Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

BEI YA MADAFU LEO


ZAIDI YA WAKULIMA 60,000 KUNUFAIKA NA MRADI WA (AMDT)

$
0
0

Pichan ni Martin Mgallah ambaye ni Meneja mradi wa Taasisi ya kuendeleza mifumo ya kimasoko katika kilimo Tanzania (AMDT)Picha na Vero Ign atus Blog 27januari2017.
Wakwanza kushoto ni akiyevaa tshirt nyekundu ni Hellen Wakuganda kutoka Asasi ya kusaidia sekta binafsi ya kilimo(PASS)akifuatiwa na aliyepo katikati Al-Amani Mutarubukwa kutoka (AMDT)akifuatiwa na Juliana Nganyangwa kutoka (AMDT)wakitoa elimu kwa wakulima Jijini Arusha.Picha na Vero Ignatus Blog.27 january 2017.


Na.Vero Ignatus,Arusha.

Taasisi ya kuendeleza mifumo ya kimasoko katika kilimo Tanzania (AMDT)imewataka wakulima kubadilisha kilimo kuwa biashara ,waondokane na kilimo cha kawaida na kuwa na kilimo cha kisasa na kufahamu kilimo mkataba.

Hayo yamesemwa na meneja mradi Martin Mgallah alipokuwa katika maonyesho ya zana za kilimo Jijini Arusha na kusema kuwa wametenga zaidi ya dola za kimarekani milioni kumi na tano kwaajili ya kuwawezesha wakulima katika zao la Alizeti pekee ndani ya miaka mitano (2016-2021)

“Taasisi itamuwezesha mkulima kuongeza kipato chake cha mwaka kwa kubadilisha kilimo kuwa biashara,tunaangalia pia mfumo wa masoko,tunamuwezesha mkulima kufahamu kilimo mkataba yaani akishalima na kuvuna mazao yake asihangaike tena kutafuta soko bali atauza mazao yake kwa bei nzuri,tunamuunganisha na soko moja kwa moja”alisema meneja mradi Martin.

Amesema kuwa wakulima zaidi ya 60,000 watanufaika na mradi huo,huku akianisha mikoa ambayo wataanza nayo ambayo ni pamoja na Manyara,Shinyanga,Singida,Dodoma,Iringa,Njombe,Mbeya Songwe ,Katavi,Lindi,Rukwa na Mtwara.

Martin amesema kuwa lengo kubwa la( AMDT) kuhakikisha kuwa mkulima anazalisha kilicho bora ,amesema mazao ambayo wataanza nayo ni Alizeti,mahindi,na jamii ya mikundekunde katika mikoa tajwa.

Aidha amesema kwaba wanampatia mkulima elimu sahihi,namna ya kulima kilimo cha kisasa,kumuelimisha mkulima kuwa na bima itakayomuwezesha kupata nyezo za kisasa za kilimo hivyo amewataka wakulima kuwatembelea ili waone ni kwa namna gani wanaweza kunufaika na program hii.

UN Tanzania yaadhimisha Siku Kuwakumbuka Wahanga wa Maangamizi ya Moto

$
0
0
Shirika la Umoja wa Mataifa nchini limeadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kuwakumbuka Wahanga wa Maangamizi Makuu ya Moto dhidi ya Wayahudi kwa kuwakutanisha wanafunzi kutoka shule mbalimbali za Dar es Salaam na kuwapa elimu kuhusu maangamizi hayo.

 Akizungumza katika maadhimisho hayo, Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Stella Vuzo alisema ni jambo jema kwa wanafunzi hao kupata elimu kuhusu maangamizi ambayo yalifanywa na kiongozi wa zamani wa Ujerumani, Adolf Hitler kwani hata wao wanaweza kuja kuwa viongozi kwa miaka ijayo hivyo kama watapatiwa elimu mapema watajifunza ni mambo gani kiongozi anapaswa kufanya na yapi hapaswi kwa faida ya kila mmoja. 

“Kwa nyie kama wanafunzi ambao kwa miaka ya baadae wengine mtakuwa viongozi mnapaswa kujifunza kwa jambo kama hili ambalo alifanya Hitler kuwa sio jambo jema, kila binadamu ana haki sawa hakuna ambaye anamshinda mwenzake na huo ndiyo msimamo wa Umoja wa Mataifa,” alisema Vuzo. 
Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Stella Vuzo akizungumza na wanafunzi kutoka shule ya Chang'ombe, Kibasila, Jitegemee, Kigamboni, Dar es Salaam, Gerezani, Airwing na vijana kutoka Temeke Youth Development Network (TEYODEN) kuhusu Siku ya Kimataifa ya Kuadhimisha na Kuwakumbuka Wahanga wa Maangamizi Makuu ya Moto ambapo watu mil. 55 wanakadiriwa kuwa walipoteza maisha. (Picha na Rabi Hume - MO Dewji Blog)

Aidha Afisa Habari huyo alizungumza kuhusu siku mauaji ambayo yalifanywa na Hitler wakati akiwa kiongozi wa Ujerumani katika kipindi cha mwaka 1933 hadi 1939, “Alikuwa akichagua watu ambao wanaonekana kuwa tofauti na kuwaondoa katika jamii ya Wajerumani, anawapeleka katika kambi maalumu na anawaua wengine wanawekwa katika kambi maalumu wanafanyishwa kazi ngumu bila malipo na waliokuwa wanashindwa na wao wanauawa kwa kuchomwa moto hadi kufa, 

Vuzo aliongeza kwa kusema kuwa, “Mauaji ya moto ni mauaji hatari kuwahi kutokea duniani, ilikuwa ni dhana ya Adolf Hitler kutaka Wanazi kuwa ni watu ambao wamenyoka lakini kumbe ilitakiwa aishi na watu wote katika jamii lakini alipinga hilo,” “Lakini pia alikuwa hawapendi Wayahudi, walikuwa wafanyabiashara wazuri lakini yeye aliwapinga na hata akawa anawambia wananchi wake kuwa Wayahudi kuwa hawafai katika jamii na wasinunue kitu chochote kutoka kwao.” 
Afisa Habari wa Ubalozi wa Ujerumani nchini, Susann Keller akizungumza kuhusu Siku ya Kimataifa ya Kuadhimisha na Kuwakumbuka Wahanga wa Maangamizi Makuu ya Moto.

Kwa upande wa Afisa Habari wa Ubalozi wa Ujerumani nchini, Susann Keller alisema kitendo ambacho kilifanywa na Hitler hakikubaliki na ni jambo ambalo Wajerumani wamekuwa wakijutia kila muda kutokana na vitendo vya kikatili ambavyo vilifanyika vilivyosababisha watu wanaokadiriwa kufikia milioni 55 na kati yao milioni sita wakiwa ni Wayahudi kupoteza maisha. Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni “Elimu kwa ajili ya maisha Bora ya Baadae.” Na Rabi Hume, MO Dewji Blog 
Wanafunzi kutoka shule ya Chang'ombe, Kibasila, Jitegemee, Kigamboni, Dar es Salaam, Gerezani, Airwing na vijana kutoka Temeke Youth Development Network (TEYODEN) wakiangalia video inayoelezea historia ya Adolf Hitler na mauaji ambayo alikuwa akiyafanya.
Baadhi ya wanafunzi wakitoa maoni na kuuliza maswali.



Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja.

KUMBILAMOTO AKABIDHI MIFUKO 12 YA SARUJI SHULE YA MSINGI MIEMBENI

$
0
0
 Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto akizungumza na mtoto mwenye ulemavu wa ngozi katika shule ya msingi Miembeni
 Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto akimkabidhi mifuko mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa shule ya miembeni, Kuruthumu Hamisi


Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii.
Katika kutekeleza sera ya elimu bure Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa Vingunguti , Omary Kumbilamoto amekabidhi mifuko 12 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi Miembeni.

Kumbilamoto amesema kuwa mifuko hiyo ya saruji ni kwa ajili ya ujenzi wa  sakafu ya madarasa mawili ambayo yamekamilika lakini yalikuwa ayana sakafu.
“mimi nilipita hapa nikafanya ziara na kujionea mapungufu yaliyopo katika ujenzi wa madarasa haya ambayo yalianza kujengwa na kamati ya maendeleo ya shule kwa kushirikiana na wananchi hivyo nimeona nichangie hii mifuko 12 ya Saruji”

Kumbilamoto amewashukuru wananchi waliofika katika hafla hiyo kwani wameweza kujichangisha  na kupata shilingi laki mojana ishirini ambazo zitaweza kununulia mchanga wa kujengea.Ametoa wito kwa wadau wengine wa maendeleo kuendelea kumuunga mkono Rais Magufuli kwa kuweza kusaidia maendeleo ya elimu katika kata ya vingunguti.
Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule hiyo Hidaya Hamisi amemshukuru Naibu meya kwa msaada huo ambao utaweza kusaidia kukamilika kwa ujenzi wa madarasa hayo na kuondoa msongamano kwa wanafunzi.
 Naibu meya wa Manispaa wa Ilala, Omary Kumbilamoto akikabidhi mifuko ya saruji kwa mwalimu mkuu wa shule ya msingi Miembeni, Hidaya Hamisi
 Picha ya pamoja na ya Naibu Meya na wazazi wa wanafunzi wanaosoma Miembeni shule ya msingi

INDIA YAFUNGUA JENGO JIPYA LA UBALOZI JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka jiwe la msingi la ufunguzi wa jengo jipya la Ubalozi wa India lililopo mtaa wa Shaaban Robert jijini Dar es Salaam mbele ya Balozi wa India Bw. Sandeep Arya .
Balozi wa India hapa nchini Bw. Sandeep Arya akimuonesha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan picha mbali mbali zenye kuonyesha historia ya urafiki baina ya Tanzania na India wakati wa ufunguzi wa jengo jipya la ubalozi wa India jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa ufunguzi wa Jengo jipya la Ubalozi wa India hapa nchini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa ufunguzi wa Jengo jipya la Ubalozi wa India lililopo mtaa wa Shaaban Robert jijini Dar es Salaam.
Balozi wa India hapa nchini Bw. Sandeep Arya akihutubia wakati wa uzinduzi wa Jengo jipya la Ubalozi wa India hapa nchini.
Vikundi vya Utamaduni wa Kihindi vikionyesha uwezo wa kuzicheza ngoma za asili.

........................................................................................

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassana ameishukuru Serikali ya India kwa ufadhili wake wa miradi ya maji katika miji 17 nchi ambayo inalenga kupunguza tatizo la maji kwa wananchi wengi nchini.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo Jijini Dar es Salaam katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 68 ya Siku ya Kitaifa ya Jamhuri ya India sherehe ambazo zimeambatana na Uzinduzi rasmi wa majengo ya ofisi mpya ya Ubalozi wa India hapa nchini.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema ufadhili wa miradi ya Maji pamoja na miradi mingine unaofanywa na Serikali ya India kwa Tanzania Bara na Zanzibar unadhihirisha wazi mahusiano mazuri yaliyopo yaliyoasisiwa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mahatma Gandhi wa India.

Makamu wa Rais amesisitiza kuwa India ni moja ya washirika muhimu katika juhudi za kuwaletea wananchi maendeleo na Serikali itaendelea kufanya kazi kwa karibu katika maeneo mengi ikiwemo ya kikanda na kimataifa kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa pande Mbili yaani Tanzania na India.

Amesema kwa miaka mingi sasa mahusiano ya kindugu yamekuwa yaakiimarika katika sekta mbalimbali ikiwemo kisiasa,kidiplomasia,kibiashara, masuala ulinzi, utamaduni na mwingiliano wa watu na watu.

Makamu wa Rais pia ameishukuru Serikali ya India kwa msaada wake wa shilingi milioni 500 alioutoa kwa wananchi wa Mkoa wa Kagera ambao walikubwa na tetemeko la ardhi mwaka jana.

Ameeleza kuwa Mahusiano kati ya India na Tanzania yamekuwa na manufaa makubwa ambapo idadi kubwa ya watanzania wanaenda kupata mafunzo mbalimbali nchini India hasa Madaktari na wamekuwa msaada mkubwa katika kuokoa maisha ya Watanzania.

Katika hafla hiyo, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan kwenye hotuba yake alitoa salamu za rambirambi kwa Serikali ya India kufuatia ajali ya treni iliyotokea katika Jimbo la Andhra Pradesh na kusababisha vifo vya watu 30 na kujeruhi wengine.

“Kwa niaba ya Serikali na wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania napenda kutoka salamu za Pole kwa familia za wafiwa na majeruhi katika kipindi hiki kigumu kwa kumwomba Mwenyezi Mungu azipumzishe roho za marehemu mahali pema peponi na tunawaombea majeruhi wapone haraka. ’’
 Kwa upande wake, Balozi wa India hapa nchini Sandeep Arya amemhakikishia Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Serikali ya India itaendelea kudumisha na kuendeleza mahusiano mazuri yaliyopo kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa pande zote Mbili.

KUWENI MAKINI NA MATAPELI WA FEDHA KUPITIA MITANDAO YA SIMU

$
0
0
Watumiaji wa simu za mkononi wameaswa kutokutoa namba za siri za simu zao wanapopigiwa simu au kutumiwa ujumbe mfupi yaani SMS. Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Bi. Jacquiline Materu, alisema“Natoa wito kwa wateja wetu kuwa makini na matapeli wanaowapigia simu na kuwafahamisha kuwa wameshinda fedha za Promosheni ya Nogesha Upendo au bonasi ya M-Pesa. 

Vodacom Tanzania haina utaratibu wa kuwapigia simu wateja kuhusiana na mgao wa fedha za bonasi ya M-Pesa bali inatoa mgao huo kwa kadri ya mteja alivyotumia huduma hii na rekodi zote za matumizi kampuni inazo sambamba na utaratibu uliowekwa na Benki Kuu. 

Materu alisema kampuni inawapigia simu wateja wa Promosheni ya Nogesha Upendo tu na kuwajulisha kuwa wameshinda na fedha zao hutumwa moja kwa moja kwa njia ya M-pesa ndani ya masaa 48 bila kuwataka wateja hao kutoa taarifa zozote za siri juu ya namba zao. Wengine wanaowapigia simu wateja kuhusiana na bonasi ni matapeli ambao wanataka kupata namba za siri na kuwatajia kiasi gani cha fedha mlizonazo ili wapate fursa ya kuwaibia fedha,” alisema Materu.
Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Bi. Jacquiline Materu

TAMKO LA WAZIRI UMMY MWALIMU KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA UKOMA DUNIANI TAREHE 29/01/2017

$
0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu

JESHI LA POLISI KANDA MAALUM YA DAR ES SALAAM LIMEKAMATA MAGARI MATANO

$
0
0
Jeshi la polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam limekamata magari matano ambayo yanasadikiwa kuwa yaliibiwa katika vipindi tofauti katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamishina wa Polisi wa kanda maalm ya Dar es Salaam CP Saimon Sirro amesema kuwa mnamo Januari 22 mwaka huu jeshi la polisi lilikamata gari aina ya Toyota karina lenye namba za usajili T 950 DFN baada ya msako  wa jeshi hilo katika maeneo ya Bandari jijini Dar es salaam.

‘’Gari jingine ambalo tumelikamata Toyota landcruseir Prado lenye namba zasajili T 959 DFT gari hili katika uchunguzi wetu liliibiwa September 16 mwaka jana na badaye kuonekana maeneo ya Mwanza januari 21 Mwaka huu’’ Alisema Kamishina Simon Sirro.

Kamishina Sirro amesema kuwa jeshi hilo pia limewakamata watuhumiwa kwa wizi  wa pikipiki katika maeneo mbalimbali ya jijini  Dar es salaam na Pwani pamoja na mkoa wa Morogoro baada ya operesheni iliyofanywa na jeshi hilo .

Amesema kuwa jeshi hilo limewakata vinara saba wa utengenezaji wa kadi bandia za chanjo ya homa za manjano ambapo huziuza kwa watu wanaofika katika hospitali ya Mnazi moja kwaajili ya kupata huduma za matibabu kabla yakusafiri nje ya nchi.

‘’Baadhi yawatuhumiwa waliokamatwa ni pamoja na Aisha Hassani(29) mkazi wa Vingunguti, Yakobo Msenga (42) mkazi wa Chanika, Oliver Bwegege mhamasishaji (58) mkazi wa Kigogo’’ Ameongeza Sirro.
 Kamishina wa Polisi wa kanda maalm ya Dar es Salaam CP Saimon Sirro akizugumza na waandishi wa habari juu ya Jeshi la polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam kuhusu kukamata magari matano ambayo yanasadikiwa kuwa yaliibiwa katika vipindi tofauti katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam. Picha na Emmanuel massaka, Globu ya jamii.
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro akionyesha silaha aina ya SHORTGUN PUMP ACTON iliyo kutwa nyumbani kwa mtuhumiwa huko Boko njiapanda leo jijini Dar es Salaam.
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro akionesha kadi bandia za chanjo ya homa ya manjano zilizokamatwa maeneo ya Hospital ya Mnazi mmoja jiji Dar es Salaam.
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro akionesha magari yaliyokuwa yameibiwa katika sehemu mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam leo. Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro akionesha mitambo ya kutengenezea Gongo jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Simon Sirro  akionesha mkasi wa kuvunja.

BENKI YA KILIMO YAJIDHATITI KUWAINUA WAKULIMA

$
0
0
 Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TABD) Bw. Francis Assenga akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es saalam kuhusu mikakati ya Benki hiyo kuwainua wakulima wadogo ili waweze kushiriki katika ujenzi wa uchumi wa viwanda. Kushoto ni Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha wa Benki hiyo, Bw. Albert Ngusaru.
  Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji  wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TABD) Bw. Francis Assenga akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam ambapo alibainisha kuwa Benki hiyo imekuwa ikitoa mikopo kwa wakulima ili kuziba pengo la upatikanaji wa fedha kwenye minyororo ya thamani katika sekta za kilimo, mifugo, uvuvi na mazao ya misitu. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara Bw. Geofrey Mtawa na kushoto Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha Bw. Albert Ngusaru.
 Kaimu Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara Bw. Geofrey Mtawa akiwaeleza waandishi wa habari kuhusu mpango wa Benki hiyo kuhakikisha kuwa wakulima wote wanawezeshwa ili kuinua kilimo hapa nchini. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji  wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TABD) Bw. Francis Assenga.
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania leo Jijini Dar es salaam.

(Picha na Frank Mvungi- Maelezo)

DKT. KIGWANGALLA ATOA SIKU 7 KWA KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA KUMALIZA CHANGAMOTO ZINAZOIKUMBA HOSPITALI YA RUFAA YA KITETE

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na watoto Dkt. Hamisi Kigwangalla ametoa siku siku 7  kwa Katibu Mkuu kumaliza changamoto zinazoikumba hospitali ya Rufaa ya Kitete iliyopo mkoani Tabora.

Dkt. Kigwangalla ameyasema hayo alipofanya  ziara ya kushtukiza  katika hospitali ya Rufaa ya Kitete Mkoani Tabora na kukagua miradi ya  chumba cha upasuaji  pamoja na Chuo cha AMOS kilichopo mkoani humo .

“Chumba hiki cha upasuaji na  Chuo vimekamilika mpaka thamani za ndani tangu miaka miwili iliyopita Sababu ni kwamba Serikali yetu haikutoa counter-part funding huku Benki ya Maendeleo ya Afrika  ikiwa imetimiza ahadi yake kwa asilimia mia moja”alisema Dkt. Kigwangalla.

Hata hivyo Dkt. Kigwangalla amesema kuwa amefurahishwa kutekelezwa kwa baadhi ya maagizo aliyoyatoa  kama vile  kuondoa msongamano wa wagonjwa kwenye wodi za wanawake wajawazito na watoto.

Kwa mujibu wa Dkt. Kigwangalla amesema kuwa uongozi wa Hospitali hiyo umefanikiwa  kuboresha huduma ya upatikanaji wa dawa zote muhimu na huduma kwa wateja ikiwemo  lugha nzuri kutoka kwa wahudumu imeboreshwa..

Aidha Dkt. Kigwangalla amesema anashukuru uongozi wa Hospitali hiyo kwa kufanya ukarabati mkubwa wa majengo ya wodi za wagonjwa na sasa hakuna tena msongamano na huduma zinatoka kwa wakati sahihi.

MUHIMBILI YATOA MSAADA WA VITANDA KWA HOSPITALI YA WILAYA YA KIBITI LEOA

$
0
0
 Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Agenes Mtawa akimkabidhi vitanda Mhandisi wa Ujenzi wa Halmashauri ya Kibiti, Ayub Ngereza kutokana na hospitali ya halmashauri hiyo kuwa na upungufu wa vitanda vinavyotumiwa na kinamama wakati wa kujifungua. Mhandisi Ngereza amepokea msaada wa vitanda hivyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Wilaya ya Kibiti. 
 Mhandisi Ngereza akizungumza na waandishi wa habari leo baada ya kukabidhiwa vitanda hivyo na uongozi wa hospitali hiyo.
 Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga, Mtawa katika hospitali hiyo akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhi msaada huo kwa Halmashauri ya Kibiti. 
Baadhi ya wafanyakazi wa Halmashauri hiyo wakipakia vitanda hivyo kwenye gari leo

Katika kuendelea kuboresha mazingira ya utoaji huduma ya afya ya uzazi kwa kina mama, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo imetoa msaada wa vitanda viwili vya kujifungulia kwa Hospitali ya Wilaya ya Kibiti mkoani Pwani.

Akikabidhi vitanda hivyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili , Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga Agnes Mtawa amesema lengo ni kuboresha huduma za afya na kumuwezesha mama kujifungua katika mazingira salama.

"Wenzetu wanahuitaji mkubwa wa vitanda vya kujifungulia hivyo tumeona tuwasaidie, natoa wito kwa Watanzania watambue kwamba hospitali hizi ni za kwetu na zinawahudumia Watanzania hivyo wale wenye nafasi ya kusaidia ni vema wakafanya hivyo ili kuendelea kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto" amesema Sister Mtawa.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo wa Huduma za Uuguzi na Ukunga tatizo la ukosefu wa vitanda husababisha Mkunga kupata shida wakati mama anapojifungua.

Naye Mhandisi Ujenzi wa Halmashauri ya Kibiti, Ayub Ngereza akipokea msaada huo kwa niaba ya Mkurugenzi wa wilaya ya Kibiti, ameushukuru uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa msaada huo kwani utasaidia kuboresha huduma za afya.

Hivi karibuni Hospitali ya Taifa Muhimbili ilikabidhi msaada wa vitanda vitano vya kujifungulia kwa Hospitali ya wilaya ya Mafya ambapo kwa mujibu wa Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Abdalah Bhai walihitaji vitanda vitano ambao ulikidhi mahitaji.

WAZIRI KAIRUKI AFUNGUA MKUTANO WA MWAKA WA WAKALA ZA SERIKALI AZITAKA ZIFANYE KAZI NA KUJITEGEMEA

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akifungua mkutano wa Watendaji Wakuu wa Wakala za Serikali leo jijini Dar es salaam.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Laurean Ndumbaro akiongea na Watendaji Wakuu wa Wakala za Serikali nchini, leo jijini Dar es salaam, kushoto kwake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb)
 
Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Serikali Mtandao (eGA), Dkt. Jabiri Bakari akimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) (hayupo pichani) alipokuwa akifungua mkutano wa Watendaji Wakuu wa Wakala za Serikali leo, jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Henry Mambo (kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Uchambuzi na Ushauri wa Kazi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Mick Kiliba wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) (hayupo pichani) alipokuwa akifungua mkutano wa Watendaji Wakuu wa Wakala za Serikali nchini leo, jijini Dar es salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akisikiliza mada pamoja na washiriki wengine wakati wa mkutano wa Watendaji Wakuu wa Wakala za Serikali nchini, uliofanyika leo jijini Dar es salaam.
Washiriki wa mkutano wa Watendaji Wakuu wa Wakala za Serikali nchini wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) (hayupo pichani) alipokuwa akifungua mkutano wa Watendaji Wakuu wa Wakala hizo nchini leo, jijini Dar es salaam.

MADEREVA WAKANUSHA TAARIFA ZA KUWEPO KWA MGOMO

$
0
0
 Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADWA) Bw. Shabani Mdemu (kulia) akikanusha taarifa za upotoshaji zilizotolewa na baadhi ya mitandao ya kijamii hapa nchini kuwa madereva wamepanga kufanya mgomo mapema mwezi Februari, amesema chama hicho hakijapanga mgomo wowote kama ilivyotangazwa hivyo wananchi wapuuze taarifa hizo kwa kuwa si za kweli. Kushoti ni Msemaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge, Kazi, Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Ridhiwani Wema.
Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi Wasafirishaji kwa Njia ya Barabara Bw. Salum Abdallah akitoa wito kwa wananchi kupuuza taarifa za kuwepo kwa mgomo wa madereva kama ilivyoripotiwa na baadhi ya mitandao ya kijamii na kuliomba Jeshi la Polisi kuchukua hatua kwa wote waliohusika kusambaza taarifa hizo za upotoshaji. Kulia ni Mwenyekiti wa chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADWA) Bw. Shabani Mdemu.
Msemaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Ridhiwani Wema akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam kuhusu taarifa za upotoshaji kuhusu kuwepo kwa mgomo wa madereva zilizosambazwa kupitia mitandao ya kijamii.


(Picha na Frank Mvungi-Maelez

MTU MMOJA AUWAWA KWA TUHUMA ZA WIZI WA KUKU MKOANI MWANZA

$
0
0

MTU mmoja Mkazi wa Kijiji cha Kanyelele , Safari Bungate (51) ameuawa na kundi la watu waliojichukulia sheria mkononi kwa kumpiga mtu huyo mawe na fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake baada ya kuiba kuku katika  nyumba ya mmiliki wa kuku, Tetema mathias (40), mkulima na mkazi wa kijiji cha Kanyelele, kitendo ambacho ni kosa kisheria.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Naibu, Kamishina, Ahmed Msangi amesema tukio hilo limetokea  Januari 26  mwaka huu majira ya saa nne usiku katika kijiji cha Kanyelele tarafa ya Usagara Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.

Taarifa  hiyo inadaiwa kuwa mwenye nyumba, Tetema Mathias akiwa amelala  na familia yake, alikuja mtu/marehemu akaingia ndani kupitia dirishani na kuiba kuku mmoja, ndipo wakati alipokuwa anataka kuondoka Mathias alimuona na kuanza kupiga yowe ya mwizi akiomba majirani waje wamsaidie kumkamata huku akimkimbiza barabarani.

Hata hivyo taarifa ilidai kuwa  watu/ majirani waliamka na kufanikiwa kumkamata  marehemu akiwa na kuku amemshikilia kisha wakaanza kumpiga  kwa mawe na fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake  kitendo kilichosababisha  mtu/ marehemu huyo  kupoteza fahamu na baada ya muda mchache  alifariki dunia.  

Taarifa  ya Kamanda Msangi amesema raia wema walitoa taarifa polisi ndipo askari walifika eneo la tukio na kukuta mtuhumiwa wa wizi akiwa tayari amefariki dunia na mwili wa marehemu tayari umefanyiwa uchunguzi na daktari na kukabidhiwa kwa ndugu wa marehemu kwa ajili ya mazishi.

Jeshi la Polisi linamshikilia Tetema Mathias kwa mahojiano zaidi kuhusiana na tukio hilo. Naibu, Kamishina Msangi ametoa  wito kwa wakazi wa Jiji na Mkoa wa Mwanza, akiwataka kuacha tabia ya kujichulia sheria mkononi kwani ni kosa la jinai, aidha anawataka wananchi pindi wanapomkamata mhalifu wamfikishe katika vyombo vya sheria ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yake.

Pia Naibu Kamishina Msangi amesema Januari 26 majira ya saa 06:00 asubuhi  na kuendelea jeshi la polisi mkoa wa Mwanza linaendesha  operesheni ya kukamata waendeshaji wa vyombo vya moto hasusani waendesha pikipiki (bodaboda) ambao hawafuati sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani. Aidha katika operesheni hii askari watakuwa wakikamata magari na waendesha pikipiki ambao hawana leseni, madereva na abiria wasio vaa kofia ngumu, kubeba abiria zaidi ya mmoja kwenye pikipiki (mshikaki), kukunja namba za usajili wa pikipiki, kuendasha wakiwa wamelewa na kutoboa au kuongeza ukubwa wa mafla. (exhaust), vitendo ambavyo ni kosa kisheria.

Aidha operesheni hii rasmi imekuja baadaya kutokea kwa matukio kadhaa ya ajali ambazo zimepelekea wananchi wengi kupoteza maisha na wengine kupata ulemavu wa kudumu, jeshi la polisi mkoa wa Mwanza kupitia kikosi cha usalama barabarani baada ya kuliona hilo lilianza kutoa elimu kupitia vyombo vya habari, kufanya vikao na vikundi vya waendesha bodaboda pamoja na kutoa elimu ya usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.

Jeshi la Polisi baada ya kubaini  hilo liliandaa gari maalumu la matangazo ambalo lilipita maeneo yote ya jiji la mwanza kwa muda wa siku tatu likiwataadharisha waendeshaji wa vyombo vya moto juu kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani, lakini pia juu ya kufanyika kwa operesheni ya kukamata madereva/ abiria wa vyombo vya moto ambavyo vitakuwa vimekiuka sheria ya usalama barabarani.

Operesheni tayari imeanza kufanyika katika maeneo yote ya jiji la Mwanza, tayari askari wamefanikiwa kukamata pikipiki 217 na bajaji 27, ambazo zilikutwa na makosa mbalimbali ya usalama barabarani. 

Aidha abiria 31 wa pikipiki wamekamtwa kwa kushindwa kuvaa kofia ngumu pindi walipokuwa wanaendeshwa barabarani, aidha taratibu za kuwafikisha mahakamani madereva na abiria ambao walipatikana na makosa ya usalama barabarani zinaendelea.

Rais Magufuli akubali ombi la kujiuzulu Bw. Gabriel Mnyele aliyekuwa DC Uyui


MAJALIWA AHUTUBIA MKUTANO WA HADHARA MJINI NJOMBE PIA ATEMBELEA MAJENGO YA POLISI YANAYOJENGWA LUDEWA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka kesho awapeleke wakaguzi wa heshabu kwenda kukagua mapato na matumizi ya  Mamlaka ya Maji ya Mji wa Njombe (NJUWASA).

Ametoa agizo hilo leo (Ijumaa, Januari 27, 2017) wakati akizungumza na wananchi katika mkutano uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya Sekondari Mpechi, Halmashauri ya Mji wa Njombe.

Waziri Mkuu amesema wakaguzi hao mbali na kukagua mapato na matumizi ya mamlaka hiyo pia waangalie kama wananchi walihusishwa katika ukokotoaji wa gharama za malipo ya bili za maji.

Ametoa agizo hilo baada ya wananchi kuilalamikia mamlaka hiyo kupitia mabango kwamba wanatozwa bili kubwa ya maji licha ya huduma hiyo kupatikana kwa kusuasua katika mji huo.

Kufuatia malalamiko hayo Waziri Mkuu alimtaka Mkurugenzi Mtendaji wa NJUWASA, Bw. Daudi Majani kutoa ufafanuzi juu ya jambo hilo ambapo alisema kwa mwezi wanakusanya sh. milioni 75 zinazotumika kuendeshea na uboreshaji wa huduma.

“Maji hakuna unasema unaboresha unaboresha huduma gani? Wananchi wanalalamika maji hakuna na mnawatoza gharama kubwa, Mkuu wa Mkoa kesho peleka wakaguzi wakakague kwa mwezi anakusanya kiasi gani na anafanyia nini,”

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amewataka watumishi wa umma kujiwekea utaratibu wa kwenda kwa wananchi na kusikiliza changamoto mbalimbali zinazowakabili ili kuzitafutia ufumbuzi badala ya kujifungia maofisini.

“Uwepo wa mabango mengi kwenye mikutano ya hadhara ya viongozi ni ishara tosha kwamba watendaji hamuendi kwa wananchi kuwasikiliza kero zao. Mabango mengi hapa si ya Waziri Mkuu ni hapahapa,” amesema.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, JANUARI 27, 2017.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa mpira wa shule ya sekondari ya Mpechi mjini Njombe Januari 27, 2017.
 Mmoja wa wananchi waliofika kwenye uwanja wa  mpira wa Shule ya Sekondari ya Mpechi mjini Njombe akitoa dukuduku lake kwa njia ya karatasi wakati Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  alipohutubia mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa mpira wa Shule ya Sekondari ya Mpechi, Januari 27, 2017. 
   Wananchi wa Mji wa Njombe wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipohutubia mkutano wa hadhara  kwenye uwanja wa mpira wa Shule ya Sekondari ya Mpechi Januari 27, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia wananchi wa mji wa Njombe wakati alipowasili kwenye uwanja wa  mpira wa Shule ya Sekondari ya Mpechi kuhutubia mkutano wa hadhara Januari 27, 2017.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua nyumba za Askari Polisi ambazo kwa muda mrefu hazijakamilika katika mji wa Ludewa Januari 27, 2017.

SERIKALI KUTUMBUA WAHUJUMU WA TAZARA

$
0
0
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akimsikiliza mmoja wa wataalam wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), akimweleza namna  wanavyosimamia mafuta yanayotumika kwenye treni za Mamlaka hiyo, alipowatembelea jijini Dar es Salaam.
 Meneja wa Karakana ya Dar es Salaaam ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), Eng. Timothy Kayani, akimwonyesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa vipuri vya treni vilivyotengenezwa katika karakana hiyo jijini Dar es Salaam, alipotembelea karakana ya Mamlaka hiyo kuona utendaji wake.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akiangalia behewa la treni lililofanyiwa ukarabati na kukamilika katika karakana ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), alipotembelea karakana hiyo jijini Dar es Salaam.
 Meneja wa Karakana ya Reli Dar es Salaaam ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), Eng. Timothy Kayani, akifafanua namna behewa la treni linavyoanza kufanyiwa ukarabati kwa   Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa (wa kwanza kushoto) katika karakana hiyo, wakati Waziri huyo  alipotembelea kuona utendaji wake. Wa pili kushoto ni Meneja wa TAZARA Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Fuad Abdalla.
 Mtaalam wa mifumo ya Tehama wa Kampuni ya Qmax Bi. Jenirose Jabakila akimweleza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, namnamfumo walioutengeneza wa kufatilia treni inapokuwa njiani unavyofanya kazi, wakati alipotembea Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA).
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akifafanua jambokwa wafanyakazi wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), alipotembelea mamlaka hiyo kuona utendaji kazi.

Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Na Chalila Chibuda

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, 
Profesa  Makame  Mbarawa  amesema Serikali haitamvumilia mtumishi yoyote ambaye ataendelea kuisababishia hasara Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) kwa kuendelea kuihujumu na kusababisha mamlaka kujiendesha kwa hasara.

Profesa Mbarawa ameyasema hayo leo wakati alipotembelea Tazara, kuangalia utendaji ambapo amebaini matumizi mabaya ya fedha zinazotolewa na Serikali na kuahidi kuchukua hatua stahiki.

“Ninafahamu kuna watu 10 hapa ambao wao ni chanzo kikubwa cha matumizi mabaya ya fedha na miongoni mwao wapo Watanzania na Wazambia, nawahakikishia kuwa kila atakayetumia vibaya fedha zinazotolewa na Serikali hatutamvumilia kwenye Serikali hii’, amesema Prof. Mbarawa.

Profesa Mbarawa amesema kumekuwa na idadi kubwa ya watumishi ambao hawana tija na kuagiza menejimenti ifanye uhakiki na kubaini mahitaji halisi ya Watumishi na watakaobainika kuzidi wahamishiwe ofisi ya tazara Mkoa waDar es Salaam.

Aidha Prof. Mbarawa ameuagiza uongozi wa Tazara Makao Makuu kuacha mara moja kutumia mtandao ya kampuni binafsi kutuma taarifa za Ofisi na kuagiza kuanza kutumia mtandao wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) mara moja.

‘Nikirudi tena hapa sitaki kuona mnatumia mitandao wa Kampuni binafsi kutuma taarifa za kiofisi ninawaomba muhakikishe mnatumia  mtandao wa TTCL’ amesisitiza Prof. Mbarawa.

Kwa upande Meneja wa TAZARA Mkoa wa Tanzania, Bw. Fuad Abdalla amemuhakikishia Waziri Prof. Mbarawa kuwa mkoa umejipanga vizuri kuhakikisha changamoto zote zinatatuliwa na Mamlaka inajiendesha kibiashara.

‘Kama mkoa tumekuja na mikakati mizuri ya kutumia mifumo ya Tehama kama njia ya  udhibiti wa mapato, kama ulivyona hivi sasa tunakamilisha mfumo wa Tehama tunaoutumia kufatilia treni kila inapoondoka kwenye Stesheni ya Makao Makuu Dar es Salaam na mfumo huu ukikamilika tutawaashawishi na wenzetu wa Zambia kutumia mfumo huu ili tuweze kudhibiti upotevu wa mapato’ Amesisitiza Bw. Fuad Abdalla.

Bw. Fuad ameongeza kuwa pamoja na mifumo mipya ya Tehama Tazara inaendeleza kwa kasi ukarabati wa mabehewa ya abiria na mizigo ili kuongeza tija na kuiwezesha Mamlaka kupata faida.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JANUARI 28,2017

TRA YATWAA TUZO YA UBUNIFU WA MIRADI KWA SEKTA ZA AFRIKA.

$
0
0
 Meneja Mifumo ya Kielektroniki ya  Forodha kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)  Bw. Tinkasimile Felix (kushoto) akipokea tuzo ya ubunifu wa mfumo wa TANCIS kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Mindi Kasiga. Mfumo huu wa TANCIA umeundwa kwa kuzingatia kanuni za hali ya juu za kiteknolojia kwa lengo la kuongeza ufanisi, uharaka, uwazi na uhakika katika usimamizi wa masuala ya forodha.
…………
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imepata tuzo kutoka Umoja wa Afrika (AU) kutokana na mfumo wa Uondoaji Mizigo Bandarini (TANCIS) ambao unafanya kazi kwa ufanisi na uharaka zaidi pamoja na kudhibiti mia nyaya rushwa.
Tuzo hiyo imetolewa na Umoja wa Nchi za Afrika jijini Addis Ababa Ethiopia,   baada ya kufanyika shindano la Taasisi za Serikali za Umoja wa Nchi hizo kutokana na kuboresha mifumo ya utendaji kazi katika taasisi zao.
Akizungumza kwa niaba ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Mindi Kisiga amesema kuwa TRA na Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii(SSRA) ndiyo taasisi pekee za Serikali zilizoweza kufanya vizuri katika ubunifu katika utendaji wa taasisi hizo.
“Tuzo hizi zinatolewa na nchi za Umoja wa Afrika kwa taasisi za Serikali ambapo hushindanishwa katika masuala ya ubunifu katika utendaji kazi wa taasisi husika,” alisema Bi. Mindi.
Akizungumza kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Alphayo Kidata, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa kodi toka Mamlaka ya Mapato Tanzania Bw. Richard Kayombo alisema TRA imeshinda tuzo hiyo kutokana na ubunifu wa mfumo wa TANCIS ambao umeundwa kwa kuzingatia kanuni za hali ya juu za kiteknolojia kwa lengo la kuongeza ufanisi, uharaka, uwazi na uhakika katika usimamizi wa masuala ya forodha.
Alisema mfumo huu umeunganishwa na mifumo mingine ya TRA ni ya wadau muhimu ambao wanahusika katika uondoshaji wa bidhaa katika udhibiti wa forodha.
“Mfumowa TANCIS humwezesha mwagizaji wa bidhaa kufuatilia hatua iliyofikiwa katika kuondosha bidhaa zake kwa kutumia simu ya kiganjani au kifaa kingine chochote cha kielektroniki hivyo mfumo huu unarahisisha utoaji huduma na kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato,” alisema Bw. Kayombo.
Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano toka Mamlaka ya Udhibiti wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) Bi. Sarah Kibonde alisema kuwa taasisi yake imepokea tuzo hiyo ya ubunifu kwa kupitia mfumo wa kanzi data yaTaifa ya Sekta ya Hifadhi ya Jamii.
Alisema TRA  iliwawezesha kupata taarifa zilizohusu walipaji kodi wa (PAYE) ambazo zilifanikisha uchambuzi wa waajiri wasiochangia Mifuko yaJamii.
TRA na SSRA wameahidi kuendelea na ubunifu zaidi ili kuhakikisha wanaendelea kubaki katika nafasi ya ushindi na kufanya vizuri zaidi katika mashindano yajayo.

Tume ya Mipango kuanza Safari ya kuhamia Dodoma Mwezi Machi

$
0
0

Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri Akiongea na watumisi wa Tume ya Mipango (hawapo pichani) wakati wa mkutano wake na watumishi hao. Kulia ni Naibu Katibu Mtendaji anayesimamia Klasta ya Sekta za Uzalishaji Bw. Maduka Kessy na wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Bw. Abdulrahman Mdimu akifuatiwa Naibu Katibu Mtendaji, Klasta ya Biashara za Kimataifa na Mahusiano ya Uchumi, Bw. Paul Sangawe.


Kaimu Katibu Mtendaji, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri akiongea jambo na Naibu Katibu Mtendaji, Klasta ya Sekta za Uzalishaji Bw. Maduka Kessy wakati wa mkutano na watumishi wa taasisi hiyo.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mipango na Ufuatiliaji, Bw. Omary Abdallah akitoa taarifa fupi ya utekelezaji wa majukumu ya Tume ya Mipango katika kipindi cha nusu mwaka, kuanzia Mwezi Julai hadi Disemba kwa mwaka wa fedha 2016/17.
Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Bw. Abdulrahman Mdimu akiwasilisha mada juu ya maadili kwa watumishi wa umma katika mkutano uliowahusisha wafanyakazi wa Tume ya Mipango.
Mwanasheria wa Tume ya Mipango, Bibi Nyanzala Nkinga akichangia jambo katika mkutano wa wafanyakazi wa Tume ya Mipango.
Watumishi wa Tume ya Mipango wakifuatilia kinachoendelea wakati wa mkutano uliofanyika katika ofisi za taasisi hiyo.


Watumishi wa Tume ya Mipango wakifuatilia kinachoendelea wakati wa mkutano uliofanyika katika ofisi za taasisi hiyo.
Watumishi wa Tume ya Mipango wakifuatilia kinachoendelea wakati wa mkutano uliofanyika katika ofisi za taasisi hiyo.
Watumishi wa Tume ya Mipango wakifuatilia kinachoendelea wakati wa mkutano uliofanyika katika ofisi za taasisi hiyo.
Watumishi wa Tume ya Mipango wakifuatilia kinachoendelea wakati wa mkutano uliofanyika katika ofisi za taasisi hiyo.PICHA ZOTE NA ADILI MHINA, TUME YA MIPANGO

…………………………………………………………………………………………

Na Adili Mhina, DSM.

Katika kuitikia na kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli la Serikali kuhamia Dodoma, Tume ya Mipango inatarajia kuanza kuhamisha watumishi wake kuelekea Makau Makuu ya Nchi ifikapo mwezi Machi Mwaka huu.

Taarifa hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri alipokutana na watumishi wa taasisi hiyo Ijumaa Januari 26, 2017 kwa lengo la kujadiliana mambo mbalimbali yanayohusu taasisi hiyo.

Pamoja na agenda zingine kujadiliwa katika kikao hicho, suala la kuhamia Dodoma lilionekana kuchukua nafasi kubwa miongoni mwa wafanyakazi mara baada ya ratiba ya zoezi hilo kutolewa rasmi ambapo wengi walionesha kufurahishwa na kutendo cha kutimiza ahadi ya Rais kwa wananchi ya kuhamia Dodoma.

Mwanri alieleza kuwa Tume ya mipango itahamisha watumishi wake katika awamu tatu ambapo makundi mawili yanatarajiwa kuhamia Dodoma ndani ya mwaka huu.

“Kundi la kwanza kwa upande wa Tume ya Mipango litaondoka mwezi Machi mwaka huu ambapo pamoja na mambo mengine, watumishi wa kundi hili watakuwa na jukumu la kuandaa mazingira kwa ajili ya kuwapokea watumishi wengine watakaohamia baadae,” alisema Mwanri.

Aliongeza kuwa sehemu ya pili ya watumishi inatarajiwa kwenda Dodoma kuanzia mwezi Septemba mwaka huu ambapo pamoja na watumishi wengine, kundi hilo linajumuisha Mkuu wa Taasisi ambaye ni Katibu Mtendaji akiambatana na Wakuu wa Klasta, Idara pamoja na Vitengo na kundi la mwisho linatarajiwa kuhama kuanzia mwezi Machi, 2018.

Kikao hicho pia kilitoa fursa ya kutolewa kwa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Tume ya Mipango katika kipindi cha nusu mwaka, kuanzia Mwezi Julai hadi Disemba kwa mwaka wa fedha 2016/17.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mipango na Ufuatiliaji, Bw. Omary Abdallah alieleza kuwa katika Kipindi hicho Tume ya Mipango imefanikiwa kutekeleza majukum mbalimbali ikiwemo; kuandaa mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 2017/18 na kuendesha mafunzo kuhusu mwongozo wa usimamizi wa Uwekezaji wa Umma katika ngazi ya Sekretarieti za mikoa na mamlaka za Serikali za mitaa nchini.

Mafanikio mengine ni kuendelea kusambaza Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2016/17 – 2020/21) kwa wadau pamoja na kuendelea kuandaa mikakati minne ya utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa unaendelea (Mkakati wa utekelezaji, Ugharamiaji, Mawasiliano na Ufuatliaji na Tathmini).

Aidha Tume ya Mipango ilifanikiwa kufuatilia utekelezaji wa baadhi ya Miradi ya Maendeleo ya Kitaifa katika mikoa ya Mwanza, Dodoma, Tabora, Mtwara, Lindi, Pwani na Dar es salaam kwa lengo la kutathmini maendeleo ya utekelezaji wa miradi na kuelewa changamoto zinazokabili utekelezaji wa miradi hiyo.
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images