Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

BODI YA UTALII NA ATCL WAINGIA MKATABA WA KUUTANGAZA UTALII WA NDANI

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

BODI ya Utalii nchini (TTB) na Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) limeingia mkataba wa pamoja leo Jijini Dar es salaam ikiwa ni lengo la kukuza soko la Utalii wa ndani na kuongeza pato la taifa nchini.

Akizungumza baada ya makabidhiano ya mkataba huo baina ya mkurugenzi wa TTB DevotAha Mdachi  na Mkurugenzi wa TTB  Laislaus Matindi, Mwenyekiti wa TTB, Jaji Mstaafu Thomas Mihayo amesema kuwa uwepo wa shirika la ndege la ATCL litasaidia katika ukuaji wa sekta ya utalii nchini kwani italeta chachu kwa watalii wa ndani na wa nje kuja kwenda kwa wingi.

Mihayo amesema kuwa TTB iliathirika kwa kiasi kikubwa sana hasa baada ya kutokuwepo kwa shirika la ndege na kutoa pongezi kwa juhudi zilizofanywa na Rais wa awamu ya Tano John Magufuli kwa kuirejesha upya na kuiwezesha kuwa na ndege zake zinazojiendesha zenyewe.

"Kwa juhudi zilizofanywa na Rais John Magufuli za kurejesha uhai kwa kampuni ya ATCL na kupata ndege zake ambazo zitasaidia kwenye kuutangaza utalii kwa watalii wa ndani na nje kwani itasaidia pia kuinua na kukuza pato ;la taifa kwa kuingiza fedha za kugeni,"amesema Mihayo.

Mkataba huo utakaowawezesha TTB kujitangaza Zaidi utawawezesha abiria watakaokuwa wanasafiri kwenda mikoa mbalimbali nchini kupata vipeperushi vilivyozinduliwa leo vinavyoelezea baadhi ya vivutio vya utalii pamoja na kuoneshwa kwa vituo hivyo kupitia TV za kwen ye ndege kuvionyesha.

Mwenyekiti wa Shirika la ndege la ATCL, Mhandisi Emmanuel Korroso amesema kuwa kwa safari za ndani katika mikoa mbalimbali, pia kwa sasa ATCL inataka kuongeza safari za ndege kwenda katika mikoa mingine.
  
Kuongezeka kwa safari hizo, pia kutachangia kwa watalii kutumia ndege za serikali na kusaidia kuinua uchumi wa nchi na utakuwa ni endelevu ili kuimarisha ushirikiano hiuo.
 Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Nchini (TTB) Devotha Mdachi akikabidhiana mkataba  na Mkurugenzi wa ATCL Laislaus Matindi wakishuhudiwa na  Mwenyekiti wa TTB Jaji Mstaafu Thomas Mihayo pamoja na Mwenyekiti wa Shirika la ndege la ATCL, Mhandisi Emmanuel Korroso leo Jijini Dar es salaam. Chini wakiwa wanaweka saini ya makubaliano ya mkataba huo wakishuhidwa na mawakili wa pande zote mbili.
  Mwenyekiti wa TTB Jaji Mstaafu Thomas Mihayo (Kulia)pamoja na Mwenyekiti wa Shirika la ndege la ATCL, Mhandisi Emmanuel Korroso  wakionesha vijarada vya Utalii vilivyozinduliwa leo Jijini Dar es salaam vitakavyokuwa vinapatikana katika ndege za Shirika la ATCL.
 wakurugenzi kutoka shirika la ndege la ATCL na bodi ya Utalii TTB wakiwa wanafuatilia kwa makini mkutano huo.
Picha ya pamoja ya viongozi wa Shirika la Ndege la ATCL na Bodi ya Utalii TTB baada ya kumalizika kwa utiaji saini wa makubaliano ya mkataba wa pande hizo mbili.

NSSF YAENDELEA KUKAMILISHA MRADI WA JENGO LA MZIZIMA TOWERS

$
0
0
Mkurugenzi wa Shirika la Hifadhi ya Jamii NSSF,Prof. Godius Kahyarara akizungumza na Waandishi kuhusiana na mradi wa Jengo la NSSF (Mzizima Tower) .
Baadhi ya Watumishi wa Shirika hilo wakiwa katika picha ya pamoja.

Na Anthony John blog Jamii.
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii limekamilisha mradi wa Jengo refu Afrika Mashariki-Mzizima Tower lililopo barabara ya  Azikiwe na Mkwepu Dar es salaam.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Makao Makuu ya Shirika hilo,Mkurugenzi wa Shirika hilo Prof. Godius Kahyarara  amesema Jengo hilo lipo hatua za mwisho za ukamilishaji wa ujenzi ambalo litakuwa na ghorofa 30 za makazi na 32 za Biashara.

Pia amesema Jengo hilo litakuwa na hoteli ya Nyota 5 na nyumba za makazi kwa ajili ya kuuza na kupangisha,Jengo linatarajiwa kukamilika mwakani 2017.Aidha Shilika hilo limesaini makubaliano na atakayekuwa muendeshaji wa Hoteli hiyo itakayokuwa katika Jengo la Mzizima na kutarajiwa kuanza kazi Mara moja baada ya Hoteli hiyo kufunguliwa.

"Baadhi ya miladi imekamilika na mengine ipo katika hatua za ukamilishwaji,NSSF inafungua rasmii upangishwaji wa litakalo kuwa Jengo refu Afrika Mashariki Mzizima Touwers" hayo amesema Kahyarara.

TIMU YA BEACH SOCCER SASA KUIVAA UGANDA DESEMBA 09

$
0
0
KOCHA  Mkuu wa timu ya Taifa ya mpira wa miguu unaochezwa ufukweni (Beach Soccer), John Mwansasu ameita kikosi cha wachezaji 12 kati ya 13 wanaotarajiwa kuivaa Uganda katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa Desemba 9, 2016 utakaofanyika Dar es Salaam.

Mwansasu ambaye hivi karibuni kikosi chake kilicheza na Ivory Coast katika michezo miwili ya kuwania nafasi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa soka la ufukweni bila mafanikio ni makipa ambao ni Rajab Galla na Khalifa Mgaya.

Mabeki ni Roland Revocatus, Juma Ibrahim, Kashiru Salum na Mohammed Rajab wakati Viungo ni Mwalimu Akida, Ahmada Ali na Samwel John huku washambuliaji wengine wakiwa ni Kassim Kilungo na Talib Ally pamoja na Ally Rabbi ambaye ni Nahodha na Mshambulaji wa timu hiyo.

Kocha John Mwansasu bado anafuatilia viwango vya wachezaji mbalimbali ili kujaza nafasi moja ya kipa kabla ya Desemba mosi, 2016 baada ya Kipa Juma Kaseja kutoa taarifa kuwa atakuwa na udhuru wakati nyota mwingine, Mohammed Banka aliyeripotiwa kuwa safarini nchini Afrika Kusini.
Kikosi cha timu ya mpira wa miguu wa ufukweni (beach soccer)

RAIS DKT MAGUFULI AFANYA ZIARA YA KUSTUKIZA GEREZA LA UKONGA JIJINI DAR ES SALAAM LEO,PIGA MARUFUKU UUZWAJI WA SARE ZA MAJESHI KWA WATU BINAFSI

$
0
0

  Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiweka saini kitabu cha wageni akiwa na  Kamishna Mkuu wa Magereza John Casmir Minja kabla ya kuongea na maafisa na askari wa Jeshi la Magereza alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam leo Novemba 29, 2016
 Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akipewa muhtasarai wa kazi  na Kamishna Mkuu wa Magereza John Casmir Minja kabla ya kuongea na maafisa na askari wa Jeshi la Magereza alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam leo Novemba 29, 2016
 Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akikaribishwa na Kamishna Mkuu wa Magereza John Casmir Minja ili aongee  na maafisa na askari wa Jeshi la Magereza alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam leo Novemba 29, 2016
 Mmoja wa askari wa Kikosi Maalumu cha Magereza wakitoa kero zao mbele ya Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli  alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam leo Novemba 29, 2016
 Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akichukua maelezo kutoka kwa  maafisa na askari wa Jeshi la Magereza alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam leo Novemba 29, 2016
  Baadhi ya maafisa na askari wa Jeshi la Magereza wakimsikiliza Rais Dkt John Pombe Magufuli alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam leo Novemba 29, 2016
  Askari wakiwa na shauku ya kutoa kero zao mbele ya Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli alipoongea  na  maafisa na askari wa Jeshi la Magereza alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam leo Novemba 29, 2016
 Mkuu wa gereza la Ukonga akieleza changamoto za kazi Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli  alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam leo 
Novemba 29, 2016
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiongea na baadhi ya maafisa na askari wa Jeshi la Magereza alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam leo Novemba 29, 2016



  
PICHA NA IKULU

FAHAMU JINSI FEDHA ZA TETEMEKO LA ARDHI MKOANI KAGERA ZILIVYOTUMIKA

$
0
0

Na Mathias Canal

Ndugu zangu kama ambavyo tunakumbuka Tarehe 10/09/2016 majira ya saa 9 na dakika 27 Alasiri maeneo ya Kanda ya ziwa hasa Mkoani Kagera kulitokea tetemeko la ardhi linalokadiriwa kuwa na ukubwa wa 5.9 katika vipimo vya Richter ambapo Kitovu cha tetemeko hilo ni kwenye makutano ya latitudo 10 06’ na longitudo 31055’ eneo ambalo ni kilomita 20 kaskazini mashariki mwa kijiji cha Nsunga na kilomita 42 kaskazini magharibi mwa mji wa Bukoba na Kitovu hicho kilikuwa kilomita 10 chini ya ardhi kwenye eneo hilo.

Tetemeko hilo la ardhi liliacha familia kadhaa zikiwa na huzuni kubwa kwa kuwapoteza ndugu, jamaa na rafiki zao ambapo idadi ya watu waliofariki walikuwa ni 17 huku watu 560 wakipatiwa matibabu kutokana na majeraha waliyoyapata sambamba na kukutikana kwa uharibifu wa makazi na miundombinu ya umma na watu binafsi.

Kwa Mujibu wa Mtendaji Mkuu, Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) alieleza sababu za kutokea kwa Tetemeko hilo la ardhi kuwa ilikuwa ni kutokana na kitovu cha tetemeko hilo kuwa kiko chini sana ya ardhi (Km 10) na kwa kutafasiri umbile la mawimbi ya tetemeko hilo yaliyonakiliwa na vituo vya kupimia matetemeko ya ardhi inaonekana kuwa tetemeko hilo limetokana na misuguano ya mapange makubwa ya ardhi iliyopasuliwa na mipasuko ya ardhi mithili ya mipasuko kwenye bonde la ufa. 

Kwa kuwa eneo lililokumbwa na tetemeko la ardhi liko karibu na mkondo wa magharibi wa bonde la ufa la Afrika Mashariki inakisiwa kuwa mtetemo huo ulisababishwa na kuteleza na kusiguana kwa mapande ya miamba juu ya mipasuko ya ardhi ya bonde hilo la ufa.

Katika siku za karibuni kumekuwepo na taarifa mbalimbali katika mitandao ya kijamii ikiwemo facebook, Twitter, Blogs, Instagram na Makundi mbalimbali ya Watsup jambo ambalo lilinilazimu kufunga safari na kuweka kambi ya takribani siku nne Mkoani Kagera ili kubaini ukweli wa namna fedha zilizopatikana na zilivyotumika ikiwa ni pamoja na mahitaji mengine jinsi yalivyopatikana na namna yalivyoelekezwa.

UKWELI WA MAMBO

Kufuatia tathmini zilizofanyika kupitia wataalamu mbalimbali, makadirio ya awali yalibaini kuwa kiasi cha jumla ya shilingi Bilioni 104.9 zinahitajika katika kukabiliana na kurejesha hali katika Mkoa wa Kagera kufuatia maafa hayo. Ambapo gharama hizi zinajumuisha:

a) Ujenzi wa makazi ya muda kwa waathirika wa nyumba zipatazo 16,667 zilizoharibika katika viwango tofauti, ambapo kiasi cha Shilingi Bilioni 41.7 zitahitajika.

b) Kiasi cha shilingi 1.92 kwa ajili ya kodi ya miezi sita kwa wapangaji waliokuwa wakiishi kwenye nyumba zilizoharibiwa.

c) Ukarabati wa shule za msingi 163 kwa gharama ya shilingi Bilioni 12.7, sekondari 57 kwa gharama ya shilingi Bilioni 45.65, vituo vya afya na zahanati 32 kwa gharama ya shilingi milioni 772 na Majengo ya taasisi nyingine 20 kwa shilingi Bilioni 1.3

MISAADA ILIYOTOLEWA

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu (WAZIRI MKUU NA BUNGE) Ndg Uledi A. Mussa ilibainisha kuwa hadi kufikia Tarehe 13 Novemba, 2016 serikali ilikuwa imepokea misaada ya vifaa, Chakula, Fedha na ahadi mbalimbali zenye thamani ya shilingi Bilioni 15.19 kutoka kwa wadau mbalimbali, washirika wa Maendeleo, Balozi wan chi marafiki ambapo tayari misaada hiyo imeshagawiwa na inaendelea kusambazwa kwa walengwa. 

Msaada ya misaada iliyopokelewa ni kama ifuatavyo:

 Fedha taslimu kiasi cha shilingi Bilioni 5,412,934.82 kimeshapelekwa Benki.


 Kiasi cha shilingi milioni 17,579,427.00 kupitia mitandao ya simu

 Ahadi za shilingi Bilioni 6,703,000,000 Hivyo jumla ya ahadi na fedha taslimu hadi sasa ni Shilingi Bilioni 12,133,564,361.82

 Serikali pia imepokea misaada mingine yenye thamani ya shilingi Bilioni 2.25 kama ifuatavyo: Unga Tani 58.12, Sukari Mifuko 1,150, Mchele Tani 133.96, Maharagwe Tani 19.666. Mahindi Tani 70.1, Majani ya Chai Tani 3, Maji Katoni 1,570, Mafuta lita 6,022, Sabuni Katoni 443, Shuka 495, Blanketi 6,125, Vyandarua 2,821, Magodoro 1,146, Mahema 367 n Turubai 6,237 vilipokelewa. 

Aidha serikali ilipokea vifaa vya ujenzi vikiwemo Saruji mifuko 24,433, Bati 20,933, Misumari kilo 1475, Nondo vipande 725, Kofia za bati 150 na mbao 250.

Lakini ifahamike kuwa baadhi ya waaliotoa ahadi kama serikali ya Uingereza wameahidi kutekeleza ahadi zao kwa kujikita moja kwa moja katika ujenzi wa Shule, Mara baada ya wakala wa majengo kuainisha viwango na gharama.

HATUA ILIYOCHUKULIWA NA SERIKALI KATIKA KUKABILIANA NA MAAFA 

Katika siku za hivi karibuni kumekuwepo na juhudi za kujaribu kufanya upotoshaji kuhusu hatua zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa katika kukabiliana na maafa haya, Ukweli ni kwamba serikali kwa kushirikiana na wadau imechukua hatua kubwa za kuwasaidia waathirika ambapo miongoni mwao yafuatayo yameshafanyika:

 Kutoa matibabu bure kwa majeruhi wote 560, kuandaa na kugharamia mazishi ya watu 17 waliofariki ambapo Mheshimiwa Waziri Mkuu alihudhuria, Aidha serikali kwa kushirikiana na wadau ilitoa mkono wa pole wa Shilingi Milioni 1.8 kwa kila familia iliyopatwa na msiba.

 Kuendelea kutoa misaada mbalimbali ya kibindamu ikiwemo chakula, Madawa, Nguo, Makazi ya muda, Huduma za tiba, Vifaa vya shule na huduma ya ushauri wa kisaikolojia kwa waathirika katika Wilaya zote za Mkoa wa Kagera zilizopata athari.

 Kushirikiana na Ofisi ya Mwakilishi Mkazi mmoja wa Mataifa na wadau mbalimbali wakiwemo Msalaba Mwekundu, Plan International (T), BRAC (T), World Vision, CARITAS, Save the Childre, JH Piego na Benki ya Dunia kufanya tathmini ya pamoja ya mahitaji ya haraka ya athari za Tetemeko la ardhi ili kubaini maeneo zaidi ya kuwasaidia wananchi.

HATUA ZA KUREJESHA HALI

Tangu kutokea kwa maafa haya serikali imeendelea kufanyia kazi masuala muhimu yaliyoainishwa katika tathmini ya Tetemeko ambapo hadi kufikia tarehe 13 Novemba, 2016 licha ya kuendelea kuwapatia wananchi mahitaji muhimu kama Chakula, Dawa na Misaada ya kujikimu katika makazi ya muda, kiasi cha shilingi Milioni 969,238,326.35, Mifuko ya saruji 17,423, Bati 5,348 na Misumari Kilo 1,107 vilitumika kwa kufanya ukarabati mkubwa na mdogo wa shule za msingi na Sekondari, Juhudi ambazo ziliwezesha wanafunzi wa shule hizo waliokuwa katika hatari ya kukosa masomo kuendelea na masomo yao.

Gharama hizo pia zimejumuisha ukarabati wa zahanati katika Halmashauri za Mkoa wa Kagera na kuanza kwa ujenzi wa kituo kipya cha afya (Ishozi/Kabyaile) kitakachojumuisha chumba cha upasuaji wa wodi ya kina mama na watoto kwa faida ya wananchi wote wa maeneo hayo. Pia serikali imegharamia urejeshwaji wa miundombinu ya barabara, maji na umeme katika maeneo kadhaa yaliyoathiriwa na tetemeko.

Shirika la World Vision kwa kushirikiana na serikali mkoani Kagera, tayari limetoa jumla ya mifuko ya saruji 2300 yenye thamani ya shilingi milioni 39,000,000 kwa kaya 460 zilizobomolewa nyumba na zilizoonekana kuwa na uhitaji zaidi ambapo katika awamu ya kwanza kila kaya ilipaa mifuko mitano ya saruji na kwa sasa utekelezaji wa awamu ya pili umeanza ambapo inatarajiwa kugawiwa mifuko ya saruji 10,645 yenye thamani ya shilingi Milioni 164,997,000.00 kwa kaya 2,129.

Aidha tayari serikali imeainisha kaya nyingine zilizoathirika zaidi zipatazo 370 za watu waliomo kwenye makundi maalumu (Wazee, Wajane na Walemavu) ambao watapatiwa vifaa vya ujenzi (Mabati 20 na mifuko 5 ya saruji kwa kila kaya) kwa ajili ya kukarabati nyumba zao. Ugawaji kwa awamu ya kwanza umeanza.

HITIMISHO

Haya ndio niliyoyabaini katika ziara yangu nilipozuru Mkoani Kagera naishauri Serikali kuchukua hatua kali dhidi ya wale wate waliokuwa wanapotosha watanzania dhidi ya matumizi ya fedha hizi kwa makusudi kwa madai kwamba zimeliwa na serikali.

Lakini niwapongeze wananchi wote Mkoani Kagera ambao waliitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuitikia wito wa kuanza ujenzi wa nyumba zao wao wenyewe huku serikali ikiunga mkono katika maeneo baadhi kama ambavyo nimeeleza katika makala yangu.

Jamii inapaswa kutambua kuwa hakuna serikali duniani ambayo inapanga Tetemeko la ardhi litokee ili liwauwe wananchi wake bali ni majanga ya asili ambayo kwa namna moja ama nyingine hayazuiliki.

Kwa wale wasomaji wa Biblia Takatifu Ukisoma Mathayo 3:2 inasema ”Tubuni, Kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribi” Nami nawasihi WATUBU wale wote waliokuwa wanapotosha kuwa hela za rambi rambi zimeliwa tena walipotosha bila kuwa hata na Data wala Taarifa sahihi za Matumizi ya fedha hizo.

Wakati Mwema...!
Mathias Canal
0756413465
Mwanza

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMATANO,NOV 30

RC SINGIDA AHIMIZA WATUMISHI KUWAJIBIKA

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Singida Mhandisi Mathew Mtigumwe, amewahimiza watumishi wa umma hasa wa ngazi ya Vijiji na Kata kuwajibika na kutimiza vyema majukumu yao kwani wao wako karibu zaidi na Wananchi, ili kutimiza adhma ya Serikali ya awamu ya tano ya kumpunguzia kama si kumuondolea kabisa kero zinazozuilika Mwananchi wa kawaida.

Mh. Mtigumwe ameyasema hayo leo katika Kijiji cha Kamenyanga kilichopo Kata ya Aghondi, Halmashauri ya Itigi, Wilayani Manyoni akiwa katika ziara yake ya kujitambulisha na kusikiliza kero za Wananchi, ambapo Wananchi wa Kata hiyo walimlalamikia Mkuu wa Mkoa juu ya utendaji mbovu wa Mtendaji wa Kata yao hasa ubadhirifu wa fedha za Kijiji na uuzaji wa maeneo ya Kijiji bila kufuata taratibu.

Kufuatia malalamiko hayo ya Wananchi, Mkuu huyo wa Mkoa ameagiza kusimamishwa kazi mara moja, ili kupisha uchunguzi kufuatia tuhuma mbali mbali zinazomkabili Bw. James Sylvester, Afisa mtendaji wa Kata ya Aghondi iliyopo halmashauri ya Itigi, Wilayani Manyoni, mkoani Singida, ambaye kwa kushirikiana na Mwenyekiti wa Kijiji cha Aghondi Bw. Mrisho Mbaruku, walikiuka taratibu za umilikishwaji wa maeneo ya Kijiji, na kumilikisha ardhi kwa baadhi ya watu kinyume na taratibu za Kijiji kwa manufaa yao binafsi.

“Nimekua nikipokea taarifa za utendaji kazi usioridhisha wa Bw. James Sylvester ambaye ni mtendaji wa Kata hii, hususani kwenye uwasilishaji wa mapato ya Halmashauri, hivyo kutokana na kashfa zinazo mkabili Mtendaji huyu, mbali na kilio cha wananchi ni vyema sasa akae pembeni na tukimkuta na hatia , sheria itachukua mkondo wake” Alisema Mh. Mtigumwe.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa wilaya ya Manyoni Mh. Geoffery Mwambe ambaye ameambatana na Mkuu wa Mkoa katika ziara hiyo amesema, kutokana na tuhuma zinazomkabili Bw. Mrisho Mussa, Mwenyekiti wa kijiji cha Kamenyanga ambacho pia kipo katika Kata ya Aghondi, kushindwa kuitisha mikutano ya Kijiji kwa muda muafaka kama miongozo ya kijiji inavyoelekeza, pia wananachi kuonesha kutoridhishwa na utendaji kazi wake, ameagiza kufanyika mkutano wa Kijiji mwishoni mwa mwezi huu, ili Mkutano huo utoe maazimio dhidi ya Mwenyekiti huyo.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mh. Mathew Mtigumwe yupo kwenye ziara maalumu akizunguka Mkoa mzima wa Singida, wenye Wilaya tano, zenye halmashauri saba, leo ikiwa ni siku ya tatu tangu kuanza kwa ziara hiyo, katika Halmashauri ya Itigi, Wilaya ya Manyoni, Mtigumwe ametembelea miradi mbali mbali ya maendeleo, na kuhimiza ushirikiano baina ya Viongozi na Wananchi katika kufanikisha malengo na mikakati inayowekwa na Serikali kwa mandeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla.

TIMU YA BUNGE YATUA TANGA KUJIFUA NA MASHINDANO YA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI

$
0
0
 Mwenyekiti wa timu ya Bunge,William Ngereja ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Sengerema mkoani Mwanza akizungumzia maandalizi ya timu ya Bunge kuelekea mashindano ya Afrika Mashariki yatakayofanyika nchini Kenya.
 Mkurugenzi wa Benchi la Ufundi la timu ya Bunge,Stephen Ngony’ani alimaarufu Proffesa Maji Marefu akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye hotel ya Tanga Beach Resort ambapo timu ya Bunge imeweka kambi.

 Mwenyekiti wa timu ya Bunge,William Ngereja ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Sengerema mkoani Mwanza katika akiteta jambo na wachezaji wa timu ya Bunge kushoto aliyevaa tisheti nyekundu ni Mkurugenzi wa Benchi la Ufundi la timu ya Bunge,Stephen Ngony’ani alimaarufu Proffesa Maji Marefu
TIMU ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania “Bunge Sports Club”imetua mkoani Tanga leo kuweka kambi ya siku tatu kwa ajili ya kujiandaa na Mashindano ya Bunge la Afrika Mashariki yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Desemba 14 mwaka huu mjini Mombasa nchini Kenya.

Kikosi cha timu ya Bunge kilichosheheni wachezaji wa michezo ya mpira wa miguu,wavu,riadhaa ,kuvuta kamba na mchezo wa gofu ambao inajumuisha wachezaji 60 ambao watashiriki kwenye mashindanio hayo yanayotazamiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na kila kuonekana kujipanga imara.

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Tanga mara baada ya timu hiyo kutua,Mwenyekiti wa timu ya Bunge,William Ngereja ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Sengerema mkoani Mwanza alisema kuwa maandalizi kwa upande wa timu yao yamekamilika kwa asilimia kubwa.

Alisema kutokana na umuhimu wa mashindano hayo waliamua kuweka kambi mkoani Tanga ili kuendana na hali ya hewa kabla ya kwenda nchini Kenya kwa ajili ya kushiriki mashindano hayo ikiwa ni mpango wa kuimarisha kikosi chao.

  “Mimi nisema tu sisi kama timu ya Bunge nia na lengo letu kubwa ni kuhakikisha tunaibuka na ushindi kwenye mashindano hayo na ndio maana tumeamua kuweka kambi mkoani Tanga lakini pia hata hivyo pia kikosi chetu kimeimarika kutokana na usajili ambao tumekuwa tukiufanya kila baada ya miaka mitano “Alisema Ngeleja.

Kwa upande wake,Mkurugenzi wa Benchi la Ufundi la timu ya Bunge,Stephen Ngony’ani alimaarufu Proffesa Maji Marefu alisema kuwa kikosi chao kimejipanga vizuri kuhakikisha wanaibuka na ushindi kwenye mchezo huo.

Alisema timu hiyo ipo kwenye mazingira mazuri ya kuhakikisha wanaibuka na ushindi kwenye mashindano hayo ili kuweza kutimiza dhamira yao waliojiwekea  ya kutwaa ubingwa.Kwa upande wake,Nahodha wa timu ya Mpira wa Pete ya Bunge,Halima Mdee ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kawe alisema kuwa wamejiandaa vizuri kuhakikisha wanafanya vizuri ili kutimiza dhamira waliojiwekea ya kuibuka na Ubingwa.

  “Nisema tu sisi kama timu ya mpira wa Pete ya Bunge tumejipanga vizuri na kikosi chetu kina hari kubwa ya kuhakikisha tunaiwakilisha nchi yetu ya Tanzania ipasavyo kwa mafanikio makubwa”Alisema.habari kwa hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

EXECUTIVE FURNISHED OFFICE SPACE AVAILABLE FOR RENT

$
0
0
A spacious fully furnished & carpeted office space is available for immediate occupancy.

Located at Hugo House Kinondoni Plot no 22 (Kinondoni Road) on the 3rd floor of the property.

The office covers a total area of 80 square metres, 4 partitioned rooms and a lobby area that could be used for meetings.

This office comes with pre installed Air Condition split units.

For inquiry please contact 0713 465 336 or 0713 272 202.



DIWANI WA CHADEMA AJIVUA UAANACHAMA NA KUJIUNGA CCM

$
0
0
Kushoto ni Diwani wa kata ya Shule ya Tanga iliyopo Songea mjini mkoani Ruvuma kupitia tiketi ya Chama Cha Demoklasia na Maendeleo ( CHADEMA )Mussa Ndomba aliyejivua uaanachama na kujiunga Chama tawala cha mapinduzi (CCM)  akimkabidhi kadi mwenyekiti wa CCM mkoa wa RUVUMA Mh. ODDO MWISHO. kwa undani zaidi wa habari hii bonyeza play hapo chini .

UFAULU DARASA LA SABA WAPANDA MKOA WA SINGIDA; ELFU KUMI NA NNE KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2017.

$
0
0
Kiwango cha ufaulu wa mitihani ya kumaliza elimu ya msingi Mkoani Singida kimepanda kutoka wastani wa asilimia 58.41 mpaka asilimia 69.25 ikiwa ni ongezeko la asilimia 11 huku wanafunzi 14,759 wakichaguliwa kujiunga na masomo ya sekondari kwa kidato cha kwanza kwa mwaka 2017.

Buhacha Baltazar Kichinda akiongoza kikao cha uteuzi wa wanafunzi wa kidato cha kwanza kwa mwaka 2017 kama Kaimu Katibu Tawala Mkoa na mwenyekiti wa kikao hicho amesema mkoa umefaulisha wavulana 6,852 na wasichana7,907 huku akiwapongeza waalimu wote kwa bidii ya ufundishaji iliyopelekea mkoa wa singida kushika nafasi ya 12 kati ya Mikao 26 ya tanzania bara.

Kichinda ameipongeza halmashauri ya Itigi kwa kushika nafasi ya kwanza kati ya halmasahuri saba za mkoa wa singida na ya 38 kitaifa kati ya halmashauri 186 za Tanzania bara huku ikifaulisha kwa asilimia 80.41. Aidha amewatia moyo halmasahuri ya Mkalama kwa ufaulu hafifu wa 57.51 na kuwa nafasi ya 155  kitaifa.

Kichinda ameongeza kuwa kwa sasa kila Mkurugenzi wa halmasahuri anapaswa kukaa na wadau wake wa elimu ili kupanga mikakati ya kuboresha zaidi elimu, amesema lengo kubwa kwa sasa ni kuhakikisha kila mwanafunzi aliyefaulu anajiunga na kidato cha kwanza na kumaliza elimu ya sekondari.

Amesema sekta ya elimu inachangamoto mbalimbali ikiwemo utoro wa walimu na wananfunzi, miundombinu ya vyumba vya madarasa kutotosheleza mahitaji halisi, upungufu wa waalimu, uhaba wa nyumba za walimu pamoja na waalimu wenyewe kuwa wachache tofauti na mahitaji halisi hivyo amewata wadau wa elimu kujipanga kutatua changamoto hizo na sio kusubiria serikali kuu kufanya kila kitu.

Aidha kichinda amesema kuwepo na utaratibu wa kuwapongeza waalimu hasa kwenye shule zilizofanya vizuri ili iwe motisha kwa kazi wanayoifanya huku akiitangaza shule ya msingi Utaho ya halmasahuri ya Ikungi kuwa ya kwanza kimkoa kwa shule zenye wananfunzi zaidi ya 40 na shule ya msingi Aghondi ya Itigi kuwa ya kwanza kimkoa kwa shule ambazo zina wanafunzi chini ya 40.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo amesema ili kuboresha elimu mkoani Singida msisitizo uwepo wa kuhakikisha wananfunzi wote wanapata chakula shuleni ili waweze kusikiliza kwa umakini mzuri.

Tarimo ameongeza kuwa wazazi wanapaswa kutambua kuwa elimu bila malipo haiwaondolei wajibu wao kama wazazi wa kuhakikisha wanafunzi wanakula, wanalala na kuvaa hivyo hivyo watakaposhirikishwa katika kuchangia chakula, ujenzi wa mabweni au shuguli za elimu wajitoe kwani wamiliki wa shule ni wazazi.

Amesema utaratibu wa kufanya ukaguzi ili kuwatambua waalimu watoro au wazembe ufanyike katika halmashauri zote na kwa viongozi wote wanaotembelea vijijini bila ya kusubiri ziara maalumu ya ukaguzi na kuongeza kuwa hali hiyo itawaongezea umakini waalimu katika kutekeleza majukumu yao lakini pia watendaji watabaini changamoto za waalimu na shule na kuzitatua kwa uharaka.

HAYA CHANGAMKIA NAFASI ZA KAZI HIZI HAPA FASTA FASTA.

UN NA EU YAWANOA MABALOZI 50 WA MALENGO YA DUNIA IRINGA

$
0
0
UMOJA wa Ulaya (EU) na Umoja wa Mataifa (UN) wameweka nguvu ya pamoja kuendesha kampeni ya uelewa wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) nchini Tanzania. Wakiwa Mkoani Iringa wamepata nafasi ya kuzungumza na wanachuo 1,000 kutoka vyuo vikuu vya Iringa na Ruaha kwenye semina iliyoelezea malengo ya dunia ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani ambapo kati ya hao, vijana 50 wamepata semina ya mwongozo wa kuwa mabalozi wa malengo hayo (Global Goals Champions). Kampeni hiyo imelenga kuwafanya vijana waelewe malengo 17 ya dunia ambayo kwa sasa yana mwaka mmoja tangu yapitishwe na kuwatanabaisha wajibu wao katika kufanikisha utekelezaji wake ndani ya mazingira ya Tanzania. 
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi Ripoti ya Umoja wa Mataifa ya mpango wa misaada ya maendeleo UNDAP II 2016-2021 Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Dr. Cephas Mgimwa alipomtembelea ofisini kwake mjini Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akifafanua jambo juu ya ripoti ya Umoja wa Mataifa ya Mpango wa misaada ya Maendeleo 2016-2021 (UNDAP II) kwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Dr. Cephas Mgimwa alipomtembelea ofisini kwake mjini Iringa
Mwanasheria wa Chuo Kikuu cha Ruaha Iringa, Martin Noel akiwa ameongozana Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano chuoni hapo sambamba Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiendesha semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia.

Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro akielezea fursa za ufadhili wa masomo nje ya nchi katika tovuti ya Umoja wa Ulaya Tanzania wakati wa semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia iliyofadhiliwa na EU.
Mkufunzi wa Malengo ya Dunia ambaye pia ni Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu akiwapiga msasa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia kwenye semina hiyo iliyofadhiliwa na EU.
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro akiwa amejumuika na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha wakati wa semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia ambapo semina hiyo imefadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) nchini.
Pichani juu na chini ni vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha walioshiriki semina maalum ya kuwa mabalozi wa malengo ya dunia (Global Goals Champions) iliyoandaliwa na UN na kufadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) mjini Iringa.
 
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez (kulia) akimkabidhi cheti Rais wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa Athman Waziri aliyehitimu kuwa balozi wa Malengo ya Dunia (Global Goals Champion).
Picha juu na chini Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiendelea na zoezi la kutunuku vyeti kwa mabalozi wa malengo ya dunia kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Mabalozi wa Malengo ya Dunia (Global Goals Champions) baada ya kuhitimisha semina maalum iliyoshirikisha vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Mwanasheria wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Martin Noel baada ya kuhitimisha semina ya malengo ya dunia mjini Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Afisa Habari wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU), Muazarau Matola
Baadhi ya Global Goals Champions katika picha ya kumbukumbu na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu.
Mkufunzi wa Malengo ya Dunia ambaye pia ni Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu akibadilishana mawazo na wahitimu wa semina malengo ya dunia (Global Goals Champions) mara baada ya kuhitimisha semina hiyo iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Ruaha mjini Iringa ambapo imefadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU).

KAMISHNA WA TRA AHITIMISHA MAFUNZO YA ‘SCANNER’ MPYA BANDARINI

$
0
0
Kamishna wa Mapato ya ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Elijah Mwandumbya akizungumza na wahitimu wa mafunzo ya usimamizi na uendeshaji wa mashine za ukaguzi wa mizigo ‘scanner’ kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) na TRA. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa TEHAMA, Bw. Abdulrahman Mbamba pamoja na Wakufunzi kutoka Kampuni iliyofunga mashine hizo.
Kamishna wa Mapato ya ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Elijah Mwandumbya akikabidhi vyeti kwa wahitimu mbalimbali kutoka TPA na TRA.
Kamishna wa Mapato ya ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Elijah Mwandumbya akiwa katika picha ya pamoja na Wahitimu na Wakufunzi

Waziri Mahiga asaini kitabu cha maombolezo ya Rais Mstaafu wa Cuba Fidel Castro

$
0
0
Mhe. Waziri Balozi Dkt. Augustine Mahiga akitoa heshima mbele ya picha ya Rais wa zamani wa Cuba hayati Fidel Castro alipoenda kusaini kitabu cha maombolezo 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisaini kitabu cha maombolezo .

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi wa Cuba nchini Mhe. Jorge Luis Lopez Tormo alipowasili nyumbani kwa Balozi huyo mapema leo kusaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Rais Msataafu wa Cuba Fidel Castrol, Jijini Dar es Salaam 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimfariji Balozi wa Cuba nchini Mhe. Jorge Luis Lopez nyumbani kwake Jijini Dar es Salaam kabla ya kusaini kitabu cha maombolezo

WAJERUMANI WATENGENEZA FILAMU NDANI YA HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI.

$
0
0
Mkurugenzi wa Utalii wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ibrahim Musa (katikati) akizungumza na Mratibu wa uzalishaji wa filamu wa kampuni ya Polyphon ya nchini Ujerumani,Mona Lessnick alipotembelea eneo la Kogatende jirani na  Mto Mara ambapo kulikuwa kukifanyika shughuli za uchukuaji wa picha za video kwa ajili ya Tamthiliya ya Dream Boat.kulia ni Meneja Mawasiliano wa TANAPA,Pascal Shelutete.
Mkurugenzi wa Utalii wa TANAPA,Ibrahim Musa akizungumza na Mona Lessnick katika eneo la Kogatende ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Mratibu wa uzalishaji wa Filamu wa kampui ya Polyphon Studio,Mona Lessnick (kulia) akiwa na Mpiga picha mkuu wa kampuni hiyo ,Manuel Schroeder na Jorg Gariel  wakati wakizungumza na wanahabari  (hawapo pichani) juu ya tukio la uchukuaji wa picha za video katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Eneo la Kogatende ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambapo picha za video za sehemu ya Tamthiliya ya Dream Boat zimepigwa hapo.
Moja ya gari lililotumika katika tukio hilo likitoka eneoo la tukio kando ya Mto Mara unopita katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Uchukuaji wa picha za video kando ya Mto Mara ukiendelea.
Magari yakiwa yamebeba sehemu ya vifaa kwa ajili ya uchukuaji wa picha za Video.
Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete akiteta jambo na Mona Lessnick katika eneo la Kogatende ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Mkurugenzi wa Utalii wa TANAPA,Ibrahim Musa( katikati) akisikiliza kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Jorg Gabriel walipoktana eneo la Kogatende katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Meneja Mawasiliano wa Tanapa,Pascal Shelutete akisaidia kubeba moja ya Kamera kubwa zilizokuwa zikitumika katika matukio ya uchukuaji wa picha katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Moja ya Kamera kubwa iliyokuwa ikichukua matukio katika upigaji picha wa Tamthiliya ya Dream Boat katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Mkurugenzi wa Utalii akiitizama Kamera ambayo ilikuwa iktumika kupiga picha za matukio mbalimbali wakati wa utengenezaji wa filamu hiyo.
Wataamu wakifunga Kamera katika ndge ndogo ya Shirika la ndege la Costal Airline kwa ajili ya upigaji wa picha za juu . 

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini.

SEKTA ya Utalii nchini inatarajia kupiga hatua baada ya wasanii maarufu wa filamu kutoka nchi za nje kuanza kutumia baadhi ya maeneo katika vivutio vya Utalii vilivyoko nchini kuandaa sehemu za tamthiliyaa zao.

Kampuni kubwa ya utengezaji wa filamu ya Polyphon Group  ya Humburg  nchini Ujerumani imekuwa ya kwanza kupiga picha za video za sehemu ya tamthiliya maarufu nchini Ujerumani ya Dream Boat ambayo imekuwa ikiooneshwa katika vituo mbali mbali vya televisheni kwa nchi zinazozugumza lugha ya Kijerumani.

Maeneo ambayo picha za video zimechukuliwa ni pamoja na Kogatende na Lobo ndani ya Hifadhi za Taifa za Serengeti ,huku picha nyingine zikipigwa katika Hifadhi ya taifa ya Arusha pamoja na Pori la akiba Endumeti.

“Tumefanya Sehemu moja ya Tamthiliya yetu Botswana,moja Zambia na nyingine Kenya katika muendelezo wa tamthiliya hii inayooneshwa kwa mika 30 sasa,Sehemu ya mwisho ya muendelezo wa filamu hii iliyochukuliwa Afrika ilikua mwa 2007,ni muda mrefu na tuliangalia wapi tunaweza enda,na tukafanya utafiti ,tukaja Tanzania,Tumeona hii nchi ni nzuri tukaamua kuleta filamu yetu hapa”.alisema Manuel Schroeder mpiga picha wa kampuni ya Polyphon Studio.

Mkurugenzi wa Utalii wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ibrahim Musa amesema hatua hii ni fursa nyingine muhimu kwa Tanzania  kutangaza vivutio vya utalii kimataifa huku mratibu wa uzalishaji wa filamu wa kampuni ya Polyphon,Mona Lessnick akieleza utalii utaongezeka kupitia tamthiliya hiyo.

“Kutokana na uzoefu ,watu wametuamini sisi , tumefanya hii kazi kwa miaka 30 sasa,hivyo baada ya kurusha sehemu ya tamthiliya ilichukuliwa hapa itaongeza soko la wageni kutoka nchi zinazozungumza kijerumani,kwa sababu wanajua tunafanya utafiti,tmekwisha fka hapa mara mbili na kukutana na mtaalamu na kutuonesha maeneo ,wanajua tunachukua maeneo mazuri,hoteli nzuri,tuna taarifa  na vifaa vya kutosha,hivyo kutakuwa na matokeo makubwa katika Utalii “alisema Lessnick.

Kuhusu Maudhui ya Tamthiliya hiyo ambayo inaoneshwa kwa zaidi ya miaka 30 sasa ,Mona Lessnick amesema imebeba maudhui ya aina tatu ambayo ni Vichekesho,Mahusiano pamoja na Drama.
“Ni Burudani kwa familia,tuna hadithi tatu,katika hadithi kuu watu wanasafiri kwa meli kuizunguka nchi,wakasafiri kuja Tanzania ,kuna hadithi nzuri za mahusiano ambazo vipande vyake vimechukuliwa Tanzania “alisema Lssnick.

“Katika muongozo tuna aina tatu ya hadithi,tuna hadithi ya mapenzi,tuna hadithi ya vichekesho na drama hii tunayofanya leo ni vichekesho,tuna watu wawili ,katika muongozo wa kwanza inaonesha watu haw wamepata tatizo katika gari lao hapa  Serengeti,lakini tulipaa ugumu kupiga picha ndio tukapata mahala hapa pazuri kwa kufanya video,tukafanya Drama hapa ya gari kukwama ndani ya maji na gari nyingine ikaja nyuma kuoka watu hawa wakiw wamekaa juu ya gari lao na kuondolewa katika maji”alisema Schroeder.

Tamthiliya ya Dream Boat imefikisha miaka 35 sasa tangu kuanza kurushwa katika vituo mbalimbali vya Televisheni nchini Ujerumani na kwamba sehemu mbili zenye urefu wa dakika 90 kila moja za tamthiliya hiyo ,picha zake hupigwa katika nchi moja ya kiafrika .

Mwisho.


VODACOM TANZANIA YAKABIDHI SIMU FEKI ZAIDI YA 500 ZILIZOKUSANYWA KUTOKA KWA WATEJA WAKE KWA AJILI YA KUTEKETEZWA

$
0
0
  Mkuu wa Bidhaa wa Vodacom Tanzania, Samson Mwongela (kushoto) akisaidiwa na Meneja Uhusiano kampuni hiyo, Matina Nkurlu (katikati), kuonyesha simu feki zilizokusanywa kutoka kwa wateja wao kwa ajili ya kuteketeza kama ilivyoagizwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), wakati  wa mkutano wa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.Kulia ni Gideon Chilambo ambaye ni  Mkurugenzi wa  kampuni ya Chilambo General Trade Company inayoteketeza bidhaa feki.
Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu (katikati) akionyesha simu halisi aina ya Smart Prime 7 yenye ubora na kiwango inayouzwa kwa Tsh 250,000/-, wakati akizungumza  na  waandishi wa habari juu ya simu feki zilizokusanywa na kampuni yake kutoka kwa wateja kwa ajili ya kuteketezwa kama ilivyoagizwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mkuu wa Bidhaa wa kampuni hiyo, Samson Mwongela na kulia ni Gideon Chilambo ambaye ni  Mkurugenzi wa  kampuni ya Chilambo General Trade Company inayoteketeza bidhaa feki.

BALOZI WA KOREA KUSINI AENDESHA MHADHARA CHUO CHA BANDARI

$
0
0
 Balozi wa Korea Kusini hapa nchini, Mhe. Song Geum-young (kushoto) akijadili jambo na Mkuu wa Chuo cha Bandari, Dk. Joseph Kakeneno wakati wa mhadhara wake na wanachuo cha Bandari hivi karibuni.
 Mkuu wa Chuo cha Bandari, Dk. Joseph Kakeneno akimkaribisha Balozi wa Korea Kusini hapa nchini, Mhe. Song Geum-young kutoa mhadhara wake kwa Wanachuo.
 Balozi wa Korea Kusini hapa nchini, Mhe. Song Geum-young akitoa mhadhara kwa wanachuo. Kulia ni Mkuu wa Chuo cha Bandari, Dk. Joseph Kakeneno.
Baadhi ya Wanachuo cha Bandari wakifuatilia mhadhara uliokuwa ukitolewa na  Balozi wa Korea Kusini.
 Baadhi ya Menejimenti ya Chuo cha Bandari ikifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Balozi wa Korea Kusini. 
Mkuu wa Chuo cha Bandari, Dk. Joseph Kakeneno akimkabidhi zawadi Balozi wa Korea Kusini hapa nchini, Mhe. Song Geum-young mara baada ya kutoa mhadhara kwa wanachuo.


WAHITIMU CHUO KIKUU MUHIMBILI WATAKIWA KUJIENDELEZA KIELIMU

$
0
0
Zainab Nyamka, Globu ya Jamii .

MKURUGENZI wa Elimu ya Juu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  Prof Silvia Temu amesema kuwawanafunzi wanaohitimu wanatakiwa kwenda kufanya kazi kwa juhudi kubwa na kutokuacha kujiendeleza na kujifunza kwani dunia inabadilika na magonjwa yanazidi kujitokeza kila siku.

Aliyasema hayo, wakati wa kongamano la Mjasiri lililowakutanisha wanafunzi waliosoma zamani katika Chuo Kikuu cha Afya, Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) na wanafunzi wanaohitimu na kuwataka kuendelea na utafiti wa magonjwa mbalimbali yanayowazunguka jamii.

Prof Temu amesema kuwa MUHAS wameweza kufanya kitu kizuri sana kwa kuwakutanisha wanafunzi waliomaliza hapa na mkusanyiko huu utasaidia kuweza kuleta mawazo mapya na zaidi yatasaidia kwenye kukuza na kuendeleza sekta ya afya.

"kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof Joyce Ndalichako, tunaoenda kuwapongeza sana MUHAS kwa jitihada nzuri waliyofanya ya kuwakutanisha pamoja wanafunzi waliosoma miaka ya nyuma pamoja na hawa wanaohitimu katika ngazi mbalimbali kwani tunachokijua ni kuwa watabadilishana uwezo hasa kwa wale waliokuwa washapata uzoefu wa muda mrefu,"amesema Prof Temu.

Makamu Mkuu wa Chuo cha MUHAS, Prof. Ephata Kaaya amesema kuwa  kongamano hili la Majasiri litaleta manufaa makubwa sana kwani kutawawezesha wanafunzi wanaohitimu na waliomaliza miaka ya nyuma kufanya kazi kwa pamoja, kwani Majasiri wanachangia kwa kiwango kikubwa katika Chuo kwa kutoa mawazo na hata fedha kwa ajili ya kuendeleza maendeleo ya chuo.

Kaaya amesema kuna changamoto nyingi sana  katika kuendeleza maendeleo ya chuo hususani kwa upande wa fedha ila kwa kuwakutanisha hawa Majasiri kutasaidia kwa namna moja au nyingine kwenye kutatua matatizo ya chuo cha MUHAS.
Mkurugenzi wa Elimu ya Juu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  Prof Silvia Temu akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia  Prof Joyce Ndalichako wakati wa Kongamano la Majasiri wa Chuo Kikuu cha Afya, Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) leo Jijini Dar es salaam.
 Mkurugenzi wa Elimu ya Juu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  Prof Silvia Temu (katikati)akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kutoka kushoto ni
Makamu Mkuu wa Chuo cha MUHAS, Prof. Ephata Kaaya, Mwenyekiti wa kamati ya Chuo Mariam Joy Mwaffisi, kutoka kulia ni makamu mwenyekiti wa kongamano Dr Ellen Senkoro na Mwenyekiti wa wa kongamano hilo  Prof Charles Mgone.
Mkurugenzi wa Elimu ya Juu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  Prof Silvia Temu akiangalia baadhi ya maonesho yaliyoandaliwa na Wahitimu wanaomaliza kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) leo Jijini Dar es salaam.
 Mkurugenzi wa Elimu ya Juu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  Prof Silvia Temu akiwa na Makamu Mkuu wa Chuo cha MUHAS, Prof. Ephata Kaaya (kushoto),  Mwenyekiti wa wa kongamano la Majasiri wa Chuo hicho Charles Mgone.
 Baadhi ya wahitimu na wahitimu wakiwa makini kufuatilia kongamano hilo. Picha zote na Zainab Nyamka.

Majaribio ya wazi Azam FC Jumamosi Mkoani Kigoma

$
0
0
KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, itakuwa mkoani Kigoma wikiendi hii  siku ya Jumamosi Desemba 3, 2016 kusaka vipaji vya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (U-17).

Huo ni mwendelezo wa mpango wa Kitaifa wa timu hiyo wa kutengeneza kikosi imara cha timu ya vijana wa umri huo, ambapo inakwenda Kigoma kutokana na mkoa huo kuwa historia ya kisoka nchini ya kutoa wanasoka wengi waliotamba.

Majaribio hayo ya pili kuelekea mwisho wa kufungwa zoezi hilo, yatafanyika ndani ya Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma Jumamosi hii kuanzia saa 2.00 asubuhi hadi saa 8.00 mchana na vijana wanaotakiwa ni wale waliozaliwa kuanzia mwaka 2000 hadi 2004.

Mpaka sasa zoezi hilo limeshahusisha mikoa sita, ambayo ni Dar es Salaam, Tanga, Morogoro & Dodoma, Visiwani Zanzibar, Mbeya na Mwanza, ambapo kiujumla Azam FC imewafanyia usaili jumla ya vijana 3, 265 na kuvuna 70 pekee kati ya hao waliochaguliwa, huku 151 wakiwekwa akiba kwenye kumbukumbu za mradi huo.

Vijana hao wote waliochaguliwa kwenye mikoa mbalimbali, wanasubiria kuitwa kwenye mchujo wa mwisho utakaofanyika ndani ya Uwanja wa Azam Complex baadaye mwezi huu Desemba, ambao ndio utatoa vijana bora watakaounda timu hiyo.
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live




Latest Images