Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI FEBRUARY 12,2017


WAZIRI MKUU, MAWAZIRI KUONGOZA MAPAMBANO DAWA ZA KULEVYA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimvalisha cheo kipya aliyekuwa Mkuu wa Chuo cha Uhamiaji Mkoani Kilimanjaro Dkt. Anna Peter Makakala kabla ya kumuapisha kuwa Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha aliyekuwa Mkuu wa Chuo cha Uhamiaji Mkoani Kilimanjaro Dkt. Anna Peter Makakala kuwa Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaini hati ya kiapo baada ya kumuapisha Dkt. Anna Peter Makakala kuwa Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Dkt. Anna Peter Makakala baada ya kumuapisha kuwa Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Bw.Rogers William Sianga kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya Bw.Rogers William Sianga akisaini hati ya kiapo baada ya kuapishwa Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaini hati ya kiapo baada ya kumuapisha Bw.Rogers William Sianga kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Bw.Rogers William Sianga baada ya kumuapisha kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi Omar Yusuf Mzee baada ya kumteua kuwa balozi Leo Jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi Joseph Sokoine baada ya kumteua kuwa balozi Leo Jijini Dar es Salaam. 
Viongozi walioapishwa leo Ikulu Jijini Dar es Salaam wakila kiapo cha Maadili katika utumishu wa umma kilichoongozwa na Kamishna wa Maadili katika Sekretariat ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Mhe. Jaji Harold Nsekela 
Kamishna wa Maadili katika Sekretariat ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Mhe. Jaji Harold Nsekela akiongoza kiapo kwa mabalozi na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya waliopishwa leo Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Mabalozi na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya waliopishwa leo Ikulu Jijini Dar es Salaam wakisaini kiapo cha Maadili katika utumishu wa umma. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati wa Hafla ya kuwaapisha Mabalozi na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya waliopishwa leo Ikulu Jijini Dar es Salaam 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa wakati wa Hafla ya kuwaapisha Mabalozi na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya waliopishwa leo Ikulu Jijini Dar es Salaam
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akiongea na viongozi mbalimbali wa serikali waliohudhuria halfa ya uapishwaji wa Mabalozi na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya ambapo alisisitiza umuhimu wa viongozi wa serikali pamoja na wananchi kuungana kwa pamoja katika mapambano dhidi ya biashara haramu ya Dawa za kulevya. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na viongozi mbalimbali wa serikali waliohudhuria halfa ya uapishwaji wa Mabalozi na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya ambapo aliwataka watanzania na viongozi wenye mamlaka ya kupambana na dawa za kulevya kufanya hivyo ili kuweza kuinusuru Tanzania dhidi ya uingizwaji na uendeleaji wa biashara haramu ya dawa za kulevya. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mawaziri waliohudhuria hafla ya uapishaji wa Mabalozi na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya leo Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha pa pamoja na Mabalozi na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya walioapishwa leo Jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri na Makatibu Wakuu baada ya kuwaapisha Mabalozi na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya Ikulu Jijini Dar es Salaam.

PICHA NA HASSAN SILAYO 

WAZIRI MKUU AKABIDHIWA KAZI YA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA

$
0
0
 Jacquiline Mrisho na Eliphace Marwa – MAELEZO.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemkabidhi Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa kazi ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya akiwa kama Mwenyekiti wa Tume ya Kudhibiti Dawa hizo nchini.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Ikulu Jijini Dar es Salaam wakati akiwaapisha Kamishna Jenerali wa Jeshi la Uhamiaji, Anna Peter Makakala, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers William Sianga pamoja na mabalozi watatu Mhe. Omary Yusuph Mzee, Mhe.Joseph Edward Sokoine pamoja na Mhe. Grace Aron Mgovano aliowateua hivi karibuni.

Dkt. Magufuli amesema kuwa Waziri Mkuu anatajwa kwenye Sheria Na.5 ya mwaka 2015 kuwa ni Mwenyekiti wa Tume hiyo ambapo Wajumbe wake ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Waziri wa Mambo ya Ndani, Waziri wa Elimu ana Mafunzo ya Ufundi, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Waziri wa Fedha na Mipango, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto pamoja na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

“Nalipongeza sana Bunge la kipindi cha mwaka 2010 – 2015 chini ya Spika mstaafu, Mhe. Anne Makinda lililopitisha Sheria hii baada ya kuona sheria za mwanzo za kupambana na dawa za kulevya hazina nguvu hivyo Wabunge wa wakati ule walisimama kwa pamoja bila kujali itikadi za vyama vyao wakapitisha sheria hii,” alisema Dkt. Magufuli.

Aidha, Dkt. Magufuli amempongeza Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete kwa kusaini sheria hiyo haraka mara baada ya Bunge hilo kuipitisha kwa sababu alijua madhara ya dawa za kulevya katika nchi yetu.

Amefafanua kuwa sheria imeeleza wazi katika kifungu cha 10 cha Sheria Na.5 ya mwaka 2015 kuwa jukumu la kupambana na dawa za kulevya linasimamiwa na Serikali pekee yaani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Makamo wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri, Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya au mtu yoyote atakayekuwa amepewa mamlaka ya kusimamia Serikali.

Kwa upande wake Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa amesema kuwa Taifa limeendelea kushuhudia kizazi chetu kikiendelea kudidimia kwa sababu ya matumizi ya dawa za kulevya na Serikali kwa mipango yake imeendelea kukemea, kudhibiti na kuchukua hatua mbalimbali dhidi ya wazalishaji, wasambazaji, wauzaji na watumiaji wa dawa hizo.

“Jambo hili limeleta athari kubwa sana kwani vijana wetu wengi wamepoteza uwezo wa kujisimamia katika shughuli zao za maendeleo kwa sababu baada ya matumizi tumeona athari kadhaa zikiwezo za kudhoofishwa kwa mwili, uwezo wa kutafakari pamoja na kutoweka kwa uwezo wa kufanya kazi,”alisema Waziri Mkuu Majaliwa.

Waziri Mkuu Majaliwa ameongeza kuwa Taifa hili la Watanzania kwa kiasi kikubwa linawategemea vijana waweze kuleta msukumo wa maendeleo ndani ya nchi hivyo jambo hili likiachiwa linaweza kuleta athari kubwa katika ukuaji wa uchumi na maendeleo yetu kwa ujumla wake.

Alisisitiza kuwa vita hii ilianza, inaendelea na itaendelea kupiganwa hadi imalizike hivyo Watanzania hawana budi kuunga mkono jitihada zozote zinazofanywa na Serikali kuhakikisha wanatokomeza uzalishaji, usambazaji, uuzaji na matumizi yake kwa namna yoyote ile, kila mmoja anatakiwa kushiriki kikamilifu ili kubaini matumizi ya dawa za kulevya ndani ya nchi hii.

RAIS DKT. MAGUFULI AMWAPISHA KAMISHNA JENERALI WA UHAMIAJI, KAMISHNA MKUU WA MAMLAKA YA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA PAMOJA NA MABALOZI WATATU IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala Ikulu jijini Dar es Salaam.
kam2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya Rogers William Sianga Ikulu jijini Dar es Salaam.
kam4
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi  Joseph Sokoine kuwa Balozi mpya nchini Ubelgiji, Ikulu jijini Dar es Salaam.
kam5
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi Omar Yusuph Mzee kuwa Balozi mpya nchini Algeria, Ikulu jijini Dar es Salaam.
kam7
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Grace Mgovano kuwa Balozi nchini Uganda, Ikulu jijini Dar es Salaam.
kam8
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi  katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali walioapishwa leo Ikulu jijini Dar es Salaam.
kam9
AHADI YA UADILIFU. Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala wakwanza kulia akiwa na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya Rogers William, Balozi  Joseph Sokoine, Balozi Omar Yusuph Mzee pamoja na Balozi Grace Mgovano wakila kiapo cha Ahadi ya Udilifu kwa viongozi mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salam.
kam11
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mara baada ya kuwaapisha Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za kulevya, pamoja na Mabalozi watatu Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU
kam12kam13
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mara baada ya kuwaapisha Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za kulevya, pamoja na Mabalozi watatu Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU



MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO AONGOZA MAZOEZI KUITIKIA AGIZO LA MAKAMU WA RAIS.

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Saidi Mecki Sadiki akiwa na viongozi wengine wa kiserikali wakiowaongoza watumishi wa kada mbalimbali ,watumishi wa umma,wanafunzi wa shule za msingi na sekondari katika uzinduzi wa kampeni ya kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza kwa njia ya mazoezi kimkoa.
Washiriki wa zoezi hilo wakipita maeneo mbalimbali ya mji  Moshi kwa kutembea na kukimbia kidogo kidogo.
Mazoezi ya awali ya kukimbia na kutembea yaliyoanzia ofsi ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,yalihitimishwa kwa mazoezi ya viungo katika uwanja wa Chuo Kikuu  chuo kikuu cha Ushirika mjini Moshi.
Askari kutoka vikosi mbalimbali vya Jeshi la Polisi pia walishiriki vyema mazoezi hayo.
Katibu Tawala mkoa wa Kilimanjaro,Mhandisi Aisha Amour alikuwa ni miongoni mwa washiriki katika mazoezi hayo.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi,Joyce Msiru pia alishiriki katika mazoezi hayo.
Wanafunzi kutoka shue mbalimbali za sekondari na msingi pia walikuwepo.
Jeshi la Magereza pia liliwakilishwa vyema na baadhi ya askari wake.Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

WAZIRI MKUU AKABIDHIWA KAZI YA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA

$
0
0
Jacquiline Mrisho na Eliphace Marwa – MAELEZO.
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemkabidhi Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa kazi ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya akiwa kama Mwenyekiti wa Tume ya Kudhibiti Dawa hizo nchini.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Ikulu Jijini Dar es Salaam wakati akiwaapisha Kamishna Jenerali wa Jeshi la Uhamiaji, Anna Peter Makakala, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers William Sianga pamoja na mabalozi watatu Mhe. Omary Yusuph Mzee, Mhe.Joseph Edward Sokoine pamoja na Mhe. Grace Aron Mgovano aliowateua hivi karibuni.

Dkt. Magufuli amesema kuwa Waziri Mkuu anatajwa kwenye Sheria Na.5 ya mwaka 2015 kuwa ni Mwenyekiti wa Tume hiyo ambapo Wajumbe wake ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Waziri wa Mambo ya Ndani, Waziri wa Elimu ana Mafunzo ya Ufundi, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Waziri wa Fedha na Mipango, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto pamoja na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

“Nalipongeza sana Bunge la kipindi cha mwaka 2010 – 2015 chini ya Spika mstaafu, Mhe. Anne Makinda lililopitisha Sheria hii baada ya kuona sheria za mwanzo za kupambana na dawa za kulevya hazina nguvu hivyo Wabunge wa wakati ule walisimama kwa pamoja bila kujali itikadi za vyama vyao wakapitisha sheria hii,” alisema Dkt. Magufuli.

Aidha, Dkt. Magufuli amempongeza Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete kwa kusaini sheria hiyo haraka mara baada ya Bunge hilo kuipitisha kwa sababu alijua madhara ya dawa za kulevya katika nchi yetu.

Amefafanua kuwa sheria imeeleza wazi katika kifungu cha 10 cha Sheria Na.5 ya mwaka 2015 kuwa jukumu la kupambana na dawa za kulevya linasimamiwa na Serikali pekee yaani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Makamo wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri, Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya au mtu yoyote atakayekuwa amepewa mamlaka ya kusimamia Serikali.

Kwa upande wake Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa amesema kuwa Taifa limeendelea kushuhudia kizazi chetu kikiendelea kudidimia kwa sababu ya matumizi ya dawa za kulevya na Serikali kwa mipango yake imeendelea kukemea, kudhibiti na kuchukua hatua mbalimbali dhidi ya wazalishaji, wasambazaji, wauzaji na watumiaji wa dawa hizo.

“Jambo hili limeleta athari kubwa sana kwani vijana wetu wengi wamepoteza uwezo wa kujisimamia katika shughuli zao za maendeleo kwa sababu baada ya matumizi tumeona athari kadhaa zikiwezo za kudhoofishwa kwa mwili, uwezo wa kutafakari pamoja na kutoweka kwa uwezo wa kufanya kazi,”alisema Waziri Mkuu Majaliwa.

Waziri Mkuu Majaliwa ameongeza kuwa Taifa hili la Watanzania kwa kiasi kikubwa linawategemea vijana waweze kuleta msukumo wa maendeleo ndani ya nchi hivyo jambo hili likiachiwa linaweza kuleta athari kubwa katika ukuaji wa uchumi na maendeleo yetu kwa ujumla wake.

Alisisitiza kuwa vita hii ilianza, inaendelea na itaendelea kupiganwa hadi imalizike hivyo Watanzania hawana budi kuunga mkono jitihada zozote zinazofanywa na Serikali kuhakikisha wanatokomeza uzalishaji, usambazaji, uuzaji na matumizi yake kwa namna yoyote ile, kila mmoja anatakiwa kushiriki kikamilifu ili kubaini matumizi ya dawa za kulevya ndani ya nchi hii.

POSHO ZA MADIWANI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA WILAYA YA MBINGA MILIONI 47 KATIKA VIKAO VYA BAJETI, WAMEAMUA ZIENDE KUMALIZIA MILADI.

$
0
0
Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga, mkoani Ruvuma wameamua kutochukua posho zao za vikao viwili vya bajeti ambazo ni shilingi milioni 47, badala yake ziende zikatumike kumalizia miladi ya maendeleo ambayo imesimama katika halmashauri hiyo. Kwa undani wa habari hii hii hapa video yake.

KIPINDI MAALUM HOTUBA YA RAIS DKT MAGUFULI BAADA YA KUMUAPISHA KAMISHNA WA DAWA ZA KULEVYA


VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMATATU FEBRUARY 13,2017

DC MUWANGO AIAMURU HALMASHAURI YA WILAYA YA NACHINGWEA KUREJESHA MAENEO YA ARDHI YALIYOVAMIWA

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mhe Rukia Muwango akisisitiza umuhimu wa kufanya mazoezi
Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mhe Rukia Muwango akionyesha mfano wa ufanayaji mazoezi
Mkuu wa wilaya ya Nachingwea ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa Wilaya hiyo Mhe Rukia Muwango akifanya mazoezi katika uzinduzi huo
 Matembezi yakiendelea vyema

Na Mathias Canal, Lindi

Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mhe Rukia Muwango ameitaka Halmashauri ya Wilaya hiyo irejeshe maeneo yote ya wazi yaliyo vamiwa na kutumika kinyume cha matumizi yaliyolengwa.

Dc Muwango ametoa agizo hilo mjini Nachingwea kwenye uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya kudhibiti magonjwa yasioambukiza na yanayoweza kuzuilika kupitia mazoezi na michezo.

Uzinduzi huo uliofanyika katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine ambapo Alisema kuwa yeye kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo anatambua na anazotaarifa za kutosha kuwa maeneo mengi ambayo yalitengwa kwa ajili michezo na shuguli nyingine za umma yamevamiwa na kubadilishwa matumizi.

Dc Muwango ameitaka halmashauri hiyo kurejesha haraka kutoka mikononi mwa wavamizi.

Katika hali inayoonesha kuwa mkuu huyo wa Wilaya amelivalia njuga suala hilo, ameitaka Halmashauri hiyo ipeleke na kumkabidhi mikakati na taarifa za utekelezaji wa agizo lake haraka iwezekanavyo.

Sambamba na agizo hilo Muwango ameitaka Halmashauri hiyo kutenga maeneo kwa ajili ya michezo.Amebainisha kuwa bila kuwa na maeneo ya wazi itakuwa vigumu kufanikiwa kukuza michezo na kuibua vipaji mbalimbali vya wanamichezo.

Amemuagiza Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kuwaandikia wakuu wa shule za sekondari na walimu wakuu wa shule za msingi ili warejeshe mbio za mchakamchaka kwenye shule zao kwani shule nyingi wanafunzi hawakimbii mchakamchaka.

"Jambo ambalo ni muhimu kwa afya na akili za wanafunz ila walimu wawe na usimamizi mzuri ili wanafunzi wasiathiriwe katika masomo na usalama wao," Alisistiza Muwango.

Akizungumzia umuhimu wa michezo na mazoezi Dc Muwango alisema kuwa licha ya kuimarisha, umoja,undugu na mshikamano.Lakini pia mazoezi na michezo ni kichocheo kikubwa cha maendeleo, utulivu na amani katika jamii.

Alibainisha kuwa chanzo cha baadhi ya migogoro katika baadhi ya jamii ni magonjwa ambayo yanaweza kuepukwa kwa kufanya mazoezi ambapo Hata hivyo jamii husika hazitambui jbo hilo Badala yake inayahusisha magonjwa hayo na sababu zisizo na msingi Ikiwa ni pamoja na Imani potofu, uchawi na ushirikina mambo ambayo hupelekea kunyoosheana vidole na kusababisha migogoro.

"Lakini mtu akiwa mgonjwa hawezi kufanya shuguli za kiuchumi na maendeleo yake mwenyewe, Taifa na hata wanaomuuguza hawawezi kufanya kazi ambazo zingewaletea maendeleo," Aliongeza Muwango.

Mkuu huyo wa Wilaya alitoa wito kwa wananchi wilayani humo kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi bila kujali rika Huku akiwaasa kuunda vikundi vya michezo na mazoezi Kwa sababu madhara ya kutofanya mazoezi ni makubwa ambapo sio rahisi kuyabaini haraka.

Uzinduzi huo ambao ni utekelezaji wa agizo la makamu wa Rais aliyetaka kuwe na kampeni ya kitaifa ya kudhibiti magonjwa yasioambukiza na yanayozuilika kupitia michezo uliandaliwa na ofisi ya mkuu huyo wa wilaya ya Nachingwea Ambapo michezo mbalimbali ilichezwa, sambamba na upimaji wa afya na uchangiaji damu kwa hiari.

RC Rukwa akutana na wadhibiti ubora wa shule kujua chanzo cha kushuka kwa elimu RukwaB

$
0
0


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen amekutana na wadhibiti ubora wa shule wa halmashauri nne za Mkoa wa Rukwa kujua changamoto wanazokumbana nazo na mambo yanayopelekea kushuka kwa elimu katika mkoa wa Rukwa.


Zelote Stephen alifikia uamuzi wa kuwaita wadhibiti hao baada ya Mkoa wa Rukwa kushuka kielimu kutoka nafasi ya 6 mwaka 2015 hadi nafasi ya 12 kati ya Mikoa 31 kwa mwaka 2016 kwa mitihani ya kidato cha 4, na pia kuteremka katika mitihani ya kidato cha pili kutoka nafasi ya 20 kwa mwaka 2015 hadi nafasi ya 21 kwa mwaka 2016.


Wadhibiti hao walielezea sababu kede kede zilizopelekea kushuka kwa kiwango cha elimu katika Mkoa wa Rukwa na miongoni mwao ni kutopewa mrejesho wa taarifa za kila wiki wanazoziandika na kukabidhi kwa wakurugenzi wa halmashauri na wakuu wa wilaya.


“Toka Mwezi July mwaka jana tumeshaandika ripoti nyingi tu zinazoelezea mapungufu kama vile, upungufu wa waalimu kwa baadhi ya masomo, matundu cha vyoo, vitabu vya kusomea, nakadhalika lakini hakuna hata mrejesho tunaoupata kutoka kwa Mkurugenzi,” Goreth Ntulo alieleza.


Kwa upande mwingine sababu zinazokwamisha ufanisi wa kazi za wadhibiti hao wanadai kutopewa motisha na mwajiri wao na kuwasababisha kuishi katika maisha magumu.


“Mimi sijawahi kwenda likizo kwa fedha ya serikali tangu nianze kufanya kazi na madarasha hatupandishwi n ahata ukipandishwa inabaki jina tu lakini mshahara upo pale pale na kuapata hiyo fedha ya daraja ulilopandishwa ni kazi kubwa ya kukatisha tamaa,” Mmoja wa wadhibiti hao Mama Jairo alifafanua.


Nae Mkuu wa Mkoa baada ya kusikiliza malalamiko hayo aliwaagiza wakurugenzi wote kuhakikisha kwamba wadhibiti hao wanapatiwa mrejesho juu ya kasoro walizozibaini baada ya kufanya ukaguzi katika mashule hayo.


“Kwani hizi shule ni za nani?, Si ni za wakurugenzi, sasa naagiza wakurugenzi wote wawe wanatoa mrejesho kwenu ili muweze kujua ni lipi linawezekana kurekebishika na kwa kipindi gani na nili lipi haliwezekani ili Mkae mkijua, bila ya hivyo itakuwa haina maana nyinyi kufanya ukaguzi halafu ripoti zikarundikwa kwenye madroo,” Zelote Stephen alikazia.


Pia Mkuu wa Mkoa aliwasisitiza wakati wakaguzi hao wanawapa wakurugenzi ripoti hizo wahakikishe kuwa wanawapa na “dead line” na wakurugeni wazingatie na wawaheshimu na kuwathamini ili kila mmoja afanye kazi yake ambayo ameajiriwa nayo.


“Kama Mlikuwa na uwoga muondoe ofisi hii itawapa sapote, na make mkijua kuwa tunawathamini sana maana kupitia nyinyi tunajifunza mengi sana ambayo ndio yanatupa mpango mkakati wa kuhakikisha tunapeleka elimu mbele,” Zelote Stephen aliwahakikishia.


Mmoja wa wadhibiti hao Pracida Rwegasira alitoa shukrani zake za dhati kwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa kwa kuchukua uamuzi wa kuwaita ili kutoa mchango wao katika kupeleka sekta ya elimu mbele na kuongeza kuwa tokea aanze kazi hiyo hawajawahi kuitwa na Mkuu wa Mkoa.


Nae Katibu Tawala wa Mkoa Tixon Nzunda aliahidi kutetea haki zao za kiutumishi na kuwa sauti ya kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elmu.


Imeandikwa na

Abdulrahman Salim

Kaimu Afisa habari Mkoa wa Rukwa

RC KILIMANJARO NA KAMISHNA MTEULE WA MAMLAKA YA YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA WATEMA CHECHE.

$
0
0
Kamishna Mteule wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za kulevya,Rogers William akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa mazoezi kwa wananchi mkoa wa Kilimanjaro,uzinduzi uliofanyika katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi.
Viongozi wa Serikali walioshiriki katika uzinduzi huo,kutoka kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kippi Warioba,Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Saidi Meck Sadiki ,Mkuu wa wilaya ya Hai,Gelasius Byakanwa na Katibu Tawala mkoa wa Kilimanjaro, Mhandisi Aisha Amour.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Saidi Meck Sadiki akizungumza juu ya Dawa za kulevya mara baada ya kumalizika uzinduzi rasmi wa siku ya mazoezi ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Makamu wa Rais ,Samia Suluhu Hassan.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna msaidizi Mwandamizi wa  Polisi,Wilbroad Mutafungwa akitoa salamu za jeshi hilo katika uzinduzi huo.
Baadhi ya viongozi wakifuatilia hotuba ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,(hayupo pichani) 
Mkuu wa Wilaya ya Hai,Gelasius Byakanwa akisalimia katika uzinduzi huo.
Katibu Tawala wilaya ya Hai,Upendo Welaakitoa salamu wakati wa uzinduzi huo.
Mwakilishi wa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi,Dkt Cyril Chami akitoa neno la ukaribisho katika uzinduzi huo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

SIKU chache  baada ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Dkt John Pombe Magufuli kuwa Kamishna wa mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (Drug Control and enforcement Authority), Rogers William ameanza kutema cheche dhidi ya Wafanyabiara na watumiaji wa dawa za lulevya.

Kamishna huyo  ametangaza kushughulika kikamilifu na baadhi ya wafanyabiashara mkoani Kilimanjaro,wanaowatumia wanawake wajasiriamali wanaosafirisha mazao kwenda mikoani, kubeba Mirungi ama Bangi ndani ya mizigo ya mazao.

William alitoa kauli hiyo wakati wa mazoezi katika uwanja wa Chuo kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) baada ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro , Saidi Mecky Sadiki kutoa nafasi kwa Mkuu huyo wa usalama wa taifa mkoa wa Kilimanjaro , baada ya kumpongeza kwa kuteuliwa kwake.

“Tunayo orodha ya wafanyabiashara wasio waaminifu na wengine wananchi wa kawaida wanaowatumia wanawake wasio na hatia kusafirisha dawa za kulevya kama Mirungi na Bangi kwenda mikoani….hilo nitahangaika nalo mara nitakaporejea mkoani hapa katika mapambano dhidi ya vita hii”alisema Sadiki.

Kauli ya William ilifuatia baada ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Saidi Meck Sadiki kulitaka jeshi la Polisi kufaya uchungizi wa kina ili kuwaachia baadhi ya wanawake watakaobainika kutokuwa na hatia ama kufahamu kama walitumika kusafirisha dawa za kulevya bila ridhaa yao.

Akizungumzia kuhusu Dawa za kulevya,Sadiki alisema vita dhidi ya dawa  za kulevya za aina mbalimbali kwa mkoa wa Kilimanjaro imeanza muda mrefu na tayari zaidi ya watuhumiwa 689 wa dawa hizo wanashikiliwa katika kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Januari mwaka 2016 hadi Januari 2017.

Sadiki alisema vita hiyo ni ya kudumu yenye changamoto kubwa baada ya mkoa wa Kilimanjaro kuwa na njia nyingi za Panya katika mipaka baina ya Tanzania na Kenya, huku ikizingatiwa kwamba Kenya inalitumia zao la Mirungi kama biashara halali.

“Watuhumiwa walikutwa na makosa 626 ambapo watuhumiwa 103 walifikishwa mahakamani nakupata adhabu za aina mbalimbali ikiwamo vifungo na faini ambapo wawili miongoni mwao walifungwa vifungo vya maisha gerezani na kesi 136 zinaendelea mahakamani”alisema Sadiki.

Sadiki alisema kadhalika watuhumiwa wengine 296 walikamatwa na Tani nne za Mirungi, watuhumiwa wengine 284 walikutwa na kilo 424 za bangi, huku magari matano na pikipiki 20 zikishikiliwa na polisi kwa tuhuma za kusafirisha dawa za kulenywa aina ya Mirungi na Bangi.

”Tumekuwa tukiendesha kampeni ya kukabiliana na dawa za kulevya kila wakati na kampeni hii ni ya kudumu, nawaasa vijana kuachana na biashara hiyo na badala yake watafute biashara halali”alisema Sadiki.

Aidha mkuu wa mkoa aliwataka wafanyabiashara na watumiaji wa dawa za kulevya wanaokimbia msako jijini Dar es salaam kutokimbilia mkoani mwake kwani kampeni ni ile ile na watakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Mwisho.

BANK OF AFRICA TANZANIA YAFUNGUA MATAWI MWANZA NA MOROGORO

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe John Mongella akizindua rasmi tawi la Nyanza-Mwanza na lile la Uluguru-Morogoro

Naibu Mkurugenzi mtendaji wa Bank of Africa Tanzania Wasia Mushi akimkabidhi mkuu wa mkoa wa Mwanza zawadi ya Visa Prepaid Card (TOUCAN CARD) ambayo itamwezesha mkuu huyo wa mkoa kufanya online purchases pamoja na kupata huduma za kifedha kwenye ATM machine Zaidi ya Milioni tatu zilizopo sehemu mbalimbali duniani.

Naibu Mkurugenzi mtendaji wa Bank of Africa Tanzania Wasia Mushi akitoa hotuba katika uzinduzi wa matawi mawili ya Bank of Africa Tanzania Mwanza na Morogoro. Uzinduzi wa matawi haya unafanya benki hiyo kua na jumla ya matawi 27 nchi nzima.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mh. John Mongella akitoa hotuba yake katika halfla ya uzinduzi rasmi wa matawi mawil ya Bank of Africa Tanzania.


Akizungumza mkoani Mwanza, wakati akizindua matawi mawili kwa pamoja ya Bank of Africa Tanzania tawi la Nyanza lililopo jijini Mwanza na wakati huo huo tawi la Uluguru lililopo jijini Morogoro, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh. John Mongella alisema ni wakati wa wanaMwanza kutumia huduma za kibenki na kwamba Mwanza ni ya pili kuchangia katika pato la taifa.

“Nimesikia kwamba mna matawi 27, huu ni wakati wa wanaMwanza kutumia huduma za kibenki. Naomba mfahamu kwamba Mwanza inachangia asilimia 7 ya pato la taifa. Bank of Africa Tanzania natambua kuwa mnasaidia juhudi za serikali kufikisha huduma za kifedha kwa wananchi,”alisema Mh. Mongella.

Awali akizungumza kabla ya ufunguzi wa matawi hayo kwa pamoja, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Bank of Africa Tanzania, Wasia Mushi alisema : “Benki ya Afrika ipo katika nchi 18 na kwamba makao yake makuu yapo Dakar, Senegal. Hapa nchini ina makao yake makuu jijini Dar es Salaam na jumla ya matawi 27.”

Mushi alisema katika kipindi cha miaka 10 benki hiyo imekuwa benki muhimu, imara endelevu kwa kutoa huduma zake za kibenki kwa watu mbalimbali wakiwamo wateja wakubwa, wadogo na wa kati.

“Mwanza inajulikana zaidi kwa shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwemo uvuvi katika Ziwa Victoria, uchimbaji wa madini, kilimo cha pamba na utoaji wa huduma katika sekta mbalibali, hivyo ni muhimu wakatumia huduma za Bank of Africa Tanzania,”alisema.

Alisema benki hiyo imedhamiria kuleta mapinduzi kwenye sekta za kibenki kwa kutoa huduma stahiki ambazo zitaweza kumfikia kila Mtanzania kwa njia nyepesi kupitia wafanyakazi wao.

“Tawi la Nyanza na tawi la Uluguru yote yamefunguliwa kwa pamoja, hii ni benki ya biashara ambayo imeanzishwa mwaka 2007. Leo ina matawi 27 katika maeneo mbalimbali nchini”

Alisema kwa sasa benki hiyo inatoa mikopo mbalimbali ikiwamo ya ukarabati wa nyumba, kutumia nyumba kama dhamana ya kupata mitaji ya biashara au kusaidia kujenga nyumba nyingine.

“Kwa pamoja Bank of Africa Tanzania imeungana na shirika la maendeleo la Ufaransa AFD kwa manufaa ya kuwezesha watu mbalimbali wanao jikita kwenye shughuli za nishati endelevu na mbadala,”alisema Mushi.

Utamaduni wa Mtanzania ni Sehemu ya Kivutio cha Utalii: Waziri Nape.

$
0
0


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye akipiga Gitaa lililotengenezwa na Msaanii wa Uchoraji na Uchongaji Bw. Washington Steven Masanja (kushoto) wakati wa kilele cha Maonyesho ya Wiki ya Utamaduni baina ya Shiraz na Tanzania jana jijini Dar es Salaam.Maonyesho hayo yalikuwa na kauli mbiu ya “Ushirikiano wa Kiutamaduni ni nguzo muhimu ya kukuza na kuendeleza Lugha,Sanaa na Filamu,Mila na desturi zake”. Kushoto kwa Waziri ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo.
NP1
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye akizungumza wakati wa kilele cha Maonyesho ya Wiki ya Utamaduni baina ya Shiraz na Tanzania jana jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo yalikuwa na kauli mbiu ya “Ushirikiano wa Kiutamaduni ni nguzo muhimu ya kukuza na kuendeleza Lugha,Sanaa na Filamu,Mila na desturi zake”.
NP2
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Makumbusho ya Taifa Profesa Audax Mabulla akizungumza wakati wa kilele cha Maonyesho ya Wiki ya Utamaduni baina ya Shiraz na Tanzania jana jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo yalikuwa na kauli mbiu ya “Ushirikiano wa Kiutamaduni ni nguzo muhimu ya kukuza na kuendeleza Lugha,Sanaa na Filamu,Mila na desturi zake”.
NP3
Balozi wa Jamhuri ya Watu wa Iran nchini Tanzania Mossa Farharng (wa pili kutoka kushoto) akifuatilia hotuba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye (hayupo pichani) wakati wa kilele cha Wiki ya Utamaduni wa Shiraz iliyofanyika katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Makumbusho ya Taifa Profesa Audax Mabulla, Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni cha Iran Ali Bagheri na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo.
NP4
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye akicheza Bao na Mwenyekiti wa Shirikisho la Michezo ya Jadi Tanzania Bw. Mohamed Kazingumbe (kulia) wakati wa kilele cha Maonyesho ya Wiki ya Utamaduni baina ya Shiraz na Tanzania jana jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo yalikuwa na kauli mbiu ya “Ushirikiano wa Kiutamaduni ni nguzo muhimu ya kukuza na kuendeleza Lugha,Sanaa na Filamu,Mila na desturi zake”.
NP5
Baadhi ya Wasanii kutoka Iran wakitumbuiza muziki wa Ala wakati wa kilele cha Maonyesho ya Wiki ya Utamaduni baina ya Shiraz na Tanzania jana jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo yalikuwa na kauli mbiu ya “Ushirikiano wa Kiutamaduni ni nguzo muhimu ya kukuza na kuendeleza Lugha,Sanaa na Filamu,Mila na desturi zake”.
NP6
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye akiangalia moja ya vitabu vyenye maneno ya Kishiraz wakati wa kilele cha Maonyesho ya Wiki ya Utamaduni baina ya Shiraz na Tanzania jana jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo yalikuwa na kauli mbiu ya “Ushirikiano wa Kiutamaduni ni nguzo muhimu ya kukuza na kuendeleza Lugha,Sanaa na Filamu,Mila na desturi zake”. Kutoka kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni Bibi. Lilian Beleko, Balozi wa Iran nchini Mossa Farharng na Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni cha Iran Ali Bagheri.
NP7
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye akisikiliza maelezo kuhusu michoro ya Kiutamaduni ya Iran wakati wa kilele cha Maonyesho ya Wiki ya Utamaduni baina ya Shiraz na Tanzania jana jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo yalikuwa na kauli mbiu ya “Ushirikiano wa Kiutamaduni ni nguzo muhimu ya kukuza na kuendeleza Lugha,Sanaa na Filamu,Mila na desturi zake”.
NP8
: Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa Utamaduni wa Bodi ya Filamu Tanzania Bw. Benson Mkenda alipotembelea meza ya Bodi hiyo wakati wa kilele cha Maonyesho ya Wiki ya Utamaduni baina ya Shiraz na Tanzania jana jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo yalikuwa na kauli mbiu ya “Ushirikiano wa Kiutamaduni ni nguzo muhimu ya kukuza na kuendeleza Lugha,Sanaa na Filamu,Mila na desturi zake”.
NP9
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye akifurahia jambo mara baada ya kupata maelezo ya namna ya kufanya marekebisho ya Vitabu kutoka kwa Ali Navidogooe Shiraz wakati wa kilele cha Maonyesho ya Wiki ya Utamaduni baina ya Shiraz na Tanzania jana jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo yalikuwa na kauli mbiu ya “Ushirikiano wa Kiutamaduni ni nguzo muhimu ya kukuza na kuendeleza Lugha,Sanaa na Filamu,Mila na desturi zake”.
NP10
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye akipiga Gitaa  lililotengenezwa na Msaanii wa Uchoraji na Uchongaji Bw. Washington Steven Masanja (kushoto) wakati wa kilele cha Maonyesho ya Wiki ya Utamaduni baina ya Shiraz na Tanzania jana jijini Dar es Salaam.Maonyesho hayo yalikuwa na kauli mbiu ya “Ushirikiano wa Kiutamaduni ni nguzo muhimu ya kukuza na kuendeleza Lugha,Sanaa na Filamu,Mila na desturi zake”. Kushoto kwa Waziri ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo.
NP11
Wasanii wa Mashairi Bw. Issa Amiri Kilimo aka. Kijoka Kidogo na Mwajuma Seleman Yombe wakiimba shairi kwa njia ya majibizano ikiwa ni kujibu shairi la Siri la mtunzi Haji Myaka bin Haji la mwaka 1405 jana jijini Dar es Salaam wakati wa kilele cha Maonyesho ya Wiki ya Utamaduni baina ya Shiraz na Tanzania.
NP12
Balozi wa Jamhuri ya Watu wa Iran nchini Tanzania Mossa Farharng akimkabidhi zawadi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye  wakati wa kilele cha Wiki ya Utamaduni wa Shiraz iliyofanyika katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam jana. 
NP13
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye akifurahia jambo na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa Iran nchini Tanzania Mossa Farharng wakati wa kilele cha Wiki ya Utamaduni wa Shiraz iliyofanyika katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam jana. 
NP14
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa Iran nchini Tanzania Mossa Farharng na baadhi ya viongozi kutoka taasisi za Serikali na ubalozi wa Iran wakati wa kilele cha Wiki ya Utamaduni wa Shiraz iliyofanyika katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam jana. 
Picha na: Frank Shija – MAELEZO.
…………………………………………………………
Na Shamimu Nyaki-WHUSM.
 Serikali chini ya Wizara ya Hbari Utamaduni Sanaa na Michezo inaendelea na juhudi za kuhakikisha kuwa Utamaduni wa Mtanzania unakuwa sehemu ya muhimu ya kivutio cha Utalii ili kutengeneza ajira na kuingizia Serikali mapato.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye alipokuwa anafungwa maadhimisho ya wiki ya Utamaduni wa Washirazi yaliyofanyika jana Jijini Dar es Salaam ambapo amesema kuwa madhimisho haya yanaimarisha undugu wa damu wa kiuchumi na kiutamaduni ulioachwa na wahenga.
“Maadhimisho ya wiki ya Utamaduni wa Shirazi ni fursa pekee ya kujifunza kutoka kwa kwa wairani namna ya kukuza ,kulinda na kuendeleza Utamaduni,Sanaa,Filamu,Mila na Desturi zetu”Alisema Waziri Nape.
Aidha ameongeza kuwa Wizara yake  itaweza kufanikisha shughuli za Utamaduni na kuziendeleza  kwa kushirikiana na wadau  wa ndani na nje ya ya nchi  kama ilivyofanyika katika maadhimisho ya mwaka huu kwani yanatangaza vikundi vya Sanaa na Wasanii.
Kwa upande wa wake Mkuu wa Kituo cha Utamaduni cha Irani hapa nchini Bw.Ally Baghari amesema kuwa ushirikiano wa Kiutamaduni baina ya Tanzania na Irani umeongeza mafanikio ya kiuchumi na kijamii katika nchi hizo hasa kupitia ubadilishanaji wa Utamaduni tangu enzi za ukoloni.
“Tumejifunza utamaduni  wa kitanzania kupitia maadhimisho haya na tunaamini watanzania pia wamejifunza utamaduni wa Irani ambao umesaidia kuimarisha ushirikiano wetu”Alisema Bw Baghari.
Maadhimisho hayo yaliyokuwa na kauli mbiu “Ushirikiano wa Kiutamaduni ni nguzo muhimu ya kukuza na kuendeleza Lugha,Sanaa na Filamu,Mila na desturi zake”.

Barclays kuendelea kuwekeza nchini, yafungua tawi mjini Morogoro

$
0
0
 Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Barclays Tanzania, Simon Mponji (katikati), akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa tawi la kisasa la benki hiyo katika jengo la Shirika la Nyumba (NHC), mjini Morogoro mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Barclays Tanzania, Abdi Mohamed na kulia ni  Mjumbe wa Bodi ya benki hiyo, Dk. Suleman Mohamed.
 Mkuu wa Mauzo wa Benki ya Barclays Tanzania, (kushoto), akieleza kuhusu huduma mbalimbali za kibenki zitolewazo katika tawi jipya Barclays la mjini Morogoro katika sherehe za uzinduzi wa tawi hilo juzi. Wengine kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji, Abdi Mohamed, mjumbe wa bodi, Dk. Suleman Mohamed na Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Barclays, Simon Mponji .

 Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Barclays Tanzania, Simon Mponji (wa pili kulia), akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya uzinduzi rasmi wa tawi jipya la benki hiyo mjini Morogoro. Wengine kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Barclays, Abdi Mohamed na  Mjumbe wa Bodi ya benki hiyo, Dk. Suleman Mohamed.
  Meneja Masoko wa Barclays, Joe Bendera (kulia) akibadilishana mawazo na baadhi ya wateja wa benki hiyo waliohudhuria hafla ya uzunduzi wa tawi hilo. 
  Wafanyakazi wa Benki ya Barclays Tawi la Morogoro wakipiga picha ya kumbukumbu pamoja na baadhi ya viongozi wa benki hiyo mara baada ya hafla ya uzinduzi wa tawi hilo.
Moja ya burudani zilizokuwepo wakati wa hafla ya uzinduzi wa tawi la Benki ya Barclays mjini Morogoro juzi.

MAANDALIZI YA TAMASHA LA PASAKA YANAENDELEA.

$
0
0
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya Tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika wakati wa sikukuu ya Pasaka jijini Dar es salaam, Msama amesema maadalizi yanaendelea vizuri na wako kwenye mazungumo na waimbaji kutoka mataifa mbalimbali kama vile Rwanda, Nigeria, Afrika Kusini Zambia na kwingineko ili kuboresha Tamasha hilo ambalo pia litafanyika katika mikoa kumi ya Tanzania.

Ameongeza kwamba Tamasha la mwaka huu pia lina kazi kubwa ya kumuombea Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dk.John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya kuleta Maendeleo kwa watanzania lakini pia kupambana na vita mbaya ya Madawa ya Kulevya.
2
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya Tamashahilo wakati alipozungumza na jijini Dar es salaam jana.

VALENTINE'S DAY AT SHEKINAH GARDEN, MBEZI BEACH (MAKONDE)

RC MAKONDA AKABIDHI ORODHA YA MAJINA 97 YA WAUZA MADAWA YA KULEVYA KWA KAMISHNA MKUU WA MAMLAKA YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA JIJINI DAR LEO

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akionyesha majina mengine 97 ya wauza Dawa za Kulevya awamu ya tatu kwa Bw. Rogers William Sianga Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya ili yaanze kushughulikiwa. RC Makonda amesema awamu hii itaitikisa nchi kwani wameanzia toka awamu ya pili iliyoongozwa na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi na kuendelea mpaka awamu ya sasa ya Rais Dkt John Pombe Magufuli, , Katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere JNCC.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akikabidhi majina mengine 97 kwa kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa Bw. Rogers William Sianga, kuwa ili yaanze kushughulikiwa.RC Makonda amesema awamu hii itaitikisa nchi kwani wameanzia toka awamu ya pili iliyoongozwa na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi na kuendelea mpaka awamu ya sasa ya Rais Dkt John Pombe Magufuli, , Katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere JNCC.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akizungumza katika mkutano huo,ambapo amekabidhi majina mengine 97 ya awamu ya tatu kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya,Bw. Rogers William sianga ili yaanze kushughulikiwa. 
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akizungumza jambo na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini, Rogers William Sianga katika mkutano maalum wa kutoa tathmini ya kampeni ya kutokomeza biashara haramu ya madawa ya kulevya katika mkoa wa Dar es salaam na nchi nzima kwa ujumla.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Khaleed Mohammed almaarufu TID akitoa ushuhuda wa namna alivyokuwa akitumia Dawa za kulevya,na sasa amekiri hadharani kuacha kutumia na kuunga mkono juhudi za kupambana na Dawa za kulevya.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishna Saimon Sirro akizungumza wakati akitoa taarifa ya kampeni hiyo leo.

WALIOTAJWA KUHUSIKA NA DAWA ZA KULEVYA KILIMANJARO HAWA HAPA.

$
0
0
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Msaidizi Mwandamizi,Wilbroad Mutafungwa akitaja majina ya watu wanadaiwa kujihusisha na usafirishaji,uuzaji na matumizi ya dawa za kulevya.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Wilbroad Mutafungwa akizungumza juu ya msako mkali ulioanza wa kuwakamata wafanyabiashara wa dawa za kulevya katika mkoa wa Kilimanjaro.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Wilbroad Mutafungwa akinyunyiza marashi juu ya Mirungi iliyofungwa katika vipande vya magazeti ikiwa ni mbinu mpya inayotumiwa na wasafirishaji wa bidhaa hizo.
Baadhi  ya watuhumiwa wa dawa za kulevya waliokamatwa katika msako uliofanyika kwa muda wa siku nne.
Sehemu ya Misokoto ya Bhangi iliyokamatwa wakati wa opereshni hiyo .

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.
 
JESHI la Polisi mkoa wa Kilimanjaro limetaja majina ya watu 47 wanaotuhumiwa kuhusika katika  kusafirisha,kuuza na kutumia dawa za kulevya huku likifanikiwa kukamata misokoto 269 na miche 13 ya Bhangi,pamoja na kilogramu 32.9 za mirungi pia ikikamatwa.

Kukamatwa kwa watuhumiwa hao pamoja na dawa hizo za kulevya kunatokana na msako mkali uliofanywa na kikosi maalumu cha jeshi hilo kwa muda wa siku nne katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Kilimanjaro .

Akitangaza majina hayo ofisini kwake ,Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ,Kamishna Mwanadamizi Msaidizi wa Polisi,Wibroad Mutafungwa alisema watuhumiwa hao tayari wamekamatwa na wako katika hatua mbalimbali za kiupelelezi na taratibu zikikamilika watafikishwa mahakamani.

Miongoni mwa watuhumiwa 47 wamo watoto wawili  waumri wa miaka 17 ambao ni Wilfred Mnubi mkazi wa Bomang’ombe wilaya ya Hai na Ruben Bakari mkazi wa Njoro katika manispaa ya Moshi.

Kati ya watuhumiwa hao wanawake ni 15 na wanaume ni 32 akiwemo mzee mwenye umri wa miaka 60,Christina Ferdinand.

“Vita hii tumeianza tangu mwaka juzi,tunajua vita hii ni kubwa bahati nzuri ni kwamba njia wanazotumia wafanyabiashara wa dawa za kulevya husani mirungi na bhangi ,tayari jeshi la polisi limezibaini,maeneo ambayo dawa za kulevya zimekithiri Jeshi la polisi limekwisha baini ,operesheni hii ambayo tumeianza ni endelevu na tutaendelea kuwakamata watu hawa kwa kutumia mbinu zote tulizonazo.”alisema Mutafungwa

Waliotajwa na kushikiliwa na jeshi la Polisi ni pamoja na:
(1)         Juma Kabwele(25).
(2)         Mohaed Kabwele (29) .
(3)         Shabani Mponda(39).
(4)         Khadija Mushiri(27).
(5)         Veronika Chuwa (39).
(6)         Mwanahamis Hussein.
(7)         Yusuph Issa(42).
(8)         Salim Massawe(48).
(9)          Hadija Mohamed(50).
(10)       Shenein Abilah(41).
(11)        Husna Mgonja(24).
(12)       Najima Desouza (46) .
(13)       Ruben Bakari (17) .
(14)       Paul Kisoka (26).
(15)       Raphael Mbuya (40).
(16)       Wilfred Mnubi(17).
(17)       Athuman Swaehe (35).
(18)       Joseph Hamis(20).
(19)       Zuber Temu(27).
(20)      Robert Kitika (18) .
(21)       Mohamed Juma (25).
(22)       Ahmad Shaban (57).
(23)      Donas Masashua(22).
(24)      Japhet Tungai (46).
(25)      Asima Mndeme (24).
(26)      Muutaz Zalia ,
(27)      Noah Singano (29).
(28)      Ramadhan Masale (40) .
(29)      Kirambati Swai(45).
(30)      Said Mrii.
(31)      Erick Henry (20).
(32)      Seif Ally(20).
(33)      Ramadhan Hassan (36).
(34)      Victor John(22).
(35)      Upendo Endkia (42).
(36)      Asia Ally(39).
(37)      Catherine Linusi (36) .
(38)      Mariam Hemed (44) .
(39)      Mwajuma Msuya (48).
(40)      Juma Yusuph (22) .
(41)      Hussein Anyokisye (17).
(42)      Musa Msangi (30).
(43)      Ramadhani Hassan (36).
(44)      Wilfred Munubi(17)
(45)       Ruben Bakar.(17)
(46)       Christina Ferdinand.(60)
(47)       Samweli Kingai(42).

Mwisho


TCCIA INVESTMENT PLC OFFERS OPPORTUNITY TO INVEST IN MORE THAN 8 COMPANIES

$
0
0
TCCIA Investment PLC (TICL) is a public limited liability Company established under the sponsorship of the Tanzania Chamber of Commerce, Industry and Agriculture [TCCIA] with an aim of expanding its financing sources.TICL has invested on 8 listed companies, blue-chip stocks at the Dar es Salaam Stock Exchange (DSE). The investment portfolio of TICL offers an opportunity for investors to diversify risk of their investments and be in a position to generate high returnsby investing in more than 8 different companies listed on the Dar es Salaam Stock Exchange. Before the listing, the investment portfolio of TICL constitutedstocks from companies namely; Twiga (TPCC), TCC, Swissport, CRDB Bank, Simba (TCCL), DCB, NMB and TBL.
Performance of TICL portfolio from 2011 to 2015
A. TICL portfolio has outperformed DSE;
From 2011 to 2015, if an investor bought all shares at DSE and another invested the same amount of fund only at TICL; the fund invested at TICL could have grown more than 4.5 times greater than the one invested in all shares at DSE. This is because all shares at DSE yielded a cumulative return of 91.91% from 2011 to 2015 quarterly, as indicated by All Share Index (ASI); while TICL portfolio yielded a cumulative return of 422.16%.That means, TICL managed to select stocks at DSE that yielded a better return.

B. Dividend Income;
From 2011 to 2015, TICL portfolio received more than 5 billion (5,249,009,156/=) of dividend from stocks which it has invested in. The dividend received has been increasing in an increasing rate since 2011, on average each year 154 million has been increased compared to the previous year. This indicates the best selection of stocks that provides better dividends every year.

C. Structure of the Portfolio
From 2011 to 2015 TICL has been selecting the best companies to invest. Up to now, 91.30% of the portfolio is invested on the leading stocks at DSE. These leading stocks are TBL, NMB and TCC, of which 74% of the dividend received by the company from 2011 to 2015 comes from those three leading stocks.

NMB is also the first bank to come out of recession in 2016 with an increasing share price from August. This shows TICL pay close attention to their portfolio in order to maintain the good performance of the portfolio. Consider the following chart of NMB share price;

Other important facts:
  • Tax Advantage: TICL has a great advantage when it comes to capital gain tax because in Tanzania there is no Capital Gain Tax. This means profits of the company derived from selling of securities will not be reduced due to tax. Therefore, the company has an opportunity to make more profit from the sale of securities.

  • Dividend Policy: TICL has a dividend policy of paying 50% of the profit after tax as dividend to the shareholders. On average, most listed companies at DSE pays a dividend of 30% to 40%; this shows that TICL investors will be receiving more of what their company yields as compared to other investors.

TICL’S FUTURE

The followingare four important facts that illustrates how bright TICL future is;
A. Stock Brokerage Business
B. Expected Liquidity of TICL shares at DSE
C. Current TICL value
D. Fixed Income Securities

A.  Stock Brokerage Business:
It is in the future plans of the company after the IPO to obtain a Broker-dealer’s license. That means, it will engage in a stock brokerage business; therefore, adding more revenue to the company due to brokerage fees.
The stock market in Tanzania is in a rapid growth more than many other sectors. The number of investors who buy and sell shares on daily basis is constantly increasing. Consider the following illustration;

Number of participants

2014
2016
Residents
196,443
464,350
Non-Residents
564
766
TOTAL
197,007
465,116
(236% rise)

For the period of 2 years (2014 to 2016), markets participants at DSE grew by 236%. This indicates the market is growing at the high rate. The market is expected to grow at a higher rate because up to now it is only 1% of the Tanzanians that are participating in the market.

B. Expected Liquidity of TICL shares at DSE:
Companies whose shares are wholly owned by Tanzanians normally have a higher trading volume at DSE. This is due to the availability of the shares in the market. Shares that are owned at a larger percentage by non-residents have a lower trading volume, for example, ACA, JHL and NMG. 1 billion shares of CRDB mostly owned by Tanzanians, as a result it has great share supply which increases its trading volume (liquidity).
TICL investors will be assured of the high trading volume of their shares because TICL is currently (before IPO)wholly-owned by Tanzanians. Investors will be in a great position to benefit in case of any price movements of TICL shares.

C. Current TICL value:
Currently, TICL are being offered at the lowest price. The valuation to determine the offering price of Tshs 400/= was conducted on September 2016, at the bottom of the current recession. Therefore, the determined price became lower than how it could have been a year before that.
Since the market has started to gain its momentum slowly, the shares of TICL will be increasing as the market increases due to the positive relationship between TICL portfolio and DSE All Share Index.
This is a great opportunity for potential TICL investors for they are able to buy the company at the cheapest price ever!
Consider the following tables which illustrate the difference in value between December 2015 and September 2016;

Valuation of TCCIA Investment PLC as at 31 December 2015
SHARES
QUANTITY
CLOSING PRICE
VALUE
Twiga
88,348
3,000
265,044,000
TCC
301,800
15,950
4,813,710,000
Swissport
101,427
7,350
745,488,450
CRDB Bank
4,249,064
405
1,720,870,920
Simba
68,269
2,670
182,278,230
DCB
656,104
570
373,979,280
NMB
2,611,886
2,500
6,529,715,000
TBL
1,183,655
14,800
17,518,094,000
TOTAL  VALUE


32,149,179,880
No. OF SHARES


71,092,400
VALUE PER SHARE (THERE ARE NO LIABILITIES) 
450


If TICL was to be sold about a year ago, the price could have been Tshs 450/=.
Therefore, investors have an opportunity of buying the shares today at a lower price!
D. Fixed Income Securities
From the letter of the chairman, he pointed about the future products and plans of TICL, he said, “We will widen investment areas in other products that are currently missing from our portfolio such as Government securities, REITs, infrastructure bonds and other debt instruments. These offer a good trade off when returns in the equities board become unattractive”
Currently, the company only invests on equities. The expansion of the portfolio to risk free asset will ensure a stable return of the portfolio. Investors will be assured with the growth of the company’s portfolio.
HINT: TICL shares are available to the general public including foreign investors and diaspora, there are no restrictions in a matter of nationality. Any person interested can subscribe for the share through any Tanzanian broker. For more information, the sponsoring broker for TICL Initial Public Offer is Tanzania Securities Limited http://www.tanzaniasecurities.co.tz.
By Brian Edward Chuwa
Stock Analyst
CEO, Beacon Financials Limited
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live


Latest Images