Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE AKUTANA NA MKURUGENZI WA IFAD WA KANDA YA MASHARIKI NA KUSINI MWA AFRIKA

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akizungumza na Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Kilimo-IFAD wa Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bw. Sana Jatta alipofika Wizarani tarehe 28 Aprili, 2017. Pamoja na mambo mengine walizungumzia namna ya kuendeleza miradi ya kilimo na ufugaji hapa nchini kwa ajili ya kujihakikishia usalama wa chakula na lishe bora kwa maendeleo. 
Sehemu ya ujumbe kutoka Ofisi za IFAD hapa nchini alioambatana nao Bw. Jatta. Kulia ni Bw. Francisco Pichon, Mwakilishi na Mkurugenzi wa IFAD nchini akiwa na Bi. Mwatima Juma Afisa Miradi Mwandamizi wa IFAD nchini. 
Bw. Jatta nae akimweleza jambo Mhe. Dkt. Susan wakati wa mazungumzo yao. 
Sehemu ya ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Jestas Nyamanga, Bi. Eva Ng'itu, Afisa Mambo ya Nje na Bw. Charles Faini, Msaidizi wa Naibu Waziri. 
Mhe. Dkt. Kolimba katika picha ya pamoja na wageni wake.

RAIS DKT. MAGUFULI APOKEA TAARIFA YA ZOEZI LA UHAKIKI WA VYETI KWA WATUMISHI WA UMMA LEO MJINI DODOMA

$
0
0
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Taarifa ya zoezi la uhakiki wa vyeti  kwa Watumishi wa umma kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora Angela Kairuki katika Ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe katika vitabu hivyo vya taarifa ya zoezi la uhakiki wa vyeti  kwa watumishi wa umma alivyopokea kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora Angela Kairuki katika Ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma. Katikati ni Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan na wakwanza kushoto ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) Profesa Idris Kikula.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa kitabu cha Taarifa ya zoezi la uhakiki wa vyeti  kwa watumishi wa umma alivyopokea kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora Angela Kairuki katika Ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma. Katikati ni Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan na wakwanza kushoto ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) Profesa Idris Kikula.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akinyanyua juu Taarifa na vitabu vye majina 9,932 ya watumishi wenye vyeti vya kugushi.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe na kufungua boksi kubwa lenye majina ya watumishi zaidi ya 9,932 waliobainika kuwa na vyeti vya kugushi mara baada ya kupokea Taarifa ya zoezi la uhakiki wa vyeti  kwa watumishi wa umma kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora Angela Kairuki katika Ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia majina hayo pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan  mara baada ya kufungua boksi kubwa lenye majina ya watumishi hao wa umma ambao wamegushi vyeti vyao .
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisoma jina mojawapo la mtumishi aliyegushi cheti katika taarifa hiyo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiwa pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan wakiangalia vitabu vyenye majina ya watumishi wa Umma zaidi ya 9,932 waliogushi vyeti vyao vya elimu ya Sekondari.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa , Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako, Spika wa Bunge Job Ndugai, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora Angela Kairuki wakiminya kitufe kuashiria maadhimisho ya miaka 10 ya Chuo Kikuu cha Dodoma UDOM katika ukumbi wa Chimwaga mkoani Dodoma.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akihutubia viongozi mbalimbali, wanafunzi wa UDOM, pamoja na watumishi wa Umma mara baada ya kupokea Taarifa ya zoezi la uhakiki wa vyeti  kwa watumishi wa umma kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora Angela Kairuki katika Ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akagana na watumishi mbalimbali wa umma, viongozi pamoja wanafunzi wa UDOM mara baada ya kumaliza kuhutubia katika Ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akihutubia katika hadhara hiyo katika Chuo kikuu cha Dodoma UDOM.
 Wanafunzi wa UDOM wakisikiliza kwa makini Hotuba iliyokuwa ikitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika maadhimisho ya miaka 10 toka kuanzishwa kwake.
 Baadhi ya viongozi mbalimbali wakifatilia kwa makini Hotuba iliyokuwa ikitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika maadhimisho ya miaka 10 ya Chuo cha UDOM toka kuanzishwa kwake.
 Baadhi ya Makatibu wakuu pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali wakifatilia kwa makini hotuba iliyokuwa ikitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika ukumbi wa Chimwaga mkoani Dodoma.
 Baadhi ya Makatibu wakuu pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali, wanafunzi pamoja na walimu wa  UDOM wakipiga makofi wakati wakimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati akiwasili katika ukumbi wa Chimwaga mkoani Dodoma.
 Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akihutubia katika Ukumbi wa Chimwaga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Taarifa ya miaka 10 ya Chuo kikuu cha Dodoma UDOM katika ukumbi wa Chimwaga mkoani Dodoma. PICHA NA IKULU

Wakazi wa Manispaa ya Musoma Mjini Wadaiwa Mil. 271 za Kodi ya Ardhi

$
0
0
Na Husna Saidi- MAELEZO

Takribani shilingi milioni 271 zinadaiwa kwa wakazi wa Manispaa ya Musoma Mjini, Mkoani Mara ikiwa ni kodi ya Pango la Ardhi. 

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi alipofanya ukaguzi wa mfumo wa kodi ya ardhi hivi karibuni Mkoani humo.

Waziri Lukuvi alisema kuwa amekagua mfumo wa kodi wa manispaa ya Musoma mjini ili kuhakikisha wamiliki wote wa ardhi nchini wanalipa kodi kwa hiari kabla ya hatua za kisheria hazijafuata dhidi yao.

“Nimeagiza kesi za madai ya kodi zitolewe hukumu ndani ya siku moja tu ili wadaiwa waweze kuchukuliwa hatua ya kuuzwa kwa mali zao haraka”, alisema Lukuvi.

Aidha Waziri Lukuvi alimtaka Afisa Ardhi wa Manispaa ya Musoma Bw.Joseph Kamonga kuwasilisha majina ya wadaiwa hao katika Mahakama ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kupiga mnada majengo na mali zao kama wakikaidi kulipa kodi hiyo.

Kwa upande mwingine Lukuvi alifanya uzinduzi wa mpango kabambe (Master Plan) wa Manispaa ya Musoma na kuwapongeza viongozi na watendaji wa Manispaa hiyo kwa kuwa Manispaa ya kwanza nchini kuweza kuzindua mpango huo kutumia kampuni za ndani katika utekelezaji wa mpango huo.

Kufuatia hatua hiyo Waziri Lukuvi amezitaka Manispaa nyingine kutumia kampuni za ndani ya nchi ambazo zimesajiliwa na Wizara ya Ardhi katika kutekeleza mipango mbalimbali ya ulipaji kodi za ardhi. 

Pia Waziri Lukuvi aliiagiza Manispaa ya Musoma kuandaa mpango mkakati wa utekelezaji wa mpango kabambe kwa kutumia wataalam wao (wa serikali) au Makampuni ya ndani na kutoa nakala za kutosha ili mpango huo uwafikie wadau wote na kutaka mpango huo utafsiriwe kwa Kiswahili ili Madiwani na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa waweze kuwafikishia wananchi kwa urahisi.

WAZIRI MHAGAMA AKUTANA NA UONGOZI WA SHIVYAWATA - DODOMA

$
0
0
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiendesha mkutano na Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu walipokutana ofisini kwake Dodoma kujadili utekelezaji wa Majukumu yanayowahusu.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa SHIVYAWATA mara baada ya kumaliza mkutano wao, kushoto kwake ni Naibu wake (Kazi, Ajira na Vijana), Mhe. Antony Mavunde.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akizungumza jambo wakati wa mkutano wake na Viongozi wa SHIVYAWATA kujadili utekelezaji wa majukumu yao katika Ukumbi wa Ofisi yake Bungeni Dodoma Aprili 27, 2017.
 Wajumbe wa mkutano wa uongozi wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu nchini wakifuatilia maelekezo kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama wakati wa kikao chao Mjini Dodoma tarehe 27 Aprili, 2017.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu Bi. Ummy Nderinanga wakati wa mkutano wao na Waziri huyo ili kujadili utekelezaji wa majukumu uliofanyika Ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo Bungeni Dodoma.
(PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU - DODOMA)

BENKI YA KCB TANZANIA YADHAMINI MKUTANO WA WATANZANIA WANAOISHI NJE YA NCHI

$
0
0

Benki ya KCB Tanzania yadhamini mkutano wa Watanzania wanaoishi nchini Marekani. Mkutano huo utafanyika tarehe 5 – 7 Mei 2017 katika hoteli ya Wyndham Dallas Suites - Park Centrale, Dallas, Texas. Na unategemewa kuhudhuriwa na watanzania elfu moja kutoka majimbo mbalimbali ya Marekani.

Akizungumza kuhusiana na mkutano huu, Meneja Mahusiano wahuduma za kibenki kwa Watanzania wanaoishi nje ya Nchi, Bi. Shose Kombe alisema Texas ni mji wenye watanzania wengi wakiwemo wanafunzi, wafanyakazi na wafanyabiashara wenye mahitaji ya huduma za kibenki kutoka Tanzania.

“Tunaelewa kuwashughuli za kutafuta kipato na elimu hupelekea watanzania wengi kuenda sehemu mbalimbali duniani na kuishi huko kwa muda mrefu na hivyo huhitaji kuwekeza na kupata huduma za kibenki nyumbani wakiwa mbali na Tanzania.” Alisema Bi. Kombe.

Meneja huyo alisema kuwa Benki ya KCB inawapatia watanzania wanaoishi nje ya nchi huduma bora za kibenki ikiwemo akaunti za akiba (savings), akaunti za uwekezaji (Investment), akaunti za wanafunzi, akaunti za watoto na fursa ya kununua nyumba (Mortgage) kwa lengo la kuwawezesha watanzania hao kuendesha shughuli zao za kibenki Tanzania huku wakiwa nje ya nchi na kupata akiba zao pindi watakaporudi nchini Tanzania. 
 
Aliongeza kwamba huduma hizi za kibenki kwa watanzania wanaoishi nje ya nchini za papo kwa hapo (real time transactions), hivyo kuwawezesha wateja wake kufanya mambo kwa wakati na bila kadhia popote pale walipo duniani.

“Watanzania wanaoishi nje ya nchi wanapaswa kupata huduma za kibenki kwa haraka, usalama na bila usumbufu” alisema Bi. Kombe. Na hivyo tunasema “JIULIZE KWANINI uhangaike kuweka akiba na kuwekeza nyumba ni ukiwa mbali na Tanzania wakati benki ya KCB ipo?”

Akamalizia kwa kuwataka watanzania wanaoishi nje ya nchi na bado hawajajiunga na benki ya KCB kujiunga leo kupitia tovuti ya www.kcbbank.co.tz na kupata huduma za kibenki wakiwa nje ya nchi.

USAFI OFISI ZA CUF WAPIGWA ’ STOP’,

$
0
0
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Kitendo cha wanachama wa CUF kukusanyika kutoka maeneo mbalimbali kwa kigezo cha kufanya usafi kinaweza kusababisha uvunjifu wa amani atakethubutu kujitokeza atachukuliwa hatua za kisheria leo jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro akionesha madumu ya pombe haramu ya Gongo yaliyo kamatwa katika oparesheni ya jeshi la polisi leo jijini Dar es Salaam.
Picha za magari yanayodaiwa kuibiwa jijini Dar es Salaam.Picha na Emmanuel Massaka,Globu jamii.

Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam imezuia wanachama wa CUF kufanya usafi katika makao makuu ya chama hicho yaliyopo Buguruni kutokana na kuwepo kwa viashiria vya uvunjifu wa amani kutokana mvutano wa makundi mawili.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema ombi la kufanya usafi katika mazingira ya ofisi za chama hicho, lililowasilishwa na Mbunge wa Temeke, Abdallah Mtolea Aprili 27 mjini Dodoma.

Amesema kutokana na sababu za kiusalama pamoja na mgogoro wa muda mrefu unaoendelea ndani ya chama hicho, Mbunge huyo pamoja na wanachama wengine na wanashauriwa kila mmoja kufanya usafi katika eneo lake analoishi au analofanyia kazi.

"Kitendo hicho cha wanachama wa CUF kukusanyika kutoka katika maeneo mbalimbali kwa kigezo cha kufanya usafi kinaweza kusababisha uvunjifu wa amani na atakayethubutu kujitokeza atachukuliwa hatua za kisheria," amesema Sirro.

Wakati huo huo Kamanda Sirro amesema sakata la watu waliovamia mkutano wa iongozi wa CUF wilaya ya Kinondoni na wanahabari hadi sasa wanawashikilia watu saba akiwemo Mkurugenzi wa Mahusiano wa wa chama hicho, Abdul Kambaya.

Amesema upelelezi wa kesi hiyo, umefanyika vizuri na tayari jalada limefikishwa kwa Mwanasheria wa Serikali kwa ajili ya hatua zaidi ikiwemo kufikishwa mahakamani.

Jeshi hilo pia limewataka wananchi waliowahi kuibiwa magari yao kujitokeza katika Kituo cha Polisi Mbezi ili kuangalia kutokana,na kupatikana kwa magari matano yanayodaiwa kuibiwa jijini Dar es Salaam.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRIL 29,2017

SERIKALI YAWATAKA WAAJIRI KUJISAJILI KWENYE MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI (WCF)

$
0
0
Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano WCF, Laura Kunenge akimkaribisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama katika banda la WCF wakati wa maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi mwaka 2017 katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi mkoani Kilimanjaro

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama ametoa wito kwa waajiri wote nchini kujisajili kwenye Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF) kama sheria inavyotaka.

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya Mahali pa kazi duniani yaliyofanyika Aprili 28,2017 kitaifa katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika mkoani Kilimanjaro, alisema bado kuna mwamko mdogo kwa waajiri kujisajili katika Mfuko huo. 

“Serikali inathamini sana juhudi zenu kama waajiri katika kuajiri wafanyakazi, niwaombe sana Chama Cha Waajiri nchini tushirikiane katika kuongeza hamasa ya kujisajili kwenye Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ili hatimaye, Wafanyakazi wenu waweze kupata stahiki (Mafao), zao pindi wapatwapo na matatizo ya kiafya wanapokuwa kazini,” alisema Waziri Mhagama. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Huduma za Matibabu na Tathmini kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi – WCF, Dkt. Abdulssalaam Omary Alisema mwitikio mpaka sasa kati ya waajiri 23,000 waliowabaini 700 pekee ndiyo wamesajiliwa katika mfuko huo hivyo kuiomba serikali isaide kuhamasisha waajiri wajisajili kwenye mfuko huo. 

Katika hatua nyingine Dkt. Omary alisema katika kipindi cha Mwezi Julai,2016 mpaka Machi 31,2017 wamepokea taarifa ya matukio 478 kutoka kwenye maeneo ya kazi. Alisema kati matukio hayo 478,matukio ya ajali ni 454,magonjwa sita na vifo 18 katika maeneo ya viwandani,migodini na vyombo vya usafiri ambapo waliopata ajali huduma ya fao la matibabu 

Aidha alisema mfuko huo unatoa mafao 7 ambayo ni mafao ya huduma ya matibabu,malipo ya ulemavu wa muda,malipo ya ulemavu wa kudumu,malipo ya anayemhudumia mgonjwa,huduma za ukarabati na ushauri nasaha,huduma za mazishi na malipo ya wategemezi. Angalia picha za matukio yaliyojiri katika banda la WCF katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi mkoani Kilimanjaro 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama amewataka waajiri nchini kujitokeza kwa wingi kujisajili katika Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (Workers Compesation Fund – WCF) kwa ajili ya kuwawezesha waajiriwa kupata mafao pindi wanapoumia,kuugua au kufariki wakiwa kazini. 
Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano WCF, Laura Kunenge akimkaribisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama katika banda la WCF wakati wa maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi mwaka 2017 katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi mkoani Kilimanjaro
Mkurugenzi wa Huduma za Matibabu na Tathmini kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi – WCF, Dkt. Abdulssalaam Omary akiwasilisha mada fupi kuhusu Mfuko huo ambapo alisema walengwa wa mafao yanayotolewa na WCF kuwa ni wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi ambao wataumia au kuugua kutokana na kazi walizoajiriwa nazo.


Dkt. Abdulssalaam Omary aliongeza kuwa walengwa wengine wa Mfuko huo ni wategemezi wa mfanyakazi atakayefariki kutokana na ajali au ugonjwa uliotokana na kazi.Katikati ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe.Jenista Mhagama akisikiliza mada fupi katika banda la WCF.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama akiuliza swali kwa Mkurugenzi wa Huduma za Matibabu na Tathmini kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi – WCF, Dkt. Abdulssalaam Omary kuhusu mwitikio wa waajiri kujisajili katika Mfuko huo ambapo Dkt. Omary alisema bado mwikitio hauridhishi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama akiongea na Mkurugenzi wa Huduma za Matibabu na Tathmini kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi,(WCF), Dkt. Abdulssalaam Omary.Katikati ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA Hadija Mwenda
Mkurugenzi wa Huduma za Matibabu na Tathmini kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi – WCF, Dkt. Abdulssalaam Omary akitoa ufafanuzi kwa wananchi waliotembelea banda la WCF kuhusu mfuko huo ambao ni taasisi ya hifadhi ya jamii iliyoundwa kwa mujibu wa kifungu cha 5 cha sheria ya fidia kwa wafanyakazi (sura 263 marejeo ya mwaka 2015).
Kulia ni Afisa Rasilimali Watu kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi – WCF,Lilian Msaki akitoa elimu kuhusu Mfuko huo kwa wananchi waliotembelea banda la WCF.Alisema lengo la kuanzishwa mfuko huo ni kushughulikia masuala ya fidia kwa wafanyakazi wanaoumia,kuugua au kufariki kutokana na kazi wanazozifanya kwa mujibu wa mikataba ya ajira zao. 
Afisa Uhusiano wa Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi - WCF, Bi.Zaria Mmanga, (kulia), akielezea kuhusu Fao la huduma ya matibabu ambapo alisema pale mwajiriwa anapoumia au kuugua atapatiwa matibabu na huduma mbalimbali ikiwemo kupatiwa viungo bandia, malipo ya dawa, kumuona daktari, huduma za upasuaji, uuguzi na kurudia matibabu pale inapobidi.
Kulia ni Mwananchi akiuliza swali kuhusu Fao la Malipo ya Ulemavu wa muda mfupi na ulemavu wa kudumu kwa Afisa Uhusiano wa Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF), Bi. Zaria Mmanga
Afisa Uhusiano wa Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF), Bi.Zaria Mmanga, (kulia), akielezea kuhusu msaada wa mazishi unaotolewa kwa familia ya mfanyakazi endapo mfanyakazi atafariki kutokana na ajali au ugonjwa uliotokana na kazi pamoja malipo yanayotolewa kwa wategemezi wa marehemu.
Afisa Fedha Mwandamizi kutoka Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw.Vicent Stephen akitoa elimu kwa wananchi juu ya malipo kwa anayehudumia mfanyakazi aliyepata ajali au kuugua kutokana na kazi na ambaye hawezi kujihudumia
Afisa Uhusiano wa Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi - WCF, Bi. Zaria Mmanga akielezea kauli mbiu ya CWF kuwa ni "Fidia Stahiki kwa wakati na maendeleo ya taifa letu" na mawasiliano zaidi namba za kupiga bure WCF ni 0800110028 au 0800110029
Afisa Utawala Afisa Mahusiano wa Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi - WCF,Ally Shekha akionesha picha za wafanyakazi walioumia kazini.(Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog)

NSSF YATOA MIFUKO YA SIMENTI 800 NA NONDO KWA AJILI YA UJENZI WA ZAHANATI KATIKA KIJIJI CHA MATAMA WILAYA SONGEA VIJIJINI

$
0
0
Shirika la hifadhi ya jamii NSSF limetoa msaada wa simenti mifuko 800 na rolu 400 za nondo kwa ajili ya ujenzi wa zahanati katika kijiji cha matama kata ya muhukuru halimashauri ya wilaya ya songea mkoani Ruvuma. Shirika hilo limechukua hatua ya kutoa msaada huo baada ya hadha kubwa waliyokuwa wanaipata wananchi hawa ya kufuata matibabu umbali wa kilometa 62 kama anavyobainisha meneja wa NSSF mkoa wa Ruvuma BI MARIAM MUHAJI

WAZIRI MUHONGO AWATAKA WATAALAM KULISAIDIA TAIFA

$
0
0

Na Veronica Simba – Dodoma

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ametoa wito kwa wataalam nchini, hususan walioko katika sekta za mafuta na gesi kulisaidia Taifa kuepukana na mikataba mibovu kwa kutumia utaalam wao badala ya wao kuendelea kulalamika kama wananchi wa kawaida.

Profesa Muhongo alitoa wito huo jana, Aprili 27, 2017 wakati akizindua Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA) katika hafla iliyofanyika makao makuu ya Wizara mjini Dodoma.

Akizungumza na wajumbe wa Bodi hiyo, Profesa Muhongo alisema kwamba, kumekuwa na kilio cha muda mrefu cha wananchi kuhusu Taifa kuibiwa rasilimali mbalimbali na makampuni ya kigeni kutokana na mikataba mibovu iliyoingiwa awali.

“Ni kwa sababu hiyo, uteuzi wa wajumbe wa Bodi hii ya PURA, umezingatia sifa za hali ya juu za kitaaluma mlizonazo, ili pamoja na mambo mengine muweze kulisaidia Taifa kunufaika ipasavyo na rasilimali hizi adhimu za mafuta na gesi, kwa kuhakikisha mikataba inayoingiwa, inakuwa yenye manufaa kwetu.”

Akifafanua zaidi, alisema kuwa, Bodi ya PURA ina wajumbe watano ambao wamebobea katika taaluma za sheria, fedha, uhasibu na mazingira; sifa ambazo zinaifanya Bodi hiyo kuwa miongoni mwa Bodi bora kabisa hapa nchini.

Aliwataka wataalam hao kuachana na kasumba ya kulalamika kuwa Taifa linaibiwa badala yake watumie utaalam na ubobezi wao kuhakikisha changamoto hiyo inabaki kuwa historia nchini hususan katika sekta wanayoisimamia.

Sambamba na rai hiyo kwa wajumbe wa Bodi ya PURA, aliwataka wataalam wengine mbalimbali nchini, kujitokeza na kulisaidia Taifa katika sekta mbalimbali walizopo.

“Watanzania wajue kuwa, hivi vilio tunavyotoa, haimaanishi kwamba hatuna wataalam hapa nchini, Wataalam wapo. Sasa wataalam wajitokeze, siyo na wao wabaki kulalamika tu kama wananchi wa kawaida wasio na utaalam. Haitatusaidia,” alisisitiza Waziri.

Aidha, akizungumzia majukumu ya Bodi hiyo, Profesa Muhongo alisema kwamba, Bodi inawajibika kuishauri Wizara katika masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na masuala ya lesni, utafutaji wa rasilimali, kuhusu mikataba, mambo ya kodi na tozo mbalimbali na mengine ya aina hiyo.

“Kazi hiyo ilikuwa ikifanywa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) hapo awali. Hivyo, kama kulikuwa na mapungufu, nyie myarekebishe. Tunategemea mtoe majibu ya kitaalam kwa kilio cha watanzania.”

Vilevile, Waziri Muhongo aliitaka Bodi hiyo kuhakikisha inasimamia ushiriki wenye tija wa watanzania katika miradi mbalimbali ya sekta husika. Alieleza kuwa, mmoja wa wajumbe wa Bodi hiyo aliteuliwa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, sehemu inayosimamia uwezeshaji, ili aweze kutekeleza jukumu hilo ipasavyo.

Waziri Muhongo pia aliwataka wajumbe wa Bodi hiyo kufanya kazi kwa uadilifu pasipo kuegemea upande wowote. Aliwataka kuepukana na vishawishi vya rushwa kutoka kwa Kampuni kubwa za Mafuta na Gesi na badala yake watangulize maslahi ya Taifa.

“Msinunuliwe na makampuni husika. Siyo kwamba nawazuia msionane nao, hapana. Suala ni mnaonanaje! Wekeni mipaka. Lazima ujue mipaka yako. Siyo unaenda huko unalishwa vitu unakuja unaipigania kampuni husika kama vile wewe siyo mjumbe wa Bodi. Hilo hatutakubali,” alisisitiza Waziri.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Mwenyekiti wa Bodi Dk. Adelardus Kilangi alimhakikishia Waziri Muhongo kuwa, watatekeleza majukumu yao kwa uaminifu na weledi ili kuleta manufaa kwa Taifa kama ilivyokusudiwa.

“Tumesikia maelelekezo yako, tunatambua uzito na umuhimu wa kazi iliyoko mbele yetu. Tunafahamu Imani ambayo Taifa limetupatia katika kusimamia Sekta ya Petroli-Mkondo wa Juu. Kwa niaba ya wenzangu, nikuahidi kuwa tutafanya kazi kikamilifu.”

Aliongeza kuwa, Bodi inatambua changamoto iliyopo mbele yao na kwamba wako tayari kukabiliana nayo.

Wajumbe wengine wa Bodi ya PURA ni Dk. Josephat Lotto, Bw. Yona Killaghane, Bibi Beng’l Issa na Mhandisi Ramadhan Suleiman.

Uhai wa kipindi cha kutumikia Bodi hiyo kwa wajumbe husika unatofautiana kuanzia miaka mitatu hadi mitano. 

 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, akisisitiza jambo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA) iliyofanyika Aprili 27, 2017 makao makuu ya Wizara mjini Dodoma.
 Kaimu Kamishna wa Nishati na Masuala ya Petroli, Habass Ng’ulilapi (kwa niaba ya Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara, Profesa James Mdoe), akiwasomea majukumu yao, wajumbe wa Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA), katika hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo, iliyofanyika makao makuu ya Wizara mjini Dodoma.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akizungumza, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA) iliyofanyika Aprili 27, 2017 makao makuu ya Wizara mjini Dodoma.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto), akiwakabidhi vitendea kazi baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA), mara baada ya kuizindua rasmi katika hafla iliyofanyika makao makuu ya Wizara mjini Dodoma.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto), akiwakabidhi vitendea kazi baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA), mara baada ya kuizindua rasmi katika hafla iliyofanyika makao makuu ya Wizara mjini Dodoma.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto), akiwakabidhi vitendea kazi baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA), mara baada ya kuizindua rasmi katika hafla iliyofanyika makao makuu ya Wizara mjini Dodoma.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto), akiwakabidhi vitendea kazi baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA), mara baada ya kuizindua rasmi katika hafla iliyofanyika makao makuu ya Wizara mjini Dodoma.
 Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA), wakielezea wasifu wao kitaaluma, mbele ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo, iliyofanyika makao makuu ya Wizara mjini Dodoma.
 Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA), wakielezea wasifu wao kitaaluma, mbele ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo, iliyofanyika makao makuu ya Wizara mjini Dodoma.
 Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA), wakielezea wasifu wao kitaaluma, mbele ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo, iliyofanyika makao makuu ya Wizara mjini Dodoma.
 Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA), wakielezea wasifu wao kitaaluma, mbele ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo, iliyofanyika makao makuu ya Wizara mjini Dodoma.
 Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA), wakielezea wasifu wao kitaaluma, mbele ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo, iliyofanyika makao makuu ya Wizara mjini Dodoma.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA), Charles Sangweni, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo, iliyofanyika makao makuu ya Wizara mjini Dodoma.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA), Charles Sangweni, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo, iliyofanyika makao makuu ya Wizara mjini Dodoma.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Mdhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA), baadhi ya wafanyakazi wa PURA, Kaimu Kamishna wa Nishati na Masuala ya Petroli, Habass Ng’ulilapi (wa pili kutoka kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Felix Ngamlagosi (wa pili kutoka kulia), mara baada ya uzinduzi wa Bodi hiyo uliofanyika mjini Dodoma hivi karibuni.

MAKAMU WA RAIS MAMA SAMIA SULUHU HASSAN KUZINDUA MRADI MKUBWA WA MAJI MKOANI TABORA

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo mafupi leo kutoka kwa mmoja wa wataalamu wa mradi huo, kuhusiana na mradi wa maji unaojengwa katika kijiji cha Mabama wilayani Uyui mkoani Tabora,Makamu wa Rais Mama Samia atazindua mradi huo wa maji utakao wafikia watu zaidi ya elfu 40 katika vijiji 32 mradi huu umedhaminiwa na serikali ya Japan kupitia shirika lake la JICA.Picha kwa hisani ya Ofisi ya Makamu wa Rais.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akileza jambo mara baada ya kupata maelezo mafupi leo kutoka kwa mmoja wa wataalamu wa mradi huo, kuhusiana na mradi wa maji unaojengwa katika kijiji cha Mabama wilayani Uyui mkoani Tabora,Makamu wa Rais Mama Samia atazindua mradi huo wa maji utakao wafikia watu zaidi ya elfu 40 katika vijiji 32 mradi huu umedhaminiwa na serikali ya Japan kupitia shirika lake la JICA.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifuatilia yaliyokuwa yakijili kabla ya uzinduzi wa mradi wa maji utakao wafikia watu zaidi ya elfu 40 katika vijiji 32 mradi huu umedhaminiwa na serikali ya Japan kupitia shirika lake la JICA.Kulia ni Waziri wa Maji na Umwagiliaji,Inj.Gerson Lwenge na kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji Mh.Prof.Kitila Mkumbo pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Tabora,Mh.Aggrey Mwanri.
Baadhi viongozi na wawakilishi wa wananchi na wadau mbalimbali wakiwa katika tukio hilo la uzinduaji mradi wa maji,ambapo Mgeni rasmi ni Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan.
Baadhi ya vijana wakishiriki kuhudhudia tukiao hilo
Baadhi ya Wanachama wa CCM na wananchi wa kwa ujumla wakifurahia kwa tukio hilo adhimu la kuzinduliwa mradi mkubwa wa maji unaozindulia katika kijiji cha Mabama wilayani Uyui mkoani Tabora,Makamu wa Rais Mama Samia atazindua mradi huo wa maji utakao wafikia watu zaidi ya elfu 40 katika vijiji 32 mradi huu umedhaminiwa na serikali ya Japan kupitia shirika lake la JICA.

MIKOPO YA TSH. BIL 1 YATOLEWA JIJINI ARUSHA, WAZEE WAPATIWA VITAMBULISHO

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo(katikati) akiwakabidhi wawakilishi wa Vikundi vya Wanawake na Vijana mfano wa hundi ya Tsh Bil 1 wakati wa Ziara yake Jijini hapa .kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya Mhe. Gabriel Daqaro na Kushoto ni Mkurugenzi wa Jiji Athumani Kihamia.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo (katikati kulia) akimkabidhi Mzee Zahran Mtweike (Mbele kulia) Kitambulisho cha Wazee.
Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Athumani Kihamia(kulia) akiteta Jambo na Naibu Meya wa Jiji Mhe. Viola Likindikoki wakati wa Ziara ya Mkuu wa Mkoa Jijini hapa.
Diwani pekee wa Cccm katika Jiji la Arusha Mhe. Abdulrasul Tojo (mbele) akifuatilia nkikao cha Mkuu wa Mkoa wakati wa siku ya kwanza ya ziara yake Jijini hapa.

Nteghenjwa Hosseah, Arusha

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo amekabidhi hundi ya Tsh Bil 1 kwa vikundi vya wanawake na Vijana ikiwa ni mchango wa asilimi kumi (10%) ya mapato ya Halmashauri Jiji la Arusha.

Akikabidhi hundi hiyo kwa Vikundi 269 ambavyo kati ya hivyo 162 ni Vikundi vya wanawake na 107 ni vijana amewataka kutumia fedha hizo kwa shughuli zilizokusudiwa ili ziweze kuwatoa katika lindi la umasikini.

“Mikopo hii inatolewa ili kuendeleza shughuli za kijasiriamali ambazo ndizo zilizopelekea mkidhi vigezo vya kupata Fedha; Nimatumaini yangu fedha hizi  zitawawezesha kuongeza mitaji yenu na kuwapa ari ya kujituma zaidi huku mkizingatia nidhamu ya pesa ili muweze kuzirejesha kwa wakati na makundi  mengine waweze kupata fedha hizo”Alisema Rc Gambo.

Mikopo hiyo inayotolewa kwa mujibu wa Sheria na miongozo inayoelekeza asilimia kumi ya Mapato ya ndani ya Halmashauri kutolewe kama Mikopo ya riba nafuu kwa vikundi vya wananwake na vijana na kwa jiji la Arusha kiasi kinachotakiwa kutolewa ni Bil 1.2 kwa Mwaka huu wa Fedha hivyo kiasi kilichotolewa ni kwa kipindi cha robo tatu kuanzia Julai 2016 – March 2017.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa Mhe. Gambo amekabidhi vitambulisho 3850 kwa Wazee wa kuanzia miaka 60 ambao ni wakazi wa Jiji la Arusha vitakavyowasaidia kutambulika katika Vituo vvya Afya na kupatiwa huduma za Afya bure.

Kukabidhi kwa Vitambulisho hivyo kunafanya jumla ya Idadi ya vitambulishbo vilivyotolewa na Jiji kwa wazee kufikia 5966 na bado zoezi hili linaendelea kuwabaini wazee wote na kuwatengenezea vitambulisho.

IRAN YAONESHA NIA KUWEKEZA NCHINI

$
0
0
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto), akifafanua jambo kwa Balozi mpya wa Iran hapa nchini, Mousa Farhang (katikati), wakati Balozi huyo alipomtembelea Waziri ofisini kwake mjini Dodoma hivi karibuni. Kulia ni Ofisa kutoka Ubalozini, Maisarah Ally.
Balozi mpya wa Iran nchini Tanzania, Mousa Farhang (kushoto) akimkabidhi zawadi Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo. Balozi Farhang alimtembelea Waziri Muhongo ofisini kwake mjini Dodoma hivi karibuni.
Balozi mpya wa Iran nchini Tanzania, Mousa Farhang (kushoto) akimkabidhi zawadi Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo. Balozi Farhang alimtembelea Waziri Muhongo ofisini kwake mjini Dodoma hivi karibuni.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto), akiagana na Balozi mpya wa Iran nchini Tanzania, Mousa Farhang (kulia). Katikati ni Ofisa kutoka Ubalozini, Maisarah Ally.


BALOZI MPYA WA IRAN AMTEMBELEA WAZIRI MUHONGO
Aomba Iran ishirikiane na Tanzania sekta za nishati, madini

Na Veronica Simba – Dodoma

Balozi mpya wa Iran hapa nchini, Mousa Farhang amemtembelea Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kwa ajili ya kujitambulisha na kuzungumzia uwezekano wa nchi za Tanzania na Iran kushirikiana katika sekta za nishati na madini.

Balozi Farhang alimtembelea Profesa Muhongo jana, Aprili 28, 2017 ofisini kwake mjini Dodoma.

Akizungumzia nia ya nchi yake kushirikiana na Tanzania katika sekta ya nishati, Balozi Farhang alimwambia Waziri Muhongo kuwa Iran inazo sifa stahiki katika sekta hiyo kutokana na maendeleo iliyofikia ambapo alieleza kuwa mbali na kuzalisha umeme wa kutosha kwa mahitaji ya nchi, imejenga viwanda vya umeme katika baadhi ya nchi zinazowazunguka.

Aidha, aliongeza kuwa, nchi hiyo huzalisha zaidi ya mapipa milioni nne ya mafuta kwa siku moja.

“Miaka 10 iliyopita, Iran ilikuwa kama nchi nyingine zilizo nyuma kimaendeleo lakini sasa tunazalisha umeme mwingi unaotosheleza mahitaji ya nchi yetu na mwingine tunauza.

Alisema kuwa, kutokana na utafiti alioufanya yeye binafsi, amegundua kuwa, sekta ya nishati ndiyo yenye nafasi kubwa na nzuri zaidi itakayowezesha nchi za Tanzania na Iran kunufaika endapo zitashirikiana.

Aliongeza kuwa, Serikali ya Iran inavutiwa zaidi kuwekeza Tanzania kutokana na sifa ya uhusiano mzuri baina ya nchi hizo mbili ambapo alifafanua kuwa, Tanzania inashika nafasi ya Tatu kwa nchi za Afrika, katika kuwa na uhusiano mzuri na Iran, ikitanguliwa na Afrika Kusini na Misri.

Kwa upande wa sekta ya madini, Balozi Farhang alimweleza Waziri Muhongo kuwa, nchi ya Iran iko tayari kushirikiana na Tanzania katika namna yoyote inayofaa.

Akijibu maombi ya Balozi Farhang, Waziri Muhongo alimweleza kuwa, Tanzania inakaribisha wawekezaji kutoka nchi ya Iran kwa ajili ya kuwekeza katika sekta za nishati na madini.

Akizungumzia maeneo muafaka ya uwekezaji katika sekta ya nishati hapa nchini, Profesa Muhongo alimweleza Balozi Farhang kuwa, kwa sasa Tanzania inahitaji umeme mwingi hivyo wawekezaji kutoka Iran wanakaribishwa kuja kuwekeza katika uzalishaji wa umeme.

Profesa Muhongo alifafanua zaidi kuwa, wawekezaji husika wanaweza kuzalisha umeme kwa kutumia vyanzo mbalimbali vilivyopo nchini ambavyo ni pamoja na gesi asilia, makaa yam awe, maporomoko ya maji, jua, upepo, jotoardhi, mawimbi ya bahari na tungamotaka.

Kuhusu uwekezaji katika sekta ya mafuta na gesi, Profesa Muhongo alimweleza Balozi Farhang kuwa, nchi ya Iran inao utaalam zaidi kuliko Tanzania hivyo ni vema timu ya wataalam kutoka Tanzania ikakutana na Timu ya wataalam kutoka Iran ili kujadiliana na kukubaliana maeneo muhimu ya ushirikiano.

Waziri Muhongo pia alieleza kuwa, eneo jingine muhimu linalohitaji uwekezaji mkubwa na makini katika sekta ya nishati hapa nchini ni usambazaji na usafirishaji wa umeme.

Aidha, kwa upande wa sekta ya madini, Profesa Muhongo alisema kuwa, wafanyabiashara kutoka Iran wanakaribishwa kuja Tanzania kununua aina mbalimbali za madini yanayozalishwa nchini, yakiwemo madini ya vito.

Profesa Muhongo na Balozi Farhang, walikubaliana kuunda timu za wataalam kutoka nchi zote mbili, ili wakutane kujadiliana na kukubaliana maeneo yanayofaa kwa ushirikiano wa uwekezaji katika sekta za nishati na madini.

MPINA AWATAKA WAKAZI WA MOROGORO KUTUNZA VYANZO VYA MAJI NA MAZINGIRA

$
0
0
Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Raisi muungano na Mazingira Mheshimiwa Luhaga Mpina, amewataka wakazi wa Mkoa wa Morogoro kutunza Vyanzo vya maji na Mazingira kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wameokoa maisha ya binadamu na viumbe hai wengine.
Naibu Waziri Mpina ameyasema hayo leo alipikuwa katika zoezi la usafi kitaifa Mjini Morogoro ambapo amesisitiza kwa kufanya hivyo wakazi wa mkoa huo watakuwa wamesaidia wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam Pamoja na pwani ambao vyanzo vyao vyingi vya maji vimetokea mkoani Morogoro.
Mpina pia aliweka msisitizo katika zoezi zima la upandaji miti ambapo kila wilaya inatakiwa kupanda miti milioni moja na nusu, "kutakuwa na ufuatiliaji wa hali ya katika utekelezaji wa zoezi hiyo katika ngazi ya Wilaya." Alisisitiza Mpina.
Aidha Mpina aliunga Mkono Jitihada za Mkuu wa Mkoa wa Morogoro katika suala zima la utunzani na usafi  wa mazingira , "Mnae Mkuu wa Mkoa anaetosha, anaujua mkoa vizuri na hwa ndiyo viongozi wa mkoa tunaowataka, wachapakazi na wenyekujituma. Alisema Mpina."
Akiongelea suala la kuhamishwa wananchi katika milima na vyanzo vya maji, NW Mpina Alisema kuwa  " Tunapowaondoa wananchi katika maeneo hayo aimaaninishi kwamba tunawatesa. tunawapenda ndo maana tunawahamishia katika maeneo salama na rafiki kwa mazingira, RC watoeni wananchi wanaokaa katika maweneo Hatarishi." Alisema.
Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bwana Kebwe Steven Kebwe, akizungumzia hali ya mazingira ya mkoa huo, alisema kuwa mkoa utajitahidi kupambana na hali ya uharibifu wa mazingira, pamoja na changamoto mkoa unazokumbana nazo akitolea mfano upungu wa vifaa vya kuzolea taka.

Jumamosi ya usafi wa Mazingira Mkoani Morogoro kwa Jumamosi ya Mwishho wa mwezi wa nne ni utegelezaji wa Agizo la Mhe. Rais la Usafi wa Mazingira. 
 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akitoa Mchanga katika moja ya Mtaro Mijini Morogoro wakati wa kufanya usafi, Leo.
Moja ya Mtaro Uliosafishwa katika zoezi la usafi wa mazingira leo Mjini Morogoro

 Kulia Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bwna Kebwe Steven Kebwe akimkabirisha Naibu Waziri Mpina kabla a kuanza kwa zoezi la Usafi kitaifa Mjini Morogoro siku ya Jumamosi ya Mwisho wa mwezi wa nne.
(Habari na Picha na Evelyn Mkokoi wa OMR)
 

NAIBU SPIKA TULIA AKSON AZINDUA MAFUNZO YA SANAA TASUBA

$
0
0

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Akson akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo maalum ya Vikundi vya ngoma za asili kutoka mkoa mbeya yanayofadhiliwa na Tulia Trust.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Akson, akiimba wimbo na Msanii wa muziki wa Bongo fleva , Nandy pamoja na Mtendaji mkuu wa chuo Cha Sanaa Bagamoyo,Herbert Makoye .
Moja ya kazi za Sanaa zilizochorwa katika chuo cha Sanaa Bagamoyo (TASUBA)
Mmoja wa Wanafunzi kitengo cha Sanaa za ufundi na uchoraji wakichora picha ya Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Akson



Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

TAASISI ya Tulia Trust inayomilikiwa na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Tulia Ackson imewafadhili wanafunzi 27 kwa ajili ya kupata mafunzo ya sanaa.

Taasisi hiyo imewadhamini wanafunzi hao kutoka Mbeya kusoma kwenye chuo cha Taasisi ya Sanaa na Utamaduni (TaSUBa), kilichopo Bagamoyo mkoani Pwani.

Wanafunzi hao watapata fursa ya kujifunza sanaa ya maonyesho ya upigaji ngoma za asili, maigizo na utumiaji jukwaa.Akizungumza kwenye uzinduzi wa kuwakabidhi wanafunzi hao chuoni hapo, Dkt. Tulia amesema lengo la kuwafadhili vijana hao ni kutokomeza tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana.

Amesema taasisi yake imedhamilia kukuza sanaa kwa vijana nchini ili kutatua tatizo la ajira na kuongeza ufanisi kwenye vipaji vyao walivyokuwa navyo awali.Alisema vijana hao wakipata mafunzo kwenye chuo hicho wataweza kufanya shughuli zao za ngoma za asili kiutaalamu zaidi, hali itakayowaongezea kipato na kuwafungulia fursa nyingi.

Dkt. Tulia alisema zoezi la kuwafadhili vijana kusoma kwenye chuo hicho litakuwa endelevu ili kukuza vipaji vya vijana kwenye sanaa.Alisema baada ya awamu ya kwanza kumalizika atahakikisha anaongeza idadi ya vijana atakaowadhamini kwa ajili ya kukuza vipaji vya sanaa nchini hususani kwenye mkoa wa Mbeya.

Tulia, alisema atahakikisha kwenye awamu ya pili atachukua wanawake wenye vipaji ili kuendeleza vipaji vyao kutoka maeneo mbalimbali ya nchi.

"Huu hautakuwa mwisho wa kufadhili vijana, nitahakikisha naongeza idadi ya vijana kwenye awamu ya pili. Juhudi hizi zitahakikisha zinasaidia vijana wanaepuka tatizo la ukosefu wa ajira nchini," alisema Tulia.

Aidha, Dkt. Tulia amewataka wadau mbalimbali wa sanaa, Taasisi na Kampuni kuunga mkono juhudi za taasisi yake kwa ajili kukuza sanaa nchini.

Naye, Mtendaji Mkuu wa TaSUBa, Dkt.Herbert Makoye, alisematahakikisha chuo chake kinawapa mafunzo mazuri vijana hao ili kuwaongezea ufanisi kwenye vipaji vyao.

Alisema watahakikisha wanawapa mafunzo mazuri ya uchezaji ngoma za asili, ngoma za ubunifu, muziki wa asili ya Tanzania, uigizaji, matumizi ya jukwaa na maleba.

Dkt Makoye, alisema ana imani vijana hao wakihitimu mafunzo hayo watakuwa tofauti na walivyokuwa hapo awali.

Mafunzo hayo yatadumu kwa kipindi cha miezi miwili watakaofuzu wataendelea na kozi ya cheti na diploma kwa ajili ya kukuza vipaji vyao.
Mtendaji mkuu wa chuo cha Sanaa Bagamoyo(TASUBA) akizungumza kumkaribisha Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Akson
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Akson akiwasili katika chuo cha Sanaa Bagamoyo kwa jili ya ufunguzi wa mafunzo kwa vikundi vya Sanaa mkoa mbeya.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Akson, akicheza ngoma pamoja na Mtendaji mkuu wa Chuo Cha Sanaa Bagamoyo , Dk Herbert Makoye

RAIS DKT MAGUFULI APOKELEWA KWA SHANGWE NA NDEREMO MKOANI KILIMANJARO

$
0
0


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na wananchi wa Karanga Wilaya ya Moshi mjini waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiagana na wananchi wa Karanga Wilaya ya Moshi mjini waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na wananchi wa Karanga Wilaya ya Moshi mjini waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017


  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa maagizo wa kutotoza ushuru wachuuzi kwa Mkurugenzi wa Wilaya ya Hai Bw. Yohana Sintoo wakati akiongea na wananchi wa Kwa Sadala waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017
    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa maagizo wa kutotoza ushuru wachuuzi kwa Mkurugenzi wa Wilaya ya Hai Bw. Yohana Sintoo wakati akiongea na wananchi wa Kwa Sadala waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017

  Mbunge Mstaafu na aliyekuwa Mkuu wa Sekondari ya Weruweru, Dk Maria Kamm akimshangilia Rais Magufuli alipoongea na wananchi wa Karanga
 Mbunge Mstaafu na aliyekuwa Mkuu wa Sekondari ya Weruweru, Dk Maria Kamm akisalimiana na Rais Magufuli aliposimamishwa kuongea na wananchi wa Karanga
 Rais magufuli akiwa na Mbunge Mstaafu na aliyekuwa Mkuu wa Sekondari ya Weruweru, Dk Maria Kamm eneo la Karanga
 Rais magufuli akiwa na Mbunge Mstaafu na aliyekuwa Mkuu wa Sekondari ya Weruweru, Dk Maria Kamm akisalimiana na wanafunzi
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na wananchi wa Karanga Wilaya ya Moshi mjini 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na wananchi wa Karanga Wilaya ya Moshi mjini  
 Wananchi wa Kibololoni wakimshangilia Rais Magufuli
  Wananchi wa Kibololoni wakimshangilia Rais Magufuli
 Rais Dkt. Magufuli akiongea na Wananchi wa Kibololoni.
PICHA NA IKULU
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Kmnda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Hamisi Issa alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Said Meck Sadick alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Said Meck Sadick alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Waziri Mkuu Mhe. Kassim majaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Said Meck Sadick alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongiozana na Waziri Mkuu Mhe. Kassim majaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Said Meck Sadick alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Rais wa TUCTA Bw. Tumaini Nyamhokwa alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Waziri Mkuu Mhe. Kassim majaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Said Meck Sadick alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aiiongiozana na Waziri Mkuu Mhe. Kassim majaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Said Meck Sadick alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na wanahabari alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na wana UVCCM alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na wananchi wa Bomang'ombe Wilaya ya Hai waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na wananchi wa Bomang'ombe Wilaya ya Hai waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisikiliza changamioto za wananchi wa Kwa Sadala Wilaya ya Hai waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017
 Kijana akiwa kabebwa mgongoni akirekodi wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na wananchi wa Karanga Wilaya ya Moshi mjini waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na wananchi wa Karanga Wilaya ya Moshi mjini waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017


UHARIBIFU WA VYANZO VYA MAJI VYAINGIZA HASARA TANGA UWASA YA MILIONI 13 KWA SIKU.

$
0
0

Waandishi wa habari wakitazama namna maji yaliyohifadhiwa kwenye kituo cha kusafishia maji cha Mowe kabla ya kufika kwa walaji wa kwanza ni Sophia Wakati wa Gazeti la Uhuru wa pili ni Mbaruku Yusuph wa gazeti la Tanzania Daima
Mwandishi wa Gazeti la Mtanzania,Sussan Uhinga naye akiangalia namna maji yanavyosafishwa kabla ya kuwafikia walaji
Waandishi wa Habari wakiongozwa na Amina Omari wa Gazeti la Mtanzania wakitembelea eneo la kusafishia maji kabla ya kufika kwa watumiaji la


Eneo la Mowe ambalo maji huchujwa kabla ya kuwafikia walaji
Mwandishi wa gazeti la Mtanzania,Sussan Uhinga na Frank wa TK wakiwa kwenye eneo hilo kujionea
Mratibu wa shughuli za Mazingira wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga Tanga Uwasa,Ramadhani Nyambukah akizungumza jambo kwa waandishi wa habari kuhusu dawa ambazo zinatumika kuwekwa kwenye maji
Mratibu wa shughuli za Mazingira wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga Tanga Uwasa,Ramadhani Nyambukah akiwaonyesha mitambo iliyopo kwenye kituo hicho wakati walipoitembelea kujionea
Waandishi wakitoka kulia ni Mashaka Mhando wa gazeti la Majira Mkoani Tanga kushoto ni William Mngazija wa ITV na Radio One Mkoani Tanga


William Mngazija wa ITV na Radio One Mkoani Tanga akiwa ongoza waandishi wengine kuingia kwenye vyanzo vya maji kuona namna hali ilivyo
Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Citizeni Mkoani Tanga, George Sembony akiwa kwenye vyanzo hivyo vya maji
Muonekano wa Maji kwenye chanzo cha Maji cha Mto Zigi
MAMLAKA ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga

Uwasa)inapoteza kiasi cha shilingi milioni 13 kila siku kutokana na kuongezeka kwa za shughuli za kibinaadamu zinazofanywa katika vyanzo vya maji vilivyopo katika Mto zigi na Muzii Wilayani Muheza. 

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea kwenye vyanzo vya maji,Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga(Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa alikiri kuwepo kwa uharibifu mkubwa katika vyanzo hivyo unaosababishwa na wananchi katika maeneo hayo. 

Mhandisi Mgeyekwa alisema shughuli za uchimbaji wa dhahabu,kilimo na maogesho ya mifugo katika vyanzo hivyo vimekuwa vikichangia kwa kiasi kikubwa kuongeza matope kwenye bwawa la Mabayani linalosambaza maji Mjini hasa kipindi hiki cha mvua za masika. 

Aidha alisema kuwa awali mamalaka hiyo ilikuwa inazalisha maji kiwango cha ujazo km 29,000 na kupungua hadi kufikia ujazo wa km 20,000 kwa sasa jambo lililopelekea kuanza kutoa huduma hiyo kwa mgao ndani ya Jiji la Tanga. 

Alisema wao kama mamlaka baada ya kugundua kuwepo kwa tatizo hilo walianza kufanya jitihada mbalimbali ikiwemo kuvitembelea vyanzo vyote vya maji ili kubaini uhalisi uliopo na namna ya kuanza kulishughulikia jambo hilo kwa haraka zaidi ili lisiweze kuleta madhara kwa wananchi. 

“Ki ukweli tatizo hili la katizo la maji na maji kutoka machafu haliwaathiri wananchi peke yake hata sisi kwenye maeneo yetu tunayokaa limekuwa likijitokeza hivyo tunaangalia namna ya kupambana nalo usiku na mchana kwa lengo la kutatua shida hiyo”Alisema. 

Mkurugenzi huyo alisema tayari mamlaka hiyo imekwisha kuanza kuchukua jitihada za haraka ikiwemo kutumia maji ya kisima cha mwakileo ambacho kina uwezo wa kutoa maji kwa ujazo wa km 30,000 hadi 35,000 ambayo yanaweza kukidhi mahitaji ya zaidi wananchi 47,000 kwa wakati mmoja sambamba na kuzibua mabomba ambayo yamekuwa na tope iliyosababishwa na mvua zinazoendelea sasa. 

Hata hivyo aliwataka wananchi kuacha kufanya shughuli za kibinadamu karibu na vyanzo vya maji kwani kufanya hivyo kunasababisha madhara makubwa kwa watumiaji wake ikiwemo kupungua kina cha maji na maji kutoka machafu jambo ambalo ni hatari kwa afya zao. 

Akizungumza wakati wa ziara ya waandishi wa habari walio tembelea vyanzo vya maji vya Mto Muzii,Zigi,Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watumiaji wa Maji Zigi Juu,Philipo Mdoe alisema hali ya uchafuzi wa maji na kupungua kina kumechangiwa kwa asilimia kubwa na shughuli za kibinadamu zinazofanywa karibu na vyanzo hivyo jambo ambalo jitihada za haraka zisipochukuliwa kunaweza kukaleta athari zaidi kwa wananchi. 

“Tunaiomba mamlaka kwa kushirikiana na serikali kupitia vyombo vya dola vifanye operesheni za kushtukiza mara kwa mara kwani hii itasaidia kupunguza ama kuondokana na uchafuzi wa mazingira unaofanywa na watu kwenye nyanzo hivyo “Alisema. 

Awali akizungumza katika mkutano huo,Mratibu wa Mazingira Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Nyambuka Ramadhani alisema suala la utunzaji wa vyanzo vya maji ni wajibu kwa jamii kuhakikisha wanakuwa mabalozi wazuri wa kuona namna ya kuvilinda ili visiweza kuharibiwa. 

“Lazima jamii itambua umuhimu wa kuvitunza na kuvilinda vyanzo vya maji kwani bila hivyo wanaweza kukumbwa na athari za kukosekana kwa maji au kupatikana kwa maji yasiyokuwa safi na salama hivyo tushirikiana kupambana na waharibifu wa mazingira “Alisema.


Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.


Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusiana na mikakati waliochukua kukabiliana na kuondoa tatizo la maji machafu yanayotoka jijini Tanga ili kuhakikisha maji yanarudi kwenye hali yake ya kawaida lakini kulia ni Meneja wa Ufundi wa Mamlaka hiyo,Farles Aram
Kushoto mwenye tisheti ya njano ni Mwandishi wa Gazeti la Majira Mkoani Tanga,Mashaka Mhando akiuliza swali katikati ni Joachim Kapembe kutoka Shirika la Utangazaji la TBC na kulia ni Mwandishi wa ITV na Radio One Mkoani Tanga,Wiliam Mngazija.
Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Citizeni Mkoani Tanga, George Sembony kulia akiuliza swali kwenye mkutano huo kushoto ni Mwandishi Zawadi Kika wa Clous TV
Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Dorrah Killo kulia ni Mwandishi wa Gazeti la Citizeni George Sembony
Mratibu wa shughuli za Mazingira wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga Tanga Uwasa,Ramadhani Nyambukah akizungumza jambo kwenye mkutano huo
Baadhi ya watumishi wa mamlaka hiyo wakifuatilia mkutano huo na waandishi wa habari leo
Waandishi wa Habari Mkoani Tanga wakichukua habari
Joachim Kapembe kutoka Shirika la Utangazaji la TBCkushoto akiwa sambamba na mtumishi wa mamlaka ya Maji Tanga Uwasa wakiingia kwenye kituo cha kusafishia Maji cha Moye

Balozi Asha Rose Migiro azindua Jumuiya ya Watanzania Waishio Wales, Uingereza

$
0
0
Tarehe 29 APRILI, 2017 Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Dkt. Asha Rose Migiro aliwatembelea Diaspora waishio Nchini Wales. 

Katika mkutano wake na Diaspora hao, Balozi alishiriki uzinduzi rasmi wa Jumuiya ya Watanzania Waishio Wales (WAWE-TZDiaspora). 

Jumuiya hiyo inawajumuisha Diaspora Waishio katika miji ya Bristol, Bath, Somerset, Wiltshire, Newport, Cardiff na Swansea. 

Katika uzinduzi huo, Balozi aliwapongeza Diaspora wa Wales na Uongozi Wao pamoja na kutoa wito wa kushirikiana kwa karibu na Ubalozi wa London kupitia uongozi wako. Alihimiza umuhimu wa Diaspora kuwa wamoja na kushirikiana bila kubaguana. 

Diaspora hao waliagana na Balozi kwa kumuandalia chakula maalum cha kumshukuru kwa kuwatembelea na kwa heshima aliyowapa kuzindua Jumuiya ya WAWE-TZ Diaspora. 
 .Balozi akizindua Jumuiya ya WAWE-TZ Diaspora kwa kupokea Katiba ya Jumuiya hiyo. 
 Balozi akizungumza na wanachama wa WAWE-TZ 

 Balozi na Uongozi wa Jumuiya ya WAWE-TZ 
Balozi akishiriki chakula alichoandaliwa na Jumuiya ya WAWE-TZ

taarifa kuhusu uzinduzi wa bodi ya kima cha chini cha Mshahara katika Sekta ya Umma.

DHANA YA ULIPAJI WA KODI YA PANGO LA ARDHI

$
0
0

Mkuu wa kitengo cha Kodi, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Dennis Masami akitoa mada kuhusu Maana na Umuhimu wa ulipaji Kodi ya pango la Ardhi kwa Waandishi wa Habari katika ukumbi wa Wizara hiyo.



Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetoa tahadhari kwa wadaiwa wa kodi ya pango la Ardhi kwa kutoa elimu ya kuhusu dhana ya Kodi hiyo.

Hivi karibuni Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetoa mafunzo mafupi kwa waandishi wa habari kwa nia ya kuhamasisha ulipaji wa kodi ya pango la Ardhi na kubainisha utofauti wake kati ya kodi hiyo na Kodi ya Majengo ambayo hukusanywa na Mamlaka ya Mapato (TRA).

Akizungumza na waandishi wa habari; Mkuu wa Kitengo cha Kodi; Dennis Masami alisema; Dhana ya ulipaji wa kodi ya pango la Ardhi inatokana na Sheria ya Ardhi namba 4 ya mwaka 1999 katika fungu la 3 kifungu kidogo cha 1 (a) kinachosema: ‘Itambulike kuwa ardhi yote ya Tanzania ni mali ya Umma iliyowekwa chini ya Mheshimiwa Rais kama mdhamini kwa niaba ya wananchi’’

Aliendelea kusema kuwa; Mfumo huu wa umiliki wa ardhi unatambulika kama lease hold na sio free hold, ambapo aina hii ya umiliki ni upangaji katika ardhi, ambao mpangaji anawajibika kufuata masharti ya upangishaji, mojawapo ya masharti hayo ni kulipa pango la kipande cha ardhi. Ambayo Mmiliki ni Rais kwa niaba ya umma na mpangaji ni Mwananchi.

Naye Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mhe. William Lukuvi ametoa tahadhari kwa wasiolipa Kodi ya Pango la Ardhi akisema; “Wale wote ambao hawajalipa Kodi ya Pango la Ardhi, wote wanao miliki viwanja na mashamba yaliyopimwa, wahusike kulipa kabla ya mwisho wa mwezi wa sita (6). Ifikapo tarehe 30/06 hatua zifuatazo zitachukuliwa dhidi yao; Watashitakiwa Mahakamani, Mali zao zikamatwe na majengo yapigwe mnada kupitia madalali na Miliki zao zifutwe.

Alisema hatua hizo zote zitachukuliwa kwa mujibu wa sheria, na kutoa tahadhari kuwa kila mmoja achukue hatua ya kulipa kwa hiari kwa Maendeleo ya Taifa.

Na kitengo cha Mawasiliano Serikalini – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live




Latest Images