Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

UAMUZI WA KAMATI YA BUNGE KUHUSU MUSWADA WA HABARI


SBL yatoa elimu kuhusu unywaji pombe kistaarabu

$
0
0

Meneja wa SBL wa Uwajibikaji Katika Jamii, Hawa Ladha akitoa maelezo katizo kuhusu kampeni ya unywaji kistaarabu katika mkutano na wadau mbali mbali wakiwepo toka vyombo vya usalama na wafanyabiashara wanaofanya kazi na SBL na wafanyakazi wa kiwanda cha SBL moshi katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika mapema jana katika mji wa Moshi mkoani Kilimanjaro.

Meneja wa mauzo wa Sbl Mkoani Kilimanjaro Godwin Seleliii akizungumza katika mkutano na wadau kuhusu kampeni ya unywaji kistaarabu iliyofanyika katika mji wa Moshi mkoani kilimanjaro mapema jana.
Mkaguzi wa polisi Mkoa wa kilimanjaro Peter Mizambwa akitoa hotuba kwa wageni waliohudhuria uzinduzi wa keampeni ya unywaji kistarabu iliyozinduliwa mapema jana na Sbl katika mji wa Moshi
Wadau mbalimbali wakifuatilia kwa makini elimu juu ya unywaji wa kistaarabu katika uzinduzi wa kampeni hiyo mapema jana
Waendesha bodaboda wakipata elimu ya unywaji kistaarabu kutoka kwa mfanyakazi wa SBL aliyekuwa anapita mitaani
Mdau akiwa na zawadi ya kava la gari mara baada ya kujibu vizuri maswali yaliyoulizwa kuhusu unywaji wa pombe kistaarabu

Moshi, Oktoba 18, 2016. Kampuni ya bia ya Serengeti imezindua kampeni inayohamasisha matumizi sahihi ya pombe au unywaji pombe kistaarabu. Kampeni hii ni hatua muhimu katika sekta ya biashara ya pombe kwa kutambua changamoto inazokabiliana nazo hususan katika masuala ya uwajibikaji kwa jamii.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo Mkaguzi wa polisi Mkoa wa Kilimanjario, Peter Mizambwa , amesema kulishirikisha jeshi la polisi, kikosi cha usalama barabarani, kunaonyesha ni kwa jinsi gani SBL wanatilia maanani suala zima la usalama barabarani hasa matokeo ya ulevi na uendeshaji vyombo vya moto. Uzoefu unaonyesha kwamba watu wengi hujisahau na kujiingiza katika ulevi wa kupindukia bila kuzingati vyombo vya moto wanavyoendesha.

“Ni jambo lilisilopingika kuwa uzembe na unywaji wa pombe kupita kiasi vina athari kubwa kwa jamii. Madhara hayo hayamuathiri mtumiaji wa pombe peke yake, bali uhatarisha maisha na kuathiri mustakabali wa watu wengi” aliongeza Mizambwa .

“Kwa matinki hiyo, ni janga la jamii nzima – huduma zetu za afya zimeelemewa kwa kiasi kikubwa na wale waliojeruhiwa katika masuala yanayohusiana na ajali na uhalifu; taasisi zetu za masuala ya sheria zimeelemewa vilivyo; uzalishaji unaathirika mno na kwa mlolongo huo, ukuaji wa pato la taifa hubakia kuwa wa kiwango cha chini”, alisema Bi Zauda.

Akielezea jinsi kampeni hii itakavyosaidia Mizambwa anasema “ma kwa hakika, sote kwa ujumla wetu tunaathirika – na sote tunalo jukumu la kuchangia namna bora ya kukabiliana na tatizo la ulevi. Nafurahi kuona kwamba wazalishaji wenyewe wa vinywaji vya pombe wametambua kuwa biashara wanayofanya kwa wateja wao inahitaji uwajibikaji na umakini wakati wa kutumia”.

Kampeni hii ya unywaji wa kistaarabu inakusudia kuwafikia vijana wengi pamoja na watu wa rika la juu kwa kuwataka kuelewa hatari ya matumizi ya pombe na kufanya maamuzi kwa faida zao – maamuzi ambayo yatanusuru mustakabali wao wa baadaye.

Naye Meneja wa SBL wa Uwajibikaji Katika Jamii, Hawa Ladha, amesema kampeni ya unywaji pombe kistaarabu inalenga kuwapa walengwa elimu kwamba mtumiaji wa pombe hahitaji kutawaliwa na pombe na kuipa nafasi ibadili mustakabali wa maisha wake na kuongeza kwamba vifo na ajali nyingi hutokana na uzembe au ulevi wa watu ambao si waathirika wakubwa wa pombe – ambao wangeweza kuwa waangalifu kama wangechukua tahadhari na kujifikiria marambili au kama marafiki zao wasingewahamasisha ku-“ongeza moja …au mbili”, alisema.

CONGO DR SLASHES VISA FEE FOR TANZANIA AND UGANDA BY 50%

$
0
0

  

CONGO DR SLASHES VISA FEE FOR TANZANIA AND UGANDA BY 50%

The Government of the Democratic Republic of Congo (DRC) has announced the reduction of Visa fee for Tanzanians and Ugandans from US $100 to US $50 effective November 1st, 2016. 

The decision comes just about a month after the DRC Ambassador to Tanzania his Excellency Jean-Pierre Mutamba and the Central Corridor Transit Transport Facilitation Agency (TTFA) Executive Secretary Capt Dieudonné Dukundane, Chief Operating Officer Mr. Sayiba Tambwe Patient held a meeting with DRC high level officials in Kinshasa on September 5th, 2016. 

An official statement issued this week by DRC’s Director General of Immigration Mr. François Beya Kasonga, said the move was part of Visa harmonization process for Central Corridor Member Countries (Burundi, DRC, Rwanda, Tanzania and Uganda). 

Already Burundi, DRC and Rwanda enjoy Visa free movement among themselves under the Economic Community of the Great Lakes Countries (CEPGL) arrangement. 

Harmonization of Visa was also one of the agreed issues during the 7th Ordinary Meeting of the Inter-State Council of Ministers of the TTFA held in Dar es Salaam on August 11th, 2016. 

Commenting on the new development Capt. Dukundane hailed DRC Officials for this move that will reduce struggles and facilitate trade within Central Corridor member countries. He also commended the useful guidance provided by the DRC Ambassador to Tanzania, Mr. Jean-Pierre Mutamba towards the achievements made so far throughout this process.

Capt. Dieudonne Dukundane
EXECUTIVE SECRETARY
From left to right: TTFA Chief Operations Officer Sayiba Tambwe Patient, TTFA Executive Secretary Captain Dieudonne Dukundane, Director General of DRC Immigration François Beya, Ambassador of DRC in Tanzania, H. E. Jean Pierre Mutamba and Deputy DG of DRC Immigration, Jean Claude during a meeting held in Kinshasa in September 5th, 2016.

UONGOZI HANDENI WAKUTANA NA WANANCHI KUWAPA ELIMU YA KUACHA KUVAMIA MAENEO YA WAWEKEZAJI WALIOMILIKISHWA KISHERIA

$
0
0
Wawekezaji wa AMC Ltd na viongozi kutoka halmashauri wakisoma ramani ya eneo la shamba la mkonge la kwamgwe.
Mkurugenzi mtendaji  Bw. William  Makufwe  akizungumza na wananchi wa vijiji vya bondo na majanini kata ya kwamgwe.
Mkuu wa wilaya ya halmashauri ya wilaya ya handeni Mh. Godwin Gondwe akizungumza na wananchi wa vijiji vya bondo na majanini  kata ya kwamgwe
Mwanasheria wa halmashauri ya wilaya ya handeni  Bw. Mangesho akiwaeleza wananchi kuwa kukaa muda mrefu sehemu haimaniishi ndio mtu anakua navumiliki halali wa eneo.
Viongozi wa kamati ya ulinzi na usalama wakijitambulisha kwa wananchi wa vijiji vya bondo na majan
Mh. Sharifa Abebe diwani wa kata ya kwamgwe  akishukuru uongozi wa halmadhauri, wawekezaji na wananchi kwa kufikia muafaka.
Baadhi ya wananchi wa vijiji vya bondo na majanini  na walioketi viti vya mbele ndio viongozi wa kampuni ya AMC ltd.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe akiambatana na kamati ya ulinzi na usalama na wataalamu mbalimbali wa Halmashauri pamoja na wawekezaji wa shamba la mkonge la Kwamgwe Kampuni ya AMC LTD wamefanya ziara na kuongea na wananchi wa Vjiji vya Bondo na Majanini namna ya kuachia maeneo ambayo wananchi hao wamevamia katika shamba hilo kwa kufanya makazi na kulima mazao ya kudumu hali iliyopelekea muwekezaji huyo kushindwa kuendelea na shughuli zake.

Akizungumza na wananchi mwakilishi wa Mkurugenzi bodi ya mkonge Bw.Fredrick Sospeter alisema shamba hilo ni mali ya kampuni ya AMC LTD ambayo walinunua toka 2002 baaada ya CRDB BANK kutangaza kuuza eneo hilo kwa kile kilichodaiwa kuwa mwekezaji wa awali aliyejulikana kwa jina la CHAVDA kushindwa kurejesha fedha za mkopo alizokuwa akidaiwa na hivyo kuamua kuliuza shamba hilo ili kufidia deni alilokua akidaiwa.

BW. Fredrick alisema kuwa awali serikali ilipanga kutoa ekari 500 kwa wanachi waliovamia ili wapate eneo la kulima na kuacha eneo la mwekezaji wazi ili kuruhusu shughuli za mwekezaji kuendelea. Dhamana hiyo imechukuliwa na mwekezaji AMC kugawa ekari 500 ambapo ekari 200 zitagawiwa kwa wananchi wa kijiji cha Bondo na ekari 300kijiji cha majanini. Ilielezwa kuwa watakao gaiwa watakuwa ni wale waliovamia na kukaa kwa muda mrefu. Mgao huo utakua pembezoni mwa Kijiji ambapo kimeishia na kwamba maeneo ya kulima yatakua ndani ya Kijiji husika.


Wananchi wanaolima mazao ya kudumu utaratibu utawekwa ili kuwawezesha wananchi hao kuvuna mazao yao na hatimaye kutoa mazao yao shambani humo, aidha wananchi ambao wanadai viinua mgongo vyao serikali inapanga utaratibu wa namna ya kuwalipa.

Mkuu wa wilaya Mh. Godwin Gondwe aliwaeleza wananchi kuwa watu watakaopewa ardhi hiyo wanafahamika kwani orodha yao ilikwisha andaliwasiku za nyuma. Pia aliwawaondoa wasiwasi wananchi kwamba shule, nyumba za ibada na zahanati ambazo tayari wamezijenga zitaendelea kutumika bila kuharibiwa kwa namna yoyote ile. 

Wananchi ambao wanaishi kwenye nyumba za mkonge wataendelea kuishi pia ila wasijenge nyingine, aliwaonya viongozi au mwanachi yeyote ambaye atathubutu kuuza eneo ambalo mwekezaji atalitoa kwaajili ya kilimo kwa wakazi wa vijiji hivyo atachukuliwa hatua za kisheria maramoja kwani serikali ya awamu ya tano inasimamia sheria na haki kwa kila mtu na hivyo wasiwe na wazo la kuuza eneo lolote.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Bw. William Makufwe aliwaeleza wananchi kwamba wamekuja kutoa ufafanuzi wa kisheria juu ya umiliki halali wa shamba hilo. Aliwaeleza kuwa wawekezaji wanakuja kufanya maendeleo katika maeneo yetu hivyo tuwape muda wafanye kazi. Aidha aliwataka wawekezaji hao kupeleka mpango kazi wa shamba hilo ili waweze kujua kama eneo wanaweza kuliendeleza au hawawezi ili hatua stahiki za kisheria ziweze kutekelezwa ikiwa kampuni itashindwa kuliendeleza shamba hilo kwa mujibu wa makubaliano.

Diwani wa Kata ya Kwamgwe Mhe. Sharifa Abebe aliwashukuru viongozi na wawekezaji, nakuwaomba waainishiwe hizo ekari ili waanze kufanya kazi maramoja,wameomba wawekezaji watakavyoanza kufanya kazi kipaumbele katika ajira kiwekwe kwa wakazi wa maeneo hayo. 

Uongozi wa kampuni ya AMC LTD uliwataka waliolima mazao ya michungwa na mazao mengine ya kudumu kuandika barua hadi kufikia tarehe 25/10/2016 kwa mwekezaji wakitaja majina yao, mazao wanayolima, wanaomba mazao yao yakae kwa kipindi gani hadi watakapoyavuna yote. Watendaji wametakiwa kukaa ofisini kuanzia saa moja na nusu hadi saa tisa na nusu kuwasaidia wananchi namna ya kuandaa barua hizo.


Alda P Sadango
Afisa habari 
Halmashauri ya Wilaya ya Handeni
18 Octoba 2016.

Wadau wa habari washindwa kusoma muswada, Kamati yawapa siku 7

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Mhe. Peter Serukamba akizungumza wakati wa majadiliano kati ya wadau wa Habari na Kamati hiyo leo Oktoba 19, 2016 Mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Mhe. Peter Serukamba(katikati) pamoja na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye(kushoto) na Naibu Sppika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Tulia Ackson wakiwasiliza baadhi ya wadau wa habari (hawapo pichani) wakitoa maoni yao kuhusu Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 katika kikao kilichofanyika leo Oktoba 19,2016 Mjini Dodoma.
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura (kulia) pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof Elisante Ole Gabriel (kushoto) wakiwasiliza baadhi ya wadau wa habari (hawapo pichani) wakitoa maoni yao kuhusu Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 katika kikao kilichofanyika leo Oktoba 19, 2016 Mjini Dodoma.
Baadhi ya wajumbe wa kamati wakifatilia maoni yaliyokuwa yakitolewa na wadau wa Habari kuhusu Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 katika kikao kilichofanyika leo Oktoba 19,2016 Mjini Dodoma.
Baadhi ya wajumbe wa kamati wakifatilia maoni yaliyokuwa yakitolewa na wadau wa Habari kuhusu Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 katika kikao kilichofanyika leo Oktoba 19,2016 Mjini Dodoma.

……………………………………………………………………….

Na Mwandishi Wetu Dodoma

LICHA ya kupewa zaidi ya mwezi mmoja tangu Bunge lilipoweka hadharani Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari, wadau mbalimbali wa Habari wameshindwa kuwasilisha maoni yao kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii kwa madai ya kutousoma na hivyo kulazimika kupewa siku saba zaidi.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Peter Serukamba alipokuwa akitoa marejesho kwa Waandishi wa Habari mara baada ya kukutana na wadau mbalimbali wa habari nchini kujadili na kupata maoni kutoka kwa wadau hao kuhusu muswada huo.

“Niwapa wadau wiki moja wawe wameleta maoni yao kwa maandishi yaani mpaka Jumatano ya wiki ijayo wawe wameyawasilisha kwa Kamati kwa kuwa leo tumewaita wakasema hawakupata muda wa kusoma,” alisisitiza Mhe. Serukamba.

Mhe. Serukamba ameongeza kuwa mchakato wa kuunda sheria unashirikisha wadau husika kwa kuleta maoni yao juu ya Mswada husika na maoni yao yanasaidia katika kutengeneza sheria iliyo nzuri kwa ajili ya Tasnia ya Habari na maendeleo yake kwa ujumla.

Ameeleza kusikitishwa na wadau hao kushindwa kusoma muswada huo au kuonekana wana ajenda yao na kusisitiza kuwa anaamini kwa muda ambao Kamati imetoa kwa wadau kuwasilisha maoni yao kwa kamati watakuwa wamewasilisha maoni kwa wakati ila kamati iyapitie kabla ya kupelekwa kwa Spika wa Bunge na kuanza kujadiliwa Bungeni.

Miongoni mwa wadau waliofika lakini wakashindwa kuwasilisha maoni ni Jukwaa la Wahariri, Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari (MoAT), Chama cha Wanasheria Nchini na Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari nchini.

Licha ya wadau hao kudai muda ulikuwa mdogo, muswada huo ulichapishwa kwenye tovuti ya Bunge katikati mwa Septemba mwaka huu huku Waziri wa Habari, Nape Nnauye akifanya mkutano na wanahabari Septemba, 16, akiuarifu umma kutoa maoni yao.

Kabla ya muswada huo kuwasilishwa Bungeni, Serikali ilishirikisha wadau katika mchakato wa ndani na walitoa maoni yao.

Katika barua ya Machi 31 mwaka huu, Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga, akiwakilisha maoni ya taasisi zaidi ya 10 ikiwemo TEF, MCT, LHRC,Citizen’s Information Bureua, walitoa maoni yao ikiwemo kupendekeza jina la muswada.



“Zaidi ya asilimia 90 ya muswada huu ni maoni ya wadau wa habari na tunayo kwa maandishi,” alisema Waziri Nape akiijulisha Kamati jana mjini Dodoma kuwa kwa upande wa Serikali wadau walishashirikishwa na sasa imebaki hatua ya kanuni za Bunge.

JELA KWA KUGHUSHI HUDUMA ZA NHIF

$
0
0
Mkazi wa Dar es Salaam Bw. Michael Francis baada ya kuhukumiwa kifungo cha miaka miwili jela au kulipa faini ya shilingi milioni moja kwa kosa la udanganyifu katika huduma za Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.
Mshitakiwa wa Pili na wa Tatu wakiwa chini ya ulinzi baada ya kutiwa hatiani na kuhumiwa kifungo cha miaka miwili jela.
Mshitakiwa Bw. Francis muda mfupi baada ya kuhukumiwa kifungo kwa makosa ya udanganyifu.
Mshitakiwa Bw. Godfrey Nyika ambaye ndiye kitambulisho chake cha matibabu kilitumiwa isivyo halali na BW. Francis baada ya hukumu.

…………………………………………………………

Na Grace Michael

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Kinondoni imewahukumu wakazi wawili wa Mkoa wa Dar es Salaam kifungo cha miaka miwili jela au faini ya shilingi Milioni moja kwa makosa ya kujipatia huduma za Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa njia za udanganyifu.

Hukumu hiyo imetolewa leo mahakamani hapo na Hakimu Mkazi Mwandamizi Bweguge Obadia ambaye alisema kuwa ushahidi uliotolewa na mashahidi wa upande wa mashitaka umeithibitishia mahakama pasipo shaka ya aina yoyote kuwa washitakiwa hao walitenda makosa hayo.

Waliohukumiwa kifungo hicho ni pamoja na Bw. Michael Francis na Bw. Godfrey Nyika ambao ni washitakiwa wa pili na wa tatu huku mshitakiwa wa kwanza Bw. Rashid Kidumule akiaachiwa huru baada ya kuthibitika kutotenda kosa hilo.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu Mkazi Mwandamizi Bw. Obadia alisema kuwa hakuna shaka yoyote juu ya washitakiwa hao kutenda makosa ya kujiwakilisha katika duka la dawa la Nakiete kwa lengo la kujipatia huduma ya dawa kwa kutumia kitambulisho cha matibabu cha mshitakiwa wa tatu ambaye ni Bw. Nyika.

“Ushahidi wa mashahidi wa mashitaka unathibitisha bila kuacha shaka yoyote kuwa mshitakiwa wa pili Bw. Francis alijiwakilisha dukani kwa lengo la kupata dawa kwa kutumia kadi isiyo yakwake na hakuna shaka kuwa mshitakiwa wa tatu ambaye ndiye mwenye kadi alimpatia kadi hiyo mshitakiwa wa pili hivyo kwa ushahidi huu Mahakama inawatia hatiani,”anasema Hakimu Mkazi Bw. Obadia.

Alisema kuwa Mahakama hiyo imezingatia makosa waliyoshitakiwa nayo washitakiwa hao pamoja na uhusika wao katika kutenda makosa hayo. Kutokana na hali hiyo, Mahakama ilimhukumu Bw. Francis kifungo cha miaka miwili jela au faini ya shilingi milioni moja huku mshitakiwa Bw. Nyika akihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja au faini ya shilingi laki tano.

Washitakiwa hao walitenda makosa hayo ya kujiwakilisha kwa lengo la kujipatia huduma mwaka 2014 ambapo kesi hiyo imehitishwa kwa wao kukutwa na hatia na kuhukumiwa adhabu hiyo.

Mfuko wa Taifa wa Bima ya afya umekuwa ukitahadharisha wanachama wake juu ya matumizi ya vitambulisho vyao vya matibabu kwa kuonya kufanya udanganyifu wa aina yoyote kwenye huduma zake.

Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bw. Bernard Konga amesema Mfuko utaendelea kuchukua hatua stahili kwa wanachama wasio waaminifu ambao watajihusisha na udanganyifu wa aina yoyote.

“Nitoe tu tahadhari kwa wanachama na watoa huduma wote kuwa kila mmoja ana wajibu wa kuulinda Mfuko kwa kuhakikisha huduma anayoitoa au kuipata iko katika njia sahihi, Mfuko hautakuwa tayari kufumba macho kwa wanaojihusisha na udanganyifu au kuhujumu Mfuko kwa namna yoyote,” alisema Bw. Konga.

KAMATI TENDAJI YA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI TANZANAIA (BAMMATA) YAFANYA MKUTANO WA MAANDALIZI YA MICHEZO YA BARAZA HILO

$
0
0
Wajumbe wa Kamati Tendaji ya BAMMATA wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Ayoub Muhammed Mahmoud (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa maandalizi ya michezo ya majeshi Tanzania itakayofanyika Zanzibar mwaka huu.
Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Ayoub Muhammed Mahmoud na Wajumbe wa Kamati Tendaji ya BAMMATA wakiwa katika picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa Mkutano wa Maandalizi ya Michezo ya Majenshi Tanzania itakayofanyika Zanzibar.
Mwenyekiti wa Baraza la Michezo ya Majeshi Tanzania (BAMMATA) Brigedia Generali Civil Mhaiki akimkaribisha Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Ayoub Muhammed Mahmoud kufungua mkutano wa Kamati Tendaji ya Bara hilo unaofanyika Makao Makuu ya Kikosi cha Valantia Mtoni Mjini Zanzibar, (kulia) Makamu Mwenyekiti wa BAMMATA, CDR wa KMKM Muhammed Ali Bakar.
Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Ayoub Muhammed Mahmoud akifungua Mkutano wa Kamati Tendaji ya BAMMATA wa maandalizi ya michezo ya Baraza hilo unaofanyika Makao Makuu ya Valantia, Mtoni Mjini Zanzibar.
Wajumbe wa Kamati Tendaji ya BAMMATA wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Ayoub Muhammed Mahmoud (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa maandalizi ya michezo ya majeshi Tanzania itakayofanyika Zanzibar mwaka huu.

MZEE AKILIMALI:YANGA HAIWEZI KUKODISHWA KAMA MASUFURIA YA MSIBANI

$
0
0
Kabla ya kufanyika mkutano Mkuu wa dharura wa klabu ya Yanga,siku ya Leo kamati ya Mwafaka wa wazee wa timu hiyo imezungumza na waandishi wa habari kuhusu maamuzi ya mwenyekiti Yusuf Manji kutaka kuitumia nembo ya Yanga kwa miaka 10 ili awe mmiliki halali.

Akizungumza katibu wa kamati hiyo Ibrahim Akilimali ,amesema kuwa kitu ambacho anataka kukifanya Manji kinapelekea kwenye vurugu kubwa kuzidi hata ile ambayo ilishawahi kutokea kipindi cha nyuma kwani atawagawa wanachama pamoja na mashabiki wanaotaka mfumo huo na wale wanaokataa mfumo huo pia.

“Sisi hatutaki kabisa kurudi kule ambapo tulipokuwepo katika migogoro ya miaka nane na mwaka 2002 ndipo tulipata mwafaka wa suluhisho na kukubaliana kuwa tutumie jina ambalo lilidhiwa na waasisi wetu na kuwa na Yanga sport club na Yanga Cooperation”alisema Akilimali
Aidha amesema kuwa Yanga kampuni ilikufa na tukaweka utaratibu wa kuwa na hisa ambazo ni 51 asilimia ni ya Yanga pamoja na asilimia 49 ni ya wanachama na tulizunguka mikoa mingi mno kwa ajili ya kuondoa migogoro,kesi na kuomba radhi wanachama wa klabu hiyo.

Hata hivyo amesema kuwa tulukuwa na mwanasheria ambaye alikuwa mwenyekiti mpaka anamaliza muda wake aliiachia Yanga Mil 200 na hapo hapo tukampata tena mwanasheria mzuri bahati mbaya Nchunga alijiuzulu baada ya kukaa miaka miwili na hatimaye tukampta bwana Manji naye akaongoza miaka miwili kwa sababu ya mahaba yetu ikabidi tuikanyange katiba kwa kumuongezea muda tena na tulimchagua tena.

“Sasa tunashangaa haijapita hata miezi nane linakuja deni la billioni 11 na laki 6 kitu ambacho kimetushutusha mno wanayanga na pia limekuja swala la kuleta hoja kuwa akodishwe Yanga na nembo ya klabu kwa muda wa mika 10 ila sisi tunasema kuwa Yanga ni kubwa sana na haiwezi kukodishwa kama masufuri ya kwenda msibani na mimi na wazee wa kamati kwa pamoja tunasema hatukubaliani na jambo hilo kwa asilimia mia”alisema Akilimali
Kwa upande wa aliyekuwa mwenyekiti wa matawi ya jiji la Dar es salaam ya Yanga,Mohammed Msumi amesema kuwa kutokana na Manji kuwa na mahitaji makubwa na timu hiyo ni vyema akakaa pembeni au kuanzisha timu yake mwenyewe na kuiacha Yanga ili iweze kujiendesha kwa mfumo wa kisasa.

“Tujiulize maswali ivi ni kwanini anataka mchakato huu ufanyike haraka huku alishawahi kusema kuwa Yanga inajiendesha kwa hasara ni mtu gani huyu anakaa sehemu ya aina hiyo na kama hawezi kufuata utaratibu wa klabu na kushindwa kufuata katiba kama anauwezo aanzishe timu yake na kuacha kutumia pesa zake kwa mabavu iili aichukue Yanga”alisema Msumari.
Katibu wa Kamati ya Muafaka ya Yanga Mzee Ibrahim Akilimali akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo leo wakati alipotoa msimamo wa kamati hiyo na baadhi ya wanachama wa Yanga kuhusu ukodishwaji wa Nembo ya timu hiyo.
Katibu wa Kamati ya Muafaka ya Yanga Mzee Ibrahim Akilimali akionyesha baadhi ya vipengele vilivyokosewa katika kukodisha timu ya Yanga kwa na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo leo wakati alipotoa msimamo wa kamati hiyo na baadhi ya wanachama wa Yanga kuhusu ukodishwaji wa Nembo ya timu hiyo.

MKOA WA SONGWE WAPIGWA JEKI MIFUKO 125 YA CEMENT KUTOKA TPB

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Songwe (katikati) Luteni Mstaafu Chiku Galawa akipokea msaada wa Cement mifuko 125 yenye thamani ya shilingi mil 2 kutoka kwa benki ya Posta Tanzania (TPB) tawi la Mbeya.kulia aliyevalia T.shart Meneja Benki ya Posta Mbeya Humphrey Julias ,kushoto Mkuu wa Wilaya ya Mbozi John Palingo na Meneja wa benki ya Posta tawi la Tunduma Teddy Msanzi aliyshikana mkono na Mkuu wa Mkoa wa Songwe. 
Mkuu wa Wilaya ya Mbozi John Palingo akishukuru mara baada ya kupata msaada wa Cement1 kutoka benki ya Posta Tanzania (TPB) 
Mkuu wa Mkoa Songwe Picha ya Pamoja na Viongozi wa Mkoa wa Songwe na wadau mbalimbali . 
BENKI ya Posta Tanzania(TPB) kupitia tawi lake Mkoani Mbeya, imetoa msaada wa mifuko ya saruji 125 thamani ya shilingi milioni 2.5 kwa serikali ya Mkoa mpya wa Songwe.


Akikabidhi mifuko hiyo , kwa uongozi wa serikali ya Mkoa wa Songwe, Meneja wa benki ya Posta mkoa wa Mbeya, Humphrey Julius amesema benki hiyo iliguswa na suala la ujenzi wa majengo mapya ya ofisi za Mkoa wa Songwe hivyo kuona umuhimu wa kuchangia ikiwa kama faida wanayoipata kutoka kwa wateja wanaowahudumia.

Amesema, mbali na kutoa msaada huo wa mifuko ya saruji, pia benki hiyo imeshakabidhi madwati 130 kwa baadhi ya shule za msingi za Wilaya ya Tunduma, Ileje zilizopo Mkoani Songwe na dawati 30 kwa shule ya Mbeya Day Mkoani Mbeya.Amesema, serikali pekee haiwezi kufanya mambo yote ni lazima wadau zikiwemo Taasisi, Mashirika, Asasi na mtu mmoja mmoja kuingiza mikono yao ili kuipungizia serikali mzigo.

Hata hivyo, akipokea msaada huo, Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Luten Mstaafu Chiku Galawa, aliishukuru benki ya Posta kwa msaada huo, muhimu kwani serikali ya Mkoinahitaji zaidi ya mifuko 50 elfu ya saruji na mabati laki moja kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa majengo ya ofisi pamoja na shule na Zahanati.

Wasiioona waaswa kutokata tamaa

$
0
0
Mkuu wa Wilaya Temeke Mh.Felix Lyaniva (kulia) akimkabidhi zawadi ya Cherehani Mkufunzi wa Mafunzo wa ushonaji kwa wasioona Bw. Abdallah Nyangalio wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo jijini Dar es Salaam,wa kwanza kusoto ni Bw. Edwin Rutageruka Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Picha na Benjamin Sawe Maelezo)
tann1
Mkuu wa Wilaya Temeke Mh.Felix Lyaniva (kulia) akiongea na Mkufunzi wa Mafunzo wa ushonaji kwa wasioona Bw. Abdallah Nyangalio wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo jijini Dar es Salaam ambapo Mkuu wa wilaya hiyo amewaasa watu wenye ulemavu kutokata tamaa kimaisha kwani jambo lolote ukiwa na nia nalo na kulifanya kwa nidhamu na kujituma utafanikiwa(Picha na Benjamin Sawe Maelezo)

WAZIRI MKUU AMSIMAMISHA KAZI MHANDISI WA MAJI LINDI

$
0
0
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Lindi (LUWASA), Mhandisi Adam Alexander (pichani mwenye mafaili) kwa kosa la matumizi mabaya ya ofisi pamoja na kushindwa kusimamia ujenzi wa kituo cha kuzalisha maji katika Manispaa ya Lindi.

Waziri Mkuu amemkabidhi Mhandisi huyo kwa Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Lindi, Bw. Stephen Chami na kumuelekeza afanye uchunguzi zaidi juu ya suala hilo.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumatano, Oktoba 19, 2016) wakati alipotembelea mradi wa maji wa Ng'apa ambapo ameagiza nafasi hiyo ikaimiwe na Mkurugenzi Msaidizi wa mamlaka hiyo, Mhandisi Idrisa Sengulo.

"Kamanda wa TAKUKURU fanya mapitio ya kina ya mshahara wake. Yeye anasema analipwa Wizarani, mimi najua analipwa na LUWASA. Angalia kazi aliyokwenda kuifanya Dar es Salaam kama inalingana na siku alizokaa,” amesisitiza Waziri Mkuu.

Mhandisi hiyo anakabiliwa na tuhuma mbalimbali ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za ofisi pamoja na kupokea mshahara bila la kulipa kodi ya mapato ya mshahara (PAYE), kujilipa kiwango kikubwa cha posho pamoja na kusafiri kwa muda mrefu.

Waziri Mkuu amesema Serikali haiwezi kuvumilia kuona wananchi wanapata shida huku watendaji waliopewa dhamana ya kuwatumikia hawaonekani kwenye vituo vyao vya kazi. "Huyu nimemuita mimi aje huku, hadi jana alikuwa Dar es Salaam."

Alipoulizwa sababu za kutokuwepo ofisini kwake kwa muda mrefu, Mkurugenzi huyo alisema kwamba alikuwa Dar es Salaam akiandika maombi ya fedha kwa ajili ya kutatulia changamoto mbalimbali zinazoikabili mamlaka hiyo.

"Unatumia siku ngapi kuandika proposal, msomi unatumia mwezi mzima kuandika proposal na unakaa Dar es Salaam hata Katibu Mkuu wako hajui na huko unajilipa posho tu! Tena baada ya kulipwa sh.120,000 kwa siku wewe unajilipa sh.150,000. Hatuwezi kuvumilia hali hii,” amesema.

Waziri Mkuu amemaliza ziara yake siku tatu mkoani Lindi na amerejea jijini Dar es Salaam.

                            
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S. L. P. 3021,
11410 - DAR ES SALAAM
JUMATANO, OKTOBA 19, 2016.

WAKAMATWA KWA MIUNDOMBINU YA SHIRIKA LA UMEME TANESCO YENYE THAMANI YA TSH 61,000,000

$
0
0
Kaimu Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Lucas Mkondya.(wa pili kushoto) akiwa na waandishi.
Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Leila Muhaji akizungumza na waandishi wa habari kuhusu wizi huo wa vifaa vya umeme vyenye thamani ya milioni 61 na kukamatwa,Kulia ni Kaimu Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Lucas Mkondya.
Kaimu Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Lucas Mkondya.(wa pili kushoto) akiwa na waandishi na walinzi wa Tanesco. 
Kaimu Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Lucas Mkondya.(wa pili kushoto) akiwa na waandishi.
 
Gari la Tanesco likiwa na shehena ya vifaa vilivyoibwa Kikuu cha Polisi Dar es Salaam. 
Gari la Tanesco likiwa na shehena ya vifaa vilivyoibwa Kikuu cha Polisi Dar es Salaam. 

jioni maeneo ya Salasala Mkoa wa Kipolisi Kinondoni Polisi wakishirikiana na Kikosi kazi cha kuzuia uharibifu wa miondo mbinu ya Shirika la umeme Tanzania Tanesco lilipata taarifa toka kwa raia mwema kuwa kuna watu wanaohujumu miundo mbinu ya Shirika hilo.

Kikosi hicho kilifika eneo hilo katika nyumba ya Willfred Barutti (45) mkazi wa Makumbusho na kufanya upekuzi kwenye nyumba hiyo ambapo walivipata vifaa mbalimbali Line Meterial ambavyo hutumika kwa ajili ya kuunganisha umeme vya Kampuni ya Tanesco.Polisi walikwenda katika nyumba nyingine mali ya Betrice Emmanuel (42) mkazi wa Salasala Mabanda wakafanya upekuzi na kufanikiwa kukamata vifaa vifuatavyo;

Nyaya aina ya Drums'02,roller ya waya aina ya AICC ya umeme wa 50 mm ambazo hutumiwa na tanesco kituo cha Kilimahewa huko Kawe Wilaya ya Kinondoni.

Thamani ya vifaa hivyo vinakadiliwa kuwa Tsh.61,000,000,Watuhumiwa wawili wanashikiliwa kwa mahojiano na Upelelezi utakapokamilika watapelekwa mahakamani kwa hatua za kisheria.

MNAKARIBISHWA KWENYE MAONESHO YA SANAA ZA KATUNI

$
0
0
Wadau wote mnakaribishwa katika maonesho ya sanaa za katuni (Cartoon) yatakayo funguliwa rasmi kesho tar 20 saa 11 jioni, Masoud Kipanya atashirikisha historia ya maisha yake katika sanaa, na tar 21 saa 1 hadi saa 3 usiku LUMUMBA THEATRE watafanya onesho la Muziki wa asili, Ngomba za asili na Sarakazi, katika ukumbi wa kisasa wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar.

TAARIFA KUTOKA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA

2016/2017 academic year begins at SUZA

$
0
0


2016/2017 Academic year begins at SUZA


The orientation week for the newly admitted students for the academic year 2016/2017 started on Monday 17th October, 2016.

Prof. Idris Rai, the Vice Chancellor of the State University of Zanzibar (SUZA) welcomed the new students for this academic intake.

In his welcoming remarks, the Vice Chancellor urged the students to intensely focus on their studies and utilize their time and SUZA resources efficiently. He told the new students that they can learn a lot from this university as it has very good accessibility of reference books and internet facility so they have to use this available technology for learning. He also advised them to make libraries found in all SUZA campuses their best friends.

Prof. Rai warned the students not to engage in delinquency and instead they should be upright in all their undertakings; he mentioned plagiarism as a severe violation of academic norm in which anyone caught practicing this undesirable tendency would not be tolerated. “Those accused and found guilty of this offence would immediately be expelled”, he reiterated.
Prof. Idris Rai (standing), the Vice Chancellor delivers welcome remarks to the newly admitted students for the academic year 2016/2017.

The Vice Chancellor informed the students that the State University of Zanzibar will very soon become a bigger university following merging with other Zanzibar higher learning institutions of Zanzibar Institute of Financial Administration (ZIFA), Zanzibar Institute of Tourism Development (ZiTOD) and College of Health Sciences (CHS), he updated them that the merging bill has recently been passed by the Zanzibar House of Representatives and now awaits the endorsement by the President of Zanzibar and Chairman of the Revolutionary Council to become operational. 
New students during the 1st day of the orientation week.


He told the students that SUZA will have not below 7,000 students after this merging. “From you our students we are preparing to be able to fit in the regional job market in terms of competitiveness from the content you will be imparted and we have enough strength to accomplish this”, he guaranteed the students. 

Earlier, Dr. Haji Mwevura Haji, the Deputy Vice Chancellor on academics, research and consultancy enlightened the students that while they are here they are free to use their freedom the way they like, but he cautioned them not to infringe others’ rights in making use of their freedom. “Your freedom ends where other colleague’s freedom starts, so utilize it wisely and by any means do not squander it”, he insisted. 

Welcoming the new students, Dean of Students, Ms. Salha Khalfan Khamis appealed to them to prevent the university environment and infrastructure by all means. “Portray yourselves that you are SUZA students, behave decently and show good conduct within and outside the university premises”, she insisted.

In this academic year, over 900 students have been admitted in different postgraduate, undergraduate, diploma and certificate programmes. Classes for all students will officially commence on Monday 24th October, 2016

Mwekezaji mzalendo sekta ya madini achangia wahanga wa tetemeko

$
0
0

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt Mhandisi Juliana Pallangyo (kushoto), akipokea hati ya malipo (Bank Slip) kwa ajili ya kusaidia wahanga wa tetemeko Kagera, kutoka kwa Aloyce Msabi (kulia). Wengine pichani kutoka kushoto ni Kaimu Kamishna wa Nishati na Masuala ya Petroli-James Andilile, Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi-Lusius Mwenda na Kaimu Kamishna wa Madini- Mhandisi John Shija.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt Mhandisi Juliana Pallangyo (kushoto), akipokea hati ya malipo (Bank Slip) kwa ajili ya kusaidia wahanga wa tetemeko Kagera, kutoka kwa Aloyce Msabi (kulia). Wengine pichani kutoka kushoto ni Kaimu Kamishna wa Nishati na Masuala ya Petroli-James Andilile, Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi-Lusius Mwenda na Kaimu Kamishna wa Madini- Mhandisi John Shija.
Kutoka kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt Mhandisi Juliana Pallangyo, Kaimu Kamishna wa Nishati na Masuala ya Petroli-James Andilile, Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi-Lusius Mwenda, Kaimu Kamishna 


Na Veronica Simba

Mwekezaji mzalendo katika Sekta ya Madini nchini, Aloyce Msabi, amechangia mifuko 400 ya saruji yenye thamani ya shilingi 4,800,000 kwa wahanga wa tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 10, mwaka huu mkoani Kagera.

Akikabidhi hati ya malipo husika (Bank Slip) aliyoyafanya katika Benki ya CRDB Tawi la Azikiwe kwenye akaunti ya ‘KAMATI YA MAAFA KAGERA,’ kwa Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo; Msabi alisema ameamua kuitikia wito wa Serikali kusaidia wahanga hao ikiwa ni sehemu ya kurudisha kwa umma kile anachopata kutokana na uwekezaji wake katika sekta ya madini.

Pia, aliongeza kuwa, akiwa ni mwananchi mzalendo, ameguswa na janga lililowapata wananchi wa Kagera na hivyo kuamua kuchangia ili kuwasaidia.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Mkuu Pallangyo, alimshukuru Msabi kwa niaba ya Serikali kwa moyo wa ukarimu aliouonesha na kutoa rai kwa watanzania wengine, hususan wawekezaji wazalendo kuiga mfano huo na kujenga tabia ya kusaidia jamii zinazowazunguka kutokana na kipato wanachopata kupitia shughuli wanazofanya.

Hati hiyo ya malipo, imewasilishwa kwa Kamati ya Maafa iliyo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu.Walioshuhudia makabidhiano ya hati hiyo katika Ofisi za Wizara ni pamoja na Kaimu Kamishna wa Madini –Mhandisi John Shija, Kaimu Kamishna wa Nishati na Masuala ya Petroli-James Andilile, Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi-Lusius Mwenda na Mratibu wa Idara ya Madini, Phillip Ngereja.

Pamoja na shughuli nyingine mbalimbali katika sekta ya madini; Msabi pia hupata asilimia moja ya uzalishaji kutoka Mgodi wa Dhahabu wa ACACIA-North Mara, ambao aliingia nao ubia kupitia leseni yake ya uchimbaji.

KINANA AKUTANA NA ABALOZI WA SUDAN JIJINI DAR ESSALAAM, LEO

$
0
0
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na Balozi wa Sudan nchini Tanzania, Mahgoub Ahmed Sharfi, Ofisini kwake, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo
  Balozi wa Sudan nchini Tanzania, Mahgoub Ahmed Sharfi, akifafanua jambo wakati alipokuwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiagana na Balozi wa Sudan nchini Tanzania, Mahgoub Ahmed Sharfi,baada ya mazngumzo yao yaliyofanyika leo katika  Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam,PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO-theNkoromo Blog.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimkaribisha Ofisini kwake, Balozi wa Sudan nchini Tanzania, Mahgoub Ahmed Sharfi, kabla ya mazungumzo yao yaliyofanyika leo, Alhamisi, Oktoba 20, 2016, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam

WACHEZAJI WATATU WA GOLF WA LUGALO WAITWA TIMU YA TAIFA

$
0
0
Na Luteni Selemani Semunyu JWTZ.

Wachezaji Watatu wa Timu ya Golf ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ya Lugalo wameteuliwa kujiunga na timu ya Taifa ya Mchezo huo ikiwa ni mara ya kwanza tangu kuanzishwa klabu hiyo miaka 10 iliyopita kupata idadi hiyo.

Akiongea na mwandishi wa habari hizi Jijini Dar es Salaam nahodha wa Klabu hiyo ya Lugalo Kapteni Japhet Masai alisema hatua hiyo ya furaha kwa klabu yao imekuja baada ya mashindano ya wazi ya Arusha Open yaliyomalizika hivi karibuni Jijini Arusha.

”Ni mara ya kwanza na imekuja Muda Mchache baada ya klabu kupata Mwenyekiti mpya Brigedia Jenerali Michael Luwongo pengine ni ishara njema ya Uongozi wake katika klabu hiyo yenye malengo makubwa ya kubor eshwa.” Alisema Masai. 

Aliongeza kuwa Klabu hiyo iliwahi kutoa Mchezaji Mmoka Mwaka 2012 sasa hii ni kwa mara ya kwanza kwa Klabu hiyo kutoa Wachezaji wa Timu ya Taifa zaidi ya mmoja tangu kuanzishwa kwa klabu hiyo Miaka 10 iliyopita na kutoa mchezaji hata mmoja Tangu Mwaka 2012.

Aliwataja wachezaji hao kutoka Lugalo ni Michael Obare ,Richard Mtweve na Henrick Nyenza ambao wataungana na wachezaji wengine 11 katika mchujo utakaofanyika katika Viwanja vya Klabu ya Lugalo Jumamosi Oktoba 22 ili kupata wachezaji 10 kati yao akiwemo mmoja wa Akiba.

Aliongeza kuwa sasa wachezaji hao wanajiandaa na mchujo ili jumamosi chini ya Uangalizi wa Wachezaji wa kulipwa waweze kufanya vizuri na wajumuishwe katika kikosi huku Wachezaji watalazimika kucheza Mikwaju ya Jumla Gross 74.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa hivi karibuni na Mwenyekiti wa chama cha Golf Tanzania Joseph Tango aliwatangaza wachezaji wengine walioitwa kuwa ni Isack Wanyenche (Kili Golf), Abbas Adam (Moshi Club),Adam Said (Moshi Club).

Wengine walioitwa ni Elisha Mbwambo (TPC),George Sembi(TPC),Victor Joseph (Dar Gymkhana),Amani Said (Dar Gymk(Dar Gymkhana),Salim Shariff (Dar Gymkhana),Idan Iziku (Dar Gymkhana) ,Jay Nathwani (Gymkhana Arusha),Pravin Singh(Gymkhana Arusha). 

Kwa Mujibu wa taarifa hiyo wachezaji hao wanatarajia kuwakilisha Nchi katika mashindano ya Afrika Mashariki East Afrika Golf Challenge Edition 2016 nchini Ethiopia na wanatarajiwa kuanza kambi Jijini Dar es Salaam.

Mchezaji wa Golf wa Klabu ya Jeshi ya Lugalo Michael Obare ambaye ameteuliwa kujiunga na Timu ya taifa akiwa kwenye harakati za Mcheo huo hivi karibuni Jijini Arusha .
Mchezaji wa Golf wa Klabu ya Jeshi ya Lugalo Michael Obare (Wakwanza kulia) ambaye ameteuliwa kujiunga na Timu ya taifa hivi karibuni Jijini Arusha akiwa kwenye mazoezi katika uwanja Lugalo jijini Da es Salaam(Picha na Luteni Selemani Semunyu).

MTANDAO WA MAWASILIANO WA SERIKALI KUIPUNGUZIA SERIKALI GHARAMA YA MAWASILIANO KWA NJIA YA SIMU

$
0
0
Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Wakala ya Serikali Mtandao (eGA) Bi. Suzan Mshakangoto akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu matumizi ya Mtandao wa Mawasiliano wa Serikali leo Jijini Dar es Salaam. Taasisi 72 za Serikali tayari zimekwishaunganishwa na Mtandao huo kupitia Mkongo wa Taifa.
: Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Wakala ya Serikali Mtandao (eGA) Bi. Suzan Mshakangoto akiongea na mtu kutoka Taasisi ya Uongozi wa Elimu (ADEM) ya Bagamoyo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu matumizi ya Simu zilizounganishwa na Mtandao wa Mawasiliano wa Serikali leo Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia maelezo kutoka kwa Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Wakala ya Serikali Mtandao (eGA) Bi. Suzan Mshakangoto (hayupo pichani) wakati wake na waandishi hao kuhusu matumizi ya Mtandao wa Mawasiliano wa Serikali, leo Jijini Dar es Salaam. Picha na: Frank Shija, MAELEZO.

Na: Lilian Lundo – MAELEZO

Serikali kupitia Wakala ya Serikali Mtandao (eGA) imeendelea kutekeleza uunganishwaji wa mtandao wa Mawasiliano wa Serikali ambapo mpaka sasa Taasisi 72 zimeunganishwa na mtandao huo. Hayo yamesemwa na Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano eGA Suzan Mshakangoto alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa miundombinu ya Tehama inayohusisha Serikali, leo Jijini Dar es Salaam.

Suzan amesema kuwa Taasisi za Serikali zilizounganishwa na mtandao huo zitakuwa zinawasiliana kwa gharama ndogo kwa kutumia simu zitakazokuwa zikitumika kama ‘extension’ ambazo zitakuwa zinatumia internet kupitia Mkongo wa Taifa. “Mtumishi wa Taasisi moja katika taasisi zilizounganishwa na mtandao huo anaweza kupiga simu kwenda taasisi nyingine ya nje ikawa kama amepiga simu ya ‘extension’ ndani ya ofisi moja,” alifafanua Suzan.

Vile vile Taasisi za Serikali zitapunguza gharama za kuchajiwa huduma za internet kutoka kwa watoa huduma binafsi ambao gharama zao ziko juu ukilinganisha na huduma inayotolewa na wakala wa Serikali. Aidha Taasisi na Idara zote za Serikali zitakuwa ndani ya mtandao na mtoa huduma mmoja wa huduma za mtandao ambapo itasaidia kwenye utunzaji wa nyaraka za Serikali na kurahisha mawasiliano ndani ya taasisi hizo.

Hivyo basi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora kwa kushirikiana na wakala imetoa mafunzo kwa wataalamu wa TEHAMA na Makatibu Muhtasi kutoka taasisi zilizounganishwa na mtandao huo juu ya uendeshaji na usimamizi wa mtandao wa Serikali pamoja na matumizi ya simu zinazotumia itifaki (IP Phones).

Mpango wa Serikali ni kuzifikia Ofisi za Mikoa na Halamashauri zote hapa nchini ili kutumia mawasiliano ya simu za itifaki, barua pepe na mifumo ya TEHAMA katika kubadilishana taarifa, ambapo kufikia Disemba 2016 taasisi nyingine 77 kutoka mikoa 20 ya Tanzania Bara zitakuwa zimeunganishwa kwenye mtandao huo.

TAHADHALI YA UWEPO WA UKAME WA CHAKULA

$
0
0
Mkurugenzi Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Brig.Jenerali Mbazi Msuya akifafanua jambo wakati wa Mkutano na waandishi wa habari uliohusu utoaji wa tahadhali ya hali ya Ukame utakaosababisha kukosekana kwa chakula kwa baadhi ya maeneo nchini Oktoba 20, 2016. Mkutano ulifanyika katika Ukumbi wa Mikutano ofisi hiyo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Bw. Paschal Waniha (wa kwanza kushoto) akitoa hoja za masuala ya umuhimu wa taarifa za hali ya hewa katika kujiandaa kukabili maafa wakati wa Mkutano na waandishi wa habari Oktoba 20, 2016. Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Chakula Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Bi. Marystela Mtalo akiwasilisha mada juu ya umuhimu wa kuhifadhi chakula na kulima mazao yenye kustahimili ukame wakati wa mkutano wa waandishi wa habari katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu 20 Oktoba, 2016.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Brig.Jenerali Mbazi Msuya (hayupo pichani) wakati wa mkutano na wanahabari hao katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu tarehe 20 Oktoba, 2016. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live


Latest Images