Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRIL 15,2017


MKUTANO BAINA YA SERIKALI NA SEKTA BINAFSI UMEKUWA WA MAFANIKIO

$
0
0

Waziri Charles Mwijage akizungumza na wadau wa Sekta Binafsi katika Mkutano maalum kati ya Sekta hiyo na Serikali.Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilikutana na wadau wa Sekta Binafsi mapema wiki hii katika mkutano maalum ulioandaliwa na Chemba ya Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo nchini (TCCIA) kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF).
Kutoka kushoto ni Godfrey Simbeye, Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF, Gotfrid Muganda Mkurugenzi Mtendaji TCCIA, Octavian Mshiu, Makamu wa Rais TCCIA ambao ni waandaaji wa Mkutano huo maalum baina ya Serikali na Sekta Binafsi wakiwa na Hussein Kamote, Mkurugenzi wa Huduma na Uanachama-CTI.Lengo la mkutano huo maalum baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi ulikuwa na lengo la kuboresha mazingira ya biashara nchini, kukuza ushirikiano kati ya Serikali na Sekta Binafsi pamoja na kuongeza njia za kukuza uchumi utakaochochea ya azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Tanzania kuwa nchi ya Viwanda.
Mkutano huo uliofanyika mjini Dodoma katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango (Treasury Square) uliongozwa na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji (MB) Mh. Charles Mwijage pamoja na Waziri wa Fedha na Mipango (MB), Mh. Dkt. Philip Mpango na kuhudhuriwa na wabunge, makatibu wakuu na manaibu katibu wakuu, Kamishna wa TRA, Mwenyekiti wa TPSF Makamu wa Rais- viwanda wa TCCIA, Mwenyekiti wa TRADEMARK EAST AFRICA, Wafanyabiashara wa Sekta mbalimbali nchini na wawekezaji, viongozi wa ACT, ATE, MOAT, TASOA pamoja na wajumbe wedau wengine wa biashara.
Makamu wa Rais Sekta ya Viwanda TCCIA Octavian Mshiu akizungumza jambo na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage (MB) katika Mkutano huo. 
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage (MB) kushoto, akifurahia jambo na Mwenyekiti wa TPSF Bw. Reginald Mengi kulia, anayeshuhudia ni Waziri wa Fedha na Mipango Mh. Philip Mpango (MB). 
Mkutano huo uliipa Serikali fursa ya kusikiliza changamoto zinazoikabili Sekta Binafsi na kukusanya maoni ya wadau wa sekta hiyo na kuahidi kuzifanyia kazi na kuzitatua ili kuweza kuimarisha mahusiano, umoja, mshikamano, ushiriakiano na uaminifu baina ya sekta hizi muhimu katika uchumi wa taifa la Tanzania.
Akizungumza katika Mkutano huo, Waziri Mwijage aliwashukuru wadau wa Sekta Binafsi kwa kujitokeza kwa wingi ili kuzungumza na Serikali na kuwa njia hii ya kukutana kwa vile imeonekana kuwa njema basi itaendelea kutumika ili kuhakikisha sekta hizi zinakutana mara kwa mara. Waziri aliahidi kushughulikia kero zinazokabili mazingira ya biashara kama kuwepo kwa kodi na kuahidi upunguzwaji wa kodi utitiri ambazo zimekuwa kero kwa wafanyabiashara na pia kuweka mazingira rafiki baina ya Sekta Binafsi na Serikali. 
Kwa upande wake Waziri Mpango alisema, “Tulipofikiria wazo hili hatukutegemea muitikio huu na kwamba ni utaratibu muafaka na napendekeza kwa kuanzia tuendeleze huu utaratibu na tukutane angalau mara moja katika kila robo ya mwaka, asanteni sana. Mmeipongeza serikali na hata mmetuelezea changamoto ambazo ni za msingi sana, mmeifanya siku hii kuwa na thamani kubwa katika kujenga Tanzania mpya”. 
Waziri Philip Mpango akizungumza na wadau wa Sekta Binafsi katika Mkutano maalum kati ya Sekta hiyo na Serikali.
Maofisa waandamizi wa Serikali na wadau wa Sekta Binafsi wakifatilia mazungumzo katika Mkutano maalum baina ya Serikali na Sekta Binafsi uliofanyika mjini Dodoma wiki hii.

WAZIRI MKUU WA ZAMANI WA TAIFA LA ISRAEL ATEMBELEA SERENGETI NA NGORONGORO

$
0
0
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisalimiana na Waziri Mkuu wa zamani wa taifa la Israel,Ehud Barak walipokutana katika eneo la Olduvai Gorge katika Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro akiwa njiani kuelekea katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (katikati) ni Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa(TANAPA) Pascal Shelutete.
Waziri Mkuu wa zamani wa Taifa la Israel,Ehud Barak (kushoto) akimueleza jambo Naibu Waziri wa Malisili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani baada ya kukutana katika eneo la Makumbusho ya kale la Olduvai Gorge ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro akiwa njiani kuelekea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (kushoto) ni Meneja Mawasiliano wa TANAPA,Pascal Shelutete.
Mhandisi Ramo Makani akimueleza jambo Waziri Mkuu wa zamani wa Taifa la Israel ,Ehud Barak baada ya kukutana katika Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro akiwa njiani kuelekea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Naibu Waziri wa Malisili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani (katikati) akimongoza Waziri Mkuu wa zamani wa Taifa la Israel ,Ehud Barak (kushoto) kutembelea eneo la Olduvai Gorge .kulia ni Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete.
Waziri Mkuu wa zamani wa taifa la Israel ,Ehud Barak akitia saini katika kitabu cha wageni huku Naibu Waziri wa Malisili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akishuhudia mara baada ya kufika eneo la Olduvai Gorge akiwa njiani kuelekea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kushudia tendo la wanyama aina ya Nyumbu wahamao kwa makundi.
Mhandisi Ramo Makani akimueleza jambo Ehud Barak.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akieleza mambo ambayo amepata kuongea na Waziri Mkuu wa Israel baada ya kukutana nae katika ene la Olduvai Gorge.
Naibu Waziri wa Malisili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akiwa katika picha ya pamoja na Watalii wa ndani baada ya kukutana nao katika eneo la Olduvai Gorge.



Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

RTO RUVUMA " WATAKAO PANDISHA NAULI KUELEKEA SIKUKUU KUKIONA

$
0
0
mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Ruvuma ABEL SWAI atoa Mambo mawili ya kuzingatia kuelekea sikukuu ya pasaka kwa madereva wa vyombo vya moto na wazazi kwa watoto wao.

MAAFISA UGAVI KUWENI NA MASHAMBA YA MFANO ILI WAKULIMA WAIGE

$
0
0
Mkurugezi wa halimashauri ya wilaya namtumbo mkoani Ruvuma MARCO KILUNGU amewaagiza maafisa ugavi wa vijiji hadi wilaya, kuwa na mfano wa shamba darasa ili kuongeza amasa kwa wananchi badala ya kupiga morojo mtaani.

MAENDELEO KWANZA SIASA BAADAE-JPM

BALOZI WA UINGEREZA NCHINI AMTEMBELEA WAZIRI MHAGAMA BUNGENI DODOMA

$
0
0
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Sarah Cooke amesema nchi yake ipo tayari kuisaidia Tanzania katika kutoa mafunzo maalum ya Menejimenti ya Maafa kwa wataalamu wetu.

Ameyasema hayo hivi karibuni wakati alipomtembelea Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Jenista Mhagama ofisini kwake mjini Dodoma.

Akielezea lengo la ziara hiyo, Balozi Cooke alisema Serikali yake inataka kuiunga mkono Serikali ya Tanzania katika kuhakikisha inajipanga kukabili na kurejesha hali pindi  yanapotokea maafa.
 “Masuala ya maafa yapo nchi nyingi ikiwemo kwetu Uingereza ingawa mafuriko na ajali za moto zimekuwa zikiikumbaa nchi yetu mara kadhaa.”Alisema Balozi.

Aliongeza kuwa,  Serikali ya Uingereza  imevutiwa na juhudi zinazofanywa na Serikali ya Tanzania katika kukabili na kurejesha hali ikiwa pamoja na  kuwasaidia wananchi na mali zao pindi yanapotokea maafa.
Kwa upande wake, Waziri Mhagama alimpongeza Balozi huyo kuona umuhimu wa kuja Tanzania na kuonesha nia ya kuisaidia nchi kwa namna mbalimbali.

“Nishukuru kipekee kwa ujio wako na kuona umuhimu wa kuunga mkono jitihada za Serikali ya Tanzania katika maswala mazima ya maafa na kumhakikishia kuwa Tanzania ipo tayari na itajiandaa kuwaunga mkono kwa utayari wa kuisaidia nchi”Alisema waziri Mhagama.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na Balozi wa Uingereza Nchini Mhe.Sarah Cooke alipomtembelea waziri Ofisini kwake Bungeni Dodoma 
 Balozi wa Uingereza Nchini Mhe.Sarah Cooke akiongea jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama alipomtembelea Ofisini kwake Bungeni Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiteta jambo na Balozi wa Uingereza Nchini Mhe.Sarah Cooke alimtembelea Ofisini kwake Bungeni Dodoma.

MKURUGENZI MTENDAJI WA TAASISI YA TIBA YA MIFUPA ( MUHIMBILI ORTHOPAEDIC INSTITUTE-MO) AZUNGUMZA NA WAFANYAKAZI WAKE

$
0
0
   Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili MOI.

Na Khamisi Mussa
Mkurugenzi Mtendaji  wa Taasisi ya MOI Dkt, Respicious Boniface  amefanya mikutano na Watumishi wa MOI Dar es Salaam jana kwa makundi kwa lengo la kujitambulisha na kusikiliza changamoto mbalimbali zinazowakabili ili kuzitafutia ufumbuzi

Dkt, Boniface amekutana na Watumishi wa idara ya utumishi ,Uuguzi na ufundi. ambapo amewapongeza kwa kufanya kazi katika mazingira magumu na alikutana na watumishi wa idara ya Tiba  Kwa upande wao Watumishi wamempongeza Dkt, Boniface kwa kuaminiwa na kupewa dhamana ya kuiongoza Taasisi ya MOI

Aidha, Dkt Boniface amewaomba Watumishi wa MOI kumpa ushirikiano kwa kutimiza wajibu na kufanya kazi kwa bidii ambapo aliwaeleza kwamba changamoto zilizotolewa atazifanyia kazi na kuzishughulikia

“Nafahamu changamoto ni nyingi sana, nawaahidi kuzishughulikia kama si zote basi kwa asilimia kubwa , lengo ni kuhakikisha Taasisi yetu ya MOI inasonga mbele na inaendelea kutoa huduma bora’’

Awali Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii  ,Jinsia ,wazee na watoto Mh Ummy Mwalimu (MB) alimteua Dkt Lespicious L. Boniface kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) , uteuzi huo ulianza tarehe 5/04/2017

 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa, Mishipa ya Fahamu na Upasuaji wa Ubongo Muhimbili MOI, Dokt. Respicious Boniface (kushoto) akiandika jambo wakati wa Mkutano na Wafanyakazi wa Taasisi hiyo kwa lengo la kujitambulisha, kuanzia kulia ni Mkurugenzi wa Uuguzi wa Taasisi hiyo, Flora Kimaro na Meneja Uhusiano na Ustawi wa Jamii wa Taasisi hiyo, Jumaa Almasi
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa, Mishipa ya Fahamu na Upasuaji wa Ubongo Muhimbili MOI, Dokt. Respicious Boniface akizungumza jambo katika Mkutano na wafanyakazi wa Taasisi hiyo Dar es Salaam jana
Baadhi ya wafanyakazi wakimsikiliza kwa umakini



 Mfanyakazi wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu MOI, Tula Gadi akizungumza jambo wakati wa Mkutano wa  Mkurugenzi Mtemdaji wa Taasisi hiyo alipokuwa akizungumza nao kwa lengo la kujitambulisha kwao
Mmoja wa wafanyakazi , Fidelis Minja akizungumza jamo wakati wa Mkutano wa Mkurugenzi Mtendaji na wafanyakazi wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa MOI
Wafanyakazi wa Taasisi ya Tiba wakiwa katika Mkutano huo

Mmoja wa wafanyakazi Bahati Mrema akizungumza katika Mkutano huo Dar es Salaam jana. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA) Mmiliki wa ujijirahaa blog

EFM YAKABIDHI PIKIPIKI MBILI SHIKA NDINGA TABATA

$
0
0
 Mshindi wa Pikipiki ya Sanmoto katika shindano la Shika Ndinga lililoandaliwa na Efm Radio kwa Wilaya ya Ilala, Jane Honga akinyosha mkono juu kuonyesha furaha yake mara baada ya kutangazwa kuwa mshindi katika shindano hilo katika uwanja wa Tabata Shule.
  Mshindi wa Pikipiki ya Sanmoto katika shindano la Shika Ndinga lililoandaliwa na Efm Radio kwa Wilaya ya Ilala, Jane Honga akitokwa na Machozi
 Mshindi wa Shindano la Shika ndinga ambaye ameweza kujinyakulia pikipiki ya Sanmoto , Amani Juma akishangilia kwa furaha mara baada ya kutangazwa mshindi wa shindano hilo katika Wilaya ya Ilala lililofanyika katika uwanaj wa Tabata shule.
 Mkuu wa Vipindi wa Redio ya Efm 93.7, Dikson Ponela 'Dizo' akikabidhi mkataba wa pikipiki kwa mshindi wa shindano la shika ndinga Wilaya ya Ilala, Jane Honga
 Mtangazaji wa kipindi cha ubaoni Mujuni Silvery 'Mpoki' akiwa na Mtangazaji mwenzie bikira wa Kisukuma katika shoo ya Shika ndinga Tabata Shule
 Wahindi wa shindano la Shika Ndinga  wakiwa wamekalia pikipiki za Sanmoto mara baada ya kukabidhiwa
 Wanawake wakiwa katika hatua ya shindano la kujaza maji hili kwenda hatu ya pili

 Afisa Uhusiano wa Benki ya watu wa Zanzibar (PBZ),Aisha Mohamed  akizungumza na Swebe juu ya huduma za benki hiyo
 Maofisa habari wa Efm na waratibu wa shindano la Shika Ndinga , Jesca na Anet wakipanga jambo katika shinadano katika uwanja wa Tabata shule
 Afisa Masoko wa Kampuni ya Property International ,Leila Mahingu akizungumza na wakazi wa Tabata juu ya huduma zinazotolewa na kampuni yake
 Mmoja wa washiriki akibebwa na walinzi mara baada ya kushindw akuendelea na shindano la shika ndinga katika Viwanja vya Taba Shule
 Mzee wa Kizingiti kutoka E.TV  Akitoa burudani kwa wakazi wa Tabata Shule
Washiriki wakiwa wameshika gari wakati shindano likiendelea

MIILI YA ASKARI NANE WALIOUAWA NA MAJAMBAZI MKOANI PWANI YAAGWA RASMI,WAZIRI MWIGULU ATANGAZA KIAMA KWA WATUHUMIWA

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchini, Mwigulu Nchemba, akitoa heshima za mwisho Dar es Salaam leo mbele ya majeneza yenye miili ya askari nane waliouawa na majambazi Kibiti wilayani Mkuranga mkoani Pwani juzi jioni.Kulia kwake ni Naibu Waziri wa wizara hiyo, Masauni.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchini, Mwigulu Nchemba, akitoa pole kwa wafiwa.
Ndugu,jamaa na marafiki wa wafiwa wakiwa katika shughuli hiyo ya kuaga miili ya wapendwa wao.
Maofisa wa Uhamiaji wakiwa kwenye shughuli hiyo.
Wananchi wakiwa katika shughuli hiyo ya uagaji wa miili hiyo.
Maofisa wa Polisi wakishiriki kuaga miili ya wenzao hao.
Foleni ya kuaga miili hiyo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchini, Mwigulu Nchemba (kulia), akiteta jambo na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Ernest Mangu wakati wa kuaga miili hiyo.
Mmoja wa ndugu za askari hao akilia kwa uchungu.






Ni kilio kwa kuwapoteza wapendwa wao.
Ni huzuni.


Na Dotto Mwaibale 

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amewatangazia kiama watu wote waliohusika kuwaua askari polisi nane Kibiti wilayani Mkuranga mkoani 
Pwani.

Akizungumza wakati wa kuaga miili ya askari hao jijini Dar es Salaam leo asubuhi Mwigulu alisema watu hao watakamatwa  wote na kufikishwa kwenye mkono wa sheria.

"Kitendo hiki cha mauaji kilichofanyika dhidi ya askari wetu hakivumiliki hata kidogo waliohusika tutawatafuta na kuwakamata" alisema Mwigulu.

Aliwaomba wananchi wa maeneo husika kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kuwapata wahusika wa tukio hilo.

Katika hatua nyingine Mwigulu ameitaka wizara husika kuhakikisha inatoa fidia kwa ndugu wa askari hao na majeruhi badala ya kuchukua muda mrefu kuitoa.

"Naomba fidia kwa askari hawa tuliowapoteza wakitumikia taifa itolewa haraka bila kucheleweshwa" aliongeza Mwigulu.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Ernest Mangu alisema watuhumiwa wote waliohusika kufanya mauaji hayo ni lazima watafikiwa na mkono wa dola.

Alisema wananchi wa eneo hilo wanawafahamu wahusika hivyo amewaomba washirikiane na polisi ili kuwapata vinginevyo nguvu itatumika.

Alisema linapotokea tukio kama hilo kuna baadhi ya watu wamekuwa wakishabikia kupitia mitandao ya kijamii hivyo akatoa onyo kuwa watakao bainika na wao watakamatwa kwa kutenda kosa.

Askari waliopoteza maisha katika tukio hilo la kinyama wametajwa kuwa ni pamoja na Mkaguzi Msaidizi Peter Kiguu, Koplo Francis, PC Haruna, PC Jackson, PC Zakaria, PC Siwale, PC Maswi na PC Ayoub

DUKA LA KISASA LA GSM MALL LAUNGUA MOTO DAR

$
0
0
 Magari ya Zimamoto na Uokoaji yakiwa nje ya Duka kubwa la GSM Mall tayari kuzima moto uliokuwa unaunguza duka hilo katika Barabara ya Nyerere eneo la Mtava, Dar es Salaam. Chanzo cha moto huo hakikuweza kujulikana mara moja. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Mmoja wa majeruhi wa ajali hiyo akiwahishwa hospitali.
 Pilikapilika katika lango kuu la kuingilia duka hilo

 Mmoja wa majeruhi akitolewa kwenda kwenye gari ili awahishwe hospitali kwa matibabu
Wananchi wakishuhudia ajali hiyo ya moto


Na Richard Mwaikenda 

DUKA kubwa la GSM Mall ililopo Barabara ya Nyerere eneo la Mtava, Dar es Salaam, linateketea kwa moto hivi sasa.

Kwa mujibu wa mashuhuda ni kwamba duka hilo lilianza kuungua majira ya 8;30,Hadi sasa chanzo cha moto huo hakijaweza julikana. 

Magari ya zimamoto na uokoaji yamejazana eneo hilo kunusuru mali na maisha ya watu waliokuwemo kwenye jengo hilo lenye ghorofa nne.

Watu wengi wakiwemo wafanyakazi wa duka hilo walionekana kutoka mkuku kuokoa maisha yao. Baadhi yao walitolewa wakiwa mahututi na kukimbizwa hospitali kwa kutumia magari ya polisi.

Duka hilo kubwa la kisasa lenye maduka yenye aina mbalimbali za bidhaa ni moja kati ya maduka makubwa yaliyopo jijini Dar es Salaam.

Waokoaji waliokuwepo wamepata wakati mgumu kuzima moto kutokana na ndani ya jengo hilo kuwa na giza nene lililotawaliwa na wingu la moshi uliosababishwa na moto huo.

Wamejitahidi kupata mwanga kwa kuwasha taa za magari karibu na lango kuu la kuingilia ndani lakini ilishindikana.

Mwisho

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi Elimu ya Juu (HESLB) yanufaika na matumizi ya Tehama katika Utoaji wa huduma

VIJANA WA CHUO CHA KODI NI HAZINA KWA FAIDA- TRA

$
0
0

Na Chalila Kibuda , Globu ya Jamii 

VIJANA wanaoandaliwa na chuo cha kodi nchini wanatakiwa kuangaliwa kwa jicho pana zaidi kwani hao  ni hazina kwa taifa katika masuala ya kodi na ushuru wa Forodha. 

Hayo ameyasema leo , Meneja wa Mafunzo na Maendeleo ya Watumishi wa TRA, Yassini Mwita wakati siku ya wanafunzi wa Chuo cha Kodi kilichopo Mwenge jijini Dar es Salaam, amesema kuwa wanafunzi wameonyesha umahiri katika masuala ya kodi ambapo ni hazina ya taifa watapotoka katika chuo hicho.

Amesema wanafunzi wamewasilisha maada mbalimbali juu ya ukusanyaji wa kodi na forodha kwa kile ambacho walifundishwa darasani na kufanyia kazi kwa mazingira na sheria watakayokutana nayo pindi wanapohitimu katika chuo hicho .

Mwita amesema wanafunzi hao wakitoka wanaweza kusaidia makampuni juu ya ukokotoaji wa kodi kuliko kampuni ikawa inafanya yenyewe bila kuwa na mtaalamu wa masuala ya kodi.

Rais wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo cha Kodi, Nadhiru Juma amesema siku ya wanafunzi wa chuo hicho ni muhimu kutokana na wanafunzi kuonyesha uwezo wa darasani na jinsi watavyofanyia kazi kile ambacho wanakisomea.

Amesema kuwa wanafunzi wameonekana kuiva kwa kile kinachofundishwa katika chuo hicho na kuweza kufanyia kazi kwa weledi taifa lao katika masuala ya kodi na ushuru wa forodha.
Meneja wa Mafunzo na Maendeleo ya Watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, Yassini Mwita akizungumza na waandishi habari juu siku ya wanafunzi wa chuo cha kodi wakizungumzia namna ya kuwaandaa wanafunzi hao kuja kuhakikushha wanazisaidia makampuni katika Ukokotoaji wa Kodi leo jijini Dar es Salaam.
Jaji Mkuu wa Kutoa Alama kwa Wanafunzi wa Chuo Kodi Tanzania , Pili Marwa akizungumza katika siku ya wanafunzi wa Chuo cha Kodi na kuwataka kujiandaa kuja kuisaidia serikali katika ukusanyaji wa kodi na ushuru wa Forodha leo jijini Dar es  Salaam.
Mwanafunzi wa Chuo cha Kodi , Charloite Adamu akionyesha umahiri wakati wa kuwasilisha mada katika siku ya wanafunzi wa chuo hicho uliondeshwa na Mamlaka na Mapato Tanzania (TRA) leo  jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wanafunzi wa Chuo cha Kodi wakifatilia maada katika siku ya kodi ya chuo hicho leo jijini Dar es Salaam.
Afisa Uhusiano wa TRA, Oliver Njunwa akizungumza wakati ushereheshaji wa Siku ya Wanafunzi wa Chuo cha Kodi leo jijini Dar es  Saalaam

MREMA AMUOMBA RAIS MAGUFULI KUIANGALIA UOYA BODI YA PAROLE

$
0
0
 Mwenyekiti wa Bodi ya Parole  Augustino Mrema


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii


Mwanasiasa mkongwe na Mwenyekiti wa Bodi ya Parole  Augustino Mrema amesema kuna changamoto nyingi sana katika kuendesha bodi hiyo na kumuomba Rais Dr John Pombe Magufuli  kumwezesha ili atimize majukumu yake.


Akizungumza  kupitia kipindi maalum cha Radio UFM (ya Azm Tv),Mrema amesema kuwa anaiomba serikali kuiangalia upya bodi hiyo kuhusu hali ya wafungwa nchini na mchakato wa kuwatoa wafungwa walio katika hatua za kisheria za Parole.

Mrema amesema , anaukumbusha umma kuwa kila mtu ni mfungwa mtarajiwa na serikali haiwezi kufanya mambo yote hivyo watanzania wakiwa na utamaduni wa kuyasaidia magereza yetu itasaidia  kupata angalau virago kwa ajili ya wafungwa. Aliongeza kuwa utaratibu wa Parole ni mchakato unaohitaji gharama hivyo bodi yake inajitahidi kupata fedha ili kufanikisha  majukumu yao.

 Akizungumzia hali ya kisiasa nchini, Mrema amesema kuwa viongozi waliopo madarakani na wale waliomaliza muda wao kufanya kazi pamoja na Rais ikiwemo na kumpa ushauri utakaojenga nchini na sio kumbeza kama watu wanavyofanya.

Watanzania waache kukosoa kazi za Rais na kuacha kuandika mabaya yake kwani siku hizi mtu akiongelea kitu kibaya ndite anaonekana anafaaa lakini kitu hicho kinajenga taswira mbaya na zaidi hata katika Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere aliongea mambo mazito  lakini hakuna chombo cha habari kilichoandika.

Mrema  amesema, katika wazalendo wa nchi hii yeye ni mmoja wao kwani anafanya kazi hiyo pasipo kujali mshahara ama posho yoyote pia alitumia nafasi hiyo kumuomba radhi Rais mstaafu wa awamu  ya tatu Mhe Benjamini William Mkapa kwa makosa aliyowahi kumfanyia katika kipindi chake kwa kumsingizia kuwa aliiba Tshs Milioni 900,  akasema ule ulikuwa ni mpango wa makusudi ingawa walipoenda mahakamani alishinda.

PASAKA HII HARMORAPA KUWEKA HISTORIA! KUSHUKA NA HELIKOPTA DAR LIVE!

$
0
0

Pasaka hii Harmorapa kuweka historia! Kushuka na Helikopta Dar Live! Mashabiki wake wa mwanzo kuingia BURE! Wengine kiingilio shs 5000 tu!


RAIS DKT MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI MAGOMENI KOTA JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na muwakilishi wa wananchi wakifunua pazia kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi kuanza rasmi ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi kuashiria kuanza rasmi ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe na viongozi wengine na muwakilishi wa wananchi kuashiria kuanza rasmi ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine na muwakilishi wa wananchi wakishangilia baada ya kukata utepe kuashiria kuanza rasmi ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine akikagua eneo la ujenzi wa nyumba za makazi baada ya kuweka jiwe la msingi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na akipata maelezo kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo (TBA) Arch. Elius Mwakalinga wakati akikagua eneo la ujenzi wa nyumba za makazi baada ya kuweka jiwe la msingi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo. Wengine ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliani, Profesa Makame Mbarawa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipongezwa kwa furaha na wasanii mbalimbali wa filamu na wananchi wakati akikagua eneo la ujenzi wa nyumba za makazi baada ya kuweka jiwe la msingi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga tumba wakati bendi ya Msondo Ngoma ikitumbuiza wananchi wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi kuashiria kuanza rasmi ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimia wananchi wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi kuashiria kuanza rasmi ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo. PICHA NA IKULU

JPM ATOA ZAWADI ZA PASAKA VITUO VYA WATOTO YATIMA NA MAKAO YA WAZEE

$
0
0

Kamishna wa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Bw. Rabikira Mushi akikabidhi zawadi za Pasaka kwa niaba ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa sista Stella Selugenge wa Kituo cha Kulelea watoto cha Msimbazi Center leo Jijini Dar es Salaam.
Kamishna wa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Bw. Rabikira Mushi akikabidhi zawadi za Pasaka kwa niaba ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa Afisa Ustawi wa Jamii wa Mahabusu ya Taifa ya watoto Upanga Bi Isabella Shitindi leo Jijini Dar es Salaam.
. Kamishna wa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Bw. Rabikira Mushi akikabidhi zawadi za Pasaka kwa niaba ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa Bibi Sherry Mavura Mlezi wa kituo cha kulelea watoto cha SOS Children village Cha Ubungo Jijini Dar es Salaam.
. Kamishna wa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Bw. Rabikira Mushi akikabidhi zawadi za Pasaka kwa niaba ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa Bibi Veronika Msanjila wa Makazi ya Wazee wasiojiweza Nunge leo Jijini Dar es Salaam.

(Picha zote na Frank Mvungi-Maelezo).
 
 


Anthony Ishengoma


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametoa zawadi zenye thamani ya Shilingi milioni 11,782,000/= kwa jumla ya vituo 9 katika Mkoa wa Dar es Salaam, 2 Zanzibar na 21 kutoka kwenye mikoa ya Tanzania Bara kwa ajili sikukuu ya Pasaka .

Akikabidhi zawadi hizo kwa niaba ya Mhe. Rais,Kamishna wa Ustawi wa jamii Bw. Rabikira Mushi amesema utoaji wa zawadi hizi umekuwa ni utaratibu wa kawaida kwa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kutoa zawadi za vyakula kama vile mchele, mbuzi na mafuta ya kupikia ili kuwawezesha makundi yenye mahitaji maalum kufurahi na kusherehekea sikukuu kama ilivyo kwa watu wengine.


Akifafanua Mushi amesema Mikoa ingine iliyofaidika na zawadi hizo ni Kilimanjaro, Mbeya, Arusha, Tanga, Shinyanga, Morogoro, Kigoma, Ruvuma, Mara, Kagera, Manyara, Tabora, Lindi Mtwara, Singida, Mwanza, na Pwani.

Aidha vitu vilivyofaidika na zawaidi hizo kwa mkoa wa Dar es Salaam na Zanzibar ni,Makao ya Taifa ya Watoto Yatima Kurasini,Makao ya Watoto Mburahati,Makao ya Watoto Msimbazi.Makao ya Watoto Kijiji cha Furaha,Makao ya Watoto SOS Children’s Village Tanzania.

Viuo vingine ni Makao ya Watoto Yatima Group Trust Fund, Temeke.Makao ya Watoto Dar Al Arqum (International Islamic Relief Organization),Mahabusu ya Watoto Dar es Salaam, Upanga,Makazi ya Wazee Wasiojiweza na wenye Ulemavu Nunge Kigamboni.

Kwa upande wa Zanzibar Bw. Mushi alitaja Vituo vilivyonufaika na zawadi hizo,Kituo cha Watoto Istima - Chakechake, PembaMakazi ya Wazee Wasiojiweza Sebleni – Unguja.

Aidha kwa Mikoa ya Tanzania Bara jumla ya vituo 21 vimefaidika na zawadi ya Mhe. Rais na baadhi yake ni Mahabusu ya Watoto Moshi,Makazi ya Wazee Wasiojiweza Njoro – Kilimanjaro,Mahabusu ya Watoto Mbeya,Mahabusu ya Watoto Arusha,Mahabusu ya Watoto Tanga,Makao ya Wazee Wasiojiweza Mwanzage Tanga,Makazi ya Wazee Wasiojiweza Misufini Tanga.

Utoaji wa zawadi umekuwa ni utaratibu wa kawaida wa Waheshimiwa Marais tangu awamu ya kwanza makundi haya maalum yamekuwa yakipatiwa zawadi za vyakula kama vile mchele, mbuzi na mafuta ya kupikia ili kuwawezesha kufurahi na kusherehekea sikukuu kama ilivyo kwa watu wengine.

RAIS DKT MAGUFULI AZINDUA MAJENGO YA HOSTELI ZA WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaidiana na viongozi wengine akizindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Elius Mwakalinga. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipata maelezo toka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Elius Mwakalinga wakati akizindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipongezwa na Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba baada ya kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Kulia ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandala Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua baadhi ya mabweni baada ya kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandala (kushoto) na Mkuu wa Idara ya Sanaa za Ubunifu wa Chuo hicho Dkt. Kedmon Mapana baada ya kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandala wakati akiwasili kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Kiushoto ni Mama Janeth Magufuli na kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Elius Mwakalinga. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongozana na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandala wakati akiwasili kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam.Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea zawadi ya mchoro toka kwa Rais wa Wanafunzi wakati wa sherehe za kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. . Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wakati wa sherehe za kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Elius Mwakalinga. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipongezwa na na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandala wakati akielekea kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
PICHA NA IKULU

KINYEREZI FAMILY YAWAKUMBUKA WATOTO YATIMA WA KITUO CHA NEW HOPE SIKUKUU YA PASAKA

$
0
0

Wadau wa Kinyerezi Family kiwa sambamba na Watoto wa kituo cha Watoto waishio katika mazingira magumu,New Hope kilichopo Tabata,wakisali kwa pamoja mara baada ya kuwakabidhi Msaada wa vitu mbalimbali,ikiwemo mchele,nyama,sukari,mayai,nguo na vinginevyo,ili  watoto hao nao wapate kusherehekea vyema sikukuu ya Pasaka
  Kinyerezi Family wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watoto wa kituo cha Watoto waishio katika mazingira magumu chaNew Hope kilichopo Tabata,mara baada ya kuwakabidhi msaada wa vitu mbalimbali,ikiwemo mchele,nyama,sukari,mayai,nguo na vinginevyo,ili na watoto hao wapate kusherehekea vyema sikukuu ya Pasaka
Pichani kushoto ni Mwenyekiti wa Kikundi cha Kinyerezi Family ,Leo Joseph Manyara na Mdau wakimkabidhi sehemu ya msaada huo Mwanzilishi na Mlezi wa kituo cha New Hope Organizationi,Bi.Consoler Eliya.Kituo hicho kilichopo Tabata,jijini Dar kinalea watoto zaidi ya 150 ambapo kati yao 32 ndio huishi kituoni hapo na wengine huja na kuondoka.
Wana Kikundi cha Kinyerezi Family wakiwa katika picha ya pamoja na Mama Mwanzilishi na Mlezi wa kituo cha Watoto waishio katika mazingira magumu.Consoler Eliya
Mwanzilishi na Mlezi wa kituo cha New Hope Organization,Consoler Eliya akiwashukuru wana Kikundi cha Kinyerezi Family kwa kuwakumbuka watu wenye matatizo mbalimbali kikiwemo kituo chake,kwa kuwapatia msaada wa vitu mbalimbali,ili na wao waweze kusherehekea kwa furaha siku ya Pasakam,Concoler amewaomba wana Kikundi hao na wadau wengine mbalimbali kuwa na moyo wa kujitolea katika suala zima la kusaidia jamii zenye matatizo,kwani kwa kufanya hivyo hata Mungu hawaongezea zaidi palipopungua na kuendelea kuwabariki wao na familia zao
Katibu Msaidizi wa Kikundi cha Kinyerezi Family,Michael Masota akitoa utambulisho na muongozo mfupi mara baada ya kufika kituoni hapo,kushoto ni Mwanzilishi na Mlezi wa kituo hicho cha New Hope,Bi.Consoler Eliya
Sehemu ya msaada huo wa vitu mbalimbali
Mmoja wa wajumbe wa Kikundi cha Kinyerezi Family,Bi Lightness Kweka akizungumza machache katika hafla hiyo fupi ya kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali katika kituo hicho cha New Hope

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRIL 16,2017

Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images