Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

Mtanzania wa Kwanza Kupanda Mlima Evarest Katika Mwaka 2012 na wa Tatu Kupanda Mlima Huo Mkubwa Duniani

$
0
0
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said (Mpaka Basi) akiwa na mgeni wake Ndg Wilfred Moshi wakiwasili katika viwanja vya Baraza la Wawakilishi Chukwani Zanzibar, kutembelea na kujionea shughuli za Mkutano wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Ndg Wilfred Moshi ni Mtanzania wa Kwanza kupanda Mlima Mkubwa Duniani wa Evarest ukiwa na Mita 8,848, Mtanzania huyo Ndg Wilfred Moshi amepanda mlima huo mwaka 2012. akiwa ni Mwaafrika wa Tatu kupanda mlima huo na mwafrika wa Pili mweusi kupanda mlima huo Duniani kwa ukubwa.
Ndg Wilfred Moshi akiwa Zanzibar kwa matembezi na kuangalia Utalii wa Zanzibar na kupata nafasi kutembelea Baraza la Wawakilishi Chukwani Zanzibar kwa mualiko wa Mhe Mwakilishi wa Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said.
Ndg Wilfred Moshi akitambulishwa kwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar akiwa Mgeni wa Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said (Mpaka Basi) akisalimia Wajumbe wa Baraza wakati wa kutambulishwa kwake.
Mtanzania wa Kwanza kupanda Mlima Evarest Ndg Wifred Moshi akiwa katika Ukumbi wa Mkutano wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar akiwa mgeni wa Mhe Simai Mohammed Said. akiwa katika sehemu ya wageni katika ukumbi huo wa Baraza Chukwani Zanzibar.
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said, akimtambulisha Mgeni wake Ndg Wilfred Moshi kwa Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe Zuberi Ali Maulid, alipofika kutembelea na kujionea shughuli za Baraza la Wawakilishi wakati wa Mkutano wake leo asubuhi.  
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Mtanzania wa Kwanza na Muafrika wa Tatu Duniani kupanda Mlima wa Evarest Ndg Wilfred Moshi alipofika katika jengo la Baraza la wawakilishi Zanzibar akiwa mgeni wa Mhe Simai Mohammed Said Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar. 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akimsikiliza Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe. Simai Mohammed Said akitowa maelezo ya mgeni wake Ndg Wilfred Moshi ambae ni Mtanzania wa Kwanza kupanda Mlima Evarest.
Ndg Wilfred Moshi akitowa historia yake kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipofika katika majengo ya Baraza la Wawakilishi kwa mualiko wa Mhe. Simai Mohammed Said Mwakilishi wa Tunguu Zanzibar. akitowa historia yake ya kufanikiwa kupanda mlima huo mkubwa duniani na kuelezea tayari ameshapanda Mlima Kilimanjaro zaidi ya mara 100.  
Ndg Wilfred Moshi akiwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kwa ajili ya kumbukumbu yake alipofika kutembelea Baraza la Wawakilishi Chukwani Zanzibar leo. 29-11-2016 akiwa mgeni wa Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said.
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wakiwa katika picha ya pamoja na Mtanzania wa Kwanza kupanda Mlima Mkubwa Duniani wa Evarest Ndg Wilfred Moshi alipofika katika jengo la Baraza la Wawakilishi Zanzibar.

Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot.
Zanzinews.com.
othmanmaulid@gmail.com



NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO AZINDUA HUDUMA MPYA YA KIKUNDI

$
0
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Mhe. Dorothy S. Mwanyika (wa pili kutoka kushoto)Akiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Accessbank Bi  Hedvig Sundberg(wa pili kutoka kulia ) pamoja na Mkuu wa kitengo cha  Maendeleo ya Biashara, Ndugu Andrea Ottina (kulia)Mwakilishi kutoka shirika la Care International Ndugu Christian Pennotti (kushoto) Akizungumza kwenye uzinduzi wa Huduma Mpya Ijulikanayo Kama KIKUNDI Inayotolewa na Access bank Mhe. Dorothy S. Mwanyika amewataka watanzania Kujiunga Kwenye Vikundi Mbalimbali na kisha  Kuchangamkia Fursa hiyo inayowawezesha wana kikundi Kujipatia Huduma Mbalimbali za Kibenki  Kupitia Simu ya Mkononi Kwa Haraka na yenye usalama zaidi.
Huduma Hii inawapa uwezo wanakikundi kuweza kufanya Mihamala ya Benki muda wowote na Mahali popote walipo kwa kutumia Simu.

 Uzinduzi huo pia umeudhuriwa na Mdau Mkubwa wa Maendeleo Mwakilishi kutoka shirika la Care International Ndugu Christian Pennotti (kulia)Ambapo amesema  Kwa sasa Hapa Tanzania  shirika hilo linasimamia vikundi zaidi ya 10,000  vyenye wanachama zaidi ya 250,000 vikundi hivyo vimekua na uhitaji mkubwa wa huduma za kisasa za kibenki jambo ambalo Wameishukuru  AccessBank kwani wamekua mojawapo ya Mabenki wanaounga mkono na kuhakikisha vikundi hivi vinapatiwa huduma za kibenki tena kwa njia za kisasa kabisa

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Mhe. Dorothy S. Mwanyika Akizindua rsmi Huduma ya KIKUNDI
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Mhe. Dorothy S. Mwanyika Akikata keki wakati wa uzinduzi huo.
Akizungumza pia juu ya hili, Afisa Masoko wa AccessBank Ndugu Sijaona Simon alisema "Kwa bahati mbaya, kwa muda mrefu vikundi vya aina hii vimekuwa vikitengwa na taasisi mbali mbali za kifedha ikiwa ni pamoja na mabenki hii ni kutokana na huduma kuwa ghali mnohuku zikiamabatana na masharti magumu ya nyaraka zinazohitajika. 
 
Akaunti  hii ya KIKUNDI ni mahususi kwa ajili yao"Mpaka sasa  vikundi zaidi ya 100 vimeshajiunga na AccessBank Tanzania na tunatarajia vikundi vingi  kujiunga na akaunti hii.”
 
Kwa kawaida vikundi hivi huwa na  jumla ya wanachama 15 hadi 30, wanachama hawa hukukutana kwa wiki mara moja kwa lengo la kununua hisa, kukopeshana  na kujadili masuala mengine ya kijamii ikiwa ni pamoja na ustawi wa jamii inayowazunguka. 

Fedha zote huhifadhiwa ndani ya kibubu, na wanachama watatu hukabidhiwa funguo za kibubu hicho.Kwa kawaida kikundi huwa na Viongozi  watano ambao huchaguliwa na wanachama, ikiwa ni pamoja na Mwenyekiti, Wahasibu wawili, Katibu na Mweka Hazina.Wanachama wengine watatu ambao hushikilia funguo za kibubu ambacho  hufunguliwa mara moja kila wiki baada ya mkutano kuanza. 

Licha ya usalama wa mfumo wa funguo, njia ya kuhifadhi fedha kwenye kibubu imeonekana kuwa si chaguo salama kwani mara nyingi huweza kuibiwa hasa mwishoni mwa mzunguko ambapo fedha zilizohifadhiwa kwenye kibubu huwa zimefikia kiasi kikubwa. Kutokana na haya , Access Bank imeamua kuja na njia mbadala ya kibubu kwa kuanzisha akaunti iyakayounganishwa na simu ya mkononi ambapo sasa kila muamala utakaofanyika utaanzishwa na Mwenyekiti na kupewa idhini na Waweka hazina wawili kupitia  simu zao za mkononi. 

AccessBank WAKALA , ni mawakala wanaotoa huduma za kibenki kwa niaba ya AccessBank watapatikana maeneo ya karibu na vikundi ili kuweza kurahisisha huduma ya kuweka na kutoa fedha kwa haraka zaidi. Tofauti na kuweka fedha kwenye akaunti ya kikundi ambapo  idhini ya watu wengine haihitajiki ,kutoa fedha kwenye Akaunti kutahitaji idhini kutoka kwa wanachama watatu.

Vikundi hivi kwa kupitia Akaunti ya KIKUNDI  inayowezeshwa na AccessMobile  vitaweza kunufaika na huduma za AccessBank kwa kufanya miamala ya bure kwa njia ya simu ya mkononi na kuungana na watumiaji wengine wa huduma hii.


PROFESA MUHONGO, WAZIRI WA NISHATI ZAMBIA WAKUTANA KUZUNGUMZIA BOMBA LA TAZAMA

$
0
0
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati), akijadiliana jambo na Waziri wa Nishati wa Zambia, David Mabumba (kushoto) na Mkurugenzi kutoka Bomba la Mafuta la TAZAMA, D. Legge (kulia).
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Kulia), na Waziri wa Nishati wa Zambia, David Mabumba wakifurahia jambo mara baada ya mazungumzo baina yao yaliyofanyika Ofisini kwa Waziri Muhongo jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) na Waziri wa Nishati wa Zambia, David Mabumba (wa tatu kutoka kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe ulioambatana na Waziri Mabumba. Wa Tatu kutoka Kulia ni Kaimu Katibu Mkuu, Profesa James Mdoe.
 Waziri wa Nishati wa Zambia, David Mabumba (kushoto) akimuaga Waziri wa Nishati na Madini nchini, Profesa Sospeter Muhongo (wa pili kutoka kushoto) baada ya kikao chao kilichofanyika ofisini kwa Waziri Muhongo. Wa pili kutoka Kulia ni Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara, Profesa James Mdoe akiagana na Mkurugenzi kutoka Bomba la TAZAMA, D. Legge.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa pili kutoka kulia) akizungumza na Waziri wa Nishati wa Zambia David Mabumba (wa tatu kutoka kulia) na Ujumbe wake, ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, akisisitiza jambo wakati wa kikao chake na Waziri wa Nishati wa Zambia, David Mabumba na Ujumbe wake (hawapo pichani) walipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Na Veronica Simba.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Waziri wa Nishati wa Zambia, David Mabumba, wamekutana na kufanya mazungumzo kuhusu kuboresha Bomba la Mafuta la TAZAMA ili liweze kuwanufaisha wananchi wa Tanzania na Zambia kama ilivyokusudiwa.

Mazungumzo yao yaliyofanyika mapema leo, ofisini kwa Waziri Muhongo jijini Dar es Salaam, ni kufuatia makubaliano ya marais wa nchi husika, Dk John Magufuli na Edgar Lungu; kuhusu kuboresha zaidi Bomba la TAZAMA na Reli ya TAZARA.

Marais Magufuli na Lungu, walifikia makubaliano hayo jana katika mazungumzo rasmi yaliyofanyika Ikulu ya Dar es Salaam ambayo ni mojawapo ya shughuli mbalimbali zilizopangwa katika ratiba ya ziara ya siku Tatu (3) ya Rais Lungu iliyoanza nchini Jumapili, Novemba 21 mwaka huu. 

Waziri Mabumba ambaye alifuatana na Ujumbe wa Viongozi na Maafisa waandamizi kutoka TAZAMA na wizarani kwake; aliafiki mapendekezo yaliyotolewa na Waziri Muhongo kuhusu namna pande hizo mbili zitakavyoshirikiana katika utekelezaji wa agizo la Marais wao ambayo ni pamoja na wataalam wa pande zote kukutana na kufanya majadiliano pamoja na kufanya ziara kukagua utendaji kazi wa Bomba hilo.

Aidha, Mawaziri hao walijadiliana kuhusu namna ambavyo Zambia itanufaika na gesi asilia iliyogunduliwa Kusini mwa Tanzania. 
Kikao hicho pia, kilihudhuriwa na viongozi waandamizi wa Wizara ya Nishati na Madini – Tanzania, akiwamo Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara, Profesa James Mdoe.

BENKI YA CRDB YAKANUSHA TAARIFA ZINAZOENEZWA MITANDAONI

$
0
0

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei akizungumza na vyombo vya habari, wakati akikanusha taarifa zinazoenezwa mitandaoni kuwa Benki hiyo iko mbioni kufunga baadhi ya matawi yake kwa madai kuwa imeyumba kiuchumi. Dkt. Kimei amekanusha taarifa hizo kwa kusema si ukweli na sasa wako kwenye mikakati ya kufungua matawi mengine 11 kabla ya Januari 2017.

KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA AFUNGUA MKUTANO WA KIMATAIFA WA MTANDAO WA KUPAMBANA NA UNYOJI WA KINGONO KWA WATOTO

$
0
0
 Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga akifafanua jambo kwa vyombo vya habari kuhusu Mkutano wa Mtandao wa Kimataifa wa kuzuia unyonyaji na usafirishaji wa watoto kwa lengo la kuwafanyisha ngono unaoendelea leo jijini Dar es Salaam.
 Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga pamoja na baadhi ya Wajumbe wa bodi ya Mtandao wa Kupambana na Usafirishaji na unyonyaji watoto Kingono Duniani wakifuatilia maendeleo ya Mkutano huo leo jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wajumbe wa Mkutano wa Mtandao wa Kupambana na Usafirishaji na unyonyaji watoto Kingono leo jijini Dar es Salaam.


NA ANTHONY ISHENGOMA.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Sihaba Nkinga leo amefungua  mkutano wa mashauriano wa kanda ya Afrika kuhusu Mtandao wa Kuzia Unyonyaji  na Usafirishaji  wa Watoto kwa lengo la kuwafanyisha ngono.

 Akiongea katika Mkutano huo Bi Sihaba Nkinga amesema Tanzania kama mwanachama wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika imeridhia na kutekeleza mikataba mbalimbali ikiwemo kutunga sera na sheria pamoja na  mikakati ya kupambana na ukatili dhidi ya watoto.

Aliendelea kusema mwaka huu Tanzania ni Nchi pekee barani Afrika ambayo imechaguliwa kama nchi ya kuigwa kwenye juhudi za dunia kupambana ukatili wa wanawake na watoto akizataja Nchi nyingine kuwa za Mexico, Indonesia na Sweden.

Katibu Mkuu Sihaba Nkinga amesema kuwa Tanzania imechaguliwa kuwa moja ya Nchi zinazounda ushirikiano wa kimataifa wa kupambana na ukatili wa Wanawake na Watoto kwasababu ilikuwa Nchi ya pili duniani kuitikia wito wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa kutaka Nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wa kufanya tafiti za ukatili dhidi ya  Wanawake na Watoto barani Afrika.  

Akiongea katika Mkutano huo wa mtandao wa kuzuia unyonyaji kingono kwa watoto Afrika Bi. Sihaba Nkinga amesema  taarifa ya utafiti huo ilyofanyika mwaka 2009 na kusambazwa mwaka 2011 ilitoa majibu ya yaliyonesha kuwepo kwa ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika ngazi zote ikiwemo ngazi ya familia, shule na njiani kuelekea shuleni.

Aidha ameviambia vyombo vya Habari vilivyokuwepo katika Mkutano huo kuwa hii ndio sababu kwasasa Tanzania inajipanga kuzindua Mpango Mkakati wa kupambana na kuzuia ukatili dhidi ya wanawake na watoto mapema tarehe 13 mwezi desemba.

Mkurugenzi wa Shirika lisilo la Kiserikali la KIWOEDE Bi. Justa Mwaitaka amesema mtandao huu unakutana kujadili namna bora ya kupeana taarifa za Watoto wanaosafirishwa kwa lengo la kunyonywa kingono ndio maana kuna Nchi 21 kutoka barani Afrika.

Aliongeza kuwa Mkutano huu utaangalia sheria zilizopo kama zinakidhi haja ya kupambana na ukatili dhidi ya watoto akizitaja sheria za Tanzania kuwa na utaratibu unaochelewesha upatikanaji wa haki za watoto pindi inagundulika kuwepo kwa ukatili dhidi ya watoto taratibu za kisheria na kimahakama zinakuwa ngumu katika utekelezajia wake.

MWAKILISHI WA UNUCEF AKUTANA DK.SHEIN

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mwakilishi wa UNICEF katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ms. Maniza S. Zaman alipofika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na ujumbe aliofuatana nao leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Mwakilishi wa UNICEF katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ms. Maniza S.Zaman alipofika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na ujumbe aliofuatana nao leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Mwakilishi wa UNICEF katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ms. Maniza S.Zaman (wa pili kulia) alipofika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na ujumbe aliofuatana nao leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifuatana na Mwakilishi wa UNICEF katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ms. Maniza S.Zaman baada ya mazungumzo yao alipofika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na ujumbe aliofuatana nao leo, [Picha na Ikulu.] 29/11/2016.

Mtanzania afungua mgahawa Sweden

$
0
0
 Mgahawa mkubwa unaotoa huduma za chakula cha Kitanzania unaomilikiwa na mpishi maarufu duniani, Issa Kapande `Chef Issa', umefunguliwa nchini Sweden na kuvunja rekodi ya dunia.Mgahawa huo ulizinduliwa na balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu.

Balozi Msechu alimpongeza Issa Kapande na mkewe kwa kufanikisha kuwapo kwa mgahawa huo ambao umeweka rekodi kuwa mgahawa mkubwa kuliko yote ya Kiafrika katika nchi za Ulaya.

Aidha, alimshukuru Torvald Brahm mwenyeji wa mji huo kwa kumuunga mkono Issa hadi kufanikisha ndoto yake ya kuwa na mgahawa wa kwanza wa Kiafrika katika mji wa Trollhattan utakatoa huduma ya chakula cha kitanzania.

Katika uzinduzi huo ambapo wenyeji wa manispaa hiyo akiwemo Meya na mwenyekiti wa Trollhattan, Paul Akerlund na msaidizi wake Peter Eriksson walikuwepo, balozi ambaye ndio kwanza ameanza kazi alielezea kufurahishwa na juhudi za Kapande.

Alisema Issa ameonesha njia kwamba inawezekana kwa watu waliopo Ughaibuni sio tu kuajiriwa, bali kujiajiri katika nyanja mbalimbali.Alisema hilo linawezekana kutokana na kufuatilia kwa karibu taratibu za wenyeji na kisha kutumia mafunzo yaliyopo kukamilisha ndoto."Ni dhahiri kuwa, Chef Issa kwa kupitia taaluma yake ya upishi amewezeshwa kumiliki mgahawa huu hapa Trollhattan,S weden kwa hilo, napenda tuishangilie na kuipigia makofi Sweden na Trollhattan."Alisema akimpongeza kijana huyo ambaye pia amewekeza mkoani Mtwara.

Katika mahojiano, Mpishi Mkuu Issa Kapande alisema mafanikio yake yanatokana na juhudi kubwa na nia aliyoiweka katika kujifunza na kufundisha wengine katika mitandao ya wapishi wakuu.

Alisema akiwa amefanyakazi katika nchi 17 na tayari akiwa na vitega uchumi nchini alianzia nia ya kuwekeza Sweden mwaka 2009 wakati alipohamia nchini humo akitokea Uswisi. Alisema alianza kwa kuomba vibali, lakini mchakato kamili ulianza mwaka 2013."Tulilazimika kufanya utafiti kidogo" alisema na kuongeza kuwa katika utafiti huo walihoji watu 300 na kujua mwelekeo hasa wa shughuli yao unastahili kuwaje.

Kapande ambaye ni mhitimu wa chuo kikuu cha Manchester Metropolitan na Chuo kikuu cha kimataifa cha menejimenti ya hoteli cha Uswis amesema amepambana vikali na mkewe hadi kufikia hatua ya kuanzisha mgahawa huo ambao upo katika eneo la ukubwa wa skwea mita 810.Kapande ambaye mwaka jana alitwaa tuzo ya dhahabu katika upishi akiwa na timu ya Sweden magharibi alisema kuna umuhimu mkubwa kwa wapishi wa nyumbani kukubali kubadilika na kufanya kazi kwa pamoja kwa lengo la kujifunza na kufunza ili kuwa na aina nyingine ya mapishi katika kuendeleza sekta.Ndani ya mgahawa huo pia watu mbalimbali watapatiwa taarifa za utalii Tanzania.

Katika kazi yake ya upishi, amebahatika kuwapikia watu mashuhuri duniani, baadhi wakiwa Andrew Young, Mchungaji Jesse Jackson, Robert Mugabe (Rais wa Zimbabwe), Paul Kagame (Rais wa Rwanda), Benjamini Mkapa (Rais mstaafu wa Tanzania), Raila Odinga (Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya), Daniel Arap Moi (Rais Mstaafu wa Kenya), Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Bi. Hillary Clinton na mumewe Bill Clinton, Mke wa Rais wa zamani wa Marekani Laura Bush.

Wengine ni Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein, mwigizaji Chris Tucker, Rais wa zamani wa Afrika Kusini hayati Mzee Nelson Mandela, Koffie Olomide, Youssour ndour, Arsene Wenger (Kocha wa Arsenal ya England), Gianluca Vialli (nyota wa zamani wa Italia aliyewahi kuichezea na kuinoa Chelsea ya England), Rais wa Congo DRC, Joseph Kabila, Billy Gates na wengine wengi.

MHE. POSSI: JAMII IWASHIRIKISHE WATU WENYE ULEMAVU KATIKA FURSA ZOTE ZA MAENDELEO

$
0
0
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi  akizungumza na baadhi ya watu wenye ulemavu (hawapo pichani) na watendaji wa Serikali juu ya umuhimu wa kuwashirikisha watu wenye ulemavu katika shughuli za maendelea wakati wa ziara yake Wilayani Peramiho mkoa wa Ruvuma Novemba, 2016.
 Baadhi ya watu wenye ulemavu wakimsikiliza Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao alipotembelea kituo cha kulelea watu wenye mahitaji maalum cha Peramiho Disabled Persons Action(PEDIPA) wakati wa ziara yake Peramiho. 
 Mhazini wa kikundi cha kulelea watu wenye mahitaji maalum cha Peramiho Disabled Persons Action (PEDIPA) Mwl.Elswida Charles akimkabidhi risala ya kikundi hicho kwa  Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi Peramiho Ruvuma.
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi   akimkabidhi Mwenyekiti wa PEDIPA Bw.Pius S.Kayombo Kiti Mwendo ili kumsaidia katika shughuli zake za kila siku.
 Mwenyekiti wa PEDIPA Bw.Pius S.Kayombo akiwa katika zoezi la kutumia kiti mwendo alichokabidhiwa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi alipotembelea kituo hicho Peramiho Ruvuma.
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi  akikabidhi mashine ya kushonea nguo  kwa Mhazini wa kikundi cha kulelea watu wenye mahitaji maalum cha PEDIPA Mwl.Elswida Charles wakati wa ziara yake kituoni hapo Wilayani Peramiho mkoa wa Ruvuma.
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi  akitoa mafuta maalum ya ngozi kwa mmoja wa washiriki wa wajumbe wa kikundi cha PEDIPA wakati wa ziara yake Ruvuma
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi akisalimiana na Bi. Cholastika Haule ambaye ni mlemavu wa viungo mara baada ya kumalizika kwa ziara yake Wilayani Peramiho Mkoa wa Ruvuma. (PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

Na.Mwandishi Wetu
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu, Mhe. Dkt. Abdallah Possi ameiasa jamii kuwashirikisha watu wenye ulemavu katika shughuli zote za maendeleo ili kusaidia kuwainua na kuondokana na dhana ya utegemezi na kuwakwamua kiuchumi.
Dkt.Possi ameyasema hayo wakati wa ziara yake katika Wilaya za Mbinga, Songea Vijijini na Nyasa mkoani Ruvuma ambapo alitembelea Shule zenye kuhudumia watu wenye mahitaji maalum za Songea Boys, Luhira, Huruma na Kituo cha Kulelea wenye ulewavu cha Peramiho Disabled Persons Action (PEDIPA) na Kituo cha kulele wazee na wenye ukoma cha Nge Wilayani Nyasa.
Katika ziara hiyo Mhe.Possi alibaini changamoto nyingi za watu wenye ulemavu na kuishauri jamii namna pekee ya kutatua changamoto wanazokabiliana nazo ni jamii kuona umuhimu wa kuwashirikisha watu hao katika mipango yote ya maendeleo.

“Halmashauri ziandae mipango ya kuwawezesha watu wenye ulemavu kuweza kushiriki kikamilifu katika kujitafutia kipato na hii itasaidia kuondokana na hali ya utegemezi na kuondoa mitazamo hasi juu ya watu wenye ulemavu kuwa hawawezi” .Alisema Mhe.Possi.

Waziri Possi alisisitiza kuwa ni lazima Halmashauri ziwe na ubunifu wa miradi ya maendeleo itakayo walenga watu wenye ulemavu, “Ni vyema sasa kuwe na jitihada za makusudi za kuunda miradi maalum kwa ajili ya kuwapa nafasi za ushiriki ili kujitafutia vipato na kuyakabili mazingira yao, ikumbukwe wakina mama waliachwa nyuma kwa muda mrefu ila baada ya kupaza sauti zao tunaona sasa wanasikika hivyo hivyo iwe kwa watu wenye ulemavu” Alisitiza Dkt.Possi.
Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Nyasa Dkt.Osca Albano alisisitiza kuyapokea maelekezo yote ya Naibu Waziri Mhe.Possi kwa vitendo na kumhakikishia kuwa Wilaya yao itakuwa mstari wa mbele katika kulitekeleza hilo.
 “Sisi tunafanya kazi kwa ushirikiano mzuri na Halmashauri hivyo ni vyema tukalichukua hilo kuangalia namna tunavyoweza kuliweka katika mipango yetu yote ya maendeleo ili kuwasaidia na kufikia lengo la serikali,” alisema Dkt. Albano.
Nae Katibu Tawala Wilaya ya Songea Bw. Edmund Siame aliomba halmashauri zote ziwe zinatoa mrejesho mapema juu ya maagizo yanayotolewa na viongozi wa juu huku Mwalimu Elswida Charles anayehudumia wanafunzi wenye mahitaji maalum akimweleza Dkt. Possi kuwa watu wenye ulemavu wanafarijika kutokana na jitihada anazofanya kuwainua watu wenye ulemavu.

MINISTRY OF WATER AND IRRIGATION, GIZ SIGNED THE IMPLEMENTATION AGREEMENT

$
0
0

Ministry of Water and Irrigation and the German Agency for International Cooperation (GIZ) have signed the Implementation Agreement at the Ministry’s HQ at Ubungo, yesterday.

The agreement outlines the interventions that will be carried out within the framework of Technical Cooperation between the Governments of the United Republic of Tanzania and of the Federal Republic of Germany.

Speaking at the signing ceremony the Ministry of Water and Irrigation’s Permanent Secretary, Eng. Mbogo Futakamba said that, with GIZ’s support, several instruments for policy coordination and implementation have been put in place, including the Water Supply and Sanitation Regulations and the Water Sector Programme Implementation Manual. 

Eng. Futakamba continued by saying, the current 3-year cycle of GIZ’s support to the Water Sector Programme, which runs from March 2016 to February 2019 with a funding envelop of Euro 9.5 million, will concentrate on a number of distinct working areas of Sectoral Framework and Sector Finance, Urban Water Supply and Sanitation, Regulatory Framework and Climate-Sensitive Water Resources Management.

Meanwhile, the GIZ Country Director, Dr. Regine Qualmann said that, it is in the interest of the Government of Germany that, through effective cooperation with Tanzanian Government the implementation of the GIZ supported water sector development programme will achieve its intended objectives and targets, and to do so in a sustainable manner. As we will always support Tanzania and its development as far as our cooperation is concerned.

The cooperation between Tanzania and Germany existed since 1975, and it has been guided by a shared vision of promoting Tanzania’s development in a sustainable manner. Over the years, the focus and priorities have somewhat changed, in order to adapt to changing conditions and priorities on site, but also to take on board changing global initiatives and development agendas.

Yesterdays’ signing ceremony signalled the continuation of the joint commitment of the two Governments, towards accomplishing some of the unfinished global commitments of the (8) Millennium Development Goals (MDGs), which have now been reformulated into (17) measurable Sustainable Development Goals (SDGs), under the Global Agenda for 2030. 
 The Ministry of Water and Irrigation’s Permanent Secretary, Eng. Mbogo Futakamba together with the Counsellor- Head of Cooperation at the Embassy of  Federal Republic of Germany in Tanzania, Julia Hannig (at the left) and the GIZ Country Director, Dr. Regine Qualmann.
 The invitees listening to the presentantion.
 The Ministry of Water and Irrigation’s Permanent Secretary, Eng. Mbogo Futakamba together with the GIZ Country Director, Dr. Regine Qualmann signing the agreement.
 The Ministry of Water and Irrigation’s Permanent Secretary, Eng. Mbogo Futakamba together with the GIZ Country Director, Dr. Regine Qualmann exchanging the agreement documents.
The Ministry of Water and Irrigation’s Permanent Secretary, Eng. Mbogo Futakamba together with the GIZ Country Director, Dr. Regine Qualmann in a group photo with ministry’s, GIZ’s and EWURA’s representatives.

DC WILAYA YA TUNDURU AELEZA MAFANIKIO YA MPANGO WA KUTOKOMEZA MIMBA MASHULENI KATIKA WILAYA YAKE SEHEMU YA PILI.

$
0
0

MKUU wa wilaya ya Tunduru JUMA HOMELA  aelezea mpango wa mahakama ya kutembea aliyoianzisha katika wilaya yake ya TUNDURU jinsi ulivyoleta mafanikio , katika kupunuza utoro mashuleni na mimba mashuleni.
Attachments area Preview YouTube video RUVUMA TV@ SEHEMU YA PILI TUNDURU yafanikiwa kupunguza mimba kwa wanafunzi RUVUMA TV@ SEHEMU YA PILI TUNDURU yafanikiwa kupunguza mimba kwa wanafunzi

RAIS LUNGU WA ZAMBIA AONDOKA NCHINI

$
0
0
Rais John Magufuli akiagana na Rais wa Zambia, Edgar Chagwa Lungu kwenye uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere wakati mgeni huyo alipoondoka nchini kurejea nyumbani Novemba 29, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
  Rais John Magufuli akiwapungia wananchi waliojitokeza kumuaga Rais wa Zambia, Edgar Chagwa Lungu kwenye uwanja wa ndege wa Julius Nyerere wakati alipoondoka nchini kurejea nchini Novemba 29, 2016. Wengine pichani ni Makamu wa Rais, Samia Suluhu na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Inspekta Jenerali wa Polisi, Ernest Mangu kwenye uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Novemba 29, 2016. Wapili kulia ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange na watatu kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi John Kijazi.
 Rais John Magufuli akiongozana na  mgeni wake, Rais Edgar Chagwa Lungu wakati mgeni huyo alipoondoka nchini kurejea nyumbani kwenye uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Novemba 29, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
  Rais John Magufuli na Makamu wa Rais, Samia Suluhu wakishuudia wakati Rais wa Zambia Edgar Chagwa Lungu akiagana na Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa kwenye uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere kabla ya kuondoka nchini kurejea nyumbani Novemba 29, 2016.

"PEDESHEEE NDAMA MTOTO WA NG'OMBE" APANDISHWA KIZIMBANI AKIKABILIWA NA MASHTAKA SITA IKIWEMO KUGHUSHI NA KUTAKATISHA DOLA 540,390.

$
0
0
Mfanyabaishara Ndama Hussein maarufu kama mtoto wa Ng’ombe amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, akikabiliwa na mashtaka sita ikiwamo kughushi na kutakatisha Dola za Kimarekani 540,390 (sawa na Sh, bilioni 1.181). Mshtakiwa huyo alisomewa mashtaka yake mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa.

Upande wa Jamhuri uliongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Christopher Msigwa akisaidiana na Wakili wa Serikali Leonard Challo.

Msigwa alidai kuwa Februari 20, mwaka 2014, jijini Dar es Salaam, mshtakiwa akiwa na lengo la kudanganya alighushi nyaraka za kusafirisha madini akionyesha kwamba Kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment Limited imepewa kibali cha kusafirisha boksi nne za vipande wa dhahabu zenye uzito wa kilo 207 zenye thamani ya Dola za Kimarekani 8.2 kwa Kampuni yenye makazi yake nchini Austaria inajulikana kama Trade TJL DTYL Limited huku akijua nyaraka hizo za uongo.

Katika shtaka la pili, Machi 6, mwaka 2014, jijini Dar es Salaam akiwa na nia ya kudanganya, aliandaa nyaraka za uongo kuonyesha kwamba hati ya kuondolea mizigo kutoka ofisi za Umoja wa Mataifa za tarehe hiyo, akiwa na lengo la kuonyesha kwamba vipande vya dhahabu vyenye uzito wa kilo 207 kutoka Jamhuri ya Congo, kuwa zinasafirishwa na Kampuni ya  Muru Platnum kwenda Austraria.

Msigwa alidai katika shtaka la tatu, Februari 20, mwaka 2014 jijini Dar es Salaam, akiwa na nia ya kudanganya alighushi nyaraka zikionyesha kuwa ni fomu ya tamko la kodi akionyesha Kampuni ya Muru Platnum imelipa Dola za Kimarekani 331,200 kama kodi ya kuingiza mzigo kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ya kilo 207 ya vipande vya dhahabu vyenye thamani ya Dola za Kimarekani 8,280,000 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo huku akijua ni uongo.

Katika shtaka nne, Februari 20, mwaka 2014 jijini Dar es Salaam, mshtakiwa akiwa na nia ya kudanganya alitengeneza nyaraka zauongo za kuonyesha kuwa ni za bima kutoka Kampuni ya Phoenix  Ltd za terehe hiyo, akilenga kuonyesha kwamba Kampuni ya Muru Platnum imekatia bima boksi nne za vipande vya dhahabu zenye uzito wa kilo 207 vyenye thamani ya Dola za Kimarekani 8,280,000 huku akijua ni uongo.

Katika shtaka la tano na sita, kati ya Februari 26 na Machi 3, mwaka 2014 jijini Dar es Salaam, alijipatia kwa njia ya uongo na kutakatisha Dola za Kimarekani, 540,390 (sawa na Sh. Bilioni 1.181) kutoka Kampuni ya Trade TJL DTYL Limited kwa madai kuwa angesambaza na kusafirisha nje ya nchi kilo 207 za vipande vya dhahabu vyenye thamani ya Dola za Kimarekani 8,280,000 lakini hakufanya hivyo.

Ilidaiwa kuwa mshtakiwa alitakatisha fedha hizo zilizopatikana kwa njia ya jinai kwa kuelekeza kiasi hicho cha fedha kuingizwa katika akaunti iliyopo benki ya Stanbic yenye jina la Kampuni ya Muru Platnum na baadaye alizitoa zote na kuzitumia kwa matumizi yake binafsi huku akijua zimepatikana kwa njia ya udanganyifu.

Upande wa Jamhuri ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na uliomba mahakama tarehe nyingine ya kutajwa.

Hakimu Nongwa alisema kesi hiyo itatajwa Desemba 13, mwaka huu.

Mshtakiwa alirudhishwa mahabusu kwa sababu mashtaka ya kutakatisha fedha hayana dhamana kwa mujibu wa sheria.

BALOZI WA KUWEIT NCHINI TANZANIA JASEM ALNAJIM ATEMBELEA HOSPITALI KUU YA MNAZI MMOJA MJINI ZANZIBAR

$
0
0
 Balozi wa Kuweit nchini Tanzania Jasem Alnajim akimkabidhi Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Juma Malik  Akili msaada wa moja ya  mashine  tatu za kupimia Presha alipotembelea Hospitali Kuu ya Mnazi mmoja mjini Zanzibar.
  Balozi wa Kuweit nchini Tanzania Jasem Alnajim akiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Juma Malik Akili wakiwapa zawadi akinamama waliojifungua katika wodi ya wazazi ya Hospitali kuu ya Mnazi mmoja.
 Balozi wa Kuweit nchini Tanzania Jasem Alnajim akimbeba mtoto mchanga alipotembelea wodi ya wazazi ya hospitali  kuu ya Mnazi mmoja Mjini Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali kuu ya Mnazi mmoja Dkt. Ali Salum Ali akimuongoza Balozi wa Kuweit nchini Tanzania Jasem Alnajim alipotembelea majengo mapya ya Hospitali hiyo yaliyofunguliwa hivi karibuni.Picha na Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar.

ASILIMIA 40 YA WATANZANIA WAWE KWENYE UCHUMI WA VIWANDA KUFIKIA 2020

$
0
0
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Bw. Charles Mwijage akiongea na wadau mbalimbali wa biashara kuhusu umuhimu wa kulipa kodi na kutumia msimbomilia(barcode) hawapo pichani wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa nne wa Taasisi isiyo ya kiserikali inayotoa msimbomilia (Barcode) za bidhaa (GS1) uliofanyika jijini dar es salaam.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Bw. Charles Mwijage wa pili kulia akikata keki kuadhimisha mwaka wa nne wa Taasisi isiyo ya kiserikali inayotoa msimbomilia (Barcode) za bidhaa (GS1) uliofanyika jijini dar es salaam wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa bodi ya GS1 Bw. Gideon Mazara.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Bw. Charles Mwijage kulia akimpa mkono wa pongezi Afisa Mkuu wa elimu kwa mlipa kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) kwa kudhamini mkutano wa mwaka wa nne wa Taasisi isiyo ya kiserikali inayotoa msimbomilia (Barcode) za bidhaa (GS1) uliofanyika jijini Dar es salaam.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Bw. Charles Mwijage kushoto akipokea zawadi kutoka kwa mwakilishi wa kampuni ya Shea illushion kulia wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa nne wa Taasisi isiyo ya kiserikali inayotoa msimbomilia (Barcode) za bidhaa (GS1) uliofanyika jijini dar es salaam. Na Mpiga picha Wetu . Dar es salaam.


 WATANZANIA takribani asilimia 40 wanatakiwa wawe wamejiingiza kwenye uchumi wa viwanda mpaka kufikia 2020 ili kuweza kusaidia kukuza ajira za vijana na kuifanya Tanzania kuwa kwenye uchumi wa kati kwa maendeleo ya jamii na nchi kwa ujumla. 

 Akizungumza hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa nne wa Taasisi isiyo ya kiserikali inayotoa msimbomilia (Barcode) za bidhaa (GS1) Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Bw. Charles Mwijage amesema kuwa Serikali imeazimia kufikisha asilimia 40 ya watanzania kufanya shughuli za uchumi wa viwanda kufikia 2020.

 “Tunataka mpaka kufikia 2020 watanzania takribani asilimia 40 wawe wamejikita kwenye uchumi wa viwanda ili kusaidia kukuza ajira kwa vijana na kuifanya Tanzania kuwa kwenye uchumi wa kati kwa maendeleo ya jamii nan chi yetu kwa ujumla” alisema Waziri Mwijage.

 Aidha Waziri Mwijage amesema kuwa Uchumi wa viwanda unatakiwa kukua nchini kuwezesha kuzalisha bidhaa bora zitakazouzwa ndani na nje ya nchi ili kukusanya kodi kwa ajili ya kupata huduma bora za kijamii kwa maendeleo ya wananchi wa Tanzania . 

 Kwa upande wa Afisa Mkuu wa elimu kwa mlipa kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) ambao ni wadhamini wa mkutano huo Bi. Rose Mahendeka alisema kuwa wafanya biashara wote ambao wanahitaji kutumia mfumo wa kuuza bidhaa kwa kuweka msimbomilia(Barcode) wanapaswa kupitia TRA kwa ajili ya usajili na uhakiki wa namba ya utambulisho ya mlipa kodi(TIN) kabla ya kwenda kupata huduma ya msimbomilia.

 “Wafanya biashara wote ambao wanahitaji kutumia mfumo wa kuuza bidhaa kwa kuweka msimbomilia(Barcode) wanapaswa kupitia TRA kwa ajili ya usajili na uhakiki wa namba ya utambulisho ya mlipa kodi(TIN) kabla ya kwenda kupata huduma” alisisitiza Bi. Mahendeka. Aidha Bi. 
Mahendeka alisema kuwa wafanya biashara ambao wanahitaji kuuza bidhaa zao kwa kutumia msimbomilia wanapasa kulipa kodi bila ya kukwepa ili kuwezesha Tanzania kupiga hatua kufikia uchumi wa viwanda ili kupata huduma bora kwa maendeleo ya jamii.

 Naye Mwenyekiti wa bodi ya GS1 Bw. Gideon Mazara amesema kuwa wafanyabiashara wanatakiwa kutumia msimbomilia wa Tanzania ili kuweza kutangaza bidhaa za nchini ili kuweza kupata soko la kimataifa na kufikia uchumi wa kati . 

 “Ni lazima kutumia msimbomilia wa Tanzania kwa kila mfanyabiashara na mjasiriamali ili kuweza kutangaza bidhaa za nchini ili kuweza kupata soko la kimataifa na kufikia uchumi wa kati kupitia viwanda vikubwa na vidogo” alisema Bw. Mazara.

Watanzania Washauriwa Kutumia Nishati Mbadala.

$
0
0
Na Lilian Lundo

Serikali itaendelea kuzuia matumizi ya mkaa na kuni ili kuendelea kutunza mazingira na kuhifadhi uoto wa asili wa nchi yetu. 

Hayo yamesemwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe alipokuwa akisoma hotuba kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa leo Jijini Dar es Salaam katika warsha ya wadau kujadili namna na njia bora ya kupunguza matumizi ya mkaa kwa usimamizi endelevu wa mazingira nchini. 

Prof. Maghembe amesema kuwa Serikali itaendelea kurekebisha sheria ya gharama ya uzalishaji wa mkaa, ili nishati hiyo iwe na gharama ya juu na kuwafanya watanzania wahamie kwenye nishati nyingine kama vile gesi ambayo gharama yake ni rahisi. 

“Uchomaji wa mkaa unaharibu mazingira kwa kiwango kikubwa, ambapo miti inapokatwa joto huongezeka, kipindi hiki mvua za vuli zilitakiwa kuwa zinanyesha lakini mvua hizo hazinyeshi kutokana na ukataji miti uliokithili,” alifafanua Prof. Maghembe. 

Aliendelea kwa kusema kuwa ukataji wa miti umesababisha wanyamapori kuhama maeneo yao ya asili kwa ajili ya kutafuta maji na chakula.
Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba amesema kuwa nishati ya mkaa inaonekana kama nishati ambayo gharama yakeiko chini ukilinganisha na nishaati nyingine. Lakini mtu wa kipato ch chini anaweza kutumia mpaka shilingi 4,000 kwa siku kwa kununua mkaa gharama ambayo ni kubwa ukilinganisha na gharama za gesi. 

Nae Mkurugenzi wa kampuni ya ORXY -Tanzania Nick McAleer amesema kwamba watumiaji wa gesi wanaongezeka kila siku na mpaka sasa kampuni hiyo ina mawakala wapatao 1,000 wanaouza nishati hiyo. 

Mkurugenzi huyo ameeleza kuwa nishati ya gesi gharama yake ni nafuu ukilinganisha na mkaa, vilevile utumiaji wa gesi unahifadhi mazingira na kuwaepushia watanzania magonjwa ya mapafu na kansa ambayo yanasababishwa na moshi wa mkaa na kuni. 

Aidha ameiomba Serikali kuondoa baadhi ya kodi hasa kwa mawakala ambao wanataka kuuza gesi kwani kwa kufanya hivyo kutaongeza idadi ya wauzaji na upatikanaji wa gesi kuwa ni wa rahisi nchi nzima.

TAARIFA RASMI KUTOKA KIWANDA CHA SARUJI CHA DANGOTE

MADAKTARI NCHINI WAMETAKIWA KUITISHA MIKUTANO YA KIJAMII ILI KUJADILI MAGONJWA

$
0
0
Katibu Mtendaji wa Chama cha Afya ya Jamii Tanzania (TPHA), Fabian Magoma  (kulia), akizungumza katika Kongamano la 33 la siku tano la Chama cha Afya ya Jamii Tanzania (TPHA) linaloendelea Hoteli ya Kebby Mwenge jijini Dar es Salaam leo asubuhi. Kushoto ni  Mwenyekiti wa TPHA anayemaliza muda wake, Daktari Bingwa  Elihuruma Nangawe.
Dk. Manase Frank akitoa mada kwenye kongamano hilo.
 Profesa Andrew Swai akitoa mada.
 Wadau wa sekta ya afya wakifuatilia kwa karibu mada zilizokuwa zikitolewa katika kongamano hilo.
 Kongamano likiendelea.
 Dk. Andronicus Aloyce Rwelamila kutoka Hospitali ya Tumbi Kibaha (kushoto) na Muuguzi wa Hospitali hiyo, Mary Gowele wakiwa kwenye kongamano hilo.
 Kongamano likiendelea

Usikivu katika kongamano hilo. Kushoto ni Mwenyekiti wa TPHA, Dk. Elihuruma Nangawe

 Profesa Japhet Kileo (kulia), akiuliza maswali kwenye 
kongamano hilo.
 Dk. Mwanahamisi Magwangwara (kushoto), akizungumza wakati akijibu maswali mbalimbali kutoka kwa wadau wa sekta ya afya katika kongamano la 33 la siku tano la Chama cha Afya ya Jamii Tanzania (TPHA) linaloendelea Hoteli ya Kebby Mwenge jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni mtoa mada, Profesa Andrew Swai. 
Dk.Chilolo Edward (katikati), akijibu maswali kuhusu changamoto ya waendesha bodaboda. Kushoto ni Profesa Andrew Swai na Dk. Manase Frank. 
Mkurugenzi wa Shirika la Wanawake katika Jitihada za Maendeleo (WAJIKI), Janeth Mawinza akielezea changamoto ya matumizi ya pombe katika Manispaa ya Kinondoni.

Na Dotto Mwaibale

MADAKTARI nchini wametakiwa kufanya mikutano ya kijamii au wananchi ili kuwapa fursa ya kujua magonjwa yanayo wakabili.

Hayo yalielezwa na Dk. Manase Frank wakati akitoa mada katika kongamano la 33 la siku tano la Chama cha Afya ya Jamii Tanzania (TPHA) linaloendelea Hoteli ya Kebby Mwenge jijini Dar es Salaam leo asubuhi.

"Changamoto kubwa tuliyonayo ni wananchi wengi kutojua magonjwa yanayowasumbua hivyo ni muhimu kwa madakatari kuitisha mikutano itakayowakutanisha na wananchi ili kuondoa changamoto hiyo" alisema Dk. Frank.

Alisema wagonjwa wengi wamekuwa wakikata tamaa kwa kuchangiwa na kauli za baadhi ya madaktari ambao wanashindwa kujua tatizo la mgonjwa husika hivyo wakati umefika wa madaktari kushirikiana kwa karibu na jamii, viongozi wa dini  ili kuondoa changamoto hiyo.

Akitolea mfano wa kijana mmoja ambaye alifiwa na ndugu zake wote wa karibu kutokana na ugonjwa wa ukimwi na kuishi kwa kunyanyapaliwa lakini baadaye afya yake ilikuja kuimarika kufuatia ushauri uliotolewa na daktari kwa  jamii iliyokuwa ikimzunguka wakati wa ugonjwa wake.

Mtoa mada mwingine Profesa Andrew Swai aliomba serikali wakati wa siku ya Jumamosi na Jumapili kufunga baadhi ya barabara ili zitumike kwa wananchi kufanya mazoezi ya kutembea ili kujenga afya za miili yako na kuepukana na magonjwa kama kisukari.

Akizungumzia changamoto ya matumizi ya bodaboda Dk.Chilolo Edward alisema kwa mwaka jana katika Hospitali za mikoa ya  Morogoro, Tumbi Pwani na Shinyanga kulikuwa na ajali 895 huku majeruhi wakiwa 4813.

Alisema majeruhi waliolazwa katika hospitali hizo walikuwa ni 4525, waliopewa rufaa kwenda hospitali za Bugando na Muhimbili walikuwa 71 na waliolazwa ni 702.

Alisema vifo vilikuwa 81 hivyo vilitokea baada ya kufikishwa Hospitalini ni 70 na vilivyotokea eneo la ajali vilikuwa 11.

Dk.Chilolo alisema ili kupunguza changamoto hiyo inapaswa watoa huduma za afya kutoa elimu kwa waendesha boda boda pale wanapofikishwa mahospitali kuhusu umuhimu wao katika familia na taifa kwa ujumla hivyo kuwa makini wanapoendesha vyombo hivyo vya moto badala ya kuacha kazi hiyo kufanywa na polisi au Sumatra.

NASSOR IDRISSA MWENYEKITI MPYA AZAM FC

$
0
0
ALIYEKUWA Makamu Mwenyekiti wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Nassor Idrissa (wa pili kutoka kulia kwenye picha), ameteuliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa timu hiyo akirithi mikoba ya Alhaji Said Mohamed Abeid, aliyefariki dunia mwanzoni mwa mwezi huu.

US charge d' Affaires visit to Tanzania Youth Alliance TAYOA

$
0
0
  US charge d’ Affaires, Virginia Blaser in a jovial mood after she launched 117 National Health Hotline run by Tanzania Youth Alliance Tayoa when she  visited the offices yesterday at her back is Center for Disease Control (CDC), Director Dr David. Left is Tayoa Director Peter Masika and ambassador  Charles Sanga who is Tayoa board Chairman.
  US charge d’ Affaires, Virginia Blaser lead a discussion on effects of violence and power imbalance in relationship when she visited Tanzania Youth Alliance (Tayoa) offices at Bahari Beach yesterday in Dar es Salaam where she also launched  117 National Health Hotline. Left is Center for Disease Control (CDC), Director Dr David Lowrance. Right is Tayoa Director Peter Masika and Jackline Kiwele from Tayoa.
 US charge d’ Affaires, Virginia Blaser  (Center) listen to the Tanzania Youth Alliance (Tayoa) Director Peter Masika about the organization activities when Virginia and her delegation visited Tayoa offices in Dar es Salaam yesterday where she launched 117 National Health Hotline and lead a discussion on effects of violence and power imbalance in relationship. Left is Center for Disease Control (CDC), Director Dr David Lowrance and Jackline Kiwele of Tayoa.

NAIBU WAZIRI DR. KOLIMBA ATEMBELEA UBALOZI NAIROBI

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba, ambaye yuko Nairobi kuhudhuria kikao cha Bunge la Afrika Mashariki, ametumia fursa hiyo kutembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Kenya na kuzungumza na watumishi.Katika kikao na Mhe. Waziri, watumishi wa Ubalozi walielezea changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo katika utendaji wa kazi, ikiwa ni pamoja na ufinyu wa bajeti. 

Hata hivyo watumishi hao walisema wameweza kukusanya maduhuli ya kuridhisha na kuhudumia Watanzania wanaopatwa na matatizo kwa kuchangishana wakati mwingine.Mhe. Kolimba alieleza kuridhishwa kwake na utendaji wa watumishi wa Ubalozi wa Nairobi na kuwapongeza kwa moyo wa kujitolea. 

Alisema Serikali itajitahidi kupatia balozi fedha na vifaa vya kazi kwa kadri ya uwezo wake, lakini akasisitiza watumishi wawe wabunifu na wajitolee kufidia pale upungufu unapojitokeza.Kikao cha Bunge la Afrika Mashariki kinachofanyika kwenye Bunge la Kenya kinatarajiwa kumalizika kesho.
 Naibu Waziri, Dkt. Kolimba (kushoto) akifurahia bidhaa za Tanzania kwenye ofisi za Ubalozi wa Nairobi akiwa na Kaimu Balozi, Bi. Talha Mohamed Waziri.
 Mhe. Kolimba akisalimiana na baadhi ya watumishi wa Ubalozi.
 Naibu Waziri akiongea na watumishi wa Ubalozi. Kushoto ni Kaimu Balozi, Bi. Waziri na Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. James Lugaganya.
Baadhi ya watumishi wa Ubalozi wakijipanga kumpokea Mhe. Naibu Waziri

Viewing all 46343 articles
Browse latest View live




Latest Images