Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

RAY KUZINDUA FILAMU YAKE MPYA 'GATE KEEPER' KESHO QUALITY CENTER JIJINI DAR

$
0
0


Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Msanii wa Bongo Movie , Vicent Kigosi 'Ray' kesho anatarajia kuzindua filamu yake mpya,itakayojulikana kwa jina la Gate Keeper katika ukumbi wa Sinema wa Quality Centre.

Ray ambaye hajatoa filamu kwa kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja,amesema kuwa filamu hiyo ni moja ya akzi zenye ubora wa hali ya juu katika soko la filamu ambazo azijawahi kutokea tangu aanze kazi hiyo.

ametaja kuwa watu ambao ameshirikiana nao katika filamu hiyo ni Kajala Masanja, Single Mtambalike na Nicole Franklin .

Amesema kuwa filamu hiyo imeandaliwa na Rj Production na kusimamiwa na kampuni ya Steps Entertiment,aidha ametaja kuwa kingilio katika uzinduzi huo ni shilingi 10000 kwakila mtu atakaye fika katika ukumbi huo wa Suncrest Cineplex Cinema.

WAZIRI MKUU APOKEA TAARIFA YA KAMATI INAYOSGHULIKIA MGOGORO WA LOLIONDO

$
0
0
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (kulia) akipokea  Taarifa ya Kamati inayoshughulikia Mgogoro wa  Loliondo Kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati  amabye ni  Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bwana Mrisho Gambo, Wanao shuhudia  Kutoka kushoto Kaimu Mkurugenzi  Mkuu  Mamlaka ya Uhifadhi Tanzania  Martine  Loiboki, Mkuu wa Wilaya ya Loliondo Rashid Taka, Mkurugenzi Mkuu Tanapa Allan Kijazi, Mkurugenzi Mkuu wa Wanyama Pori  Prof Alexander  Songorwa, Mkurugenzi Mkuu wa Thomson Safari s John Bearcroft , Naibu Waziri wa Kilimo na Mifugo Milian Ole Nasha (MB) ,Mwenyekiti wa CCM Arusha  Lekule Laiser  , Mkurugenzi wa Baraza la Wafugaji Wanawake Bibi Maanda Ngoitika , Kikao hicho cha Kukabidhi Tarifa kimefanyika katika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma leo tarehe 2 Februari 2017.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  akionyesha Kitabu cha Taarifa ya Kamati inayoshughulikia Mgogoro wa  Loliondo Kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati  amabye ni  Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bwana Mrisho Gambo, Wanao shuhudia  Kutoka kushoto Kaimu Mkurugenzi  Mkuu  Mamlaka ya Uhifadhi Tanzania  Martine  Loiboki, Mkuu wa Wilaya ya Loliondo Rashid Taka, Mkurugenzi Mkuu Tanapa Allan Kijazi, Mkurugenzi Mkuu wa Wanyama Pori  Prof Alexander  Songorwa, Mkurugenzi Mkuu wa Thomson Safari s John Bearcroft , Naibu Waziri wa Kilimo na Mifugo Milian Ole Nasha (MB), Mwenyekiti wa CCM Arusha  Lekule Laiser  , Mkurugenzi wa Baraza la Wafugaji Wanawake Bibi Maanda Ngoitika, Kikao hicho cha Kukabidhi Tarifa kimefanyika katika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma leo tarehe 2 Februari 2017 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  akisikiliza Tarifa ya Mgogoro  wa  Loliondo  kutoka kwa Mwenyekiti wa kamati na Mkuu wa Mkoa  wa Arusha , Bwana Mrisho Gambo.
 Waziri Mkuu Kassi Majaliwa akiwa katika kikao cha Wanakamati wanaoshugulikia Mgogoro wa Loliondo Kikao hicho kimefanyika katika  Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma
(Picha na PMO)

VIONGOZI WA MIKOA NA WILAYA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA USHIRIKIANO KUIBUA FURSA ZA UWEKEZAJI NCHINI

$
0
0

Na Rhoda Ezekiel Kigoma,

VIONGOZI wa Mikoa na Wilaya wametakiwa kufanya kazi kwa ushirikiano katika kuibua fursa za uwekezaji na kuibua miradi itakayo wawezesha Wananchi kunufaika na ukuaji Wa uchumi katika kuelekea kuwa Nchi ya viwanda ilikuwawezesha Wananchi kuepukana na umasikini .

Wito huo ulitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora , Agrey Mwanry ambae pia ni mwenyekiti wa Baraza la uwezeshaji kanda ya ziwa Mkoani kigoma katika  Semina ya mafunzo ya uwezeshaji kwa Viongozi wa Mikoa na Wilaya za Kigoma, Kagera , Tabora na Katavi ya kanda ya Mgharibi ambayo iliandaliwa na Baraza la uwezeshaji Taifa iliyo lenga kuwawezesha viongozi kuwajengea uwezo wananchi katika kukuza uchumi.

Mkuu huyo alisema ilikuwawezesha Wananchi kunufaika na uchumi ni lazima Viongozi kushirikiana katika kuibua Fursa za uwekezaji na kuboresha  Miundombinu itakayo saidia Wananchi kunufaika na uchumi katika kufanya  shughuri zao katika mazingira mazuri na yanayo wavutia katika kuboresha uthamani wa bidhaa Wanazo zalisha.

Mwanry alisema Viongozi kazi yao kubwa ni kuonyesha njia ya maendeleo kwa Wananchi juu ya ukuaji wa kiuchumi, fursa zinazotakiwa kuibuliwa ni pamoja na kila halmashauri kutenga bajeti ya maendeleo ya wananchi kwa Asilimia tano ilikuweza kuwawezesha Wananchi kuepukana na umasikini na kunufaika na Ukiaji wa uchumi.

"Mimi kwa upande wangu katika Mkoa wa Tabora kitendo cha baadhi ya viongozi wa Wilaya na Wakurugenzi kuwa miongoni mwa walalamikaji dhidi ya kero zinazo wakabiri Wananchi na kushindwa kuzitatua ni kutotambua nafasi zao katika jamii , kwa upande wa Mkoa wa Tabora siwezi kukubari kupitisha bajeti za Halmashauri ambayo haitatenga asilimia tano ya bajeti yake kwaajili ya fedha za maendeleo ya Wananchi ni tatizo kubwa katika kudidimiza uchumi kwa Wananchi.

Kwa upande wake katibu mtendaji baraza la uwezeshaji Taifa , Beng'i Issa alisema lengo ni kuwawezesha Viongozi kutambua majukumu yao kushirikiana na Wadau wa maendeleo kuwawezesha Wananchi katika fursa za maendeleo pamoja na kuboresha miundombinu itakayo saidia kukuza uchumi katika maeneo yao.

Alisema semina hiyo itawasaidia viongozi kuweza kuibua fursa mbalimbali za kiuchumi katika kuwawezesha Wananchi kujishughurisha katika biashara mbalimbali na kuinua uchumi Wa Wananchi wa kipato cha chini hadi serikali ilikuwezesha na Wananchi kunufaika na uchumi huo.

Beng'i alisema kigezo kinacho tumika kupima ukuaji wa uchumi ni jinsi Maisha ya wananchi wa eneo husika yalivyo badilika katika pato lao kiuchumi pamaja na maisha wanayo ishi kwa ujumla endapo Mkoa utafanikisha masuala hayo itakuwa imefikia lengo hilo.

TAHMEF YAENDELEA NA KAMPENI YAKE YA KUBORESHA AFYA YA WANAWAKE NA WATOTO NCHINI.

$
0
0

Na Bakari Issa Madjeshi,Globu ya Jamii

Shirika la Afya na Elimu ya Tiba-TAHMEF linatarajia kuendelea na Kampeni yake ya kuboresha Afya ya Wanawake na Watoto ili kuboresha Afya Bora na Ustawi.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam,Mwenyekiti na Mwanzilishi wa Shirika hilo,Juliana Busasi amesema TAHMEF inatarajia kufanya shughuli maalum yakuchangia Mfumo wa Kuboresha Afya ya Mama na Mtoto siku ya Jumamosi Machi 04,2017.

Amesema shughuli hiyo italenga mambo mawili ambayo ni Kuwekeza Bima za Afya ya Mama na Mtoto ikiwa kuchangia pesa,Kuwasaidia Bima ya Mwaka mmoja kukaa katika Mfumo na kuwekeza.

Pia kuboresha Mazingira katika Hospitali na kuchangia vifaa katika hospitali za Serikali.

Kwa upande wao Wanachama wa Shirika hilo,Kenneth Munanu na Consolata Msambichaka wamesema vijiji vingi hapa nchini vina uhitaji wa Bima ya Afya.

Pia wamewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi kuchangia shughuli hiyo ili kufanikisha Kampeni hiyo ya Nuru ya Afya.


Mwenyekiti na Mwanzilishi wa Shirika la Afya na Elimu ya Tiba (TAHMEF),Juliana Busasi (katikati) akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na Maandalizi ya Kampeni ya kuboresha Afya Wanawake na Watoto ijulikanayo kama Nuru ya Afya inayotarajiwa kufanyika siku ya Jumamosi Jijini Dar es Salaam.

WATU WATATU RAIA WA BURUNDI WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKAONI KIGOMA

$
0
0
Na Rhoda Ezekiel Kigoma.

WATU watatu raia wa Nchi ya Burundi waliopewa hifadhi katika Kambi ya wakimbizi ya Mtendeli Mkoa wa Kigoma,wanashikiliwa na Jeshi la Polisi la hapo,kwa tuhuma za upangaji wa magogo katika barabara kuu ya Kigoma ,Kasulu na Kakonko kwa lengo la utekaji wa magari hasa mabasi ya abiria yaendayo mikoani.

Pia, walipokaguliwa walikutwa na vitu vifuatavyo Bomu moja la kutupwa kwa mkono(Offensive hand Grenade),Bunduki moja ya bandia,panga mbili,rungu 3,viatu aina ya raba jozi moja,viatu vya kike jozi moja,simu aina ya nokia Nne,Tecno tatu,vipodozi vya kike,laptop ,power benki,saa,sanjari na nguo mbalimbali za kiume.

Akizungumzia tukio hilo leo mbele ya wandishi wa habari ofisini kwake kigoma Ujiji,Kamanda wa Polisi Ferdinand Mtui alisema walibaini hilo baada ya askari polisi waliokuwa katika doria kwenye njia hiyo yenye mapori makubwa ndipo waliwakamata watuhumiwa hao ambao walikuwa
kwenye mtego.

Aliyataja majina ya watuhumiwa hao ni pamoja na Hakizimana David(21),Nepomseni Niogere(25) na Nduwamahoro Justine(20) wote ni wakimbizi wanaoishi katika kambi ya mtendeli iliyopo wilaya ya Kakonko
na watafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.

Alitoa mwito kwa raia wote wa kigeni waliopewa hifadhi katika kambi mbalimbali za wakimbizi mkoani humo watii sheria,kanuni na taratibu
zote za nchi na waache kujihusisha na vitendo

SERIKALI MKOANI MBEYA KUWACHUKULIA HATUA KALI ZA KISHERIA ASKARI POLISI WANAOTUHUMIWA KWA WIZI WA DHAHABU CHUNYA

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla akizungumza na wachimbaji wadogo wadogo katika mgodi wa dhabau wa Itumbi kata ya Matundasi Wilayani Chunya Mkoani Mbeya Februry 2 mwaka huu. 


Na EmanuelMadafa,Mbeya

Serikali Mkoani Mbeya imeahidi kuwachukulia hatua kali za kisheria baadhi ya askari Polisi wanao tuhumiwa kuhusika na ubebaji wa mawe ya dhahabu katika shughuli za uokoaji wa wachimbaji waliofukiwa na kifusi mwezi February mwaka huu Wilayani Chunya Mkoani Mbeya.

Hatua hiyo inakuja kufuatia baadhi ya wachimbaji madini wadogo katika mgodi wa dhahabu wa Itumbi Kata ya Matundas Wilayani Chunya kutoa malalamiko yao mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amosi Makalla, ambaye alifika katika eneo hilo kujionea hali halisi ya maafa hayo, ambapo inaelezwa kuwa zaidi ya wachimbaji wadogo 25 katika mgodi wa dhahabu wa Itumbi,walifukiwa na kifusi na kusababisha majeruhi na vifo vya watu wanne, mwezi February mwaka huu.

Wachimbaji hao walidai mbele ya Mkuu wa Mkoa kuwa baadhi ya askari polisi ,walishindwa kutekeleza wajibu wao katika kufanya kazi ya uokoaji wa watu na mali zao, badala yake wao walikimbilia kubeba mawe ya dhahabu ambayo yalikuwa tayari yamechimbwa na wachimbaji hao, kisha kuyapakia kwenye gari ya polisi na kuyasafirisha mahala pasipojulikana.

Wachimbaji hao, walimweleza Makalla kuwa askari hao ambao wanadaiwa kuwa si waadilifu, wao waliendelea na shughuli ya ubebaji wa mawe ya dhahabu ambayo yalikuwa yamechimbwa na wachimbaji na yapo nje yakisubili kuchenjuliwa ili kupatikana madini aina ya dhahabu.

Aidha, kutokana na malalamiko hayo, Makalla aliwataka wananchi pamoja na wachimba madini hayo kuwa watulivu na wapole, kwa kuwahakikishia kwamba serikali italishughulikia suala hilo na kuwachukulia hatua baadhi ya askari watakaothibitika kuhusika na tuhuma hizo. 

“Serikali haitalinyamazia suala hili, nimeunda kikosi kazi cha watu kadhaa ambao watayafanyia kazi malalamiko haya na kama kutakuwa na ushahidi wa bila kuacha shaka juu ya askari kuhusika na ubebaji wa mawe ya dhahabu, basi hatua za kinidhamu zitachukuliwa sambamba na kufikishwa mahakamani,”alisema. 

Amesema, wakati zoezi hili linafanyika, serikali imeufunga mgodi huu wa Itumbi, na kuwataka wachimbaji kutofanya shughuli yoyote kwani mbali na maafa yaliyotekea pia mgodi huo umeghubikwa na changamoto nyingi, ukiwemo mgogoro baina ya wananchi na mfanyabiashara Vicent Minja juu ya nani mmiliki halali wa eneo la mlima huo unaosemekana kuwa na madini aina ya dhahabu. 
Mmoja wa wachimbaji wadogo wadogo katika mgodi wa Itumbi kata ya Matundasi Wilayani Chunya Mkoani Mbeya akitoa malalamiko yake mbeya ya Mkoa wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla (hayupo Pichani). 
Wachimbaji wadogo wadogo katika mgodi wa Itumbi kata ya Matundasi Wilayani Chunya Mkoani Mbeya wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla (hayupo pichani) katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kitongoji cha Itumbi Kata ya Matundasi Wilayani Chunya Mkoani Mbeya February 2 mwaka huu. 
Mkutano ukiendelea. 

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO MACHI 3,2017

MAKALA SHERIA:NAMNA YA KUOMBA KUKAA NA MTOTO PANAPO MGOGORO NA MZAZI MWENZAKO .

$
0
0
Na  Bashir  Yakub.

Tumesikia  mara  kadhaa  wazazi  wakigombania  kukaa  na mtoto/watoto. Haya  hujitokeza  baada  ya  kuvunjika  kwa  ndoa  kwa  talaka,  baada  ya  kutengana  bila  talaka   au  pasi  na  ndoa  wazazi  tu  wamezaa  na  sasa  hawaelewani  na  mgogoro  wa  nani  akae  na  mtoto  umeibuka.

Tunahitaji  kujua ikiwa kuna  haja  ya  kugombania  mtoto kwa matusi  na  ugomvi    wakati  zipo  taratibu  za  kisheria. Tujue  kama yafaa  kutumiana  jumbe  chafu  za  kudhalilishana pale   unapotaka  ukae  na  mtoto. Jibu  ni  hapana  ila  ni  watu  tu  wajue  taratibu.

Ifahamike  kuwa  iwe  kwa  ndoa  au  bila  ndoa   haki  ya  mtoto  kukaa  na  wazazi  au  mzazi   iko  kwa  yeyote. Ni  aidha  atakaa  na wote  wawili  au  mmoja  wao. Sheria  namba  21 ya  2009, Sheria  ya  Mtoto  ndiyo  sheria  ambayo  kwasasa  inasimamia  ustawi  na  haki  za  mtoto.  Hivyo  makala  yataeleza  yaliyo  katika  sheria  hii.

1.MTOTO  NI  NANI.
Kifungu  cha 4( a ) cha  sheria  ya  mtoto  kinatafsiri  neno  mtoto  kumaanisha  mtu  ambaye  yuko  chini  ya umri  wa  miaka  18. Kwa  maana  hii  miaka  18  kamili  sio  mtoto  isipokuwa sasa  chini  yake  ndiye  mtoto  kwa  tafsiri  ya  kifungu  hiki.

Sambamba na  hilo  kifungu  cha  7( 1 ) kinaeleza  haki  ya  mtoto  kukaa  na  wazazi  wake  wote  wawili. Basi  yaje  hayo   ya  kutengana   na  mtoto  kuishi  maisha ya  mzazi  mmoja , bado  uhalisia  ni  haki  ya  msingi   ya  mtoto  kukaa  na  wazazi  wake  wawili  kama  ilivyoainishwa  hapa.

KUSOMA  ZAIDI  sheriayakub.blogspot.com.


WAKURUGENZI BENKI YA AfDB WARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI INAYOFADHILIWA NA BENKI HIYO NCHINI TANZANIA

$
0
0
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Ashatu Kijaji (Mb) akisisitiza kuhusu jitihada zinazofanywa na Serikali katika kutatua changamoto ya deni la Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco) kwa kuendeleza juhudi za kutumia nishati mbadala ya Gesi badala ya Mafuta mazito katika kuendesha mitambo ya Uzalishaji wa umeme, katika kikao na Wakurugenzi Watendaji wanaoziwakilisha nchi zao katika Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb)(kushoto) akiongoza Mkutano wa Wakurugenzi Watendaji wanaoziwakilisha nchi zao katika Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), katika kufanya tathmini ya maendeleo ya Miradi inayofadhiliwa na Benki hiyo, ambapo Wakurugenzi hao waliipongeza Tanzania kwa kutekeleza miradi kwa ufanisi. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji kutoka Afrika ya Kusini Bi. Mmakgoshi Lekhethe aliyeongoza ujumbe wa Wakurugenzi Watendaji wengine 12 (hawapo pichani), katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji kutoka Afrika ya Kusini Bi. Mmakgoshi Lekhethe (kulia) wakipeana mikono baada ya kumalizika kwa mkutano wa tathmini ya maendeleo ya Miradi inayofadhiliwa na Benki hiyo nchini Tanzania, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (wanne kulia) na Mkurugenzi Mtendaji kutoka Afrika ya Kusini Bi. Mmakgoshi Lekhethe (wa tano kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi Watendaji wanao ziwakilisha nchi zao katika Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), baada ya kumalizika kwa mkutano wa tathmini ya maendeleo ya Miradi inayofadhiliwa na Benki hiyo nchini Tanzania, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa Wakalimani aliyeambatana na Wakurugenzi Watendaji wanao ziwakilisha nchi zao katika Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), akisalimiana kwa bashasha na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), (kulia) baada ya kumalizika kwa mkutano wa tathmini ya utekelezaji wa miradi inayofadhiliwa na Benki hiyo nchini Tanzania, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es salaam, ikiwa ni ishara njema kwa Taifa kwa kuwa walipongeza jitihada zinazofanywa na Serikali za kupambana na umaskini.

Na Benny Mwaipaja, WFM

Naibu Waziri Wizara ya Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) amesema Serikali inaendelea kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) katika kuhakikisha miradi yote ikiwemo ile inayofadhiliwa na Benki hiyo inatekelezeka kwa ufanisi Mkubwa.

Dkt. Kijaji ameyasema hayo alipokutana na Wakurugenzi Watendaji 12 wanaoziwakilisha nchi zao katika Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), katika Mkutano uliofanyika Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dar es salaam, baada ya ujumbe huo kutembelea miradi mbalimbali inayofadhiliwa na Benki hiyo hapa nchini.

“Madhumuni makubwa ya ziara ya Wakurugenzi watendaji wa Benki ya AfDB waliokuja nchini tangu Februari 25, ni kukaa pamoja na Serikali ili kujadiliana kuhusu sera na mipango mikakati ya maendeleo, lakini pia kutembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa kupitia ufadhili wa Benki ya hiyo” Alifafanua Dkt. Kijaji.

Wakurugenzi hao ambao ndio watoa maamuzi katika Benki hiyo, wametembelea miradi ya maji Zanzibar na kwa upande wa Tanzania Bara wametembelea mradi wa kufua umeme wa Sokoine substation uliopo Manispaa ya Ilala.

Katika Mkutano huo, Serikali ya Tanzania imeendelea kuiomba Benki ya AfDB kuharakisha kazi za upembuzi yakinifu na hatimaye kutoa fedha ili utekelezaji wa miradi ya Maendeleo uanze mapema kwa kadri inavyowezekana.

Miradi hiyo ni pamoja na ule wa North – West grid wa kusafirisha Nishati ya Umeme kutoka Shinyanga hadi Mbeya kupitia Kigoma Katavi na Rukwa. Mradi utakaowezesha Mikoa ya Ukanda wa Magharibi kupata Nishati ya uhakika ya umeme na kufungua fursa za Maendeleo mbalimbali yakiwemo ya ujenzi wa Viwanda vidogo na vya kati.

Kwa kushirikiana na Benki hiyo ya AfDB mradi mwingine unaofanyiwa kazi ili kupata fedha za kuanza kuutekeleza ni ule wa kujenga barabara ya Nyakanazi, kupitia Kibondo, Kasulu hadi Manyovu, kwa kiwango cha lami na iwapo mradi huo ukipatiwa fedha na kukamilika kwa wakati kutasaidia kuchochea biashara ya wakazi wa maeneo hayo pamoja na Nchi ya Burundi.

Kwa upande wa Wakurugenzi Watendaji wa AfDB wanaoziwakilisha nchi zao, wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji kutoka Afrika ya Kusini Bi. Mmakgoshi Lekhethe, wameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Pombe Joseph Magufuli kwa ufanisi katika Nyanja zote ikiwemo ya kupambana na umaskini.

Wageni hao wamefurahishwa na namna Tanzania invyotekeleza miradi inayofadhiliwa na Benki hiyo, kwa kuwa kila walipopatembelea, wameona uthabiti na umadhubuti wa miradi, jambo ambalo limewaongezea hamasa ya kufanya kazi kwa karibu na nchi hiyo.

Wameitaka Serikali kuendelea kulishughurikia suala la deni la Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania-TANESCO, ili kuongeza ufanisi wa kiutendaji kwa lengo la kuchochea maendeleo ya nchi mijini na Vijijini.

Naibu Waziri Dkt. Kijaji amebainisha kuwa ipo mikakati iliyowekwa na Serikali ya kutatua suala la deni hilo kwa kuwa tatizo kubwa lilikuwa matumizi ya Mafuta ya dizeli katika kuendeshea mitambo TANESCO.

Aidha alisema kuwa kwa sasa upatikanaji wa Nishati ya Gesi katika maeneo mbalimbali ya Tanzania, utasaidia katika kuendesha mitambo hiyo badala ya Mafuta hivyo kutatua suala la deni hilo linalo likabili Shirika na hatimaye kutimiza ndoto ya watanzania ya kuimarika kwa uchumi utakao chochewa na Sekta hiyo.

NJOO TUFURAHI KWA PAMOJA WEEKEND HII NDANI YA SHEKINAH GARDEN, MBEZI.

SERIKALI YAKOMAA NA OPERESHENI YA VIROBA

$
0
0

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 

Operesheni ya kukagua pombe zinazofungashwa kwenye vifungashio vya Plastiki (Viroba) ambapo jana katika manispaa ya Temeke na Kinondoni wamefunga viwanda na maghala kutoendelea na uzalishaji ,kuuza wala kusambaza. 

kiwanda cha Global Distillers Limited watengenezaji wa pombe kali aina ya viroba aina ya Premium Vodka na Ginja ambapo walifanikiwa kukamata katoni 1500 na ghala ambalo lilikutwa na katoni 650 na Wilaya ya Kinondoni na Ubungo kiwanda cha Kibo Spirit na True Bell navyo vilizuiwa uzalishaji baada ya kukuta pombe hiyo ya viroba ikiwa imesheheni aina ya Kitoko na Rivella Vodka kimakosa. 

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ukaguzi huo kwa upande wa Wilaya Kinondoni na Ubungo Mwanasheria wa Baraza la Mazingira (NEMC ) Heche Suguta amesema operesheni hiyo endelevu lengo ni kuhakikisha agizo laserikali linatekelezeka kwa wafanyabiashara hao kusitisha utengenezaji wa vileo katika vifuko ‘ viroba’. 

Amesema wanafunga na kusitisha uzalishaji huo hadi hapo utaratibu mwingine utakapofuatwa ikiwa ni pamoja na kutumia teknolojia mpya.
Amesema lengo ni kusimamisha uzalishaji na hata uingizwaji kwa kuwa vileo vingine vinatoka nje ya nchi na aliongeza kuwa hata kwa wale wa mpakani tayari wameshawasiliana na Jeshi la Polisi kuhakikisha wanazuia uingizwaji na kama mtu amekamatwa basi anatakiwa mzigo wake urudishwe ulipotoka. 

Katika manispaa ya Kinondoni pia ukaguzi ulifanyika katika maghala mbalimbali ikiwemo la Triple S Investment Company Ltd na muhusika kukimbia ambapo timu ya ukaguzi ilikuta makufuli yakiwa yamefunguliwa na jengo zima kutokuwa na mtu. 

Katika ghala hilo pia ambalo muhusika alikimbia walikutana na vifungashio kwa nje aina ya Signal true Vodka ujazo asilimia 100.Katika ghala la Kibo Sprit uongozi wa hapo walisema hawajaanza uzalishaji zaidi ya kuwa na ghala hilo na upande Temeke ,Kiongozi wa msafara katika timu hiyo Mkaguzi kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Aron Nzalla alisema ukaguzi wameufanya kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama. 

Katika ukaguzi wa kiwanda cha Global distillers mkaguzi huyo alimweka chini ya ulinzi wafanyakazi wa kampuni hiyo akiwemo mhasibu ,Ofisi Ugavi na Manunuzi pamoja na mlinzi (majina yamehifadhiwa ).


Mwanasheria toka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Manchare Heche (kushoto) akikagua nyaraka toka kwa Msimamizi wa Kiwanda cha True Bell (T) Limited Bw. Godwin Mungere mapema leo hii jijini Dar es Salaam wakati wa siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.
Baadhi ya Maafisa wa Serikali wakikagua ghala la Kiwanda cha True Bell (T) Limited mapema hii leo Jijini Dar es Salaam wakati wa siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.
Msimamizi wa Kiwanda cha True Bell (T) Limited Bw. Godwin Mungere (mwenye shati la njano) akionesha baadhi ya vifungashio vya pombe kali aina ya kiroba mapema hii leo Jijini Dar es Salaam wakati wa siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika, kulia ni Mwanasheria toka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Manchare Heche
Baadhi ya shehena ya maboksi ya pombe ya viroba aina ya bonanza ikiwa imehifadhiwa katika ghala la kiwanda cha True Bell (T) Limited kilichopo Sinza Bamaga mapema leo hii jijini Dar es Salaam wakati wa siku ya pili ya operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.

HUAWEI DONATES 10M/- TO THE TANZANIA SCOUTS ASSOCIATION (TSA)

$
0
0



Dar es Salaam. Huawei Technologies Co. Ltd, a leading global ICT solutions provider over the weekend donatedTsh10 million to the Tanzania Scouts Association (TSA) to honor 100 years of Scouting in Tanzania as well as to mark the African Scouts Day 2017.

The donation was part of Huawei’s Cooperate Social Responsibility (CSR) strategies to support the government efforts in improving children and youth development as well as education sector in the country.

As a responsible citizen, Huawei has been in Tanzania for 17 years with a mission to grow together with Tanzania by empowering local Tanzanians especially in Information and Communication Technologies (ICT), and the company has invested a lot in supporting children, women and other vulnerable people in Tanzania.

Speaking at the fundraising dinner, the Prime Minister of Tanzania Mr Kassim Majaliwa said the donation was one of the efforts made by various institutions to support the Tanzania Scouts Association (TSA) which will celebrate its 100th birthday 2017, July in Dodoma region.

“This will be in recognition of the memorable contributions that Scouts have made in this country. The Association is the real kiln for producing responsible leaders and executives. It will be during the celebrations that will look back to harness the past to improve the future,” he said

He said that the Tanzania Scouts Association (TSA) is the national Scouting organization of Tanzania. Scouting in Tanzania was founded in 1917, and became a member of the World Organization of the Scout Movement (WOSM) in 1963. The coeducational association has 91,057 members as of 2010.

Minister of Education, Science, Technologies and Vocational Training Prof Joyce Ndalichako who is also TSA President said that scouting is a global, educational Youth movement. It is organized through Scout Associations at National levels including the Tanzania Scouts Association (TSA).

She said that scouting has a clear purpose which includes helping young people to achieve their full physical, intellectual, emotional, social and spiritual potential as individuals, as responsible citizens and as members of the local, national and international community.

“Even though the Scouts cannot solve all the problems of the world, Scouts can help to make it a better place. Scouting makes very positive contribution to society by helping young people to develop as active members of the community who are self reliant, caring, responsible and committed” she said.

JARIDA LA NCHI YETU LA MWEZI FEBRUARY

TANZANIA YAADHIMISHA SIKU YA WANYAMAPORI DUNIANI LEO

Waziri Mahiga akutana na Rais wa Mahakama ya Afrika ya haki za Binadamu na Watu

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifafanua jambo alipokutana na Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Jaji Sylvain Ore yenye Makao Makuu Jijini Arusha,Tanzania. Katika mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Mhe. Wiziri Mahiga mjini Dodoma, wamejadili masuala mbalimbali ya kuboresha miundombinu ya mahakama hiyo ikiwemo majengo ya ofisi ili kuiongezea ufanisi zaidi. 
Mazungumzo yakiendelea; Kushoto ni Wafanyakazi wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu na kulia kwa Rais wa Mahakama, ni Mtumishi wa Wizara Bw. Beatus Kalumuna 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika picha na Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Jaji Sylvain Ore mara baada ya mazungumzo 

Picha ya Pamoja 
Waziri Mhe. Mahiga akiongea na wanahabari (hawapo pichani) mara baada ya mazungumzo 
Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Jaji Sylvain Ore akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mazungumzo

MAMLAKA YA BIMA TANZANIA YAITAKA NIC KUWA KINARA WA BIMA NCHINI

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC), Sam Kamanga kushoto akizungumza na ujumbe wa Mamlaka ya Bima nchini ukiongozwa na Kamishina wa Mamlaka hayo Dk. Baghayo Saqware (kulia), alipotembea Makao Makuu ya NIC jana Jijini Dar es Salaam 
Kamishina wa Mamlaka Bima nchini Dk. Baghayo Saqware,akisisitiza jambo wakati alipotembelea Makao Makuu ya NIC jana. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC), Sam Kamanga kushoto akisisitiza jambo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) mara baada ya ziara hiyo ya ujumbe wa Mamlaka ya Bima Nchini. 
Picha ya pamoja: Mkurugenzi Mtendaji wa NIC Sam Kamanga (wa tatu kushoto) na Kamishina wa Mamkala ya Bima Nchini Dk. Baghayo Sakware (wa Wa nne kushoto) wengine pichani ni maofisa wa taasisi hizo. 

JARIDA LA WIZARA YA NISHATI NA MADINI TOLEO NA. 161

HATMA YA DHAMANA YA MBUNGE LEMA KUJULIKANA LEO JIJINI ARUSHA

$
0
0
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mhe. Freeman Mbowe ( wa pili kutoka kulia) akiwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA Taifa, Dkt. Vincent Mashinji ( Wa kwanza kulia), Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu, Mhe. Edward Lowassa (Wa pili kushoto) na Waziri Mkuu Msaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu, Mhe. Federick Sumaye wakiwa ndani ya Mahakama Kuu jijini Arusha, Leo Ijumaa 03/03/2017 ambapo kesi ya Mbunge wa Arusha, Mhe. Godbless Lema kuhusu dhamana yake.

BADO SIKU MOJA KUTHIBITISHA KWENDA KWENYE MKUTANO WA UWEKEZAJI ITALY

$
0
0
Chemba ya biashara, viwanda na kilimo( TCCIA) inatarajia kufanya ziara ya kibiashara nchini Italy na Uturuki ambapo Chemba inapenda kuwakaribisha  wafanyabiashara walio wanachama na wasio wanachama kuungana nasi kwenye mkutano huu wa wawekezaji. Chemba inawakumbusha kwamba, imabaki siku moja kwa wafanyabiashara wa Italy kuthibitisha ushiriki wao ambapo mwisho ni tarehe 3 March 2017. Kwa 3wafanyabiashara wa Uturuki wana muda mrefu ambapo muda wa mwisho wa kuthibitisha ushiriki wao ni tarehe 30 March 2017. Ziara hii inatarajia kufanyika mwanzoni mwa mwezi May. 
Akizungumza na waandishi wa habari Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TCCIA Ndugu Gotfrid Muganda alisema “Lengo kubwa la ziara hii ni kuwawezesha wafanyabiashara wa Tanzania kutanua wigo wa masoko na fursa za kibiashara na kubadilishana ujuzi”. 

Akizungumza juu ya ziara hiyo Mkurugenzi wa EAG Group ambao ni washauri wa biashara na masoko wa TCCIA Imani Kajula alisema “Ukuzaji wa masoko ya nje ni mkakati endelevu ambao sio tu utaongeza soko nje lakini pia kuleta urari mzuri wa biashara na hivyo kusaidia kuimarisha thamani ya shilingi”. 

 Aliwaambia wafanyabiashara ambao ni wanachama na wasio wanachama wanakaribishwa kijiandikisha ambapo mwisho kwa wanaoenda Italy ni tarehe 3 March 2017.Kwa taarifa zaid helen.mangare@eaggroup.co.tz au muganda@tccia.com.

BALOZI WA KUWAIT , JASEM AL-NAJEM AZINDUA VISIMA VINNE KATIKA SHULE NNE ZA MSINGI MANISPAA YA ILALA

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Ubalozi wa Kuwait nchini umekabidhi visima vinne katika shule za msingi Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam jana.

Shule za Msingi zilizopata visima hivyo ni Yombo, Umoja , Mwale pamoja na Bwawani

Akizungumza wakati wa kukabidhi visima hivyo, Balozi wa Kuwait , Jasem Al-Najem amesema kuwa wanatambua umuhimu wa maji ndio maana wameona umuhimu wa visima hivyo katika shule hizo.

Amesema wataendelea kutoa misaada hiyo kutokana na mahitaji yaliyopo katika jamii kutokana na ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Kuwait.

Al-Najem amesema kuwa wamefanikiwa kuchimba visima 16 vyenye thamani ya Dola za Kimarekani 63,000 na watu wengine wanaweza kujitokeza kusaidia jitihada mbalimbali .

Ubalozi huo pia umekabidhi dawa za binadamu katika Hospitali ya Amana zenye thamani sh.milioni tatu.
Balozi wa Kuwait nchini , Jasem Al-Najem akizundua kisima cha maji katika shule ya Yombo iliyopo Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam jana, Kulia ni Naibu Mkurugenzi wa Red Cresene , Anwari Abdallah Al-Hasawi.
Balozi wa Kuwait nchini , Jasem Al-Najem kushoto na Naibu Mkurugenzi wa Red Cresene , Anwari Abdallah Al-Hasawi wakinywa maji mara baada kuzindua kisima katika shule ya msingi Yombo jana jijini Dar es Salaam.picha zote na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.
Afisa Elimu, Elimu ya Watu Wazima wa Manispaa ya Ilala , Hamisi Mlangala akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa visima ambapo alishukuru msaada huo jana jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem akikabidhi dawa kwa Mganga Mkuu Msaidizi wa Hospitali ya Amana, Amimu Kilomoni jana jijini Dar es Salaam. 
Balozi wa Kuwait nchini , Jasem Al-Najem akitembelea Wodi ya Watoto katika Hospitali ya Amana jana jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Kuwait nchini , Jasem Al-Najem akimsikiliza Mganga Mkuu Msaidizi wa Hospitali ya Amana, Amimu Kilomoni jana jijini Dar es Salaam.
 
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live




Latest Images