Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46340 articles
Browse latest View live

BALOZI WA LUPEMBE AIPA MKONO WA BARAKA AZAM KWENYE MECHI YA MARUDIANO J'PIL

$
0
0
BALOZI wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Richard Lupembe, ameweka wazi kuwa Azam FC ni moja ya timu zinazowatia moyo  Watanzania wanoishi nje ya nchi, huku akiipa mkono wa ushindi kuelekea mchezo wa marudiano dhidi ya Mbabane Swallows ya Afrika Kusini.

Lupembe alitoa kauli hiyo wakati alipoitembelea timu hiyo jana kwenye kambi yake katika Hoteli ya Acardia jijini Pretoria, nchini humo ikijiandaa na mchezo huo wa Kombe la Shirikisho Afrika utakaofanyika Uwanja wa Taifa wa Somhlolo nchini Swaziland Jumapili hii saa 10.30 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

“Kwa kweli nimefarijika sana kwa kuiona Azam FC tena kama nakumbuka mlikuja hapa mwaka jana, mlikuja hapa kucheza na  Bidvest nikawa mgeni rasmi na mkono wangu ukawa wa kheri mkashinda, nawahakikishieni nitawashika tena mkono na ninauhakika mtashinda tena,” alisema Lupembe

Alisema kuwa atakuwa pamoja na timu hiyo kwa kipindi chote itakapokuwa jijini hapa hadi Jumamosi itakapoelekea Swaziland huku akiitakia kila la kheri kuelekea mtanange huo unaosubiriwa na mashabiki wengi wa timu hizo.

“Ndio tunafahamu kuwa kuna timu kubwa za Simba na Yanga, lakini Azam FC inatia moyo kwa sisi watu ambao tulioko nje nawatakia kila la kheri, mazoezi mema mimi nipo hapa kama balozi, na nitahakikisha nitakuwa na nyie mpaka siku mtakapoenda kucheza mpira,” alisema,

Lupembe aliitembelea Azam FC jioni wakati ikielekea kwenye mazoezi kujiandaa na mchezo huo.
Mara mwisho Balozi huyo kuishika mkono Azam FC iliichapa Bidvest Wits mabao 3-0 jijini Johannesburg katika mchezo wa raundi kama hii, ambapo kutokana na ushindi wa 1-0 katika mchezo wa kwanza kwa sasa timu hiyo inahitaji ushindi wowote au sare ili iweze kusonga mbele.

Balozi  wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Richard Lupembe akiwa pamoja na wachezaji wa Azam wakati alipoitembelea timu hiyo jana kwenye kambi yake katika Hoteli ya Acardia jijini Pretoria, nchini humo ikijiandaa na mchezo huo wa Kombe la Shirikisho Afrika utakaofanyika Uwanja wa Taifa wa Somhlolo nchini Swaziland Jumapili hii saa 10.30 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.alip
Kocha wa Azam ... akitoa maelekezo kwa wachezaji wake wakati wa mazoezi  ya kujiandaa na mechi ya marudiano dhidi ya Mbabane Swallows siku ya Jumapili.
Beki wa Kulia wa Azam, Shomari Kapombe akiwa anagombania mpira na Kingue wakati wa mazoezi ya timu hiyo  kujiandaa na mechi ya marudiano dhidi ya Mbabane Swallows siku  ya Jumapili.
Kiungo wa timu ya Azam, Frank Domayo (kushoto) akijaribu kumtoka mchezaji mwenzake wakati wa mazoezi ya kujiandaa na mechi ya marudiano dhidi ya Mbabane Swallows siku  ya Jumapili.
Nahodha wa timu ya Azam Himid Mao akijaribu kuutuliza mpira ulipigwa kwake wakati wa kujiandaa na mechi ya marudiano dhidi ya Mbabane Swallows siku ya  Jumapili.
Ramadhani Singano akiwa anapambana na Shomari Kapombe wakati wa mazoezi ya kujiandaa na mechi ya marudiano dhidi ya Mbabane Swallows siku ya Jumapili.
Makipa wa timu ya Azam wakiwa katika mazoezi.
Wachezaji wa Azam wakiwa katika mazoezi ya mwisho ya kuelekea mechi yao ya marudiano dhidi ya Mbabane Swalllows itakayofanyika Jumapili nchini Swaziland.Picha na Abducado Emmanuel.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amekutana na Waziri Mkuu Msumbiji Mbabane- Swaziland

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na kuzungumza na Waziri Mkuu wa Msumbiji Mhe. Carlos Agostinho do Rosario walipokutana na kufanya mazungumzo ya kikazi mjini Mbabane Swaziland leo March 17,2017

VICE CHANCELLOR OF THE OPEN UNIVERSITY OF TANZANIA VISITS UNESCO DAR ES SALAAM OFFICE

$
0
0
On the morning of Friday,17thMarch 2017 Prof. Elifas Tozo Bisanda, the Vice Chancellor of the Open University of Tanzania (OUT) visited the UNESCO Office in Dar es Salaam. Prof. Bisanda, who is also the Chairperson of the UNESCO National Commission of the United Republic of Tanzania, had a meeting with the UNESCO Dar es Salaam Head of Office and Country Representative, Ms. Zulmira Rodrigues followed by a meeting with all office staff. UNESCO Dar es Salaam Head of Office and Country Representative Ms. Zulmira Rodrigues talking during the visit of Prof. Bisanda[/caption] During his meeting with staff members, Prof. Bisanda introduced the Open University of Tanzania, and outlined its history, mission, programs and innovative solutions in education and management introduced by the University. 

These included blended learning (combining online and face-to-face methodologies) and solutions for visually and hearing impaired learners. UNESCO Dar es Salaam Head of Office and Country Representative Ms Zulmira Rodrigues encouraged staff to take advantage of the learning opportunities that the OUT provides. 

The Open University of Tanzania is a long-time partner of UNESCO Dar es Salaam in implementation of education programs and projects in Tanzania, including the ongoing Chinese funded project, “Enhancing Teacher Education for Bridging the Quality Gap in Tanzania”. Prof. Elifas T. Bisanda Vice Chancellor of the Open University of Dar es Salaam and Chairperson of the UNESCO National Commission of the United Republic of Tanzania talking to UNESCO Dar es Salaam staff members.[/caption]

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AKUTANA NA BALOZI WA IRAN

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi wa Iran Nchini, Mhe. Mousa Farhang kabla ya mazungumzo yao, kwenye Makazi yake, Oysterbay jijini Dar es salaam, Machi 17, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu). 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Balozi wa Iran Nchini, Mhe. Mousa Farhang kwenye Makazi yake, Oysterbay jijini Dar es salaam, Machi 17, 2017

RC NDIKILO ,RIDHIWANI, BHARWANI WAUNGA MKONO UJENZI WA MADARASA S/M VIGWAZA

$
0
0
Katibu wa Mbunge Ridhiwani Kikwete, bw. Iddi Swala akizungumza na wakazi wa kijiji cha Vigwaza kuhusu utekelezaji wa mfuko wa jimbo na Ridhiwani alivyosaidia kijiji hicho na kata kijumla. (picha na Mwamvua Mwinyi)

Katibu wa mbunge wa Ridhiwani Kikwete, anaeitwa Iddi Swala akionyesha saruji waliochangia ujenzi wa shule ya msingi Vigwaza. (picha na Mwamvua Mwinyi)



Mifuko 50 ya saruji iliyochangiwa na mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete, na mifuko 50 aliyochangia diwani wa kata ya Vigwaza Mohsin Bharwani kwa ajili ya ujenzi wa madarasa sita shule ya msingi Vigwaza. (Picha na Mwamvua Mwinyi)

………………………………………………………………

Na Mwamvua Mwinyi,Vigwaza

WAKAZI wa kijiji cha Vigwaza,Kata ya Vigwaza,jimbo la Chalinze,wameanza kuchangia matofali matano kila mmoja na kujitolea nguvu kazi ili kujenga vyumba vitano vya madarasa na chumba kimoja cha chekechea katika shule ya msingi Vigwaza.

Mwenyekiti wa kijiji hicho, Ramadhani Kirumbi, alisema serikali ya kijiji imekubaliana na wananchi kuongeza majengo shuleni hapo.

Kutokana na juhudi hizo, mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo, alieleza anatambua jitihada za wananchi hivyo atawaunga mkono kwa kuchangia sh. Mil mbili.

Mhandisi Ndikilo, alisema jamii ishirikiane na serikali kwa kutatua changamoto za kijamii hasa elimu ili kuwajengea mazingira bora wanafunzi.

“Tulijikita kwenye kuondoa matatizo ya uhaba wa madawati lakini kwasasa haina budi tujiongeze kumaliza changamoto ya majengo na madarasa “alibainisha .

Nae mbunge wa jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete, alichangia mifuko ya saruji 50 na mabati 50 yenye thamani ya mil. 1.9 .

Katibu wa mbunge huyo Iddi Swala,alisema Ridhiwani amechangia pia zahanati ya kijiji kipya cha Mnindi mifuko 50,ukarabati nyumba ya mwalimu shule ya msingi Mnindi mifuko 30.

Hata hivyo, Ridhiwani alitoa mifuko mingine 30 kwa ajili ya kufanya ukarabati zahanati ya Kitonga.

Katibu Swala, alieleza kwamba, mh mbunge kapeleka mifuko ya saruji mingine 50 katika shule ya msingi Milo na zahanati ya Buyuni ametoa mifuko 30 ya saruji.

“Kati ya fedha za jimbo mil 48 kata ya Vigwaza imechangiwa mil. tano “alisema Swala kwa niaba ya Ridhiwani.

Diwani wa kata Vigwaza,Mohsin Bharwani, alitoa mifuko 50 ya saruji na taasisi ya lions Dar es salaam -Panorama imesaidia mifuko ya saruji 50.

Bharwani alisema kwasasa, katika sekta ya elimu wanajikita kumaliza tatizo la upungufu wa madarasa kwenye shule mbalimbali.

PROF.GABRIEL AMEWATAKA MAAFISA MAWASILIANO SERIKALINI KUJIONGEZEA UWEZO WA KITAALUMA KUTIMIZA MAJUKUMU YAO.

$
0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akizungumza na Maafisa Mawasiliano wakati wa ufungaji wa Kikao kazi kwa Maafisa hao kilichofanyika Mjini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Bibi Nuru Millao akitoa mrejesho wa kikao kazi cha Maafisa Mawasiliano kwa mgeni rasmi wakati wa ufungaji wa hicho kwa Maafisa hao kilichofanyika Mjini Dodoma.
Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO) Dkt. Hassan Abbasi akisisitiza jambo wakati wa ufungaji wa Kikao kazi kwa Maafisa hao kilichofanyika Mjini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akitoa vyeti kwa kwa wadhamini kutoka TSN, TTCL, Multichoice Tanzania, TANAPA, SSRA mara baada ya kumalizika kwa kikao kazi cha Maafisa Mawasiliano Serikalini kilichofanyika Mjini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akiwa katika poicha ya pamoja na Maafisa Mawasiliano Serikalini na wadhamini wa kikao hicho mara baada ya kufungwa kwa kikao kilichofanyika Mjini Dodoma.
Baadhi ya Maafisa Mawasiliano Serikalini wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel( Hayupo Pichani) wakati wa ufungaji wa kikaokazi cha mafia hao kilichofanyika Mjini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akiwa katika poicha ya pamoja na Maafisa Mawasiliano Serikalini na wadhamini wa kikao hicho mara baada ya kufungwa kwa kikao kilichofanyika Mjini Dodoma.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI MACHI 18,2017

MASHA ATENGUA USHIRIKI WAKE TLS,AAMUA KUMUUNGA MKONO MGOMBEA MWENZAKE TUNDU LISSU

$
0
0
Mgombea wa kiti cha urais  wa Chama cha wanasheria Tanganyika(TLS) Lawrence Masha ametengua uamuzi wake kwa kusema   kuwa  ameamua kuumuunga mkono mgombea mwenzake Tundu Lissu.

Maamuzi hayo ameyafanya wakati alipokaribishwa ili kujinadi mbele ya wapiga kura wake  katika mkutano mkuu wa Tls  unaoendelea katika kituo cha mkutano cha kimataifa Aicc Jijini Arusha Leo.

Aidha mwenyekiti wa uchaguzi amesema kuwa Kwa kuwa Lawrence Masha siyo mgombea tena haruhusiwi kuulizwa maswali tena.Uchaguzi utafanyika kesho siku ya jumamosi saa kumi na mbili asubuhi hadi saa tatu endelea kukaa karibu na sisi tutakuhabarisha kila kinachoendelea kutokea Arusha. 
Pichani ni  Lawrance Masha Akiwa anamnadi Mgombea mweza Mh: Tundu lisu.Picha na Imma msumba
Mgombea wa Urais wa Tls Mh: Victoria Mandari Pichani akiwa anajinadi na kuomba kura kwa wapiga kura wake.
Pichani ni Mke wa Mh: Tundu Lisu Akiwa anachangia mada kwenye Mkutano wa Tls Arusha .
Kutoka kulia ni Mh: Tundu lisu akiwa anateta jambo na wakili msomi Kibatala.
Pichani ni wakili John Malya Akiwa anafuatilia kwa makini sera za mgombea wa urais wa Tls Tundu Lisu. 
Baadhi ya wadau wa Sheria wakifuatilia kwa umakini mkutano wa Tls uliofanyika leo Jijini Arusha .Picha na Imma msumba


KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII YAIPONGEZA TASUBA.

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akimkaribisha Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Peter Serukamba (kulia) pamoja na Wajumbe wengine mara baada ya kuwasili katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) kwa ajili ya kukagua mradi wa ukarabati wa taasisi hiyo, 17 Machi, 2017. 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akiwa ameongozana na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Peter Serukamba pamoja na Wajumbe wengine mara baada ya kuwasili katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) kwa ajili ya kukagua mradi wa ukarabati wa taasisi hiyo, 17 Machi, 2017. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA), Dkt. Helbert Makoye akiwaeleza jambo Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, mara baada ya kuwasili katika taasisi hiyo kwa ajili ya kukagua mradi wa ukarabati wa taasisi hiyo, 17 Machi, 2017. 
Mkuu wa Kitengo cha Muziki wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) Bi.Rhoda Mitanda (kushoto) akiwaeleza Wajumbe wa Kamati ya Kudumua ya Bunge ya Huduma na Maendeleo kuhusu namna vifaa mbalimbali vya muziki na kazi zake mara walipowasili katika Taasisi hiyo kwa ajili ya kukagua mradi wa ukarabati wa taasisi hiyo, 17 Machi, 2017. 
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, wakionyeshwa vifaa vitumikavyokatika uhariri wa kazi za sanaa walipoingia katika moja ya Studio ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) kujionea utendaji kazi wa taasisi hiyo, 17 Machi, 2017. 
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Peter Serukamba akiongea na Wafanyakazi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) mara baada ya kuwasili katika Taasisi hiyo kwa ajili ya kukagua mradi wa ukarabati wa taasisi hiyo, 17 Machi, 2017. 
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii pamoja na Wafanyakazi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) wakijadiliana wakati wa kikao 17 Machi, 2017. 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akiongea na Wafanyakazi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) wakati wa kikao cha kukagua mradi wa ukarabati wa taasisi hiyo, 17 Machi, 2017. 




Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii wakitoa maoni yao wakati wa kikao cha kujadili na kukagua mradi wa ukarabati wa taasisi hiyo, 17 Machi, 2017. 
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii pamoja na Wafanyakazi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) wakisikiliza maoni mbalimbali yaliyolenga kuiboresha taasisi hiyo wakati wa kikao cha kujadili na kukagua mradi wa ukarabati wa taasisi hiyo, 17 Machi, 2017. 
Wanafunzi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) wakionyesha umahiri wao katika sanaa mbalimbali mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii baada ya kumalizika kikao kilicholenga kukagua mradi wa ukarabati wa taasisi hiyo, 17 Machi, 2017. 
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii wakiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi pamoja na Wanafunzi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) mara baada ya kumalizika kwa ziara iliyolenga kufanya ukaguzi wa mradi wa ukarabati wa taasisi hiyo, 17 Machi, 2017. 


(Picha/Habari na Benedict Liwenga-WHUSM)


KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii imeipongeza Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) kwa juhudi zake inazozifanya katika kuibua na kukuza vipaji vya Vijana nchini.

Pongeza hizo zimetolewa leo Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani na Wajumbe wa Kamati hiyo wakati walipoitembelea taasisi hiyo kwa ajili ya kukagua mradi wa ukarabati wa taasisi hiyo.

Akiongea wakati wa kikao na Watendaji wa Taasisi hiyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Peter Serukamba amesema kwamba, suala la muziki, filamu na utamaduni ni suala la kipaji, hivyo halihitaji elimu kubwa kwa vijana, bali kuwepo na mazingira mazuri yatakayowezesha wenye vipaji na wasio na vipaji waweze kupata fursa ya kujifunza na kuonyesha vipaji vyao.

Mhe. Serukamba amelishauri Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) kuweka mazuri ambayo hayatawabana vijana ambao hawakupata fursa ya elimu lakini wana vipaji, hivyo ameshauri vijana nchini wapewe fursa ya kujifunza na vipaji vyao viendelee kuibuliwa.

Sambamba na hilo, Mhe. Serukamba ameishauri taasisi hiyo kutoa elimu ya lugha mbalimbali kama vile lugha za Kiingereza, Kiswahili, Kifaransa, Kijerumani, Kichina na nyinginezo ili ziweze kuwasaidia vijana hao wawapo nje ya nchi na pindi wanapokuwa wameiva katika masomo yao ndani ya chuo hicho.

“Chuo hiki naomba kione namna ya kufundisha lugha pamoja kwamba mnafundisha muziki, basi vema mkawafundisha vijana wetu lugha mbalimbali ili waweze kwenda Duniani, kwasababu kama watakuwa na tatizo la lugha itawapa shida”, alisema Serukamba.

Kuhusu suala la bajeti katika taasisi hiyo, ameshauri kwamba, Uongozi wa taasisi hiyo haunabudi kujitangaza ili waweze kupata fedha za kutosha badala ya kulalamika kwamba hawana fedha.

“Lazima Mkuu wa Chuo uende mbali zaidi kwasababu vitu mnavyofundisha hapa katika taasisi yenu ni vya kipekee, havifundishwi kwingine, hivyo una fursa kubwa ya kujitangaza na kuweza kupata fedha za kukisaidia chuo hiki, kwa mfano unaweza kuwatafuta watu toka sekta binafsi ambao hawa wataweza kukusaidia kama vile makampuni mbalimbali hapa nchini”, aliongeza Serukamba. 

Kwa upande wake Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye amesema kwamba, moja ya changamoto kubwa ambayo imekuwa ikiikabili taasisi hiyo ni mmomonyoko wa kingo za mpaka wa taasisi hiyo ambao umesababishwa na bahari kusogelea eneo la taasisi hiyo hali ambayo inahatarisha majengo yake, hivyo amefafanua kuwa tayari Wizara iliwasiliana na Ofisi ya Makamu wa Rais upande wa Mazingira ambao wao tayari walifika na kupima athari za mmonyoko huo.

Ameongeza kuwa, kwa hivi sasa kinachosubiriwa ni fedha ambazo zitatumika kuanza ujenzi wa kingo ambayo itasaidia kuepusha mmomonyoko huo unaofanywa na maji ya bahari.

“Hili eneo la taasisi ya TaSUBA watu wa NEMC walishafika na kupima na tunategemea katika mwaka ujao wa fedha, fedha itapatikana ili kuanza ujenzi wa kingo katika eneo hili ili tuweze kuzuia maji ya bahari kuendelea kuharibu eneo la taasisi hii”, alisema Mhe. Nnauye.

Kuhusu suala la elimu itolewayo katika taasisi hiyo, amesema kwamba anakubaliana na mapendekezo ya Kamati kwamba, vijana wapewe fursa ya kufundishwa kwa kuangalia vipaji vyao na isiwe lazima sana kuangalia elimu waliyonayo kwani wako vijana wengi ambao wana vipaji lakini hawakupata fursa ya kuelimika, lakini pia na wale walioelimika wanayo nafasi ya kujifunza ndani ya chuo hiko.

Awali akitoa taarifa ya taasisi hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, Dkt. Helbert Makoye amesema kwamba, taasisi anayoiongoza ni taasisi iliyotukuka na inafundisha masuala mbalimbali ya Sanaa, inakuza viwango vya Sanaa, inakuza matumizi ya Sanaa kama vile maonyesho mbalimbali yenye kutoa elimu kwa jamii.

“Hapa chuoni pia tunafundisha watendaji kwenye masuala ya Sanaa lakini pia Wasimamizi, tunawandaa Watafiti na Washauri wa Sanaa na utamaduni kwa ngazi ya Taifa na Kimataifa”, alisema Dkt. Makoye.

MAKAMU WA RAIS MAMA SAMIA AHUDHURIA MKUTANO WA ASASI YA SIASA ULINZI NA USALAMA SADC

$
0
0
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, usiku huu anahudhuria Mkutano wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama unaojulikana kama SADC Double Troika, mjini Mbabane Swaziland. Mkutano ambao unajadili kwa kina hali tete ya usalama katika Nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo( DRC) na Nchi ya Lesotho, ambapo Tanzania ni Mwenyekiti wa Asasi hiyo.

(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

DK.SHEIN AZUNGUMZA NA WANA CCM PEMBA

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCm Zanzibar Dk.Ali Mohamed Sheuin (katikati) akimkabidhi Mwakilishi wa Jimbo la Mkoani Pemba CCM pia Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Mhe,Mmanga Mjengo Mjawiri (kulia) vifaa vya Michezo kwa niaba ya Jimbo lake vitakavyotumika katika mashindano ya mpira wa miguu kwa majimbo 18 ya Pemba,chini ya ufadhili wa Mfanya bishara na Kada wa CCM Mohamed Raza Daramsi (kushoto) hafla iliyofanyika ukumbi wa Fidel Castro leo.
Miongoni mwa Vijana wa CCM wa Majimbo 18 ya mikoa ya Pemba CCM wakiwa katika sherehe za kubabidhiwa vifaa vya Michezo vya Mpira wa Miguu vitakavyofanikisha mashindano ya Majimbo hayo,vilivyotolewa na Mfanya bishara na Kada wa CCM Mohamed Raza Daramsi na kukabidhiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCm Zanzibar Dk.Ali Mohamed Sheuin (hayupo pichani) katika ukumbi wa Fidel Castro wilaya ya Chake chake Pemba leo
Miongoni mwa Vijana wa CCM wa Majimbo 18 ya mikoa ya Pemba CCM wakiwa katika sherehe za kubabidhiwa vifaa vya Michezo vya Mpira wa Miguu vitakavyofanikisha mashindano ya Majimbo hayo,vilivyotolewa na Mfanya bishara na Kada wa CCM Mohamed Raza Daramsi na kukabidhiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCm Zanzibar Dk.Ali Mohamed Sheuin (hayupo pichani) katika ukumbi wa Fidel Castro wilaya ya Chake chake Pemba leo,
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Sheuin (katikati) akimkabidhi Mwakilishi wa Jimbo la Ziwani Suleiman Makame Ali (kulia) vifaa vya Michezo kwa niaba ya Jimbo lake vitakavyotumika katika mashindano ya mpira wa miguu kwa majimbo 18 ya Pemba,chini ya ufadhili wa Mfanya bishara na Kada wa CCM Mohamed Raza Daramsi (kushoto) hafla iliyofanyika ukumbi wa Fidel Castro leo,
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCm Zanzibar Dk.Ali Mohamed Sheuin akizungumza na Viongozi wa CCM na Vijana UVCCM wa Majimbo 18 ya Mikoa ya Pemba katika hafla ya kukabidhi vifaa vya Michezo vilivyotolewa na Mfanyabishara na Kada wa CCM,pia Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Unguja, Mohamed Raza Daramsi, hafla iliyofanyika ukumbi wa Fidel Castro leo,
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCm Zanzibar Dk.Ali Mohamed Sheuin akipiokea Kombe la Mashindano ya Mpira wa miguu katika Timu mbali mbali za majimbo 18 ya Mikoa ya Pemba,kutoka kwa Mwanamichezo, Mfanyabishara na Kada wa CCM,pia Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Unguja, Mohamed Raza Daramsi,(kushoto) katika hafla ya kukabidhi vifaa vya Michezo vilivyotolewa na Raza katika hafla iliyofanyika ukumbi wa Fidel Castro leo,

[Picha na Ikulu.]

WAMILIKI WA HOTELI MKOANI MBEYA WAASWA KUAJILI WAHUDUMU WENYE SIFA

$
0
0
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Constantine Mushi akiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kufunga mafunzo ya jumla ya wahitimu 74 waliopewa mafunzo ya siku tatu katika maeneo ya mapokezi, utoaji huduma ya chakula na vinywaji pamoja na upishi katika fani ya Utalii na Ukarimu. Mafunzo hayo yaliandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii na SPANEST Mkoani Mbeya, lengo likiwa ni kuongeza ubora wa huduma zinazotolewa katika sekta hiyo ili kukidhi mahitaji ya soko, pamoja na kukuza hadhi ya huduma za malazi zilizopo chini ya kiwango. Wengine ni Mratibu wa Mradi wa SPANEST nchini, Godwell Meing’ataki (kushoto) Mkurugenzi Msaidizi wa idara ya Utalii, Paskas Mwiru (kulia)
Baadhi ya wahitimu waliohitimu jana mafunzo katika maeneo ya mapokezi, utoaji huduma ya chakula na vinywaji pamoja na upishi katika fani ya Utalii na Ukarimu yaliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii na SPANEST yaliyofanyika Mkoani Mbeya kwa muda wa siku tatu na kuhudhuriwa na jumla ya washiriki 74.

Mkufunzi kutoka Chuo cha Taifa cha Utalii,Jesca William akiwaonesha baadhi ya video zinazotumika katika kutoa mafunzo ya mapokezi, utoaji huduma ya chakula na vinywaji pamoja na upishi katika fani ya Utalii na Ukarimu yaliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii na SPANEST yaliyofanyika Mkoani Mbeya kwa muda wa siku tatu.
Mmoja wa Wahitimu wa mafunzo katika maeneo ya mapokezi, utoaji huduma ya chakula na vinywaji pamoja na upishi katika fani ya Utalii na Ukarimu, Lyimo Leb akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi kabla ya mafunzo hayo kufungwa.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Constantine Mushi akizungumza na wahitimu kabla ya kufunga jana mafunzo hayo fani ya Utalii na Ukarimu yaliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii na SPANEST yaliyofanyika Mkoani Mbeya kwa muda wa siku tatu na kuhudhuriwa na jumla ya wahitimu 74. Wengine ni Mratibu wa Mradi wa SPANEST nchini, Godwell Meing’ataki (kushoto) Mkurugenzi Msaidizi wa idara ya Utalii, Paskaz Mwiru (kulia)

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Constantine Mushi akikabidhi cheti kwa Mwenyekiti wa wenye hoteli katika mkoa wa Mbeya, Jeremiah Mchange cha ushiriki wa mafunzo katika maeneo ya mapokezi, utoaji huduma ya chakula na vinywaji pamoja na upishi
Mratibu wa Mradi wa SPANEST nchini, Godwell Meing’ataki akizungumza na wahitimu waliohitimu jana mafunzo katika maeneo ya mapokezi, utoaji huduma ya chakula na vinywaji pamoja na upishi katika fani ya Utalii na Ukarimu yaliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii na SPANEST yaliyofanyika Mkoani Mbeya kwa muda wa siku tatu na kuhudhuriwa na jumla ya washiriki 74.
Mkurugenzi Msaidizi wa idara ya Utalii, Paskaz Mwiru akizungumza na wahitimu kabla ya kufungwa mafunzo hayo jana katika maeneo ya mapokezi, utoaji huduma ya chakula na vinywaji pamoja na upishi katika fani ya Utalii na Ukarimu yaliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii na SPANEST yaliyofanyika Mkoani Mbeya kwa muda wa siku tatu na kuhudhuriwa na jumla ya washiriki 74. (Picha na Lusungu Helela- WMU)

…………………..

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Constantine Mushi amewataka wamiliki wa hoteli kuajiri wafanyakazi wenye ujuzi katika fani ya ukarimu na utalii baadala ya kuajiri ndugu zao wasio na ujuzi wowote na kuwalipa ujira mdogo hali inayochangia kuzorotesha huduma za utalii mkoani hapo.

Alisema wahudumu walio wengi katika hoteli hizo wamekuwa kero katika utoaji wa huduma kwa watalii pindi wanapotembelea kuja kuona vivutio vya utalii vilivyopo mkoani hapo.

Ametoa raia hiyo jana wakati akifunga mafunzo hayo kwa jumla ya wahitimu 74 yaliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kupitia mradi wa SPANEST unaotekelezwa na Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA).

Amesema mafunzo hayo yamefanyika kwa muda wa siku tatu kwa lengo la kuongeza ubora wa huduma zinazotolewa katika sekta ya ukarimu na utalii ili kukidhi mahitaji ya soko, pamoja na kukuza hadhi ya huduma za malazi zilizopo chini ya kiwango kwa mikoa ya Nyanda za juu kusini.

Amesema Wahitimu hao wamepewa mafunzo katika maeneo ya mapokezi, utoaji huduma ya chakula na vinywaji pamoja na upishi kwa ufadhili wa asilimia 75 uliofanywa kupitia mradi wa SPANEST

Aidha, Mushi alisema kwa kutambua umuhimu wa sekta ya utalii tayari umejipanga katika kuboresha sekta ya utalii ambapo kwa mkoa wa Mbeya imeshaandaa Mpango Mkakati wa kuendeleza utalii .

Kwa upande wa Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utalii, Paskas Mwiru amesema mafunzo hayo yatakuwa endelevu kwa wahudumu na pamoja na wamiliki wa hoteli ili waweze kutambua umuhimu wa wafanyakazi wao.

Naye, Mratibu wa Mradi wa SPANEST, Godwell Mengiaediek amewataka wahudumu wa hoteli waunde chama chao ambacho kitawasaidia katika kupaza sauti zao.

KIKAO CHA UPITIAJI/UHAKIKI WA MIPANGO KABAMBE YA AFYA YA MWAKA 2017/18 CHAFANYIKA MJINI DODOMA

$
0
0
 Naibu Katibu Mkuu  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya , Dkt Zainabu Chaula akizungumza na  baadhi ya wajumbe wa timu za uendeshaji wa huduma za afya,waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na waganga wafawidhi wa Hospitali za Rufaa na Mikoa nchini juu ya Upitiaji/Uhakiki wa Mipango Kabambe ya Afya ya mwaka 2017/18 kwa kuhusisha ngazi za Mikoa, Halmashauri na Wizara ,Mjini Dodoma. 
 Naibu Katibu Mkuu  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya , Dkt Zainabu Chaula akiwaonyesha  Ilani ya Uchaguzi baadhi ya wajumbe wa timu za uendeshaji wa huduma za afya,waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na waganga wafawidhi wa Hospitali za Rufaa na Mikoa nchini juu ya Upitiaji/Uhakiki wa Mipango Kabambe ya Afya ya mwaka 2017/18 kwa kuhusisha ngazi za Mikoa, Halmashauri na Wizara ,Mjini Dodoma. 
 Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya, Dkt Zainabu Chaula akizungumza na  baadhi ya wajumbe wa timu za uendeshaji wa huduma za afya,waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na waganga wafawidhi wa Hospitali za Rufaa na Mikoa nchini juu ya Upitiaji/Uhakiki wa Mipango Kabambe ya Afya ya mwaka 2017/18 kwa kuhusisha ngazi za Mikoa, Halmashauri na Wizara ,Mjini Dodoma.
 Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Huduma za Afya   Idara ya Afya Ustawi wa Jamii na Lishe Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OR-TAMISEMI), Dkt Anna Nswira  akizungumza na  baadhi ya wajumbe wa timu za uendeshaji wa huduma za afya,waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na waganga wafawidhi wa Hospitali za Rufaa na Mikoa nchini juu ya Upitiaji/Uhakiki wa Mipango Kabambe ya Afya ya mwaka 2017/18 kwa kuhusisha ngazi za Mikoa, Halmashauri na Wizara ,Mjini Dodoma.
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Wizara ya Afya ,Dkt Doroth Gwajima  akizungumza na  baadhi ya wajumbe wa timu za uendeshaji wa huduma za afya,waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na waganga wafawidhi wa Hospitali za Rufaa na Mikoa nchini juu ya Upitiaji/Uhakiki wa Mipango kabambe ya Afya ya mwaka 2017/18 kwa kuhusisha ngazi za Mikoa, Halmashauri na Wizara ,Mjini Dodoma.

HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI NAPE NNAUYE KWENYE KIKAO KAZI CHA MAAFISA HABARI MKOANI DODOMA

LAPF WATOA REFLECTOR JACKET 500 KUSAIDIA BODA BODA WILAYANI KISARAWE MKOANI PWANI

$
0
0
 Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF, James Mlowe (wa pili kulia), akimkabidhi moja ya jaketi angavu (Reflector Jacket) kati ya majaketi 500 Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Happyness Seneda katika hafla iliyofanyika wilayani humo jana. LAPF imetoa majaketi hayo kwa ajili ya kusaidia waendesha bodaboda ili waweze kutambulika wakiwa katika shughuli zao za kila siku.Kutoka kushoto ni Meneja wa Mfumo wa Uchangiaji wa Hiari wa LAPF, Hanim Babiker, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, William Gama na Meneja wa LAPF, Kanda ya Mashariki,  Lulyalya Sayi. 
 Waendesha boda boda wa Wilaya ya Kisarawe wakiwa kwenye mkutano huo.
  Waendesha boda boda wa Wilaya ya Kisarawe wakiwa kwenye mkutano huo.
  Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF, James Mlowe, akionesha moja ya jacket katika mkutano huo. Kushoto ni Diwani wa Kata ya Kisarawe, Abel Mudo na kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri wa wilaya hiyo, Khamis Dikupatile.
 Waendesha bodaboda, Edward Akwilini (ukushoto) na Jackson Clavery wakijadiliana jambo kwenye mkutano huo.
 Mkutano ukiendelea.
 Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF, James Mlowe (kulia), akisisitiza jambo kwenye mkutano huo.
 Meneja wa Mfumo wa Uchangiaji wa Hiari wa LAPF, Hanim Babiker, akitoa ufafanuzi wa mambo kadhaa kuhusu mfuko huo.
 Mwendesha bodaboda,  Jackson Clavery akiuliza swali 
kwenye mkutano huo.
 Meneja wa LAPF, Kanda ya Mashariki,  Lulyalya Sayi, akichangia jambo kwenye mkutano huo.
 Pikipiki za waendesha bodaboda zikiwa zimeegeshwa nje 
wakati wa mkutano huo.
 Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Happyness Seneda (katikati), akitoa shukurani baada ya kupokea msaada huo.
 Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Happyness William Seneda, akijaza fomu wakati akijiunga kwa hiari na mfuko wa LAPF. Kushoto ni   Meneja wa Mfumo wa Uchangiaji wa Hiari wa LAPF, Hanim Babiker.

 Muonekano wa jengo la mikutano la Halmashauri ya 
Wilaya ya Kisarawe.
Na Dotto Mwaibale

MFUKO wa Pensheni wa LAPF umetoa jaketi angavu (Reflector Jacket) 500 kwa ajili ya kuwasaidia vijana waendesha 
bodaboda wa Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo kwa Mkuu wa Wilaya hiyo, Happyness Seneda, katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri hiyo ya Wilaya ya Kisarawe jana,  Meneja Masoko na Mawasiliano wa mfuko huo, James Mlowe alisema wametoa msaada huo baada ya kuombwa na mkuu wa wilaya hiyo pia ni moja ya kazi yao ya kusaidia jamii.

"Tumetoa msaada huu baada ya kuombwa na mkuu wa wilaya lakini pia ni moja ya shughuli za jamii zinazofanywa na mfuko 
huu kwa wanachama wake" alisema Mlowe.

Kabla ya kukabidhi msaada huo Mlowe alieleza shughuli mbalimbali zinazofanywa na mfuko huo na namna ya kujiunga nao na katika hatua nyingine aliwataka waendesha bodaboda hao kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha wanazozipata katika shughuli hiyo ili akiba watakayoweka iweze kuwasaidia siku za usoni.

Mlowe alitumia fursa hiyo kuwaambia waendesha bodaboda hao kujiunga na mpango wa hiari wa kuweka akiba ya fedha 
zao katika mfuko huo wa LAPF ambao unamanufaa makubwa.

Mkuu wa wilaya hiyo Seneda aliwaambia bodaboda hao kuwa serikali itaendelea kushirikiana nao na kuwaomba kudumisha 
hali ya usalama wilayani humo.

"Jaketi hizi mlizokabidhiwa leo hii zitasaidia kuwatambueni hivyo kuwa rahisi kumtambua mhalifu na kila mmoja wenu 
atasajiliwa kulingana na namba iliyoandikwa katika jaketi lake" alisema Seneda.

Alisema mpango wa vijana kujiunga katika vikundi imesaidia kuwezeshwa kupitia mfuko wa maendeleo wa wilaya hiyo ingawa 
alisema muitikio wa vijana wa kiume ni mdogo ukilinganisha na wanawake.

Seneda aliwataka waendesha bodaboda hao kubuni miradi mingine kama kilimo na ufugaji ili kuinua vipato vyao badala ya 

kutegemea kazi hiyo pekee.


WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AONDOKA NCHINI KWENDA MOURITIUS KUMWAKILISHA JPM KATIKA UZINDUZI WA JUKWAA LA UCHUMI LA AFRIKA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda kwenye uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam kabla ya kuondoka nchini kwenda Port Louis, Mauritius kumwakilisha Rais John Magufuli katika Uzinduzi wa  Jukwaa la Uchumi la Afrika (The Inaugural  Session of The African Economic Platform) , Machi 18, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MAKAMU WA RAIS AHUDHURIA MKUTANO WA DHARURA WA WAKUU NCHI NA SERIKALI WA JUMUIYA YA SADC.

$
0
0


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo March 18,2017 amehudhuria mkutano wa dharura wa  Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya maendeleo ya kusini mwa Afrika SADC akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, mkutano huo umefunguliwa na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mfalme Mswati wa III wa Swaziland mjini Mbabane Swaziland ambapo amezitaka Nchi wanachama wa SADC kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa maendeleo ya Jumuiya hiyo kama hatua ya kuwakwamua wananchi na umasikini

Hotuba ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari wakati wa ufungaji wa Kikao kazi cha Maafisa Mawasiliano.

AJALI YA GARI YATOKEA KIMARA SUKA JIJINI DAR ES SALAAM, WAMSHAMBULIA MWANDISHI ALIYEKUWA AKICHUKUA PICHA ZA TUKIO

$
0
0
Gari aina ya Mark II Grand yenye namba za usajili T145AMZ likiwa limeivaa daladala lenye namba za usajili T992DGZ lililokuwa limepaki kituoni KIMARA -SUKA jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwa wapo eneo la tukio ilionyesha dereva wa gari hilo dogo alikuwa amelewa na ndipo aliposhindwa kukamata breki na kujikuta uvunguni kwa daladala hilo.
Vijana wakijaribu kuiba katika gari ndogo iliyokuwa imepata ajali eneo la Kimara Suka jijini Dar es Salaam.
Vijana ambao walivamia gari ndogo na kuanza kuiba wakishangaa kuona kamera ya Kajunason Blog imetinga eneo hilo na ndipo walipoungana na mwenye gari kumfanyia fujo na kumpiga kwa kumshambulia mwandishi wa habari Cathbert Angelo Kajuna aliyekuwa eneo la tukio. 

Kwa msaada wa wasamalia wema waliweza kumnasua mwandishi huyo na kumshika kijana aliyekuwa mmiliki wa gari ndogo ambaye ndiye alitoa amri ya kumshambulia mwandishi wa habari.

 Kijana aliyemshambulia mwandishi wa habari Cathbert Angelo Kajuna amekamatwa na kufunguliwa jarada la KMR/RB/3987/2017 na mpaka sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi kituo cha Mbezi kwa Yusuph.

DK. AYUB RIOBA AWANOA KWA SEMINA YA WELEDI WAANDISHI WA HABARI WA GAZETI LA UHURU, JIJINI DAR ES SALAAM, LEO

$
0
0
 Mwandishi wa habari nguli wa siku nyingi,Dk. Ayub Ryoba, akiendesha semina ya kunoa weledi wa taaluma ya uandishi wa habari kwa waandishi wa habari na baadhi ya watumishi wa Kampuni ya Uhuru Publications Ltd, Wachapishaji wa Magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani, leo katika Ukumbi wa Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam. Dk. Ryoba ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), ana shahada ya Udaktari wa Falsafa (PhD) katika Sayansi ya Jamii aliyoipata katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 Mwandishi wa habari nguli wa siku nyingi,Dk. Ayub Ryoba, akiendelea kutoa 'nondoz' kwa wafanyakazi hao wa UPL, huku wafanyakazi hao wakimsikiliza kwa makini sana
 Mwandishi wa habari nguli wa siku nyingi,Dk. Ayub Ryoba, akifafanua mada zake kwenye semina hiyo ya kunoa weledi wa kitaaluma
 Washiriki wa semina hiyo wakiwa ukumbini
 Dk. Ayub Ryoba, akiendelea kutoa mada kwenye semina hiyo
 Washiriki wakifuatilia kwa makini mafunzo ya Dk. Ryoba
 Yassin Kayombo (aliyesimama) akijitambulisha kwa Ryoba (kulia) na kwa washiriki wengie wa semina hiyo
 Mgaga akijitambulisha
 Jongo akijitambulisha
 Mnkondo akijitambulisha
 Ally akijitambulisha
 Furaha Omari akijitambulisha 
 Gailanga akijitambulisha
 Utambulisho ukiedelea
 Utambulisho ukiendelea
 Washiriki wakiwa ukumbini
 Dk. Ryoba akiendelea na semina hiyo
 Washiriki wakiwa katika kundi la kwanza kujadili mada
 Washiriki katika kundi la pili kujadili mada
 Washiriki katika kundi la tatu kujadili mada
 Washiriki kundi la nne wakijadili mada
 Dk Ryoba akipitiapitia mada zake wakati akisubiri mrejesho wa maswali aliyowapa washiriki 
 Dk. Ryoba akijadiliana jambo na baadhi ya washiriki wa semina hiyo wakati wa mapumziko. Kulia ni Furaha Omar na Bashir Nkoromo
 Dk. Ryoba akijadiliana jambo na baadhi ya washiriki wa semina hiyo wakati wa mapumziko. Kulia ni Furaha Omar na Bashir Nkoromo
(PICHA ZOTE NA KAMERA YA BASHIR NKOROMO)
Viewing all 46340 articles
Browse latest View live




Latest Images