wa timu hiyo, Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ baada ya kufunga bao pekee katika mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Azam FC uliofanyika leo Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. (Picha na Francis Dande).
Himid Mao akichuana na Mohamed Ibrahim.
Mashabiki wakishuhudia mchezo huop huku wakinyeshewa na mvua.
Mashabiki wa Simba wakishuhudia pambano la timu yao na Azam. 
Kipa wa Azam FC, Aishi Manula.
Mohamed Ibrahim 'Mo' (katikati), akiwania mpira na wachezaji wa Azam.
Beki wa Azam, Shomari Kapombe akichuana na Ibrahim Ajibu.
Mshambuliaji wa Simba, Mohamed Ibrahim 'Mo' akimlalamikia mwamuzi, Mathew Akrama kutoka Mwanza baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu.
Kocha wa Simba, Jackson Mayanja akitoa maelekezo kwa wachezaji wake.
Mshambuliaji wa Simba, Laudit Mavugo akiwania mpira na wachezaji wa Azam FC.
Mshambuliaji wa Simba, Laudit Mavugo akichuana na wachezaji wa Azam FC.
Mshambuliaji wa Simba, Fredrick Blagnon akipiga shuti.
Nahodha wa Simba, Jonas Mkude akitoa maelekezo kwa wenzake.
Nahodha wa Simba, Jonas Mkude akitoa maelekezo kwa wenzake.
Mwamuzi, Mathew Akrama kutoka Mwanza akimsimamia kipa wa Simba wakati akivaa gloves zake. 
Kocha wa Simba Joseph Omog akipeana mkono na kocha msaidizi wa Azam FC, Idd Cheche.
Kocha wa Simba Joseph Omog akipeana mkono na kocha msaidizi wa Azam FC, Idd Cheche.
Waamuzi wakitoka chini ya ulinzi baada ya mchezoa kumalizika.
Waamuzi wakitoka chini ya ulinzi baada ya mchezoa kumalizika.
Kocha wa Simba, Joseph Omog akipongezana na msaidizi wake, Jackson Mayanja.

Ngoma Africa band na muziki wao imetua kwa Wayaudi kutumbuiza sherehe za uhuru Yom Haatzmaut

$
0
0
Habari nyeti zimevuja kuwa Ngoma Africa band aka FFU bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya yenye makao kule ujerumaniinatua nchini Israel kutumbuiza katika onyesho maalum la siku ya uhuru wa nchi ijulikanayo kama  Yom Haatzmaut siku ya tarehe 1 mpaka 2 Mai 2017 mjini Tel Aviv,mmoja ya wanaitifaki wa maonyesho hayo Bi.Shimone amesema bendi hiyo ndio ya kwanza ya kiafrika kupata mwaliko wa kutumbuiza katika maonyesho hayo lakini akutaka kuelezea zaidi.Habari za uhakika zimevuja kuwa bendi hiyo imesafiri kimya kimya kutoka ujerumani kuelekea kwa wayaudi kwa ajili ya onyesho.

MKUU WA MKOA WA PWANI MHANDISI NDIKIRO AISHUKURU TANESCO KWA MSAADA WA VIFAA VYA USAFI.

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikiri, (kulia), akipeana mikono na Kaimu Meenja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), Bi. Leila Muhaji, wakati akipokea msada wa vifaa vya kufanyia usafi kwa ajili ya kituo cha Afya Mkoani mjini Kibaha Aprili 29, 2017.

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

MKUU wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikiro, ameishukuru TANESCO kwa msaada wake wa vifaa vya kufanyia usafi kwa ajili ya Kituo cha Afya Mkoani Mjini Kibaha.

Mhandisi Ndikiro alisema, hatua hiyo yaTANESCO ni ushahidi tosha wa kuunga mkono jitihada za serikali za kuhakikisha wananchi wanapatiwa huduma afya katika mazingira ya usafi.

"Niseme tu mlichokifanya ni kitu kizuri sana, na ningeshauri taasisi nyingine za umma na binafsi, kutoa sehemu ya faida wanayopata kutokana na shughuli zao na kurudisha kwa umma kwa njia ya kusaidia shughuli za kijamii kama hii ya usafi." Alisema.

Naye Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), Bi Leila Muhaji alisema, TANESCO kama mtoa huduma ya umeme kwa Wananchi na ikitambua kuwa wananchi ndio wateja wake wakubwa, pia imeona ni busara kusaidia serikali katika kuhakikisha mazingira yanayowazunguka kama vile kituo hiki cha afya yanakuwa safi." Alisema.

Bi. Leila pia alisema, TANESCO imetoa vifaa hivyo ili kuunga mkono juhudi za serikali za kuhamasisha umma kufanya usafi wa jumla kila mwisho wa wiki. "Tumeungana nanyi leo Jumamosi ambayo ni siku ya usafi, ili tufanye usafi pamoja kwenye kituo chetu hiki cha afya, kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, napenda muwashukuru sana na mpokee msada wetu huu mdogo ambao nina hakika utasaidia kwa sehemu fulani katika kuweka mazingira ya hospitali yawe safi." alsiema

Awali Mkuu wa Mkoa Mhandisi Ndikiro, aliwaongoza watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha, wafanyakazi wa TANESCO Mkoa wa Pwani na wachache kutoka makao makuu katika zoezi la kufanya usafi wa mazingira kwa kufyeka nyasi kuzunguka mazingira ya kituo hicho cha afya.
Mhandisi Ndikiro, akiwa na Mganga Mkuu wa Mji wa Kibaha, akitoa hotuba yake
Bi leila Muhaji, (katikati), akitoa hotuba yake, Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikiro, na Meneja Rasilimali watu TANESCO mkoa wa Pwani, Bi.Nisile Mwakalinga
Wafanyakazi wa TANESCO mkoa wa Pwani
Mhandisi Ndikiro akimshukuru Bi.Nisile, huku Bi. Leila (wapili kushoto) na Bi Salama Juma, ambaye ni Afisa Uhusiano TANESCO
Wafanyakazi hawa wa TANESCO wakiwa wamebeba sehemu ya vifaa hivyo
Mhandisi Ndikiro, (kulia) na Bi. Leila Muhaji wakifyeka majani kwenye eneo la Kituo hicho cha Afya
Wafanyakazi wa TANESCO wakifagia mazingira kuzunguka kituo hicho 
Mganga Mkuu wa Mji wa Kibaha, akifafanua baadhio ya mambo kwa waandishi wa habari
Watumishi wa Halmashauri ya mji wa Kibaha, wakifyeka nyasi
Baadhi ya wafanyakazi wa TANESCO
Baadhi ya wafanyakazi wa TANESCO
Mhandisi Ndikiro akiwa amenyanyua baadhi ya vifaa alivyokabidhiwa
Watumishi wa kituo hicho cha afya wakikusanya sehemu ya vifaa hivyo
Mtumishi wa kituo cha Afya cha Mkoani mjini Kibaha, akwia amebeba sehemu ya vifaa hivyo

JUMUIYA YA WATANZANIA WANAOSOMA BEIJING WAADHIMISHA MIAKA 53 YA MUUNGANO

$
0
0

Mwenyekiti wa Jumuiya ya watanzania wanaosoma Beijing Nchini Husein Mtoro ( katikati) aliyemwakilisha Balozi,aliambatana na Viongozi wote Wakuu akiwemo Makam Mwenyekiti Khamis Ngwali,Katibu Mkuu Ndugu Remidius Emmanuel,Naibu Katibu Mkuu Ndugu Alinanuswe Mwakiluma na Mweka Hazina Ndugu Kulwa Gamba.
 
Pamoja nao,Viongozi waasisi wa Umoja huo Ndugu Suleiman Serera na Irenius Kagashe nao walishiriki sambamba na Viongozi wastaafu wengine akiwemo Makam Mwenyekiti Mstaafu Ndugu Kassim Jape,Katibu Mkuu Mstaafu Angelina Makoye,Mtunza Hazina Mstaafu Lusekelo Gwassa katika maadhimisho ya muungano yaliyofanyika mapema wiki hii kwa kushriki maonesho ya utalii na utamaduni.
Baadhi ya watanzania wanaosoma katika chuo cha Beijing nchini China wakiwa katika maonesho ya utamaduni na utalii kama moja ya maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanzania mapema wiki hii.
Wadau wakipozi kwa picha
Maonesho ya utalii na utamaduni yakiendelea Jijini Beijing


Mmoja wa watanzania anayesoma Beijing akipamba maonesho hayo kwa bendera ya Tanzania wakati wa maonesho ya utalii na utamaduni ikiwa ni maadhimisho ya miaka 53 ya Mungano Hafla hizo zilifanyika mapemaa wiki hii.
Picha ya pamoja


Jumuiya ya Wanafunzi Watanzania wanaosoma nchini China,wameadhimisha kumbukumbu ya Miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa kushiriki MAONYESHO YA KIMATAIFA YA UTALII NA UTAMADUNI katika Viwanja vya Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Biashara na Uchumi jijini Beijing.
 
Akizungumza kwa niaba ya Balozi wa Tanzania nchini China Balozi MBELWA KAIRUKI,Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo,ndugu HUSSEIN MTORO aliwaasa Watanzania hao kudumisha Amani,Mshikamano na kushiriki katika ajenda muhimu za Taifa ikiwemo,kushiriki katika kukuza soko la Utalii kwa kutangaza Vivutio vya asili vya nchi yetu,kuhamasisha Watalii wengi wa kimataifa kutembelea vivutio mbali mbali vilivyopo Tanzania.Pia Mwenyekiti alifikisha salam za Balozi Mbelwa za kuwatakia kila la heri Wanafunzi wote walio katika hatua mbalimbali za kukamilisha Tafiti zao kwa ajili ya kukamilisha masomo yao.

MICHUANO YA COPA -UMISSETA YAZINDULIWA KWA KISHINDO DODOMA

$
0
0
 Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Selemani Jaffo akisalimiana na baadhi ya wachezaji wa timu zilizoshiriki uzinduzi wa michezo ya shule za sekondari nchini (Copa-UMISSETA) katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma jana, mara baara ya uzinduzi rasmi wa michuano hiyo itakayoendeshwa nchini kote kwa udhamini wa kampuni ya vinywaji baridi ya Coca-Cola. Hafla ya uzinduzi ilihudhuriwa na wanafunzizaidi ya elfu 20 kutoka shule mbalimbali za sekondari mkoani Dodoma. (Picha na Mpiga Picha Wetu, Dodoma).
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Selemani Jaffo akipiga penati kuashiria uzinduzi wa michezo ya shule za sekondari nchini (Copa-UMISSETA) katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma jana, mara baara ya uzinduzi rasmi wa michuano hiyo itakayoendeshwa nchini kote kwa udhamini wa kampuni ya vinywaji baridi ya Coca-Cola. Hafla ya uzinduzi ilihudhuriwa na wanafunzizaidi ya elfu 20 kutoka shule mbalimbali za sekondari mkoani Dodoma. (Picha na Mpiga Picha Wetu, Dodoma).
Vifaa vya michezo.
* Wanafunzi zaidi ya elfu 20 kutoka sekondari wahudhuria
Na Mwandishi wetu, Dodoma
Kiu ya wanafunzi na wadau wa michezi nchini kote kuhusiana na mashindano ya michezo na sanaa kwa shule za sekondari nchini imekatwa rasmi siku ya jana, baada ya kufanyika uzinduzi wa michuano hiyo kwenye uwanja wa Jamhuri, Dodoma.
Akifungua michuano hiyo kwa mkoa wa Dodoma,Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Selemani Jaffo alitoa pongezi kwa mchango wa kampuni ya Coca-Cola kuendeleza michezo mashuleni, huku akiwataka wakurugenzi wa halmashauri kote nchini kuhakikisha kuwa wanatenga viwanja vya michezo.
Vile vile, aliwaelekeza maafisa elimu ngazi ya tarafa, kata, wilaya, mikoa pamoja na wakurugenzi wa halmashauri nchini kuhakikisha kuwa vipindi vya michezo mashuleni vinaimarishwa na kutumika kwa ajili ya shughuli za michezo na si kufundisha masomo mengine.
“Mtoto anayekosa kushiriki michezo, hata akili yake huweza kufubaa. Michezo hujenga na kuimarisha afyaya mwili na akili, upendo, ushirikiano na uzalendo”, alisema Jaffo.
Aidha, aliongeza kuwa wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mitaa na makaibu tawala wa mikoa kuhakikisha kuwa kila shule ina viwanja vya michezo vyenye vipimo sahihi na kusimamia sharia ya elimu inayotaka shule inaposajiliwa lazima kuwa na eneo la viwanja vya michezo.
Ofisi ya Rais Tamisemi haitowaangusha walimu wote wa michezo nchini katika kutekeleza majukumu yao.
Kwa upande wake, wakati akihutubia hafla ya ufunguzi wa michuano hii, mwakilishi wa kampuni ya Coca-Cola nchini, Pamela Lugenge aliwahakikishia washiriki kuwakampuni hiyo itaendelea na dhamira yake ya kuunga mkono jitihada ya vijana mbalimbali nchini kote katika kuwasaidia kudhihirisha vipaji vyao kupitia mashindano mbalimbali ya michezo, ikiwa ni pamoja na uendelezaji wa udhamini wa michuano ya Copa-UMISSETA.
“Dhamira yetu katika kudhamini mashindano haya na kushirikiana TAMISEMI ni endelevu, tukiwa tumejidhatiti kuhakikisha tunaendelea kuunga mkono jitihada za kutambua na kuinua vipaji vya vijana ambao watakuja kuifikisha nyanja ya michezo nchini katika kiwango cha juu zaidi”, alisema Pamela.
Mbali na hayo, aliongeza kuwa “Pamoja na kuwepo changamoto ndogondogo za hapa na pale, tutaendelea kufanya kazi bega kwa bega na washirika wetu serikalini, pamoja na wadau wengine wote wa michezo nchini, ili kwa pamoja tuweze kufanikisha na kusaidia kukua kwa sekta ya michezo nchini, hususani mashindano ya mpira wa miguu pamoja na mpira wa kikapu kwa vijana”.
Alimalizia kwa kuwahakikishia wadau wa michezo nchini ya kwamba kwa mwaka huu kampuni ya Coca-Cola imejipanga kwa dhati, kudhihirisha ya kwamba michezo ni zaidi ya ushindani, kwa kuweza kuambatanisha mashindano haya na kujenga mshikamano wa timu shindani, urafiki na hata nidhamu kwa wachezaji na timu zinazoshiriki.

MBUNGE WA BUKOMBE AWATAKA WANANCHI KUVUNJA MAKUNDI YA VYAMA NA KUWA WAMOJA

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Dotto Biteko akiwa kwenye Mkutano wa kutatua na kusikiliza Kero za wananchi kijiji cha Bwenda Kata ya Kantente.
Meza Kuuu hakiwepo Mbunge wa Jimbo la Bukombe pamoja na viongozi wa Kijiji cha Bwenda na wa kata ya Kantente. 
Wananchi wakitoa kero zao mbele ya Mbunge wa Bukombe. 
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Dotto Biteko akikabidhi mpira kwa Mwenyekiti wa Kijiji ambayo ilikuwa imeombwa na vijana kwaajili ya kujiandaa na Kombe la Dotto Cup 
Diwani wa Kata ya Bulangwa Yusuf Mohamedi akielezea wananchi juu ya serikali ambavyo imejipanga kutatua Kero za wananchi juu ya Elimu pamoja na Huduma ya Afya.


Wananchi wa jimbo la Bukombe Mkoani Geita,wametakiwa kuachana na siasa ambazo zinaweza kusababisha kutokuwa wamoja katika kuleta maendeleo.

Hayo yamesemwa na Mbunge wa Jimbo la hilo Dotto Biteko wakati akizungumza na wananakijiji wa kijiji cha Bwenda Namba 9 Kata Ya Kantente ambao ulikuwa na lengo la kusikiliza Kero za wananchi na kutatua changamoto walizo nazo.

Amesema kuwa maendeleo ya sehemu yoyote hile hayawezi kuletwa kwa watu kutokuwa na umoja na upendo.

"Wana Bwenda inahitajika nguvu ya pamoja ili kuhakikisha tuna maliza changamoto za eneo letu, zikiwemo ukosefu wa miundo mbinu ya barabara, kituo cha Afya, miradi ya maji na kuzorota kwa ufaulu wa wanafunzi na niombe wazazi mshirikiane na walimu kwa kufuatilia kwa ukaribu zaidi maendeleo ya vijana mashuleni" Alisisitiza Dotto .

Hata hivyo ameongezea kuwa kwa vijana wameanza kutenga asilimia kumi ya mapato na tayari vikundi kumi vimekwisha kupatiwa Mkopo na kwamba ameshapata fedha nyingine ambazo ni milioni hamsini na moja kwaajili ya maendeleo na mikopo kwa vijana na wanawake.

Pia amewataka wanakijiji hao kutokuwaogopa viongozi wao na kuwaambia kama wameshindwa kutekeleza majukumu yao ambayo waliyahaidi wakati wakiomba Ridhaa ya kuongoza kwani ni wajibu wao kuakikisha wanawatumikia wananchi ambao waliwaomba kura wakati wa kampeni.

WADAU MICHAEL KESSY NA FRANSISCA WAMBURA WANG'ARA JIJINI MWANZA.

$
0
0
Wadau wetu wa nguvu, Bwana Michael John Kessy na Miss Fransisca Wambuwa hii leo April 29,2017 wameng'ara baada ya kufunga pingu za maisha katika Kanisa la Roman Catholic (RC) Kirumba Jijini Mwanza.

Ndugu, jamaa na marafiki wameungana na wadau hao kwenye hafla ya kuwapongeza kwenye ukumbi wa Sun City Hotel Jijini Mwanza ambapo kama kawaida, Mshereheshaji mahiri Jijini Mwanza, Katumba Maduwa ameongoza vyema sherehe hiyo.
Binagi Media Group
Muda wa kufungua shampeni
Maharusi wakikata keki
Wasaa wa maharusi kukata keki
Kwa upendo mkubwa, maharusi wakilishana keki
Best man Simba Akida na best lady Keflen Ezekiel wakijilisha keki

RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI ASHIRIKI IBADA YA JUMAPIL MJINI MOSHI

$
0
0
Rais Dkt John Pombe Magufuli amejiunga na waumini kwenye ibada ya Jumapili katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Usharika wa Moshi Mjini asubuhi hii. Rais Magufuli yuko mkoani Kilimanjaro kwa ziara ya kikazi ya siku tatu

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRIL 30,2017

TAARIFA POTOFU ZINAZOMHUSISHA BALOZI WA TANZANIA NCHINI UINGEREZA DKT ASHA-ROSE MIGIRO

$
0
0
Ubalozi wa Tanzania London umepokea Habari inayozagaa kwenye ukurasa wa mtandao wa kijamii wa instagram ikiwa na nukuu ifuatayo:

''Binafsi bado sijaona umuhimu na mafanikio ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zaidi ya vingozi kujikusanyia mali na utajiri mkubwa sambamba na kung'an'gania madaraka kwa nguvu. Mfano uchaguzi uliofanyika mwaka 2015 kwa yaliyotokea Zanzibar ni miongoni mwa Athari mbaya kabisa zinazotokona na Muungano,nadhani kila Mtanzania aliyaona"

Ukurasa huo wenyewe jina la UKUTA inaihusisha nukuu hiyo na jina la Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Dkt Asha Rose Migiro. 

Ubalozi wa Tanzania London unapenda kutumia fursa hii, kuwajulisha Watanzania Waishio Uingereza na Watanzania kwa ujumla kuwa Balozi Migiro ahusiki na nukuu hiyo kama inavyosambazwa.Hivyo ni wazi kuwa wanayoisambaza wana malengo ya kulichafua jina la Balozi Migiro kwa sababu wanazozijua wao. 

Ubalozi wa Tanzania London unaendelea kutoa wito kwa Watanzania Waishio Uingereza kutumia muda wao na mitandao ya kijamii kutoa mawazo chanya yatakayo imarisha Muungano wa Taifa letu na mustakabali wa maendeleo ya Nchi yetu na Watanzania wa pande zote za Muungano. 

Ubalozi wa Tanzania London 
29 Aprili 2017.

NSSF YASAIDIA UJENZI WA ZAHANATA KATIKA KIJIJI CHA MATAMA MKOANI RUVUMA

$
0
0

SHIRIKA la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), limetoa msaada wa vifaa vya ujenzi wa kituo cha Afya katika Kata ya Muhukuru, Kijiji cha Matama, Mkoani Ruvuma.

Vifaa hivyo, ni mifuko 800 ya saruji na nondo 400 zitakazosaidia kufanikiwa ujenzi wa kama njia yakuleta maendeleo katika jamii.Katika kufanikisha ujenzi huo, NSSF imetoa mifuko 800 ya saruji pamoja na nondo zipatazo 400.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano hayo Meneja wa NSSF Mkoa wa Ruvuma, Mariam Muhaji, alisema NSSF ni shirika kubwa la hifadhi ya jamii lenye ofisi katika kila mkoa wa Tanzania na wilaya zake.

Mpango wa ujenzi wa zahanati hiyo umetokana na ombi la Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kwa NSSF kuona jinsi ya kusaidia jamii inayoshi katika Kata ya Muhukuru ambao walikuwa wanatumia kilometa 62 kufika katika zahanati ya Muhukuru.

Msaada huo wa NSSF, unalenga kufanikisha mpango huo wa kuwapa wananchi unafuu wa kupata huduma za afya, hivyo kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo ya kukabidhi vifaa vya ujenzi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Songea Mjini, Oraleti Komando aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.

Naye Diwani wa Kata ya Muhukuru, Manfred Mzuyu alisema msaada huo umekuja kwa wakati muafaka kwani baada ya kukamilika, utapunguza kero wanayopata wakazi wa kijiji cha Matama.

Aidha, diwani huyo aliongeza kuwa ujenzi huo utasimamiwa kwa ukaribu kuhakikisha hakuna atakayehujumu ujenzi wa kituo hicho na kutoa wito kwa wengine kuiga mfano huo wa NSSF.
Mkuu wa Wilaya ya Songea, Oraleti Komando, akipokea sehemu ya msaada wa mifuko 800 ya saruji na nondo 400 kutoka kwa Meneja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Ruvuma, Mariam Muhaji. Hafla hiyo ilifanyika mkoani Ruvuma mwishoni mwa wiki.

Mkuu wa Wilaya ya Songea Mjini, Oraleti Komando, akimkabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na NSSF kwa Diwani wa Kata ya Muhukuru, Manfred Mzuyu. Kulia ni Meneja wa NSSF Mkoa wa Ruvuma, Mariam Muhaji.

Meneja wa NSSF Mkoa wa Ruvuma, Mariam Muhaji (wa tatu kulia), Ofisa Mwandamizi wa Masoko na Uhusiano, Amina Mmbaga (wa pili kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na maofisa wengini wa NSSF baada ya kukabidhi mifuko 800 ya saruji pamoja na nondo 400 kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati katika Kijiji cha Matama, Songea.
Wakzi wa Kijiji cha Matama Kata ya Mahukuru wakiwa katika hafla hiyo.
Sehemu ya msaada wa mifuko ya saruji iliyotolewa na NSSF kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Matama, Songea mkoani Ruvuma.

Kijana aliyetoka Dar hadi Arusha kwa baiskeli azindua rasmi kitabu chake

$
0
0
Mheshimiwa Nabii Mkuu Dr GeorDavie Royal Mkuu ,   jana amezindua rasmi kitabu cha " KUKIWA NA FOLENI" kilichoandikwa na Wiseman Luvanda.
Pia Nabii Dr.GeorDavie alimpongeza kwa kitendo chake  alichoamua kufanya kwa kuwa balozi wa barabarani  kwa kutoka Jijini Dar es salaam hadi mkaoni Arusha wa usafiri wa baiskeli.

Akizungumza na wadau waliohudhuria hafla hiyo mtunzi wa kitabu hicho alisema vijana wanapaswa kutumia vipaji vyao kwa kujituma, kuthubutu na kufanya kazi kwa nguvu  na si kulalamika kila siku,  jambo linalopelekea kuibuka kwa makundi mbalimbali kama vile Panya Road na mengineyo.

Aidha mwandishi huyo amewataka wadau mbalimbali kumuunga mkono katika kukinunua kitabu hicho cha " KUKIWA NA FOLENI" , ambacho pia amekiandika kwa lugha ya Kiswahili  ili kuweza kukisambaza nchi nzima.
Tazama baadhi ya picha za tukio hili hapo chini
Pichani ni Mwandishi wa kitabu hicho Wiseman Luvanda, Akizungumza na baadhi ya wadau waliohudhuria kongamano hilo jana Jijini Arusha. Picha na msumbanews blog
Nabii Mkuu Dr GeorDavie Royal Mkuu akipokea kitabu kutoka kwa Mwandishi Wiseman Luvanda.Picha na msumbanews blog
Baadhi ya wadau mbali waliojitokeza kwenye kongamano  la kuinuliwa viwango na uzinduzi wa kitabu hicho.Picha na msumbanews blog
Mwandishi Wiseman Luvanda akifuatilia kwa makini kongamano la kuinuliwa viwango ambalo lilifuatana na uzinduzi wa kitabu chake.Picha na msumbanews blog

RAIS DKT MAGUFULI AHUDHURIA IBADA YA JUMAPILI MAKANISA MAWILI TOFAUTI MJINI MOSHI

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitakiana amani na mmoja wa mapadre katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi Mjini alikohudhuria ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipokea Ekaristi Takatifu toka kwa Askofu Isaac Aman katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini alikohudhuria ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiungana na waumini  katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini katika ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
 Waumini wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli aliposalimia waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini katika ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
 Waumini wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimia waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini katika ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
 Waumini wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimia waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini katika ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
 Waumini wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli aliposalimia waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini katika ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiombewa na Askofu Isaac Aman katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini alikohudhuria ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiombewa na Askofu Isaac Aman katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini alikohudhuria ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiombewa na Askofu Isaac Aman katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini alikohudhuria ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na watawa katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini baada ya  ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini baada ya  ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
 Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo akitoa mahubiri wakati wa ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na waumini wengine wakimsikiliza Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo akitoa mahubiri wakati wa ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akikaribishwa na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo kuongea na wananchi baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akikaribishwa na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo kuongea na wananchi baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na waumini na wananchi baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na waumini na wananchi baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiombewa sala maalumu na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo kuongea na wananchi baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Said Meck Sadick wakati wa kuhitimisha ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongozana na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo, Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Muhagama, Askofu Mstaafu Evarist Kweka wakipata picha ya pamoja  baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo na Askofu Mstaafu Evarist Kweka baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo na Askofu Mstaafu Evarist Kweka na kiongozi mwingine baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017. PICHA NA IKULU

WAZIRI MAGHEMBE AZIPA HADHI HOTEL ZA DAR ES SALAAM

$
0
0

Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe akizungumza kabla ya kukabidhi vyeti vya kutambua hadhi za Hotel zilizopo jijini Dar es Salaam na kwa kuzipa madaraja mpaka nyota tano katika sokola utali hapa nchini
Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe akikabidhi cheti kwa Meneja Masoko na Mauzo wa Serena Hoteli,Seraphin Lusala mara baada ya Hoteli hiyo kutambuliwa kuwa na hadhi ya Nyota tano katika mkoa wa Dar es Salaam, katika hafla fupi iliyoandaliwa na Wizaraya Maliasili na Utalii katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam
Majaji ambao waliokuwa wakitoa maksi ya hadhi za hoteli hapa nchini wakisimama kujitambulisha kwa wageni waliofika
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Generali Gaudence Milanzi akizungumza na Wamiliki wa Mhoteli jijini Dar es Salaam leo kabla ya kukabidhi vyeti vya madaraja ya hotel zao
Afisa utalii kutoka bodi ya Utalii Tanzania (TTB),Irene Mville akitoa maelekezo kwa wadau wa mahoteli ambao walifika katika hafla ya ugawaji wa madarajana viwango katika Hoteli zilizopo jijini Dar es Salaam
Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe akiwa katika picha ya pamoja na wamiliki wa Hotel jijini Dar es Salaam

VODACOM YATOE ELIMU YA HISA SAUT MWANZA

$
0
0
Meneja wa wateja wakubwa kutoka wakala wa hisa(Orbit Securities) Godfrey Gabriel,akiwasilisha mada ya umuhimu wa kununua hisa kwa wanafunzi wa chuo cha Mtakatifu Augustine Mwanza leo, wakati wa semina iliyofanyika chuoni hapo leo. 
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano Vodacom Tanzania Jacqueline Materu,akizungumza na wanafunzi wa chuo cha Mtakatifu Augustine Mwanza leo, wakati wa semina ya elimu ya ununuzi wa hisa. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Oparesheni wa Kampuni ya uwakala wa hisa ya Oarbit Security Juventus Simon, akijibu maswali ya wanafunzi wa chuo cha Mtakatifu Augustine Mwanza leo, wakati wa semina ya umuhimu wa ununuaji wa hisa iliyofanyika chuoni hapo leo. 
Rais wa Serikali ya wanafunzi wa chuo cha Mtakatifu Augustine Makamba Bahati,akizungumza jijini Mwanza leo,wakati wa semina ya umuhimu wa ununuaji wa hisa iliyofanyika chuoni hapo. 
Wanafunzi wa chuo cha Mtakatifu Augustine, wakijisomea vipeperushi vinavyoonyesha jinsi ya kununua hisa za Vodacom Tanzania, wakati wa semina ya umuhimu wa ununuaji wa hisa iliyofanyika chuoni hapo jijini Mwanza leo.

WAWILI WAONDOKA NA PIKIPIKI SHIKA NDINGA BAGAMOYO

$
0
0
 Meneja wa Matukio na Mawasiliano wa Efm Radio, Neema Ukurasi Akizungumza na wakazi wa Wilaya ya Bagamoyo juu Shindano la Shika Ndinga ambalo limeweza kuwazawadia washindi wawili pikipiki aina ya Sunmoto  mara baada ya kufanikiwa kupita katika vipengele vyote katika shindano lililofanyika shule ya Msingi Majengo Bagamoyo
 Meneja wa Matukio na Mawasiliano wa Efm Radio, Neema Ukurasi akikabidhi  Pikipiki kwa mshindi kwa upande wa kina Dada Kawale Halidy  ambaye ameweza kuondoka na pikipiki ya SUNMOTO
 Meneja wa Matukio na Mawasiliano wa Efm Radio, Neema Ukurasi akikabidhi zawadi ya pikipiki kwa Mshindi wa Shika Ndinga upande wa Wanaume , Valerian Gilbert katika shindano lililofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Majengo Bagamoyo.
 Said Magongo akimbusu mkewe Kawale Halidy mara baada ya kufanikiwa kuondoka na pikipiki ya Sunmoto katika shindano la shika ndinga lililofanyika mkoa wa Pwani Wilaya ya Bagamoyo.
 Washiriki upande wa kina Dada wakiwa katika zoezi la mbio za kukimbia na vikombe vya maji
 Mchekeshaji kutoka Efm akitoa burudani kwa wakazi wa Wilaya ya Bagamoyo
 Washiriki wa shika ndinga upande wa Wanaume wakiwa katika hatua ya kujaza vikombe na kukimbia navyo
 Msanii wa michezo ya Sarakasi za Baiskeli , Junior Talent akiwa amekaa juu ya Baiskeli kwa satili isiyokuwa ya kawaida na kuwashangaza wakazi wengi wa Bagamoyo

 Majaji wakimshusha mmoja wa washiriki katika kipengele cha mwisho cha Shindano la Shika Ndinga
 Washiriki upande wa kiume wakiwa wameshikilia gari kisawa sawa katika hatua ya mwisho ya shindano hilo
Mmoja wa Watangazaiwa EFM radio akizungumza na wakazi wa bagamoyo walifurika katika kiwanja cha Shuleya msingi Majengo

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AWASILI MKOANI KILIMANJARO

$
0
0
 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasili mkoani Kilimanjaro na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Said Meck Sadik pamoja na viongozi wengine wa Serikali pamoja na Chama Cha Mapinduzi katika uwanja wa ndege wa KIA. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).Makamu wa Rais atahudhuria sherehe za wafanya kazi Mei Mosi zitakazofanyika kitaifa mkoani Kilimanjaro.

ORODHA YA MAJINA YA WATUMISHI WA UMMA WANAODAIWA KUWA NA VYETI VYA KUGHUSHI 'FEKI' HAWA HAPA

Dkt. Harrison Mwakyembe awataka Vijana kutenga muda wao kujisomea Vitabu.

$
0
0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mkwakyembe (kulia) akiwa amepokelewa na Mwandishi wa kitabu cha "Colour of Life", Bi. Ritha Tarimo siku ya uzinduzi wa kitabu hicho leo 30 Aprili, 2017 Jijini Dar es Salaam. 



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mkwakyembe pamoja na wageni waalikwa wakiangalia video inayoelezea maduhui ya kitabu cha "Colour of Life" kilichoandikwa na Mwandishi wa vitabu Bi. Ritha Tarimo, 30 Aprili, 2017 Jijini Dar es Salaam. 


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mkwakyembe akiongea na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa kitabu cha "Colour of Life" kilichoandikwa na Mwandishi wa vitabu Bi. Ritha Tarimo 30 Aprili, 2017 Jijini Dar es Salaam.

Mwandishi wa vitabu Bi. Ritha Tarimo akiongea na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa kitabu chake cha "Colour of Life"leo 30 Aprili, 2017 Jijini Dar es Salaam. 

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mkwakyembe akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kitabu cha "Colour of Life" kilichoandikwa na Mwandishi wa vitabu Bi. Ritha Tarimo. 30 Aprili, 2017 Jijini Dar es Salaam. 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mkwakyembe akiwa katika picha ya pamoja na familia ya Mwandishi wa vitabu Bi. Ritha Tarimo mara baada ya uzinduzi wa kitabu hicho 30 Aprili, 2017 Jijini Dar es Salaam. 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mkwakyembe akiwa katika picha ya pamoja na familia ya Mwandishi wa vitabu Bi. Ritha Tarimo pamja na wageni waalikwa mara baada ya uzinduzi wa kitabu hicho 30 Aprili, 2017 Jijini Dar es Salaam. (PICHA/HABARI NA BENEDICT LIWENGA-WHUSM)



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amewataka vijana kutumia muda wao kujenga utamaduni wa kujisomea vitabu badala ya kupoteza muda wao mwingi katika mitandao ya kijamii kwakuwa kusoma vitabu ndiyo msingi mzuri wa elimu.

Kauli hiyo ameitoa leo Jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa akizindua Kitabu cha “Colour of Life” kilichoandikwa na Mwandishi Bi. Ritha Tarimo ambapo katika hotuba yake aliyoitoa mbele ya wageni waalikwa amesisitiza suala la vijana kujenga utamaduni wa kupenda kusoma vitabu ili kukuza elimu yao.

Mhe. Mwakyembe ameeleza kuwa, baadhi ya vijana siku hizi wamekuwa wakitumia muda wao mwingi katika mitandao ya kijamii badala ya kujisomea, hivyo amewashauri wajifunze kutoka kwa Mwandishi wa Kitabu hicho ili waje kuwa waandishi hodari wa kutegemewa na Taifa.

Sambamba na rai hiyo, Waziri Mwakyembe amempongeza Bi. Ritha Tarimo kwa juhudi zake kubwa na maarifa katika kutunga na kuandika kitabu hicho ambacho amesema kuwa kitabu hicho ni kizuri na kina maudhui mazuri kwa vijana hususani wanafunzi, hivyo ameitaka jamii kumuunga mkono kwa kukisoma ili jamii ipate kuelimika.

“Ukimkuta mtu kama Ritha Tarimo anaandika kitabu katika kipindi hiki ambapo vitabu vinaonekana kuondolewa kwasababu ya maendeleo ya teknolojia, ni vema kumpa moyo na kumuunga mkono kwakuwa yeye ametuonyesha Watanzania kuwa hata sisi tunaweza, na kitabu hiki niwaambie ukweli kina maudhui ya kumtia moyo kijana ya kutokata tamaa katika maisha”, alisema Dkt. Mwakyembe.

Ameongeza kuwa, Serikali inauunga mkono juhudi zake za uandishi wa vitabu vyake na amechukua baadhi ya nakala za kitabu hicho kwa ajili ya kuzipelekeka kwa Waziri husika wa masuala ya Elimu Sayansi na Teknolojia ili kuona namna gani kitabu hicho kinaweza kuisaidia jamii.

Kwa upande wake Mwandishi Ritha Tarimo ameishukuru Serikali kwa kukubali wito wa kukizindua kitabu chake na pia utayari wa Serikali katika kumuunga mkono ili uandishi wake uwe wenye tija kwa jamii ya Watanzania.Ameeleza kwamba, kazi ya uandishi ameinza muda mrefu na leo ameweza kupata nafasi ya kuungwa mkono na Serikali pamoja na Watanzania mbalimbali ikiwemo familia yake na hatimaye kukamilisha kitabu hicho na kukizindua rasmi.

“Nakushukuru Mhe. Waziri kwa kutumia muda wako kuja kukizindua kitabu hiki, nakushukuru sana na sasa naamini ndoto zangu zinatimia, kitabu hiki nimekitengeneza katika umbo dogo ili kiweze kuwavutia watu wengi kwani kina maudhui mazuri kwa vijana na jamii nzima ya Kitanzania”, alisema Ritha.

Kitabu cha Colour of Life ni moja kati ya vitabu saba alivyoandika Mwandishi huyo ambacho pia kimepata fursa ya kuzinduliwa na Waziri Dkt. Harrison Mwakyembe na kwa mujibu wa mwandishi huyo, kitabu hicho kina maudhui mazuri kwa vijana katika kuwajenga kimaisha.
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images