Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live

JAMII YATAKIWA KUWAHESHIMU NA KUWASAIDIA WAZEE NCHINI

$
0
0
Mratibu wa Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya METDO Tanzania  Mathias Canal akimkabidhi Kaimu Mkuu wa Kituo cha Wazee KIILIMA Bi Gladness Lwiza baadhi ya mahitaji kwa ajili ya wazee waishio kituoni hapo.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Asasi isiyokuwa ya Kiserikali ya METDO Tanzania (Mining and Environmental Transformation for Development  Organization) Bw Ashraf Omary akimsikiliza kwa makini mzee aliyelala kutokana na homa kali inayomsumbua
Kushoto ni Dkt Peter Shija Mganga Mfawidhi kutoka zahanati ya Ibosa akisisitiza jambo kwa Afisa ustawi wa Jamii Wilaya ya Nyamagana ambaye pia ni katibu wa TAWSO Mwanza Bi Abigali Mhingo
 Meneja Mradi wa METDO Tanzania Bw Hussein Sungura akisaini kitabu cha wageni kwa niaba ya uongozi wa METDO Tanzania katika kituo cha Wazee KIILIMA Manispaa ya Bukoba, Mkoani Kagera
 Hiki ndicho Choo kinachotumiwa na wazee waishio kambi ya KIILIMA-Bukoba
Moja ya Mzee katika Kituo cha Wazee KIILIMA akiwa amelala kutokana na homa kali iliyokuwa inamsumbua
 Mahitaji yamepokelewa kwa furaha na wazee wote kupitia uongozi wao
Pichani katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Salum Kijuu, Kushoto kwake ni Mathias Canal Mratibu wa Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya METDO Tanzania, Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Kagera Ndg Charles  Mafimbo, Kulia kwa Mkuu wa Mkoa ni Hussein Sungura Meneja Mradi METDO Tanzania na Mkurugenzi wa METDO Tanzania Ndg Ashrafu Omary
Mkurugenzi wa Asasi isiyokuwa ya Kiserikali ya METDO Tanzania (Mining and Environmental Transformation for Development  Organization) Bw Ashraf Omary akifanya usafi katika jiko la watumishi wa kituo cha wazee KIILIMA
 Mjadala ukiendelea baada ya kazi kumalizika Kijijini KIILIMA kambi ya wazee
Kaimu Mkuu wa Kituo cha Wazee KIILIMA Bi Gladness Lwiza akipanda mti kwa ajili ya kumbukumbu
Tafakuri pana kwa Mzee Wilson Ziraimanikabla ya kukabidhiwa mahitaji na uongozi wa METDO Tanzania
 Nyumba ya kulala wazee wa kituo cha KIILIMA kilichopo Kata ya Nyakato Mkoani Kagera
 Viongozi wkibadilishana mawazo mara baada ya kuzuru kituo cha Wazee KIILIMA
Kijana ni mzee ajaye na Mzee ni kijana aliyekuwa
Hili ndilo jiko linalotumiwa na viongozi wa kituo cha KIILIMA kilichopo nje kidogo ya Manispaa ya Bukoba
Katikati ni Dkt Peter Shija Mganga Mfawidhi kutoka zahanati ya Ibosa akipata maelezo ya awali kwa Moja ya mzee aishie kambini KIILIMA kabla ya kumfanyia vipimo
Mathias Canal Mratibu wa Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya METDO Tanzania akipanda mti wa matunda aina ya Mlimao kwa ajili ya kumbukumbu ya kuzuru kituo cha Wazee KIILIMA
 Majadiliano ya namna ya kuchimba mashimo kabla kupanda miti
 Moja ya nyumba anayoishi Mtumishi wa Kituo cha wazee KIILIMA Kilichopo Mkoani Kagera
Mkurugenzi wa METDO Tanzania Bw Ashraf Omary mwenye Jembe akimsaidia kazi Mzee Wilson Ziraimani, Mzee huyu alikuwa anafanya kazi za kilimo katika mashamba mbalimbali nchini, yeye ni mkazi wa Ngara na wakati akiwa mtoto alikuwa analelewa na Mama wa kambo.
Aliwasili katika kituo cha kulelea Wazee cha KIILIMA Mwaka 1986 hapo alipo anatambaa kwani alivunjika kiuno enzi za ujana wake baada ya kuanguka mtini wakati alipokuwa anakata kuni kwa ajili kupikia.
Viongozi wa METDO Tanzania, Kiongozi wa TASWO, na Viongozi wa kituo cha Wazee KIILIMA wakipanda mti wa matunda aina ya Parachichi kwa ajili ya kumbukumbu na kampeni ya upandaji miti

Na Mathias Canal, Bukoba

Kukosekana kwa huduma bora na msingi kwa wazee nchini imetajwa kuwa changamoto kubwa kwa Wazee waishio katika kambi mbalimbali za serikali na zile za binafsi.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Asasi isiyokuwa ya Kiserikali ya METDO Tanzania (Mining and Environmental Transformation for Development  Organization) Bw Ashraf Omary wakati akikabidhi mahitaji kwa wazee wa kituo cha KIILIMA kilichopo Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera.

Bw Omary alisema kuwa Asasi hiyo yenye usajili No. ooNGO/08317 inajishughulisha na kutoa Elimu ya Mazingira kwa wananchi wanozunguka migodi pamoja na wafanyakazi wa migodini ambapo pia imejikita kuwasaidia wazee waishio katika kambi mbalimbali nchini katika huduma za kuwapatia mahitaji ya msingi ya kila siku kama vile (Chakula, na Mavazi) sambamba na kutoa huduma ya upimaji wa afya zao kupitia wataalamu wa tiba na kuwapatia dawa kwa ajili ya matibabu ya magonjwa mbalimbali.

Alisema kuwa kumekuwa na wimbi kubwa la wazee kutopatiwa huduma bora ikiwemo chakula na matibabu jambo ambalo kwa kiasi kikubwa linachangia wazee wengi kufariki pasina huduma yoyote ya kitabibu sambamba na kukosa Lishe Bora.

Bw Omary ameushukuru uongozi wa kampuni ya ZONGII PUMBLING LTD ya Jijini Mwanza kwa kushirikiana na METDO Tanzania kufanikisha kupatikana mahitaji mbalimbali kwa ajili ya wazee wa kambi ya KIILIMA sambamba na kuupongeza uongozi wa Mkoa wa Kagera kwa ushirikiano ulioonyesha ikiwa ni pamoja na kuruhusu madaktari kwa ajili ya kwenda kuwapima afya wazee hao.

Kwa upande wake Meneja Mradi wa METDO Tanzania Bw Hussein Sungura amebainisha kadhia zinazowakumba wazee katika kituo cha KIILIMA sambamba na vituo vingine nchini kuwa ni pamoja na ukosefu wa huduma za usafiri ili kurahisisha wazee kufikishwa haraka hospitalini pindi wauguapo, Ufinyu wa Bajeti, Ukosefu wa vitendea kazi kama vile vifaa vya usafi na ucheleweshaji wa Ruzuku ya serikali.

Sungura alisema kuwa Mpaka sasa Asasi hii ya METDO Tanzania imesaidia katika maeneo mbalimbali ikiwemo tukio la Agosti 13, 2016 la kumuenzi Mwl Julius Kambarage Nyerere katika Makao ya wazee wasiojiweza BUKUMBI Mwanza, Tukio la Octoba Mosi 2016 SIKU YA WAZEE DUNIANI katika wilaya ya Shinyanga ambapo jamii ilishirikishwa kutambua changamoto zilizopo katika kituo cha Wakoma na Wazee wasiojiweza cha KOLANDOTO pamoja na Kituo cha Wakoma na  Wazee wasiojiweza cha NYABANGE BUTIAMA  na kuwa sehemu ya kuzitatua changamoto hizo.

Kutokana na kazi hiyo ya wito inayofanywa na METDO Tanzania Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Salim Kijuu ametoa wito kwa Asasi hiyo kuwekeza Mkoani Kagera katika sekta mbalimbali ikiwemo kilimo ili ushirikiano wa kusaidia wazee uweze kukomaa na kusaidia wazee wote nchini kirahisi sambamba na kutoa fursa kwa vijana kutambua umuhimu wa kufanya kazi sawia na kujiajiri.

Kijuu alisema kuwa kutokana na Mkoa wa Kagera kuwa na hali nzuri ya hewa na udongo wake kuwa na rutuba ni vyema Asasi ya METDO Tanzania ikafanya kazi yake kwa misingi ya katiba lakini pia inapaswa kuwasaidia vijana wengi nchini ili kuachana na uvivu walionao badala yake kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli katika kuisimamia na kutekeleza kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu.

Akisoma taarifa ya kituo hicho Kaimu Mkuu wa Kituo cha Wazee KIILIMA Bi Gladness Lwiza alisema kuwa Kituo hicho kina jumla ya wahudumiwa 24 ambapo kati yao kuna watoto 6 waliokuwa kwenye mazingira hatarishi baada ya kutelekezwa na wazazi wao huku wengine wakipokelewa baada ya wazazi wao kufariki kutokana na janga la UKIMWI lililotokea mwaka 1984.

Hata hivyo amewaomba wadau mbalimbali kujitokeza na kuwachukua watoto hao kwani kuendelea kubaki katika kituo hicho sio jambo jema kwao kwani wanachanganyikana na wazee ambao wengi wao wana matatizo ya akili.

Lwiza amesema kuwa kufuatia uharibifu wa majengo kutokana na Tetemeko lililotokea hivi karibuni Mkoani Kagera na kuharibu majengo mengi kituoni hapo imesababisha kukosekana kwa nyumba za watumishi, na choo kwa ajili ya matumizi ya wazee pamoja na watumishi wa kituo hicho.

Naye Dkt Peter Shija Mganga Mfawidhi kutoka zahanati ya Ibosa ameiomba serikali kusaidia upatikanaji wa sehemu maalumu ya kuhifadhia dawa, kutolewa mafunzo ya tiba kwa wahudumu waliopo kituoni hapo sambamba na kupatikana kwa vifaa tiba kwa ajili ya kupima damu, Sukari, MRTD, Presha na wingi wa damu.

Kituo cha Wazee KIILIMA kilichopo Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera kilicho chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ni moja kati ya vituo vya kulelea wazee hapa nchini ambapo awali kilikuwa chini ya kanisa la Roman Catholic na baadaye kilikabidhiwa rasmi kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mnamo mwaka 1974.

Baada ya kutembelea vituo vyote vya Wazee kanda ya Ziwa METDO Tanzania inataraji kuzuru Mikoa ya Kanda ya kati kwa ajili ya kujionea changamoto za wazee mbalimbali waishio kambini na kuzifikisha sehemu husika wakiwemo viongozi wa dini, Wafanyabiashara, Serikali na Wadau mbalimbali nchini.

JAMII YATAKIWA KUWAHESHIMU NA KUWASAIDIA WAZEE NCHINI

$
0
0
Mratibu wa Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya METDO Tanzania  Mathias Canal akimkabidhi Kaimu Mkuu wa Kituo cha Wazee KIILIMA Bi Gladness Lwiza baadhi ya mahitaji kwa ajili ya wazee waishio kituoni hapo.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Asasi isiyokuwa ya Kiserikali ya METDO Tanzania (Mining and Environmental Transformation for Development  Organization) Bw Ashraf Omary akimsikiliza kwa makini mzee aliyelala kutokana na homa kali inayomsumbua
Kushoto ni Dkt Peter Shija Mganga Mfawidhi kutoka zahanati ya Ibosa akisisitiza jambo kwa Afisa ustawi wa Jamii Wilaya ya Nyamagana ambaye pia ni katibu wa TAWSO Mwanza Bi Abigali Mhingo
 Meneja Mradi wa METDO Tanzania Bw Hussein Sungura akisaini kitabu cha wageni kwa niaba ya uongozi wa METDO Tanzania katika kituo cha Wazee KIILIMA Manispaa ya Bukoba, Mkoani Kagera
 Hiki ndicho Choo kinachotumiwa na wazee waishio kambi ya KIILIMA-Bukoba
Moja ya Mzee katika Kituo cha Wazee KIILIMA akiwa amelala kutokana na homa kali iliyokuwa inamsumbua
 Mahitaji yamepokelewa kwa furaha na wazee wote kupitia uongozi wao
Pichani katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Salum Kijuu, Kushoto kwake ni Mathias Canal Mratibu wa Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya METDO Tanzania, Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Kagera Ndg Charles  Mafimbo, Kulia kwa Mkuu wa Mkoa ni Hussein Sungura Meneja Mradi METDO Tanzania na Mkurugenzi wa METDO Tanzania Ndg Ashrafu Omary
Mkurugenzi wa Asasi isiyokuwa ya Kiserikali ya METDO Tanzania (Mining and Environmental Transformation for Development  Organization) Bw Ashraf Omary akifanya usafi katika jiko la watumishi wa kituo cha wazee KIILIMA
 Mjadala ukiendelea baada ya kazi kumalizika Kijijini KIILIMA kambi ya wazee
Kaimu Mkuu wa Kituo cha Wazee KIILIMA Bi Gladness Lwiza akipanda mti kwa ajili ya kumbukumbu
Tafakuri pana kwa Mzee Wilson Ziraimanikabla ya kukabidhiwa mahitaji na uongozi wa METDO Tanzania
 Nyumba ya kulala wazee wa kituo cha KIILIMA kilichopo Kata ya Nyakato Mkoani Kagera
 Viongozi wkibadilishana mawazo mara baada ya kuzuru kituo cha Wazee KIILIMA
Kijana ni mzee ajaye na Mzee ni kijana aliyekuwa
Hili ndilo jiko linalotumiwa na viongozi wa kituo cha KIILIMA kilichopo nje kidogo ya Manispaa ya Bukoba
Katikati ni Dkt Peter Shija Mganga Mfawidhi kutoka zahanati ya Ibosa akipata maelezo ya awali kwa Moja ya mzee aishie kambini KIILIMA kabla ya kumfanyia vipimo
Mathias Canal Mratibu wa Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya METDO Tanzania akipanda mti wa matunda aina ya Mlimao kwa ajili ya kumbukumbu ya kuzuru kituo cha Wazee KIILIMA
 Majadiliano ya namna ya kuchimba mashimo kabla kupanda miti
 Moja ya nyumba anayoishi Mtumishi wa Kituo cha wazee KIILIMA Kilichopo Mkoani Kagera
Mkurugenzi wa METDO Tanzania Bw Ashraf Omary mwenye Jembe akimsaidia kazi Mzee Wilson Ziraimani, Mzee huyu alikuwa anafanya kazi za kilimo katika mashamba mbalimbali nchini, yeye ni mkazi wa Ngara na wakati akiwa mtoto alikuwa analelewa na Mama wa kambo.
Aliwasili katika kituo cha kulelea Wazee cha KIILIMA Mwaka 1986 hapo alipo anatambaa kwani alivunjika kiuno enzi za ujana wake baada ya kuanguka mtini wakati alipokuwa anakata kuni kwa ajili kupikia.
Viongozi wa METDO Tanzania, Kiongozi wa TASWO, na Viongozi wa kituo cha Wazee KIILIMA wakipanda mti wa matunda aina ya Parachichi kwa ajili ya kumbukumbu na kampeni ya upandaji miti

Na Mathias Canal, Bukoba

Kukosekana kwa huduma bora na msingi kwa wazee nchini imetajwa kuwa changamoto kubwa kwa Wazee waishio katika kambi mbalimbali za serikali na zile za binafsi.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Asasi isiyokuwa ya Kiserikali ya METDO Tanzania (Mining and Environmental Transformation for Development  Organization) Bw Ashraf Omary wakati akikabidhi mahitaji kwa wazee wa kituo cha KIILIMA kilichopo Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera.

Bw Omary alisema kuwa Asasi hiyo yenye usajili No. ooNGO/08317 inajishughulisha na kutoa Elimu ya Mazingira kwa wananchi wanozunguka migodi pamoja na wafanyakazi wa migodini ambapo pia imejikita kuwasaidia wazee waishio katika kambi mbalimbali nchini katika huduma za kuwapatia mahitaji ya msingi ya kila siku kama vile (Chakula, na Mavazi) sambamba na kutoa huduma ya upimaji wa afya zao kupitia wataalamu wa tiba na kuwapatia dawa kwa ajili ya matibabu ya magonjwa mbalimbali.

Alisema kuwa kumekuwa na wimbi kubwa la wazee kutopatiwa huduma bora ikiwemo chakula na matibabu jambo ambalo kwa kiasi kikubwa linachangia wazee wengi kufariki pasina huduma yoyote ya kitabibu sambamba na kukosa Lishe Bora.

Bw Omary ameushukuru uongozi wa kampuni ya ZONGII PUMBLING LTD ya Jijini Mwanza kwa kushirikiana na METDO Tanzania kufanikisha kupatikana mahitaji mbalimbali kwa ajili ya wazee wa kambi ya KIILIMA sambamba na kuupongeza uongozi wa Mkoa wa Kagera kwa ushirikiano ulioonyesha ikiwa ni pamoja na kuruhusu madaktari kwa ajili ya kwenda kuwapima afya wazee hao.

Kwa upande wake Meneja Mradi wa METDO Tanzania Bw Hussein Sungura amebainisha kadhia zinazowakumba wazee katika kituo cha KIILIMA sambamba na vituo vingine nchini kuwa ni pamoja na ukosefu wa huduma za usafiri ili kurahisisha wazee kufikishwa haraka hospitalini pindi wauguapo, Ufinyu wa Bajeti, Ukosefu wa vitendea kazi kama vile vifaa vya usafi na ucheleweshaji wa Ruzuku ya serikali.

Sungura alisema kuwa Mpaka sasa Asasi hii ya METDO Tanzania imesaidia katika maeneo mbalimbali ikiwemo tukio la Agosti 13, 2016 la kumuenzi Mwl Julius Kambarage Nyerere katika Makao ya wazee wasiojiweza BUKUMBI Mwanza, Tukio la Octoba Mosi 2016 SIKU YA WAZEE DUNIANI katika wilaya ya Shinyanga ambapo jamii ilishirikishwa kutambua changamoto zilizopo katika kituo cha Wakoma na Wazee wasiojiweza cha KOLANDOTO pamoja na Kituo cha Wakoma na  Wazee wasiojiweza cha NYABANGE BUTIAMA  na kuwa sehemu ya kuzitatua changamoto hizo.

Kutokana na kazi hiyo ya wito inayofanywa na METDO Tanzania Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Salim Kijuu ametoa wito kwa Asasi hiyo kuwekeza Mkoani Kagera katika sekta mbalimbali ikiwemo kilimo ili ushirikiano wa kusaidia wazee uweze kukomaa na kusaidia wazee wote nchini kirahisi sambamba na kutoa fursa kwa vijana kutambua umuhimu wa kufanya kazi sawia na kujiajiri.

Kijuu alisema kuwa kutokana na Mkoa wa Kagera kuwa na hali nzuri ya hewa na udongo wake kuwa na rutuba ni vyema Asasi ya METDO Tanzania ikafanya kazi yake kwa misingi ya katiba lakini pia inapaswa kuwasaidia vijana wengi nchini ili kuachana na uvivu walionao badala yake kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli katika kuisimamia na kutekeleza kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu.

Akisoma taarifa ya kituo hicho Kaimu Mkuu wa Kituo cha Wazee KIILIMA Bi Gladness Lwiza alisema kuwa Kituo hicho kina jumla ya wahudumiwa 24 ambapo kati yao kuna watoto 6 waliokuwa kwenye mazingira hatarishi baada ya kutelekezwa na wazazi wao huku wengine wakipokelewa baada ya wazazi wao kufariki kutokana na janga la UKIMWI lililotokea mwaka 1984.

Hata hivyo amewaomba wadau mbalimbali kujitokeza na kuwachukua watoto hao kwani kuendelea kubaki katika kituo hicho sio jambo jema kwao kwani wanachanganyikana na wazee ambao wengi wao wana matatizo ya akili.

Lwiza amesema kuwa kufuatia uharibifu wa majengo kutokana na Tetemeko lililotokea hivi karibuni Mkoani Kagera na kuharibu majengo mengi kituoni hapo imesababisha kukosekana kwa nyumba za watumishi, na choo kwa ajili ya matumizi ya wazee pamoja na watumishi wa kituo hicho.

Naye Dkt Peter Shija Mganga Mfawidhi kutoka zahanati ya Ibosa ameiomba serikali kusaidia upatikanaji wa sehemu maalumu ya kuhifadhia dawa, kutolewa mafunzo ya tiba kwa wahudumu waliopo kituoni hapo sambamba na kupatikana kwa vifaa tiba kwa ajili ya kupima damu, Sukari, MRTD, Presha na wingi wa damu.

Kituo cha Wazee KIILIMA kilichopo Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera kilicho chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ni moja kati ya vituo vya kulelea wazee hapa nchini ambapo awali kilikuwa chini ya kanisa la Roman Catholic na baadaye kilikabidhiwa rasmi kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mnamo mwaka 1974.

Baada ya kutembelea vituo vyote vya Wazee kanda ya Ziwa METDO Tanzania inataraji kuzuru Mikoa ya Kanda ya kati kwa ajili ya kujionea changamoto za wazee mbalimbali waishio kambini na kuzifikisha sehemu husika wakiwemo viongozi wa dini, Wafanyabiashara, Serikali na Wadau mbalimbali nchini.

RAIS MAGUFULI AWATUNUKU MAOFISA 194 CHEO CHA LUTENI USU

$
0
0
Bendi ya Jeshi la Ulinzi la WananchiV (JWTZ) likiingia uwanjani wakati wa sherehe za kutunuku Maafisa 194 wa Jeshi hilo katika viwanja vya Ikulu leo Jijini Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akishiriki kuimba wimbo wa Taifa wakati wa sherehe za kutunuku kamisheni Maafisa 194 wa Jeshi hilo katika viwanja vya Ikulu leo Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua gwaride wakati wa sherehe za kutunuku Maafisa 194 wa Jeshi hilo katika viwanja vya Ikulu leo Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa zawadi kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika mafunzo wakati wa sherehe za kutunuku Maafisa 194 wa Jeshi hilo katika viwanja vya Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwatunuku kamisheni Maafisa wapya 194 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ)
Maafisa wapya 194 wakila kiapo cha uadilifu baada ya kutunukiwa kamisheni katika viwanja vya Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimueleza jambo Mkuu wa Chuo cha Maafisa wa Jeshi (TMA) Meja Generali Paul Massao(Kulia) kushoto ni Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange akiongea na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, wakati wa sherehe za kutunuku Maafisa 194 wa Jeshi hilo katika viwanja vya Ikulu leo Jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Chuo cha Maafisa wa Jeshi (TMA) Meja Generali Paul Massao akitoa taarifa fupi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ya mafunzo kwa maafisa wa jeshi ambapo alisema kozi ya mafunzo hiyo ya mafunzo ilianza na wanafunzi 222 kabla ya kuchujwa na kubaki 194 kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kutofikia viwango.

PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO

………………………………………………………………..
Na Jonas Kamaleki- MAELEZO
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli leo ametunuku kamisheni maofisa194 wa jeshi Ikulu jijini Da re Salaam.

Kati ya waliotunikiwa cheo cha luteni usu, 26 ni wanawake na 168 ni wanaume ambapo watatu kati ya wahitumu hao wamepewa tuzo kwa kufanya vizuri zaidi ya wenzao katika mafunzo. Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Chuo cha kijeshi Monduli, Meja Jenerali Paul Peter Massao amesema ni ofisa mmoja tu kati ya wote ambaye alisomea Uingereza, waliobaki wamesomea Monduli na ni Watanzania.

Kwa mujibu wa taratibu za kijeshi, Mtanzania yeyote anayesomea nje ya nchi akihitimu inabidi arudi nchini ili atunukiwe kamisheni na Amiri Jeshi Mkuu. Walianza wanafunzi 224 ambapo waliohitimu ni 194 na wengine hawakuweza kuhitimu kutokana na sababu mbali mbali zikiwemo changamoto za kimafunzo,” alisema Meja Jenerali Massao.

Tukio hili ni la kihistoria kwani limefanyika Ikulu tofauti na miaka yote iliyopita ambapo Amiri Jeshi Mkuu hutunuku kamisheni katika chuo hicho Monduli tangu chuo hicho kilipohamia huko miaka ya 70. Sherehe hizo zilipambwa na gwaride kutoka kwa maofisa hao na kukolezwa na gwaride la kimya ambalo lilifanyika kwa kwa umahili.

Waliohitimu leo ni awamu ya 59 tangu chuo hicho kianzishwe zaidi ya miongo minne iliyopita. Chuo cha Kijeshi kilianza mwaka 1969, Kurasini jijini Dar es Salaam kutokana na mahitaji ya mafunzo yanayozingatia maadili ya Kitanzania, na baadae kilihamishiwa Monduli, Arusha mwaka 1976.

Rais Magufuli atunuku Kamisheni kwa Maafisa Wapya wa JWTZ Ikulu DSM

$
0
0
 :Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akikagua gwaride la heshima linaloundwa na Maafisa Wanafunzi wa Kundi la 59/15 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) kabla hajawatunuku kamisheni katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 26, 201
  Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akitunuku kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi wa Kundi la 59/15 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 26, 2016
  Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akitunuku kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi wa Kundi la 59/15 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 26, 2016
 Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiweka saini kwenye hati  ya  kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi wa Kundi la 59/15 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) kabla hajawatunuku katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 26, 201

 Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiweka saini kwenye hati  ya  kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi wa Kundi la 59/15 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) kabla hajawatunuku katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 26, 201
 Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiongea baada ya kutunuku  kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi wa Kundi la 59/15 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 26, 201.
 Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiongea baada ya kutunuku  kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi wa Kundi la 59/15 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 26, 201

PICHA NA IKULU



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 26 Novemba, 2016 ametunuku Kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi 194 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)  kundi la 59/15 katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Hii ni mara ya kwanza kwa Maafisa Wanafunzi wa JWTZ kutunukiwa Kamisheni nje ya Chuo Cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli kilichopo mkoani Arusha, na ni mara ya kwanza kwa Maafisa Wanafunzi wa JWTZ kutunukiwa Kamisheni ndani ya  Ikulu.

Maafisa hao ambao 168 ni wanaume na 26 ni wanawake, wametunukiwa Kamisheni katika cheo cha Luteni Usu na sasa wamekuwa Maafisa Wapya wa JWTZ.

Kabla ya kutunuku Kamisheni, Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli amekagua gwaride rasmi lililoandaliwa na Maafisa wanafunzi wa JWTZ na baadaye akashuhudia uhodari wa askari kutoka kikosi cha maadhimisho cha JWTZ waliofanya onesho la gwaride la kimyakimya.

Akizungumza baada ya chakula cha mchana katika ukumbi wa Ikulu, Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli amempongeza Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange, Makamanda na Askari wote wa JWTZ kwa jukumu kubwa wanalolitekeleza la kuhakikisha nchi ipo salama na amesema Serikali itahakikisha inaboresha zaidi maslai na mazingira ya kazi kwa Jeshi hilo na vyombo vingine vya ulinzi na usalama.

Aidha, Rais Magufuli amesema ameamua tukio hili la kutunuku Kamisheni lifanyike Ikulu Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kutoa heshima kwa Maafisa wa JWTZ kama ambavyo Viongozi wengine Serikalini wamekuwa wakipata heshima ya kuapishiwa Ikulu.

"Kwamba Mawaziri tunapotaka kuwaapisha tunawaapishia hapa, Wakuu wa Mikoa tunawaapishia hapahapa, Makatibu Wakuu tunawaapishia hapahapa, kwa nini hawa Maafisa wa Jeshi tusiwaapishie hapahapa kwenye nyumba yao? Nyinyi ndio mnalinda nchi, nyinyi ndio mnasimamia usalama wa nchi hii, lakini nikiuliza hapa inawezekana wengine mpaka wamekuwa Mabrigedia Jenerali hawajawahi kukanyaga Ikulu, wakati hapa ni kwenu" amesema Rais Magufuli.

Sherehe za kutunuku Kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi hao zimehudhuriwa na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi na Wakuu wa Jeshi la Ulinzi wastaafu na Majenerali wastaafu wa JWTZ.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

26 Novemba, 2016

Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Rais Fidel Castro

$
0
0
 Rais Mstaafu wa Cuba Mhe. Fidel Castro enzi za uhai wake




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, John Pombe Magufuli, amemtumia salamu za rambirambi Rais wa Jamhuri ya Cuba Mhe. Raul Castro kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Cuba Mhe. Fidel Castro kilichotokea tarehe 25 Novemba, 2016.
Katika Salamu hizo Rais Magufuli amesema;

"Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Cuba Mhe. Fidel Castro. Kwa niaba ya Serikali, Wananchi wa Tanzania na kwa niaba yangu mwenyewe natoa pole nyingi kwako, familia, Serikali ya Cuba na wananchi wa Cuba kwa kumpoteza mtu muhimu.

Fidel Castro alikuwa kiongozi shupavu wa karne, atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika na pia kwa misaada mikubwa aliyoitoa katika kuboresha huduma za kijamii kwa wananchi.

Alikuwa rafiki wa Tanzania na Afrika nzima, historia ya Tanzania na Afrika haziwezi kukamilika bila kumtaja Fidel Castro, hakika kifo chake sio tu ni pigo kwa Cuba bali pia kwa Tanzania na Afrika.
Naungana nawe na wananchi wa Cuba katika kipindi hiki kigumu cha majonzi, na pia nakuombea kwa Mwenyezi Mungu wewe, familia na wananchi wote wa Cuba muwe na nguvu, subira na ustahimilivu kutokana na kuondokewa na mpendwa wenu."

Pia Rais Magufuli amemuombea marehemu Fidel Castro apumzishwe mahali pema peponi, Amina.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
26 Novemba, 2016

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOV 27

RAIS MSTAAFU JAKAYA KIKWEETE AWAUNGA MKONO VIJANA WAKULIMA WA VITUNGUU RUAHA MKUU MKOANI IRINGA

$
0
0
Rais Mstaafu awamu ya nne,Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa njiani kurejea kijijini kwake Msoga, alisimama Ruaha Mkuu mkoani Iringa na kununua vitunguu na kuwaungisha vijana hao wanaojishughulisha na kilimo cha vitunguu.
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akiwa na vijana wajasiliamali hao ambao ni maarufu kwa ulimaji na uuzaji wa vitunguu

DKT SHEIN AZINDUA HOSPITALI YA ABDALLA MZEE MKONI PEMBA

$
0
0

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) na Mkurugenzi wa huduma za Hospitali Mohamed Dahoma na Viongozi wengine wakiwa katika chumba cha uchunguzi wa matatizo ya uti wa mgongo baada ya kuizindua rasmi Hospitali ya Abdalla Mzee iliyopo Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba leo ,[Picha na Ikulu.] 26/11/2016.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) na katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt.Juma Malik Akil wakifuatana na Viongozi wengine wakati alipotembelea Hospitali ya Abdalla Mzee iliyopo Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba baada ya kuizindua rasmi leo (kulia) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe, Mwanajuma Majid hospitali hii imejengwa na Kampuni ya Kichina Jiang SU Ltd,

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwapungia mkono wananchi mara baada ya kutembelea sehemu mbali mbali za Hospitali ya Abdalla Mzee iliyopo Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba baada ya kuizindua rasmi leo (kulia) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe, Mwanajuma Majid hospitali hii imejengwa na Kampuni ya Kichina Jiang SU Ltd,
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitoa hutuba yake kwa wananchi wa Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba na Viongozi mbali mbali baada ya kuizindua Hospitali ya Abdalla Mzee leo ambayo imejengwa na Kampuni ya Kichina Jiang SU Ltd

WAKAZI WA KIBAMBA WILAYANI UBUNGO WAZUIA MSAFARA MAKONDA WAKITAKA WASIKILIZWE KERO ZAO

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda akizungumza na wananchi wa Kibamba Wilayani Ubungo huku wakiwa wamebeba mabango yanayoonesha kuwa wamedhulumiwa ardhi yao.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo,Humphrey Polepole akizungumza na wananchi wa Kibamba Wilayani Ubungo huku wakiwa wamebeba mabango yanayoonesha kero zao mbalimbali wanazotaka zipatiwe majibu
wananchi wa Kibamba Wilayani Ubungo wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda alipokuwa akizungumza nao kwenye ziara yake ya kusikiliza na kutatua kero za Wananchi.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii


Wakazi wa Kibamba Wilayani Ubungo wamezuia msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda huku wakiwa wamebeba mabango yanayoonesha kero zao mbalimbali ikiwemo na kero ya kudhulimiwa maeneo yao ya.

Akizungumza na wakazi hao waliokuwa wamesimamisha msafara huo, Mkuu wa Wilaya hiyo Humphrey Polepole aliwataka wakazi hao kufuata utaratibu Kwani madai yao yamefika mezani kwake na baadhi yameanza kushughulikiwa kwa watu kulipwa fidia zao kutokana na kupisha eneo la chuo na hospitali ya MUHAS .

DC Polepole amesisitiza kuwa serikali ipo pamoja na wananchi hao ambao wengine wanadai fidia ya eneo la kwembe na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete aliahidi kuwa watalipwa, vilevile Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliwahidi kuwa serikali itazifanyia kazi ahadi zote zilizoachwa na serikali iliyopita. 

DC Polepole ameongeza kuwa kwa wale wakazi waliopo maeneo ya hifadhi ya barabara serikali itaendelea na msimamo wake wa upanuzi wa barabara kama alivyohaidi Rais Magufuli jana kwenye Mkutano wa hadhara wa RC Makonda uliofanyika Maramba Mawili.

Kwa upande wake RC Makonda ambaye alishuka baada ya wakazi hao kuonekana kugoma kupisha msafara hu na kuwaambia kufuata utaratibu kutokana na majibu ya awali ya DC Polepole.

VIJANA WAKISEBENEKA KWA FURAHA BAADA YA KUMALIZA MAFUNZO YA UJASILIAMALI

$
0
0


Afisa Mradi, Kitengo cha Kujenga Uwezo kutoka shirika lisilo la Kiserikali la 'The Foundation For Civil Society' Nasim Losai, akizungumza na Vijana wajasiliamali kutoka Mikoa mbalimbali ya Tanzania walioshiriki Mafunzo ya Siku tano ya Ujasiliamali, Fursa na Taratibu za kufanya biashara kuelekea Soko la Jumuiya ya Afrika Mashari. Nasimi alifunga mafunzo hayo yaliyomalizika juzi Nov 25, 2016 kwenye Hoteli ya Blue Pearl Ubungo Plaza.
Afisa Mradi, Kitengo cha Kujenga Uwezo kutoka shirika lisilo la Kiserikali la 'The Foundation For Civil Society' Nasim Losai, akizungumza na Vijana wajasiliamali kutoka Mikoa mbalimbali ya Tanzania walioshiriki Mafunzo ya Siku tano ya Ujasiliamali, Fursa na Taratibu za kufanya biashara kuelekea Soko la Jumuiya ya Afrika Mashari. Nasimi alifunga mafunzo hayo yaliyomalizika juzi Nov 25, 2016 kwenye Hoteli ya Blue Pearl Ubungo Plaza.
Afisa Mradi, Kitengo cha Kujenga Uwezo kutoka shirika lisilo la Kiserikali la 'The Foundation For Civil Society' Nasim Losai, akizungumza na Vijana wajasiliamali kutoka Mikoa mbalimbali ya Tanzania walioshiriki Mafunzo ya Siku tano ya Ujasiliamali, Fursa na Taratibu za kufanya biashara kuelekea Soko la Jumuiya ya Afrika Mashari. Nasimi alifunga mafunzo hayo yaliyomalizika juzi Nov 25, 2016 kwenye Hoteli ya Blue Pearl Ubungo Plaza.
Afisa Mradi, Kitengo cha Kujenga Uwezo kutoka shirika lisilo la Kiserikali la 'The Foundation For Civil Society' Nasim Losai, akifurahia na Vijana hao wakati wakiimba wimbo maalum.
Afisa Mradi, Kitengo cha Kujenga Uwezo kutoka shirika lisilo la Kiserikali la 'The Foundation For Civil Society' Nasim Losai, akifurahia na Vijana hao wakati wakiimba wimbo maalum.
''Sasa Mafunzo yamefungwa rasmi'' .......

Waratibu wakiweka mabo sawa wakati wa kufunga mafunzo hayo.
Vijana wakijaza Fomu za Mpango kazi baada ya kumalizika mafunzo hayo.
Mkufunzi Peninah akiwaelekeza baadhi ya Vijana kujaza Fomu za Mpango kazi baada ya kumalizika mafunzo hayo.
Vijana wakijaza Fomu za Mpango kazi baada ya kumalizika mafunzo hayo.
Vijana wakielekezana kujaza Fomu za Mpango kazi baada ya kumalizika mafunzo hayo.
Vijana wakijaza Fomu za Mpango kazi baada ya kumalizika mafunzo hayo.
Vijana wakijaza Fomu za Mpango kazi baada ya kumalizika mafunzo hayo.
Vijana wakijaza Fomu za Mpango kazi baada ya kumalizika mafunzo hayo.
Vijana wakijaza Fomu za Mpango kazi baada ya kumalizika mafunzo hayo.
Vijana wakijaza Fomu za Mpango kazi baada ya kumalizika mafunzo hayo. Ila wengine walikuwawakipiga chabo kama Class wakati wa Mtihani mwananguuuuuu........
Vijana wakijaza Fomu za Mpango kazi baada ya kumalizika mafunzo hayo.

JAFO AWAKOMALIA WAHANDISI WA HALMASHAURI ZA MKOA WA TANGA KWA KUTOZINGATIA MAHITAJI YA WANAFUNZI WALEMAVU

$
0
0




Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo amehitimisha ziara yake Mkoani Tanga huku akionesha kuchukizwa na kitendo cha Wahandisi wa ujenzi Katika Halmashauri za mkoa huo kwa kutozingatia mahitaji ya wanafunzi wenye ulemavu.

Jafo alifanikisha ziara yake ya siku tatu kwa kutembelea Halmashauri zote za mkoa wa Tanga. Katika ziara yake mkoani huo, Jafo alikagua ujenzi wa vyoo vinavyo jengwa katika shule mbalimbali za sekondari mkoani Tanga kupitia mradi wa SEDEP II.

Akizungumza mara baada ya ziara yake, Jafo alisema amegundua vyoo vyote vilivyo kamilika na vinavyo endelea kukamikishwa mkoani huo havijazingatia kuweka miundombinu ya watu wenye ulemavu.

“Katika kila shule niliyopita nimekuta vyoo vizuri sana vimejengwa lakini vina kasoro ya kukosa hata tundu moja kwa maeneo yote ya wasichana na wavulana yaliyo andaliwa kwaajili ya watoto walemavu,”alisema Jafo

Aliwaagiza wakurugenzi wote kuhakikisha hitaji hilo la msingi kwa watoto walemavu linazingatiwa kwa kufanya marekebisho kwa upande wa vyoo vya wavulana na wasichana ili kupata tundu moja kwa lengo la kuwasaidia watoto wenye ulemavu.

Jafo mara baada ya kuhitimisha ziara yake mkoani Tanga anaelekea kuanza ziara nyingine katika mkoa wa Ruvuma, Mtwara, Lindi na Pwani.



 Waatumishi wakimsikiliza Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo katika ziara yake aliyoifanya mkoani Tanga.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akizungumza katika kikao cha watumishi wilaya ya Handeni.Pichai kati ni Mkuu wa Wilaya ya Handeni.Mh.Godwin Gondwe.

Wadau watoa Maoni yao Kuhusu Sera Mpya ya Ardhi ya Mwaka 2016

$
0
0


Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na maendeleo ya Makazi Dkt Yamungu Kayandabila Akiwahakikishia wadau kwamba Maoni yao yatafanyiwa kazi.Dkt kayandabila ameyasema hayo wakati wa zoezi la kukusanya maoni kutoka kwa Wadau Ukumbi wa VETA Mkoani Morogoro.
Dkt. Ringo Tenga wa Chuo Kikuu Dar es salaam akishiriki kutoa maoni kuhusu marekebisho ya Sera mpya ya Ardhi ya Mwaka 2016 Ukumbi wa VETA Mkoani Morogoro.

“Pamoja na kuwaalika wawekezaji Tulinde maeneo ambayo ni Vyanzo vya chakula” hayo ni baadhi ya Maoni ya Dr Ringo Tenga kutoka Chuo kikuu cha Dar es salaam aliyo wasilisha wakati wa zoezi la kukusanya maoni ya wadau kuhusu Sera Mpya ya ardhi ya mwaka 2016 katika ukumbi wa VETA Mkoani Morogoro.

WAZIRI MBARAWA AONGOZA UJUMBE WA SERIKALI YA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA KIMATAIFA WA USAFIRISHAJI DUNIANI,NCHINI TURKMENISTAN

$
0
0

Mkutano huuo ukiendelea

Mhe.Makame Mbarawa waziri wa Ujenzi uchukuzi na mawasiliano akiongoza ujumbe wa serikali ya Tanzania kwenye mkutano wa Usafirishaji Duniani unaofanyika jijini Ashgabat nchini Turkmenistan, mkutano huo wa kimataifa umefunguliwa leo na katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban ki moon. Picha na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Makame Mbarawa akiongea na Waziri wa Uchukuzi wa Nchini Urusi Maksin Sokolov masuala muhimu yanayohusu sekta ya usafitishaji katika nchi zao.
Waziri Mbarawa anahudhuria mkutano wa kimataifa wa usafirishaji Duniani unaofanyika jijini Ashgabat nchini Turkmenistan.

Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Makame Mbarawa akiongea na Waziri wa Usafirishaji wa Oman Ahmed Mohamed Salim Al- Futaisi masuala muhimu yanayohusu sekta ya usafirishaji katika nchi zao. Waziri Mbarawa anahudhuria mkutano wa kimataifa wa usafirishaji Duniani unaofanyika jijini Ashgabat nchini Turkmenistan.

RC MAKONDA ATINGA UWANNJA WA FISI,AAMURU BIASHARA YA NGONO IFUNGWE

$
0
0
 Mkuu wa mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam ,Paul Makonda akiangalia barabara ya Tandale inayounganisha eneo la Mwananyamala ambayo imekuwa haihpitiki kwa uraisi kwa kipindi chote kutokana mashimo ya yaliyokithiri  na kupelekea usumbufu mkubwa kwa waendeshaa magari na kwa miguu pia,leo jijini Dar es Salaam. 
 Mkuu wa mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam ,Paul Makonda akiteta na Mlemavu ambaye amemkuta katika eneo la uwanja wa fisi akinywa pombe za kienyeji na kumsihi aache kunywa pombe hizo, leo jijini Dar es Salaam. 
 Mkuu wa mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam ,Paul Makonda akiwa ameongozana na Kamanda   wa kanda maalum ,Simon Sirro kugonga nyumba za baadhi ya akina dada  ambao hufanya biashara ya kujiuza katika eneo la uwanja wa fisi, leo jijini Dar es Salaam. 
 Mkuu wa mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam ,Paul Makonda akiwa na Kamanda wa kanda maalum ,Simon Sirro wakiangalia bia ambazo zinauzwa uwanja wa fisi zikiwa zimekwisha muda wake,ambazo inaelezwa zimekuwa zikitumika kwa ajili ya matumizi ya Binadamu, leo jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam ,Paul Makonda akisalimiana na dereva wa daladala katika kituo cha Tandale kwa mtogole,leo jijini Dar es Salaam. 
 Mkuu wa mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam ,Paul Makonda akiangalia mfereji wa Tandale ambao umeharibiwa kutokana na wananchi ambao wamekuwa wakitupa taka hovyo  katika mfereji huo,leo jijini Dar es Salaam. 
 Mkuu wa mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam ,Paul Makonda, akiteta jambo na mmoja wa wakazi wa jiji la eneo la Tandale.

BENKI YA UBA YATOA MSAADA PUGU SEKONDARI

$
0
0
Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii

Benki ya United Bank of Africa (UBA), jana imetoa msaada wa viti, Magodoro, Magongo ya kutembelea na vitabu vya kujisomea kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu ya shule ya sekondari ya wavulana Pugu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kutoa vifaa hivyo, Meneja wa benki hiyo nchini ,Peter Makao, amesema kuwa wamechagua kutoa vifaa hivyo katika shule hiyo kutokana na mahitaji ya watoto hao ambao wamekuwa wakisoma katika mazingira magumu.

“Vitu hivi ambavyo tumevitoa leo vitasaidia kwa kiasi kikubwa kuwapunguzia watoto hawa wenye mahitaji maalum kusoma kwa mawazo kwa kujiona kwamba wao ni sehemu hii ya shule kwa kupata mahitaji yao wote kama ilivyo kwa wengine”Amesema Makao 

Ametoa wito kwa wanafunzi hao kusoma kwa bidii ili waweze kufanikiwa katika jamii na baadae wajivunie kuwa walisoma pugu .
Wanafunzi wa Pugu sekondari wakishusha kwenye gari vifaa vilivyokabidhiwa na benki ya UBA kwa ajili ya wanafuzni wenye mahitaji maalum
Mkurugenzi mkuu wa Benki ya UBA,Peter Makao akiwa na Meneja Operesheni Omary wakikabidhi mafuta ya ngozi kwa kijana mwenye ulemavu wa ngozi ,Daudi Nyangusi na Meneja ufadhili wa eleimu kutoka TEA , Tito Mganwa.
Mkurugenzi mkuu wa Benki ya UBA,Peter Makao akiwa meneja operesheni Omary wakikabidhi vitabu kwa wanafunzi Salum Mohamed na Ramadhani Juma pamoja na Meneja ufadhili wa eleimu kutoka TEA , Tito Mganwa.
Wafanyakazi waUnited Bank of Afrika wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wenye ulemavu wa shule ya Sekondari ya wavulana pugu jijini Dar es Salaam.


RAIS DKT MAGUFULI AMEAMUA KULETA MABADILIKO YA KWELI NA TUMUUNGE MKONO-ULEGA

$
0
0
 Mbunge wa mkuranga Mh Abdala Ulega akimkabidhi Pikipiki Mwenyekiti wa vianz Bw Rashid Gadaf . Picha zote na Yasir Adam Blogu ya Jamii.

 Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Mh Abdala Ulega akizungumza na wajumbe wa Halmashaur kuu kupitia chama cha CCM kata ya vianzi wilayani Mkuranga ,Wakati huohuo Mh.Ulega  alikabidhi Pikipiki Kwa Viongozi wa  Chama cha Mapinduzi CCM Kata  Viazi Mara baada ya kualikwa Kwenye mkutano wa ndani wa  Halmashauri kuu  ya CCM  Kata hiyo.
Diwani wa Kata ya Vianzi akizungumza na wajumbe ya Halmashaur kuu wa kata ya vianzi kupitia chama cha Ccm wilayani mkuranga
Mwenyekuti wa Kata ya Vianzi Bw Rashid Gadafi akizungumza na wajumbe wa halmashauri kuu kutoka chama cha Ccm wilayani mkuranga


MBUNGE wa Jimbo la Mkuranga Abdallah Ulega amewataka vijana wa Chama cha Mapinduzi kujitokeza Kwa wingi katika uchaguzi Mkuu ujao wa Chama unaotarajia kufanyika mapema mwakani 2017.

Amesema kuwa wanatakiwa kujitokeza Kwa wingi ili kushika nafasi mbalimbali za uongozi ndani Chama na lengo hasa kutaka kumsaidia Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa Ambaye ni rais wa Tanzania Dkt John Magufuli katika kutekeleza majukumu Yake.

Akizungumza na Halmashauri kuu ya CCM kata ya Viazi Jana wilayani humo .alisema kuwa Kwa Dkt.Magufuli hakuna jambo la uzoefu kwake yeye ni Kazi tu.nakudai watu walidhani wimbo wa mabadiliko Kwa Dkt. Magufuli ilikuwa ni mzaha na sasa namba inasomeka kweli.

"Mkitaka kujuwa Kuwa rais Dkt.Magufuli hakuna uzoezi angalieni Leo anachofanya Paul Makonda Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Kazi anayoifanya nikijana ambaye ametoka chuo juzi na akaaminiwa na wakubwa Leo anapiga Kazi hivyo lazima vijana tujiamini "alisema Mbunge Ulega.

Akizungumza na Halmashauri kuu ya Kata ndani ya CCM alitumia mkutano huo kuwapongeza Kwa Kazi kubwa ya kukipambania Chama ambayo waliifanya katika Uchaguzi ulimalizika mwaka 2015.

Alisema kutokana na Kazi hiyo kubwa ambayo wameifanya yeye kama Mbunge ameamua kutoa Zawadi Kwa Kata Kumi ambazo kiukweli waliongoza Kwa kukipa kura nyingi Chama cha Mapinduzi CCM hivyo ameamua kutoa zawaidi ya Pikipiki.

Mbunge Ulega aliwasisitiza wanaCCM kuhakikisha wanamuunga mkono Kwa asilimia mia moja Rais Dkt.Magufuli ambaye amedhamiria kuwatumikia watanzania kivitendo.

"Lazima tufanye Kazi ya kuwatimikia watanzania na hasa kutimiza ahadi zetu ambazo tulizitoa Kwa wananchi ili hata tutakaporudi mwaka 2020 ili iwe kazi nyepesi kuwaambia wananchi kwamba tumetekeleza moja mbili Tatu."alisema Ulega

Aidha aliwataka wanaCCM kuondoa fitina na majungu katika kipindi hiki bali kazi iliyokuwa mbele ni kuchapa Kazi Kwa ajili ya wananchi na si vinginevyo.

Ulega pia aliwaeleza makada hao wa Chama cha Mapinduzi aliwahakikishia kuwa hadi kufikia mwaka 2020 kushirikiana na wanaCCM kujenga Ofisi za Kata ndani Chama

ZIARA YA MAKONDA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI KINONDONI YANOGA LEO, AKATIZA VICHOCHORO KUSAKA KERO, ACHAPA KAZI KIKAMILIFU NA AFANDE SIRRO, AMTUMBUA MGANGA MKUU

$
0
0
 TUCHAPE KAZI KIONGOZI: Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, akimwaga kicheko na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya mkoa huo, walipokuwa wkijadili jambo, baada ya kuzungumza na viongozi na watendaji kutoka wilaya ya Kinondoni, katika Bwalo na Maofisa wa Polisi, Msaki mwanzoni mwa ziara yake katika mkoa wa Dar es Salaam, leo. Zifuatazo ni taswira katika picha kama alivyowanasa Mmiliki wa theNkoromo Blog, Bashir Nkoromo aliyekuwa katika ziara hiyo.



  




 TANDALE
🔻
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akikagua chumba cha biashara cha Mamalishe (kushoto), aliyemkuta akiwa kazini eneo la Tandale, akiwa katika ziara ya kusikiliza kero za wananchi
Makonda akimwangalia mamalishe huyo wakati akiandaa chakula 
 Makonda na msafara wake wakikatiza mitaa ya Tandale wakati akisaka kero za wananchi wakati wa ziara hiyo ya aina yake. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Salum Ali Hapi, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida na wanne ni Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro.
 Salum Ali Hapi akimpa maelezo Makonda walipofika kukagua eneo maarufu kwa jina la Uwanja wa Fisi, lililopo Tandale, Kata ya Manzese
 Makonda akizungumza na wateja wa pombe za kieyeji aliowakuta katika kwenye kilabu cha pombe hizo, eneo la Uwanja wa Fisi
Jamaa aliyejitambulisha kwa jina la Mandela akikata funda la pombe ya kienyeji mbele ya Makonda bila wasiwasi kuwa yupo na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam  
 Makonda akijaribu kupiga hodi kwenye moja vya vyumba inayoelezwa kuwa ni ya madanguro ya ukahaba katika eneo hilo la Uwanja wa Fisi. Pamoja naye ni Hapi na Sirro 
 Kamanda Sirro naye akijaribu kumsaidia Makonda kupisha hodi lakini pia bila mafanikio ya kuitikiwa na waliokuwa wamejifungia ndani 
 Makonda akichukua bia kutoka kwa mhudumu wa baa pekee aliyoikuta wazi wakati myinge zote zikiwa zimefungwa kuhofia ujio wake.
 Makonda akiitazama kwa makini bia hiyo kuona tarehe yake ya mwisho wa matumizi, ili kujiridhisha kwa kuwa huelezwa kwamba baa zilizopo eneo hilo la Uwanja wa Fisi huuza vinywaji hadi vilivyokwisha mda wake wa matumizi. Bia hiyo aliikuta bado inafaa kwa matumizi.

 SHULE
 Makonda akitazama paa la chumba cha darasa katika shule ya Msingi Tandale, lililoporomoka wakati wa upepo mkali ulioambatana na mvua

MIUNDOMBINU YA BARABARA
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akitazama majitaka yakitiririka kwenye daraja la barabara kutoka Tandale kwenda Mwananyamala. Makonda aliahidi barabara hiyo kujengwa kwa kiwango cha lami, la kwamba kabla ya hatua hiyo itafanyiwa matengenezo ya awali kuziba makorogoro ili iweze kupitika. 
 Makonda akipita pembeni pembeni kukwema maji machafu yaliyotuama kwenye sehemu ya barabara hiyo
 Mara huyu mama naye akamvaa na kumweleza kero zake wakati akipita

MKUTANO UWANJA WA SHULE YA MSINGI TANDALE
 Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Salum Ali Hapi akimkaribisha Makonda kuanza kuunguruma ili kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia majibu papo hapo au baadae, katika mkutano wa hadhara uliofayika kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi Tandale, leo
 Makonda akizungumza 
 Makonda akizungumza kwenye mkutano huo. Kulia ni Meya wa Kinondoni Benjamin Sitta.
 Umati wa wananchi waliofika kwenye mkutano huo
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo akifuatilia jambo kwenye simu yake wakati wa mkutano huo. Mpogolo ni miongoni mwa waratibu wa ziara hiyo ya siku kumi ya Makonda katika wilaya zote za mkoa wa Dar es Salaam.
 Watu wa huduma ya kwanza wakimpeleka kwenye gari ili kupelekwa haraka hospitali baada ya kuangua wakati wa mkutano huo
 Akiingizwa kwenye gari la wagonjwa la Manispaa ya Kinondoni
 Wananchi kwenye mkutano huo
 Makonda akianza kujibu kero kwa kuwahoji watendaji kulingana na wananchi walivyotaka kujibiwa kero husika.
 Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni, Azizi Msuya (aliyeshika kinasa sauti), akisubiri hukumu ya Makonda baada ya kushindwa kueleza ikiwa alikuwa anajua au hajui kadhia ya dawa kuibwa mara kwa mara katika Zahanati ya Tandale kama wananchi walivyolalamika, ambapo alisema hajui
" Haiwezekani uwe Mganga Mkuu wa Wilaya katika mkoa wangu halafu hujui kuhusu kuibwa kwa dawa kwenye zahanati, hii haikubaliki, kuanzia sasa si mganga Mkuu wa Kinondoni, Nitawaambia wizara inayokuhusu wakupangine wilaya katika mikoa mingine ambako watavumilia uzembe kama papo", alisema Makonda wakati akimtumbua Msuya kwenye mkutano huo wa hadhara uliofanyika shule ya Msingi Tandale. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO- theNkoromo Blog

Swedish Lucia to be marked on December 8, 2016 in Dar es salaam

Vodacom Tanzania yapeleka maombi ya kujiunga na Soko la Hisa (DSE)

$
0
0
Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania imetangaza dhamira yake ya kuuza hisa kwa umma itakayofuatiwa na   kujiunga kwenye   Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) ikiwa ni utekelezaji wa sheria ya  Elektroniki na Mawasiliano ya Posta (EPOCA) na sheria ya Fedha ya mwaka 2016 ambayo inaelekeza makampuni ya simu  kumilikisha  asilimia 25 ya hisa zake kwa wananchi kwa kujiunga na Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).
Akizungumzia  hatua hiyo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Vodacom, Bwana Ian Ferrao (pichani) alisema “Tunayo furaha kutangaza kuwa tumeanza rasmi mchakato wa kuuza hisa kwa umma kwa mujibu wa matakwa ya sheria na  tumewasilisha maombi na utaratibu mzima utakaotumika kuuza hisa zetu na ratiba yetu nzima kuhusiana mchakato huu kwenye Mamlaka ya Usimamiaji wa  Masoko ya Mitaji  na Dhamana (CMSA) na Soko la Hisa  (DSE).   Hatua hii ni kubwa na inadhihirisha kuwa Vodacom ipo mstari wa mbele katika kutekeleza agizo la kuuza hisa zake kwa umma  na inadhihirisha jinsi ilivyojipanga  kuendelea kuboresha na kukuza sekta ya mawasiliano nchini Tanzania katika siku za usoni”.
Uuzaji wa hisa kwa umma  na kujiunga na Soko la Hisa kunapitia  hatua mbalimbali za  kupata vibali kutoka taasisi za serikali zenye mamlaka ya kupitia maombi na kutoa  vibali vya utekelezaji wake.Ferrao aliendelea kueleza “Tunaamini uuzaji wa hisa zetu kwa umma utazidi kukuza shughuli za Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE),kunufaisha watanzania kiuchumi na kukuza uchumi wa nchi kwa ujumla.Kampuni yetu haitajulikana kwa jina la mwanzo la Vodacom Tanzania Limited bali imekuwa na jina la
Vodacom Tanzania Public Limited Company (Plc) ikiwa ni hatua ya awali ya kujiandaa kuingia sokoni. Tunawahakikishia kuwa mchakato wa kuingia kwenye hatua hii umeanza vizuri kwa mafanikio na tunaendelea kuwashirikisha wadau mbalimbali kutoka serikalini kuhakikisha tunatimiza dhamira ya kuanza  kuuza hisa kwa wananchi yenye dira ya kuleta manufaa kwa wote.”
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Ian Ferrao,(kulia) akimkabidhi hati ya maombi ya kujiunga na soko la hisa la Dar es Salaam,(DSE)  Mkurugenzi wa Mamlaka ya Masoko na Mitaji na Dhamana (CMSA) Nicodemus Mkama(wapili kushoto) wakati wa hafla fupi iliyofanyike mwishoni mwa wiki katika ofisi za CMSA jijini Dar es Saalaam,Kushoto ni Meneja Uhusiano wa CMSA, Charles Shirima.
Mkurugenzi wa  Ushauri wa kutoka huduma za Orbit Securities Company Ltd. Gerase Kamugisha(kushoto)Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Ian Ferrao, Mkurugenzi Mtendaji wa DSE,Moremi Marwa, Mkuu wa masuala ya kifedha  wa Orbit Securities Company Ltd, Godfrey Gabriel, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia,wakionyesha hati za maombi ya kuijiunga na soko la hisa la Dar es Salaam,(DSE) mwishoni mwa wiki.
Ferrao alitoa msisitizo kuwa Vodacom inalo jukumu kubwa kuhakikisha hatua hii inaleta manufaa kwa pande zote zinatazohusika kuanzia  wanunuaji wa hisa, kuendelea kuwekeza , kuendelea kuleta mapinduzi ya ubunifu wa kiteknolojia na kuimarisha ubora wa huduma za kampuni kwa wateja wake “Tutaendelea kutoa mchango mkubwa wa ufanikishaji wa sera ya nchi ya miaka 5 ya kukuza sekta ya mawasiliano.Tutaendelea pia kuwaletea taarifa mbalimbali kuhusiana na mchakato wa kuuza hisa kwa umma unavyoendelea”Alisema Ferrao.

Wanafunzi wawili wa Shule ya Academic International washinda mitihani ya Cambridge

$
0
0
Wanafunzi wa shule ya Academic International school, Harshvardhan Kabla (kushoto) ambaye ameshika nafasi ya kwanza duniani katika somo la Kompyuta kwa wanafunzi wa “A Level” kwa mitihani ya Cambridge na Abishek Sankaranarayanan(kulia) ambaye ameshinda nafasi ya kwanza kwa somo la hisabati kwa mitihani ya Cambridge kwa wanafunzi wa kidato cha nne wakiwa katika picha ya pamoja katika sherehe maalum ya kuwapongeza.
Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni wa India, Inder Jit Sagar akimkabidhi cheti na kombe mwanafunzi wa Shule ya Academic International, Harshvardhan Kabla (kulia) kwa kushinda nafasi ya kwanza duniani katika somo la Kompyuta kwa wanafunzi wa “A Level” kwa shule zinazofuata mtahala wa Cambridge.
Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni wa India, Inder Jit Sagar akimkabidhi cheti na kombe mwanafunzi wa Shule ya Academic International, Abishek Sankaranarayanan(kulia) kwa kushinda nafasi ya kwanza duniani katika somo la Hisabati kwa wanafunzi wa “O Level” kwa shule zinazofuata mtahala wa Cambridge.
Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni wa India, Inder Jit Sagar (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na walimu wawili wa shule ya Academic International, Walter Mlowe ambaye anafundisha somo la Hisabati na Thadei Mwinuka ambaye anafundisha somo la kompyuta. Walimu hao walitunukiwa vyeti kwa kazi nzuri ya ufundishaji.
Mkurugenzi wa shule ya Academic International, Yusuf Kalindaga akizungumza katika hafla maalum ya kuwapongeza wanafunzi , walimu na wafanyakazi wa shule hiyo kwa kufanya vyema katika mitihani ya Cambridge.
Mkuu wa shule ya ya Academic International, Shyama Santhosh ( wa kwanza  kushoto) akisema jambo katika sherehe hiyo ya kuwapongeza wanafunzi hao  na walimu.


Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Academic International wakishiriki katika hafla hiyo.
Baadhi ya wazazi na wanafunzi wa shule ya Academic International wakiwa katika hafla hiyo 


Wanafunzi wawili wa shule ya Academic International ya Tanzania wameweka historia katika mitihani ya mtahala wa Cambridge baada ya kushinda nafasi ya kwanza duniani katika masomo ya hisabati na kompyuta.

Wanafunzi hao ni Harshvardhan Babla aliyekuwa wa kwanza katika mtihani wa somo la kompyuta kwa wanafunzi wa kidato cha tano Abishek Sankaranarayanan aliyeshinda nafasi ya kwanza katika mtihani wa hisabati kwa wanafunzi wa kidato cha nne.

Wanafunzi hao walikabidhiwa vikombe na vyeti na mgeni rasmi, Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni wa India, Inder Jit Sagar. Pia walimu wa masomo hayo, Thadei Mwinuka ambaye anafundisha somo la kompyuta na Walter Mlowe wa somo la hisabati nao walikabidhiwa vyeti vya pongezi kwa kufanya vizuri.

Akizungumza katika halfa maalum ya kuwapongeza wanafunzi hao na walimu wa masomo hayo, Mkuu wa shule hiyo, Shyama Santhosh alisema kuwa wamefarijika na ushindi huo ambao umeiletea sifa shule, walimu nan chi kwa ujumla.

“Huu ni ushindi mkubwa kwa shule, walimu nan chi kwa ujumla, mtihani wa Cambridge unafanywa na maelfu ya shule duniani na shule yetu imeibuka katika nafasi ya kwanza kwa masomo hayo mawili, ni jambo la kujivunia sana, hii inaonyesha kuwa walimu wetu wapo makini katika kufundisha,” alisema Santhosh.

Mkurugenzi wa shule hiyo, Yusuf Kalindaga amesema kuwa wanajivunia kwa matokeo hao mazuri ambayo yamewafanya kuwa shule pekee Tanzania kushika nafasi hizo za kwanza.

“Nimefarijika na kuvutiwa sana na matokeo ya wanafunzi hawa wawili, walimu wetu, Mwinuka ambaye anafundisha somo la kompyuta na Mlowe wa somo la hisabati kwa kufanya kazi kubwa kuhakikisha kuwa wanafunzi wanaowafundisha wanashika mafundisho yao na shule kwa sasa inafarijika kwa matokeo mazuri.

Akizungumza katika hafla hiyo Harshvardhan Babla aliyekuwa wa kwanza katika mtihani wa somo la kompyuta aliwapongeza walimu na viongozi wengine wa shule hiyo kwa mafundisho mazuri na kushika nafasi ya kwanza Duniani.

Babla alisema kuwa haikuwa kazi rahisi kwa mitihani ilikuwa migumu sana, lakini alizingatia mafunzo na kujibu vizuri maswali na kuibuka katika nafasi ya kwanza. Abishek Sankaranarayanan aliyeshinda nafasi ya kwanza katika mtihani wa hisabati alisema kuwa ushindi huo si faraja kwake tu, bali kwa wanafunzi wote wa shule hiyo, walimu na wafanyakazi wengine.

Abishek alisema kuwa amejituma kwa lengo la kushinda na bado anaaamini kuwa atafanya vyema katika mitihani mengine.
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live




Latest Images