Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

Benki ya KCB yatoa mafunzo kwa ajili ya wanawake wajasiriamali nchini inayoitwa “2jiajiri”.

$
0
0
Benki ya KCB Tanzania yatoa mafunzo kwa ajili ya wanawake wajasiriamali inayoitwa 2JIAJIRI. Programu hii inalenga kumkomboa mwanamke mjasiriamali kutoka katika matatizo yanayosababisha biashara yake ishindwe kuendelea. Programu hii itaongeza ajira nchini kwa wanawake na hivyo biashara zao zitapanuka na kuwa na uwezo wa kuajiri wengine. 

Mafunzo haya yataendeshwa na wataalamu kutoka Tanzania Entrepreneurship and Competitiveness Center -TECC waliobobea katika masuala ya kijasiriamali, kifedha na ushindani wa biashara

“Mpango huu ni endelevu na tumepanga kufundisha wajasiriamali 315 nchi nzima. Leo tunafundisha wajasiriamali 100 katika makundi mawili tofauti. Mafunzo haya ni bure kabisa, KCB Bank itagharimia gharama zote. Tunachokihitaji kutoka kwao ni mahudhurio ya siku zote tatu na usikivu wa hali ya juu.” Alisema Godfrey Ndalahwa, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya KCB.

Bw. Ndalahwa aliendelea kwa kusema kuwa mafunzo hayo yatafanyika mikoa yote ambako benki ya KCB ina matawi, Dar Es salaam, Mwanza, Morogoro, Arusha, Moshi na pia Zanzibar. Na tunalenga wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati ambao tayari wanaendesha biashara lakini wanataka kuziimarisha zaidi. 

Lengo ni kuwawezesha kudhibiti vipengele vya uzalishaji na mgawanyo wa mapato na faida {control over factors of production and distribution of income and benefits) lakini zaidi ni kuwawezesha kuyatawala maisha yao kiuchumi na kijamii. 

“Matatizo tunayotarajia kutatua kutoka kwa wanawake wajasiriamali ni elimu ya kifedha, kufikia huduma za kifedha, Ukosefu wa dhamana, kutokujua vizuri masuala ya kisheria, uelewa finyu wa sera za serikali na kiuchumi, njia hafifu za kuendesha biashara endelevu, ukosefu wa mtaji na utaalamu wa kuanzisha biashara kubwa” alisema.

Mkurugenzi aliongeza kwamba baada ya mafunzo hayo benki itawapatia wanawake wajasiriamali hao maafisa watatu watakaotembelea bishara zao na hii ni kwa wale tu ambao watahudhuria mafunzo ya siku tatu yote na kuonyesha nia ya kubadilika/kuendelea kibiashara). Maafisa hao watakua ni afisa fedha, afisa sheria na afisa masoko.

Alimaliza kwa kuwaambia wanawake wajasiriamali “JIULIZE KWANINI uhangaike wakati benki ya KCB tupo!”
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya KCB Tanzania Godfrey Ndalahwa akizungumza na baadhi ya wanawake waliohudhuria mafunzo ya ujasiriamali yaliyotolewa na benki hyo mkoani Dar es salaam. 
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya KCB Tanzania Godfrey Ndalahwa, akiongea na wanawake wajasiriamali waliohudhuria mafunzo ya ujasiriamali yaliyotolewa na benki hyo mkoani Dar es salaam. 
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya KCB Tanzania Godfrey Ndalahwa, akiongea na wanawake wajasiriamali waliohudhuria mafunzo ya ujasiriamali yaliyotolewa na benki hyo mkoani Dar es salaam.


Baadhi ya wanawake wajasiriamali waliohudhuria mafunzo ya ujasiriamali yalitolewa na Benki ya KCB mkoani Dar es salaam.

KAMANDA WA POLISI KILIMANJARO,SACP MUTAFUNGWA AKAGUA UJENZI WA KITUO CHA POLISI URU

$
0
0
 Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,SACP,Wilbroad Mutafungwa (kushoto mwenye fimbo) akizungumza jambo wakati akikagua maenedeleo ya ujenzi wa kituo cha Polisi cha Kimanganoni Uru wilaya ya Moshi. 
Kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro akikagua ujenzi wa kituo cha polisi kinachojengwa kwa nguvu za wananchi eneo la Uru Kimanganoni kati. Kushoto ni askari mstaafu,mkazi eneo hilo Philipo mushi akimpokea Mutafungwa .Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini.

RAIS DKT. MAGUFULI AWASALIMIA WAKAZI WA KISESA, MAGU, NA BUSEGA MKOANI SIMIYU

$
0
0
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa Nyamikoma Wilayani Busega wakati akiwa njiani kuelekea mkoani Simiyu kwa ajili ya ufunguzi wa barabara ya Bariadi-Lamadi.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa Kisesa mkoani Mwanza wakati akiwa njiani kuelekea mkoani Simiyu kwa ajili ya ufunguzi wa barabara ya Bariadi-Lamadi.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa Magu mkoani Mwanza wakati akiwa njiani kuelekea mkoani Simiyu kwa ajili ya ufunguzi wa barabara ya Bariadi-Lamadi.
. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe magufuli mara baada ya kushuka kwenye kivuko cha Mv Misungwi wakati akitokea Chato mkoani Geita. PICHA NA IKULU

UTEUZI WA MKURUGENZI WA MAENDELEO YA MICHEZO

$
0
0

Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw.Yusuph Singo Omari

TEA Yatoa Milioni 496 Kujenga Uzio wa Hosteli Mpya za UDSM.

$
0
0
 Na  Lilian Lundo - MAELEZO

Mamlaka ya Elimu Tanzania Tanzania (TEA) imetiliana saini na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mkataba wa ujenzi wa uzio katika hosteli za Mwalimu J.K. Nyerere Kampasi ya Mlimani.

Mradi huo umedhaminiwa na TEA kupitia Mfuko wa Elimu (Education Fund) utakaogharimu jumla ya shilingi 496,646,868 hadi kukamika kwa ujenzi huo.

Mkataba huo umesainiwa leo  Jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo Graceana Shirima na Makamu Mkuu wa Chuo cha UDSM Profesa Rwekaza Mukandala wakati wa mkutano na waandishi wa habari.

Alisema kuwa utekelezaji mradi huo unatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi 12 ijayo.Kwa upande wake Prof. Mukandala aliwashukuru TEA kwa msaada huo na kuongeza kuwa ujenzi wa uzio hizo ni suluhisho kubwa kwa wanafunzi watakaoishi katika eneo la kampasi hiyo.

Alisema kuwa uzio utasaidia kuimarisha usalama wa wanachuo na mali zao kutokana na kuwepo eneo ambalo lina mzunguko mkubwa wa watu unaotokana na stendi ya mabasi ya simu 2000 , maduka ya Mlimani City pamoja na viwanja hivyo kutumika kama njia ya mkato na vijiwe kwa watu wasio na kazi.

TEA tayari imefadhili miradi mbalimbali Chuo Kikuu cha UDSM ikiwemio ujenzi wa vyumba vya mihadhara, ununuzu wa vitabu vya kiada, vifaa kwa ajili ya wanafunzi kwenye mahitaji maalum, ufadhili wa kozi za "Pre Entry" kwa wanafunzi wa like katika masomo ya sayansi, ununuzi wa mitambo na vifaa vya Tehama

NAIBU WAZIRI JAFO AHAIDI KULIVALIA NJUGA SUALA LA WANANCHI WA MAFIA KUKOSA HUDUMA YA X-RAY

$
0
0
NA VICTOR MASANGU, MAFIA  

WAKATI serikali ya awamu ya tano ikiwa ni mpango wa kuhakiisha inajenga zahanati katika kila kijiji katika nchi nzima wananchi katika baadhi ya maeneo mengine wanakabiliwa na  changamoto mbali mbali ikiwemo ukosefu wa vifaa tiba, madawa, wauguzi, madaktari  pamoja na huduma ya upatikanaji wa mashine ya X-Ray  hali inayopelekea  wagonjwa kushindwa kupatiwa matibabu kwa wakati unaotakiwa.

Changamoto hizo zimebainika baada ya Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa(TAMISEMI) Seleman Jafo wakati wa ziara yake ya kikazi  katika Wilaya ya Mafia iliyopo Mkoani Pwani  kwa ajili ya kuweza kukagua shughuli mbali mbali za miradi ya  kimaendeleo ikiwa pamoja na   kuweza kubaini changamoto  na matatizo yanayokakabili wananchi.

Naibu Waziri Jafo mara baada ya kuhitimisha ziara yake ya siku moja ameweza kuzungumza na watumishi na kusema kwamba amesikitishwa sana na hali  inayowakabili wananchi wa Mafia hususan katika sekta ya afya kwani kwa sasa  wapo katika wakati mgumu kutoka na na kukosa huduma ya mashine ya X-Ray kwa kipindi cha miezi sita sasa hivyo kuwalazimu baadhi ya wagonjwa kwenda kupatiwa matibabu Jijini Dar es Salaam kwa kutumia usafiri wa boti au ndege.

“Kwa kweli mimi kama kiongozi wenu hili jambo la wananchi wa Wilaya ya Mafia kutokuwa na huduma ya X-Ray sio sahii kabisa hata kidogo yani wataalamu ndani ya miezi mitatu mmeshindwa kulitafutia ufumbuzi wakati wananchi wanaendelea kupata tabu na ukizingatia mtu akiumwa wakati yupo huku mafia inakuwa ni vigumu sana kumsafirisha kwenda Dar es Salaam kutibiwa, na ukizingatia gharama yenyewe ni kubwa”alisema Jafo kwa masikitiko.
Jafo alisema kwamba kutokana na kuwepo kwa changamoto hiyo ya ukosefu wa  huduma ya X-ray aliahidi kulishughulikia kwa hali na mali ili  kuweza kuwasaidia wananchi wa Mafia waweze kupatiwa matibabu yanayostaili na sio kupata tabu wakati serikali yao ipo kwa ajili ya kuweza kuzitatua changamoto walizonazo.

Kwa upande wake  Mganga mkuu wa Wilaya ya Mafia Joseph Mzimbe amekiri kuwepo kwa tatizo hilo la kutokuwa kwa huduma ya X-Ray na kudai kwa sasa wagonjwa wengine pindi wanapohitaji huduma hiyo wanashindwa kufanyiwa vipimo kutoka na gharama ya usafiri kutoka Mafia hadi kupelekwa katika hospitali zilizopo  Dar es Salaam ni kubwa

Naye mmoja wa wananchi aliyejitambulisha kwa jina la Hamisi Mshilazi  akizungumza kwa niaba ya wenzake,amesema kuwa mashine hiyo ya X-ray  kwa upande ni tatizo sugu kutokana na kuharibika mara kwa mara hivyo kuzolotesha utoaji wa huduma kwa wagonjwa na kubainisha gharama ya usafiri  wa boti na ndege ni kubwa hivyo wanajikuta  baadhi yao wenye kipato cha chini wanashindwa  kwenda  kupelekwa kwa ajili ya kupatiwa matibabu zaidi katika hospitali ya Taifa ya  Muhimbili.

Riziki Mngwari  yeye ni Mbunge wa viti maalumu ambaye anaiwakilisha Wilaya ya Mafia Mkoa wa Pwani kupitia  (CUF) ambaye alikuwepo katika ziara hiyo hakusita kutoka kilio chake kwa serikali ya awamu ya tano katika kuwaboreshea huduma ya afya  wananchi eneo hilo kwani wanateseka sana katika kupatiwa matibabu yanayostahili.

WANANCHI wa Wilayani ya Mafia Mkoa  Pwani  kwa sasa hawana  huduma yoyote ya mashine ya X-ray hivyo kuwalazimu baadhi ya wagonjwa kutumia gharama kubwa kwa ajili ya kwenda kupatiwa matibabu zaidi katika hopsitali zilizipo Jijini Dar es Salaam kwa kutumia usafiri wa ndege au kwa boti ambayo kutokana na gharama yake kuwa ni kubwa wanashindwa kuimudu hivyo kunahitajika juhudi za makusudi kutoka serikalini ili kuweza kuboresha sekta ya afya.
 Naibu Waziri ofisi ya Rais Tamisemi Seleman Jafo akiwasili katika uwanja wa ndege wa Mafia Mkoani Pwani kwa ajii ya ziara yake ya kikazi kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo na kuweza kubaini changamoto za wananchi zinazowakabili.
  Naibu Waziri Ofisi ya Rais Seleman Jafo akisaliamina na baadhi ya viongozi na watumishi wa halmashauri ya Wilaya ya Mafia Mkoani Pwani mara baada ya kuwasali kwa ajili ya kuendelea na ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo
Naibu Waziri akizungumza na baadhi ya watumishi wa halmashauri ya Wilaya ya Mafia wakiwemo walimu wa sekondari  hawapo pichani wakati wa ziara yake ya kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo Wilayani humo,(PICHA NA VICTOR MASANGU)

TANZIA

VODACOM TANZANIA FOUNDATION YAWAKUMBUKA WATOTO WA SHULE MAALUMU MKOANI NJOMBE

$
0
0
 Mtoto mwenye ulemavu wa ngozi wa shule maalumu ya msingi ya Mundindi wilayani Ludewa Mkoani Njombe, Yohana Mwaifuge(katikati) akipokea moja ya msaada toka kwa Meneja wa Vodacom Tanzania wa Mkoa huo, Benedict Kitogwa aliyekabidhi msaada huo jana  kwa niaba ya Vodacom Tanzania Foundation.Msaada huo wenye thamani ya shilingi Milioni 15/- ni Vyakula,Sabuni, Magodoro pamoja na mablanketi.
 Meneja wa Vodacom Tanzania Mkoa wa Njombe, Benedict Kitogwa(kushoto) akimsalimia mtoto mwenye ulemavu wa macho wa shule maalumu ya Mundindi wilayani Ludewa Mkoani humo, Robert Lwaizala wakati alipotembelea shule hiyo jana  kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali wenye thamani ya shilingi Milioni 15/- kwa niaba ya Vodacom Tanzania Foundation.
Baadhi ya watoto wanaosoma katika  shule maalumu ya Mundindi wilayani Ludewa Mkoani Njombe, wakila chakula cha mchana na Meneja wa Vodacom Tanzania wa mkoa huo, Benedict Kitogwa(katikati)baada ya kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali jana kwa niaba ya Vodacom Tanzania Foundation wenye thamani ya shilingi Milioni 15/- kama vile Vyakula, Sabuni, Magodoro pamoja na mablanketi.


SERIKALI KUFANYA MAPITIO YA SHERIA YA SEKTA YA SANAA NA BURUDANI –WAZIRI NAPE

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

WAZIRI wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye amesema wanatarajia kufanya mapitio ya sheria zinazohusu sekta ya sanaa na burudani nchini ili kutoa fursa kwa taasisi binafsi kuwekeza zaidi.

Katika kufanya mapitio hayo wataangalia jinsi ya kufanyia kazi sheria mbovu zinazokandamiza sekta ya sanaa na burudani nchini na kuziondoa kabisa ili kuleta manufaa kwa wasanii na wadau wanaohusika na sanaa.

Nape ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam alipokuwa akizindua rasmi urushwaji wa matangazo ya Kombe la mataifa Afrika (AFCON) pamoja na kumkabidhi bendera kwa msanii wa Bongofleva Nasib Abdul(Diamond Platnum) anayekwenda kutumbuiza katika ufunguzi wa mashindano hayo yatakayofanyika Januari 14 nchini Gabon.

Amesema wasanii na watu wengine kwenye sanaa wamekuwa wakifanya kazi kwa juhudi kubwa licha ya kutofaidika na kazi wanazozifanya na hatimaye wakijikuta wakiwa chini kadri siku zinavyozidi kwenda mbele.

Amesema serikali imedhamiria kushughulikia masuala yote yanayofanya wasanii na wadau wngine kuwa wanyonge kutokana na uwepo wa sheria hizo.

‘Natambua Kampuni ya Multichoice kupitia king’amuzi chake cha DStv katika kuhakikisha wanakuza na kuendeleza masuala ya michezo na burudani nchini, na sisi kuonesha tunaunga mkono jitihada zao tutapitia sheria zote ambazo zimekuwa ni kikwazo kwenye ukuzaji tasnia ya sanaa hapa nchini’ amesema Nape.

Nape alimpongeza Diamond Platnum kwa kupata nafasi ya kwenda kutumbuiza katika mashindano hayo na kudai kuwa kitendo hicho kinaipa faraja Tanzania licha ya kuwa hawajapeleka timu katika mashindano hayo makubwa barani Afrika.

Nae Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Salum Salum amesema watanzania wataweza kujioneamashindano hayo Mubashara kutoka nchini Gabon kupitia king’amuzi chao cha DStv kwenye kifurushi cha bei ya chini cha Shilingi 19,975 pekee.

Amesema kampuni hiyo itagharamia tiketi za watu sita kutoka kundi la WCB ili kufanikisha adhma ya msanii Diamond Platnum kufanya shoo yenye uwezo wa kuijulisha dunia kuwa Tanzania inavipaji vingi vya uimbaji mziki licha ya kutopewa sifa katika baadhi ya maeneo mengine.

Aidha Salum amesema mashindano yatakuwa yakionyeshwa mubashara(Live) ili kuweza kutoa fursa ya watanania na kujikita zaidi kwenye michezo ili na wao wapate nafasi ya kushiriki mashindano hayo katika kipindi cha miaka ijayo.
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye akizungumza wakati wa hafla ya kumkabidhi bendera kwa msanii wa Bongofleva Nasib Abdul(Diamond Platnum) anayekwenda kutumbuiza katika ufunguzi wa mashindano hayo yatakayofanyika Januari 14 nchini Gabon iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye, akimkabidhi bendera msanii wa Bongofleva Nasib Abdul(Diamond Platnum) anayekwenda kutumbuiza katika ufunguzi wa mashindano yatakayofanyika Januari 14 nchini Gabon iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Salum Salum akizungumza wakati hafla ya kumkabidhi bendera msanii wa Bongofleva Nasib Abdul(Diamond Platnum)anayekwenda kutumbuiza katika ufunguzi wa mashindano yatakayofanyika Januari 14 nchini Gabon iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Msanii wa Bongofleva Nasib Abdul(Diamond Platnum) anayekwenda kutumbuiza katika ufunguzi wa mashindano yatakayofanyika Januari 14 nchini Gabon akizungumza na waandishi habari juu ya safari hiyo leo jijini Dar es Salaam.
Balozi DSTV, Joti akizungumza wakati wa hafla ya kumkabidhi bendera msanii wa Bongofleva Nasib Abdul(Diamond Platnum) anayekwenda kutumbuiza katika ufunguzi wa mashindano yatakayofanyika Januari 14 nchini Gabon iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.

MABULA: SERIKALI YA AWAMU YA TANO IMEDHAMILIA KUMALIZA MIGOGORO YA ARDHI NCHINI

$
0
0
Na Ofisa habari Mufindi.

Naibu Waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi Mh. Angelina Mabula, amesema serikali ya awamu ya tano imedhamilia kwa dhati kupunguza kwa asilimia kubwa kama si kuondosha kabisa kero ya migogoro ya ardhi nchini ili kuondokana malumbano yanayozikabili jamii nyingi hapa nchini.

Mh. Mabula ameyasema hayo mjini Mafinga wakati wa ziara ya kikazi aliyofanya Wilayani Mufindi akiwa na lengo la kukagua masuala mbalimbali yaliyo chini ya wizara yake sanjari na kusikiliza kero za wananchi zinazohusiana na migogoro ya ardhi.

Amesema kwa muda mrefu jamii nyingi hapa nchini zimekuwa katika migogoro ya kugombea ardhi, jambo ambalo linachochea mafarakano miongoni mwa wananchi hivyo serikali ya awamu ya tano imejidhatiti kuhakikisha inapunguza au kuondosha kabisa migogoro iliyopo na akatoa rai kwa wakurugenzi wa halmshauri kuhakikisha wanasimamia vema masuala ya ardhi ili kuzuia kuibuka kwa migogoro mipya.

Aidha, amemtaka Mkurugenzi mtendaji wa Mji wa Mafinga kuhakikisha anarasimisha makazi ya wakazi wa kata ya Kinyanambo iliyopo mjini Mafinga kwa kuhakikisha kuwa makazi yao yanapimwa na wanapatiwa hati ili wamiliki maeneo yao kisheria jambo ambalo litawafanya waishi kwa kujiamini katika maeneo yao lakini pia waweze kuzitumia hati hizo kama dhamana katika taasisi za kifedha.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula akiongea na wananchi katika ukumbi wa CCM mjini Mafinga kabla hajaanza kusikiliza kero zao.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula akikagua mfumo wa kielektroniki wa wamiliki wa ardhi alipotembelea ofisi za ardhi Wilayani Mufindi.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula akiwa ameongozana na Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Jamhuri William mara baada ya kukagua mfumo unaohifadhi takwimu za wamiliki wa ardhi Wilayani Mufindi.

WAKAZI WA MIJINI WAHIMIZWA KUJIKTA KWENYE BUSTANI ZA MAKOPO NA MIFUKO

$
0
0
#LakeFm Habari
Wakazi wanaoishi maeneo ya mijini nchini wamehimizwa kujikita kwenye kilimo cha mbogamboga kwa kutumia masalia ya makopo na mifuko ya aina mbalimbali ili kuondokana na uchafunzi wa mazingira.

Mwanamama Victoria Buzare ambaye ni mjasiriamali kutoka Kata ya Buhongwa Jijini Mwanza, ameyasema hayo wakati akizungumza na Lake Fm huku akiongeza kwamba kilimo hicho pia kinawaepusha wanajamii na athari za kutumia mbogamboga zenye kemikali.

Amesema kilimo hicho kinagharimu mtaji kidogo hadi shilingi 5,000 ambazo mkulima anaweza kulima aina tatu za mbogamboga ikiwemo sukumawiki, nyanya chungu, biringanya na nyinginezo.

Buzare amewashauri wanafamilia wote wanaoishi mijini kuhakikisha wanakuwa na bustani za makopo na mifuko kwani ni salama kwa matumizi ya chakula na pia rahisi kusimamia ikizingatiwa ndoo moja ya maji kwa siku inatosheleza mahitaji yake.
Kwa maoni na ushauri ama swali, wasiliana na Victoria Buzare (pichani) kwa nambari za simu 0754 21 85 55.

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI KATIKA MRADI WA UJENZI WA NYUMBA 252 ZA MAKAZI MBWENI ZANZIBAR

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa nyumba 252 za makazi zinazojengwa na Shirika la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) zilizopo Mbweni, Zanzibar ikiwa moja ya maadhimisho ya miaka 53 ya Mapinduzi. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia mara tu alipoweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa nyumba 252 za makazi zinazojengwa na Shirika la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) zilizopo Mbweni, Zanzibar ikiwa moja ya maadhimisho ya miaka 53 ya Mapinduzi.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa ndani ya moja ya nyumba hizo 252 mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa nyumba hizo za Shirika la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) zilizopo Mbweni, Zanzibar ikiwa moja ya maadhimisho ya miaka 53 ya Mapinduzi.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia ramani ya ujenzi wa nyumba 252 za makazi zinazojengwa na Shirika la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) zilizopo Mbweni, Zanzibar ikiwa moja ya maadhimisho ya miaka 53 ya Mapinduzi.



Pichani ni Nyumba za makazi zinazojengwa na Shirika la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) zitakazokuwa na nyumba 252, Viwanja vya Michezo kwa Watoto,Sehemu ya kuogelea na Ukumbi mkubwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasalimia wananchi waliojitokeza wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa nyumba 252 za makazi zinazojengwa na Shirika la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) zilizopo Mbweni, Zanzibar ikiwa moja ya maadhimisho ya miaka 53 ya Mapinduzi.
Sehemu ya Wananchi wakimsikiliza Makamu wa Rais Mhe. Samia Hassan Suluhu
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akfurahia jambo na wanafunzi waliojitokeza kushuhudia uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa nyumba 252 za makazi zinazojengwa na Shirika la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) zilizopo Mbweni, Zanzibar ikiwa moja ya maadhimisho ya miaka 53 ya Mapinduzi.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimwa Samia Suluhu Hassan ameuagiza uongozi Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) uchangamkie fursa za uwekezaji wa ujenzi wa nyumba za makazi Tanzania Bara hasa kwenye Makao Makuu ya nchi Dodoma hatua ambayo itauwezesha mfuko huo kuongeza maradufu mtaji wake kwa uuzaji wa nyumba hizo.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo wakati anaweka jiwe la msingi katika mradi mkubwa wa ujenzi wa nyumba 252 za makazi katika eneo la MBWENI kisiwani Unguja ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Makamu wa Rais amesema kutokana na kazi kubwa na nzuri inayofanywa na mfuko huo wa ZSSF hasa ujenzi wa nyumba za makazi ya wananchi ni muhimu kwa mfuko huo kuangalia namna bora ya kwenda kuwekeza katika mikoa mbalimbali ya Tanzania bara kutokana maeneo mengi kuwa na mahitaji makubwa ya nyumba za makazi.

Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amesema ujenzi wa nyumba za makazi Tanzania Zanzibar ulitokana na fikra na ahadi za hayati mzee Karume kupitia ASP wakati wa haraka za kudai uhuru za kuhakikisha wananchi wanapata makazi bora ya kuishi katika kisiwa cha Pemba na Unguja kutokana na idadi kubwa ya wananchi katika kipindi hicho kuishi katika mazingira yasiyoridhisha.

“Miradi yote hii ni katika kuenzi utekelezaji wa kauli ya Mapinduzi Daima yanayotaka kuleta maendeleo yanayoonekana kwa wananchi kila uchao hususani kipindi hiki tunapotimiza miaka 53 ya Mapinduzi yetu ya Matukufu ya Zanzibar”

Makamu wa Rais pia amewahimiza wananchi wote wachangamkie fursa za kununua na kumiliki nyumba kwa bei nafuu na zenye miundombinu ya kisasa na huduma zote za kijamii ikiwemo viwanja vya michezo.

Kuhusu umiliki wa nyumba kwa Watanzania wanaoishi nje ya nchi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameziagiza Wizara zinazoshughulika na masuala ya ardhi Tanzania Bara na Zanzibar kutoa ufafanuzi au tafsiri sahihi ya sheria zinazoongoza masuala ya ardhi na umiliki wa nyumba ili kuondoa sintofahamu iliyopo kuhusu wana diaspora kumiliki nyumba.

Amesisitiza kuwa Serikali zote mbili zimekuwa zikisisitiza wana diaspora kuchangia maendeleo ya nchi na kutumia fursa mbalimbali zilizoko nyumbani ikiwemo kununua nyumba zinazojengwa na mifuko na mashirika mbalimbali hivyo ni muhimu kwa wizara zinazoshughulikia masuala ya ardhi kutoa maelekezo haraka ili kuondoa sintofahamu iliyopo kwa sasa kuhusu wana diaspora kulimiki nyumba kwa ajili ya makazi.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amesema ni muda muafaka sasa hivi kwa mifuko hiyo kuwekeza katika sekta ya viwanda hasa kwenye miradi yenye tija kwani viwanda vitatoa fursa kwa vijana wengi kuajiriwa na kuongeza kipato na kuongeza huduma za kijamii na kupunguza umaskini kwa wananchi.

Kwa upande wake, Waziri wa Fedha na Mipngo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt Khalid Salum Mohamed amemhakikishia Makamu wa Rais kuwa Serikali hiyo inaendelea kumuezi Mzee Karume kwa vitendo kwa kujenga nyumba za makazi na kukarabati nyumba zilizopo ili kuhakikisha wananchi katika Kisiwa cha Pemba na Unguja wanapata makazi bora ya kuishi.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI


MUFTI AWATAKA WAISLAMU KUOMBA NCHI IPATE MVUA IONDOKANE NA UKAME NA BAA LA NJAA

$
0
0
Na Dotto Mwaibale

WAISLAM nchini wametakiwa kuomba nchi ipate mvua ili kuondokana na ukame na kuepusha baa la njaa.

Mwito huo umetolewa na Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Bin Zubeir Bin Ali wakati ukitolewa kwa niaba yake na Msemaji wa Baraza Kuu la Waislam Tanzania, Sheikh Khamis Said Mataka wakati akizungumza na wanahabari Dar es Salaam leo.

"Taarifa mbalimbali zinaashiria nchi kukabiliwa na ukame kwa kukosa mvua za msimu zilizotarajiwa kutokana na hali hiyo Mufti anawaomba Masheikh, Maimamu na Waislamu wote kwa ujumla kuleta toba,kumuomba msamaha Mwenyezi Mungu ili 

aijaalie nchi yetu na nchi jirani zetu kupata mvua za kheri zitakazotusaidia kutuepushia ukame na madhara yake ikiwemo baa la njaa" alisema Sheikh Mataka.Katika hatua nyingine Mufti wa Tanzania amewateua Mwenyekiti wa Halmshauri Kuu Bakwata Taifa, Sheikh Khamis Said Mataka na Mkurugenzi wa Daa'wa na Tabligh Bakwata Makao Makuu Sheikh Hassan Said Chizenga kuwa wasemaji rasmi wa Baraza

Kuu la Waislamu wa Tanzania (Bakwata) uteuzi ambao umeaanza mara moja.Akizungumzia matumizi ya wadhifa wa Sheikh Mkuu alisema kumekuwa na matumizi yasiyosahihi kwa baadhi ya masheikh wa mikoa na wilaya kujiita masheikh wakuu wa maeneo hayo.

Alisema wadhifa wa Sheikh Mkuu ni Mufti pekee na si vinginevyo na akasisitiza kuwa masheikh wa mikoa na wilaya na mitaa wanakumbushwa kutumia nyadhifa zao kama ilivyoainishwa katika katika ya Bakwata.

Katika mkutano huo aliyekuwa Katibu Mkuu wa Bakwata Sheikh Suleiman Lolila alitumia fursa hiyo kutangaza rasmi kustaafu kutokana na kutumikia nafasi hiyo kwa muda mrefu na kuwa na umri mkubwa.Nafasi hiyo hivi sasa itashikiliwa kwa muda na Ustadhi Salm Ahmed.
Msemaji wa Baraza Kuu la Waislam Tanzania, Sheikh Khamis Said Mataka (katikati), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo kwa niaba ya Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Bin Zubeir Bin Ali, kuhusu waislamu kote nchini kuiombea nchi ipate mvua na iondokane na ukame na baa la njaa. Kulia ni Katibu Mkuu wa Bakwata aliyemaliza muda wake, Suleiman Lolila na kushoto ni Mshauri Mkuu wa Mufti, Sheikh Abubakar Ali.
Mshauri Mkuu wa Mufti, Sheikh Abubakar Ali (katikati), akizungumza katika mkutano huo.
Katibu Mkuu wa Bakwata aliyemaliza muda wake, Suleiman Lolila (kushoto), akitangaza rasmi kustaafu wadhifa huo.
Mkurugenzi wa Daa'wa na Tabligh Bakwata Makao Makuu Sheikh Hassan Said Chizenga (wa pili kushoto), akiongoza dua maalumu katika mkutano huo.
Dua likifanyika.

Enjoy ‘Travel Wednesday’ offers from Jumia Travel

$
0
0

By Jumia Travel Tanzania

Every Wednesdays Jumia Travel (www.travel.jumia.com) presents ‘Dream Deals’ offers to its customers from different hotels in Tanzania which last until Fridays.

These offers enable customers to book their dream hotels at huge discounted prices unlike normal days. The aim for these offers are to make sure everybody enjoys beautiful places across the country at affordable rates.

As we are in the middle of the second week of the New Year 2017, the following luxury hotels have offered their best dream deals as follows:

Mermaids Cove Beach Resort & Spa

This hotel is situated in Uroa, Tanzania just an hour’s drive from the Stone Town facing the attracting view of the Indian ocean. The resort has free WiFi internet, a restaurant, a fully stocked bar, sea foods, board games, table tennis, gym equipments and snooker table. Conference facility, a lounge and a mini supermarket are also available among others.      

Nashera Hotel

Probably this could be a wonderful place to visit during the start of this year. Nashera is a luxury hotel situated in Morogoro region whereby it overlooks the Uluguru mountains. Your perfect stay at this hotel will be complemented by exceptional amenities such as a restaurant that serves several Tanzanian and foreign dishes, a telephone, tea making facilities, a lounge, hair dryers as well as security guards to mention a few.    

New Kwetu Hotel   

New Kwetu Hotel is located in a peaceful area in Kisosora, Tanga region surrounded by beautiful tropical gardens. This place guarantees you with Swahili inspired menus and other intercontinental delicacies, a restaurant that serves both alcohol and soft drinks, laundry, airport on-site shuttle, and parking.

Apart from the above hotels also, Jangwani Sea Breeze Resort, Golden Tulip Hotel, and Skippers Haven situated in Dar es Salaam as well as Paradise Beach Resort and Golden Tulip Zanzibar Boutique Hotel both located in Zanzibar Island; have offered their customers the dream deals starting this Wednesday, 11th January.

For more information on how the Travel Wednesdays’ dream deals work, a customer can visit Jumia Travel (www.travel.jumia.com) to see options available at his/her disposal.  

RAIS DKT. MAGUFULI AWASILI BARIADI MKOANI SIMIYU, AWEKA JIWE LA MSINGI HOSPITALI YA RUFAA YA SIMIYU PIA AFUNGUA BARABARA YA BARIADI-LAMADI (KM 71.8)

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma za asili pamoja na kikundi cha Ngoma za asili Baseki cha Bariadi mkoani Simiyu mara baada ya kuwasili mkoani humo kwa ajili ya ufunguzi wa barabara ya Bariadi-Lamadi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono wakati alipowasili Bariadi kwa ajili ya kuifungua rasmi barabara ya Bariadi-Lamadi yenye urefu wa kilometa 71.8. Wengine katika picha ni Mkuu wa mkoa wa Simiyu Antony Mtaka na Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono wakati alipowasili Bariadi kwa ajili ya kuifungua rasmi barabara ya Bariadi-Lamadi yenye urefu wa kilometa 71.8.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma za asili pamoja na kikundi cha Ngoma za asili Baseki cha Bariadi mkoani Simiyu mara baada ya kuwasili mkoani humo kwa ajili ya ufunguzi wa barabara ya Bariadi-Lamadi.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kabla ya kufungua rasmi barabara hiyo la Bariadi-Lamadi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Antony Mtaka kabla ya kufungua barabara ya Bariadi-Lamadi na kuwahutubia wananchi wa mkoa huo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga makofi pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Antony Mtaka wakati vikundi vya kwaya mbalimbali vilipokuwa vikitumbuza Bariadi mkoani Simiyu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua moja ya nguzo katika ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na viongozi mbalimbali pamoja na madaktari na manesi mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu. PICHA NA IKULU

RAIS DK. SHEIN AFANYA UZINDUZI WA SKULI YA SEKONDARI KWARARA 2

$
0
0
 Chumba cha Kompyuta katika Skuli ya Sekondari ya Kwarara iliyozinduliwa na Rais wa Zanzibar na Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein ambayo imejengwa na  Ushirikiano  wa Serikali ya Mapinduzi na Shirika la Kimataifa la Maendeleo kutoka Korea (KOICA), Ikiwa ni shamra shamra za miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar
  Rais wa Zanzibar na Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kulia)  akifuatana na   Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof.Joyce Lazaro Ndalichako (katikati) na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali (kulia) wakati alipotembea katika madarasa mbali mbali ya  Skuli ya Sekondari ya Kwarara na Kituo cha Elimu ya Habari ,iliyoizindua rasmi leo, iliyojengwa kwa Ushirikiano  wa Serikali ya Mapinduzi na Shirika la Kimataifa la Maendeleo kutoka Korea (KOICA), Ikiwa ni shamra shamra za miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar
 Rais wa Zanzibar na Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipanda mti aina ya muembe baada ya kuizindua Skuli ya Sekondari ya Kwarara na Kituo cha Elimu ya Habari,aliyoizindua rasmi  leo, Ikiwa ni shamra shamra za miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar, ujenzi wa Skuli hiyo umefadhiliwa na Serikali ya Mapinduzi na Ushirikiano  wa Serikali ya Mapinduzi na Shirika la Kimataifa la Maendeleo kutoka Korea (KOICA)
 Rais wa Zanzibar na Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akipokea zawadi kutoka kwa  Balozi wa Korea Kusini Bw.Song Geumyoung wakati wa sherehe za uzinduzi wa Skuli ya Sekondari ya Kwarara na Kituo cha Elimu ya Habari,uliofanyika leo Skulini hapo, Ikiwa ni shamra shamra za miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar, ambapo ujenzi wake umejengwa kwa Ushirikiano  wa Serikali na Shirika la Kimataifa la Maendeleo kutoka Korea (KOICA)
Rais wa Zanzibar na Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitoa Hutuba yake katika sherehe za uzinduzi wa Skuli ya Sekondari ya Kwarara na Kituo cha Elimu ya Habari, aliyoizindua rasmi  leo ,Ikiwa ni shamra shamra za miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar,ujenzi wa Skuli hiyo umejengwa kwa ushirikiano wa  Serikali ya Mapinduzi na Ushirikiano  wa Serikali ya Mapinduzi na Shirika la Kimataifa la Maendeleo kutoka Korea (KOICA). (Picha  na Ikulu)

KAMATI YA BUNGE YA PIC YATEMBELEA EPZA

$
0
0

  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Ukanda wa Uwekezaji (EPZA) Bw.  Lamau Mpolo akizungumza mbele ya Kamati ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) wakati Kamati hiyo ilipotembelea eneo hilo mapema leo.
   Mkurugenzi wa Raslimali Watu wa Kiwanda cha Tanzania Tooku Garments kilichopo eneo la EPZA Bw.  Bakanga Paul akizungumza mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) wakati Kamati hiyo ilipotembelea Kiwanda hicho.
 Mwanasheria  wa Kiwanda cha Tanzania Tooku Garments Bw  Ibrahim Gamba (kushoto) kilichopo eneo la EPZA akimuelezea Mwenyekiti wa Kamati ya ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji wa Umma (PIC) Mhe Albert Obama akimuelezea jinsi uzalishaji wa nguo unavyofanyika Kiwandani hapo wakati Kamati hiyo ilipotembelea Kiwanda hicho.
   Wajumbe wa  Kamati ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji wa Umma (PIC) wakiangalia shughuli za uzalishaji nguo zinafofanyika Kiwandani hapo.
  Msajili wa Hazina (kulia) Dkt Oswald Mashidano pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) Mhe Albert Obama (katikati) wakiangalia jinsi shughuli za ushonaji nguo zinavyofanyika Kiwandani hapo.(Picha na Ofisi ya Bunge).

TTCL YAZINDUA HUDUMA YA 4G ZANZIBAR

$
0
0
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais na Mwenyekiti w Baraza la Mapinduzi Issa Haji Gavu akiwa na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Waziri Waziri Kindamba wakinyanyua mabango ya matangazo kuashiria kuzinduliwa kwa  huduma ya 4G  ya Kmpuni hiyo  Zanzibar (kushoto)  Mkuu wa Kanda ya Zanzibar Franscis Mabula.
 Afisa wa kutengeneza bidhaa wa TTCL Rashid Maggid  akimueleza Waziri Gavu namna ya huduma ya 4G inavyofanyakazi kwa urahisi na kwa haraka wakati wa sherehe za uzinduzi wa huduma hiyo iliyofanyika makao Makuu  ya TTCL Zanzibar, Kijangwani.
 Waandishi wa Habari wakifanya mahojiano na Waziri Gavu na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL (hawapo pichani) baada ya uzinduzi wa huduma ya 4G Zanzibar.
 Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Waziri Waziri Kindamba akijibu maswali ya waandishi wa Habari wakati wa uzinduzi wa huduma ya 4G uliofanyika Ofisi Kuu Kijangwani.
Picha ya pamoja ya wafanyakazi wa TTCL na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa Haji Gavu baada ya uzinduzi wa huduma ya 4G Zanzibar.
Picha na Makame Mshenga.

Na Khadija Khamis, MAELEZO Zanzibar.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na  Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,  Issa Haji Ussi Gavu amewataka wananchi kujiunga na huduma ya mawasiliano ya 4G LTE Zanzibar ambayo inauwezo mkubwa wa mawasiliano ya haraka .
Akizundua huduma  za 4G LTE  katika ofisi za Kampuni ya simu Tanzania (TTCL) , Waziri Gavu alisema kwamba ukuaji wa teknolojia unawalazimu watumiaji wa simu za mkononi kuwa na mawasiliano ya uhakika.
Waziri Gavu alisema kwamba huduma hiyo itawarahisishia wananchi wa Zanzibar  mawasiliano katika kazi zao za kilimo, biashara ufugaji pamoja na  wafanyakazi wa serikalini  na sekta binafsi .

“Teknolojia inaendelea kukua na kuja na ugunduzi mpya, nakuombeni wananchi wenzangu tutumie teknolojia hizi katika kuharakisha maendeleo yetu maana huduma za mawasiliano ni sehemu muhimu katika kuchapuza maendeleo” Alisema Waziri Gavu.

Alisema anaimani kuwa kuanza kutumia teknolojia hizo za 4G LTE kutawezesha sasa kuwaunganisha wananchi katika maeneo mbalimbali kimawasiliano ikiwa pamoja na kutumia huduma hizo katika kukuza biashara ya mtu mmoja mmoja au kikundi.

Waziri Gavu  alisema kwamba Aidha  sekta za serikali na binafsi zitaimarishwa kwa kupata huduma nzuri kutokana na mawasiliano ya  4G ambayo yamejipanga kwa mwaka mmoja tu kuenea kwa Tanzania nzima.
Nae Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu  wa TTCL, Waziri Kindamba  alisema  huduma ya mawasiliano ya 4G  ina gharama nafuu  kwa wateja wake,lakini pia mawasiliano yake ni ya uhakika zaidi.

“Mheshimiwa Waziri gharama za 4G ni shilingi  moja kwa sekunde kwa mtumiaji, kiwango cha tozo hiki ni nafuu sana   kulinganisha na kampuni nyengine  hapa nchini.”Alieleza.

Kaimu  Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL alisema kwamba kuzinduliwa kwa huduma hizo wakati huu wa kilele cha maadhimisho ya miaka 53 ya Mapinduzi Zanzibar ni kielelezo tosha cha namna TTCL inavyoenzi kwa vitendo Mapinduzi matukufu ya Zanzibar ambayo yaliwakomboa wananchi wa Visiwa hivi katika ukoloni mkongwe wa Kisultan.

 “katika kuadhimisha miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar na kuweza  kuungana na wenzetu kwa pamoja  kitu kizuri cha kuwapa kama ni zawadi  ni 4G ni mawasiliano yaliobora na  ya  kisasa “alisema Kindamba .
Aidha alisema huduma hizo ni kiungo muhimu katika kustawisha maendeleo ya jamii kupitia katika Nyanja zote ikiwemo kiuchumi kisiasa na  kijamii.

“Mheshimiwa mgeni rasmi, kauli mbiu yetu ya kutambulisha huduma za 4G LTE Zanzibar ni “Chei chei Zanzibar tumefanikisha” alisema Kindamba.
Aliwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi katika kujiunga na huduma za 4G LTE ikiwa ni kampuni ya kizalendo ya hapa Tanzania.

Alisema kuwa lengo kuu la kampuni hiyo ni kuifanya kampuni  kuwa namba moja kwa Tanzania  ambayo itatoa huduma ya simu ya mezani na mkononi  na kurudi katika ubora wake wa awali   na pia ni mdau wa TEHAMA.

TEA Yatoa Milioni 496 Kujenga Uzio wa Hosteli Mpya za UDSM.

$
0
0
Makamu Mkuu wa Chuo cha UDSM Prof. Rwekaza Mukandala na Kaimu Mkurugenzi Mkuu TEA Graceana Shirima wakisaini mkataba huo.
Makamu Mkuu wa Chuo cha UDSM Prof. Rwekaza Mukandala na Kaimu Mkurugenzi Mkuu TEA Graceana Shirima wakibadilishana mkataba huo mara baada ya kuusaini. Kulia ni Kaimu Meneja Miradi ya Elimu TEA, Anne Mlimuka.



Meneja Habari, Elimu na Mawasiliano wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Sylivia Lupembe akitoa utambulisho wa viongozi kutoka TEA na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kabla ya kusaini mkataba wa ujenzi wa uzio wa hosteli mpya za Mwalimu J. K. Nyerere Kampasi ya Mlimani unaodhaminiwa na TEA ambao utakaogharimu shilingi Mil. 496. Kutoka kushoto ni Kaimu Mwanasheria wa UDSM Dkt. Saudin Mwakaje, Makamu Mkuu wa Chuo cha UDSM Prof. Rwekaza Mukandala, Kaimu Mkurugenzi Mkuu TEA Graceana Shirima na Kaimu Meneja Miradi ya Elimu TEA Anne Mlimuka.


Uongozi wa TEA na UDSM wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kusaini mkataba wa ujenzi wa uzio wa hosteli za Mwalimu J. K. Nyerere zinazojengwa kandokando ya barabara ya Sam Nujoma, Jijini Dar es Salaam.

……………………………………………………………………..

Na Lilian Lundo – MAELEZO

Mamlaka ya Elimu Tanzania Tanzania (TEA) imetiliana saini na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mkataba wa ujenzi wa uzio katika hosteli za Mwalimu J.K. Nyerere Kampasi ya Mlimani.

Mradi huo umedhaminiwa na TEA kupitia Mfuko wa Elimu (Education Fund) utakaogharimu jumla ya shilingi 496,646,868 hadi kukamika kwa ujenzi huo.

Mkataba huo umesainiwa leo Jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo Graceana Shirima na Makamu Mkuu wa Chuo cha UDSM Profesa Rwekaza Mukandala wakati wa mkutano na waandishi wa habari.

Alisema kuwa utekelezaji mradi huo unatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi 12 ijayo.

Kwa upande wake Prof. Mukandala aliwashukuru TEA kwa msaada huo na kuongeza kuwa ujenzi wa uzio hizo ni suluhisho kubwa kwa wanafunzi watakaoishi katika eneo la kampasi hiyo.

Alisema kuwa uzio utasaidia kuimarisha usalama wa wanachuo na mali zao kutokana na kuwepo eneo ambalo lina mzunguko mkubwa wa watu unaotokana na stendi ya mabasi ya simu 2000 , maduka ya Mlimani City pamoja na viwanja hivyo kutumika kama njia ya mkato na vijiwe kwa watu wasio na kazi.

TEA tayari imefadhili miradi mbalimbali Chuo Kikuu cha UDSM ikiwemio ujenzi wa vyumba vya mihadhara, ununuzu wa vitabu vya kiada, vifaa kwa ajili ya wanafunzi kwenye mahitaji maalum, ufadhili wa kozi za “Pre Entry” kwa wanafunzi wa like katika masomo ya sayansi, ununuzi wa mitambo na vifaa vya Tehama.

MAJALIWA AZINDUA BARABARA YA MWANAKWEREKWE HADI FUONI- ZANZIBAR

$
0
0
   Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua barabara ya Mwanakwerekwe hadi Fuoni yenye urefu wa kilomita 4.1 iliyopo Zanzibar Januari 11, 2017.  Kushoto ni  Waziri wa  Ujenzi,  Mawasiliano na  Usafirishaji, Ali Karume . (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifurahia baada ya kuzindua barabara yenye urefu wa kilomita 4.1  ya kutoka Mwanakwerekwe hadi Fuoni Zanzibar ikiwa ni moja ya shughuli za sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar, Januari 11, 2017.  Katikati ni Waziri wa Nchi Afisi ya Makamu wa Pili wa rais wa Zanzibar, Mohammed Abood na Kulia ni  Mkuu wa mkoa waMjini Magharibi, Mohammed Mahmoud. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim  Majaliwa akiwapungia wananchi wa Zanzibar wakati alipowasili kwenye eneo la  Barabara ya Mwanankwerekwe  hadi Fuoni kufungua barabara hiyo yenye urefu wa Kilomita 4.1 Januari 11, 2017. Kushoto ni Waziri wa Ujenzi, , Mawasiliano na Usafirishaji, Ali Karume. (Picha na  Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Baadhi ya wananchi wa Zanzibar wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza baada ya kuzindua barabara ya Mwanakwerekwe hadi Fuoni yenye urefu wa Kilomita 4.1 ilyopo Zanzibar Januari 11, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akishiriki katika dua iliyosomwa baada ya kuzindua barabara ya Mwanakwerekwe hadi Fuoni yenye urefu wa Kilomita 4.1 iliyopo Zanzibar Januari 17, 2017.Wengine pichani kutoka kushoto ni Spika wa Baraza la Wawakilishi,   Zubri Ali Maulid, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Mohammed Mahmoud na kulia ni Waziri wa Ujenzi, Mawsiliano na  Usafirishaji, Ali Karume. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watendaji wa Serikali wahakikishe wanawasimamia vizuri wakandarasi wanaojenga miradi mbalimbali nchini ikiwemo ya barabara ili viwango vyake vifalingane na thamani halisi ya fedha zinazotolewa.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Januari 11, 2017) wakati akizundua mradi wa ujenzi wa barabara ya Kwerekwe/Fuoni yenye urefu wa kilomita 4.01 iliyogharimu sh. bilioni 10.07 zilizotolewa na Mfuko wa Barabara. Ujenzi huo ni utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2015.

Waziri Mkuu amezindua barabara hiyo kwa niaba ya Mheshimiwa Rais Dk. John Magufuli ikiwa ni sehemu ya sherehe za maadhimisho ya miaka 53 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Amesema Serikali inatumia fedha nyingi katika miradi ya ujenzi wa barabara hivyo watendaji wake hawana budi kuhakikisha miradi hiyo inalingana na thamani halisi ya kiwango cha fedha kinachotolewa.

Aidha, Waziri Mkuu amewataka watendaji hao kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kulinda na kuhifadhi miundombinu hiyo na kuwachukulia hatua wote watakaobainika kufanya uharibifu ikiwemo uchomaji wa matairi katikati ya barabara.

Pia amewataka wananchi kutojenga majengo ya kudumu katika hifadhi ya barabara ili kuepusha usumbufu pale Serikali inapotaka kuyatumia maeneo hayo. “Lazima wananchi wazingatie sheria ya hifadhi ya barabara,”

“Serikali imedhamiria kuboresha mawasiliano kwa kujenga barabara zetu kwa kiwango cha lami. Hatatutakubali kuona mtu anaharibu miundombinu hii tunayoijenga kwa gharama kubwa ikiharibiwa. Lazima tuilinde ili iweze kutunufaisha wote,” amesema.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amewataka madereva wote kuhakikisha wanakuwa makini na kufuata sheria za usalama barabarani ikiwemo kusimama kwenye alama za kuvukia watembea kwa miguu na atakayekaidi achukuliwe hatua.

Awali Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Bw. Mustafa Aboud Jumbe alisema barabara hiyo ni sehemu ya awamu ya kwanza ya mradi wa ujenzi wa barabara ya kutoka Kwerekwe hadi Tunguu.

Alisema awamu ya pili ya ujenzi wa mradi huo wa barabara itakuwa na urefu wa kilomita saba na itaanzia Fuoni hadi Tunguu inatarajiwa kuanza katika kipindi cha mwaka ujao wa fedha.

Katika hatua nyingine, Bw. Mustafa alitaja changamoto zinazoikabili barabara hiyo kuwa ni pamoja na upungufu wa mitaro ya maji ya mvua jambo linalosababisha maji kutuama barabarani hivyo kutishia uhai wa barabara hiyo.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATANO, JANUARI 11, 2017
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images