Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

MAKAMU WA RAIS AHANI MSIBA WA KAHAMA

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini kitabu cha maombolezo ya Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani wa kwanza katika serikali ya awamu ya kwanza, Sir George Kahama ,nyumbani kwa marehemu Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akimfariji mjane wa Marehemu Sir George Kahama Bibi.Janet Bina nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

MAZISHI YA SIR GEORGE KAHAMA KUFANYIKA KESHO, SPIKA MSTAAFU ANNE MAKINDA ATOA POLE KWA WAFIWA

$
0
0

Na Dotto Mwaibale


MAZISHI ya aliyekuwa Waziri na Mwanasiasa Mkongwe Sir George Kahama yanatarajiwa kufanyika kesho kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana mwili wa marehemu utawasili nyumbani kwake eneo la Mikocheni B kituo cha mabasi kijulikanacho kama Business leo hii saa 11 jioni na kukesha hadi asubuhi.

Kesho mwili wa marehemu utaondolewa nyumbani kwake kuelekea Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC) kuanzia saa mbili kamili kwa ajili ya viongozi mbalimbali na wananchi kutoa heshima zao za mwisho kabla ya kuelekea Kanisa la Mtakatifu Petro ( St. Peters) Oysterbay Dar es salaam saa tano na nusu 5.30 asubuhi kwa ibada.

Ibada ya mazishi itafanyika katika makaburi ya Kinondoni kuanzia saa tisa na nusu 9.30 alasiri.
Marehemu Sir George Kahama enzi za uhai wake.
Spika Mstaafu, Anne Makinda akisaini katika kitabu cha maombolezo cha Sir George Kahama nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam leo.
Spika Mstaafu, Anne Makinda akimfariji mjane wa marehemu Janeth Kahama.
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), Sofia Simba akimpa pole mjane wa marehemu, Janeth Kahama.
Sophia Simba akisalimiana na aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Bakari Mwapachu katika msiba huo.
Pole zikiendelea kutolewa kwa mjane wa marehemu.
Waombolezaji wakiwa msibani.

RAIS DKT MAGUFULI AENDESHA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI IKULU YA CHAMWINO, DODOMA, LEO

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza kikao cha Baraza la Mawaziri kwenye ukumbi wa mikutano katika Ikulu ya Chamwino mjini Dodoma leo Machi 15, 2017
PICHA NA IKULU

WAAJIRI NA WATUMISHI WA UMMA NCHINI: OPRAS IPO KWA SHERIA HIVYO NI WAJIBU KUITEKELEZA IPASAVYO.

$
0
0
Mkurugenzi wa Idara ya Uchambuzi na Ushauri wa Kazi, Ofisi ya Rais-Utumishi, Bw. Mick Kiliba (wa kwanza kulia) akizungumza mapema leo katika kipindi cha JAMBO kinachotangazwa na TBC One kuhusu Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi (OPRAS). Wengine katika picha ni Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Utendaji Kazi kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi, Bi. Veila Shoo (katikati) na Mwongozaji wa kipindi hicho, Bw. Rashid Salim.
Mtangazaji wa Kipindi cha “JAMBO” kinachotangazwa na TBC One, Bw. Rashid Salim (kushoto) katika mahojiano na Mkurugenzi wa Idara ya Uchambuzi na Ushauri wa Kazi wa Ofisi ya Rais-Utumishi, Bw. Mick Kiliba, pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Utendaji Kazi kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi, Bi. Veila Shoo. Kipindi cha Jambo maudhui yake yalikua kutoa elimu kuhusu umuhimu wa Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi (OPRAS) kwa Waajiri na Watumishi wa Umma nchini.
Mkurugenzi wa Idara ya Uchambuzi na Ushauri wa Kazi wa Ofisi ya Rais-Utumishi, Bw. Mick Kiliba (kulia) akifafanua jambo kuhusu umuhimu wa Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi (OPRAS) kwa Waajiri na Watumishi wa Umma mapema leo katika kipindi cha JAMBO kinachotangazwa na TBC Taifa. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Utendaji Kazi kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi, Bi. Veila Shoo. Wengine ni waongozaji wa kipindi hicho, Bi. Anna Mwasyoke na Bw. Paul Alphonce.
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Utendaji Kazi kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi, Bi. Veila Shoo (kushoto) akizungumza mapema leo katika kipindi cha JAMBO kinachotangazwa na TBC Taifa kuhusu umuhimu wa Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi (OPRAS) kwa Waajiri na Watumishi wa Umma nchini. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Uchambuzi na Ushauri wa Kazi wa Ofisi ya Rais-Utumishi, Bw. Mick Kiliba. Wengine ni waongozaji wa kipindi hicho kushoto ni Bi. Anna Mwasyoke na Bw. Paul Alphonce.

NI WAJIBU WA MAOFISA MAWASILIANO KUHUISHA TOVUTIZAO-DKT JABIRI

$
0
0
 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo BI. Nuru Milao (kulia)  akichangia mada katika kikao  Kazi cha Maafisa Mawasiliano Serikalini kinachoendelea katika ukumbi wa Hazina mkoani Dodoma,kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari Bw. Hassan Abbas. 
 Mkurugenzi wa Idara ya Habari Bw. Hassan Abbas (kushoto) akichangia mada katika kikao  Kazi cha Maafisa Mawasiliano Serikalini kinachoendelea katika ukumbi wa Hazina mkoani Dodoma, kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo BI. Nuru Milao.
 Mtendaji Mkuu Wakala wa Serikali Mtandao Dkt. Jabiri Bakari akitoa mada juu ya hali halisi ya uhuishaji wa Taarifa za Serikali kwenye Tovuti Kuu ya Serikali na Taasisi za Serikali katika Kikao Kazi cha Maafisa Mawasiliano  Serikalini kinachoendelea katika ukumbi wa Hazina mkoani Dodoma. 
 Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Idara ya Habari (Maelezo) Bi. Zamaradi Kawawa akichangia mada katika kikao  Kazi cha Maafisa Mawasiliano Serikalini kinachoendelea katika ukumbi wa Hazina mkoani Dodoma. 
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TBC Bi. Edna Rajabu akichangia mada katika kikao  Kazi cha Maafisa Mawasiliano Serikalini kinachoendelea katika ukumbi wa Hazina mkoani Dodoma. 
 : Afisa Habari Mwandamizi Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bi. Margareth Chambili akichangia mada katika kikao  Kazi cha Maafisa Mawasiliano Serikalini kinachoendelea katika ukumbi wa Hazina mkoani Dodoma. (Picha na Benjamin Sawe-Maelezo).
 : Afisa Habari Mwandamizi Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bi. Margareth Chambili akichangia mada katika kikao  Kazi cha Maafisa Mawasiliano Serikalini kinachoendelea katika ukumbi wa Hazina mkoani Dodoma. (Picha na Benjamin Sawe-Maelezo).
Mkuu wa Kitengo cha Intelejensia ya kidigitali kutoka  Kampuni ya Push Observer Kanali Mstaafu Dkt Abas Katalla akichangia mada katika kikao  Kazi cha Maafisa Mawasiliano Serikalini kinachoendelea katika ukumbi wa Hazina mkoani Dodoma. (Picha na Benjamin Sawe-Maelezo).

Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.

Maafisa Mawasiliano Serikalini wametakiwa kutumia tovuti za ofisi na tovuti kuu ya Serikali kwa kuweka taarifa mbalimbali zinazohusu huduma na bidhaa zinazotolewa na taasisi hizo ili kuwawezesha wananchi kuzifahamu huduma hizo kirahisi.

Rai hiyo imetolewa leo Mkoani Dodoma na Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Serikali Mtandao (EGA), Dkt. Jabir Bakari alipokuwa akitoa semina juu ya matumizi na umuhimu wa tovuti za Serikali katika kikao kazi cha Maafisa Mawasiliano Serikalini kinachoendelea Mkoani humo.

Dkt. Bakari amesema dhana ya Serikali Mtandao ni  kuhuisha matumizi ya TEHAMA kwenye utoaji wa taarifa mbalimbali za Serikali kwa wananchi hivyo ni muhimu kwa kila taasisi kuwa na tovuti zenye taarifa za uhakika na zinazoendana na wakati ili  kurahisisha upatikanaji wa huduma hizo.

“Wakala kwa kushirikiana na TAMISEMI pamoja na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo tumetengeneza mfumo unaotumia muda mfupi kwa taasisi za Serikali kutengeneza tovuti zao ili ifikapo Juni mwaka huu taasisi zote ziwe na tovuti zao zitakazowarahisisha wananchi kufahamu huduma kirahisi,”alisema Dkt.Bakari.

Mtendaji Mkuu huyo ameongeza kuwa tovuti za taasisi zisitumike tu katika kutoa taarifa za huduma na bidhaa zao bali zitumike kuelezea mambo mengine muhimu yanayofanywa na taasisi hizo.

Akielezea kuhusu tovuti kuu ya Serikali, Dkt. Bakari amesema ni muhimu kuhakikisha taarifa muhimu na za kudumu za taasisi husika zinawekwa ili kusaidia wananchi kufahamu kiundani kazi wanazozifanya.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Mawasiliano   (TAGCO), Bw.Innocent Mungy amesema mbali na kuweka taarifa katika tovuti za Serikali, ni wajibu wa Maafisa Mawasiliano Serikalini kutumia mitandao ya kijamii kufikisha taarifa muhimu kwa wananchi .
“Kutokana na maendeleo ya teknolojia duniani hasa katika upande wa mawasiliano, matumizi ya mitandao ya kijamii yamekuwa yakileta tija kwa taasisi za Umma kwani yanasaidia Serikali kujibu haraka hoja zinazowasumbua wananchi”alisema Mungy.
Pia aliwataka Maafisa Mawasiliano kuwa wabunifu katika kutumia mitandao ya kijamii kwani mitandao hiyo inatoa fursa ya kushirikiana, kutangaza huduma na bidhaa za taasisi, kufahamu matatizo ya wananchi.

Kivuko cha MV Sabasaba chaendelea kupiga mzigo

$
0
0
Kivuko cha MV Sabasaba kinachotoa huduma ya kuvusha magari na abiria kati ya Kigongo na Busisi katika Ziwa Victoria kikiwa kinaelea katika ziwa hilo mjini Mwanza.
Baadhi ya magari ya watu binafsi na mabasi ya abiria yakisubiri kuingia katika kivuko cha MV SENGEREMA kinachotoa huduma zake kati ya Kigongo na Busisi katika ziwa Victoria jijini Mwanza tayari kwa kuvuka kuelekea Kigongo kutokea Busisi.PICHA ZOTE NA ALFRED MGWENO TEMESA

NAIBU MEYA TEMEKE AAGIZA SOKO LA STERIO APEWE MZABUNI

$
0
0
Na Humphrey Shao, Globu ya jamii

Naibu Meya wa Manispaa ya Temeke, Feysal Salum, ameagiza kuanzia sasa Soko la Matunda la Temeke Sterio kupewa mzabuni wa ukusanyaji mapato ili kuongeza ufanisi katika mapato ya Halmashauri.

Salum ametoa agizo hilo mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa kujifunza kazi kwa maofisa masoko wa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke na Madiwani, ambao walikwenda kujifunza namna jinsi gani halmashauri ya Ilala imeweza kufanikiwa kupata mapato kupitia masoko kupewa wazabuni kukusanya masoko.

“lazima niwaambie ukweli kuwa soko hili tunalipeleka kwa wazabuni,ili tuweze kupata mapato, haiwezekani kukusanya mapato milioni 50 kwa mwezi na gharama za uzalishaji kuwa juu ya hiyo fedha, hivyo hapa hakuna namna lazima tuligawe hili soko ili tuweze kupata faida” amesema Salum.

Amesema kuwa kwa ziadi ya miaka mitano soko hilo lilikuwa likiendeshwa kwa hasara kwa fedha kutoka Halmashauri, hivyo kuanzia sasa imefikia tamati .

Kwa upande wake Naibu Meya Manispaa ya Ilala, Omary Kumbilamoto amewataka wanasiasa kuacha kukumbatia wafanyabiashara ambao wamekuwa wakiwaletea jeuri maofisa masoko na wakusanya ushuru kwa sababu wanafahamiana na viongozi.

Ametaja kuwa kama viongozi wa juu watakuwa mstari wa mbele kusimamia makusanyo bila ya kumwangalia mtu wataweza kufanikiwa katika mfumo huo wa ukusanyaji kupitia mzabuni ambao una manufaa makubwa sana kwa Halmashauri.
Naibu Meya wa Manispaa ya Temeke Faysal Salum akitoa maagizo ya soko la Sterio kupewa mzabuni mara baada ya kumalizika kwa kikao cha mafunzo kutoka kwa watendaji wa Manispaa ya Ilala
Baadhi ya Madiwani na Watendaji kutoka Temeke wakisikiliza kwa makini maelekezo kutoka kwa Naibu Meya wa Manispaa ya Temeke.
Naibu Meya Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto akizungumza katika kikao hicho cha madiwani na maofisa masoko kutoka Temeke na Ilala.

QUALITY GROUP WADHAMIRIA KUKUZA KIPATO CHA WANANCHI NCHINI

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii


KAMPUNI ya Quality Group imedhamiria kuendelea kujikita zaidi katika sekta mbalimbali zikiwemo za madini, kilimo cha sukari na kuanzisha kwa kiwanda na  usambazaji wa  matrekta nchini.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa makampuni hayo Nicholaus Raphl   Wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam.

Amesema kuwa kampuni ya Quality toka ianzishwe nchini imeweza kuajiri wafanyakazi zaidi ya laki sita (667,300) na imejikita zaidi katika kuwaajiri wazawa.

Quality Group katika kukuza sekta ya viwanda nchini imeingia mkataba na kampuni ya Solanika International Tractors Limited na mradi huo utaanzia mkoa wa Morogoro ambapo takribani matreka 1000 yataanzia kule na watanzania takribani 1200 watapata ajira na mradi huu utakamilika 2018.

Uanzishwaji wa mradi huo utawasaidia watanzania kupata matreka yatakayokuwa na ubora mzuri na yatakuwa ya bei nafuu na kila mkulima anaweza kuwa nalo kwani yatatengenezwa hapa hapa nchini kwa kushirikiana na kampuni ya Solanika.

Pia, Raphl amesema Quality wamedhamiria kuwekeza zaidi katika sekta ya afya kwa kujenga vituo 4,000 vya afya sehemu mbalimbali nchini na itamuwezesha kila mwananchi kupata tiba sahihi na itakayokidhi umuhimu wa mgonjwa na tayari kampuni kutoka nchini Urusi wameshaingia nao makubaliano ya kusambaza dawa kwenye vituo hivyo.

Mbali na hayo, Quality wameweza kujikita katika kukuza elimu ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo ya ujasiriamali wa uvuvi kwa wananchi wanaoishi kando ya Ziwa Victoria na kuwapatia vifaa vinavyostahili kwa kutumika kwenye uvuvi.
 Mkurugenzi wa Makampuni ya Quality Group Nicholaus Ralph akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mikakati ya kimaendeleo itakayofanywa na kampuni hiyo.
Baadhi ya Wanabari wakifuatilia mkutano huo


WANAFUNZI WA S/SEK KATA YA PANGANI WATEMBEA KM 34 AMA KUTUMIA PIKIPIKI SH.10,000

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha

WANAFUNZI wa shule ya sekondari ya kata ya Pangani,Kibaha Mji,wanakabiliwa na adha ya kutembea umbali wa km.34 kila siku,hali inayosababisha baadhi yao kuwa watoro, kukatisha masomo na kupata mimba.

Aidha shule za msingi zilizopo katika kata hiyo,zina uhaba wa walimu ambapo shule yenye wanafunzi 950 ina walimu kumi pekee hivyo kusababisha muda mwingi wanafunzi kucheza.

Hayo aliyasema diwani wa kata ya Pangani,Agustino Mdachi,wakati alipokuwa akizungumzia changamoto za kielimu ,kwenye ziara ya mbunge wa jimbo la Mji wa Kibaha,Silvestry Koka,aliyoifanya katika kata hiyo.

Alisema,wanafunzi wanaosoma kwenye ya shule ya kata wanapata usumbufu na wapo katika wakati mgumu.

Mdachi alieleza kwamba,hakuna usafiri wa daladala zaidi ya kutumia miguu na pikipiki ambazo wanalipa 10,000 hivyo kusababisha wanafunzi hasa wa kike kurubuniwa na madereva bodaboda na kupata mimba.

“Watoto wetu huku hawamalizi shule ya sekondari,ni watoro,wanakatiza masomo na wengine wakipewa mimba ,hii inatokana na shule yetu ya kata kuwa mbali”alisema Mdachi.

Akizungumzia tatizo la upungufu wa walimu katika shule za msingi ,alisema shule ya msingi kama Lumumba na Kidimu zina wanafunzi zaidi ya 900 na walimu ni 10 pekee hivyo watoto wengi wanacheza ,hawafundishi na kufeli.

Nae mbunge wa jimbo la Mji wa Kibaha,Koka amemuagiza diwani na kamati ya maendeleo kata,kuandika barua ambayo ataisaini na kisha ipelekwe kwa mkurugenzi kuhakikisha anaongeza walimu katika shule hizo.

Alitoa siku 30 kwa mkurugenzi wa halmashauri ya mji huo,kushughulikia suala hilo kwa kuangalia taratibu zinazotakiwa kufuata ili kupeleka walimu watakaosaidia kupunguza adha hiyo.

Koka alifafanua,yawekwe mazingira bora kwa wanafunzi ikwemo kuongeza walimu wa kutosha ,kama ilivyo kwa shule za Mailmoja ambako shule moja ina wanafunzi 500 na walimu 30.Alimtaka mratibu wa elimu kata na idara ya elimu halmashauri ya mji wa Kibaha kusimamia changamoto hiyo kwa kushirikiana na mkurugenzi na kupanga walimu kwa uwiano .
 
Koka alieleza suala la kutembea umbali mrefu linaumiza watoto,hivyo ingaliwe namna ya kutafuta eneo mtaa wa Kidimu ili jamii ianze kujitolea kujenga shule nyingine na yeye ataongeza nguvu zake.
Diwani wa kata ya Pangani,Agustino Mdachi akizungumza na wananchi wa kata hiyo kwenye ziara ya mbunge wa jimbo la Kibaha Mji,Silvestry Koka aliyoifanya katika kata hiyo.
Baadhi ya wakazi wa kata ya Pangani,wakisikiliza jambo katika ziara ya mbunge wa jimbo la Mji wa Kibaha, Silvestry Koka kwenye kata hiyo.
Mbunge wa jimbo la Mji wa Kibaha ,Silvestry Koka,akizungumza jambo katika ziara yake kata ya Pangani .(picha na Mwamvua Mwinyi).

UBA Bank yazindua mashine zake za ATM katika Vituo Vinne Jijini Dar.

$
0
0
 Mkurugenzi wa Bank ya UBA Tanzania, Peter Makau akieleza kwa ufupi kuhusiana na uzinduzi wa mashine za kutolea pesa za benki ya UBA ambapo Benki hio imezindua mashine hizo za kutolea pesa katika vituo vinne kwa hapa Dar Es Salaam
 Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya UBA Bank, Jenerali Mstaafu Robert Mboma akikata utepe pamoja na Mkurugenzi wa Benki ya UBA Tanzania Mh Peter Makau kuashiria uzinduzi wa mashine za kutolea pesa katika vituo vinne ndani ya jiji la Dar Es Salaam
 Mwenyekiti wa bodi ya Benki ya UBA Tanzania, Jenerali Mstaafu, Robert Mboma akikata utepe mbele ya Mashine ya kutolea pesa ya benki hiyo mapema leo katika uzinduzi wa vituo vya kutolea pesa vya benki hiyo.
 Mkurugenzi wa benki ya UBA Tanzania, Mh Peter Makau akitoa pesa katika mashine ya kutolea pesa ya benki ya UBA Tanzania mara baada ya uzinduzi kufanyika katika kituo cha Mikocheni. Mashine hiyo ya kutolea pesa ya UBA bank ipo katika Kituo cha Mafuta cha Oilcom kilichopo Mbezi chini.
 Mkurugenzi wa benki ya UBA Tanzania, Mh Peter Makau akisubiria pesa katika mashine ya kutolea pesa ya benki ya UBA Tanzania mara baada ya kuiamuru mashine kutoa pesa mara baada ya uzinduzi wa mashine hizo uliofanyika leo katika kituo cha Mafuta cha oilcom kilichopo mbezi chini
 Mkurugenzi wa benki ya UBA Tanzania, Mh Peter Makau akichukua pesa katika mashine ya kutolea pesa ya benki ya UBA Tanzania mara baada ya kuiamuru mashine huku anayeshuhudia kushoto kwake akiwa mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo Jenerali Mstaafu, Mh Robert Mboma.
 Baadhi ya wafanyakazi wa benki ya UBA wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa benki hiyo kumaliza kuzindua Mashine hiyo ya UBA Bank, uzinduzi uliofanyika leo Mbezi chini katika kituo cha mafuta cha Oilcom.
Mkurugenzi wa benki ya UBA Tanzania, Mh Peter Makau akiongea na waandishi wa habari mara baada ya mwenyekiti wa bodi ya benki ya UBA Tanzania Jenerali Mstaafu Robert Mbona kumaliza kuzindua mashine hizo.Picha zote na Josephat Lukaza
Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa Benki ya UBA Tanzania, Jenerali Mstaafu, Robert Mboma leo amezindua mashine nne za kutolea pesa za benki ya UBA katika kituo cha Mbezi chini huku uzinduzi huo ukiwa ishara ya kuzindua mashine nyingine tatu zinazopatikana katika maeneo ya Oilcom Mabibo, Oilcom Segerea, Oilcom Mbezi chini na Oilcom Mkuki Mall ambayo inatarajiwa kufunguliwa hivi karibuni.
Uzinduzi wa mashine hizi umeenda sambamba na malengo ya benki hiyo ya kuhakikisha katika ukuaji wake inawasogezea huduma karibu wateja wake.
Akielezea katika UZinduzi huo Mkurugenzi wa Benki hiyo Hapa Tanzania, Mh Peter Makau amesema kuwa UBA benki ilikua na ndoto ya kusogeza karibu huduma zake huku lengo lao likiwa ni kuwa na mashine za kutolea pesa nje ya matawi yake na kwa kuanza tumeanza na Mashine za ATM nne ambazo zipo kwenye maeneo muhimu kama vile Oilcom Mabibo, Oilcom Segerea, Oilcom Mbezi chini na nyingine ndani ya jengo la manunuzi la Mkuki ambalo litafunguliwa hivi karibuni.
Vilevile Mwenyekiti wa bodi ya benki hiyo amesema kuwa aliruhusu kuanzishwa kwa mashine hizo za ATM kwaajili ya kuhakikisha inaendelea kukuza uchumi kwa Watanzania huku pia wakitarajia kufungua matawi mengine ndani ya Tanzania hivi karibuni.

NAIBU WAZIRI JAFFO AKAGUA MAANDALIZI YA UJENZI WA DARAJA LA KIJICHI-TOANGOMA TEMEKE

$
0
0
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jaffo (katikati) akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Mbagala, Issa Mangungu alipokwenda kukagua ujenzi wa daraja linalounganisha Kata za Toangoma na Kijichi, Dar es Salaam leo. Kushoto ni Diwani wa Kata ya Toangoma, Mohamed Mketo. (PICHA NA DALILA SHARIF)

Na Dalila Sharif

NAIBU Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo amekagua ujenzi wa Daraja linalounganisha Kijichi hadi Toangoma wilayani Temeke.


Akizungumza Jijini Dar es Salaam leo, alipokuwa akikagua ujenzi wa daraja hilo, Naibu Waziri alisema ameridhishwa na maandalizi ya ujenzi wa daraja hilo


“Daraja hilo lenye urefu wa mita 600 na inatakiwa matayarisho yaanze mapema kwa kuchonga barabara  ili ujenzi ukamilike mapema tayari kwa wananchi kulitumia,”alisema Jafo.


Mkuu wa Wilaya  hiyo, Felix Lyaniva alisema anampongeza Naibu Waziri kwa kukagua ujenzi wa daraja hilo kwa kuwa ni nia njema katika kuendeleza maendeleo ya wilaya hiyo.


“Wapo katika harakati za mandalizi ya ujenzi wa daraja hilo litakaloweza kusaidia kupunguza kero za wananchi wanaotembea umbali mrefu kwa miguu katika maeneo hayo,”alisema Lyaniva.


Hata hivyo, Mbunge wa Jimbo la Mbagala, Issa Mangungu alimuomba waziri  kuwatatulia wananchi wa eneo hilo  kero inayowakabili ya kutolipwa fidia zao.



“Wakazi wa eneo ambao hadi sasa hawajalipwa fidia ya nyumba zao wamekuwa wakikumbwa na mafuriko yanayosababishwa na mvua hivyo kuathirika kwa kiasi kikubwa,”alisema Mangungu.


 Mbunge wa Jimbo la Mbagala, Issa Mangungu akifafanua jambo kwa wanahabari kuhusu maendeleo ya mradi huo
 Jaffo akiwasili kukagua mradi huo

 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jaffo akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Mbagala, Issa Mangungu alipokwenda kukagua ujenzi wa daraja linalounganisha Kata za Toangoma na Kijichi, Dar es Salaam leo. Kushoto ni Diwani wa Kata ya Toangoma, Mohamed Mketo. (PICHA NA DALILA SHARIF)
Jaffo akitoa maagizo baada ya kukagua mradi huo

FEDHA YA UBORESHAJI WA MIJI ZINATAKIWA KUSIMAMIWA KWA UMAKINI –JAFFO

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Naibu Waziri Ofisi ya Rais –Tamisemi Suleiman Jaffo amesema kuwa fedha zinazotolewa na Benki ya Dunia kwa ajili ya mradi wa uboreshaji wa miji zinatakiwa kusimamiwa kwa umakini.

Jaffo ameyasema hayo leo wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa daraja katika eneo la Tuangoma jijini Dar es Salaam, amesema kuwa Temeke inakwenda kwa kasi katika utekelezaji wa mradi uboreshaji wa miji.

Amesema kuwa baada ya miaka mitano jiji la Dar es Salaam itakuwa imebadilika kutokana na mradi wa uboreshaji miji na kuondokana na mafuriko ya mara kwa mara inayotokana na tatizo la miundombinu.

Jaffo amesema wakandarasi wanaosimamia miradi lazima wafanye kazi kwa kufatilia ili miradi hii iweze kudumu kwa muda mrefu na sio kuwa miradi ambayo baada ya mwaka mmoja kukamilika na kuanza nyufa.

Aliongeza kuwa watu ambao wanatakiwa kufidiwa atafatilia kwa mthamini mkuu wa serikali waweze kufidiwa ili mradi uende kwa kasi na Temeke iwe ya kwanza kuwa mji wa kisasa.

Aidha amesema kwa kutokana na mradi huo uko chini ya ofisi yake atafatilia kwa ukaribu katika kuhakikisha jiji la Dar es Salaam linakuwa na ubora na maji mengine duniani.
.Naibu Waziri Ofisi ya Rais –Tamisemi Suleiman Jaffo akizungumza na watendaji wa Manispaa ya Temeke pamoja na wakandarasi wa mradi wa uboreshaji miji DMDP la Tuangoma leo alipofanya ziara katika maradi huo.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.
.Mkuu wa Wilaya ya Temeke , Felix Lyaniva akimpa maelezo Naibu Waziri Ofisi ya Rais –Tamisemi Suleiman Jaffo juu ya mradi wa Mji wa Temeke katika eneo la Tuangoma.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais –Tamisemi Suleiman Jaffo akiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa manispaa ya Temeke na wakandarasi wa mradi DMDP.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais –Tamisemi Suleiman Jaffo akiwa katika picha pamoja na wakandarasi wa mradi wa DMDP leo.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.
Muonekano wa mradi katika mji waTuangoma leo 

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA DKT. JUMA MALEWA AONGOZA KIKAO KAZI CHA SHIRIKA LA MAGEREZA, JIJINI DAR

$
0
0
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akiongoza Kikao kazi cha Shirika la Uzalishaji mali la Magereza ambapo katika Kikao hicho cha siku mbili Wakuu wa miradi watapata fursa ya kuelezea maendeleo ya miradi mbalimbali ya shirika hilo. Kikao hicho kimeanza leo Machi 15, 2017 katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga – Dar es Salaam.
Baadhi ya Wakuu wa miradi mbalimbali ya Shirika la Magereza wakifuatilia kwa makini maelekezo kutoka kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa katika Kikao kazi cha Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza(hayupo pichani).
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akimkaribisha Mkurugenzi wa Manunuzi wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Bw. David Mwangosi ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi katika ufunguzi wa Kikao kazi hicho.
Meza Kuu ikiongozwa na Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(kulia) akitolea ufafanuzi wa hoja mbalimbali(kushoto) ni Mdhibi Mkuu wa Shirika la Magereza, ACP. Joel Bukuku(katikati) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga.
Mkuu wa Magereza Mkoa Mara, ACP. Goleha Masunzu akichangia hoja katika Kikao hicho.
Mkurugenzi wa Manunuzi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Bw. David Mwangosi ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi katika ufunguzi wa Kikao kazi cha Shirika la Magereza (wa pili toka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Miradi ya Shirika la Magereza(wa pili toka kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa kwanza kushoto) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga (wa kwanza kulia) ni Naibu Kamishna wa Magereza, Edith Mallya (Picha zote na Jeshi la Magereza).

WIZARA YAKEMEA UBAKAJI WA MTOTO MKOANI IRINGA

$
0
0
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inakemea vikali tukio la kubakwa kwa binti wa miaka saba (jina limehifadhiwa) mkazi wa kata ay Kitanzini, mwanafuzi wa darasa la awali shule ya SUN Academy iliyoko kata ya Kwakilosa, manispaa ya Iringa.

Wizara imesikitishwa na taarifa za awali kuwa mtoto alibakwa katika mazingira ya shule mahali ambapo tunategemea pawe salama kwa mtoto kuishi. Wakati wote Serikali imekuwa ikisisitiza walezi wa watoto kuhakikisha wanalinda watoto dhidi ya vitendo vyote vya ubakaji kwani vitendo hivi vimekuwa vikitaarifiwa kuwahusisha watu wa karibu wanaomzunguka mtoto katika familia, shuleni na jamii.

Wizara inapongeza vyombo vya habari vyote vinavyoibua matukio ya ukatili, kwa kufanya hivyo ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya wanawake na watoto ambao utekelezaji wake unahusisha wadau wote nchini.

Wizara inamini kuwa Polisi kwa kutumia weledi na umahiri wao watashirikiana na wananchi, walezi, walimu na marafiki wa mtoto, kuhakikisha kuwa watuhumiwa wanafichuliwa na kuchukuliwa hatua stahiki.

Wizara inawakumbusha wazazi na walezi kuwa vitendo vya ukatili ukiwemo ubakaji dhidi ya watoto wa kike havikubaliki katika nchi yetu kwani vitendo hivyo vinatia doa kubwa taifa letu. Natoa rai kwa wananchi wote kutoa ushirikiano katika kuwafichua waliohusika na ubakaji wa mtoto aliyeripotiwa kwa kutoa taarifa kwenye mamlaka husika, ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua stahiki.


Erasto T. Ching’oro
Mkuu wa Kitengo cha Mawasilino Serikalini
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Mashindano Ya Taifa Ya Kuogelea Kufanyika Aprili 7 na 8 Jijini Dar es Salaam

$
0
0
Mashindano ya kutafuta bingwa wa Taifa wa mchezo wa kuogelea yamepangwa kufanyika Aprili 7 na 8 kwenye bwawa la kuogelea la shule ya Heaven of Peace Academy (Hopac) iliyopo Kunduchi Mtongani.
Mashindano hayo yatashirikisha jumla ya timu 19 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara na visiwani.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Kuogelea Tanzania (TSA), Ramadhan Namkoveka alizitaja timu ambazo zinatarajia kushiriki kuwa ni Dar es Salaam Swimming Club, Taliss swimming club, Bluefins, JKT, Morogoro International School, Champions Rise, Braeburn International School na shule ya sekondari ya Makongo.

Timu nyingine ni ISM Leopards, Arusha Swim Club, Mwanza Swim Club, Kennedy School Arusha, Stingrays Swim Club, Tanzania Marines, Hopac Swim Club, Genesis Swim Club, KMKM, Wahoo –IZS na Zanzibar Dolphins.
Waogeleaji hao watashinda katika stali nne ambazo ni freestyle, backstroke, Individual Medley na breaststroke. Pia kutakuwa na mashindano ya ‘relay’ ambayo yatashirikisha waogeleaji wa kike na wa kiume.

“Tunatarajia kuwa na mashindano myenye ushindani mkubwa kutokana na maandalizi ya kila timu, mchezo unakuwa na timu zinazidi kuongezeka, kwa kifupi kuna mwamko mkubwa sana katika mchezo, tunawaomba wadhamini wajitokeze kutusaidia,” alisema Namkoveka.

Alisema kuwa kwa sasa wapo katika maandalizi ya kuhakikisha mashindano hayo yanafanyika kwa kiwango cha kimataifa na kwa kutumia sheria za shirikisho la mchezo huo duniani, Fina.

“Mashindano yatakuwa ya umri, kutakuwa na umri kati ya miaka 9 -10, 11-12, 13-14, 15-16 ba zaidi ya 17, hakuna muogeleaji atakayeruhusiwa kushiriki katika shindano zaidi ya moja, viongozi wote wa timu watanakiwa kufika kwenye mkutano utakaofanyika Hopac kabla ya mashindano kuanza, mkutano huo utaendeshwa na kamati ya ufundi,” alisema.
 Peter Itatiro ‘akikata’ maji katika mashindano yaliyopita ya kuogelea.

Wogeleaji wakishindana katika mashindano yaliyopita ya kuogelea.
 

TFF YAGONGA MWAMBA TRA, OFISI ZAENDELEA KUFUNGWA

$
0
0
TFF YAGONGA MWAMBA TRA, OFISI ZAENDELEA KUFUNGWA


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini TFF limeendelea kuwa katika sintofahamu baada ya ofisi zake kufungwa na Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) baada ya kuwa na malimbikizi ya mda mrefu.

Maofisa hao kutoka kampuni ya YONO Auction Mart walipewa mamlaka na TRA ya kufungia ofisi hizo za TFF huku wakiwambia hawaruhusiwi kuendelea na kazi mpaka pale watakapomalizana na TRA.

Kwa mujibu wa deni hilo, TFF wanadaiwa deni la nyuma ambalo lilikuwa chini ya uongozi wa Leodigar Tenga ikiwemo kodi ya aliyekuwa kocha wa timu ya taifa Marcio Maximo na kodi ya mechi ya Taifa Stars na Brazil.

Katika sakata hilo ambapo timu ya Serengeti Boys ipo kambini ndani ya Shirikisho hilo, wameendelea kusalia lakini wamepewa masharti ya kutokutumia uwanja huo kwa mazoezi mpaka pale watakapomalizana na TRA.

Baadhi ya viongozi wa TFF walijaribu kwenda ofisi za TRA mkoa wa Ilala kujua ni jinsi gani wanalimaliza sakata hilo liligonga mwamba na kushindwa namna ya kujikwamua kwenye adha hiyo.
 Maofisa wa Yono Auction wakiwa pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa TFF wakiwapa maelezo ya kutokuendelea kuwepo ndani ya viunga vya ofisi hizo
 Ofisi za TFF zikiwa zimefungwa.

MISS TANZANIA 2014 NARGIS MOHAMED NA NAFUE NYANGE WAFUNGUA DARASA LA UREMBO KWA NJIA YA DIGITALI

$
0
0
 Miss Tanzania 2004, Nargis Mohamed na Nafue Nyange wameamua kufungua shule ya urembo watakayokuwa wakitoa elimu kwa njia ya mtandao. Akizungumza jijini Dar es Salaam Nargis alisema kuwa wameamua kuandaa mafunzo hayo maalum katika fani ya urembo ili kuweza kuwawezesha wanawake na vijana waweze kujikwamua kiuchumi. 

Nargis aliongeza kuwa mafunzo hayo maalum yamewalenga watu wote na wanaweza kuyapata kidigitali, ikiwemo kwa njia ya simu au mtandao kwa gharama ya shilingi elfu kumi (10,000) tu za Kitanzania kwa mwezi. "Mafunzo hayo hayachagui jinsia; nia yetu kubwa sisi ni kuwawezesha wenzetu kwa kuwapa ujuzi ili waweze kujiinua kiuchumi kama wajasiliamali na kujijenga kimaisha sambamba na mpango wa serikali yetu kujenga ajira na kujikwamua kutoka kwenye umaskini," alisema Nargis.

 Kwa upande wake Nafue Nyange aliongeza kuwa mafunzo hayo yanapatikana kwa bei nafuu kabisa kupitia tovuti ya www.glammadamlive.com
Pia anawaomba watanzania wasajili wataweza kufanya malipo kupitia Vodacom M-pesa na Tigo Pesa. Kwa wale walio nje ya nchi wanaweza kutumia kadi tofauti kama VISA, MasterCard, American Express.
Miss Tanzania 2004, Nargis Mohamed (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari leo nia yao ya kuanzisha darasa la urembo la kidigitali. Pembeni ni Mjasiliamali Nafue Nyange. 
Mjasiliamali Nafue Nyange akisisitiza jambo. 

RAIS DKT MAGUFULI ATENGUA UTEUZI NA KUMSIMAMISHA KAZI KATIBU MKUU,OFISI YA WAZIRI MKUU (BUNGE),ULEDI ABBAS MUSSA

RC PAUL MAKONDA ATIMIZA MWAKA MMOJA SASA,AZUNGUMZA NA KULA NA WAATHIRIKA WA DAWA ZA KULEVYA

$
0
0
Mkuu wa Mkoa Paul Makonda akizungumza mbele ya wageni waalikwa mbalimbali,wakiwemo Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa jiji la Dar,viongozi wa Dini mbalimbali,Wasaniii na vijana kutoka vituo mbalimbali vya matibabu ya dawa za kulevya walijitokeza kumsikiliza RC Paul Makonda ambaye leo alikuwa anatimiza mwaka wake mmoja wa Uongozi tangu aapishwe na Rais wa awamu ya tano,Dkt John Pombe Magufuli.
Baadhi ya waathirika wa Madawa ya Kulevya wapato zaidi ya 1500 kutoka vituo mbalimbali vinavyotoa matibabu ya Dawa za kulevya,wakiwa ndani ya bwalo la Polisi Oysterbay jijini Dar,wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa Paul Makonda alipokuwa akizungumza nao mambo mbalimbali,ya kimaendeleo pamoja na kupewa elimu mbalimbali ihusuyo dawa za kulevya.RC Makonda leo anatimiza mwaka mmoja tangu aapishwe kuwa mkuu wa mkoa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe Magufuli,
Baadhi ya Viongozi mbalimbali wa dini,walialikwa kwenye hafla hiyo fupi ya kutimiza mwaka mmoja kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar,Paul Makonda
Pichani ni baadhi ya wasanii walioshiriki na kutoa neno katika hafla hiyo,wasanii hao ni TID,Diamond Paltnumz,Harmonize,Banana Zorro,Mrisho Mpoto na wengineo ambao walijitokeza kumuunga mkono RC Makonda katika suala zima la kupambana na Dawa 
za kulevya.
Vijana waliothiriwa na Madawa ya kulevya ambao kwa sasa wameahidi kuacha kutumia wakiwa wameandika bango lao la kumshukuru RC Makonda kwa kazi yake nzuri aifanyayo ya kupambana na Dawa za Kulevya.
Vijana mbalimbali walikokuwa wakitumia dawa za kulevya wakimshukuru RC Makonda kwa juhudi zake kubwa za kuhakikisha dawa za kulevya zinatokea ndani ya jiji la Dar kwa namna moja ama nyingine
 

Ajali Mbaya ya Lori lililobeba mawe, Laua Mtu Mmoja

$
0
0
Makete

Lori lililokuwa limebeba mawe limepinduka katika kijiji cha Masisiwe na kusababisha majeruhi na kifo cha mtu mmoja ambaye alikuwa katika lori hilo


Taarifa za awali kutoka eneo la tukio zinasema kuwa lori hilo limepoteza muelekeo ghafla kisha likaanza kupinduka kwa kubiringika mara kadhaa umbali unaokadiriwa kuwa zaidi ya mita 80 kutoka barabarani

Ajali hiyo inadaiwa kutokea kati ya saa nane na saa tisa alasiri hii leo

Baadhi ya mashuhuda waliokuwa eneo la tukio ambao hawakutaka kutaja majina yao wamesema Lori hilo lilikuwa linatoka kubeba mawe kwa ajili ya kujenga daraja katika kata ya Ipepo ndipo lori hilo lilipopoteza mwelekeo likiwa njiani na kupinduka kisha kuporomokea bondeni

Jeshi la polisi Makete limefika eneo la tukio na kuuchukua mwili wa marehemu kwa uchunguzi zaidi

Tutawaletea taarifa kamili ya tukio hilo pindi mamlaka husika zitakapatia

habari/picha na Edwin Moshi wa Eddy Blog
Polisi wakipima jinsi ajali hiyo ilivyotokea 
 Askari Polisi akiangalia mawe yaliyokuwa yamebebwa na lori hilo kabla ya kutokea ajali





Mwili wa marehemu ukiingizwa kwenye gari

Mwili wa marehemu ukiwa ndani ya gari la polisi
Lori hilo likionekana kwa mbali baada ya ajali


Muonekano wa lori hilo baada ya ajali





Ajali ilipoanzia, hapa ndipo lori hilo lilipotumbukia 

Viewing all 46343 articles
Browse latest View live




Latest Images