Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46201 articles
Browse latest View live

TAARIFA YA TAHADHARI KWA WADAIWA WA PANGO LA KODI YA ARDHI

0
0
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Yamungu Kayandabila akiongea na waandishi wa habari kwamba Serikali kupitia Wizara yake haitamuacha mtu au kampuni yoyote inayodaiwa kodi ya Ardhi hata kama ni Taasisi ya Serikali.
 Watumishi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kushirikiana na kampuni ya Udalali ya Msolopa Investment wakiwa nje ya ofisi Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA) ili kuwasilisha notisi ya madai ya kodi ya ardhi.
Wafanyakazi wa Lamada Hotel (kushoto) wakiangalia kwa makini Notisi ya madai ya kodi ya Ardhi wakati ikiwasilishwa na watumishi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kushirikiana na kampuni ya Udalali ya Msolopa Investment.


Na Mboza Lwandiko

Lipa Kodi ya Ardhi kwa wakati, uepuke kutozwa Tozo, Kutangazwa kwenye Vyombo vya Habari, Kupelekwa Mahakamani na Kufutiwa umiliki wa ardhi yako, kwani Sheria ya Ardhi Na. 4 ya mwaka 1999 inaainisha gharama hizo kwa wasiozingatia ulipaji Kodi. kutozingatia kulipa Kodi ya pango la Ardhi kwa wakati, ambapo mmiliki asiyezingatia hilo kwanza; atatozwa Tozo na baadae Kupelekewa hati ya madai na kufikishwa Mahakamani kulingana na kifungu Na. 50 na hatimaye kufutiwa umiliki wa ardhi kulingana na Sheria hiyo hiyo katika kifungu Na. 49-51.

Akizungumza na Waandishi wa habari hivi karibuni wakati wa zoezi la kutoa notisi ya siku 14 kwa wadaiwa sugu wa Kodi ya Pango la Ardhi. Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Dkt. Yamungu Kayandabila amesisitiza kwa umma kuwa wadaiwa wote wa Pango la Ardhi wamekumbushwa na Serikali kwa muda mrefu, na hivyo ni wakati wao kuhakikisha wanalipa madeni yao yote ipaswavyo. Aliendelea kusema kuwa; kwa Mwaka wa fedha 2016/17 Wizara imepanga kukusanya Sh. bilioni 111.77 kutokana na Kodi ya Pango la Ardhi. 

Dkt. Kayandabila alisema kwakuwa Kodi ya Ardhi inatambulika bayana chini ya Sheria, kila mmiliki wa Ardhi hana budi kuzingatia hilo. Malipo ya pango la ardhi yanatozwa kwa wamiliki wa viwanja na mashamba yaliyopimwa na kumilikishwa kisheria. 

Pia mtu yeyote anayemiliki ardhi iliyopimwa kisheria iwe imeendelezwa au haijaendelezwa bado anapaswa kulipa kodi ya pango. Kila mmiliki anaongozwa na mkataba wa kulipia kodi ya pango la ardhi kila mwaka tarehe 1 (Mosi) Julai, Sheria ya Ardhi Na.4 ya mwaka 1999 kifungu cha 33 na kifungu kidogo cha 11 imetoa mwanya kwa walipa kodi kuendelea kulipa bila adhabu hadi tarehe 31 Desemba ya mwaka unaohusika. Baada ya hapo adhabu inatozwa. Mteja anapaswa kufanya malipo ya Kodi ya pango la Ardhi kwa kuwa ananufaika na matumizi ya ardhi hiyo.

Vile vile, Mkuu wa Kitengo cha Kodi katika Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Bwn. Dennis Masami ameeleza kwa waandishi wa habari kuwa opereshini iliyoanza ya kutoa notisi ya siku 14 kwa wadaiwa ni endelevu na kueleza kuwa hati za madai zaidi ya 5000 zimeshasambazwa jijini Dar es Salaam. 

Alitaja baadhi ya Kampuni ambazo zina madeni sugu ambazo zimepewa notisi ya siku 14 kulipa madeni ni pamoja na; Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA) anayedaiwa Shilingi milioni 144 na Mwananchi Engineering wana deni la milioni 22. Kampuni nyingine ambazo zilipatiwa notisi ni; Mohamed Interprise waliokuwa na deni la milioni 73 na wameshalipa deni lote hivi karibuni na Lamada/Ilala – waliokuwa na deni la milioni 54, wamepunguza deni kwa kulipa milioni 25. 

Utaratibu wa ukadiriaji wa kodi ya ardhi hufanyika kwa kuzingatia ukubwa wa ardhi inayomilikiwa na thamani ya ardhi mahali ilipo (land value), vilevile kwa kuzingatia huduma muhimu zilipo (miundombinu) na Matumizi ya ardhi husika kama vile Biashara, viwanda, makazi, kilimo.

Aidha, Makadirio na malipo ya kodi ya ardhi Kwa wamiliki wa ardhi yanafanyika katika maeneo mbalimbali. Dar es Salaam; malipo ya kodi hufanyika Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi – Kivukoni, kwenye Kitengo cha Kodi na pia kwenye Ofisi za Ardhi za Manispaa za Ilala, Kinondoni na Temeke. Katika Mikoa; makadirio hufanywa kwenye Ofisi za Ardhi zinazotambulika za Manispaa na Halmashauri za Miji na Wilayani kote nchini.

Aidha, Kumbukumbu za muhimu zinahitajika wakati malipo yanapofanyika, kwa wale ambao kumbukumbu zao za umiliki zilishaingizwa kwenye Kompyuta wanatakiwa wakumbuke namba ya kumbukumbu ya kulipia yenye tarakimu sita (Lot Id Number). Hatahivyo, wengine wote wanapaswa kufika katika maeneo yao ya kufanyia malipo na risiti/ stakabadhi ya mwisho ya malipo na hati au barua ya toleo (Original Letter of Offer).

Malipo ya kodi kwa toleo jipya la Kiwanja (Letter of Offer) yanapaswa kulipwa ndani ya muda wa siku 30 kuanzia tarehe ya toleo, vinginevyo itachukuliwa kwamba kiwanja kimekataliwa ambacho kilikuwa kimeshakabidhiwa kwa muhusika.


Katika Kampeni ya uhamasishaji ulipaji Kodi ya Pango la Ardhi, katika eneo la Mbagala – Dar es Salaam, zoezi lililofanywa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kwa kushirikiana na Kitengo cha Kodi. Afisa Sheria; Seif Mahiza, aliyekuwa akiongea na Wananchi wa Mbagala alisisitiza kuwa; “Mwananchi ataona mzigo wa kulipa pango lake la Kodi ya Ardhi pale tu atakapoacha kulipa kwa wakati na kuwa na malimbikizo, lakini Mwananchi akijitahidi kulipa kodi yake ya pango la Ardhi kila mwaka kwa wakati hataona mzigo katika kutimiza jukumu hilo”.

Malipo ya kodi ya Pango la Ardhi ni ya manufaa kwa Mmiliki ili kumhakikishia miliki salama na uhalali wa mali yake ambayo ina uwezo wa kuzalisha katika nyanja mbalimbali; mfano katika kukopa, kuzalisha mazao, kukodisha n.k. Lakini pia Ardhi hiyo hiyo hutumika kunufaisha Taifa kwa ujumla kwa Maendeleo ya nchi nzima.


“Lipa Kodi ya Pango la Ardhi kwa Maendeleo ya Taifa Letu”

TAARIFA YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI KUHAMIA DODOMA

0
0
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA NISHATI NA MADINI


  
TAARIFA KWA UMMA

AWAMU YA KWANZA YA WATUMISHI KUHAMIA MAKAO MAKUU YA NCHI - DODOMA TAREHE 10 FEBRUARI, 2017

Wizara ya Nishati na Madini inapenda kuufahamisha umma kuwa, Awamu ya Kwanza ya Watumishi wa Wizara kuhamia Makao- Makuu ya Nchi, Dodoma inaanza tarehe 10 Februari, 2017.

Miongoni mwa watakao hamia katika awamu hiyo ni pamoja na Viongozi na Watendaji Wakuu wa Wizara ambao ni Waziri wa Nishati na Madini, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini na Naibu Makatibu Wakuu wa Nishati na Madini.

Watumishi wengine ni pamoja na Kamishna wa Madini Tanzania, Kamishna wa Nishati na Masuala ya Petroli, Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala na Maafisa. Jumla ya Watumishi wanaohamia Dodoma Awamu ya Kwanza ni 47.

Aidha, kutokana na uhamisho huo, anuani ya Wizara  Dodoma ni;
Katibu Mkuu,
Wizara ya Nishati na Madini,
Barabara ya Kikuyu,
S.L.P 422,
DODOMA
Imetolewa na;

KATIBU MKUU
WIZARA YA NISHATI NA MADINI
9/2/2017

MAHAFALI CHUO KIKUU CHA AGA KHAN YAFANA

0
0

Wahitimu wa Chuo kikuu cha Aga khan wakiingia katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam
Wahitimu wa chuo kikuuucha Aga Khan miaka wakingia katika mahafali ya chuo hiyo

Wazazi na wageni waalikwa waliofika katika mahafali hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Aga Khan jijini Dar es Salaam


Naibu Gavana wa Benki Kuu nchini Tanzania, Lila Mkila akizungumza na wanafunzi wa chuo kikuu cha Aga Khan
Rais wa Chuo Kikuu cha Aga Khan Firoz Rasul akikabidhi cheti kwa mmoja wa wahitimu wa chuo hichi
Baadhi ya wahitimu wa chuo kikuu cha Aga Khan wakiwa katika picha ya pamoja na wahitimu wa chuo hicho

MKUTANO WA KIUCHUMI WA 2017 KUFANYIKA MACHI 6 JIJINI DAR ES SALAAM

0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

Shirika lisilo la kiserikali la Kingdom Leadership network Tanzania (KLNT) limeandaa mkutano wa pili wa Tanzania National Prayer Breakfast na mkutano wa Kiuchumi ujulikanao kama 2017 Kingdom Economic Summit.

Mkutano huo utakaofanyika kuanzia machi 6-8 utajumuisha shirika la huduma la kimataifa ya Bill Winston kutoka nchini Marekani na unatarajiwa kuhudhuriwa na Makamu wa Raisi wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania Samia 

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam, katibu mkuu wa KLNT Charles Sokile amesema kuwa mkutano huo wa uchumi unatoa nafasi ya kipekee kwa watu binafsi, wafanyabiashara, mashirika ya kibiashara na viongozi wa makanisa kuweza kujipatia ujuzi na uzoefu kutoka kwa wasemaji mkuu wa mkutano mkuu.

"Tunajivunia kuweza kuleta tena mkutano huu kwa mwaka wa pili sasa na kuweza kuleta wageni rasmi ili kuja kuhamasisha watanzania na kuleta mabadiliko chanya kimaadili katika uongozi na biashara kwa mtu mmoja mmoja na hatimaye taifa kwa ujumla," amesema Sokile.

Mwanzilishi wa KLNT Isaac Mpwata amesema kuwa kila mara wanajikita katika kuhakikisha wanatoa fursa za mafunzo ya kiongozi na biashara yanayojikita kwenye suala zima la maadili kama msingi wa mafanikio.

Mpwata amesema kwa kupitia mkutano huu wanategemea kuendelea kujenga uwezo wa viongozi wetu na wafanyabiashara kwa ajili ya kubadili taifa letu kwa kutumia kanuni za uongozi wa kimaadili ili kuleta mabadiliko chanya katika nyanja za kiuchumi, kisiasa na kijamii.
Suluhu.
 Mwanzilishi wa Kingdom Leadership Network Tanzania (KLNT) Issac Mpwata akizungumza na waandishi wa habari kuhusinana na mkutano wa pili wa kiuchumi utakaofanyika Machi 6-8 Jijini Dar es salaam
Katibu Mkuu wa Kingdom Leadership Network Tanzania Charles Sokile akizungumza na waandishi wa habari kuelekea maandalizi ya mkutano wa pili wa kiuchumi na kuwataka viongozi mbalimbali kujitokeza, Kulia ni Mwanzilishi wa KLNT Issac Mpwata na Kushoto ni Afisa masoko  Carol Maajabu

TAARIFA YA SERIKALI TOKA BUNGENI LEO JIONI 09/02/2017

0
0

DKT SHEIN AKABIDHIWA RIPOTI YA TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipokea Ripoti ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar ya mwaka 2015 kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume hiyo Mhe,Jecha Salim Jecha (kushoto) katika hafla fupi iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.] 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa kizungumza na mawaziri mbali mbali,watendaji wa Serikali (hawapi pichani), Wajumbe wa Tume ya uchaguzi baada ya kukabidhiwa Ripoti ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar ya mwaka 2015 na Mwenyekiti wa Tume hiyo Mhe,Jecha Salim Jecha (katikati) katika hafla fupi iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.] 09/02/2017.

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Mhe,Jecha Salim Jecha (kulia) akitoa maelezo mafupi kabla ya kukabidhi Ripoti ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar ya mwaka 2015 hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja
Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Washauri wa Rais waliohudhuria katika hafla ya kukabidhiwa Ripoti ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar ya mwaka 2015 kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume hiyo Mhe,Jecha Salim Jecha (hayupo pichani) katika hafla fupi iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja.
Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu (kushoto) na Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakiwa katika hafla ya kukabidhiwa Ripoti ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar ya mwaka 2015 kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume hiyo Mhe,Jecha Salim Jecha (hayupo pichani) katika hafla fupi iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja

VALENTINE'S DAY AT SHEKINAH GARDEN, MBEZI BEACH

0
0

KINANA AONGOZA MAZISHI YA ALIYEKUWA MWENYEKITI WA UWT TAWI LA SHIRIKISHO LA WANAFUNZI VYUO VYA ELIMU YA JUU-CCM, CHUO KIKUU CHA USHIRIKA MOSHI

0
0
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisaini kitabu cha maombolezo ya kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa UWT, Tawi la Shirikisho la Wanafunzi vyuo vya Elimu ya Juu-CCM, Anastazia Malamsha, wakati wa mazishi ya kiongozi huyo, yaliyofanyika leo katika eneo la  Shimbo, Rombo Mkuu mkoani Kilimanjaro. Anastazia alifariki dunia Jumapili, Feb 5, 2017,  katika ajali ya gari wakati akitoka kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 40 ya CCM mkoani huo ambapo pamoja naye viongozi wengiewatatu walifariki pia katika ajali hiyo.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitoaheshima za mwisho kwa mwili wa Anastazia, kabla ya mazishi hayo
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kilimanjaro, Iddi Juma akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Anastazia wakati wa mazishi hayo.
 Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM, Shaka Hamdu Shaka akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Anastazia kabla ya mazishi hayo
 Katibu Katibu Mtendaji wa Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu Daniel Zenda akitoa heshima za mwisho wa mwili wa marehemu Anastazia wakati wa mazishi hayo
 Muombolezaji akisadiwa wakati akilia kwa uchungu wakati wa mazishi ya marehemu Anastazia
 Bangolilialondikwa kuomboleza kifo cha anastazia, nyumbani kwao
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiwa na Mjumbe wa NEC, Cyril Chami
 Katibu Mkuu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadick Mkuu huyo wa mkoa alipowasili kwenye mazishi hayo
 Kinana na baadhi ya viongozi wa Chama na serikali wakiwa kwenye mazishi hayo. Kulia ni Said Mecky Sadick 
 Waombolezaji wakiandamana kutangulia mbele wakati mwili wa Anastazia ulipokuwa ukipelekwa eneo la kusaliwa wakati wa mazishi hayo
 Waombolezaji wakiandamana kutangulia mbele wakati mwili wa Anastazia ulipokuwa ukipelekwa eneo la kusaliwa wakati wa mazishi hayo
 Vijana wa Umoja wa Vijana wa CCM wakibeba jeneza lenye mwili wa marehemu Anastazia kulipeleka kwenye eneo la kusaliwa wakati wa mazishi hayo
 Vijana hao wa UVCCM wakiwa wamelibeba kikakamavu jeneza lenye mwili wa marehemu Anastazia
 Huyu ndiye marehemu Anastazia wakati wa uhai ake
 Waombolezaji wakiwa msibani wakati wa mazishi hayo
 Baba na Mama wa marehemu Anastazia, Innocent Malamsha na Devota Malamsha wakiwa na nyuso za huzuni wakati wa mazishi hayo
 Baba na Mama wa marehemu Anastazia, Innocent Malamsha na Devota Malamsha wakiwa na nyuso za huzuni mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu, wakati wa mazishi hayo
 Baadhi ya wanakwaya ambao ni Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi, wakiimba nyimbo za maombolezo wakati wa mazishi hayo. Anastazia alikuwa mwanafunzi wa Mwaka wa tatu katika chuo hicho Kikuu cha Ushirika Moshi.
 Waombolezaji wakiwa kwenye mazishi hayo
 Baadhi ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi, wakiwa kwenye mazishi hayo. Anastazia alikuwa mwanafunzi wa Mwaka wa tatu katika chuo hicho Kikuu cha Ushirika Moshi.
 Wana CCM wakiwa kwenye mazishi hayo
 Wana CCM na wananchi wakiwa kwenye mazishi hayo 
 Waombolezaji
 Badhi ya madereva waliowafikisha viongozi kwenye mazishi hayo
 Mshauri wa Wanafunzi Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi Dk.Gervas Machim, akitoa maneno ya rambirambi kwenye mazishi hayo
 Naibu Mkuu wa Kitivo cha Ushirika na Maendeleo ya Jamii katika Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi, Dk. Cyril Komba akitoa maneno ya rambirambi kwenye mazishi hayo
 Rais wa Serikali ya Wanafunzi Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi, William Mbogo akitoa maneno ya rambirambi kwenye mazishi hayo
 Rais wa Serikali ya Wanafunzi Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi, William Mbogo akikabidhi fedha za mchango wa rambirambi kwa Baba na mama wa Marehemu Anastazia, Innocent Malamsha na Devota Malamsha, kwenye mazishi hayo
 Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akiwa na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadik na viongozi wengine wa CCM kwenye mazishi hayo
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitoa salama za rambirambi za kwake binafsi, CCM na Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli wakati wa mazishi hayo
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitoa salama za rambirambi za kwake binafsi, CCM na Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli wakati wa mazishi hayo
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitoa salama za rambirambi za kwake binafsi, CCM na Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli wakati wa mazishi hayo
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwapa pole baba na mama wa marehemu Anastazia baada ya kutoa salama za rambirambi za kwake binafsi, CCM na Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli wakati wa mazishi hayo
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimpa pole baba wa marehemu Anastazia baada ya kutoa salama za rambirambi za kwake binafsi, CCM na Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli wakati wa mazishi hayo
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akikabidhi fedha za mchango wa rambirambi kutoka CCM na Jumuia zake, kwa Baba na mama wa Marehemu Anastazia, Innocent Malamsha na Devota Malamsha, baada ya kutoa salam za rambirambi kwenye mazishi hayo
Katibu Mkuu wa CCM, Adrahman Kinana akimshukuru mmoja wa padri aliongoza misa ya kumuombea marehemu Anastazia wakati wa mazishi hayo
 Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro said Mecky Sadick akitoa heshima za msiho kwa mwili a marehemu Anastazia
 Abubakary Assenga akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Anastazia
 Abubakary Assenga akimpa pole mama wa marehemu Anastazia
 Waombolezaji wakati wakiaga mwili kwa mara ya pili wakati wa mazishi hayo
 Baba wamarehemu Anastazia akiweka udogo kaburini wakati wa maziko
 Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka akiweka udogo kaburini wakati wa maziko
 Kaimu Katibu Mtendaji wa Shirikisho la Vyuo vya Elimu ya juu CCM, Daniel Zenda akiweka udongo kaburini wakati wa maziko
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiweka udongo kaburini wakati wa maziko
 Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadick akiweka udongo kaburini 
 Mwenyekiti wa CCMmkoa wa Kilimanjaro akiweka udongokaburini
Mwombolezaji ambaye ni mwanafamilia ya marehemu Anastazia akisaidiwa wakati akiweka udogo kaburini.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiweka shada la maua kwenye kaburi la Anastazia, mwishoni mwa maziko.PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

WITO KWA WALIOKUWA WAFANYAKAZI WA MGODI WA DHAHABU BULYANHULU WALIOPIMWA AFYA KATIKA HOSPITALI YA BUGANDO

0
0
WITO KWA WALIOKUWA WAFANYAKAZI WA ULIOKUWA MGODI WA DHAHABU 

BULYANHULU

UPIMAJI ULIOFANYIKA HOSPITALI YA BUGANDO

Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) unawakaribisha walioorodheshwa hapo chini kufika katika ofisi za OSHA zilizopo katika jengo la Idara ya Kazi, Barabara ya Stesheni mkabala na Lake Hotel kwa tarehe zilizotajwa katika makundi yao kuanzia saa 2.30 asubuhi ili waweze kupewa majibu yao. Tangazo hili linawahusu waliopimwa Bugando tu.


13/02/2017

 1

GODFREY RAPHAEL BULUBA

  2

EDWARD JOSEPH MANG'ONG'O

3

PROSPER MICHAEL KIDALO

4

SALVATORY SAMSON NGAVANGA

5

CLEOPHAS JOSEPH KANUTI

6

BISEKO WILLIAM FAUSTINE

7

BAKARI OMARY SHARIFU

8

KIZITO PHILIP BUJIKU

9

CHARLES MISANGA MAKOLO

10

DOMICIAN MZEE CHAMI

11

LEONARD EDWARD DOTTO

12.

ALPHONCE PAULO LUNYALULA

13.

ERNEST JAMES MWIDIMA

14.

CHARLES SIMBA KATUNDU

15.

NICOMEDES MODEST KAJUNGU


14/02/2017

1

AYUBU HAMZA KAGOMA

2

MICHAEL JOHNSON MWIHAMBI

3

IBRAHIM SUDD KAGOLO

4

ATHUMANI SUFIAN HAJI

5

JUMA DAUDI MWAKALONGE

6

JOSEPH ANGEITAGA KYAMBA

7

DAMAS EDWARD KOMORE

8

WINFRID ANDREW KARIA

9

KULWA JOHN SINGU

10

JOSEPH MALOMA NDULI

11.

JOSEPH NYITIKA CHACHA

12.

WILLIAM DAUDI MOSHA

13.

GEORGE NGASSA SAMSON

14.

ABEL DOTTO BULALA

15.

BAHATI SIMON KALIKUNZILA

                


15/02/2017

1

SOSPETER SUKA STANSLAUS

2

AKIDA ALLY SALUM

3

JUMA RAMADHANI WITIKA

4

NOVATUS PETRO RUGAKIKULA

5

CHARLES DOTTO KALOGI

6

GODFREY MSENGI MBOGO

7

HUSSEIN KATELLA MASHA

8

BONIPHACE MWENDI SOLOGWA

9

ERASMUS KIMARIO BERNAD

10

MBAROUK JUMA URASSA

11

SALUM MANG'OMBE DEREFA

12.

MAJID ISSA HAMAD

13.

JOSEPH MWITA NYABAGAAKA

14.

MICHAEL COSMAS MWAMBYALE

15.

MACHERA DAVID CHACHA


16/02/2017

1

BILDADI J. MAKUNDII

2

SAYI GIBU MAGIDA

3

JUSTINE CHARLES LUBIGILI

4

MPAMBA MLINGWA ROBERT

5

WILBERT SYLIVESTER MAKUNGU

6

MALIMI PETER MAZULIKA

7

ELIAS EMILIASON MASHINI

8

JAPHET ALEX MOREMI

9

SIASA IGOBO MUNGOYA

10

NASSORO RAMADHANI MWANDU

11.

ELPHAS MANYONYI KISAJI

12.

JOHN GERVAS STEPHEN

13.

SEIF RASHID DULLE

14.

GOGO WAZIRI HASSAN

15.

ISSA RAMADHANI MWANDU


17/02/2017

1

NICKSON KATANI IGOKO

2

JOSEPH MASANJA NTINDA

3

JANUARY DATUS MSAFIRI

4

SAMSON HANGO KHANGA

5

JASSON TAIFA BATIGIRIZA

6

FADHILI JUMA KINANDA

7

ABAS JOSEPH PETRO

8

JUMA SIMBA TAMAMBELE

9

RAMADHANI SAIDI KOROGWA

10

DASTAN ILOLE BULUNGA

11.

MOHAMED A. MNGWALI

12.

BENEDICT BUKURU LULIKELA

13.

MABINA FIDELIS GEORGE

14.

SYLVANUS GERVAS KAMALA


                                                                   Imetolewa na:

MTENDAJI MKUU

WAKALA WA USALAMA NA AFYA MAHALI PA KAZI (OSHA)

S.L.P 519, MAHAKAMA ROAD KINONDONI


DAR ES SALAAM

RC MTAKA AKABIDHI NG'OMBE KWA FAMILIA YA MD KAYOMBO KWA AJILI YA AROBAINI YA KIFO CHA MZEE KAYOMBO

0
0

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kijiji cha Misasi
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka (kulia) akiwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo (kushoto)
 Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo
 Ng'ombe aiyetolewa na Rc Mtaka kwa ajili ya Arobaini ya Mzee Kayombo
 Mwenyekiti wa Asasi ya Wazalendo na Maendeleo Tanzania (AWAMATA) Chief Mrindoko Babu Mwidadi akisaini kitabu cha wageni ishara ya ushiriki wa asasi hiyo katika msiba wa Mzee Kayombo
 Mazungumzo yamenoga mara baada ya makabidhiano ya Ng'ombe
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka (katikati) na Mkewe wakifanya maombi katika kaburi la marehemu Mzee Kayombo, Kulia kwao ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Kayombo ambaye ni mjukuu wa Marehemu Mzee Kayombo
 Rc Antony Mtaka Mtaka
 Rc Mtaka akiwasalimu ndugu wa marehemu Mzee Kayombo mara baada ya kukabidhi Ng'ombe

Rc Mtaka (kulia) akisisitiza jambo, kulia MD Kayombo na katikati ni Mathias Canal Mhariri wa Tovuti ya (www.wazo-huru.blogspot.com) wakisikiliza kwa makini busara za mkuu huyo wa Mkoa wa Simiyu
MD Kayombo akiwa na ndugu na jamaa katika mazungumzo ya jioni
Na Mathias Canal, Mwanza 
 
Ikiwa ni siku tatu zimepita tangu Marehemu Mzee Antony Raphael Kayombo kuhifadhiwa katika nyumba yake ya milele (kaburini) Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka amezuru kijijini Misasi, Wilayani Misungwi kwa ajili ya kutoa pole kwa familia ya Mzee huyo.

Rc Mtaka aliyeambatana na Mkewe wamefanya sala ya kumuombea mapumziko mema Mzee Kayombo ikiwa ni ishara ya ukamilifu wake wa haki na kheri hapa Duniani.

Pamoja na mkono wa pole kama mila za kiafrika zinavyoarifu Rc Mtaka pia ameikabidhi familia hiyo Ng'ombe kwa ajili ya Arobaini itakayofanyika kijijini hapo ikiwa ni ishara ya ukamilisho wa Msiba huo (HITMA)).

 "Binafsi naamini katika matendo mema hapa Duniani, Mzee wetu ametutoka ni pigo kwa familia na kwetu sote lakini hakuna namna tuna kila sababu ya kulipokea jambo hili kama jambo la kila mmoja wetu japo halizoeleki" Aliongeza RC Mtaka

Akipokea Ng'ombe huyo na kuzungumza kwa niaba ya familia Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo ambaye ni mjukuu wa marehemu Mzee Kayombo amesema kuwa kwa kuwa safari ya kifo ni ya kila mmoja hivyo familia imepokea kifo hicho kama safari ya mwisho kwa Mzee wao lakini inaendelea kumuombea ili aishi maisha ya amani huko alipo.

MD Kayombo amemshukuru Mkuu huyo wa Mkoa wa Simiyu kwa kufika na kuwasalimu waombolezaji ambao bado wapo kijijini hapo sawia na kumtakia majukumu mema katika utendaji wake ili kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo kote nchini.

Marehemu Mzee Kayombo aliugua ugonjwa wa kibofu cha mkojo ambao ulianza ghafla tarehe 29/1/2017 na kupelekwa katika hospitali ya Misasi, Baadae hospitali ya Sekou Ture na mwishowe Hospitali ya Bugando ambapo alifanyiwa upasuaji ambapo hata hivyo hali yake iliendelea kudhoofika mpaka mauti ilipomkuta tarehe 4/2/2017 majira ya saa mbili usiku.

MUNGU AILAZE MAHALA PEMA PEPONI ROHO YA MAREHEMU MZEE ANTONY RAFAEL KAYOMBO. AMENI 

Shamrashamra za Burudani za Uzinduzi wa Tamasha la Sauti za Busara Viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani Zanzibar

0
0
Mwenyekiti wa Tamasha la Busara Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said akiwa na Mabalozi wa Norway na Uswisi kulia kwa Mhe Simai ni Balozi wa Uswisi Tanzania Balozi Florence Tinguely na Balozi wa Norway Tanzania Balozi Hanne Marie wakiangalia wakiangalia vikundi vya Utamaduni wakati wa Uzinduzi wa Tamasha la Sauti za Busara katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani Kisongo leo wakiangalia burudani hizo.
Wasanii wa Kikundi cha Utamaduni kutoka Nchini Burundi wakitowa burudani kwa Wananchi wa Zanzibar katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani Zanzibar kabla ya kuaza kwa maandamano ya Uzinduzi huo yalioazia katika viwanja hivyo hadi katika viwanja vya bustani ya forodhani.
Wasanii kutoka burundi wakionesha umahiri wao wa kupiga ngoma za utamaduni wa Kwao. 


Wananchi waliofika katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani wakifuatilia burudani za wasanii mbalimbali kabla ya kuaza kwa maandamano ya ufunguzi wa Tamasha la Busara Zanzibar.
Mwenyekiti wa Tamasha la Sauti za Busara Zanzibar akitowa maelezo kwa Mabalozi wa Uswisi na Norway walipokuwa katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu wakipata maelezo ya Mnara huo

Kikundi cha Six Unity wakionesha umahiri wao wa kujenza Dance wakati wa uzinduzi huo katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani.
Wasanii wakitowa Burudani katika Viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani Kisonge.
Wanafunzi wa Skuli ya Maandalizi Jangombe wakicheza ngoma ya Bomo katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu kabla ya kuaza kwa maandamano ya Uzinduzi wa Tamasha la Busara Zanzibar.


Wananchi wakifuatilia burudani zilikuwa zikitolewa  na Vikundi mbalimbali vya Utamaduni vinavyoshiriki Tamasha la Busara Zanzibar.
Imeandaliwa na OthmanMapara.
Zanzinews.com.
othmanmaulid@gmail.com.

RC IRINGA AAGIZA WANAFUNZI WASIORIPOTI SEKONDARI WASAKWE

0
0
Mkuu  wa Iringa  Amina  Masenza  akisalimiana na walimu  wa shule ya sekondari  Lundamatwe  Kilolo
Mkuu  wa mkoa wa Iringa  Amina  Masenza  akikagua  vyumba vya madarasa

Mkuu  wa mkoa  wa  Iringa  Amina Masenza  akizungumza na wanafunzi wa  kidato cha  nne katika  shule  ya sekondari  Lundamatwe  wilaya ya  kilolo


Mkuu  wa mkoa  wa Iringa  Amina Masenza akikagua madaftari  ya wanafunzi  shule ya  sekondari  Lundamatwe  wilaya ya  kilolo  wakati wa ziara  yake 





Mkuu  wa mkoa  wa Iringa Amina Masenza akikagua  idadi ya  wanafunzi  walioripoti  kuanza na  kidato  cha kwanza  shule ya  sekondari Lundamatwe  Kilolo  huku wanafuzi hao  wakiwa  wamekaa kwa kubanana  viti  vitatu  wakikaa wanafunzi  wanne


Mkuu  wa  wilaya ya  Kilolo  Asia Abdalah  kushoto  akimsikiliza  mkuu  wa  mkoa wa Iringa Amina Masenza wakati wa kikao  cha majumuisho wilayani Kilolo


Na matukiodaima blog ,Kilolo

SERIKALI ya Mkoa wa Iringa imeagiza wazazi walioshindwa kupeleka Watoto waliofaulu kujiunga na sekondari wasakwe .

Agizo hilo imetolewa leo na mkuu  wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza wakati wa ziara yake  ya ukaguzi wa vyumba vya madarasa kwenye Shule za sekondari wilaya ya Kilolo.

Alisema kuwa ni wajibu wa watendaji wa vijiji na kata kushirikiana na Walimu wakuu wa Shule pamoja na waratibu Elimu kata  kujua idadi ya Watoto waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kuona wameripoti Shule.

" Nawaagiza watendaji wote kufanya msako wa watoto walioshinda kujiunga na elimu ya sekondari"

Alisema mbali ya Watoto hao kusakwa pia lazima wazazi wabanwe kutokana na kushindwa kutimiza wajibu wao  wa kupeleka Watoto Shule

Mkuu alisema lengo la serikali ya awamu ya tano  chini ya Rais Dkt John Magufuli ni kuona  kila mtoto anakwenda Shule na ndio sababu ya kufuta ada.

Hivyo alisema kwa mazazi atakayeshindwa kusomesha mtoto anapaswa kuchukuliwa hatua  Kali za kisheria.

Alisema mfano katika Shule ya sekondari Lundamatwe kati ya Watoto waliopaswa kujiunga na sekondari hadi sasa ni Watoto wanne ndio walichelewa kujiunga ila baada ya wazazi kubanwa Watoto
Wawili wameripoti na Watoto wawili wanasakwa na kwa wilaya asilimia 17.89 ya Watoto waliochaguliwa kujiunga sekondari hawajaripoti.

"Naagiza hawa Watoto wawili waliokaa nyumbani watafutwe na waletwe Shule kama suala ni umbali wa Shule basi  waletwe kuishi Hosteli "

Kuhusu maabara mkuu  huyo alisema bado kuna changamoto kubwa ya maabara kutokana na wilaya hiyo kugeuza vyumba vya madarasa kuwa maabara hivyo kupelekea upungufu vya vyumba vya madarasa pamoja na maabara zilizo nyingi kuwa chini ya kiwango.

Masenza alimwagiza mkuu  wa wilaya ya Kilolo Asia Abdalah na uongozi wa halmashauri ya kilolo  kufanya jitihada za ujenzi wa vyumba vya madarasa na maabara borabora

Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdalah alisema kuwa kasi  ya kuwabana wazazi wasiopeleka Shule Watoto inaendelea na wametoa muda hadi  machi wazazi wote kupeleka Watoto wao  Shule.

Kwa mujibu wa Afisa Elimu Kilolo Stephen Mrosso jumla ya wanafunzi 3734 ndio walichaguliwa kujiunga na sekondari kati yao wavulana 1658 na wasichana 2076 wanafunzi walioripoti ni 2987 wavulana 1287 na wasichana1693

Wakati wanafunzi ambao hawajaripoti ni 747 wasichana 383 na wavulana 364 kuwa taarifa zilizopo wanafunzi 82 wakiwemo wavulana 36 na wasichana 46 wamejiunga na Shule nyingine nje ya wilaya ya Kilolo na kufanya jumla ya wanafunzi waliopo Shule kufikia 3069 sawa na asilimia 82.19 hivyo bado asilimia 17.89 kuripoti shule
Mwisho

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO DKT.ASHATU KIJAJI AZINDUA HUDUMA MPYA YA ‘ECOBANK MOBILE APP’

0
0


Naibu Waziri wa fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa huduma mpya ya ‘Ecobank Mobile App’ iliyozinduliwa jana jijini Dar es salaam. Programu hii ya kidijitali kutoka Ecobank ni mahususi kwa ajili ya kurahisisha huduma za kibenki kwa njia ya haraka na usalama kupitia simu za mkononi.
Naibu Waziri wa fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akipeana mkono na Kaimu Mwenyekiti wa bodi ya Ecobank Bw. Peter Machunde mara baada ya kuzindua rasmi huduma mpya ya kidijitali ya ‘Ecobank Mobile App’ iliyozinduliwa jana jijini Dar es salaam. Anayeshuhudia (katikati) ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Ecobank-Afrika Bw. Ade Ayeyemi na Mkurugezi Mkuu wa Ecobank Tanzania Bw. Enoch Osei-Safo.
Mkurugenzi Mkuu wa Ecobank Tanzania Bw. Enoch-Osei Safo akisoma hotuba yake wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma mpya ya ‘Ecobank Mobile App’ ambayo ilizinduliwa jana jijini Dar es salaam. Programu hii ya kidijitali kutoka Ecobank ni mahususi kwa ajili ya kurahisisha huduma za kibenki kwa njia ya haraka na usalama kupitia simu za mkononi.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Ecobank wakifuatilia kwa makini hafla ya uzinduzi wa huduma mpya ya kidijitali ya ‘Ecobank Mobile App’ iliyozinduliwa jana jijini Dar es salaam. Programu hii ya kidijitali kutoka Ecobank ni mahususi kwa ajili yakurahisisha huduma za kibenki kwa njia ya haraka na usalama kupitia simu za mkononi.
Kaimu Mwenyekiti wa bodi ya Ecobank Tanzania Bw. Peter Machunde akiteta jambo na Naibu Waziri wa fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma mpya ya kidijitali ya ‘Ecobank Mobile App’ iliyozinduliwa rasmi jana jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri wa fedha na Mipango Dr. Ashatu Kijaji akipakata maelezo kutoka kwa baadhi ya wafanyakazi wa Ecobank Tanzania kuhusiana huduma mbalimbali zinazopatikana kwenye programu ya kidijitali ya ‘Ecobank Mobile App’ iliyozinduliwa jana jijini Dar es salaam. Pamoja nae ni Kaimu Mwenyekiti wa bodi ya Ecobank Tanzania Bw. Peter Machunde.Mkuu wa kitengo cha huduma za kidijitali za kibenki Bw. Nachona Hussein akifafanua jambo wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma mpya ya ‘Ecobank Mobile App’ uliofanyika jana jijini Dar es salaam. Programu hii ya kidijitali kutoka Ecobank ni mahususi kwa ajili ya kurahisisha huduma za kibenki kwa njia ya haraka na usalama kupitia simu za mkononi.


Ecobank Tanzania (ETZ) imezindua huduma mpya ya Ecobank Mobile App, hii ni njia rahisi na ya haraka ya kibenki kupitia simu za mkononi. Ecobank Mobile App itawawezesha wateja kufanya miamala mbalimbali ya kifedha ikiwemo kuhamisha fedha - kote baina ya matawi na baina ya benki, kununua muda wa maongezi, Malipo ya Ankara, kuangalia viwango vya kubadilisha fedha za kigeni, maombi na kuangalia taarifa za benki, Malipo ya kibiashara, pamoja na huduma za Kadi na hundi.

Zaidi, Ecobank Mobile App itawawezesha wateja wa benki kuweza kuzifikia akaunti zao kupitia simu za mkononi na chaneli USSD, hivyo kuwahakikishia unafuu, upatikanaji, na kasi kwa saa 24 kwa juma huku ikiwaondolea ulazima wa kwenda au kupanga foleni kwenye matawi ya benki hiyo ambayo kwa sasa yapo nane (8).

Tukio hilo kwa sehemu kubwa lilihudhuriwa na halaiki ya watu ikiwa ni pamoja na Bodi ya Wakurugenzi wa Ecobank, Wateja na Wafanyakazi wa benki, Watendaji wa Kampuni ya Ecobank, Wanafunzi, Wanadiplomasia, Viongozi wa Serikali, Wawakilishi kutoka Benki Kuu na washirika wa kibiashara wa benki hiyo.

Mheshimiwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, alikuwa Mgeni Rasmi katika tukio hilo. Aliishukuru ETZ kwa ubunifu huo ambao, alisema utaenda mbali sana katika kuharakisha na kuimarisha juhudi za ushirikishwaji kifedha nchini Tanzania.

Aliipongeza benki hiyo kwa kuunga mkono juhudi na kauli mbiu ya awamu ya tano ya “Hapa kazi tu” kutokana na kuzindua bidhaa ambazo zimelenga kuwarahisishia maisha watanzania.

“Badala ya watu kubeba fedha mkononi sasa watabeba kidigitali” alisema na kuongeza kuwa utaratibu huu sio salama tu bali ni rafiki kwa kuokoa muda hasa katika kipindi hiki cha “Hapa kazi tu”.

Aliongeza kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi katika kuhakikisha benki zinafanya kazi kwa usalama na kuunga mkono uchumi wa kutembea bila fedha taslim.

Kwa mujibu wa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Ecobank Bw. Ade Ayeyemi, idadi ya watu ya kuvutia na sifa nyingine za pekee nchini Tanzania zinaenea vema katika dira ya kampuni ya kuongoza ushirikishwaji wa kifedha barani Afrika. 
 
"Ecobank Mobile Appinawafungulia fursa kubwa wateja kwa kuwawezesha kununua, kufanya miamala na kufanya biashara bila kubeba fedha taslimu. Ni huduma unganishi ya aina yake na ya kwanza kuwahi kutolewa na taasisi yoyote na kutumiwa kwa pamoja katika nchi 33 za Afrika. Tunataka kuinua uwezo wa kidijitali kwa kuuweka kiuhalisia uwezo huo katika vidole vya viganja vyenu." Alisema.

Mkurugenzi Mtendaji wa ETZ, Bw. Enoch Osei-SAFO alisema: "Siku ya leo ni ishara ya kilele cha safari yetu ya kuiweka mahali pazuri ETZ kama lango la kidijiti la kuvutia nchini Tanzania kwa watu binafsi, wafanyabiashara, wachuuzi na taasisi za serikali. 
 
Ecobank Mobile App pamoja na mambo mengine, itawasaidia wateja wetu kununua na kulipa bila kutumia fedha taslimu tena kwa urahisi zaidi kuliko walivyowahi kufikiri". Mbali na huduma zake za kibenki za kwenye mtandao kwa watu binafsi na wafanyabiashara pamoja na Ecobank Mobile App na visa/MasterCard za benki, “msukumo wa kidijiti” wa ETZ utashuhudia benki hii ikisonga mbele katika ufumbuzi zaidi wa ubunifu wa kidijitali ikiwa ni pamoja na kadi Prepaid, Akaunti ya Ecobank Xpress na Masterpass QR katika miezi ijayo mara tu vikwazo vyote vya udhibiti vitakapokuwa vimeondolewa. Ecobank Mobile App ilizinduliwa kwa mara ya kwanza huko Lagos, Nigeria, tarehe 20 Oktoba, 2016.

Katika kipindi kifupi kijacho, wateja wa ETZ watakuwa pia na uwezo wa kutumia Ecobank Mobile App kufungua akaunti ya Ecobank Xpress, ambayo ni akaunti rahisi ya kidijitali inayotamba kwenye e-KYC. Ecobank pia ni benki ya kwanza barani Afrika kushirikiana na Mastercard, huduma inayoongoza katika malipo ya kimataifa na teknolojia, kuleta wateja wake Masterpass QR.
 
Ufumbuzi huu mpya, usiotumia fedha taslimu katika kufanya malipo, utawezesha kuhifadhi kwenye mtandao na katika kupitia simu ya mkononi. Tunaishukuru Ecobank, kwani wafanyabiashara nchini Tanzania katika siku za usoni watakuwa na uwezo wa kutumia huduma ya Masterpass QR kukuza biashara zao.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 10, 2017

0
0























DC KOROGWE AWAONYA WATUMISHI WA HALMASHAURI KUACHA KUTUMIA VIBAYA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO.

0
0
Mkuu wa wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga,Mhandisi Robert Gabriel akizungumza jambo na Mkurugenzi wa Taasisi ya isiyoyakiserikali ya Vuga Development Initiative ya Jijini Arusha Azidu Kaonekana wa pili kulia ambao wameshirikiana na A Better World kutoka Canada kufanya ujenzi wa majengo matatu ya maabara kwenye shule ya sekondari ya Patema iliyopo kata ya Mpale Wilayan
Kaimu Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Korogwe Vijijini,Martha Kusare kulia akipokea msaada wa sola ya mobisol  kutoka kwa Mkurugenzi wa Taasisi isiyoyakiserikali ya Vuga Development Initiative ya Jijini Arusha,Azidu Kaoneka ikishirikiana na A Better World kutoka Canada kwa shule ya sekondari ya Patema ili kuweza kutumia nishati ya umeme kwa ajili ya matumizi yao ambapo sola hiyo na ujenzi wa maabara tatu zilizojengwa na taasisi hiyo  iligharimu kiasi cha sh.milioni 75
Mkurugenzi wa Taasisi isiyoyakiserikali ya Vuga Development Initiative ya Jijini Arusha,Azidu Kaoneka akifuatilia maendeleo ya wanafunzi wa shule ya sekondari Patema wilayani korogwe Mkoani Tanga
Mkurugenzi wa Taasisi isiyoyakiserikali ya Vuga Development Initiative ya Jijini Arusha,Azidu Kaoneka kulia akiteta jambo na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Patema Jerome Massawe wakati wakitembelea maabara hiyo
Mkurugenzi wa Taasisi isiyoyakiserikali ya Vuga Development Initiative ya Jijini Arusha,Azidu Kaoneka wa pili kulia akiangalia namna wanafunzi wa shule ya sekondari Patema wanayofundishwa masomo ya sayansi mara baada ya kukamilika maabara hiyo
Mkurugenzi wa Taasisi isiyoyakiserikali ya Vuga Development Initiative ya Jijini Arusha,Azidu Kaoneka kulia akiteta jambo na mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Patema,Jerome Massawe
 Muonekano wa Majengo ya  maabara hizo


WATUMISHI katika Halmashauri ya wilaya ya Korogwe mkoani Tanga wameonywa kuacha kutumia vibaya fedha za miradi zinazotokana na wafadhili kwenye maeneo yao kwani watakaobainika kufanya hivyo watashughulikiwa ikiwemo kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Hayo yalisemwa  na Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Mhandisi Robert
  Gabriel wakati akipokea taarifa ya umalizaji wa majengo ya matatu ya maabara yalijengwa na taasisi isiyoyakiserikali ya Vuga Development Initiative ya Jijini Arusha ikishirikiana na A Better World kutoka Canada kwa shule ya sekondari ya Patema iliyopo kata ya Mpale Wilayani humo.

Aidha wao kama viongozi wa serikali wilayani humo hawatakuwa na mdhara
  na watumishi ambao watabainika kuihujumu miradi ya maendeleo inayopelekwa kwenye maeneo yao na wafadhili mbalimbali kwani kufanya hivyo kunachangia kurudisha nyuma kasi ya ukuaji wa maendeleo.

“Nisema wazi kuwa watumishi badilikeni kwani mimi kama kiongozi wa
  wilaya hii sitamfumbia macho mtu yeyote ambaye atakuwa kikwazo cha maendeleo kwenye wilaya hii na niwaonye wenye tabia kama hiyo waiache mara moja.

Aidha alisema lazima watu wabadilike hasa wale wanaopewa majukumu ya
  kusimamia miradi hiyo kutoka kwa wafadhili na wawe wawazi wakati wa utekelezaji wake ili kujenga heshima kwa jamii na Taifa kwa ujumla.

“Baadhi yetu tunatumia fursa hizo vibaya na kujinufaisha kupitia fedha
  za wafadhili kinyume na hitaji husika,kufanya hivyo kunaweza kuwakimbiza wadau hao wa maendeleo na kutia doa kwa Taifa”Alisema Gabriel.

Awali akizungumza katika kikao hicho Afisa Elimu sekondari Halmashauri
  ya Korogwe Vijijini Patricia Mbigili alisema pamoja na jitihada kubwa ambazo wanazifanya kuhakikisha wanakamilisha suala la maabara lakini mpaka sasa zilizokamilika ni 5 kati ya 78 katika shule 26,ambapo kunahitajika maabara 3 kwa kila shule ikiwa ni za chemia,physician na bioligia.

Alisema ili kukabiliana na tatizo la ufaulu wa masomo ya sayansi
 
katika shule za sekondari maabara na uwepo wa walimu wa masomo hayo unahitajika kwa kiasi kikubwa ili kuweza kuwajengea uwezo wanafunzi kujifunza kwa vitendo.

Mbigili alisema jukumu la kuboresha miundombinu ya shule na makazi ya
  walimu ni la wananchi wote,serkali na taasisi zinazojitolea ili kutimiza azma ya serikali ya kuboresha sekta ya elimu kama ilivyoanza kwa madawati na elimu bure.

Naye kwa upende wake, Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Azidu Kaoneka
  alisema umaliziaji wa maabara 3,nyumba 1 ya walimu na kuwawekea kifaa cha kuzalisha umemekupitia jua (mobisol) ambapo kiasi cha shilingi milioni 75 zimetumika.

Azidu alisema taasisi hiyo inaimani kubwa kwa kushirikiana na wananchi
 pamoja na serikali wanaweza kujenga mazingira rafiki ya walimu na wanafunzi kwa kuboresha miundombinu ya mashule pamoja na nyumba za walimu kama ilivyofanyika shuleni hapo.
 Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

TADB YAANZA KUTEKELEZA MKATABA WA USHIRIKIANO KATI YA TANZANIA NA MOROCCO

0
0
Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imeanza kutekeleza kwa vitendo Mkataba wa Ushirikiano uliosainiwa kati ya Serikali ya Tanzania na Morocco wakati wa Ziara ya Mfalme wa Morocco Mtukufu Mohammed VI alipotembelea Tanzania kwa mwaliko wa Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli mnamo mwezi Oktoba 2016.

Katika kutekeleza makubaliano hayo, ujumbe wa TADB ukiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Bw. Francis Assenga na Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha, Bw. Albert Ngusaru upo nchini Morocco, pamoja na mambo mengine kuainisha maeneo ambayo Benki hiyo itashirikiana na Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Morocco (GCAM) na kuwekeana mikakati ya utekelezaji. 

Kwa mujibu wa Bw. Assenga, pamoja na kupanga mikakati hiyo, ujumbe huo ulipata fursa ya kukagua miradi kadhaa ya kilimo na ufugaji ambayo Tanzania inaweza kuianzisha kwa mafanikio.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TAD, Bw. Francis Assenga (Katikati) akiwa na Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha, Bw. Albert Ngusaru (Watatu kushoto) wakiwa na wenyeji wao Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Morocco (GCAM).
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) Bw. Francis Assenga (wa pili toka kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na mwenyeji wake Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Kilimo ya Morocco (Credit Agricole) Bw. Jamal Eddine Wl Jamali (Katikati). Wengine ni Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha wa TADB  Bw. Albert Ngusaru na Wakurugenzi wawili wa Benki ya Credit Agricole Bi. Dkhil Mariem (Kushoto) na Bi Leila Akhmisse (Kulia).
Ujumbe wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ukipatiwa maelezo juu ya miradi ya kilimo inavyoendeshwa nchini Morocco wakati Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB Bw. Francis Assenga (Mwenye Kaunda Suti) na Bw. Albert Ngusaru Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha (Mwanye Daftari) walipotembelea Morocco wiki hii kuanza utekelezaji wa Mkataba wa Ushirikiano kati ya TADB na GCAM.
Ujumbe wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ukipatiwa maelezo juu ya miradi ya kilimo inavyoendeshwa nchini Morocco wakati Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB Bw. Francis Assenga (Mwenye Kaunda Suti) na Bw. Albert Ngusaru Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha (Mwanye Daftari) walipotembelea Morocco wiki hii kuanza utekelezaji wa Mkataba wa Ushirikiano kati ya TADB na GCAM.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania Bw. Francis Assenga (Katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Credit Agricole na Tamwil El Fellah wakati walipokagua miradi mbalimbali ya kilimo na ufugaji katika vijiji vya mji wa Khemisset nchini Morocco jana. Kulia kabisa ni Bw. Albert Ngusaru ambaye ni Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha wa TADB.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) Bw. Francis Assenga (kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na mwenyeji wake Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Kilimo ya Morocco (Credit Agricole) Bw. Jamal Eddine W. Jamali (Katikati). Kulia ni Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha wa TADB  Bw. Albert Ngusaru. 
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Bw. Francis Assenga (Kushoto) akiwa na Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha wa TADB  Bw. Albert Ngusaru (Kulia) walipotembelea Benki ya Kilimo ya Morocco (Credit Agricole).

Rwanda yapitisha muswada wa sheria ya kufanya Kiswahili kuwa lugha rasmi

0
0

Na. Immaculate Makilika -MAELEZO


Wabunge nchini Rwanda wamepitisha kwa kauli moja muswada wa sheria ya kuifanya lugha Kiswahili kuwa lugha rasmi nchini humo.

Kufuatia hatua hiyo, sasa Kiswahili nchini Rwanda kinakuwa moja kati ya lugha tatu za Kinyarwanda, kiingereza na kifaransa zinazozungumzwa na wananchi kama lugha rasmi miongozi mwao na kukifanya Kiswahili kuwa lugha ya nne nchini humo.

Lugha ya Kiswahili nchini Rwanda inatazamiwa kuanza kutumika katika shughuli za uongozi na katika nyaraka za kiofisi.

Aidha, Waziri wa Michezo na Utamaduni nchini Rwanda, Julienne Uwaci alisema kuwa uamuzi huo umefikiwa kutokana na lugha hiyo kuwa na wazungumzaji wengi katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki hivyo kuweza kurahisisha ushirikiano katika sekta mbalimbali za maendeleo.

Aliongeza kuwa, “Kiswahili ni lugha rasmi ambayo nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wanatakiwa kuitumia kwa kuwa kitaongeza tija kwa nchi ya Rwanda kufaidi matunda ya utengano wa kiuchumi”

Wabunge mbalimbali wa nchi hiyo wametoa maoni, akiwemo mbunge Jean Baptiste Rucibigango ambapo alisema kuwa “Kiswahili ni lugha inayozungumzwa na watu wengi katika ukanda wa Afrika Mashariki na hakika itakuwa na faida kuzungumzwa nchini Rwanda”.

Kiswahili kuwa lugha rasmi katika nchi za ukanda wa Afrika Mashariki, kunaleta faida nyingi ikiwemo kuongeza wigo wa shughuli za kibiashara na kukuza uchumi wa nchi wananchama ambazo ni Tanzania, Kenya, Rwanda, Uganda, Burundi na Sudani ya Kusini, pamoja na kuimarisha ushirikiano na mahusiano ya kidiplomasia baina ya nchi hizi.

Hatua hiyo ya Rwanda kuifanya lugha ya Kiswahili kuwa lugha ya rasmi ya Taifa ni fursa ya adhimu kwa nchi jirani zinazozungumza zaidi Kiswahili ikiwemo Tanzania, kwani itasaidia raia wake kuwa na nafasi murua kushiriki katika shughuli za kibiashara na elimu.

MABALOZI WA JAMHURI YA MUUNGANO WAKUTANA NA RAIS SHEIN

0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mabalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioteuliwa hivi karibuni kuiwakilisha Tanzania katika Nchi mbali mbali (pichani) Rais akipeana mkono na Mhe,Balozi Emmanuel  John Nchimbi atakayekwenda nchini Brazil
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na   Mabalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioteuliwa hivi karibuni kuiwakilisha Tanzania katika Nchi mbali mbali Duniani (Picha na Ikulu)

KINANA AMJULIA HALI DEREVA WA GARI LILILOPATA AJALI NA KUUA VIONGOZI WANNE WA CCM MKOANI KILIMANJARO

0
0
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimjulia hali jana, Jackson Kimambo ambaye amelazwa katika hospitali ya KCMC Moshi mkoani Kilimanjaro baada ya kupata ajali wakati akiendesha gari kutoka kwenye Maadhimisho ya miaka 40 ya CCM mkoani humo, Jumapili, Feb 5, 2017. Katika ajali hiyo watu sita walikufa wakiwemo viongozi wanne wa CCM ambapo Kinana yupo mkoani hapa, kuongoza mazishi ya vingozi hao. Wapili kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Sid Mecky Sadick
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akisaini kitabu ha wageni Ofisini kwa Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya KCMC ya Moshi, Kilimanjaro, Dk. Gileard Masenga (kulia), baada ya kumjulia hali dereva huyo
  Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya KCMC ya Moshi, Kilimanjaro, Dk. Gileard Masenga, akiwaaga Katibu Mkuu wa CCM Abdulraman Kinana na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Said Mecky Sadick
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiagana na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadick, baada ya zara hiyo ya kumjulia hali, dereva huo. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

KAMANDA SIRRO:UPEPELEZI BADO UNAENDELEA KWA WASHTAKIWA WA DAWA ZA KULEVYA

0
0
Viewing all 46201 articles
Browse latest View live




Latest Images