Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46329 articles
Browse latest View live

DC SHINYANGA AFUNGUA MAFUNZO USAJILI WA WATOTO CHINI YA MIAKA MITANO KUPATA VYETI VYA KUZALIWA

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro leo Jumatano Machi 15,2017 amefungua mafunzo ya siku tatu kuhusu usajili wa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga. 

Mafunzo hayo yanahudhuriwa na maafisa watendaji wa kata 26 pamoja na wasaidizi wao na watoa huduma katika vituo vya afya na zanahati zilizopo katika halmashauri hiyo. 

Mafunzo hayo yameandaliwa na Wakala wa Usajili wa Vizazi na Vifo nchini RITA kwa ufadhili wa shirika la watoto la UNICEF. 

Akizungumza wakati wa kufungua semina hiyo Matiro alisema kuanzia sasa vyeti vya kuzaliwa vya watoto vitatolewa katika ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri badala ya ofisi ya mkuu wa wilaya ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma hiyo. 

“Zoezi la kusajili watoto sasa linakabidhiwa kwenye ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri na taarifa za watoto zitaanza kuchukuliwa katika ofisi za kata na vituo vya afya na zahanati ambapo maafisa watendaji na watoa huduma watawajibika kuwatafuta watoto walio chini ya miaka mitano ili wapatiwe vyeti vya kuzaliwa bure”,alieleza Matiro. 

Mkuu huyo wa wilaya alisema zoezi la kutoa huduma ya usajili kuanzia ngazi ya kata litapunguza msongamano katika ofisi ya mkuu wa wilaya ambapo wananchi walikuwa wanatumia muda mwingi na kusafiri umbali mrefu kutoka vijijini kutafuta huduma ya kusajili watoto wao. 

Naye Ofisa usajili kutoka makao makuu (Rita ) Emiliana Mmbando alisema zoezi la kusajili limeanza kufanyika katika mkoa wa Shinyanga na Geita na kuongeza kuwa changamoto iliyopo ni wazazi wengi kutokuwa na uelewa kuhusu vyeti na wengi wakilalamikia umbali wa kufuatilia vyeti hivyo. 
Alisema zoezi la kusajili watoto litaanza rasmi tarehe 21,mwezi Machi mwaka 2017. 
kuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza katika semina kuhusu usajili wa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano katika ukumbi wa vijana Center uliopo katika kanisa la Mama Mwenye Huruma Ngokolo Mjini Shinyanga leo Jumatano Machi 15,2017-Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog 
Washiriki wa semina hiyo wakiwemo maafisa watendaji wa kata na watoa huduma za afya katika vituo vya afya na zahanati katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza ukumbini ambapo mbali na kuwahamasisha kuandikisha watoto pia aliwataka maafisa watendaji wa kata kuhakikisha kuwa watoto wote wanaotakiwa kuandikishwa shuleni waandikishwe 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na washiriki wa semina hiyo 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza ukumbini.Kulia ni Afisa Maendeleo halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Daudi Kisangure,kushoto kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Julius Mlongo 
Afisa Maendeleo halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Daudi Kisangure akizungumza wakati wa semina hiyo ambapo alisema 
Wawezeshaji wakiwa ukumbini 
Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Julius Mlongo 
Afisa wa usajili kutoka RITA ,Emiliana Mmbando akizungumza ukumbini ambapo alisema zoezi la kuandikisha watoto linaloanza Machi 21,2017 litatolewa bure na vyeti vitatolewa bure kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano 
Mwenyekiti wa maafisa watendaji katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Emmanuel Maduhu akizungumza kwenye semina hiyo. 

Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MACHI 16,2017

WALENGWA WA TASAF WILAYANI KILOMBERO WAITIKIA WITO WA SERIKALI WA KUANZISHA VIWANDA VIDOGO VIDOGO KWA FEDHA ZA RUZUKU YA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASIKINI.

$
0
0

NA ESTOM SANGA-TASAF.

Wahenga walinena ‘’mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe’’na ‘’penye nia pana njia’’ni semi zilizoanza kuonekana kwa vitendo miongoni mwa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaotekelezwa na Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF katika halmashauri ya wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro.

Baadhi ya walengwa wa Mpango huo wameanzisha viwanda vidogo vidogo vya kusindika mafuta ya mawese kwa kutumia fedha za ruzuku inayotolewa na Serikali kupitia TASAF.

‘’ Baada ya kupata fedha za TASAF niliamua kununua mbegu za mawese na kisha kuanza kuzisindika kwa lengo la kukamua mafuta ya mawese na hadi sasa nimepiga hatua ya kujivunia’’ ninaishukuru sana serikali na TASAF amesema bi.Coletha Emilliani Nipala mkazi wa eneo la Mbasa katika mji wa Ifakara.

Anasema mbali ya changamoto ya udogo wa mtaji hajakumbana na tatizo la soko kwani mafuta ya mawese yanahitajika kwa kiwango kikubwa kwa matumizi ya walaji na hata kutengenezea sabuni.

Walengwa wengine pia wameweza kuanzisha miradi midogo midogo ya uzalishaji mali ikiwemo ufugaji wa nguruwe, mbuzi kuku, na hata kuanzisha migahawa midogo midogo inayowaongezea kipato na hivyo kuboresha maisha yao.

Walengwa waliotembelewa na Waandishi wa Habari wameeleza kuwa hali zao za maisha zimeboreshwa baada ya kuingizwa katika Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini ikiwa ni pamoja na kuwawezesha watoto wao kuhudhuria masomo ambalo ni mojawapo ya masharti ya Mpango.

Zifuatazo ni picha za baadhi ya Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika maeneo mbalimbali ya wilaya ya Kilombero wakinyesha mafanikio yao.
Bi.Lucia Ngalota (aliyevaa kitambaa kichwani) mkazi wa kijiji cha chita wilaya ya Kilombero akiwaonyesha waandishi makazi yake mpya aliyoijenga baada ya kupata ruzuku kutoka TASAF.
Hii ni nyumba aliyokuwa akiishi bi Lucia kabla ya kuorodheshwa kwenye Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini ambayo imeanza kubomoka.
Mmoja wa Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini B.Stela Samson Samusam- mkazi wa kijiji cha Chita akiwa nje ya nyumba aliyoijengwa kwa fedha za Mpango unaotekelezwa na TASAF.
Mmoja wa Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini B.Stela Samson Samusam- mkazi wa kijiji cha Chita akiwa nje ya nyumba aliyoijengwa kwa fedha za Mpango unaotekelezwa na TASAF.
Mmoja wa walengwa wa TASAF Bi.Mchilo Omary Kibwana mkazi wa kijiji cha mchombe akiwa katika mgahawa wake aliouanzisha kwa fedha za Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini.Picha ya chini ni nyumba aliyoijenga kutokana na faida aliyoipata kupitia mpango huo.
Mmoja wa walengwa wa TASAF Bi.Mchilo Omary Kibwana mkazi wa kijiji cha mchombe akiwa katika mgahawa wake aliouanzisha kwa fedha za Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini.Picha ya chini ni nyumba aliyoijenga kutokana na faida aliyoipata kupitia mpango huo.
Nguruwe wanaofugwa na mmoja wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika eneo la Mbasa wilaya ya Kilombero kama njia mojwapo ya kujiongezea kipato.
Nyumba ya walimu iliyojengwa TASAF kupunguza tatizo la makazikwa walimu katika shule ya msingi Mbasa shule anbayo pia kuna wanafunzi kutoka kaya za walengwa wa mpango wa kunusuru kaya masikini.
Mbali na kutoa ruzuku kwa walengwa, TASAF pia imeendelea kujenga majengo ya shule na nyumba za walimu kama anathibitisha Mkuu wa Shule ya msingi Mbasa katika wilaya ya Kilombero Mwl. Aman Ngowi akihojiwa na waandishi wa habari juu ya ujenzi wa nyumba inayoonekana nyumba yake.
Mmoja wa Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Mbasa wilaya ya Kilombero Bi. Coletha Emilian Nipala (aliyevaa kitambaa chekundu kichwani) akihojiwa na Waandishi wa Habari namna alivyoweza kutumia fedha zaruzuku kutoka TASAF kuanzisha kiwanda kidogo cha kusindika mawese na kujiongezea kipato.Picha ya chini ni mbuzi anaowafuga baada ya kununua kwa ruzuku kutoka TASAF.
Bi. Victoria Johnson Nguge mmoja wa walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya masikini katika kijiji cha Chita akihojiwa na Waandishi wa Habari juu ya mafanikio aliyoyapata tangu aorodheshwe kwenye Mpango ikiwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba.

SERIKALI YA WATU WA CHINA YAKABIDHI MSAADA WA DAWA KWA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR WENYE THAMANI YA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 420

$
0
0
 Balozi mdogo wa China aliepo Zanzibar Xie Xiaowu akimkabidhi Waziri wa Afya Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo msaada wa dawa uliotolewa na Serikali ya China makabidhiano haya yamefanyika Bohari Kuu ya dawa Maruhubi Mjini Zanzibar.
 Waziri wa Afya Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo na Balozi mdogo wa China aliepo Zanzibar  Xie Xiaowu wakisaini hati ya makabidhiano ya dawa zilizotolewa Serikali ya watu wa China.
 Wafanyakazi wa Bohari Kuu ya Dawa Zanzibar na wanafunzi wa fani ya ufamasia wakifuatilia sherehe ya kukabidhiwa dawa zilizofanyika Bohari Kuu ya Maruhubi.

Mkurugenzi wa Bohari Kuu ya Dawa Zanzibar Zahran Ali Hamadi akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu kubore kwa hali ya dawa Zanzibar baada ya Waziri wa Afya Zanzibar kukabidhiwa msaada wa dawa kutoka Serikali ya watu wa China.
Picha na Makame Mshenga-Maelezo.

Wanawake wa Tanga Cement waadhimisha Siku ya Wanawake kwa kufanya mazoezi na kupima afya.

$
0
0

Meneja Rasilimali Watu wa Kampuni ya Saruji Tanga (TCPLC), Diana Malambugi (wa pili kulia), Meneja Mawasiliano na Mahusiano ya Nje wa Kampuni hiyo, Mtanga Noor (kulia), pamoja na baadhi ya wanawawake wafanyakazi wa Kampuni ya Saruji Tanga pamoja na wake wa wafanyakazi, wakishiriki mbio za pole pole kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani zilizoanza eneo la Kange na kumalizikia katika kiwanda cha kampuni hiyo, Pongwe, nje kidogo ya mji wa Tanga juzi.
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dk. Amina Mchalaganya (wa pili kulia), baadhi ya wanawawake wafanyakazi wa Kampuni ya Saruji Tanga pamoja na wake wa wafanyakazi, wakishiriki mbio za pole pole (jogging), kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani zilizoanza eneo la Kange na kumalizikia katika kiwanda cha kampuni hiyo, Pongwe nje kidogo ya mji wa Tanga.
Meneja Rasilimali Watu wa Kampuni ya Saruji Tanga (TCPLC), Diana Malambugi (wa pili kulia), Meneja Mawasiliano na Mahusiano ya Nje wa Kampuni hiyo, Mtanga Noor (kushoto), Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dk. Amina Mchalaganya (wa pili kushoto), pamoja na baadhi ya wanawawake wafanyakazi wa Kampuni ya Saruji Tanga pamoja na wake wa wafanyakazi, wakishiriki mbio za pole pole kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani zilizoanza eneo la Kange na kumalizikia katika kiwanda cha kampuni hiyo, Pongwe, nje kidogo ya mji wa Tanga.
Meneja Mawasiliano na Mahusiano ya Nje wa Tanga Cement, Bi. Mtanga Noor (kulia), akitoa zawadi kwa baadhi ya wanawake waliohudhuria maadhimisho hayo.
Baadhi ya washiriki katika hafla hiyo wakiselebuka mara baada ya kumaliza mbio na tukio la kupima afya zao ambapo wanawake hao walipimwa na kupewa elimu kuhusu ugonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi.
Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa Kampuni ya Saruji Tanga wakipiga picha ya kumbukumbu katika hafla hiyo.
Baadhi ya washiriki wakifanya vitu vyao katika sherehe za maadhinisho ya Siku ya Wanawake Dunia ambayo kwa mwaka 2017 Kampuni ya Tanga Cement waliadhimisha kwa kufanya mazoezi, kupima afya na kupata mafundisho kuhusu masuala ya ujasiriamali.

KITUO CHA EATV NA TAASISI YA HAWA YAWASHUKURU WATANZANIA KWA KUFANIKISHA KUCHANGIA KAMPENI YA 'NAMTHAMINI'

$
0
0
Afisa Masoko wa East Afrika Radio Basilisa Biseko akizungumza mbele ya waandishi wa Habari (hawapo pichani),mapema leo jijini Dar,kuhusua mafanikio yaliyopatikana kupitia kampeni ya 'NAMTHAMINI',Basilisa amebainisha kuwa kupitia EATV na East Africa Radio pamoja na Taasisi ya Haki za Wanawake (Hawa Foundation) imefanikiwa kukusanya michango ya fedha taslim na pakiti za pedi zitakazowawezesha takribani wanafunzi wa kike wapatao 673 kutokukosa masomo yao kwa muda wa mwaka mzima.Pichani kulia ni Mratibu wa Vipindi Eastafrika Radio,Irene Tillya na kushoto ni Mratibu wa Vipindi EATV,Sophie Proches.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Haki za Wanawake (HAWA) , Joyce Kiria akifafanua jambo kuhusiana na mafanikio makubwa waliyoyapata kupitia kampeni hiyo ya 'NAMTHAMINI',Kiria emesema kuwa Katika kampeni hiyo ambayo wananchi walijitokeza kuichangia katika kuonesha kumjali mtoto wa kike aliyepo shuleni zilichangwa jumla ya shilingi 20,176,110, ambazo fedha taslim shilingi 11,774,610 na pedi za thamani ya shilingi 8,401,500.
 Afisa Masoko wa East Afrika Radio Basilisa Biseko akifafanua zaidi mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani),kuhusiana na mafanikio ya kampeni hiyo 'Namthamini',iliyolenga katika kuchangia pedi (Taulo za Kike) kwa wanafunzi wa Sekondari,ambapo takwimu zinaeleza kuwa karibia asilimia 45 ya wanafunzi wa kike hukosa masomo wakiwa katika hedhi kutokana na kukosa pedi za kujistiri.
 Baadhi ya Waandishi wa habari wakifuatilia mkutano huo uliofanyika mapema leo jijini Dar.

-------   ------   ------  ----------


Kituo namba moja kwa vijana East Africa Television (EATV) Limited kikishirikiana na Taasisi ya Haki za Wanawake (HAWA foundation) kinapenda kutoa shukrani za dhati, kwa umma wa watanzania  kwa  kufanikisha kuchangia kwenye kampeni ya Namthamini.



Namthamini  ni kampeni iliyolenga katika kuchangia pedi (Taulo za Kike) kwa wanafunzi  wa Sekondari, kutokana na takwimu kuonesha karibia asilimia 45 ya wanafunzi wa kike hukosa masomo wakiwa katika hedhi kutokana na kukosa pedi za kujistiri.



Kwa wastani wanafunzi wa kike wengi hupoteza siku tano hadi saba kila mwezi kutokana na ukosefu wa pedi za kujisitiri, na kwa mwaka inakadiriwa kukosa masomo kwa takribani siku 60 hadi 70.



EATV na East Africa Radio katika kufikisha mchango wake kwa jamii, na kwa kuangalia Siku ya Wanawake Duniani, Machi mosi tuliamua kuanzisha kampeni hii kwa kuishirikisha jamii ili kumuwezesha mwanafunzi wa kike asikose masomo yake na kumfanya kutofikia lengo lake kimasomo kwa kukosa pedi pale awapo kwenye hedhi.



EATV na East Africa Radio pamoja na Taasisi ya Haki za Wanawake (Hawa Foundation) imefanikiwa kukusanya michango ya fedha taslim na pakiti za pedi zitakazowawezesha takribani wanafunzi wa kike wapatao 673 kutokukosa masomo yao kwa muda wa mwaka mzima.



Katika kampeni hii ambayo wananchi walijitokeza kuichangia katika kuonyesha kumjali mtoto wa kike aliyepo shuleni zilichangwa jumla ya shilingi 20,176,110, ambazo fedha taslim shilingi 11,774,610 na pedi za thamani ya shilingi 8,401,500.



Michango yote ya fedha iliyopatikana itatumika katika kununua pedi na zitaelekezwa moja kwa moja katika shule za Sekondari 20 zenye uhitaji zilizoteuliwa kupata msaada huu, katika mikoa ya Morogoro, Iringa, Lindi, Pwani na Tanga.



Uongozi wa EATV Limited na Taasisi ya Haki za Wanawake (Hawa Foundation) inapenda kutumia nafasi hii kwa dhati kuwashukuru wananchi wote walioguswa na tatizo la pedi kwa wanafunzi wa kike na kuichangia kampeni ya Namthamini na kuonyesha kuwa kwa pamoja tunaweza. Sisi EATV husema Together Tunawakilisha.



Mwisho kabisa tunapenda kusisitiza kuwa tatizo la wanafunzi wa kike kukosa kuhudhuria shuleni kutokana na kukosa pedi za kujisitiri ni la kwetu sote hivyo East Africa Television Limited pamoja na Taasisi ya Haki za wanawake inatoa wito kwa jamii kuendelea kuungana kwa pamoja katika kusaidia watoto wa kike kupata mahitaji muhimu wawapo shuleni, ili wapate kusoma kwa amani pasipo kukosa kuhudhuria darasani.

MARAIS WASTAAFU WAONGOZA KUAGA MWILI WA MAREHEMU SIR GEORGE KAHAMA

$
0
0
 Mke wa Marehemu Sir Georeg Kahma, Janeth Kahama akiaga mwili wa Mumewe katika ukumbi Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam
 Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dk Jakaya Mrisho Kikwete akiaga Mwili wa Marehemu Sir George Kahama
 Rais Mstaafu wa awamu ya tatu , Benjamini Mkapa  akitoa pole kwa watoto wa Marehemu Sir George Kahama katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam
 Rais Mstaafu wa awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi akiaga mwili wa Marehemu Sir George Kahama.
 Waziri wa Habari Sanaa  Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye akiaga Mwili wa Marehemu Sir George Kahama,katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Waziri mkuu Mstaafu, Salim Ahmed Salim akiaga mwili wa Marehemu Sir George Kahama katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam
 Spika Mstaafu wa Bunge , Anna Makinda akitoa pole kwa wanafamilia ya Marehemu Sir George Kahama.
 Kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni , Freeman Mbowe  akiaga mwili wa Marehemu Sir George Kahama katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam
Mtoto wa Marehemu Sir George Kahama  akiaga mwili wa babake
 Sehemu ya ndugu wa familia wakiaga mwili wa Marehemu Sir George Kahama
 Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowasa akitoa pole kwa watoto Marehemu Sir George Kahamakatika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam
 Mawaziri wakuu wa Staafu pamoja na wake zao wakiwa katika msiba huo kwa uhuzuni
 Marais Wastaafu na wake zao wakiwa wanatafakari  kabla ya kuaga mwili wa Marehemu Sir George Kahama.
Mawaziri wakuu wastaafu wakitafakari jambo kabla ya kuaga Mwili wa Marehemu Sir George Kahama  katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam

AHMAD AHMAD AMNYUKA ISSA HAYOTOU UCHAGUZI WA CAF

$
0
0
\
Rais Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) Ahmad Ahmad kutoka nchini Madagascar

Uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) umemalizika kwa mgombea Ahmad Ahmad kutoka nchini Madagascar kupata kura 34 dhidi ya 20 za aliyekuwa rais wa zamani Issa Hayatou uliofanyika leo nchini Ethiopia.

Uchaguzi huo uliokuwa na ushindani mkubwa kutoka kwa pande zote uliweza kuhitimishwa na wanachama washiriki kutoka nchi mbalimbali barani Afrika kupiga kura za kumchagua ni nanai atakayeongoza shirikisho hilo kwa kipindi kijacho.

Pamoja na uchaguzi huo, CAF wameweza kuipitisha Zanzibar kuwa mwanachama rasmi ambapo kwa sasa atakuwa mshiriki rasmi wa michuano ya kimataifa iliyo chini ya CAF pamoja na kuwa na timu ya Taifa inayojitegemea.

Nchi takribani zote ziliweza kukubali kupatiwa kwa uanachama huo na nchi 51 kukubali na 3 kukataa ambazo ni Benini, Sychells na Madagascar.

Jesca Honole maarufu kama ‘Jesca BM.’achomoza tamasha la pasaka

$
0
0

KAMATI ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka chini ya mwenyekiti wake Alex Msama, limeanza kutaja waimbaji wa nyimbo za injili watakaoshambulia ‘tamasha la mwaka huu.

Mwimbaji wa kwanza kutajwa na Kamati hiyo katika mkutano wake na waandishi habari jijinin Dar es Salaam leo , ni Jesca Honole maarufu kama ‘Jesca BM.’

Msama amesema leo kwamba, mwimbaji huyo amepata bahati ya kipekee ya kuwa wa kwanza na kwamba wengine watawekwa hadharani baada ya kupitishwa rasmi na Kamati.“Tunamshukuru Mungu kwa sababu maandalizi ya Tamasha letu la Pasaka ambalo safari hii linakuja kitofauti zaidi, waimbaji wameanza kupitishwa, ikiwa ni hatua nzuri ya tukio hili la kimataifa,” alisema Msama na kuongeza.

‘Mwimbaji aliyebahatika kuwa wa kwanza kuthibitishwa ni Jesca Honoli maarufu kama ‘Jesca BM’, mmoja wa waimbaji mahiri kwa sasa.Alisema nguvu ya kuanza kutangaza waimbaji watakaohudumu katika Tamasha hilo litakaloanzia Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam April 16, ni baada ya kupata kibali rasmi cha tukio hilo.

Kuhusu kibali, Msama ametoa shukrani kwa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) kwa kutoa baraka kwa tukio hilo la kimataifa ambalo litatikisa katika mikoa ipatayo mitano ya Tanzania bara.Alisema, baada ya Tamasha hilo kuzindiliwa April 16 katika Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam, litahamia Uwanja wa Jamhuri, mjini Dodoma kabla ya kutua katika mikoa mingine mitatu.

Alisema mbali ya Tamasha hilo kubeba malengo yake ya msingi yakiwamo ya kueneza neno la Mungu na kutumia sehemu ya mapato kufariji makundi maalumu, safari hii litatumika kama jukwaa la kumuombea nch Rais John Pombe Magufuli na nchi kwa ujumla.

Manufaa mengine ya Tamasha hilo linalofanyika tangu mwaka 2000, ni kuweza kukuza muziki wa injili kiasi cha kuwa ajira kwa vijana wenye vipaji.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akifafanua jambo jambo kwa kina mbele ya waandishi wa Habari (hawapo pichani) jijini Dar leo kuhusu maandalizi ya tamasha la Pasaka ambalo linatarajiwa kufanyika Aprili 16 mwaka huu kwenye uwanja wa Taifa likishirikisha waimbaji mbalimbali wa muziki wa injili.
Muimbaji wa nyimbo za Injili Jesca Honole maarufu kama ‘Jesca BM.’ambaye amechomoza katika tamasha la Pasaka,akionesha uwezo wake wa kuimba na kupiga kinanda kwenye moha ya maonesho yake

WAZIRI UMMY MWALIMU ATEMBELEA HOSPITALI YA MKOA WA IRINGA

$
0
0
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto Mhe Ummy Mwalimu ameagiza kuanzishwa duka la Dawa ndani ya miezi 3 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa.

Hayo ameyasema wakati wa ziara ya kikazi mkoani Iringa leo tarehe ambapo ametembelea Kituo cha Damu Salama cha Mkoa pamoja na Hospitali ya wilaya ya Mafinga

“Pia naagiza Uongozi wa Hospitali zote za Mikoa na Wilaya kuanzisha Wodi za Watoto Wachanga na Watoto Njiti mara moja” alisema Mh. Ummy.

Mbali na hayo Waziri Ummy ameagiza kujengwa kwa Kitengo cha Wagonjwa wa Dharura (Emergency Unit) kwa hospitali hizo mara moja ili kuboresha huduma ya afya kwa wakazi wa Iringa.

Akitoa taarifa ya utoaji wa huduma za Afya katika mkoa mbele ya Waziri wa Afya, mhe. Amina Masenza, mkuu wa Mkoa wa Iringa alieleza hatua mbalimbali wanazochukua katika kuboresha utoaji wa huduma ikiwemo kuboresha miundombinu ya vituo vya Afya, upatikanaji wa dawa, vifaa na vifaa tiba, utoaji wa elimu ya uzazi wa mpango pamoja na lishe kwa wananchi bila kusahau kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).

Hata hivyo, zipo changamoto kadhaa zinazowakabili mkoa kufikia lengo la lao kutoa huduma bora za Afya. Mathalani katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Iringa haina wodi/kitengo cha dharura, upungufu wa watumishi, Ufinyu wa eneo la Hospitali, ukosefu wa Gari la Kubebea Wagonjwa na ukosefu wa baadhi ya vitendanishi.

Mhe.Ummy Mwalimu amewapongeza viongozi na watumishi wa mkoa kwa juhudi kubwa wanazofanya katika kuboresha huduma za afya ikiwemo kufanikisha ujenzi wa wodi ya watoto waliozaliwa kabla ya wakati na watoto wachanga. Wodi hiyo yenye vifaa vyote muhimu imejengwa kwa ufadhili wa Kampuni ya ASAS ya Mjini Iringa. Mhe Ummy amewataka wadau wengine waendelee kusaidia sekta hii hususani eneo la Afya ya Mama na Mtoto kwa kuwa linawagusa wananchi wengi hasa wa kipato cha chini.

Kufuatia malalamiko aliyoyapokea kutoka kwa wananchi waliofika kupata huduma katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa, Mhe.ummy aliagiza utekelezaji wa masuala yafuatayo; ujenzi wa wodi ya wagonjwa wa dharura na duka la dawa la Hospitali ili kuondoa usumbufu wanaoupata wagonjwa wa kwenda kununua dawa kwenye maduka binafsi. Pia,aliahidi kulifuatilia suala linalohusu gereza lililopo jirani na Hospitali ya mkoa ili liweze kuhamia sehemu nyingine na kutoa eneo kwa Hospitali. Vile vile, ametoa muda wa miezi 9 kuanzia leo tarehe 16 March kwa wakurugenzi wa Halmashauri zote Nchini kuhakikisha vituo vyote vya Afya vinatoa huduma kamili za uzazi za dharura ikiwemo upasuaji wa kumtoa mtoto tumboni.

Akiwa katika Hospitali ya wilaya ya Mufindi, mhe. Ummy aliagiza yafuatayo; uongozi wa wilaya uhakikishe maji yanapatikana muda wote hospitalini, waanzishe mara moja wodi maalum kwa ajili ya watoto wanaozaliwa kabla ya wakati na Watoto wachanga. Pia, aliwakumbusha juu kuhakikisha kuwa wazee wote wanatambuliwa na kupewa vitambulisho lakini alipongeza juhudi zinazofanywa na Halmashauri ya Wilaya ya kuwakatia Wazee kadi za Bima (TIKA).

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AWASILI MBABANE SWAZILAND LEO KUHUDHURIA MKUTANO WA SADC

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewasili mjini Mbabane – Swaziland leo 16-Mar-2017 kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). 

Mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Kimataifa wa Mfalme Mswati III mjini Mbabane – Swaziland, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amepokelewa na Viongozi mbalimbali ambao wameongozwa na Waziri wa Utumishi wa Umma wa Serikali ya Swaziland Owen Nxumalo.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan baada ya kuwasili uwanjani hapo amekagua gwaride la heshima lililoandaliwa kwa ajili yake na kushuhudia vikundi mbalimbali vya burudani uwanjani hapo.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan atamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Dakta JOHN POMBE MAGUFULI ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama inayojulikana kama SADC DOUBLE TROIKA kwenye mkutano huo.

Hapo kesho tarehe 17-Marchi-2017, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan atahudhuria mkutano wa Wakuu na Serikali wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama unaojulikana kama SADC Double Troika ambao utajadili kwa kina hali ya ulinzi na usalama katika nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC)na Falme ya Lesotho.

Mkutano huo wa SADC Double Troika utafanyika kwa kuzingatia mapendekezo ya mkutano wa Mawaziri wa Kamati Ndogo ya Siasa na Diplomasia uliofanyika Dar es Salaam tarehe 24 februari 2017 ambapo mawaziri hao walionyesha ipo haja ya kuitisha mkutano huo ili kujadili kwa kina hali ya ulinzi na usalama kwenye hizo.

Mkutano wa SADC Double Troika utahusisha nchi Sita wanachama wa asasi hiyo ambazo ni Tanzania,Swaziland, Afrika Kusini, Angola, Botswana na Msumbiji.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan katika msafara wake amefuatana na Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Kikanda na Kimataifa Dakta Augustine Mahiga, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage na Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Balozi Amina Salum Ali.

Imetolewa na 
Ofisi ya Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mbabane – SWAZILAND.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akikagua gwaride la Heshima lililoandaliwa kwa ajili yake mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa kimataifa wa Mfalme Mswati wa III mjini Mbabane Swaziland leo march 16,2017 kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na serikali wa Jumuiya ya maendeleo kusini mwa Afrika (SADC) ambapo Makamu wa Rais amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiangalia vikundi vya Burudani mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa kimataifa wa Mfalme Mswati wa III mjini Mbabane Swaziland leo march,16, 2017 kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jumuiya ya maendeleo kusini mwa Afrika (SADC) ambapo Makamu wa Rais amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwasili Heshima kwenye Uwanja wa kimataifa wa Mfalme Mswati wa III mjini Mbabane Swaziland leo march 16,2017 kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na serikali wa Jumuiya ya maendeleo kusini mwa Afrika (SADC) ambapo Makamu wa Rais amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Swaziland alipowasili kwenye Uwanja wa kimataifa wa Mfalme Mswati wa III mjini Mbabane Swaziland leo march 16,2017 kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na serikali wa Jumuiya ya maendeleo kusini mwa Afrika (SADC) ambapo Makamu wa Rais amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Dawasa yachangia Kuongezeka kwa Maji; yajipanga kujenga Mitambo ya Majitaka

$
0
0
Mkuuwa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda akiongea na baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Mashirika ya DAWASA na DAWASCO pamoja na Waandishisho wa habari kuhusu Maadhimi ya Wiki ya Maji Duniani yanayoanza leo tarehe 16 hadi kilele chake 22 Machi, 2017 katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam. 
Katibu Tawala Msaidizi wa Huduma za Maji Mkoa wa Dar es Salaam, Bi. Elizabeth Kingu akiongea na baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Mashirika ya DAWASA na DAWASCO pamoja na Waandishi wa habari kuhusu Maadhimisho ya Wiki ya Maji Duniani yanayoanza leo tarehe 16 hadi kilele chake 22 Machi, 2017 katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam. 
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) Bw. Kiula Kingu akijibu baadhi ya maswali toka kwa Waandishi wa habari kuhusu Maadhimisho ya Wiki ya Maji Duniani yanayoanza leo tarehe 16 hadi kilele chake 22 Machi, 2017 katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam. 
Meneja Mahusiano ya Jamii Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) Bi. Neli Msuya akifafanua baadhi ya hoja na kujibu maswali toka kwa Waandishi wa habari kuhusu Maadhimisho ya Wiki ya Maji Duniani yanayoanza leo tarehe 16 hadi kilele chake 22 Machi, 2017 katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam. 
Baadhi ya Waandishi wa Habari pamoja na Watendaji toka Mashirika ya DAWASA na DAWASCO wakifuatilia taarifa mbalimbali toka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda pamoja na Watendaji wa DAWASA na DAWASACO kuhusu Maadhimisho ya Wiki ya Maji Duniani yanayoanza leo tarehe 16 hadi kilele chake tarehe 22 Machi, 2017 katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam. (Picha/Habari na Benedict Liwenga-WHUSM)


Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) imechangia kwa kiasi kikubwa katika kuhakikisha kuwa upatikanaji wa maji safi na salama nchini unaongezeka.

Akiongea leo na Baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Mashirika ya DAWASA na DAWASCO pamoja Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Maji Duniani ambayo huadhimisha kila mwaka kuanzia siku ya tarehe 16 hadi 22 Machi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda amesema kwamba, katika kuadhimisha Wiki hiyo ya Maji, Mkoa wa Dar es Salaam umelenga kuwahamasisha na kuwaelimisha Wananchi, Viongozi wa Serikali za Mitaa pamoja na Kamati za Maji kuhusu namna bora ya usimamizi wa shughuli za maji katika maeneo yao ikiwemo na tarataibu za umiliki wa visima.

Amesema kwamba, lengo la maadhimisho hayo ni kuongeza upatikanaji wa maji, uzalishaji na usambazaji wa maji safi na salama ambayo yatatumika kwa uangalifu ili kupunguza kiwango cha matumizi yake.

Ameongeza kuwa, hali ilivyo sasa, kiwango kikubwa cha Majitaka kutoka viwandani na majumbani kinaachwa kutiririka bila kutibiwa na kurudishwa kutumika tena ambapo jambo hilo husababisha virutubisho vingi vilivyomo katika maji hayo kupotea.“Katika kuhakikisha maendeleo endelevu na mzunguko wa uchumi, Majitaka ni rasilimali muhimu na hivyo kuyasindika, kuyasafisha kwa kuyatibu na kuyatumia tena ni jambo la lazima”, Alisema Makonda.

Aidha, ameongeza kuwa, katika maadhimisho ya Wiki ya Maji, shughuli za usafi na upandaji miti katika maeneo ya vyanzo vya maji zitafanyika, miradi mitatu ya maji katika maeneo ya Mbagala pamoja na Pugu itazinduliwa na pia miradi 20 ya Jamii itakabidhiwa rasmi DAWASCO.

Amefafanua kuwa, huduma ya maji kwa wakazi wa Dar es Salaam hutolewa na DAWASA ambayo imekodisha shughuli za uendeshaji huduma kwa Shirika la Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) ambapo vyanzo vikuu vya maji ni Mto Ruvu, Mto Kizinga pamoja na maji chini ya ardhi.

Mhe. Makondaa ameongeza kuwa, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa Wakazi wa Dar es Salaam ni asilimia 75 ambapo uzalishaji wa maji hayo kwa sasa ni lita Milioni 390 kwa siku wakati mahitaji ya maji hayo kwa sasa ni ni lita Milioni 510 kwa siku.

Kuhusu Huduma ya Majitaka, Mhe. Makonda amesema kwamba, mfumo uliopo sasa unahudumia asilimia 10 tu ya wakazi wote wa Jiji, lakini kuna mitambo mitatu ambayo inatarajiwa kujengwa katika maeneo ya Jangwani, Kurasini pamoja na Kunduchi na mifumo mingine 50 midogo itajengwa katika maeneo ambayo yanakumbwa na kipindupindu mara kwa mara.

Makonda ameeleza pia kuhusu miradi ya visima vya dharura katika maeneo yasiyo na maji ya bomba ambapo amesema kwamba, DAWASA ina idadi ya visima 147, Manispaa 789 na Taasisi na Watu binafsi visima 600.

Kuhusu mafanikio katika sekta hiyo, amesema kwamba, moja ya mafanikio yaliyopatikana katika utoaji wa huduma ya maji safi na usafi wa mazingira kwa Mkoa wa Dar es Salaam toka mwaka jana hadi mwezi Machi mwaka huu ni pamoja na kukamilika kwa Mradi Mkubwa wa Ruvu Chini ambao umeongeza upatikanaji wa maji toka lita Milioni 182 kwa siku hadi kufikia lita Milioni 270 kwa siku, pia Mradi Mkubwa wa Ruvu Juu ambao utaongeza upatikanaji wa maji kutoka lita Milioni 82 kwa siku hadi kufikia lta Milioni 196 kwa siku ambapo mradi huu unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Machi mwaka huu baada ya kukamilika kwa kazi ya kuunganisha umeme mkubwa kutoka Chalinze.

“Elimu juu ya maji zitolewazo na Serikali kupitia DAWASA na DAWASCO itatolewa, hivyo DAWASCO wameandaa Madawati maalum kwa wananchi wote katika maeneo yote ya huduma na yatakuwa wazi wiki nzima kuanzia leo tarehe 16 hadi 22 Machi, 2017 kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni kila siku”, alisema Makonda.

Kwa upande wake Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) Bw. Kiula Kingu amesema kwamba, DAWASCO pamoja na DAWASA wamefanikiwa kuzuia upotevu wa maji kwa kiasi kikubwa ambapo kwa mwaka jana ulikuwa ni asilimia 47 na mwaka huu umepungua na kufikia asilimia 38.6.

Ameongeza kuwa, wao kama taasisi wamekuwa wakijitahidi kuhakikisha kuwa wanaendelea kupunguza upotevu wa maji kwa kubadilisha miundombinu chakavu ya maji na kuweka miundombinu mipya, pia ubadilishaji wa mita zilizozidi umri wa miaka mitano umeendelea kufanyika hali ambayo imesaidia watu wengi kupata maji.

Naye Meneja Mahusiano ya Jamii Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) Bi. Neli Msuya ameeleza kwamba, maeneo yote ya Dar es Salaam yasiyo na mtandao wa maji yamekuwa yakitengenezewa ramani (design) ili yawekewe mitandao hiyo ya maji ili maji yaweze kupatikana kwa wakazi wa maeneo hayo.

Wiki ya Maji huadhimishwa Duniani kote kuanzia tarehe 16-22 ya mwezi Machi ambapo Kaulimbiu ya Maadhimisho hayo kwa mwaka huu ni “Majisafi na Majitaka-Punguza Uchafuzi yatumike kwa Ufanisi (Water and Waste Water-Reduce and Reuse).

WADAU WA ZAO LA MKONGE WAFANYA MKUTANO SHINYANGA

$
0
0

Alhamis ,Machi 16,2017 kumefanyika Mkutano wa wadau wa zao la mkonge kutoka wilaya ya Meatu mkoa wa Simiyu na wilaya ya Kishapu mkoa wa Shinyanga. 

Mgeni rasmi katika mkutano huo ulioandaliwa na shirika la OXFAM na asasi isiyo ya kiserikali inayojishughulisha na Maendeleo ya Jamii (Relief to Development Society- REDESO) alikuwa mkuu wa wilaya ya Kishapu mheshimiwa Nyabaganga Talaba.

Awali akizungumza katika mkutano huo,Mratibu Miradi (uchumi) kutoka shirika la OXFAM Haji Kihwele alisema lengo la mkutano huo kuwaweka pamoja wadau hao ili waweze kufahamiana sambamba na kujadili namna ya kulifanya zao hilo kuwa na tija na manufaa zaidi kwa wakulima na kuwasaidia wakulima hao kupata masoko. "Tumekutana hapa ili tujadili pia namna ya kumuunganisha mkulima wa mkonge anufaike na masoko yenye faida na kupata uwakilishi mzuri katika sekta hii",alisema Kihwele. 

Akizungumza katika mkutano huo,mkuu wa wilaya ya Kishapu mheshimiwa Nyabaganga Talaba aliwataka wadau wa zao la mkonge kwenda kuwekeza kwa kujenga viwanda katika wilaya yake kwani ardhi ipo ya kutosha. 

"Wadau wa mkonge njooni Kishapu muwekeze,tunayo ardhi ya kutosha,hivi sasa maji kutoka ziwa Victoria yamefika Kishapu,umeme na barabara zinazopitika kipindi chote zipo,tunataka kulifanya zao la mkonge kuwa rasmi badala ya kutumika kwenye mipaka kutenganisha mashamba na milingoti kwa ajili ya kujengea nyumba",alieleza Nyabaganga. 

"Kipindi cha majaribio kimekwisha,tunalima pamba lakini pia tumeamua kulima mkonge,tunataka kilimo hiki kiwe rasmi,wananchi wanajitahidi kulima zao la mkonge lakini changamoto kubwa iliyopo ni ukosefu wa soko hivyo ni vyema ofisi za bodi ya mkonge zikawa na ofisi katika maeneo yanayolima,wakulima wanahitaji kunyanyuliwa kwani hata mikopo inayotolewa haitoshi",aliongeza Nyabaganga. 

Miongoni mwa wadau walioshiriki katika mkutano huo ni wakulima na wasindikaji wa zao la mkonge,wazalishaji wa bidhaa za mkonge,taasisi za kifedha ikiwemo Vision Fund,bodi ya mkonge (TSB),Chemba ya wafanyabiashara,wakulima na viwanda (TTCIA),Shirika la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO),Umoja wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA),Mtandao wa Asasi za Wakulima (Agriculture Non- State Actors Forum -ANSAF) na viongozi mbalimbali kutoka halmashauri ya wilaya ya Kishapu na Meatu. 
Mratibu Miradi (uchumi) kutoka shirika la OXFAM Haji Kihwele akizungumza wakati wa mkutano wa wadau wa zao la mkonge uliofanyika katika ukumbi wa Virgimark Hotel mjini Shinyanga leo Alhamis Machi 16,2017-Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog 
Wadau wa zao la mkonge wakimsikiliza Mratibu Miradi Kiuchumi kutoka OXFAM Haji Kihwele 
Meneja Mradi wa asasi isiyo ya kiserikali inayojishughulisha na maendeleo ya jamii (Relief to Development Society- REDESO) Charles Buregeya akizungumza katika mkutano wa wadau wa zao la mkonge kutok wilaya ya Kishapu na Meatu 
Mkuu wa wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga mheshimiwa Nyabaganga Talaba akizungumza wakati wa mkutano huo 
Washiriki wa mkutano huo wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Kishapu mheshimiwa Nyabaganga Talaba 
Mkuu wa wilaya ya Kishapu mheshimiwa Nyabaganga Talaba akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa zao la mkonge kutoka wilaya ya Meatu na Kishapu 
Mkuu wa wilaya ya Kishapu mheshimiwa Nyabaganga Talaba akizungumza ukumbini 
Mkuu wa wilaya ya Kishapu mheshimiwa Nyabaganga Talaba akizungumza ukumbini ambapo alisema serikali imedhamiria kuanzisha viwanda na kwamba kinachotakiwa ni kuwa tayari kuzalisha zao la mkonge.Kulia ni kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu George Kessy
Kulia ni Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu Boniphace Butondo na Afisa Biashara halmashauri ya wilaya ya Kishapu Konisaga Mwafongo 
Mratibu wa Miradi (Ardhi) kutoka OXFAM bi Amina Ndiko akisisitiza jambo kwenye mkutano huo 
Meneja Mradi REDESO Charles Buregeya (kushoto) na Mratibu Miradi (uchumi) shirika la OXFAM Haji Kihwele 
Mratibu wa Miradi (Ardhi) kutoka OXFAM bi Amina Ndiko akizungumza ukumbini 
Washiriki wa mkutano huo wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini 
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu Boniphace Butondo akichangia hoja katika mkutano wa wadau wa zao la mkonge 
Mwakilishi wa Shirikisho la Wakulima na Wasindikaji wa zao la mkonge wilaya ya Kishapu( SHIWAKI),Yusuph Mboje akielezea kuhusu kazi zinazofanywa na shirikisho hilo lililoanzishwa mwaka 2016 ambalo linakabiliwa na changamoto ya kukosa soko la mkonge na kukosekana kwa mkataba na mnunuzi wa kudumu wa zao hilo 
Mwakilishi wa akina mama wanaojishughulisha na kilimo cha mkonge Anastazia Christopher kutoka Kishapu akielezea faida wanazozipata kupitia kilimo cha mkonge ambazo ni pamoja kuacha kuwa tegemezi kwa waume zao,kusomesha watoto n.k 
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu Boniphace Butondo na mkuu wa wilaya ya Kishapu Nyabaganga Talaba wakiwa ukumbini 
Mratibu wa Miradi (Ardhi) kutoka OXFAM bi Amina Ndiko akiongezea maelezo kutoka kwa akina mama kutoka Kishapu wanaolima mkonge 
Mkulima wa zao la mkonge kutoka Kishapu Fredina Said akimuonesha mkuu wa wilaya ya Shinyanga Nyabaganga Talaba zulia lililotengenezwa kwa mkonge 
Mraghbishi kutoka Taasisi ya Kuimarisha Demokrasia na Utawala Bora (ADLG) ambaye pia ni Mwakilishi wa Mtandao wa Asasi za Wakulima (Agriculture Non- State Actors Forum -ANSAF) bwana Nicholaus Luhende Ngelela akizungumza kwenye mkutano huo ambapo alisisitiza umuhimu wa wakulima wa zao la mkonge kuunda mtandao wao 
Katibu mtendaji Chemba ya wafanyabiashara,wakulima na viwanda (TTCIA) mkoa wa Mwanza Hassan Karambi akizungumza ukumbini 
Taasisi isiyo ya kiserikali yenye kusaidia sekta ya kilimo (Private Agricultural Sector Support - PASS) Emilian Barongo akizungumza ukumbini 






Jeremiah Maleko kutoka Vision Fund akieleza namna wanavyotoa mikopo kwa wakulima
Afisa udhibiti Ubora kutoka Bodi ya Mkonge Olivo Mtunge akielezea kuhusu hali ya soko la mkonge hivi sasa na fursa za mkulima mdogo ili aweze kunufaika na kilimo hicho
Picha ya pamoja washiriki wa mkutano wa wadau wa zao la mkonge kutoka wilaya ya Meatu na Kishapu
Picha ya pamoja washiriki wa mkutano huo .Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

TANGA UWASA INAHITAJI BILIONI 15 KUTEKELEZA MPANGO WA KUSAFISHA MAJITAKA

$
0
0

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa)Mhandisi Joshua Mgeyekwa akizungumza na waandishi wa habari mkoani Tanga kuhusu maadhimisho ya wiki ya Maji
Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Dorra Killo akizungumza jambo wakati wa kikao hicho leo
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa)Mhandisi Joshua Mgeyekwa akizungumza na waandishi wa habari mkoani Tanga kuhusu maadhimisho ya wiki ya Maji
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa kulia akiteta jambo na Meneja Rasilimali watu na Utawala wa Mamlaka hiyo,Haika Ndalama.

Waandishi wa Habari Mkoani Tanga wakifuatilia hotuba ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa ambaye hayupo pichani.
Waandishi wa Habari Mkoani Tanga wakifuatilia hotuba ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa ambaye hayupo pichani katikati mwenye hijabu ni Amina Omari wa Gazeti la Mtanzania
Watumishi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga Tanga Uwasa wakiandaa baadhi ya dondooo kuhusiana na wiku ya maji
Mwandishi wa Gazeti la Daily News Mkoani Tanga Amina Kingazi akiuliza swali kwenye mkutano huo kulia ni Mwandishi wa Gazeti la Mwananchi Mkoani Tanga,Raisa Saidi.
Mwandishi wa Azam TV Mkoani Tanga,Mariam Shedaffa akifuatilia kwa umakini taarifa mbalimbali za mamlaka ya Maji Safi na Usafiri wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa)
Waandishi wa Habari Mkoani Tanga Amina Omari wa Gazeti la Mtanzania wa pili kulia wakifuatilia kwa umakini mada mbalimbali zilizokuwa zikiwakilishwa kwenye semina hiyo
Mwandishi wa Gazeti la Mtanzania,Amina Omari akuliza swali kwenye mkutano huo

MAMLAKA ya Majisafi na Majitaka katika Jiji la Tanga (Tanga-Uwasa), linahitaji kiasi cha shilingi bilioni 15 hadi 20 kwa ajili ya kutekeleza mpango wa kusafisha majitaka yaweze kutumika kwa shughulinyingine za kibinadamu ikiwemo kilimo cha umwagiliaji.

Akizungumza katika semina kwa wanahabari Jijini hapa Mkurugenzi wa Tanga-Uwasa Injinia Joshua Mgeyekwa, alisema kutokana na kuzaliza kiasi cha mita za ujazo zipatazo 2,700, wameonelea wayasafishe kwa kujenga mfumo utakaosaidia maji hayo kutumika tena.Mgeyekwa alisema tayari wametenga eneo la Utofu kama sehemu itayokusanya maji taka ambayo kwa sasa kiasi cha asilimia 10 cha wateja wao maji wanayoyazalisha kupelekwa baharini hivyo mfumo huo utasaidia suala zima la uchafuzi wa mazingira.

“Tupo na mpango wa kuyatumia maji taka kwa shughuli nyingine kama kilimo cha mbogamboga, unaimani kwa kufanya hivyo tutaongeza kipato cha mtu mmoja moja…Lakini ili mpango huu uweze kutimia tunahitaji kiasi cha shilingi bilioni 15 hadi 20 kutekelezwa,” alisema.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa mfumo wa kutumia majitaka kwa shughuli nyingine za kibinadamu umekuwa ukitumika katika nchi zilizoendelea kama China, Israel na kwingineko ambako teklonojia hiyo imeanza.

Katika hatua nyingine Mamlaka hiyo imeanza mpango wa kufunga mita za watumiaji maji wa malipo ya kabla zinazojulikana kwa jina la ‘Lipa Maji Kadiri Unavyotumia’ (LIMAKU) ambazo tayari wamezifunga katika baadhi ya maeneo yakiwemo vikosi vya jeshi hapa nchini.

Mkurugenzi huyo alisema hadi sasa wamefunga katika vikosi vya jeshi vilipo mkoani hapa pamoja na shule 20 za msingi zilizopo katika Jiji la Tanga na maendeleo yake yanaenda vizuri.

“Tumeagiza mita nyingine za Limaku zipatazo 300 hizi pia tutazifunga katika taasisi za serikali na watu wengine hasa wateja wetu wenye madeni makubwa,” alisema Mgeyekwa.


Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

Wakulima na wafugaji wa kata ya Nkiniziwa , Nzega wanufaika na huduma za mawasiliano za Airtel

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Nzega Godfrey Ngupula katikati akikata utepe wakati wa kuzindua manara wa mawasiliano wa mwakashahala ulipo kijiji cha Ngukumo kata ya Nkiniziwa Wilayani Nzega ambapo pamoja na mnaro huu Airtel imewasha minara mingine mitatu ya mawasiliano katika kata za Kahamanhalanga , Songambele na Itumba na kuwawezesha wakazi zaidi ya elfu 32 kupata huduma za mawasiliano mkoani Tabora. wakishuhudia wapili kulia ni Meneja Mauzo wa Airtel Tabora, Fidelis Lugangila akiwa pamoja na wajumbe wa serikali ya kijiji cha Ngukumo.

wakulima na wafugaji wa kijiji cha Ngukumo  kata ya Nkiniziwa wilaya ya Nzega mkoani Tabora wameipongeza Airtel kwa kuwezesha upatikanaji wa huduma za mawasiliano ya uhakika na kuwawezesha kuangalia bei za bidhaa na kutafuta masoko kupitia simu zao za mkononi

 Hayo yalisemwa na wakazi wa kijiji cha Ngukumo wakati wa uzinduzi huduma za mawasiliano utakaowawezesha wakazi zaidi ya elfu 32 kutoka katika vijiji 6  kupata huduma za mawasiliano baada ya Airtel kuwasha minara ya mawasiliano  katika maeneo ya Mwakashahalala Kahamanhalanga, Songambele  Itumba mkoani hapo

 ‘’Tumekuwa tukipata changamoto nyingi sana ikiwemo mawasiiano hafifu ambapo ilibidi kusafiri umbali mrefu kupata huduma za mawasiliano, Tunaishukur kampuni ya Airtel kwa kuona ni vyema kutufikishia huduma za mawasiliano hapa na kutuunganisha na ndugu jamaa  na wafanyabiashara   katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi alisema mkazi wa kata ya Nkiniziwa, John

 Akiongea wakati wa uzinduzi, Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Godfrey Ngupula  alitambua na kupongeza juhudi zinazo fanya na Airtel katika kuhakikisha huduma za mawasiliano zinapatikana kwa wote kufatia mchango wake muhimu katika kukuza uchumi wa nchi na kusema ni muhimu kuwa na mawasilino bora kwani kichocheo kikubwa katika kuboresha maisha ya watanzania na kurahisisha shughuli zao za kijamaa na kiuchumi.

 “naamini mawasialiano haya yataweesha biashara katika wilaya hii kukua, na wakulima watanufaika na huduma mbalimbali za simu zitakazowawezesha kutafuta masoko ya bidhaa zao, kuangalia bei ya mazao, lakini pia watatumia huduma ya Airtel Money kwaajili ya kufanya malipo na manunuzi kwa njia ya simu. Nawaasa wakazi wa wilaya ya Nzega kutumia mawasiliano haya vyema na kuboresha maisha yao” aliongeza Ngupula

  Kwa upande wake Meneja wa Airtel mkoa wa Tabora, Phidelis Lugangila  alisema “Airtel imejipanga kutoa huduma bora na za uhakika na kuwaomba wakazi wa kijiji cha Ngukumo na vijiji vya jirani kutumia huduma na bidhaa za Airtel kupata kipato  kupitia huduma zetu kama vile Airtel Money kwa kuwa mawakala na kupata kamisheni kila mwezi na vilevile kutengeneza ajira kwa vijana wengi.


Wakazi wa mwashala wanajishughulisha zaidi na kilimo cha mahindi,pamba ,Karanga na Mpunga pamoja na ufugaji

ALI KIBA NA DIAMOND KUSHIRIKI PAMOJA NYIMBO YA KUHAMASISHA SERENGETI BOYS

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

KUELEKEA fainali ya kombe la Mataifa Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 nchini Gabon, kamati ya hamasa kwa Serengeti Boys inayoongozwa na Mwenyekiti Charles Hilal imeandaa wimbo wa pamoja utakaoimbwa na wasanii maarufu wa muziki wa Bongo Fleva, Naseebb Abdul ‘Diamond’ na Ali  Saleh ‘King Kiba' pamoja na wasanii wengine.

Wimbo huo wa pamoja ni maalum kwa ajili ya kuhamasisha kampeni za kuchangia timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys itakayofanyika mwezi wa tano nchini Gabon ambapo zitapatikana nchi nne zitakazokwenda kombe dunia la vijana nchini India.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Charles Hilal amesema kuwa kwa pamoja wimbo utakaowahusisha wasanii wengine mbalimbali utakuwa na lengo kuu la kuhamasisha wananchi, wadau na wapenda michezo kuichangia timu hiyo ya vijana kwa lengo la kuisaidia malengo waliyokuwa wameyafikia ya kuipeleka timu hiyo kwenye fainali za kombe la Dunia nchini India.

Hilal amesema kuwa hatua hii ya kusaidia Serengeti Boys kutawajenga vijana hawa kufanya vizuri katika michuano ya mataifa Afrika kwa vijana ikiw ani pamoja na kupata kambi nje ya nchi na kuchgeza mechi kadhaa za kirafiki kutoka nchini jirani lakini hata hivyo bado wanafikria kutafuta mechi ya kirafiki itakayochezwa hapa hapa Jijini Dar es salaam ikiwa ni kwa ajili ya kuwaaga kuelekea nchini Gabon.

Mjumbe wa Kamati ya Serengeti Boys, Maulid Kitenge amesema kwamba tayari ala za wimbo huo zimekwishatengenezwa na wasanii hao wote wametumiwa kwa ajili ya kuingiza sauti, ili mara moja wimbo huo ukamilishwe na kuanza rasmi kusaidia kampeni ya kuhamasisha Serengeti Boys.

“Tayari wasanii Ali kiba na Diamond wameshakubali kurekodi nyimo hiyona wameahidi kufanya haraka kuingiza sauti kwenye ala ambazo tumeshawatumia na baadae wasanii wengine kama Mwasiti Almasi, Darasa na Vanesa Mdee nao wataweka sauti zao,"amesema Kitenge.

Kiba na Diamond wote wapo kwenye Kamati iliyoundwa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye ya kuhamasisha na kuwaunganisha Watanzania kwa pamoja ili kuichangia Serengeti Boys iliyofuzu Fainali za Afrika nchini Gabon Mei mwaka huu.

Katibu wa Kamati hiyo ni Mwesigwa Selestine ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wakati wajumbe ni Kitenge wa EFM Radio na TV, Mkurugenzi wa Mahusiano wa kampuni ya Airtel Tanzania, Beatrice Singano na Mrembo wa Tanzania wa mwaka 1999, Hoyce Temu, yumo Mkurugenzi wa Habari katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hassan Abbas, Mkurugenzi wa Global Publishers Limited, Eric Shigongo na Mkurugenzi wa Radio Clouds, Ruge Mutahaba.

Pia, Serikali iliridhia kuwa mshiriki wa karibu kwa kila hatua kuanzia Bodi ya Mfuko wa Maendeleo ya timu za taifa, Kamati ya Hamasa kwa lengo la kupanga pamoja na kushirikiana kwa pamoja.
Mwenyekiti wa kamati ya hamasa kwa Serengeti Boys , Charles Hilal akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na maendeleo ya Serengeti Boys kueleka kwnye kombe la Mataifa Afrika chini ya miaka 17 yatakayofanyika nchini Gabon. Kushoto ni Mkurugenzi wa Habari katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hassan Abbas na Mkurugenzi wa Mahusiano wa kampuni ya Airtel Tanzania, Beatrice Singano 
Mwenyekiti wa kamati ya hamasa kwa Serengeti Boys , Charles Hilal akiwa pamoja na Mjumbe wa Kamati ya Serengeti Boys, Maulid Kitenge wakiwasikilizisha waandishi ala za wimbo unaotarajiwa kutumika kwa ajili ya kuhamasisha kuichangia Serengeti Boys.

RAIS DKT MAGUFULI ATEMEBELEA ENEO LA UJENZI WA IKULU MPYA KIJIJINI CHAMWINO, DODOMA

$
0
0
  
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na wahandisi na maafisa wa Wakala wa Majengo ya Serikali wakati alipowasili kukagua eneo linapojengwa Ikulu mpya kijijini Chamwino nje kidogo ya mji wa Dodoma leo Machi 16, 2017
  Sehemu ya matofali katika eneo linapojengwa Ikulu mpya kijijini Chamwino nje kidogo ya mji wa Dodoma leo Machi 16, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akitoa maelekezo  wakati alipotembelea na  kukagua eneo linapojengwa Ikulu mpya kijijini Chamwino nje kidogo ya mji wa Dodoma leo Machi 16, 2017
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akitoa maelekezo  wakati alipotembelea na  kukagua eneo linapojengwa Ikulu mpya kijijini Chamwino nje kidogo ya mji wa Dodoma leo Machi 16, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa wakimsikiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu  (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) wakati walipotembelea na  kukagua eneo linapojengwa Ikulu mpya kijijini Chamwino nje kidogo ya mji wa Dodoma leo Machi 16, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisikiliza wakati  Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiongea na wafanyakazi wa TBA  wakati wakikagua matofali walipotembelea na  kukagua eneo linapojengwa Ikulu mpya kijijini Chamwino nje kidogo ya mji wa Dodoma leo Machi 16, 2017
 Mkurugenzi Mkuu wa CDA, Paskasi Muragili,akitambulishwa  kwa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa walipotembelea na  kukagua eneo linapojengwa Ikulu mpya kijijini Chamwino nje kidogo ya mji wa Dodoma leo Machi 16, 2017
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akitoa maelekezo  wakati alipotembelea na  kukagua eneo linapojengwa Ikulu mpya kijijini Chamwino nje kidogo ya mji wa Dodoma leo Machi 16, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa wakikagua matofali walipotembelea na  kukagua eneo linapojengwa Ikulu mpya kijijini Chamwino nje kidogo ya mji wa Dodoma leo Machi 16, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa wakikagua matofali walipotembelea na  kukagua eneo linapojengwa Ikulu mpya kijijini Chamwino nje kidogo ya mji wa Dodoma leo Machi 16, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa wakiangalia ufyatuaji wa  matofali walipotembelea na  kukagua eneo linapojengwa Ikulu mpya kijijini Chamwino nje kidogo ya mji wa Dodoma leo Machi 16, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa wakichanganya mchanga na saruji na kusaidia kufyatua matofali walipotembelea na  kukagua eneo linapojengwa Ikulu mpya kijijini Chamwino nje kidogo ya mji wa Dodoma leo Machi 16, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa wakikagua mchanga unaotengezewa matofali walipotembelea na  kukagua eneo linapojengwa Ikulu mpya kijijini Chamwino nje kidogo ya mji wa Dodoma leo Machi 16, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa wakimwangalia Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Jenista Muhagama (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) akiagana na  Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Elius Mwakalinga   kagua matofali walipotembelea na  kukagua eneo linapojengwa Ikulu mpya kijijini Chamwino nje kidogo ya mji wa Dodoma leo Machi 16, 2017.
PICHA NA IKULU

TANGAZO LA KUPOTEA KWA KIJANA ERICK RAPHAEL MSYALIHA ,ANATAFUTWA NA NDUGU ZAKE

$
0
0


Pichani ni Kijana anayefahamika kwa  jina la ERICK RAPHAEL MSYALIHA anayeishi Sinza-Mugabe ametoweka Ghafla Tarehe 13.03.2017 majira ya usiku alipochukuliwa na watu wasio famika akiwa mitaa ya  nyumbani kwake. Mpaka sasa hajarejea nyumbani, hivyo anatafutwa na ndugu zake, Tunaomba  yeyote atakayemuona au kupata Taarifa zake atujulishe kwa namba +255718105959 au atoe Taarifa katika Kituo cha Polisi kilicho jirani nae,Tunatanguliza Shukurani zetu

Msifungishe ndoa bila ya kuona vyeti vya kuzaliwa vya wahusika

$
0
0
 Waziri wa Mambo ya Katiba Na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe ameagiza kuwa kuanzia tarehe 1 Mei, 2017  ndoa zote zifungwe baada ya wanaotaka kufunga kuwasilisha kwa vyeti vya kuzaliwa kwanza. 

Hivyo, amewataka wananchi wote wanaotarajia kufunga ndoa waanze kutafuta vyeti vya kuzaliwa mapema kwa sababu hawataweza kufunga ndoa kuanzia tarehe 1 Mei, 2017. 

Agizo hilo amelitoa kwa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) leo tarehe 16/3/2017 akiwa ziarani mkoani Morogoro kukagua utendaji wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria.

DAWASA yachangia Kuongezeka kwa Maji; yajipanga kujenga Mitambo ya Majitaka

Viewing all 46329 articles
Browse latest View live


Latest Images