Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46371 articles
Browse latest View live

VYAMA VYA USHIRIKA MANYARA KUNUNUA MAZAO YA WAKULIMA

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Manyara, Dk Joel Bendera amesema katika msimu huu wa kilimo, serikali kupitia bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko (CPB) itanunua mazao ya wakulima kwa kutoa bei nzuri inayokidhi bei ya soko.

Dk Bendera aliyasema hayo mjini Babati kwenye jukwaa la vyama vya ushirika vya mkoa huo ambapo hotuba yake ilisomwa kwa niaba yake na ofisa elimu wa mkoa huo Arnold Msuya.

Alisema watafanikisha zoezi hilo kupitia vyama vya msingi Amcos na chama kikuu Rivacu, kwa kuvitumia kama vituo vya kununulia mazao ya wakulima kwa bei itakayokidhi gharama za uzalishaji.

Alitoa rai kwa viongozi na watendaji wa vyama vya ushirika kutumia fursa hiyo vizuri kukusanya mazao kutoka kwa wakulima katika ubora unaostahili na kutojihusisha na vitendo vya ubadhirifu na wizi.

“Katika kueleka uchumi wa viwanda, vyama vya ushirika hususani AMCOS na RIVACU vina fursa kubwa kuchangia uchumi wa viwanda kwenye  mkoa huu kwani vinategemewa kuwa wazalishaji wa malighafi za viwanda vidogo vya kati na vikubwa,” alisema.

Mrajisi wa vyama vya ushirika nchini Tito Haule aliwataka mrajisi msaidizi wa ushirika wa mkoa huo na maofisa ushirika wa wilaya kuwajengea uwezo wanaushirika kupitia vikundi vyao.

“Wana ushirika wanatakiwa kila mara kupewa elimu ya ushirika na pia kukaguliwa mahesabu yao ili vikundi vyao viimarike na endapo mtashindwa hilo ninyi ndiyo mtakaobeba lawama,” alisema Haule. 

Mrajisi msaidizi wa ushirika wa mkoa huo, Venance Msafiri alisema Manyara ilianzishwa mwaka 2002 ikiwa na vyama 93 hadi sasa wapo 246 na wana ushirika hao huweka hisa za sh1.1 bilioni, akiba ya sh3.4 bilioni na amana ya sh133.2 milioni.

Alisema kati ya idadi hiyo, vyama vya ushirika 104 vipo sinzia yaani havifanyi kazi ya kutoa huduma kama ilivyotarajiwa ila vyama vya ushirika vinaendelea kuimarika na kufanya kazi zao ipasavyo.

“Kuna chama kikuu cha ushirika kimoja cha Rivacu, kuna Saccos 150, vyama vya ushirikia vya mazao 67, mifugo 17, viwanda vidogo sita, madini vitatu, taasisi mbili na duka moja” alisema Msafiri.

Alisema mitaji ya Saccos siyo mikubwa kutokana na viwango vidogo vya hisa, akiba, amana na viingilio vidogo, ila ili kuhakikisha vyama hivyo vinaimarika wana hamasisha viungane ili viwe na nguvu.
Mrajisi wa vyama vya ushirika nchini, Tito Bathelemeo Haule akizungumza mjini Babati Mkoani Manyara, kwenye jukwaa la vyama vya ushirika, lililojumuisha wanachama wa wilaya za Simanjiro, Kiteto, Mbulu, Hanang' na Babati.
 Ofisa elimu wa Mkoa wa Manyara, Arnold Msuya akifungua jukwaa la vyama vya ushirika la mkoa huo mjini Babati, kwa niaba ya mkuu wa mkoa huo Dr Joel Bendera.
 Mwanachama wa Hekima SACCOS ya Wilayani Hanang' Mkoani Manyara Jackson Mtesi akizungumza mjini Babati kwenye jukwaa la vyama vya ushirika vya mkoa huo.
 Mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Manyara, Venance Msafiri akizungumza kwenye jukwaa hilo mjini Babati.

FANYIENI KAZI TAFITI ZA AZASI ZA KIRAIA-JAFO

$
0
0
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI Seleman Jafo akiongea na wageni waalikwa wakiwamo wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa hafla ya utoa wa matokeo wa Tafiti za Uwezo ambapo alipongeza tafiti za TWAWEZA na kuwataka watendaji serikalini kuzitumia tafiti hizo ili kuleta matokeo chanya kwenye sekta ya elimu, leo Mjini Dodoma.
 Mkurugenzi Mtendaji wa TWAWEZA Bw. Aidan Eyakuze akiongea na wageni waalikwa wakiwamo wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa hafla ya utoa wa matokeo wa Tafiti za Uwezo ambapo aliwaeleza kuwa Tafiti hii inasaidia kuonesha hali halisi ya iliyopo mashuleni ili kuboresha sekta ya elimu, leo Mjini Dodoma
 Meneja Uwezo Tanzania Zaida Mgalla akiongea na wageni waalikwa wakiwamo wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa hafla ya utoa wa matokeo wa Tafiti za Uwezo ambapo mbali na changamoto nyingine takwimu mpya za uwezo zinaonesha mwenendo mzuri katika somo la Kiswahili na uwiano mzuri uliopo kati ya wanafunzi na vitabu, leo Mjini Dodoma.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI Seleman Jafo na Mkurugenzi Mtendaji wa TWAWEZA Bw. Aidan Eyakuze wakimsikiliza Meneja Uwezo Tanzania Zaida Mgalla wakati akitoa Matokeo ya tafiti za Uwezo Tanzania, leo Mjini Dodoma.
 Mkurugenzi Mtendaji wa TWAWEZA Bw. Aidan Eyakuze akimkabidhi Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI Seleman Jafo matokeo ya Tafiti ya Uwezo Tanzania yaliyopo katika ripoti ya Je, Watoto wetu wanajifunza? leo Mjini Dodoma.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI Seleman Jafo akimkabidhi Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Jamii Mhe. Peter Serukamba matokeo ya Tafiti ya Uwezo Tanzania yaliyopo katika ripoti ya Je, Watoto wetu wanajifunza? leo Mjini Dodoma.
Baadhi ya Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakichangia mjadala mara baada ya kuwasilishwa kwa matokeo ya Tafiti ya Uwezo Tanzania yaliyopo katika ripoti ya Je, Watoto wetu wanajifunza? Ambapo walitoa mapendekezo kwa Serikali yenye lengo la kuboresha sekta ya elimu Nchini. PICHA NA HASSAN SILAYO

NA HASSAN SILAYO
Serikali imewataka watendaji serikalini kuzifanyia kazi tafiti mbalimbali zinazotolewa na asasi za kiraia ili kuleta matokeo chanya na kuboresha maisha ya watanzania.

Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Seleman Jafo wakati akipokea ripoti ya Takwimu Mpya za Uwezo Tanzania  iliyopo katika TWAWEZA.

Akiongea katika Hafla hiyo Naibu Waziri Jafo amesema kuwa Watendaji Serikalini sasa wana budi wa kufanyia kazi tafiti mbalimbali zinazotolewa na Azaki za kiraia zinazolenga  masuala yaliyopo katika jamii ili kuiwezesha serikali  kuyafanyia kazi matokeo ya tafiti na kuboresha hali ya watanzania.

“Kwa matokeo haya ya Tafiti ya TWAWEZA kupitia Uwezo Tanzania ni kipimo tosha cha kutuonesha sisi kama viongozi yapi tunayotakiwa kufanya na yapi hatutakiwi kufanya na yapi tunatakiwa tuyarekekebishe katika sekta ya elimu na matokeo haya tutayafanyia kazi”-Naibu Waziri Jafo.

Aidha Naibu Waziri Jafo aliwastaka wabunge kutumia vikao muhimu vya kisheria kwenye maeneo yao ya kazi katika kuhakikisha matokeo ya tafiti yanasaidia kuboresha sekta ya elimu  katika Halmashauri huku serikali ikiendelea kuwekeza katika sekta ya elimu.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza Aidan Eyakuze alisema kuwa tathmini hii inayopima matokeo ya kujifunza ambayo ambayo ni kubwa barani afrika inayotekelezwa kwenye baadhi ya nchi ikiwamo Kameruni, Nigeria, Senegali,Mali, Ghana na Burkina Faso inasaidia kuonesha hali halisi ya iliyopo mashuleni ili kuboresha sekta ya elimu.

Naye Meneja wa Uwezo Tanzania Zaida Mgalla amewataka viongozi wa Serikali na wabunge kutumia tafiti hii ya uwezo katika kuhakikisha wanashiriki katika kuboresha elimu katika maeneo yao na Tanzania kwa Ujumla ikiwa ni lengo kuu la kuhahakikisha wanaifikisha sekta ya elimu pale inapotakiwa.

WASANII WAAHIDI BURUDANI KALI TAMASHA LA BURUDANI "NYANZA FESTIVAL 2017" JIJINI MWANZA.

$
0
0
#BMGHabari
Wanatasnia wa burudani hususani wanamuziki mastaa na chipukizi kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa, wameahidi kudondosha burudani kali kwenye tamasha la kwanza na la aina yake la Nyanza Festival litakalofanyika April 15 na 16, 2017 Uwanja wa CCM Kirumba.

"Zaidi ya wasanii 30 kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa tayari wamethibitisha kupanda jukwaa la Nyanza Festival hivyo niwasihi wapenzi wa burudani wakae tayari kwa burudani hiyo ambapo kiingilio itakuwa elfu tano tu". Amesema Afisa Habari wa tamasha hilo, George Binagi.

Nyanza Festival ni tamasha lililoasisiwa na Wanatasnia mbalimbali kutoka Kanda ya Ziwa wakiwemo wanamuziki, watangazaji, waandishi wa habari, Madjz na wadau wengine wengi kupitia umoja wao wa Mwanza.Com chini ya kampuni ya Famara Entertainment, lengo nikiwa ni kuukuza na kuuendeleza muziki wa Kanda ya Ziwa.

RAIS DKTMAGUFULI APOKEA TAARIFA YA UTENDAJI KAZI YA TAKUKURU YA 2016/2016

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU Kamishna Valentino Mlowola akitoa muhtasari wa Taarifa ya Utendaji Kazi wa TAKUKURU ya mwaka 2015/2016 Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne 11, 2017.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea toka kwa Mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU Kamishna Valentino Mlowola Taarifa ya Utendaji Kazi wa TAKUKURU ya mwaka 2015/2016 Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne 11, 2017.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli baada ya kupokea Taarifa ya Utendaji Kazi wa TAKUKURU kwa mwaka 2016/2017 Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne 11, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na Mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU Kamishna Valentino Mlowola na watendaji wa taasisi hiyo baada ya kukabidhiwa Taarifa ya Utendaji Kazi wa TAKUKURU kwa mwaka 2015/2016 Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne 11, 2017.


PICHA NA IKULU

LHRC YAWANOA VIONGOZI WA DINI KUHUSU MCHAKATO WA KATIBA MPYA

$
0
0
 Mkurugenzi wa Baraza la Dini na Amani Tanzania (IRCPT), Mchungaji Thomas Godda, akihutubia wakati akifungua semina ya siku mbili ya viongozi wa dini kuhamasisha uhiishaji wa katiba mpya inayoendelea Hoteli ya Golden Tulip Posta jijini Dar es Salaam leo. Semina hiyo imeandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC).
 Mkurugenzi wa Utetezi na Maboresho wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anna Henga akizungumza kuhusu umuhimu wa semina hiyo kwa viongozi wa dini.
 Meneja Mipango Msaidizi wa (IRCPT), Rogers Fungo akizungumza katika semina hiyo.
Mwenyekiti wa Taifa wa Wanawake wa Baraza la Kiislam Tanzania (Bakwata), Shamim Khan (kulia), akizungumza katika semina ya siku mbili ya viongozi wa dini kuhamasisha uhiishaji wa Katiba mpya iliyofanyika Dar es Salaam leo. Semina hiyo imeandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)
 Semina ikiendelea.
 Wawakilishi kutoka taasisi za dini wakiwa kwenye semina.
Viongozi wa dini wakiwa kwenye semina.

RAIS DKT. MAGUFULI AWAAPISHA WAJUMBE WA KAMATI YA PILI YA UCHUNGUZI WA MADINI YALIYOMO KWENYE MCHANGA KUTOKA MIGODINI

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli akimuapisha Profesa Nehemiah Eliachim Osoro kuwa mwenyekiti wa Kamati Maalum ya Pili itayofanya Uchunguzi wa Madini yaliyomo kwenye Mchanga kutoka kwenye migodi mbalimbali hapa nchini kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Aprili 11, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli akimuapisha Profesa Longinus Kyaruzi Rutasitara kuwa mjumbe wa  Kamati Maalum ya Pili itayofanya Uchunguzi wa Madini yaliyomo kwenye Mchanga kutoka kwenye migodi mbalimbali hapa nchini kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Aprili 11, 2017.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt Oswald Joseph Mashindano  kuwa mjumbe wa  Kamati Maalum ya Pili itayofanya Uchunguzi wa Madini yaliyomo kwenye Mchanga kutoka kwenye migodi mbalimbali hapa nchini kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Aprili 11, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli akimuapisha Bw. Casmir Sumba Kyuki kuwa mjumbe wa  Kamati Maalum ya Pili itayofanya Uchunguzi wa Madini yaliyomo kwenye Mchanga kutoka kwenye migodi mbalimbali hapa nchini kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Aprili 11, 2017.

Makampuni ya simu yaungana kutoa huduma za kifedha

$
0
0
Meneja wa Airtel Money kutoka kampuni ya Airtel Tanzania Moses Alphonce akitoa elimu kwa mmoja wa watumiaji wamitandano ya simu kwa namna Makampuni ya simu za mikononi nchini yameungana kwa kutoa huduma za kutuma na kupokea fedha kwenda mitandao yeyeto nchini kwa kiwango cha gharama ile ile.

Makampuni ya simu za mikononi nchini yameungana kwa kutoa huduma za kutuma na kupokea fedha kwenda mitandao yeyeto nchini kwa kiwango cha gharama ile ile. 

Kwenye muungano huo ambao unaitwa Taifa Moja, makampuni matatu makubwa ya kutoa huduma za simu za mkononi ya Tigo Tanzania, Airtel Tanzania na Zantel, wateja wanaweza kutuma pesa na kupokea kutoka kwenye moja ya mitandao hiyo kwa gharama zile zile.

 Hapo awali, kutuma pesa au kupokea pesa kutoka mtandao tofauti mteja alikuwa akipokea ujumbe mfupi ambao ilikuwa ni lazima apeleke kwa wakala wa mtandao ambao amepokea fedha kutoka na ilikuwa izizidi siku saba tofauti na hapo fedha hiyo ilikuwa inarudi kwa aliyetuma. 

Kwa huduma hii, mteja anapaswa kuchangia huduma ya kutuma pesa kutoka kwa menu ya kawaida, halafu anachangua kutuma pesa kwenda mitando mingine. 

Akizungumza jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki wakati wa kutembelea watumiaji wa huduma za kutuma na kupokea pesa, Meneja wa Airtel Money kutoka kampuni ya Airtel Tanzania Moses Alphonce alisema kupitia muungano wa Taifa Moja wameweza kuwafanya wateja wapate njia rahisi ya kutuma na kupokea fedha.

Tunajua hapo zamani kuna baadhi ya wateja walikuwa wanapata wakati mgumu linapokuja suala la kutuma na kupokea fedha. Ilikuwa aidha upokee fedha kwa ujumbe mfupi au uwe na laini ya simu zaidi ya moja. Ukipokea fedha kwa ujumbe na kwa bahati mbaya ukaufuta ilikuwa inamaanisha fedha imepotea, alisema Alphonce. 

Lakini vile vile si kila mtu anayepokea fedha kupitia simu ya mkononi anahitataji kutoa. Wengine wanataka kulipia huduma mbali mbali kupitia huduma ya simu kama kulipia maji, kununua umeme au matumizi mengineyo. Kwa huduma hii mpya ya Taifa Moja imekuwa ni njia rahisi kwa wateja wetu, aliongeza Alphonce 

Kupitia huduma hii ya kutuma pesa na kupokea kutoka mitandao yeyote itachangia kuongeza idadi ya watu wanaotumia huduma za kutuma na kupokea fedha kwa kutumia simu za mkononi na pia kuongeza faida kwa makampuni ya simu. 

Hii ni mara ya kwanza Tanzania kwa makampuni ya simu kuungana pamoja kwa huduma ya pamoja. Hata hivyo, Taifa Moja sio huduma au mtandao mpya mbali ni njia ambayo imepewa promosheni hii ya kutuma na kupokea fedha kutoka mtandao wowote. 

Kwa upande wake, Mkuu wa usambazaji mkoa wa Dar es Salaam kutoka kampuni ya Tigo Tanzania Lloyd Kaaya. alisema ni furaha kwao kuona kwamba wateja wa simu za mkononi kwa sasa hivi anaweza kutuma na kupokea pesa kutoka mtandao wowote kwa gharama zile zile. Hii inaamanisha matumizi wa kutuma pesa yataongeza na yatakuwa na manufaa kwa upande wetu, alisema Kaaya.

PROF. MUHONGO AKUTANA NA KAMPUNI YA JUMEME

$
0
0
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto), akisisitiza jambo kwa Ujumbe kutoka Kampuni ya JUMEME, waliomtembelea ofisini kwake mjini Dodoma kuzungumzia masuala ya uzalishaji umeme wa jua. Kutoka kulia ni Leo Schiefermueller, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT), Padre Dk. Thadeus Mkamwa na Kaimu Kamishna wa Nishati na Masuala ya Petroli, Mhandisi Innocent Luoga.
 Mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya JUMEME, Leo Schiefermueller (kulia), akifafanua jambo kwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto). Wengine pichani ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT), Padre Dk. Thadeus Mkamwa (wa pili kutoka kulia) na Kaimu Kamishna wa Nishati na Masuala ya Petroli, Mhandisi Innocent Luoga.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa pili kutoka kushoto), akitoa maelekezo kwa Ujumbe kutoka kampuni ya JUMEME ambao ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT), Padre Dk. Thadeus Mkamwa (kushoto) na Leo Schiefermueller kutoka Ujerumani (kulia). Wa pili kutoka kulia ni Kaimu Kamishna wa Nishati na Masuala ya Petroli, Mhandisi Innocent Luoga.
Mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya JUMEME, Leo Schiefermueller (kushoto), akifafanua jambo kwa Kaimu Kamishna wa Nishati na Masuala ya Petroli, Mhandisi Innocent Luoga (kulia). Pamoja nao pichani, ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT), Padre Dk. Thadeus Mkamwa.

Na Veronica Simba - Dodoma.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amekutana na ujumbe kutoka kampuni ya JUMEME inayojishughulisha na uzalishaji wa umeme kwa kutumia nishati ya jua.

Ujumbe huo ulijumuisha baadhi ya wakurugenzi wa kampuni ya JUMEME ambao ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT), Padre Dk. Thadeus Mkamwa na Leo Schiefermueller.
Ujumbe huo ulifika ofisini kwa Waziri Muhongo mjini Dodoma, kumweleza mipango na mikakati yao ya kuendelea na uzalishaji wa umeme wa jua katika maeneo ya Tanzania yaliyo nje ya gridi ya Taifa ya umeme.
Kampuni hiyo, inaendesha mradi wa kuzalisha umeme wa jua katika Kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe na imelenga kuwafikia watu milioni moja ndani ya Tanzania kupitia mitambo 300 katika vijiji vilivyo nje ya gridi ya Taifa ifikapo mwaka 2022.
Profesa Muhongo, kwa upande wake, aliwahakikishia JUMEME kuwa Serikali itawapa ushirikiano unaotakiwa ili kuhakikisha wananchi wa vijijini wanapata umeme kwa kutumia njia mbalimbali muafaka kama ilivyodhamiriwa.

MABALOZI WAPYA WA JAMHURI YA MUUNGANO WAMUAGA RAIS DK. SHEIN

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mabalozi wapya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioteuliwa kuiwakilisha  Tanzania  katika Nchi mbali mbali walipofika kumuaga Rais Ikulu Mjini Zanzibar leo,[Picha na Ikulu.] 11/04/2017.
MAB2
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Ujumbe Mabalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioteuliwa kuiwakilisha  Tanzania katika Nchi mbali mbali,  walipofika kumuaga Rais Ikulu Mjini Zanzibar leo/ [Picha na Ikulu.] 11/04/2017. 

MATUKIO KATIKA PICHA WAKATI WA KUJADILI NA KUPITISHA BAJETI YA OFISI YA WAZIRI MKUU BUNGENI DODOMA.

$
0
0


 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama na Naibu wake anayeshughulikia masuala ya Kazi, Ajira na Vijana, Mhe. Antony Mavunde wakifuatilia uwasilishwaji wa michango ya wabunge kuhusu bajeti ya Ofisi hiyo wakati wa Bunge la Bajeti Dodoma Aprili 11, 2017.
A 1
Baadhi ya Watendaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) wakinukuu hoja mbalimbali za wabunge wakati wa kujadili na kuipitisha bajeti ya Ofisi hiyo wakati wa Bunge la Bajeti linaloendelea Dodoma.
A 3
Makatibu Wakuu Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia michango ya wabunge wakati wa kujadili na kuipitisha bajeti ya Ofisi hiyo katika Bunge linaloendelea Dodoma, wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi na anayemfuata ni Katibu Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Bw. Erick Shitindi Bungeni tarehe 11 Aprili, 2017.
A 4
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiongea na Mbunge wa Chambani (CUF) Mhe. Yusuf Salim nje ya Viwanja vya Bunge Dodoma wakati wa Bunge la Bajeti Aprili 11, 2017.
A 5
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Vijana), Mhe. Antony Mavunde akisalimiana na Mbunge wa Viti Maalumu Kilimanjaro Mhe. Shally Raymond nje ya Ukumbi wa Bunge Dodoma wakati wa Bunge la Bajeti linaloendelea Dodoma tarehe 11 Aprili 2017.
(PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU-DODOMA)

SERIKALI YAZINDUA USAMBAZAJI WA VIFAA VYA HOSPITALI NCHINI

$
0
0
Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai , Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy na Mkuu wa wilaya ya Kongwa Bw.Deogratius Ndejembi wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa mpango huo .
Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai akipokea vitanda hivyo kutoka kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy , kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Kongwa Bw.Deogratius Ndejembi.

Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai , Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy , kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Kongwa Bw.Deogratius Ndejembi.wakikagua vitanda hivyo mara baada ya makabidhiano.






Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai akizungumza wakati wa uzinduzi wa ugawaji wa vitanda vya hospitali nchi nzima uliofanyika wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma leo katikati ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy na kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Kongwa Bw.Deogratius Ndejembi
 
 
……………………………………………………………………..
Serikali ya awamu ya tano nchini imezindua rasmi usambazaji wa vifaa vya hospitali kwa halmashauri zote nchini katika kutekeleza mkakati wa kuboresha huduma za afya nchini kwa kuhakikisha wananchoi wanapata huduma kwa kiwango stahiki 

Akizindua usambazaji huo leo wilayani hapa,Waziri wa Afya,maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy mwalimu alisema serikali imetekeleza ahadi iliyotoa kwa wananchi ambapo serikali inawekeza katika afya ya wananchi hivyo kuweza kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa uchumi wa viwanda 

Akizungumza kwenye hadhara ya wanachi wa Wilaya ya Kongwa,Waziri Ummy alisema serikali imefanya uwekezaji mkubwa kwa baadhi ya maeneo ikiwemo ya upatikanaji wa dawa ambapo bajeti ya dawa imeongezeka kutoka shilingi bilioni 31 mwaka 2015/16 hadi shilingi bilioni 251 mwaka 2016/17. 

“Hatua hii imeleta mapinduzi makubwa katika upatikanaji wa dawa,vifaa na vifaa tiba kwenye vituo vya Umma vya kutolea huduma za afya,hivyo wanaomba wananchi kuhakikisha mnafika kwnye vituo vya kutolea huduma za afya ili kupata matibabu sahihi” 

Aidha, Waziri Ummy alisema kufuatia ahadi ya Mhe. Rais ya kununua na kusambaza vitanda kwenye vituo vya Umma ,Wizara yake kwa bajeti ya mwaka 2016/17 ilitenga kiasi cha shilingi biliuoni 4 za kuwezesha kununua pamoja na kusambaza vifaa hivyo kwa halmashauri 184 nchini
Alivitaja vifaa vilivyonunuliwa na kuvikabidhi kwa Mhe. Job Ndungai (Mb), Mbunge wa Kongwa na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungazo wa Tanzania Mhe. John Ndugai ni pamoja na vitanda vya hospitali (20),vitanda vya kujifungulia wajawazito (5), magodoro (25) na mashuka (50). 

Vifaa vya Hospitali vitakavyopasambazwa kwenye Halimashauri zote 184 nchini ni pamoja na vitanda vya hHospitalini 3,680; vitanda vya kujifungulia akinamama wajawazito 920; magodoro 4,600; na mashuka 9,200. Thamani ya vifaa hivi ni shilingi bilioni 2,933, 125,600. Zoezi la kugawa vifaa hivi linatarajiwa kukamilika kabla ya Juni 30, 2107. 

Akipokea vifaa hivyo, Mhe. Ndugai ameishukuru Serikali kwa msaada wa vifaa vilivyotolewa kwa Hospitali na vituo vya Afya katika mkoa wa Dodoma ikiwemo Halmashauri Kongwa. Vifaa hivyo vitaboresha afya ya wananchi wa jimbo la Kongwa na maeneo mengine nchini na hivyo kusaidia kuwawezesha wananchi kukutumia mudao wao mwingi katika shughuli za kiuchumi.

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AZINDUA KIKOSI KAZI CHA UOKOAJI WA MFUMO-IKOLOJIA WA BONDE LA MTO RUAHA MKUU

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza mkutano wa uzinduzi wa kikosi kazi cha kuokoa mfumo-ikolojia wa bonde la mto Ruaha Mkuu uliofayika kwenye ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.
Mhe. January Makamba akithutubia juu ya umuhimu wa mto Ruaha ambao unahudumia watu zaidi ya milioni 6 na namna ambavyo umeathirika na shughuli za binadamu kwenye warsha ya uzinduzi wa kikosi kazi cha kuokoa mfumo- ikolojia wa bonde la mto Ruaha Mkuu uliofayika kwenye ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi (MB) Mhe. Wiliam Lukuvi (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe.Amina Masenza wakati wa mkutano wa uzinduzi wa kikosi kazi cha kuokoa mfumo-ikolojia wa bonde la mto Ruaha Mkuu uliofayika kwenye ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.



Waziri wa Maji na Umwagiliaji wa Tanzania Mhandisi Gerson Lwenge akihutubia wakati wa warsha ya uzinduzi wa kikosi kazi cha kokoa mfumo -ikolojia wa bonde la mto Ruaha mkuu.

Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa Jumanne Maghembe akichangia mawazo yake wakati wa warsha ya uzinduzi wa kikosi maalum cha kuokoa mfumo-ikolojia katika bionde la mto Ruaha mkuu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba wakati wa mkutano wa uzinduzi wa kikosi kazi cha kuokoa mfumo- ikolojia wa bonde la mto Ruaha Mkuu uliofayika kwenye ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela akichangia mtazamo wake wakati wa uzinduzi wa kikosi kazi cha kuokoa mfumo-ikolojia wa bonde la mto Ruaha mkuu.


....................................................................................................


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amezindua Kikosi Kazi Maalum kwa ajili ya kuokoa mfumo wa ikolojia katika bonde la mto Ruaha Mkuu ambalo lipo katika hatari ya kutoweka kutokana na uharibifu mkubwa wa mazingira unaoendelea kwenye bonde hilo kutokana na shughuli za Kibinadamu.

Kikosi kazi hicho ambacho kimezinduliwa mjini Iringa kitafanya kazi chini ya usimamizi wa Makatibu Tawala wa mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe kwa kuchambua kwa kina tafiti na matokeo ya tafiti hizo ili kupendekeza hatua za haraka zitakazochukuliwa katika kudhibiti uharibifu kwenye bonde hilo ambao umechangia kupungua kwa maji kwenye mto Ruaha Mkuu.

Akizindua Kikosi kazi hicho mjini Iringa ambacho ambacho kimehudhuriwa na Mawaziri kutoka Wizara Tano, Makamu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amesema ofisi yake imeamua kuunda kikosi hizo ili kuokoa hali mbaya ya uharibifu wa mazingira unaoendelea kufanyika hivi sasa katika Bonde la Mto Ruaha Mkuu.

Amesema kutokana hali kuwa tete kwenye bonde hilo ndio maana hatua ya haraka na za dharura zimechukuliwa na ofisi yake kwa kuunda kikosi kazi hicho ambacho kinaundwa na wataalamu mbalimbali wa serikali, washirika wa maendeleo ambao wana uwezo wa kufanya maamuzi ya kisera na kiutendaji ili kutoa suluhu ya kudumu ya kuhifadhi bonde hilo.

“Muda wa kusema bila kutenda umeshaisha nataka kikosi kazi hiki kifanye kazi usiku na mchana na kuleta matokeo bora na kwa muda mfupi”. Amesisitiza Makamu wa Rais.
Makamu wa Rais amewataka wajumbe wa kikosi kazi hicho washirikishe wadau wote katika kufanya kazi hiyo ili kujenga dhana ya uwajibikaji katika uhifadhi wa mazingira ya Bonde la Mto Ruaha Mkuu.

Amesema anaimani kubwa kuwa wajumbe wa kikosi kazi kilichoundwa na ofisi yake kitakuwa na mchango mkubwa katika kufikia azma ya serikali ya kuokoa mfumo wa ikolojia katika bonde hilo kwa kubuni mikakati kabambe na endelevu ya kukabiliana na uharibifu huo.

Makamu wa Rais alinukuu hotuba ya Papa Mtakatifu Francis Mjini Rome, Italia katika Mkutano wa Pili wa Lishe wa Duniani uliofanyika mwaka 2014 aliyesema kuwa Mungu anasamehe lakini Mazingira hayasamehi akimaanisha kuwa ni muhimu kwa wadau wote wakashiriki kikamilifu katika utunzaji wa mazingira kwa ajili ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January makamba amemhakikishia Makamu wa Rais kuwa Kikosi kazi kilichoundwa kitafanya kazi kwa viwango vinavyotakiwa ili kuhakikisha mfumo wa ikolojia katika bonde la mto Ruaha Mkuu unalindwa na kutunzwa ipasavyo.

Amesema kuwa kikosi kazi hicho pia kitakuwa na jukumu la kukusanya maoni na mapendekezo ya wadau wote ikiwemo wananchi wanaoishi katika bonde hilo kuhusu namna ya kutunza bonde pamoja na kuandaa rasimu ya Mapango wa Kitaifa wa Hifadhi ya Mazingira ya Bonde la Mto Ruaha Mkuu.

Aidha kikosi kazi hicho kitakuwa na mamlaka ya kuchukua hatua za moja kwa moja kwa kutumia mamlaka ya sheria mbalimbali kwa masuala ya kisekta na kuwakilisha mapendekezo kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais.

Kikao hicho cha uzinduzi wa Kikosi Kazi Maalum kwa ajili ya kuokoa mfumo wa ikolojia katika bonde la mto Ruaha Mkuu kimehudhuriwa na Mawaziri Watano ambao ni Waziri Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge, Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa Jumanne Maghembe.

Mawaziri wengine ni Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dakta Charles Tizeba, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba ambaye ameunda kikosi kazi hicho.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

RAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI MGENI RASMI UZINDUZI WA RELI YA KISASA KESHO

$
0
0
RAIS Dk. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa  uwekaji wa jiwe la msingi wa ujenzi reli ya kisasa itakayofanyika  kesho Pugu, Ilala jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jijini Dar es Salaam katika sehemu ya uzinduzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kuwa watanzania waunge mkono jitihada zinazofanywa na serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Dk. John Pombe Magufuli.

Amesema reli hiyo ni ya kisasa ambayo itarahisisha usafiri wananchi kuondokana na adha ya kusafiri kwa muda mrefu.Makonda amesema baada ya uzinduzi ajira zitatoka katika ujenzi wa reli hiyo na kuwataka wataopata ajira kuwa walinzi reli hiyo.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli (TRL)  Mhandisi Massanya Kadogosa amesema kuwa ujenzi huo utaanza kwa awamu .Amesema miundombinu hiyo hiyo ikikamilika gari moshi litatembea kilomita 160 kwa sasa hivyo kwa safari zote zitakuwa ni fupi na wananchi wanaweza kujenga uchumi.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akioneshwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema   maandalizi ya uzinduzi wa uwekaji wa jiwe la msingi wa reli ya kisasa Standard Gauge Pugu jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda  akipata maelekezo kwa Mkurugenzi Mtendaji  wa Shirika la Reli Tanzania (TRL),  Mhandisi ,Massanja Madogosa  juu ya katika maandalizi ya a uzinduzi wa uwekaji wa jiwe la msingi wa reli ya kisasa Standard Gauge Pugu jijini Dar es Salaam.
 .Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akitoa maelekezo  kwa watendaji walipotembelea  maandalizi ya uzinduzi wa uwekaji wa jiwe la msingi wa reli ya kisasa 'Standard Gauge' kesho Pugu jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRL) Mhandisi Massanja Kadogosa akizungumza na waandishi wa habari juu  ya uzinduzi wa uwekaji wa jiwe la msingi wa reli ya kisasa utaofanyika kesho  Pugu jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wananchi waliofika kushuhudia eneo hilo la tukio hapo kesho

TIB CORPORATE YAWAKUTANISHA WADAU WA MAENDELEO JIJINI MWANZA

$
0
0
  Mkuu wa kitengo Cha masoko na mahusiano ya Benki ya TIB CBL ,  Bi Theresia Soka akiwasilisha mada juu ya huduma zinazopatikana katika benki hiyo kwa washiriki wa jukwaa la biashara lililofanyika katika ukumbi wa Rock City jijini Mwanza.

Jukwaa hili limehusisha wadau mbalimbali ili kujadili na kutambua fursa mbalimbali zinazopatikana katika mkoa wa Mwanza.
Wadau mbalimbali wa kiwa kwenye picha ya pamoja walioshiriki kwenye jukwaa la biashara lililofanyika katika ukumbi wa Rock City jijini Mwanza.

YANGA WATOA TAMKO JUU YA KAMATI YA SAA 72, YAIONYA KUTENDA HAKI RUFAA YA SIMBA

$
0
0
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji wa Yanga Salum Mkemi akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tamkom lao juu ya maamuzi na utendaji wa kmati ya saa 72 dhidi ya rufaa ya timu ya Simba dhidi ya Kagera. Kushoto ni Katibu  Mkuu wa Yanga Charles Mkwasa.


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

WAJUMBE wa kamati ya Utendaji wa Yanga wameweka wazi maamuzi yao ya kutakuwa na imani na maamuzi na utendaji wa kamati ya saa 72 kwa rufaa mbalimbali zilizowakilishwa wao kubwa ikiwa rufaa ya Simba SC kwa Kagera Sugar.

Viongozi hao wakiongozwa na Mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya Yanga Mhandisi Paul Malume , wamesema hawana imani na kamati hiyo na kinachoendelea ni kutaka kuvuruga utulivu wa ligi kuu na soka kiujumla .

Mjumbe wa kamati ya Utendaji Salumu Mkemi mjumbe kamati kuu Yanga SC amesema kamati hiyo haina usawa pia ni kamati inayoundwa na zaidi ya wanachama 6 wandamizi wa Simba SC na wao kama Yanga wakiwa na wanachama wawili tu.

Mkemi amesema kuwa tayari wameziangazia harufu na fununu ya kubadilishwa kwa ripoti za michezo ambayo Simba wanasema mlinzi wa Kagera Mohamedi Fakhi alipata kadi 3 za njano .

" kamati hii imechelewa kutoa maamuzi kwa kuandaa ripoti za uongo za michezo dhidi ya Fakhi pia tuna taarifa za kughushiwa email na nyaraka zingine ili kuipa alama tatu Simba SC yenye zaidi ya wajumbe 6 katika kamati hiyo sisi kama Yanga tumeanza uchunguzi wetu na kutoa taarifa kwa vyombo husika vya dola pia maamuzi yoyote ya kuibeba Simba tutakwenda mahakamani licha ya sheria za FIFA kukataza hivyo kama hawataki tufike huko lazima haki itendeke. .." alieleza mjumbe huyo.

Mkemi amesema kuwa tayari wameshavijulisha vyombo husika yaani Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na watu wa makosa ya mtandao (cyber crime) na Mamlaka ya mawasiliano Nchini (TCRA)  juu ya uchunguzi wa mawasilano ya waamuzi wote waliosika na kutajwa kwenye rufaa hiyo.

" tuache kumtafuta bingwa wa mezani na sisi tumefungwa karibu mechi tatu na hatujalilia alama za mezani kwanini wao,  mbona jana wamecheza mchezo mzuri mwishoni na kupata ushindi wa jioni dhidi ya Mbao na hakuna kelele tena na tunawapongeza kwa come back ile . Hiki ndicho mashabiki wa timu hizi wanakitaka . Ushindi wa uwanjani sio figisu . "
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji wa Yanga Salum Mkemi akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tamkom lao juu ya maamuzi na utendaji wa kmati ya saa 72 dhidi ya rufaa ya timu ya Simba dhidi ya Kagera. Kulia ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji wa Yanga, Siza Lyimo, shoto ni Katibu  Mkuu wa Yanga Charles Mkwasa na Mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya Yanga Mhandisi Paul Malume .


SERIKALI YAANDAA MUSWADA WA SHERIA KUSIMAMIA NA KUDHIBITI BIASHARA YA VYUMA CHAKAVU.

$
0
0
Waziri wa Viwanda , Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage akijibu hoja mbalimbali za wabunge katika kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.

Na Daudi Manongi-MAELEZO, DODOMA.

Serikali kupitia Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji imeandaa Rasimu ya Muswada wa Sheria itakayoweka bayana taratibu na mfumo wa usimamizi na udhibiti wa bishara ya chuma chakavu katika hatua mbalimbali za uzalishaji, ukusanyaji, usambazaji, uuzaji na uyeyushaji wake kwa kuzingatia uhifadhi na usimamizi wa mazingira kwa manufaa ya Taifa.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mhe.Charles Mwijage wakati akijibu hoja mbalimbali za wabunge Mjini Dodoma.

“Biashara ya Chuma chakavu imeshamiri hapa nchini na duniani kwa ujumla,na hili limetokana na mahitaji ya vyuma chakavu ambapo kumetumiwa na wahalifu kuaharibu miundombinu iliyojengwa kwa vyuma kwa nia ya kupata chuma ili waiuze kama chuma chakavu”Alisema Mwijage.

Amesema ili kukabiliana na hujuma hizi Mamlaka husika zikiwemo TANESCO, TANROADS  na  RAHACO wamekuwa wakifanya kazi kwa karibu na jeshi la Polisi ikiwemo kutumia walinzi wa Taasisi husika ili kulinda rasilimali hizo.

Amesisitiza kuwa Muswada huu umeweka wazi na bayana adhabu itakayotolewa kwa mtu atakayebainika kuharibu miundombinu.
Aidha Mhe.Mwijage ametoa wito kwa watanzania kutoa taarifa pindi waonapo mtu anayehujumu  miundombinu kwa namna yote ile.

“Natoa wito kwa wenye viwanda na wafanyabiashara wa vyuma chakavu jiepusheni na ununuzi wa vyuma  ambavyo asili yake ina mashaka na tutaharakisha sheria  hii ili kutatua tatizo hili”Aliongeza Mwijage.

YALIYOJIRI KATIKA KIKAO CHA TANO CHA MKUTANO WA SABA WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA LEO MJINI DODOMA.

$
0
0
Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mussa Azzan Zungu akiongoza kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Naibu waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Suleimani Jafo akijibu hoja mbalimbali za wabunge katika kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Waziri wa Viwanda , Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage akijibu hoja mbalimbali za wabunge katika kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Edwin Ngonyani akijibu hoja mbalimbali za wabunge katika kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Mbunge wa Mwibara(CCM) Mhe. Kangi Lugola akiuliza swali katika kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Fakharia Shomar Khamis (CCM) akiuliza swali katika kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Mh. Eng. Isack Aloyce Kamwelwe akijibu hoja mbalimbali za wabunge katika kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt Hussein Mwinyi akijibu hoja mbalimbali za wabunge katika kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Mbunge wa Ukonga (CHADEMA) Mwita Waitara akiuliza swali katika kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Naibu Waziri wa Kilimo Uvuvi na Ufugaji Mhe. William Ole Nasha akijibu hoja mbalimbali za wabunge katika kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Mbunge wa Urambo (CCM) Magreth Sitta akiuliza swali katika kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Mbunge wa Iringa Mjini (CHADEMA), Mhe. Peter Msigwa akiuliza swali katika kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Naibu Waziri wa Elimu Sayansi Teknolojia na Ufundi Mhe. Stella Manyanya akijibu hoja mbalimbali za wabunge katika kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Mbunge wa Shaurimoyo (CCM), Mattar Ali Salum akiuliza swali katika kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bungela Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa(kulia) akimsikiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Ajira kazi na watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama(kushoto) wakati wa kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma katikati ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju.
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni sanaa na Michezo Mhe. Anastazia wambura(Kushoto) na Naibu Waziri wa Elimu Sayansi Teknolojia na Ufundi Mhe. Stella Manyanya wakifuatilia kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya waziri Mkuu Sera Bunge Ajira Kazi na watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akijadiliana jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angellah Kairuki katika kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakifuatilia kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.
Wajumbe nane kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakifuatilia shughuli za kikao cha tano cha mkutano wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma.

Picha zote na Raymond Mushumbusi MAELEZO Dodoma.

……………….

SERIKALI YAFAFANUA KUSHAMIRI KWA BIASHARA YA VYUMA CHAKAVU, MPANGO WA KUUNDA BODI MPYA YA TUMBAKU NA UTENGAJI ASILIMIA MAALUM KWA WANAFUNZI KUTOKA TANZANIA BARA NA ZANZIBAR


Dodoma,Jumanne, 11 April, 2017.

Serikali imetoa ufafanuzi kuhusu kushamiri kwa Biashara ya vyuma chakavu,Mpango wa kuunda bodi mpya ya Tumbaku na Utengaji wa asilimia maalum kwa wanafunzi kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, Ufafanuzi huo umetolewa leo Bungeni mjini Dodoma.


Kushamiri kwa Biashara ya Vyuma Chakavu

Serikali imesema kuwa, imekwishaandaa Rasimu ya Muswada wa Sheria itakayoweka bayana taratibu na mfumo wa usimamizi na udhibiti wa biashara ya chuma chakavu katika hatua mbalimbali za uzalishaji,ukusanyaji,usambazaji,uuzaji na uyeyushaji wake kwa kuzingatia uhifadhi na usimamizi wa mazingira kwa manufaa ya Taifa.

Hatua hiyo imekuja baada ya kuongezeka kwa mahitaji ya vyuma chakavu hapa nchini na duniani kwa ujumla na kubainisha maeneo yaliyoathirika sana kuwa ni mifumo ya kusafirisha Umeme,Reli na Barabara.

Akifafanua kuhusu hoja hiyo, Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mhe.Charles Mwijage amesema Muswada huo umeweka bayana adhabu itakayotolewa kwa mtu atakayebainika kuharibu miundombinu.

Aidha Mhe.Mwijage ametoa wito kwa Wananchi wote kutoa taarifa pindi waonapo mtu anayehujumu miundombinu kwa namna yoyote ile.


Mpango wa kuunda Bodi mpya ya Tumbaku.

Serikali imesema kuwa, iko katika maandalizi ya kuunda Bodi mpya ya Wakurugenzi wa Tumbaku haraka iwezekanavyo na Wananchi watajulishwa kupitia tamko la Serikali mara baada ya taratibu kukamilika.

Naibu Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mhe.William Ole Nasha amesema kuwa, Serukali ilivunja Bodi ya Tumbaku kwa lengo la kufanya maboresho katika utendaji kazi wake.

Ameongeza kuwa, hatua ya kuvunja Bodi hiyo haihusiani na kusitisha shughuli zinazotekelezwa katika Kilimo cha Tumbaku kwani wapo wataalamu wanaondeleza utekelezaji wa mpango uliopo wa kuendeleza zao la Tumbaku nchini.

Aidha kwa kuzingatia kuwa wakulima wanahitaji huduma muda wote hasa kipindi hiki cha kuelekea masoko ya tumbaku kwa msimu wa 2017/18,Serikali kupitia mrajis wa vyama vya Ushirika nchini imeshateua timu nyingine ambayo ipo Mkoani Tabora ikiendelea kuratibu na kusimamia masuala mbalimbali ya wakulima ikiwa ni pamoja na kuandaa upatikanaji wa pembejeo kwa msimu ujao.

Serikali kuendelea kutenga fedha kwa wahitaji wa Mikopo ya Elimu ya juu.


Serikali imesema kuwa itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya juu kwa kuzingatia Sheria,kanuni na taratibu na miongozo itolewayo mara kwa mara na serikali kupitia bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya juu.

Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi Mhe. Stella Manyanya amesema kuwa utoaji wa Mikopo unazingatia muombaji awe raia wa Tanzania,muhitaji,mlemavu au yatima na mabaye amedahiliwa katika elimu ya juu na mwenye kuchukua programu za vipaumbele vya Taifa kama Sayansi, Hisabati,uhandisi wa Gesi na Mafuta, Sayansi za Afya na Sayansi za Kilimo na Maji.


Aidha Mhe.Manyanya amesema kuwa katika Mwaka wa 2015/16 Serikali ilitoa kiasi cha Tsh.bilioni 480 kugharamia Mikopo pamoja na ruzuku kwa wanafunzi wapatao 124,358.

Ameongeza kuwa Serikali inalifanyia kazi suala la wanafunzi kutopata Mikopo ili kuongeza idadi ya wanafunzi.



Imetolewa na:

Idara ya Habari-MAELEZO.

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Kuzindua Klabu za Elimu ya Uzimaji Moto Shule za Sekondari Nchini

$
0
0


Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,Thobias Andengenye, akizungumza na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali(hawapo pichani) wakati wa mkutano wa kueleza mipango mbalimbali ya jeshi hilo ikiwemo uzinduzi wa klabu katika shule za sekondari nchini, zitakazotoa elimu ya uzimaji moto kwa wanafunzi.Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Idara ya Habari(Maelezo),jijini Dar es Salaam leo, Kushoto ni Afisa Habari Mwandamizi, Casmir Ndambalilo.

Mmoja wa waandishi wa habari waliohudhuria mkutano wakuelezea mipango mbalimbali ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ikiwemo uzinduzi wa klabu katika shule za sekondari, zitakazotoa elimu ya uzimaji moto kwa wanafunzi, akiuliza swali kwa Kamishna Jenerali wa jeshi hilo,Thobias Andengenye(hayupo pichani), wakati wa mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Habari(Maelezo), jijini Dar es Salaam leo.
Waandishi wa habari waliohudhuria mkutano wakuelezea mipango mbalimbali ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ikiwemo uzinduzi wa klabu katika shule za sekondari nchini, zitakazotoa elimu ya uzimaji moto kwa wanafunzi, wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa jeshi hilo, Thobias Andengenye wakati wa mkutano huo uliofanyika leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari(Maelezo), jijini Dar es Salaam leo.

Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRIL 12,2017

MSANII IZZO BUSINESS ATUMBUIZA ONESHO LA COCA-COLA JIJINI MBEYA

$
0
0
 
Msani Izzo Business akiwa kwenye jukwaa la Coca-Cola kutoa burudani kwa wakazi wa Mbeya. Burudani hiyo ilitolewa katika uwanja wa Nzovwe, mjini Mbeya.
Viewing all 46371 articles
Browse latest View live




Latest Images